Je, bado na wewe ni mshamba wa fursa?


Kila mara huwa wanakuja watu kwa kusema kwamba kitu fulani kinalipa ukilinganisha na kitu kingine. hiki kitu ndio kinanifanya leo hii intake kukuuliza, hivi na wewe bado ni mshamba wa fursa.

Hkauna fursa moja ambayo unaweza kusema kwamba inalipa zaidi kuliko nyingine.

Kila ulimwona mjomba amenunua gari kupitia fursa fulani, haimaanishi kwamba na wewe ukimbilioe huko.

Moja ya stori ambayo imekuwa ikipagawisha watu kwenye kilimo ni stori KILIMO CHA TIKITI.

Watu wengi wamekuwa wakikimbilia kulima tikiti kwa kujua kwamba tikiti linalipa sana. wapo ambao wamekuwa wanafanikiwa kwa viwango vikubwa huku wengine wakiangukia pua.

Ujumbe wangu kwako siku ya leo ukiona mtu kafanikiwa kwenye fursa fulani, badala ya kukimbilia kuiga na kufanya kama alivyofanya, jiulize maswali yafuatayo.

Je, amekuwa akiifanyia kazi hii fursa hii kwa miaka mingapi?

Hiki kitu kitakusaidia kujua nje ndani kuhusiana na fursa husika na hivyo kujua  muda na nguvu utakazopaswa kuweka. Wengi  wanaposikia kuhusu fursa wanadhani kuwa ni kitu ambacho utafanya kwa siku moja na kitu hicho kikaleta matokeo makubwa. wengi unaowaona wamefanikiwa kwenye fursa fulani, wamekuwa wakizifanyia kazi hizo fursa kwa miaka mingi mpaka leo hii unaona tayari wamefanikiwa. Na hiki kitu kimewafanya waijue fursa husika nje ndani, kiasi kwamba inafikia hatua wanafanya maamuzi ambayo yanawasaidia kufika kule wanapotaka.

Ni msimu gani zao hili linafanya vizuri?

Kama umemwona mtu amefanikiwa kwenye kilimo. Na wewe unataka kuingia kwenye kilimo. Usiingie kichwa kichwa, la sivyo utakuja kuangukia pua. Kabisaaa. Badala yake jiulize ni  msimu gani zao lipi huwa linakuwa na bei ya juu. Hili lipo karibia kwenye kila zao. Hivyo, ni muhimu kwako kutambua hiki kitu, la sivyo utaingia kwenye kilimo kichwa kichwa halafu utaangukia pua.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X