Vitu Vitano Vya Kuepuka Unapoamka Asubuhi


Moja, epuka kusikiliza taarifa ya habari. Asubuhi ni muda ambao akili inakuwa inafanya kazi kwa viwango vya juu, utumie muda huu kusoma na kujifunza mambo ya maana badala ya kusikiliza taarifa ya habari ambayo ni hasi.

Soma Zaidi: Sababu Tano Kwa Nini Unashindwa Kuamka Asubuhi Na Mapema Na Kitu Gani Unaweza Kufanya Sasa Hivi

Pili, epuka kuingia mtandaoni.  Mtandaoni hakuna jipya unaloweza kujifunza Asubuhi. Utumie muda huu kufanya kazi zako za maana. Labda tu Kama unautumia mtandao kuingiza fedha.

Tatu epuka kutopangilia malengo ya siku
Unaenda kufanya nini leo. Pangilia malengo yako vizuri, la sivyo utajikuta ukifanya kila kitu siku ikianza.

Nne epuka kutosoma mipango yako ya siku, wiki, mwaka.
Ni muhimu sana kujikumbusha malengo yako ya muda mfupi na muda mrefu. Hii Safari ya mafanikio ni ndefu, hivyo inahitaji kuendelea kujikumbusha wapi unaenda. Hivyo, soma mipango yako ya muda mrefu na mfupi.

Soma Zaidi: Kuamka Asubuhi Na Mapema Ni Tabia (Njia Sita Za Uhakika, Zilizothibitishwa Na Zisizoshindwa Zitakazokuwezesha Kujenga Tabia Ya Kuamka Asubuhi Na Mapema)

Tano epuka kutokutengeneza kitanda chako.
Kama ndani ya siku yako utaenda na kufanya vitu vingine bila mafanikio, utakuwa na uhakika kuwa ulitengeneza kitanda na huo ndio ushindi wako kwa siku hiyo.

Nakushukuru sana kwa kuweza kufuatilia somo hili mpaka mwisho. Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli Godius Rweyongeza

Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi wa vitabu kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

Kupata nakala ngumu ya kitabu cha KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI na kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO basi tuma ujumbe au piga kwa 0755848391

Kujifunza namna ya kutengeneza fedha kupitia blogu tuwasiliane kwa 0755848391

Kunialika kwa ajili ya kutoa mafunzo au semina kwenye kikundi chako, taasisi, kongamano n.k. wasiliana nami kwa email: songambele.smb@gmail.com au simu 0755848391


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X