AKILI NENE vs MWILI MNENE


Kuna kitu ambacho  watu wamekuwa wanakiona kama sifa. Na pengine kama ishara ya kuwa ya pesa. Kitu hiki ni mtu kunenepa. Kwa hiyo watu wanawekeza pesa kwenye kunenepa mwili ila wanasahau kitu muhimu zaidi ambacho kinapaswa kunenepa kwa mtu sio mwili. ila akili. Yaani hata iweje, fanya ufanyavyo ila hakikisha kwamba kila siku unanenepesha akili yako kwanza, kisha unakuja kunenepesha vitu vingine.

Hivi kwa mfano tungekuwa tupo kwenye jamii ambapo kila mtu amenenepa akili unadhani jamii hii ingekuwaje! Bila shaka tungekuwa na magwiji, wabunifu, watu wanaothubutu na watu wanaochukua hatua za tofauti.

Sasa je, tukibadilika sasa hivi si inawezekana? Ndio ni kweli inawezekana.

Basi, kuanzia leo wewe hapo anza kuweka mpango wa kunenepesha akili yako kwanza kabla hujafiria kunenepesha kitu kitu kingine.

Ninachofahamu kwamba
AKILI NENE=HATUA NENE=MATOKEO MANENE😊.

2020 ni mwaka wa kunenepesha akili.

2020 ni mwaka kuwa na akili kubwa.

kumbuka AKILI NENE=HATUA NENE=MATOKEO MANENE. Iila sasa hapa kuna kitu cha ziada nataka niongeze kwenye mlinganyo wetu.

kitu hiki ni kwamba.
VITABU SAHIHI=AKILI NENE=HATUA NENE=MATOKEO MANENE.

Umeona ee! Vitabu sahihi huleta akili nene, akili nene husababisha tuchukue hatua kubwa, hatua kubwa huleta matokeo makubwa.

Soma zaidi: Hili ni Jambo Linalowafanya Watu Washindwe Maishani


2 responses to “AKILI NENE vs MWILI MNENE”

  1. Nimependa mafundisho yenu zaidi ya formula hii
    VITABU SAHIHI = akili nene =Hatua nene = matokeo makubwa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X