Shukrani Zangu Na Taarifa Rasmi Ya Upatikanaji Wa Kitabu Cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni


Jana tarehe 02.02.2020 ilikuwa ndio siku rasmi ya uzinduzi wa kitabu cha kutoka sifuri mpaka kileleni. Kitabu hiki ambacho kwa sasa kinapatikana katika mfumo wa nakala ngumu (hard copy) kilizinduliwa jana kwenye ukumbi wa Morogoro Hotel hapa Morogoro.
Kwanza kabisa nichukue nafasi hii kuwapongeza sana watu waliohudhuria huu uzinduzi wa kipekee sana. Kiukweli nimefurahi sana kuwa nanyi na kujumuika nanyi kwenye hiyo siku ya kipekee sana, jana. Tarehe 02.02.2020 itabaki kuwa ni historia  kuwa kitabu hiki kilizinduliwa. na watu wote waliokuwepo walichukua nakala zao.


Siku ya leo nimekuja na taarifa kwako wewe ambaye hukuweza kupata nafasi ya kuhudhuria uzinduzi huu wa kitabu.  Taarifa hii ni kwamba kitabu hiki sasa hivi kipo sokoni na unaweza kukipata popote pale ulipo Tanzania. Nakala moja ya kitabu hiki hapa inapatikana kwa shilingi 10,000 tu. na wewe hapo unaweza kuipata popote pale ulipo katika hii nchi.
Kikubwa ni kwamba utaniambia uko wapi na mimi nitakupa utaratibu. Unaweza kuwasiliana na namba hii 0755848391 sasa hivi ili utaratibu wa kukuletea kitabu hiki hapa ufanyike.
Mwaka huu ni mwaka wako wa mafanikio makubwa, hivyo jipange kuhakikisha kwamba kweli unafanyia kazi kile ambacho umeamua kufanya. Kitabu hiki hapa kitaweza kukufikisha kwenya malengo yako makubwa uliyojiwekea.
Kumbuka kwamba gharama ya kitabu hiki hapa ni elfu 10,000/- ila kama utakuwa mkoani utaongeza 5,000/- ikiwa ni pamoja na gharama ya kutuma. Namba ya kufanya malipo ni 0755848391 karibu sana

SOMA ZAIDI: KITABU; kutoka sifuri mpaka kileleni

Ni mimi anayejali mafanikio yako,
Godius Rweyongeza
0766848391
MOROGORO


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X