Hii Ndiyo Sehemu Ambayo Unaopaswa kuilenga Siku Zote Ili Uweze Kufika Kwenye Kilele Cha Mafanikio


Kila umayemwona yuko juu kuna siku alikuwa chini. Kila jogoo anayewika  kuna siku pia alikuwa kifaranga.
Suala hili linatupa mwelekeo mzuri kabisa wa kujua kwamba tunaweza kuwa tunayotaka kama tutaamua  kuwa hivyo.

Lakini ili uweze kufikia kwenye kilele chochote kile mfano cha mlima lazima utokee chini. Na Unapaswa kupanda kuelekea juu. Unapokuwa umefika huko ndipo unapongezwa kama mshindi.

Na ili uweze kufikia juu kabisa kwenye kilele cha Mafanikio makubwa basi kitu kikubwa unachopaswa kuwa nacho ni ndoto yako kubwa. Ndoto kubwa ya kufikia huko. Sio kwamba vitu vingine vinatokea kwa ajali, bali vinatokea kwa sababu maalumu sana. Na hizi sababu zipo kwenye ndoto ya mtu. Ndoto ya kuona mbali.

Katika maisha unapaswa kuona mbali hamna jinsi.  Kuona mbali sio kwa macho tu, lakini kwa fikra. Ndio maana tunaaswa kwa kuambiwa kwamba tunapaswa kulenga  kulifikia jua, kiasi kwamba tukilikosa jua basi hata walau tuweze kuufikia mwezi

Ndimi,
Godius Rweyongeza
0755848391

KUPATA KITABU CHA KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI BONYEZA HAPA


HUDUMA NYINGINE UNAZOWEZA KUPATA KWANGU HIZI HAPA
KUPATA MAKALA MAALUM KWA WATU MAALUM KILA WIKI BONYEZA HAPA


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X