Hii Ndiyo Sheri Ambayo Itakusaidia Wewe Kupata Chochote Kile Unchotaka


Profesa mmoja alifanya kijiutafiti chake binafsi. Zilikuwa ni nyakati za krismasi, hivyo alichofanya ilikuwa ni kuandika kadi za krismasi kwa watu ambao walikuw hawamjui huku akiwatakia kheri ya krismasi.

Profesa akakaa huku akisubiria majibu. Baadaye alikuja kugundua kuwa asilimia kubwa ya watu walijinu kwa kushukuru kwa kadi ile ya krismasi ambayo alitoa na , ila wengi sana hata hawakumuuliza kuwa alikuwa nani na mawasiliano yao aliyapataje.

Hiki kitu ndiyo ninataka kianze kutupa mwanga kwa ajili ya somo letu la leo

Leo tunaizungumzia kamnuni ya RECIPROCAL. Kulingana na kanuni hii ni kwamba, ukifanyia mtu kizuri. mtu huyo anahisi kama ana deni na anapaswa kukulipa kulingana na kile ulichomfanyia.

Ukimpa mtu labda msaada, anajiona kwamba kuna deni ambalo anapaswa kukulipa kulingana na msaada ambao umempa.

Hivyo, unaweza kuitumia kanuni hii kwenye biashara yako pia au kwenye kitu ambacho unafanya pia. Kadiri unavyotoa kitu chenye thamani kubwa, ndivyo watu wataona kwamba kama wana deni vile ambalo wanapaswa kukulipa na hivyo utajenga timu ya watu ambao wanakuamini kwenye kile unachofanya na hata wateja wa kudumu.

Kila la kheri.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X