Kuwa Mkarimu


Habari za leo rafiki na ndugu msomaji wa SONGA MBELE BLOG . Imani yangu unaendelea vyema katika hatua ya kutafuta na kuelekea mafanikio.Karibu sana katika makala yetu ya leo ambapo tunaenda kujifunza kitu kipya ambacho kitabadili mwelekeo wa maisha yetu

Mara nyingi huwa watu wanaamini kwamba mtu unapaswa kuishi maisha kiasi kwamba ukifa utokee kwenye ukurasa wa mbele wa  magazeti .
Lakini je hii ni kweli? Shida sio kutokea mbele ya gazeti lakini je ulipotokea mbele ya gazeti, gazeti lenyewe limeandika nini juu yako.Kuna watu wametokea mara nyingi sana mbele ya magazeti wakiwa wameandikwa maneno tofauti. Chukulia mtu katokea mbele ya gazeti na gazeti kenyewe limeandika,
MUUZA MADWA YA KULEVYA AFARIKI DUNIA au
JAMBAZI AUAWA NA POLISI DAR.

Je kwa hali hii kuna haja ya kuishi maisha kiasi kwamba ukifa utokee mbele ya gazeti?

Simaanishi kwamba kutokea mbele ya gazeti ni kitu kubaya kwa sababu wapo watu wengi sana  wametokea mbele ya magazeti wakiwa  wamefanya mambomazuri sana, siwezi kuwataja wote katika makala hii maana ni wengi sana, ila kitu cha msingi ninachopenda kusisitiza ni kwamba tuishi maisha kama alivyoyataja Aldous Huxley kwenye kitanda chake alipokuwa anakarbia kufariki alisema

“Tuwe wakalimu kwa kila mtu”

Maisha mazuri ni yale ambayo unaishi kwa adabu na ukarimu. Unaishi vizuri kwa kila mtu, na kila sehemu unapokutana na mtu.

Kiukweli kama utaishi maisha ya kuwafanya watu wenye furaha hata kama utamfanya mtu mmoja mwenye furaha kwa siku basi utakuwa unastahili tuzo.

Robert sharma anasema

“ulipozaliwa ulilia wakati dunia wakati dunia ilishangilia, ishi maisha kiasi kwamba ukifa watu walie wakati wewe ukishangilia”

 Endelea kusoma makala za kuelimisha kutoka kwenye blogu hii


Ili upate makala maalumu kutoka songambele blogu BONYEZA HAPA ILI KUJIUNGA
Ni mimi rafiki na ndugu yako
Godius Rweyongeza
Tuwasiliane
godiusrweyongeza1@gmail.com
Asante

BONYEZA HAPA KUPATA KITABU CHA BIASHARA NDANI YA AJIRA

Kujiunga kundi la wasapu la SONGA MBELE BONYEZA HAPA

BIDEISM BLOG


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X