Kwenye vitabu vitakatifu wanaeleza wazi kuwa mlango wa kuingia mbinguni ni mwembamba. Muda mwingine watakuambia kwamba wanaoitwa ni wengi ila wanaochaguliwa ni wachache.
Sasa kitu hiki pia huwa kinajitokeza kwenye maisha ya kawaida ya mafanikio. Ni vigumu sana kupata mafanikio makubwa kirahisi, wengi wanapenda mafanikio makubwa ila wachache ambao wanaweza kufanikiwa na kufika mbali. Hii ni kutokana na ukweli kwamba mlango wa kufikia mafanikio ni mlango usiopitwa na wengi. Ila huwezi kukutana na mtu ambaye amefanikiwa huku akiwa amepitia njia laini.
Japo njia hii ni ngumu na mbovu, ila ukiweza kuhimili vishindo na kuipita, itakufanya kuwa imara zaidi.
Hivyo kama kuna sifa kubwa ambayo unaihitaji ili kuweza kufikia ndoto yako kubwa ni kuwa tayari kuhimili vishindo na magumu unayopitia kwenye kazi au biashara au kitu chochote unachofanya.
Magumu ambayo unapitia japo unaweza kuyaona mabaya, ila yanakuwa yanalenga kukuimarisha na kukufanya wewe kuwa bora zaidi. na hii ndiyo sifa kubwa sana ambayo unaihitaji sana ili kuweza kufikia mafanikio makubwa.
Umekuwa nami,
GODIUS RWEYONGEZA
Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA
Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA
Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA
Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391
kila la kheri