Dakika moja ya vitendo, ni bora kuliko maelfu ya dakika za maneno


Wakati tunasoma O-Level tulikuwa na jamaa mmoja hivi ambaye angeweza kukutisha kuwa atakupiga. Kwa vitisho vyake tu, ungeweza kudhani jamaa ana manguvu kama HAWAFU? Kwanza unamjua Hawafu kweli? HAHAH.

Hii stori ya Hawafu mwenye nguvu tuiache kwa ajili ya siku nyingine. Ila kama umeikumbuka vizuri unaweza kunijuza kikashani kwa kujibu ujumbe huu.

Ssasa tuendelee na jamaa yetu. Jamaa angeweza kukutishia kwa maneno tu mpaka ukanyoosha mikono juu kuwa umeshindwa. Sasa kutokana na vitisho vyake, siku moja alikuja kumtishia jamaa ambaye hatishiki. Siku hiyo moto uliwaka…..

Unataka kujua nini kilitokea…

Hahah, niache kwanza. Maana ilikuja kugundulika kuwa jamaa hana nguvu ila vitisho tu.

Sasa ninataka kukwambia nini siku ya leo.

Ninachotaka kusisitiza kwako siyo kwamba uanze kupigana na watu kuonesha kwamba una nguvu. Badala yake, nataka nikusisitize jambo moja la msingi sana. na jambo hili ni kwamba mwaka huu ukawe wa vitendo kwako kuliko maneno. Ndio maana mwaka huu tunaenda kwa kauli mbiu kwamba haturembi mwandiko.

Ni vitendo tu rafiki yangu.

Kwa hiyo mwaka huu, punguza maneno. weka kazi. punguza maneno. weka kazi. punguza maneno weka kazi

Ni hivyo tu.

Kwenye kitabu changu cha KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI nimemwongolea jamaa mmoja ambaye alikuwa anapenda sana kazi. na yeye muda wa kufanya kazi alikuwa anajua maneno matatu tu pale ulipokuwa ukimwongolesha.

Nashauri na wewe utumie haya maneno pia. Kujua haya maneno muhimu ya kutumia wakati wa kazi na kupata kitabu chenyewe basi fanya hivi.

Pata nakala yako leo hii.

Nakala laiani ni 10,000/- na nakala ngumu ni 15,000/.

Kitu kingine muhimu sana kwako ni kwamba tuna semina.

SEMINA YA KUFUNGUA MWAKA MPYA 2023. Na semina hii itaanza tarehe 15. Januari, hii. na itadumu kwa siku 15 mfululizo mpaka tarehe 30.

Semina hii itafanyi ka kwa njia ya mtandao. Na kwa siku 15 zote za semina utalipia 15,000/-.

Ili kujiunga na semina hii. wasilina nami kwa 0755848391.

Karibu sana.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X