Kinachokukwamisha Ni Uoga


Ujue kuna watu ambao wewe unawazidi kwa kipaji cha kuimba ila wanazunguka dunia nzima wanaimba.

Kuna watu  ambao wewe unawazidi kwa viwango vya kucheza mpira, ila leo hii watu wanakaa kwenye runinga kuwatazama dakika 90.

Wengine wewe unawazidi viwango vya kuchekesha, ila leo hii watu wanaingia YouTube kuwatazama ili wacheke na wewe upo hapo umejificha.

Kuna watu wana viwango vya kawaida sana vya uongozi, ila leo hii wanazunguka dunia kama viongozi na kushangiliwa. Na wewe mwenye viwango vikubwa vya uongozi upo hapo!

Kuna watu hawajui kuchambua mpira kama wewe hapo! Ila leo hii wakichambua tu, hata kama wanasema vitu vya kawaida wanasikilizwa sana. Wewe mwenye uwezo mkubwa upo hapo!

Kuna watu uwezo wa kuandika vitabu ni mdogo sana, ila leo hii vitabu vyao vinasomwa kila kona ya dunia.

Yaani wewe kinachokukwamisha ni uoga. Kwenye kitabu cha KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI ukurasa wa 87 nimezungumzia vitu ambavyo vinazuia watu kufikia mafanikio yao.  Moja ya kikwazo hiki ni UOGA.

Ebu fungua ukurasa huu hapa uone uoga unavyokukwamisha.

Kama hauna kitabu tuwasiliane kwa namba 0755848391 ili wewe upate kitabu hiki uanze kutengeneza kesho bora sasa hivi.

Gharama ya kitabu ni 10,00/- tu.
na utakipata popote pale ulipo tanzania.

pia nafasi za kuwa wakala wa kitabu hiki mkoani kwako ziko wazi. Niandikie ujumbe kwa 0755848391 ili nikupe utaratibu. Karibu sana


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X