SIku ya leo (valentine) napenda nimtambulishe kwako….. (sijawahi kufanya utambulisho mkubwa kama huu, ila leo imebidi tu nifanye hivyo)


Kheri ya sikukuu ya wapendanao, rafiki yangu. Siku kama hii hujitokeza mara moja tu kwa mwaka, hivyo huna budi kuhakikishakwamba unafurahi na kuitumia kwako. Siku ya leo binafsi kuna mtu mmoja tu ambaye ningependa nimtambulishe kwako. na mtu huyu si mwingine bali ni wewe mwenyewe. Kwa nini ninafanya hivi? Ninafanya hivi kwa sababu katika dunia ya sasa unakuta kwamba inakuwa ni rahisi sana kufuatilia maisha ya watu wengine zaidi ya unavyofuatilia maisha yako. Hivyo unaweza kukuta kwamba unajua kiudani kwamba mtu fulani akifanya hiki, au akiepuka hiki lazima tu atafanikiwa maishani mwake. Lakini ukawa hujijui wewe mwenyewe. Yaani ukawa hujui ni kitu gani unapaswa kufanya au kuepuka ili uweze kuwa na maisha mazuri sana. Ndio maana siku ya leo nimeona waziwazi kwamba nikutambulishe wewe kwako wewe mweyewe.
Kama kuna upendo unapaswa kuwa nao basi ni upendo wa kujijua wewe mwenyewe. Jua wapi unatoka na wapi unaelekea maishani mwako. Ni zawadi ya kipekee ya upendo ambayo unaweza kujipa maishani mwako.
Kwa hiyo napenda kuanzia leo hii ujifuatilie wewe mwenyewe kuliko mtu mwingine. Najua wewe ulidhani nitambulisha mtu mwingine na ulitaka umjue. Lakini unaonaje ukijijua wewe kiundani kabla ya kumjua mtu mwingine.
Ujue unaweza  kukuta kwamba kila siku kunafuatilia maisha ya watu ya watu wengiine. Ila ukashidwa kujifuatilia wewe mwenyewe. Hivi kwa mfano nikikuuliza jana ulitumia kiasi gani unakumbuka?
Je, ulitumia muda gani mtandaoni? Je, ulitumia muda gani kusoma kitabu?
Je, ulitumia muda kiasi gani kuongea kwenye simu?
Uliingiza shilingi ngapi?
Je, baada ya hayo yote ambayo yametokea jana upo tayari kufanya marekebisho ili kuhakikisha kwamba unakuwa mtu bora zaidi siku ya leo zaidi ya ulivyokuwa siku ya jana?
Kama hujijui mwenyewe, sasa kwa nini uwekeze nguvu kwenye kuwajua watu wengine? Kwa hiyo kuanzia leo hakikisha kwamba unawekeza kwanza katika kujijua wewe mwenyewe zaidi ya unavyowafuatilai wengine na kuwajua watu wengine.
Ukiweza kujijua wewe mwenyewe unaweaza kuboresha maisha yako kutokana na kile ambacho unaona kwamba haufanyi vizuri sana. Nakutakia kila lakheri.
Unaweza kukuta kwamba mtu anamfahamu msanii fulani au mtu fulani maarufu zaidi ya anavyojifahamu yeye mweyewe. Sasa naomba kujua kama kweli wewe unajifahamu kweli au la!
Kwa kusema hayo rafiki yangu, naomba kwa leo niishiei hapo


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X