Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Kwa Nini Watu Wengi Na Hasa Vijana Wanashindwa Kuzifikia Ndoto Zao

     

    Juzi niliomba watu wapendekeze mada ambazo nitaandikia kwenye blogu yangu kupitia status yangu ya whatsap. Nilipokea maombi kadha wa kadha ambayo nitakuwa nayafanyia kazi moja baada ya jingine. Ombi mojawapo lilikuwa ni kuandika makala maalumu kueleza kwa nini watu wanashindwa kufikia NDOTO zao.

    Kabla sijaenda mbali nataka ufahamu kuwa tayari nimeandaa makala nyingi kuhusu ndoto na jinsi unavyoweza kufikia NDOTO zako. Makala zote hizo nitajidi kuzihusisha kwenye makala ya leo ili uweze kurejea na kuzisoma.

    Lakini pia nimeandika kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO. Unaweza kupata kitabu hiki kwa kuwasiliana na 0755848391 utatumiwa popote ulipo duniani.
    Natamani sana siku moja nikuone ukiwa umeweza KUFIKIA NDOTO ZAKO KUBWA

    kupata kitabu hiki wasiliana na 0755848391. Utatumiwa popote ulipo duniani

    1. KINACHOKUKWAMISHA kufikia ndoto zako ni kuchelewa kuchukua baadhi ya hatua.

    Ulipaswa kuwa umechukua hatua fulani ila sasa unachelewa aidha kwa kutoelewa au kwa kuelewa na kupuuza, au kwa uoga.

    Mfano, kwenye ulimwengu wa sasa ulipaswa kuwa umeweka biashara yako au kipaji chako mtandaoni, ila hujafanya hivyo.

    Na haikugharimu chochote. Kwa bando lako tu unafungua na kuendesha blogu yako, unatengeneza akaunti za biashara kwenye mitandao ya kijamii na mengine mengi.

    Ulipaswa kuwa unatunza kumbukumbu za hesabu za mapato na matumizi ya biashara yako, ila hufanyi hivyo, halafu ukija unasema kwamba biashara ni mbaya.
    Kwani inakugharimu wewe shilingi ngapi kufanya kitu kama hiki.

    Kuna baadhi ya hatua unachelewa kuzichukua, na hapo unakuwa unakwama kufikia ndoto zako.

    2. Kutaka kuishi maisha kama ya wengine wakati una ndoto kubwa

    Unapokuwa na ndoto kubwa matumizi yako, mwenendo wako, ulaji wako na mambo mengine yote yanabadilika.

    Huwezi kuwa na ndoto ya kuwa mkimbiaji wa Marathon ukawa hufanyi mazoezi huku ukila chipsi kila siku. Vitendo vyako vinapaswa kuendana na ndoto yako.

    Kuna vitu bila kulazimishwa wala kuambiwa na mtu yeyote utapaswa kuachana navyo, sio kwa sababu ni vibaya ila tu kwa sababu havieneani na ndoto zako kubwa.

    Huwezi kuwa na ndoto za kuwa bilionea huku ukiwa unataka kumhonga kila binti anayepita mbele yako.


    3. Hujafanya uamuzi wa dhati wa kuzifikia NDOTO ZAKO.

    Ngoja nikwambie kitu, kuna uamuzi unapaswa kuufanya kwenye maisha yako. Na uamuzi huu ni au utazifikia ndoto zako au utakufa ukiwa ukiwa unazipambania au hutazifanyia kazi kabisa ndoto zako.

    Hapo unapaswa KUCHAGUA maana maisha ni kuchagua.
    Ukichagua kuzifanyia kazi ndoto, fahamu kuwa umechagua kitu kigumu ila kinachowezekana.

    Kama ndoto ingekuwa ni barabara basi ni sawa na kuchagua barabara mbaya, yenye makorongo ila inayokufikisha ikulu.
    Nadhani umewahi kusikia kuwa mlango wa kuingia mbinguni ni mwembamba, hivyohivyo mlango wa kufikia ndoto zako. Haupitiki mara kwa mara ndio maana watu wengi kwenye jamii yako wameamua kuishi maisha ya kawaida.

    Mwaka 1968 kwenye mbio za marathon; mshiriki mmojawapo alikuwa ni Mtanzania John Stephen Akhwari

    Mtanzania John Stephen Akhwari kwenye mbio za marathon mwaka 1968.

    Mtanzania huyu naweza kusema siku hiyo alikuwa miongoni mwa watu waliotegemewa kushinda. Hii ni kutokana na rekodi yake ya mashindano ya nyuma likiwemo moja la olimpiki na jingine la jumuia ya madola ambayo alikuwa amefanya vizuri sana.

    Sijui kama kubeti kulokuwepo miaka hiyo, ila kama vijana wa siku hizo wangekuwa wa kubeti, basi siku hiyo wangempa ushindi wote JOHN STEPHEN AKHWARI.

    Alianza mbio kama ambavyo watu wengine walikuwa wameanza. Baada ya kufikia kilomita kama thelathini hivi, aliumia na kupata maumivu ambayo kwa mtu wa kawaida yalitosha tu kumfanya asiendelee na mbio. Ila hali haikuwa hivyo kwa Bwana John Stephen Akhwari.

    Alitulia pembeni kwanza. Alipewa huduma ya kwanza, kisha baada ya hapo akaendelea kusonga mbele. Zamu hii akiwa anajikongoja. Gari la kumbeba lililetwa ila alikataa kulipanda.

    Wale ambao hawakuumia walimaliza mbio mapema na Mwethiopia siku hiyo ndiye alishindwa

    Saa moja baada ya mashindano kuwa yamekamilika na watu wameanza kuondoka uwanjani pale, ndipo vyombo vya habari vilipata taarifa kuwa kuna mtu bado anakimbia.

    KUMBUKA hapa watazamaji wengine wameshaondoka uwanjani na tuzo zilishatolewa. John Stephen Akhwari ambaye aliumia ndipo alikuwa anaingia.

    Vyombo vya habari vilituma watu wao ili warekodi kinachoendelea. Walimwona John Stephen Akhwari alivyokuwa anachechemea ila akipambama kumaliza mbio. Na mwisho alimaliza huku akipigiwa makofi ma watazamaji wachache waliokuwepo pale uwanjani.

    Alipoulizwa kwa nini uliendelea kukimbia wakati ulikuwa umeumia, alisema. Nchi yangu haikunituma maili elfu tano ili nianze mbio bali nimalize mbio.
    Tokea hapo kauli hiyo imekuwa kauli inayotumika sana kwenye ulimwengu wa michezo kuwahamasisha wachezaji.

    Ninachotaka utoke nacho hapa Ni kwamba, unapaswa kuamua kwa DHATI kuifanyia kazi ndoto yako au kutoifanyoa kazi kabisa. Ila hakuna kitu cha katikati

    Kwa Leo naishia hapo. Kuna makala nyingi za nyuma ambazo nimewahi kuandika kuhusu mada hii. Nimeziunganisha kwenye makala ya leo. Naomba UBONYEZE viunzi husika ili uweze kuzisoma.

    Mimi naitwa
    GODIUS RWEYONGEZA
    0755848391
    MOROGORO

     

    [block rendering halted]

  • Chukua Mambo Haya 10 Kuhusu Namna Ya Kuanza Kidogo Na Kufikia Pakubwa

    1. Mti wowote ule mkubwa haukuanza ukiwa hivyo, ulikua taratibu mpaka kufikia ulipofikia.

    Wewe pia kuwa tayari kuanza kidogo na kuendelea mbele zaidi.

    2. Ukitaka kupanda ghorofa kuna njia mbili. Unaweza kupanda ngazi moja baada ya nyingine au unaweza kupanda lift.

    Ila fahamu kuwa njia ya kwanza itakuimarisha na kukufanya uwe bora zaidi.

    3. Ukianza kupita eneo mara ya kwanza, nyayo zako hazitaonekana. Ila ukiendelea kupita mara kwa mara njia itatengenezeka.

    4. Njiti ndogo tu ya kiberiti ina uwezo wa kuwasha moto wa kuunguza msitu mkubwa. Usidharau kitu kwa udogo wake.

    5. Safari ndefu ya maili elfu moja, huanza na hatua moja.

    6. Ukikata mti kwa shoka, haukatiki kwa shoka la kwanza bali kwa muunganiko wa mashoka mengi unayopiga.

    7. Ukitaka kuhamisha mlima, Anza kwa kuondoa jiwe moja.

    8. Ukitaka kujenga ghorofa, anza kuweka jiwe moja.

    9. Kuna vitu katika maisha havihitaji haraka. Huwezi kupata mtoto ndani ya mwezi mmoja kwa kuwapa mimba wanawake tisa.

    10. Katika maisha, hakikisha una ndoto kubwa. Zifanyie kazi kila siku.


  • KUWA MABADILIKO UNAYOTAKA KUYAONA

    Kama kuna mabadiliko unataka kuyaona kwenye jamii yako wewe kuwa wa kwanza kuonesha njia.

    Badala ya kukaa na kulalamika kwamba unataka ufanyiwe kitu fulani. Onyesha njia. Fanya unachotaka kuona.

    Mabadiliko yanaanza na mimi na wewe.

    Ni mabadiliko gani unayotaka kuona?

    Picha hiyo hapo juu inaonesha kijana aliyetaka kufanya mabadiliko kwenye jamii yake kwa kuwasaidia kusoma vitabu. Aliweka maktaba kwenye saloon yake badala ya TV na kila mtu aliyesoma kitabu alipewa punguzo wakati wa kunyolewa.

    Wewe ni mabadiliko gani unataka uyaone kwenye jamii yako. Utachukua hatua gani ndogo kuhakikisha na wewe unakuwa sehemu ya hayo mabadiliko?

    Nishirikishe kupitia godiusrweyongeza1@gmail.com

    SOMA ZAIDI: TATIZO LAKO WEWE

    Hapa Ndipo Mabadiliko Makubwa Huanzia

    Kama Unataka Kubadili Dunia Fanya Haya Hapa

    Ni mimi
    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

    .

  • Sifa Moja Kuu Ya Watu Wanaofanya Vitu Visivyo Vya Kawaida

    Wanaofanya vitu visivyo vya kawaida siyo kwamba wao wameshuka kutoka mbinguni au wana upekee ambao wewe huna.

    Ni watu tu kama wewe ambao wamejitoa kufa na kupona kuhakikisha kwamba wanafika mbali. Na huo ndio mwanzo wao wa kufanya vitu visivyo vya kawaida

    Godius Rweyongeza

  • Unawezaje Kupata Wazo La Biashara La Kipekee?

    Unachohitaji sana wewe, siyo wazo la kipekee ambalo halijawahi kufanyika. Unachihitaji ni kUchagua kitu kimoja na kuhakikisha kwamba unashughulika na hicho.

    Angalia jamii yako ina tatizo gani kisha tatua hilo tatizo. Ebu fikiria kuhusu sehemu unapopata huduma mtaani kwako. ebu fikiria juu ya supermarket yoyote mjini kwako. au fikiria kuhusu basi ambalo huwa unatumia kusafiri, hawa jamaa hawa hawakuwa wa kwanza kuingia kwenye soko.

    Kitu kikubwa ni kwamba walifanya uamuzi wa kwamba tunaenda kuzalisha bidhaa na kutatua tatizo ambalo linawakumba watu. Basi. Hawakuwa wagunduzi wa hicho kitu, hawakuwa waanzilishi wala wa kwanza kufanya hicho kitu.

    Ebu kwa mfano fikiria kampuni inayotengeneza redio. Haikugundua hiyo redio. Na walikuwa wanajua kwamba kuna redio nyingine huko mitaani zinauzwa. Hawakukaa na kuanza kufikiri juu ya wazo gani jipya na la kipekee waje nalo.

    Kitu pekee walichokuwa na uhakika nacho ni kwamba, kila mtu anahitaji redio na watu wananunua redio mara zore. Hivyo, ngoja na sisi tutengeneze moja na kuiuza.

    Hivyo, huhitaji kuwa wa kwanza kwenye soko. Wanunuaji wanapoenda kununua hawanunui kwa sababu mtu au kampuni ili kuwa ya kwanza kutengeneza bidhaa husika.

    Bali wenyewe wananunua kwa sababu,

    • Wana tatizo na
    • Wameona bidhaa ambayo inatatua tatizo lao

    Hivyo. Badala ya wewe kuanzakufuta wazo ambalo halijawahi kufanyika hapa duniani, fanya hivi:

    • Angalia tatizo walilonalo watu
    • Tengeneza bidhaa inayoweza kutatua hilo tatizo lao
    • Ilete mbele ya wahusika.

    Acha kulisubiria wazo la kipekee. Ukisubiria wazo la aina hii, utakufa ukiwa bado unasubiri.

    Kila la kheri

    Godius Rweyongeza

    0755848391

    SOMA ZAIDI

  • E-BOOK MPYA: KIPAJI NI DHAHABU: Jinsi Ya Kukigundua, Kukinoa Na Kutumia Kipaji Chako Kwa Manufaa

    Najua umekuwa unajiuliza, hivi mimi nimezaliwa na kipaji? Kipaji changu Ni kipi?
    Nawezaje Kukigundua?

    Nakiendelezaje na kinawezaje kuninufaisha?

    Kwa majibu ya maswali yote hayo na zaidi, karibu usome ebook ya kipaji ni dhahabu. Ebook hii ya kipekee sana imejaa mambo mengi muhimu kuhusu kipaji, unavyoweza kukinoa, kukiendeleza mpaka kikakufikisha mbali.

    E-book hii ya kipekee itakusaidia wewe kugundua kipaji chako na kukitumia kwa manufaa.

    Kuona yaliyomo na kusoma utangulizi BONYEZA HAPA

    E-book hii unaweza kuipata sasa kwa elfu 5 tu. Tuma fedha kwa 0684 408 755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Baada ya hapo utaniambia nikutumie e-book hii.

    SOMA ZAIDI:Kipaji Ni Dhahabu: Jinsi Ya Kukigundua, Kukinoa Na Kutumia Kipaji Chako Kwa Manufaa

    /

    KIPAJI NI DHAHABU: Jinsi Ya Kukigundua, Kukinoa Na Kutumia Kipaji Chako Kwa Manufaa

  • Ungekuwa wewe umewekeza kwenye hii kampuni ungefanyaje?

    Brown Unaendeleaje? Bila shaka umeamka salama  kabisa.

    Leo ninataka niongee na wewe kuhusu uwekezaji.

    Kwanza ebu niambie mimi, Ni kampuni gani unaikubali hapa Tanzania? Ni kampuni gani ambayo kwa vyovyote vile unapenda  huduma zake na kamwe huchoki kwenda kwao. Ebu niambie ni ipi hiyo?

    Inaweza hata isiwe kampuni kubwa, ikawa biashara yoyote ya kawaida tu, pengine hata mtaani kwako, ila wewe binafsi unaikubali. Kila mara lazima uende kwao kupata huduma zao.

    Sasa ebu fikiria kwa jinsi ambavyo wewe unaikubali hiyo kampuni, biashara au taasisi hiyo, ungekuwa wewe ndiye mmiliki au mmoja wa watu wenye maamuzi makubwa kwenye hiyo kampuni ni kitu gani cha ziada ungefanya kuhakikisha kwamba kampuni yako inazidi kusongambele?

    Ebu andika jibu lako chini. Ujue jibu lolote utakalopata litakusaidia wewe pia.

    Nataka jibu lolote utakalopata uende na wewe ullitumie kwenye biashara au kipaji chako.

    Kama  umeona hicho kitu ndicho kinaweza kuifanya biashara unayoikubali bora zaidi, na wewe ukikitumia ni wazi kuwa kitaboresha biashara yako pia. Kwa hiyo kakitumie wewe KWENYE kampuni au biashara yako.

    Pia tumia mbinu nyingine ambazo unaziona kwa hiyohiyo kampuni unayoikubali.  Angalia mbinu ambazo wanatumia kuhudumia wateja, kuwasiliana nao n.k.

    ZITUMIE kuboresha biashara yako na kuifanya kuwa Bora zaidi.

    Kama unaikubali biashara hiyo kwa sababu ya huduma nzuri. Na wewe Anza kutoa huduma nzuri Kama wao wanavyofanya. Iga kwao. Inashangaza kuona kwamba watu huoenda kuiga vibaya na kuacha sifa nzuri kama hizi. Sasa ebu wewe ziige hizi sifa.

    Muda siyo mrefu utaweza kuifikisha mbali sana hiyo biashara yako.

    Kama unaikubali biashara au kampuni hiyo kwa sababu ya bidhaa Bora, ebu na wewe anza kuzalisha bidhaa Bora.

    Kwa vyovyote vile. Endelea kusonga mbele. Utaweza kufanya makubwa zaidi pale utakapokuwa na mtu unayemwangalia na kujifunza masomo kwake. Ukajifunza na kufanyia kazi unachojifunza.

    Kila la kheri.

    Godius Rweyongeza
    Morogoro-Tz
    0755848391
    https://songambele.co.tz

  • KIPAJI NI DHAHABU: Jinsi Ya Kukigundua, Kukinoa Na Kutumia Kipaji Chako Kwa Manufaa

    Nakumbuka mwaka 2013 nilikutana na vijana wenzangu ambao walikuwa kwenye mjadala mkali kuhusiana na Messi, Ronaldo na Neymar. Kwenye mjadala huu walikuwa wakijadili kuhusiana na uwezo wa wachezaji hawa, huku wengine wakisema kwamba Messi na Neymar wana kipaji ila Ronaldo akiwa anatumia nguvu.

    Nadhani kama wewe ni mpenzi wa soka, mijadala kama hii utakuwa unaifahamu ambavyo huwa inatokea sana. Na jinsi ambavyo huwa inateka umakini wa watu.

    Kwenye mijadala kama hii watu huwa wanatoa hoja zao kwa nguvu kuonesha kwamba mchezaji fulani ni mzuri na ana kipaji kuliko mwingine.

    Mijadala mingine ya aina hii huwa ni mijadala ya wasanii, ambapo huwa wanalinganishwa wasanii wawili. Umewahi kushiriki mjadala kama huo?

    Hivi kwanza wewe mwenyewe unakijua kipaji chako?

    Mjadala kama huu ndio ulinifanya nitafakari na kujiuliza hivi mimi mwenyewe nina kipaji gani? Je, hawa wanaozungumzia kipaji cha Messi, Neymar na Ronaldo wanajua vipaji vyao? Ukiwauliza wewe una kipaji gani wanaweza kukujibu? Na tokea hapo nikaianza safari ya kujitafuta ili niweze kujua kipaji changu. Maswali kama kipaji ni nini? Hivi ni kweli kila mtu amezaliwa na kipaji au kuna baadhi ya watu wachache tu ambao wamebarikiwa ndio walizaliwa na kipaji? Kipaji ni kitu cha kuzaliwa nacho au unaweza kukipata ukubwani?

    Safari hiyo tu imenifunza mengi ambayo unaenda kukutana nayo kwenye ebook hii hapa ya kipekee.

    Kila Mtu Kazaliwa Na Kipaji Ila Hapaswi Kulinganishwa Na Mwingine

    Nakummbuka Albert Einstein aliwahi kunukuliwa akisema kwamba kila mtu ni gwiji, ila tatizo ni pale ambapo unamhukumu samaki kwa uwezo wake wa kupaa.

    Hapo ndipo nilipogundua kumbe mimi na wewe tuna vipaji, ila sasa kipaji changu hakiwezi kufananishwa wala kulinganishwa na wewe.

    Ni wazi kuwa kwa vyovyote vile samaki hawezi kuwa gwiji kwenye somo la kupanda mti, kupaa wala kukimbia. Yeye uwezo wake mkubwa upo kwenye kuogelea na huko lazima atafanya vizuri tu.

    Sasa hivyo hivyo kwa kipaji chako. Hakiwezi kulinganishwa na mtu mwingine, unacho wewe na ni kwa ajili yako tu. Hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kuwa na kipaji kama cha kwako.

    Mgawanyo Wa Kitabu

    Kwenye ebook hii hapa nimeeleza kipaji kwa kina hasa ili hata kama ebook hii anaisoma mtoto wa miaka sita aweze kunielewa kuhusiana na kipaji.

    Kwenye sura ya kwanza nimeanza kwa kueleza kwamba kipaji ni kitu gani? Ambapo nimeeleza dhana nzima ya kipaji na jinsi kinavyofanya kazi.

    Kwenye sura ya pili nimeeleza namna ambavyo unaweza kugundua kipaji chako. Je, unajiuliza ni kwa namna gani ambavyo unaweza kugundua hicho kipaji chako? Basi nenda moja kwa moja kwenye sura ya pili.

    Kwenye sura ya tatu nimeonesha mbinu unazoweza kutumia kwenye kunoa na kuendeleza kipaji chako. Hapa utakutana na mbinu za kukusaidia wewe kuweza kupeleka kipaji chako mbali. Na kwenye sura ya nne tutaona kwa nini watu hawathamini vipaji vyao.

    Kwenye sura ya tano tutaona mbinu zitakusaidia wewe kutengeneza fedha kwa kutumia kipaji chako.

    Tunaishi kwenye ulimwengu wa intaneti. Na hapa tutaingia kwenye sura ya sita ambapo tutaona namna ambavyo unaweza kupeleka kipaji chako kwenye mtandao na kunufaika na inatenti.

    Kwenye sura ya saba  tutaona kipaji na elimu. Kwa nini elimu inapewa kipaumbele zaidi kuliko kipaji na je, kuna ulazima wowote wa kuendeleza kipaji chako au ukomae tu na elimu?

    Uko tayari kwa ajili ya safari hii ya kipekee? Basi wacha tuianze kama ifuatavyo.

    Kupata YALIYOMO YA EBOOK HII BONYEZA HAPA

    Mafunzo haya yapo kwenye ebook ambayo unaweza kuipata kwa elfu 5 tu. kuipata ebook hakikisha kwamba lipie elfu 5 kwa  0684 408 755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA. ukishalipia utanitaarifu kwa namba hiyohiyo ili niweze kukutumia hiyo ebook.

    Kupata YALIYOMO YA EBOOK HII BONYEZA HAPA

  • Kipaji Ni Dhahabu: Jinsi Ya Kukigundua, Kukinoa Na Kutumia Kipaji Chako Kwa Manufaa

    Nakumbuka mwaka 2013 nilikutana na vijana wenzangu ambao walikuwa kwenye mjadala mkali kuhusiana na Messi, Ronaldo na Neymar. Kwenye mjadala huu walikuwa wakijadili kuhusiana na uwezo wa wachezaji hawa, huku wengine wakisema kwamba Messi na Neymar wana kipaji ila Ronaldo akiwa anatumia nguvu.

    Nadhani kama wewe ni mpenzi wa soka, mijadala kama hii utakuwa unaifahamu ambavyo huwa inatokea sana. Na jinsi ambavyo huwa inateka umakini wa watu.

    Kwenye mijadala kama hii watu huwa wanatoa hoja zao kwa nguvu kuonesha kwamba mchezaji fulani ni mzuri na ana kipaji kuliko mwingine.

    Mijadala mingine ya aina hii huwa ni mijadala ya wasanii, ambapo huwa wanalinganishwa wasanii wawili. Umewahi kushiriki mjadala kama huo?

    Hivi kwanza wewe mwenyewe unakijua kipaji chako?

    Mjadala kama huu ndio ulinifanya nitafakari na kujiuliza hivi mimi mwenyewe nina kipaji gani? Je, hawa wanaozungumzia kipaji cha Messi, Neymar na Ronaldo wanajua vipaji vyao? Ukiwauliza wewe una kipaji gani wanaweza kukujibu? Na tokea hapo nikaianza safari ya kujitafuta ili niweze kujua kipaji changu. Maswali kama kipaji ni nini? Hivi ni kweli kila mtu amezaliwa na kipaji au kuna baadhi ya watu wachache tu ambao wamebarikiwa ndio walizaliwa na kipaji? Kipaji ni kitu cha kuzaliwa nacho au unaweza kukipata ukubwani?

    Safari hiyo tu imenifunza mengi ambayo unaenda kukutana nayo kwenye ebook hii hapa ya kipekee.

    Kila Mtu Kazaliwa Na Kipaji Ila Hapaswi Kulinganishwa Na Mwingine

    Nakummbuka Albert Einstein aliwahi kunukuliwa akisema kwamba kila mtu ni gwiji, ila tatizo ni pale ambapo unamhukumu samaki kwa uwezo wake wa kupaa.

    Hapo ndipo nilipogundua kumbe mimi na wewe tuna vipaji, ila sasa kipaji changu hakiwezi kufananishwa wala kulinganishwa na wewe.

    Ni wazi kuwa kwa vyovyote vile samaki hawezi kuwa gwiji kwenye somo la kupanda mti, kupaa wala kukimbia. Yeye uwezo wake mkubwa upo kwenye kuogelea na huko lazima atafanya vizuri tu.

    Sasa hivyo hivyo kwa kipaji chako. Hakiwezi kulinganishwa na mtu mwingine, unacho wewe na ni kwa ajili yako tu. Hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kuwa na kipaji kama cha kwako.

    Mgawanyo Wa Kitabu

    Kwenye ebook hii hapa nimeeleza kipaji kwa kina hasa ili hata kama ebook hii anaisoma mtoto wa miaka sita aweze kunielewa kuhusiana na kipaji.

    Kwenye sura ya kwanza nimeanza kwa kueleza kwamba kipaji ni kitu gani? Ambapo nimeeleza dhana nzima ya kipaji na jinsi kinavyofanya kazi.

    Kwenye sura ya pili nimeeleza namna ambavyo unaweza kugundua kipaji chako. Je, unajiuliza ni kwa namna gani ambavyo unaweza kugundua hicho kipaji chako? Basi nenda moja kwa moja kwenye sura ya pili.

    Kwenye sura ya tatu nimeonesha mbinu unazoweza kutumia kwenye kunoa na kuendeleza kipaji chako. Hapa utakutana na mbinu za kukusaidia wewe kuweza kupeleka kipaji chako mbali. Na kwenye sura ya nne tutaona kwa nini watu hawathamini vipaji vyao.

    Kwenye sura ya tano tutaona mbinu zitakusaidia wewe kutengeneza fedha kwa kutumia kipaji chako.

    Tunaishi kwenye ulimwengu wa intaneti. Na hapa tutaingia kwenye sura ya sita ambapo tutaona namna ambavyo unaweza kupeleka kipaji chako kwenye mtandao na kunufaika na inatenti.

    Kwenye sura ya saba  tutaona kipaji na elimu. Kwa nini elimu inapewa kipaumbele zaidi kuliko kipaji na je, kuna ulazima wowote wa kuendeleza kipaji chako au ukomae tu na elimu?

    Uko tayari kwa ajili ya safari hii ya kipekee? Basi wacha tuianze kama ifuatavyo.

    Mafunzo haya yapo kwenye ebook ambayo unaweza kuipata kwa elfu 5 tu. kuipata ebook hakikisha kwamba lipie elfu 5 kwa  0684 408 755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA. ukishalipia utanitaarifu kwa namba hiyohiyo ili niweze kukutumia hiyo ebook.

    Kupata YALIYOMO YA EBOOK HII BONYEZA HAPA

  • Kitu Kimoja Muhimu Usichokijua Kuhusu Darasa Rasmi La Uandishi Mwaka 2022

    Kuanzia tarehe 16 machi, 2022 tutakuwa na darasa rasmi la uandishi. Darasa hili maalumu litahusisha watu wachache tu. Watu 10.

    Ukihudhuria darasa hili:

    👉Utaandika kitabu chako na kitakamilika ndani ya siku 30.

    👉 Nitakusimamia na kusoma kazi zako unazoandika kila siku na kukusaidia kuziboresha.

    👉 Nitakufungulia blogu ya bure.

    👉 Utajifunza mengi kutokana na yale wanayoandika wenzako na maoni nitakayokuwa natoa kuhusu kazi za wenzako.

    👉 Utapata kitabu Cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU NDANI YA SIKU 30 bure.

    👉 Utapata jarida lenye hatua 15 za kufuata ili kuandika magazetini.

    👉 Utapata mafunzo ya audio zaidi ya 10. Yakiwemo mahojiano na waandishi wakubwa hapa nchini.

    👉 Utaungana na waandishi wengine wanaoandika na kujifunza mengi kutoka kwao.

    Pamoja na hayo leo nataka nikwambie kitu kimoja tu usichokijua kuhusu darasa hili.

    Kitu hiki ni kwamba ukihudhuria darasa hili huna chochote cha kupoteza.

    Gharama ya kuhudhuria darasa hili la kipekee ni laki mbili (200,000/-)
    Ila huna chochote cha kupoteza

    Huna cha kupoteza.

    Wakati wa darasa au baada ya darasa kuisha, ukiona kwamba kile ulichopata hakiendani na thamani ya fedha uliyotoa. Utaniambia na mimi nitakurudishia fedha yako bila kukuuliza swali lolote.

    Yaani, sentensi hiyo ulivyoisoma ndivyo ilivyo leo na ndivyo itakuwa tarehe 17.Aprili siku moja baada ya kumaliza darasa letu.

    Huna chochote cha kupoteza.

    Unaweza kuuliza kama ni hivyo, sasa si bora watu wahudhurie bure tu kwenye hili darasa? Itakuwaje kama watu wote watadai fedha zao baada ya darasa.

    Ninachotaka ufahamu ni kwamba darasa hili ni la kipekee sana. Nina uhakika na kile unachoenda kujifunza. Nimealiandaa likaandalika, nimelipika likapikika. Kwa hiyo mtu yeyote ambaye atahudhuria darasa hili atapata thamani mara 10 zaidi ya atakavyolipia.

      Thamani ya darasa hili ni kubwa Sana. Ndio maana kwa uhakika kabisa nasema kwamba endapo mtu atakuwa hajaridhika  na hii thamani ambayo ni mara kumi zaidi basi nitamrejeshea fedha yake. Darasa limepikwa, likapikika!

    Kama kweli upo siriazi kujifunza kuhusu uandishi. Basi fanya hivi.
    JIUNGE na darasa hili leo hii.

    Nakuhakikishia kuwa huu unaenda kuwa uamuzi wako bora kuwahi kutokea.

    Fanya malipo sasa hivi kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA ili ujihakikishie nafasi yako.

    Wako,
    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

X