Notice: Function _load_textdomain_just_in_time was called incorrectly. Translation loading for the uncanny-automator domain was triggered too early. This is usually an indicator for some code in the plugin or theme running too early. Translations should be loaded at the init action or later. Please see Debugging in WordPress for more information. (This message was added in version 6.7.0.) in /home/songambele/public_html/wp-includes/functions.php on line 6121

Notice: Function _load_textdomain_just_in_time was called incorrectly. Translation loading for the health-check domain was triggered too early. This is usually an indicator for some code in the plugin or theme running too early. Translations should be loaded at the init action or later. Please see Debugging in WordPress for more information. (This message was added in version 6.7.0.) in /home/songambele/public_html/wp-includes/functions.php on line 6121
Uwezo mkubwa ulio ndani yako - SONGA MBELE

Uwezo mkubwa ulio ndani yako


Leo nimeikumbuka sana siku nilipoenda kumtembelea rafiki  yangu. Kama ulivyo utaratibu wetu waafrika. Alinikaribisha kwa kuleta vinywaji pale mezani.

Lilikuwa Jambo la furaha sana kukutana na hiyo rafiki yangu na stori zilianza bila kuchelewa, huku tukikumbushana baadhi ya mambo yaliyowahi kutokea siku za nyuma na hata kutaniana.

Wakati stori zinazidi kukolea, glasi mojawapo pale mezani ilidondoka chini na kupasuka.

Hili hambo lilinifanya nitafakari sana, ukizingatia zile glasi zilikuwa bado mpya kabisa.

Nilibaki najisemea kimoyomoyo kwamba hii glasi imeharibika ikiwa bado na uwezo makubwa ndani yake ambao ulikuwa haujatumika.

Hiki kitu kunatokea kwa watu wengi pia..
Kuna watu wengi wenye uwezo mkubwa ila huwa hawautumii hata kidogo. Uwezo huu wa kipekee ungeweza kuinufaisha dunia…

Pengine hata wewe uko kwenye hili kundi.

Labda swali la kujiuliza hapa ni kwamba unautumia KWELI uwezo wako? Unautumia?

Kama hautumii uwezo wako ipasavyo, unadhani kitu gani kinakuzuia wewe kuweza kufanya hivyo?

Amua kuanzia leo hii kuwa nitakutumia uwezo wangu.
Nitakutumia kipaji changu, nitatumia ubunifu wangu au chochote kile nilichonacho.

Kitumie tafadhali, manufaa siyo kwa ajili yako tu. Bali yanakuwa kwa watu wote

Mpaka hapo umenielewa?

Kama umenielewa, weka email yako hapa chini, ili niendelee kukuelewesha zaidi kupitia jumbe zangu za kipekee nikazotuma kwa njia ya email kila siku.

Jaza taarifa zako hapa👇🏿👇🏿


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X