Ukifanya kitu unachopenda Ubunifu unakuwa mwingi.


…….muda si mrefu nimetoka kuongea na mteja wetu mmoja ambaye yuko mkoani Mara (Msoma mjini).
Ambaye amepokea kitabu Cha jinsi ya kufikia NDOTO ZAKO na kuanza kukisoma.

Kitu cha pekee nilichopenda kutoka kwake ni usemi wake anaosema kuwa ukifanya kitu unachopenda, Ubunifu unakuwa mwingi.

Na hiki kitu nimeona nikushirikishe na wewe pia.

Kuna utafiti unaonesha kuwa watu wengi wanakufa siku ya jumatatu baada ya kula Bata wikendi halafu jumatatu wanaamka na kwenda kufanya kazi wasiyopenda. Hicho kitu tu, kinawakatisha tamaa.

Ndiyo maana nimeupenda huu usemi, kiasi cha kuwa tayari kukushirikisha huu usemi na wewe.

Ujumbe mkubwa nilio nao kwako siku ya leo ni kwamba ufanye kazi au kitu unachopenda.

Ukifanya kitu unachopenda hutachoka
Ukifanya kitu unachopenda ubunifu unakuwa mwingi.

Thomas Edison alikuwa analala saa tatu kwenye maisha yake na kuamka mapema kwenda kazini. Siku moja aliulizwa kwa nini unafanya sana kazi.

Aliwajibu watu kwa kuwaambia kuwa sijawahi kufanya kazi.

Umeona ee! Alikuwa anafanya kitu anachopenda. Hivyo, kwake hakuona kama hiyo ilikuwa kazi.

Hivi wewe unafanya unachopenda kweli? Unafanya unachopenda?

Ngoja nikukumbushe, “ukifanya kitu unachopenda, ubunifu unakuwa mwingi”.

Kwa jioni ya leo naishia hapa.

Halafu ujue kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO kipo tayari. Na watu wanapokea nakala zao popote pale walipo. Wewe pia unaweza kupata nakala yako kwa Bei ya oda. Ujue gharama ya kitabu hiki ni 20,000/- Ila habari njema ni kuwa ukilipia kitabu hiki kabla ya tarehe 20 Mei. Utakipata kwa 15,000/- unaanzaje Sasa kwa mfano kukosa nakala yako.

Ebu nitumie ujumbe wako sasa hivi

Tuma ujumbe kwa
0755848391
Au WhatsApp
https://wa.me/message/3PMZSAFONLHAP1

Ili utumiwe kitabu chako.

Umewkuwa nami
Godius Rweyongeza
0755848391
Morogoro-Tz

Ukifanya kitu unachopenda ubunifu unakuwa mwingi.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X