Tofauti kati ya ISBN na hakimiliki, USIJICHANGANYE


Habari,

Kinacholinda kitabu siyo ISBN, kinacholinda kitabu ni Hakimiliki.

Hakimiliki ni tamko la kisheria linalompa mwandishi au mzalishaji wa kazi ya kiubunifu haki ya kipekee ya kutumia, kunakili, kuchapisha, au kusambaza kazi yake. Hii ina maana kwamba mtu mwingine hawezi kutumia au kuchapisha kazi hiyo bila ruhusa ya mwenye hakimiliki.

Kwa upande mwingine, ISBN (International Standard Book Number) ni namba ya utambulisho wa kitabu inayotumika kibiashara. ISBN husaidia maduka, maktaba, na wachapishaji kutambua na kufuatilia vitabu kwa urahisi, lakini haiwezi kulinda kazi yako kisheria.

Kwa hiyo, ukimaliza kuandika kitabu, hakikisha kwanza ISBN maana ni rahisi kuipata, lakini kabla ya kutoa kitabu au mara tu baada ya kutoa kitabu, hakikisha unapata hakimiliki.

Kumbuka: ISBN ni namba ya utambulisho wa kitabu, lakini Hakimiliki ni kinga ya mwandishi.

Kwa Tanzania ISBN inatolewa na Maktaba ya taifa. Na hakimiliki inatolewa na COSOTA

Kwa maelezo zaidi kuhusu jinsi ya kupata hakimiliki au ISBN kwa kazi yako, wasiliana nasi Songambele Consultants kupitia:


WASAP   bonyeza HAPA


📞 0655 848 392

 


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X