Wewe Ni Nani Kuacha?


Ukiona unafanya kitu ila haukifanyi kwa namna ya kueleweka. Ukiona unafanya kitu  ila ukahisi kama bado unakosa kitu fulani hivi, basi hapo unapaswa kujua kwamba hauna maarifa ya kutosha.

Usikimbie kitu hicho kwa sababu hujaweza kukifanya vizuri. Badala yake kimbilia kutafuta maarifa zaidi na zaidi ili uweze kukifanya kwa ubora.

Moja kati ya watu wa namna hii walikuwa ni Thomas Edison. Katika kazi kushindwa kwake mara elfu kumi hakuacha. Bali kila mara alitafuta maarifa mapya ambayo hakuwa nayo ili aweze kufanya kitu kwa ubora zaidi.

Sasa kabla ya wewe kuacha jiulize mimi ni nani kuacha? Badala yake kaa kwenye meza na jifunze kisha endelea kufanya ili uweze kufanya kwa ubora zaidi.

Asante sana,
Tukutane kwenye jukwaa la wanamfanikio

Ndimi,
Godius Rweyongeza
0755848391

KUPATA KITABU CHA KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI BONYEZA HAPA


HUDUMA NYINGINE UNAZOWEZA KUPATA KWANGU HIZI HAPA

KUPATA MAKALA MAALUM KWA WATU MAALUM KILA WIKI BONYEZA HAPA


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X