Vitu viwili vinavyokufanya ushindwe kufikia ndoto zao


Ukiingia kwenye mitandao ya kijamii utakuta vijana mbalimbali wameandika kwenye mitandao yao mambo kadha wa kadha, unaweza kukuta mtu ameandika mfanyabiashsra, CEO, mjasiriamali na vungine vingi.

Kati ya hayo matamanio mengi wanayokuwa nayo, ni wachache sana sana ambao huwa wanafikia na ndoto hizo. Kwa nini?

Ninaenda kutoa sababu kuu mbili lakini kwanza, angalia video hiyo hapo juu👆🏿

Sababu ya kwanza kwa Nini vijana wengi hawafikii ndoto zao kuwa na mambo mengi.

Naam, huu ndiyo sababu ya kwanza kwa nini wengi hawafikii ndoto zao. Tena utakuta mtu anasema kuwa mambo ni mengi muda ni mchache. Ukweli ni kuwa unapokuwa na ndoto, akili yako na muda wako mwingi unapaswa kuuweka kwenye ndoto yako, sahau mambo mengine yasiyohusiana na ndoto zako na weka umakini wako wote kwenye ndoto zako.

Ukiweza kuachana na mambo mengi unayopambana nayo na kuweka nguvu zaidi kwenye ndoto zako, ni wazi kuwa hii ndoto yako kubwa lazima tu utaifikia. Sasa swali ambalo unapaswa kujiuliza ni mambo gani ambayo umekuwa unafanya nje ya ndoto yako kuu? Je, ni vijitabia gani hasa ambavyo vinakupotezea muda ambao ungeweza kuuweka kwenye ndoto yako kubwa? Hivi vijitabia unapaswa kuachana navyo ili ujenge ndoto yako kubwa au la achana na ndoto yako kubwa ili ujenge vijitabia…..

Ukweli ndio huo …
Hakikisha umepata kitabu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO utanishukuru kwa kukisoma, hiki mtandaoni hapa
https://www.getvalue.co/prod/jinsi__ya_kufikia_ndoto_zako

Au piga 0684408755 sasa uletewe nakala yako

Sababu ya pili ni kuiga maisha ya watu wengine

Kwenye clip fupi ambayo nimekushirikisha hapo juu nimekuonesha mhusika ambaye kila anapotembea kidogo anawaona wengine wanavyotembea anaanza kuiga mwenenedo wao wa kutembea. Sasa naomba unisikilize vizuri ili tuweze kuelewana; kuna vijana wengi wanapokuwa wanafanyia kazi ndoto zao wanakuwa hivi.

Wanakuwa kama bebdera na kila wakati wanafuata upepo. Ukivuma kwa kasi kutoka kaskazini kuelekea kusini, wanaanza kuelekea kusini, baadaye ukibadili mwelekeo na wao wanabadili mwelekeo. Sikiliza, ukishajua ndoto yako kubwa ni ipi, kinachofuata ni wewe kukomaa nayo, haijalishi upepo unatokea wapi kuelekea wapi. Wewe komaa kwanza na ndoto yako moja mpaka kieleweke

Usiwe mtu wa kuiga rafiki zako wanafanya nini. Ukweli ni kuwa ukienda kwa staili hiyo huwezi kufanikisha ndoto zako. Kwa sababu kila mara utakuta kuna mtu ambaye anafanya kitu fulani au ambaye amekuzidi.

Lakini ukweli mwingine mchungu ni kuwa kadiri unavyobadili mwelekeo wako, ndivyo ambavyo utakosa kutumia UBUNIFU mkubwa ulionao. Nimeandika kitabu kizima kinachozungumzia namna unavyoweza kuibua ubunifu ulio ndani yako, unaweza kukipata mtandaoni ndani dakika mbili tu hapa.
https://www.getvalue.co/prod/jinsi_ya_kuibua_ubunifu_ulio_ndani_yako

Kwa kumalizia Ningependa kusema kuwa ndoto uliyonayo, inawezekana kabisa kuitimiza. Unaweza kuitimiza kwa asilimia 100. Ila inahitaji ujitoe, ufanye kazi kwa bidii na ujitume mpaka kieleweke.

Kuwa wewe mwenyewe.

Makala hii imeqndikwa na Godius Rweyongeza
Kujifunza zaidi kutoka Kwa Godius Rweyongeza tembelea www.songambele.co.tz
Wasiliana naye Kwa 0755848391
Morogoro-Tz

Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza wasiliana na 0684408755

Kujifunza UANDISHI na kupata usimamizi wa Moja Kwa Moja kutoka Kwa Godius Rweyongeza wasiliana na 0678848396

Karibu sana


2 responses to “Vitu viwili vinavyokufanya ushindwe kufikia ndoto zao”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X