Home


  • Kitu Kimoja Ambacho Hakuna Mtu anaweza Kukifanya Kwa Niaba Yako

    Rafiki yangu mpendwa salaam. Naamini UNAENDELE VYEMA kabia ana majukumu yako ya kila siku,  siku ya leo nimekuja kwako kukwambia kitu kimoja tu rafiki yangu. Naam, kitu ambacho hakuna mtu anaweza kukifanya kwa niaba yako, Isipokuwa wewe tu ndiye unaweza kufanya hivi vitu.

    Naomba kwanza ufahamu umuhimu wa kuwapa wengine majukumu. Siyo kila jukumu unaweza kulifanya mwenyewe. Baadhi ya majukumu unapaswa kuyaacha na kuwapa wengine wayafanye ili uweze kuweka nguvu zako na muda wakokwenye majukumu machache ambayo unyaweza zaidi.

    Hata hivyo ifahamike kuwa siyo kila jukumu unaweza kuwapa wengine walifanye kwa niaba yako.

    Moja ya jukumu ambalo huwezi kuwapa wengine walifanye kwa niaba yako ni JUKUMU LA KUONGEZA THAMANI YAKO. Thamani yako ni muhimu sana na hasa kwenye ulimwengu wa leo ambao unabadilika na unakabiriwa na mabadiliko mengi ambayo yanazidi kutokea.

    Hivyo, jukumu la kuhakikisha thamani yako imeongezeka ni jukumu lako mwenyewe na wala hakuna mtu yeyote anayeweza kufanya hili jukumu kwa niaba yako.

    Ndiyo maana nimeandika kitabu kizima cha JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO, nikiwa nakuonesha hatua kwa hatua ni kwa namna gani unaweza kuongeza thamani binafsi.

    Kama ulikuwa hujui ni kwamba ukiongeza thamani yako, utaweza kukuza Uchumi wako binafsi pia.

    Kwenye ulimwengu wa leo wanaolipwa zaidi ni wale ambao wamekuza thamani yao kwa viwango vikubwa.

    Kumbe kwenye kazi au jukumu lolote ambalo unafanya. Hakikisha unapambania kitu kimoja muhimu sana rafiki yangu. Thamani yako.

    Kupata nakala ya kitabu cha JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO, wasiliana nami kwa 0755848391 sasa.

    Karibu sana

  • 📢 Audiobook: JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO 📢

    Unataka kuongeza thamani yako binafsi? Unatafuta njia ya kuwa bora zaidi kwenye kazi, biashara, na maisha kwa ujumla? Audiobook hii ni JIBU LAKO!

    “JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO” imejaa mbinu na siri za kuongeza thamani yako, kukuza uwezo wako, na kujenga heshima yako katika jamii na kazi yako.

    Ndani yake utajifunza:
    ✅ Namna ya kujiweka katika nafasi ya mafanikio
    ✅ Mbinu za kujiimarisha kiujuzi na kimaarifa
    ✅ Jinsi ya kujenga mtandao wenye nguvu wa watu sahihi
    ✅ Hatua za kuongeza kipato chako kwa kuongeza thamani yako binafsi

    Hii sio hadithi! Ni mwongozo wa hatua kwa hatua utakaokusaidia kujiboresha na kufikia viwango vya juu.

    SIKILIZA SASA!
    LIPIA 10,000/-, leo hii upate nakala Yako. Uko tayari kuwekeza katika thamani yako?

    📲 Lipia sasa kwa namba 0655848392 jina GODIUS RWEYONGEZA na utumiwe audiobook yako kupitia Telegram!

    Umejipanga kuongeza thamani yako? Hii ndio fursa yako! Usikubali ipite hivi hivi.

  • Haya hapa ni mambo 101 unayoweza kuandika kwenye kitabu chako

    Rafiki yangu mpendwa salaam. Hongera sana kwa siku hii nyingine ya leo. Leo ninataka nikwambie mambo 101 unayoweza kuandika kwenye kitabu chako.

    Ni ukweli usiopingika kwamba watu wengi wangependa kuandika vitabu vyao kwa wakati na kwa haraka. Hata hivyo wengi hawajuia hata wapi pa kuanzia. Kwenye somo la leo tunaenda kuona mambo 101 unayoweza kuandika kwenye kitabu chako. Ni mambo yapi hayo, fuatilia hili somo hapa

  • Kwa nini ni muhimu kuhakikisha unautumia ulimwengu wa mtandao kwa manufaa

    Kuna kipindi ilikuwa inaaminiwa kwamba mitandao ya kijamii na mtandao wa intaneti ni kwa ajili ya vijana, ila leo hii sote tunaona wazi kuwa mtandao wa intaneti siyo tu kwa ajili ya vijana. bali ni kwa ajili yetu sote. Kumbe mimi, wewe au mwingine yeyote anaweza kuutumia mtandao huu tena kwa manufaa makubwa.

    Sote leo hii tunaona wazi kuwa tunaweza kuutumia mtandao wa intaneti kufanya mambo tofauti tofauti.

    Kama bishara yako leo hii ipo mtandaoni, ni wazi kuwa kuna matokeo ambayo unapata. Kuna wateja ambao unawapata kutokana na biashara yako kuwa mtandaoni.

    Na kama biashara yako haiko mtandaoni, maana yake kuna wateja unawakosa kwa sababu tu ya biashara yako kutokuwa mtandaoni.

    Kitu kikubwa ambacho nataka nikusishi siku ya leo ni kwamba iweke biashara yako mtandaoni rafiki yangu. Tafuta namna ya kuhakikisha kwamba unaiweka biashara yako mtandaoni.

    Njia rahisi ya kuweka biashara yako mtandaoni.

    Ni moja kuhakikisha unakuwa blogu au tovuti.

    Pili ni kuhakikisha unakuwa na kurasa kwenye mitandao yote muhimu ya kijamii

    tatu ni kuhakikisha unakuwa unaweka maudhui ya mara kwa mara kwenye hii mitandao ya kijamii.

    Nne ni kuhakikisha unakuwa na mawasiliano ambayo wateja au watakaopenda kufuatilia kazi zako zaidi wanaweza kukupata. kwa kuanzia mawasiliano haya yawe ni barua pepe, namba ya simu ya kawida na ya whatsap.

    Tano USIPOE na WALA USIBOE.

    Fanyia kazi kwanza haya kwa leo. Uwe na siku njema sana.

    Nakutakia kila la kheri rafiki yangu wa ukweli.

    Uwe na si

  • Nukuu 10 Za Kufikirisha

    1.

    2.

    3.

    4.

    5.

    6.

    7.

    8.

    10.

  • Muda Sahihi ni…

    1. Muda mzuri wa kupanda mti ulikuwa Miaka 20 iliyopita, muda mwingine mzuri zaidi ni Sasa.
    2. Ukianza Leo utaanza kuona matokeo siku Moja kabla kuliko pale ambapo ungeanza kesho.ttps://youtu.be/SOiq8Ui_aWQ

    Chukua hatua sasa

    Ungependa kuanza kuandika kitabu chako👇🏿

    https://chat.whatsapp.com/G9kNW2SIIoR6DL8s8GuyRe

  • Nukuu 13 Za Kufikirisha:

    1:

    2:

    3:

    4.

    5.

    6.

    7.

    8.

    9.

    10.

    11.

    12.

    13.

  • Nukuu Za Kufikirisha:

    1:

    2:

    4:

    5.

    6:

    7:

    8:

    9:

    10:

    11:

    12:

    13:

    14:

    15:

    16:

    17:

  • Jinsi Ya Kupanga Kitabu Chako Kwenye Simu

    Umeandika kitabu chako kwenye simu na ungependa kukipanga kwa haraka ili kujua kina kurasa ngapi? Karibu sana kwenye video ya leo ambayo ninaenda kukueleza namna ya kufanya hivyo pamoja na mengine zaidi.

    Bonyeza hapa kuitazama

    Rafiki yangu kuna mafunzo mengi zaidi ambayo huwa natoa kwenye audio na mafunzo haya unaweza kuyafuatilia zaidi kwenye youtube hapa.

  • Mambo muhimu ya kuzingatia kuhusu vyanzo vingi vya kipato

    Rafiki yangu mpendwa salaam, leo nataka nikwambie mambo machache kuhusu vyanzo vingi vya kipato

    Kwanza hakikisha kwamba unakuwa na chanzo zaidi ya kimoja cha kipato. kwa vyovyote vile, usikae na chanzo kimoja tu cha kipato, mara nyingi chanzo kimoja cha kipato kikipata changamoto basi huwa unakuta kwamba watu wengi wanakutana na changamoto za kipato. Hivyo., rafiki yangu, kazi yako kubwa ambayo uanapaswa kuifanya kuanzia leo hii. Ni wewe kujiondoa kwenye lindi la kutengenea chanzo kimoja cha kipato. Badala yake kuwa na vyanzo vingi vya kipato

    Mbili, kama una chanzo kimoja cha kipato. Pigana uwe navyo viwili. kama unavyo viwili, pambana uwe navyo vitatu, kama unavyo vitatu walau kuwa navyo vinne. Kiwango cha vyanzo vinne na kuendelea ni kiwango cha kuanzia walau. baada ya hapo unaweza kuendelea mbele zaidi lakini walau hakikisha unakuw na vyanzo vinne vya kipato.

    Tatu, anza kulifanyia kazi hio sasa hivi rafiki yangu.

X