Ukipenda pesa, lazima upende na kazi


Rafiki yangu mpendwa, vitu vingi vilivyo hapa duniani huwa vinaenda viwili viwili.
Mfano ukiongelea juu, lazima kuwepo chini.
Ukisema mbele lazima kuna nyuma
Ukizungumzia kulia sharti kuwepo kushoto pia

Sasa hiki kitu kina funzo kubwa sana kwetu na hasa kwenye kutafuta fedha na mafanikio.
Na ujumbe ni kuwa ukipenda fedha lazima upende kazi.

Ni wazi kuwa huwezi kupata fedha bila ya KUWEKA kazi kwanza. Lakini pia ili upate fedha zaidi Unapaswa kuijua misingi ya fedha kwenye uwekezaji, na kuifanya fedha ukifanyie kazi zaidi. Komaa humohumo.

Fanya kazi kwa bidii
Pata pesa.
Weka akiba
Wekeza
Rudia tena hayo.

Kila la kheri
Godius Rweyongeza


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X