Home


  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

     

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Anza tu

    Wewe anza, kisha endelea mbele. wanaokubeza leo, wanaoona kwamba huwezi leo, kuna siku watakushangilia huku wakisema kwamba nilijua tu mwamba lazima atafanikiwa

    ✅

  • Njia Bora Na Ya Uhakika Ya Kunufaika Elimu Na Elimu Yako Ya Chuo

    Kumekuwa na wimbi kubwa la vijana ambao wanahitimu chuo huku wakiwa bado wakiwa hawana mwelekeo. na ambacho kimekuwa kinatokea ni kwamba hawa vijana ambao wamesoma  chuo na kufaulu vizuri, baadaye wanaingia mtaani, wanakutana na maisha ya huku kitaani, yanawapiga, wanaishia kufanya kazi ambazo hata wao wenyewe walikuwa hawapendi.

    SIKU YA LEO nipo hapa kukuonesha namna unavyoweza kunufaika na elimu yako ya chuoni.

    KAMA BADO UKO CHUONI: Fuatilia masomo yako vizuri. Hudhuria masomo yale ambayo ni ya lazima uwepo na usipokuwepo hutaweza kuelewa vizuri.

    Usipoelewa uliza.

    Kama kuna mazoezi yakufanya yafanye.

    Halafu angalia kati ya hayo yote unayojifunza, ni kitu gani ambacho unapenda zaidi. Ukifuatilia kozi zako vizuri kuanzia mwaka wa kwanza mpaka unapomaliza mwaka wa tatu, wa nne au wa tano. Utagundua kwamba kuna kozi moja au mbili ambazo unazipenda zaidi na unaweza kuzitumia kwenye maisha yako ya kila siku.

    Amua kuzichagua hizi kozi na kuzitumia kwenye maisha yako ya kila siku. Angalia ni kwa namna gani unaweza kupata pesa kutokana na hizo kozi ambazo umejifunza.

    Angalia ni mambo gani ambayo watu wana uhitaji nayo na namna ambavyo wewe unaweza kutatua hayo mahitaji. Kisha tatua hizo changamoto kwa kuwaletea suluhisho.

    Kwa namna hiyo, utajikuta kwamba unawasaidia watu huku wewe mwenyewe ukiwa unazidi kufnaya kitu unachopenda na unapata pesa.

    KAMA UMESHAHITIMU: Najua unaijua hiyo kozi ambayo uliilewa sna, kozi ambayo ulikuwa unaipensa sana wakati ukiwa chuoni.

    Hiyo kozi moja ambayo leo hii, hata ukiamshwa tu usingizini unaweza kuileza hata kwa bibi yako akakuelewa vyema kabisa.

    ANZA kuangalia ni kwa namna gani ambavyo hii kozi sasa unaweza kuileta kwenye uhalisia wa maisha yako ya kila siku. Anza kuangalia ni kwa namna gani unaweza kuifanyia kazi hiyo kozi na watu wakawa tayari kutoa pesa zao mfukoni na kukulipa.

    Kisha fanyia kazi kile utakachokuwa umepata.

    Ukweli ni kuwa kwa fikra hizi sitegemi kwamba baada ya hapa uendelee tu kukaa nyumbani ukiwa unasema kwamba hauna kitu cha kufanya.

    BADALA yake unapaswa kuanza kupambania lengo lako kubwa na ndoto zako kubwa za sasa hivi ambazo ni kuwasaidia kupiti kile unachojua.

    Nimeandika kitabu kizuri sana, kinaitwa, TENGENEZA FEDHA KWA KUUZA KILE UNACHOJUA. Ni moja ya kitabu bora sana kabisa ambacho kila mwanachuo anapaswa kuhakikisha kwamba amesoma. Kimeeleza kwa undani kuhusu dhana nzima ya kutumia unachojua (ujuzi, maarifa, konekisheni, au chochote unachojua).

    Kupata nakala ya kitabu hiki ni rahisi sana.

    Wasiliana nasi kwa +255 684 408 755 sasa ili uweze kupata nakala yako. Utaletewa popote pale ulipo duniani.

    SOMA ZAIDI:

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu.

    Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea.

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Utajiri ni asili ya mwanadamu yeyote. Ni kitu muhimu kwake kuwa nacho

  • Unakwepa Hatari Zipi?

    Moja ya kitu ambacho huwa kinawakwamisha walio wengi ni kuogopa hatari. Wengi wanaogopa kuchukua hatua katika baadhi ya vitu kwa kuogopa hatari ambazo zinaweza kuwatokea kwenye maisha yao ya kila siku.

    Huwa napenda kuwaambia watu kuwa hatari kwenye maisha tunatembea nazo kila sehemu. Hatari tunazo kila wakati na hatari ni kama sehemu ya maisha yetu.

    Kutembea tu hatari.

    Kuongea na watu ni hatari.

    Na hata kulala ni hatari.

    Hakuna sehemu ambayo haina hatari.

    Linapokuja suala zima la hatari, watu wengi huwa wanakwepa hatari na hasa kwenye uwekezaji. Mtu anaogopa kuwekeza kwa sababu anaogopa, atapoteza

    Ila ninachoweza kukwambia siku ya leo ni kwamba, chagua kwa usahihi. Pata elimu sahihi ya uwekezaji, kisha wekeza kwa nguvu zako zako zote.

    rafiki yangu, kwenye maisha, hatari zipo kila sehemu. Hivyo, usiogope hatari. maana unaweza kukutana nazo popote utakapokuwa.

    SOMA ZAIDI:

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Misingi Sahihi Ya Kujenga Urafiki Kwenye Biashara

    Uache urafiki ubaki kwa ajili ya urafiki na wewe

    1.  Fanya kazi na watu wanaojua kufanya kazi
    2. Fanya biashara na watu wanaojua misingi ya biashara na amba watakukwa tayari kuisimamia mara zote.

    Kwenye biashara, urafiki mzuri ni ule unaotengenezwa na biasahara. Ila siyo mtu mlikuwa rafiki halafu eti mnaanzisha biashara, mara nyingi mtajikuta mnaweka urafiki kwenye biashara na hivyo kuharibu biashara

     

    Hivyo kama unafikiri kuanzisha biashara, kwa kiwango kikubwa utakuta kwamba rafiki yako wa sasa hivi anaweza asiwe mtu ambaye atakufaa sana kwenye biashara. 

    Najua utakuwa umesikia stori nyingi sana za watu walioanzisha biashara na marafiki zao.

    Ila wengi ukifuatilia, urafiki ulikuwa umejengwa kwenye misingi ya biashara.

    Siyo wewe unaanzisha biashara na rafiki yako ambaye msingi mkubwa wa urafiki wenu mmeujenga kwenye kubeti, kushangilia mpira, kuangalia movie na vitu kama hivyo.

    Baadaye unafika wakati ambapo mnapata pesa kidogo tu, kila mmoja anafikiri juu ya kupata pesa asepe.

    Angalia urafiki wa watu maarufu kama Steve Jobs na mweza Stephen Wozniak, hawa watu walikuwa marafiki, ila urafiki wao ulikuwa umeunganishwa kwenye ubunifu. Wote walikuwa wanapenda ubunifu na kubuni vifaa kama kompyuta, na ndiyo maana waliweza kufanya makubwa kwa pamoja.

    Au chukulia mfano wa urafiki kama Bill Gates na Allen Paul, hawa pia urafiki wao ulikuwa umejengwa kwenye kupenda kompyuta na ubunifu.

    Urafiki mzuri ni ule ambao utatokana na kazi, au biashara

    Kama urafiki wa Bill Gates na Warren Buffet au urafiki wa 

    kWA KUMALIZIA: Leo ningependa tu kukwambia kwamba urafiki wako wa kweli ujengwe kwenye misingi ya biashara, ila siyo urafiki ambao utabomoa biashara.

    SOMA ZAIDI:

  • Mtu Pekee Atakayekusaidia Kufanikisha Makubwa, Cha Kushangaza Ni Kwamba Humtumii. Mfahamu Sasa

    Ngoja nikwmabie kitu rafiki yangu.

    Kuna vitu ambavyo unapaswa kufanya mwenyewe. Siku za nyuma nimewahi kuandika hapa kwamba hakuna mtu anayeweza kupiga pushup kwa ajili yako.

    Makala hiyo bado ina nguvu kubwa sana kama ambavyo niliiandika miaka hiyo. Kama ulivyo ukweli usiopingika kuwa hakuna mtu anayeweza kupiga pushup kwa ajili yako. Hivyohivyo ni ukweli usiopingika kuwa kuna vitu ambavyo hata ukiwa na watu bora kuliko wote duniani hawawezi kuvifanya kwa niaba yako.

    • Hakuna Daktari ambaye atakufanya wewe kuwa mwenye afya bora
    • Hakuna mtalaamu yeyote atakufanya uwe na mwili wa kawaida
    • Hakuna mwalimu ambaye atakufanya wewe kuwa mwenye akili
    • hakuna Guru yeyote ambate atakufanya uwe na utulivu
    • Hakuna mshauri yeyote atakayekufanya uwe tajirii

    Mtu pekee anayeweza kukupa hayo yote ni wewe mwenyewe.

    Ni wewe mwenyewe ambaye unapaswa kubeba hayo majukumu yako bila ya kurudi nyuma. Lakini kama utasubiri watu wakufanyie kazi, nakuhakikishia kwamba utasubiri sana.

    SOMA ZAIDI: 

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Kama una Simu Janja na huingizi Kipato, Unakosea hapa. Rekebisha Mara moja

    Siku Moja Robert Kiyosaki alisema kwamba kama una simu janja na Bado wewe ni maskini, basi fahamu wazi kuwa Kuna sehemu unakosea.

    Ukitafakari maneno ya Robert Kiyosaki unagudua Kuna ukweli mkubwa sana hasa katika ulimwengu wa Leo ambapo unaweza kufanya makubwa Kwa dhana ambazo zinetuzunguka.

    Kwa mfano ukiangalia

    🌐 ChatGPT inapatikana bure

    🔍 Google ni Bure pia

    ▶️ YouTube ipo bure

    🎨 Canva unaweza kuipata burr

    🎙 Unaweza kusikiliza au kufanya Podcasts bure

    📚 Mtandaoni Kuna kozi kibao ambazo Nazo zinapatokana bure. 

     

    Kitu pekee unachohitaji ni intaneti Ili uweze kuvitumia hivi vitu Kwa manufaa, na Cha kushangaza zaidi ni kwamba tayari intaneti unayo, kama umeweza KUSOMA ujumbe huu maana yake intaneti unayo. 

     

    Kitu pekee unachohitaji ni nidhamu ya kuamua na kuanza kufanya mara Moja

     

    Sijui umenielewa hapo.

     

    Acha visibgizio kuanzia Leo hii na Anza kuzalisha matokeo.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza 

    Jifunze zaidi Kutoka Kwa GODIUS RWEYONGEZA Kwa kujiunga naye hapa

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Madebe tupu huvuma

    Leo kuna kauli mbili muhimu sana ambazo nataka tuzijadili kwa ufupi tu.

    Kauli ya kwanza ni kauli ya wahenga watu wanaosema kwamba, madebe tupu huvuma.

    Na kauli ya pili ni kauli inayosema kwamba, an idle mind is a devil’s workshop. ikiwa na maana kuwa akili tupu ni karakakana ya shetani.

    hizi kauli zote mbili zinatusisitiza mimi na wewe kitu kimoja kikubwa sana. Na kitu hiki ni kufanya kazi.

    Tunaishi katika dunia ambayo vijana na watu wengi hawapendi kufanya kazi. LAKINI WANAPENDA PESA.

    Wanapenda kulipwa sana, LAKINI HAWAPENDI KUTOA THAMANI KUBWA.

    Cha kushangaza zaidi ni kwamba baadhi ya vijana unaweza kukuta kwamba wapo vijiweni wamekaa, wakiwa hawafanyi jambo lolote la maana la kuwaongezea aidha wao thamani au kuwaongezea kipato, lakini bado wanadharau kazi.

    Ifike hatua ambapo wewe rafiki yangu, utapangilia ratiba yako na kuwa bize muda wote. Kuwa na fikra za kuchapa kazi mara zote.

    ili uwe unachapa kazi mara zote, hakikisha mara zote unapangilia ratiba yako. Ratiba yako ndiyo njia pekee ya wewe kupata chochote kile unachotaka kwenye maisha yako.

    Kamwe rafiki yangu usikubali kuwa debe tupu! Na kamwe usikubali kuwa karakana ya shetani. Lengo la makala hii isiyo kukuhubiria, bali ni kukupa ukweli ambao utaufanyia kazi.

    Ukweli ni kuwa kelele nyingi unazosikia kwenye maisha yetu ya kila siku. Iwe ni kwenye mitandao ya kijamii, kwenye vyombo vya habari au sehemu yoyote ile ni kutoka kwa watu ambao hawana kitu cha kufanya. Yaani, madebe tupu.

    Kama kila mtu akiwa bize kuanzia leo hii. Tutaifanya hii dunia kuwa bora zaidi kuliko ilivyo sasa hivi.

    Na njia bora ya dunia hii kuwa bora zaidi ni kwa mimi na wewe kuanza kutimiza wajibu wetu.

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Jinsi ya kuwakomesha watu wanaokukatisha tamaa kistaraabu kabisa (Ila Utakuwa Umewakomesha)

    Ngoja nikwambie kitu rafiki yangu. Kama hujawahi kukutana na watu ambao wanakukatisha tamaa, inawezekana hujawahi kuthubutu kufanya kitu cha tofauti na vile vilivyozoeleka kwenye jamii au hufikirii kwa ukubwa kabisa. Ni hivyo tu.

    Ila kama unafanya vitu vya tofauti, ni wazi kuwa watu wataanza kukukatisha tamaa kwenye kile unachofanya.

    Inawezekana watu wakakukatisha tamaa moja kwa moja kwa kauli zao. Mfano ni Kauli Hizi Tatu (03) za Kukatisha Tamaa ambazo nimezieleza kwenye hii makala, na ubora ni kwamba nimekueleza namna ya kuziepuka pia

    Lakini habari njema ni kwamba, njia nyingine ya kuwanyamazisha watu wanaokukatisha tamaa, ni kwa wewe kufanyia kazi kile unachotaka kufanyia kazi bila ya kuacha, haurudi nyuma na wala hukwamishwi na kitu chochote.

    Maneno yao yanakuwa  kama moto wa kuchochoea zaidi kile unachofanya. Hivyo, kitendo cha wewe kusikia kile wanachosema, unaamua kuongeza juhudi zaidil ili uweze kupata matokeo ambayo ni bora zaidi.

    Hawa wanaokukatisha tamaa, wewe unapaswa kuwashangaza kwa kuwaonesha kwa vitendo kwamba umeweza kufanya na hicho kitu kimekuja kwenye uhalisia.

    Kamwe rafiki yangu, usikubali kukata tamaa wala kurudi nyuma. MARA ZOTE SONGA MBELE

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Sahau Yote Kwenye Pesa Na Fedha Zako Ila Usisahau Haya Matano (05) Tu

    Kwenye fedha mengi ambayo unapasawa kuzingatia na kuhakikisha kwamba umeyafuata, wakati vyote vikiwa ni vya muhimu ila kuna kitu kimoja ambacho kamwe haupaswi kusahau hata siku moja.

    Na kitu hiki ni kwamba kamwei haupaswi kutumia pesa zaidi ya kipato chako

    pili haupaswi kuacha kuweka akiba

    tatu, hakikisha kwamba mara zote unawekeza na kuifanya fedha ikufanyie kazi hata kama umelala

    Nne, hakikisha kwamba mara zote unaongeza kipato chako. Kipato chako cha mwaka jana kisiwe sawa na kipato cha mwaka huu. Mwaka huu hakikisha kwamba unapambana kuhakikisha kwamba unaongeza kipato chako zaidi.

    Tano, hakikisha kwamba watu hawajui, kamwe ni lini huwa unaingiza fedha au ni lini hauna fedha. Maisha yako yawe yaleyale ukiwa na fedha, na hata ukiwa hauna fedha.

    Maisha yako kila mara yawe yaleyale.

    Hayo ndiyo mambo matano ambayo kamwe haupaswi kusahau linapokuja suala zima la pesa. Yazingatie, utanishukuru maisha yako. Hata hivyo ninavyohitimisha makala ya leo, ningependa tu kukwambia maneno ya Warren Buffet anayesema kwamba, usipoteze fedha zako na kamwe usisahau hiyo sheria hata siku moja.

    SOMA ZAIDI:

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

X