Pavel Durov ambaye ni bilionea na mwanzilishi wa telegram kwenye channel yake ya telegram ametoa ushauri kwa wanafunzi ambao wanatafuta kitu gani cha kusoma.
Anasema hivi,
Ikiwa wewe ni mwanafunzi unayechagua nini ubobee, basi chagua HESABU. Itakufundisha kutegemea akili yako mwenyewe bila kuchoka, kufikiri kwa mantiki, kugawa matatizo vipande vipande, na kuyatatua hatua kwa hatua kwa mpangilio sahihi. Huo ndiyo ujuzi wa msingi utakaohitaji kujenga kampuni na kusimamia miradi.
Huu ni moja ya ushauri muhimu sana hasa ukizingatia bilionea huyu ni mwanzilishi wa kampuni kubwa na kabla ya hii aliwahi kuanzisha kampuni nyingine.
Bilionea huyuhuyu siku za nyuma aliwa kusema kwamba wachina wanafanya vizuri kwenye sekta nyingi kwa sababu hesabu wamezipa kipaumbele kwenye mfumo wao wa elimu na hivyo akawa anashauri nchi mbalimbali kuiga mfumo wa elimu wa china
WEWE UNA MAONI KUHUSIANA NA HIKI ANACHOSEMA DUROV?