Hiki ni kitu ambacho kinaenda kukupa matokeo makubwa kama utakifanyia kazi


Rafiki yangu mpendwa salaam,

Bila shaka unaendelea vyema na kazi zako. Hongera sana kwa kazi. Siku ya leo ningependa nikwambie kitu kimoja ambacho kinaenda kukupa matokeo makubwa.

Kitu hiki siyo kingine bali ni kufanya kazi ambayo unapenda. Kama unahairisha sana kufanyia kazi majukumu yako, kuna uwezekano mkubwa kuwa unafanya kazi ambayo wewe mwenyewe hupendi. Kama utaanza kufanya kazi ambayo unapenda, ni wazi kuwa utajikuta kwamba unaifanya kwa bidii na kwa muda mrerfu na hata bila kuhairisha.

Muda mwingine unaharishisha majukumu ambayo unapasw akuwa unayafanyia kazi kwa sababu huyapendi. Fanya kile unachopenda na ukweli ni kuwa hutajihisi kama unafanya kazi. Na hili litakufanya uweze kupata matokeo makubwa huku ukiwa unajisikia vizuri kwa kile unachofanya.

Ujumbe wangu wa leo kwako ni mmoja tu; kama unataka kupata matokeo makubwa fanya kazi ambayo unapenda.

Thomas Edison ni mmoja wa watu waliokuw awanafnaya kazi sana na kwa muda mrefu. Siku moja aliulizwa ni kwa nini anafanya kazi muda mrefu sana. Alijibu kwa kutoa jibu la kushangaza sana. Alisema, sijawahi kufanya kazi; inashangaza sana.

Unajua kwa nini alisema kwamba sijawahi kufanya kazi. Alisema hivyo kwa sababu, alikuwa anafanya kazi anayoipenda na hivyo alikuwa hajisikii kama anafanya kazi japo alikuwa anafanya kazi kwa muda mrefu kuliko watu wote wlaiokuwa wamemzunguka.

Kama huwezi kunisikiliza mimi, basi msikilize vizuri Thomas Edison.

Kila la kheri.

Makala imeandikwa na Godius Rweyongeza.

Unaweza kuwasiliana na mwandishi kwa 0755848391 au baruapepe ya godiusrweyongeza1@gmail.com

Kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza, jiunge na mfumo wake wa kupokea mafunzo kwa baruapepe. hapa chini

Je, na wewe ungependa kujifunza uandishi? BONYEZA HAPA


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X