BARUA YA WAZI KWA WAZAZI NA WALEZI WA WATOTO


 

 Ndugu wazazi, siku ya leo nimeona niongee nayi kitu kimoja tu kuhusu malezi na makuzi ya watoto hasa kwa upande mzima wa usomaji wa vitabu.

 Ndugu mzazi nadhani inafahamika sana kuwa watoto huwa wananunuliwa midoli kwa ajili ya kucheza kadiri wanavyokua. Ila inashauriwa pia mzazi umununulie mwanao kitabu kama mdoli anapokuwa anakua. Hiki kitamsaidia kuanza kumjengea mazingira ya kuzungukwa na vitabu akiwa bado mdogo na hivyo  kuanza kumjengea tabia ya kusoma vitabu mapema. 

Badala ya kumununulia midoli yenye asili ya bunduki, unaweza hata kununua kitabu kimoja chenye picha mwanzo mpaka mwisho na mtoto akawa anafurahia kufunua na kuangalia picha. Kwa jinsi hiyo, ni wazi kuwa utakuwa umeweza kumjengea tabia nzuri ya kuanza kusoma mapema.

 Miongoni mwa amri kumi za malezi. Basi kumfundisha mwanao tabia ya kusoma vitabu ni amri mojawapo ambayo inapaswa kufuatwa vizuri.

Hakikisha umefuatilia video hii hapa yenye NJIA 13 ZA KUWAFANYAWATOTO WAKO WAPENDE KUSOMA VITABU HAPA

USISAHAU PIA KUSUBSCRIBE

 


WASHIRIKISHE NA WENGINE


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X