Habari Njema Sana Kwa Wapenzi Wa Kusoma Vitabu


Habari ya muda huu rafiki yangu. Kama ulikuwa hujui basi leo naomba nikupe habari njema.

Kuna idadi kubwa ya watu ambao huwa wananiomba vitabu mbalimbali vya kusoma mara kwa mara.
Ambacho huwa nafanya mtu akiniomba vitabu ninamtumia. Kwa hali ilivyo unaweza kukuta siku moja unatumia watu 3-5 na idadi hii inajirudia kwa nyakati tofauti na unakuta kila mtu anahitaji vitabu  tofauti na vile ulivyotuma kwa mwingine.

Sasa nimeona nirahisishe maisha kwa kuwawekea vitabu hivi sehemu ambapo mtaweza kuvipata. Lakini pia nimeona niweke vitabu ambapo kila mtu anaweza kuomba huko. Na kila mtu anaweza kutuma au kutumiwa vitabu huko.

Kitu kingine ni kwamba hapa nilipoweka vitabu, nitakuwa silazimiki kuvituma mara mara kwa watu tofauti. Nikituma mara moja tu, ndio nitakuwa nimetuma. Mtu anaweza kuvipakua na kuvisoma baadae mwingine anaweza kupakua na kusoma. Lakini nitakuwa navituma mara moja tu na maelfu ya watu wanapata kuvipakua na kusoma.

Na vitabu hivyo vitakuwa vinawekwa hapa kwa ajili ya kila mtu mwenye uhitaji. Jiunge ili upate vitabu hivyo. Lakini pia washirikishe wengine juu ya habari hii njema.

JIUNGE HAPA

👉ukiwa humu utaruhusiwa kuomba vitabu.

👉utaruhusiwa kutuma vitabu ulivyosoma na kuona ni vizuri wengine wasome.

👉utaruhusiwa kutuma kitabu ambacho utaona kinafaa kisomwe na wengine.

👉HAUTARUHUSIWA kutuma tangazo, link, makala, video au audio yoyote ambayo SI kitabu. UKIFANYA hivyo utaondolewa kwenye kundi mara moja.

Wewe ingia kwa ajili ya vitabu tu. Ukiona huwezi kukaa pakua vitabu unavyopenda kisha uondoke upaache pakiwa salama.

JIUNGE HAPA

Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
Unaweza kuwasiliana naye kwa namba hii hapa 0755848391


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X