Anza wewe kubadilika.


Unazikumbuka kampeni za mwaka 2015!!! Unazikumbuka? Ni miongoni mwa kampeni zilizokuwa motomoto. Kila mgombea alikuwa na hoja zake kubwa ambazo alikuwa akitoa kwa wapiga kura ili waweze kumchagua.

Kitu kikubwa kwenye kampeni hizi yakikuwa mabadiliko.

Kila mgombea alikuwa akiongelea namna ambavyo ataleta mabadiliko endapo atapewa madaraka.
Magufuri alikuwa anasema Tanzania ya viwanda.
Lowassa alikuwa anasema Movement For Change.

Wote walikuwa wanazungumzia mabadiliko Ila kwa namna tofauti.

Na maelfu kwa maelefu walikuwa wanakuaanyika kuwasikiliza.

Kila mtu alikuwa anapenda mabadiliko…..

Kiufupi hakuna mtu asiyependa mabadiliko…

Wote wanapenda mabadiliko. Au wewe hutaki?

Lakini changamoto kubwa ni kwamba unataka mabadiliko pasipo kutaka kubadilika wewe.

Wewe mwenyewe ndiwe unapaswa kuwa chachu ya mabadiliko kabla ya mtu mwingine yeyote yule.

Kama kuna mabadiliko unataka, Anza wewe kubadilika.

Ukisubiri mabadiliko yatokee juu, halafu wewe uyapokee, utasubiri sana.

Kama unataka mabadiliko ya kiuchumi, Anza kubadili uchumi wako kwanza.

Napenda Sana usemi wa Martin Luther King Jr. Anasema kila mtu akifangia mbele ya nyumba yake, dunia yote itakuwa Safi.

Au kwa lugha rahisi sana kwamba kila mtu akifanikisha majukumu yake, mambo mengine yote yataenda sawa.

Kuna hii nukuu ambayo niliwahi kuambiwa kuwa ni ya mwalimu Nyerere. Inasema kwamba play your part.

Yaani, timiza wajibu wako. Ukitimiza wajibu wako na mwenzako akatimiza wajibu wake, Basi hakuna kitakachokwama.

Sijui naeleweka….

Kama umenielewa jiunge na mfumo wetu wa kupokea mafunzo zaidi, ili niendelee kukuelewesha zaidi kila siku kwa baruapepe. Jaza taarifa zako hapa chini👇🏿👇🏿


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X