Hiki Kitu Tu,Kitakufanya Uwe Na Maisha Ya Kawaida


Imewahi kukutokea ukaangalia labda igizo au ukasoma kitabu na kuona ni cha kawaida sana na wewe ungeweza kabisa kuigiza hilo igizo au ungeweza pia kuandika kitabu husika?

Unajua kitu gani kinakutofautisha wewe na huyo aliyeigiza hilo igizo au aliyeandika kitabu husika?

Kinachokutofautisha ni kuchukua hatua. Mwenzako anachukua hatua na kuigiza igizo alilo nalo ndani yake, wewe unaogopa na kusubiri kila kitu kikae sawa kwa upande wako, unasubiri mpaka ubobee kwenye kuigiza ili uanze kuigiza. Kitu Kikubwa ni kwamba huwezi kubobea bila ya wewe kuchukua hatua ya kwanza na kukamilisha kazi yako ya kwanza, hata Kama ni kidogo.

Kazi ya kufanya leo: fikiria kitu ambacho umekuwa unafikiria kufanya kwa siku nyingi, kisha anza kukifanya mara moja. Kuanza kufanya kitu ndiyo kutakupelekea kwenye kubobea ba hatimaye kuwa bingwa.

Umekuwa nami,

GODIUS RWEYONGEZA

Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

kila la kheri


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X