Hili Ndilo Suluhisho la Kudumu Kwa Tatizo La Ajira Linaloendelea


Rafiki yangu mpendwa, bila shaka unaendelea vizuri, changamoto kubwa kwenye zama tunazoishi sasa hivi ni ajira. Kuna vijana wengi ambao wamehitimu chuo ila hawana ajira, kila siku wanahangaika kuomba kazi kwenye taasisi moja baada ya nyingine. Ukweli ni kuwa kwenye zama tunazoishi sasa hivi hakuna ajira kama ilivyokuwa kwenye zama za viwanda. Hata hivyo kazi za kufanya zipo nyingi na mahitaji ya msingi kabisa ya kila siku ya mtu yapo palepale. Kila siku kuna watu ambao wanahitaji kula, kila siku na watu ambao wanaendelea kutafuta elimu, watu wanaendelea kujenga kila siku…

Kumbe tatizo siyo kazi maana zimejaa ila watu wa kufanya hizo kazi ndiyo hawapo.

Kama unaweza kuchagua kazi yoyote ile na kujikita kwenye hiyo, ukaifanya kwa ubora na kutoa thamani kubwa kwa watu, maana yake mwisho wa siku utapata fedha kutoka kwa hao watu.


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X