Moja ya ushauri maarufu sana ambao umekuwa unatolewa kwa watu ni ushauri wa kuwa mind your own business. Kwa lugha yetu sisi vijana wa siku hizi ni saawa na kusema kwamba pambana na hali yako.
Yaani, kwamba achana na mabo mengine ya watu wengine halafu
Nguvu zako
Muda wako
Akili yako
Fedha zako na
RASILIMALI ZAKO zote ziweke kwenye mambo yanayokuhusu wewe.
Mambo ya wengine waachie na wao wapambana na mambo yao.
Ya Ngoswe mwachie ngoswe
Ya Kaisari mwachie Kaisari…
Ni mara ngapi wewe umekuwa unavunja ushauri huu? Badala ya kupambana na hali yako unapambana na hali za watu wengine.
Unaanza kufuatilia maisha ya watu wengine,
Wanaishije
Wanatoka na nani
Hali ya mahusiano yao ikoje
AU MUDA MWINGINE UNAjiingiza kwenye mijadala isiyokuwa na ulazima wowote…
Unaanza kujadili kati ya mtu A na B nani ana hela.
Au kati ya fulani na fulani nani ana kipaji zaidi..
Nani ana wafuasi zaidi kwenye mitandao ya kijamii.
Wew haya hata uyafuatilie kiasi gani, hayakusaidii.
Leo nataka nikurahisie tu.
Kama kitu hakikuiuingizii pesa leo, au kama hakitakuja kukuingizia pesa siku zijazo. Usikifuatilie.
Kama kitu siyo lengo lako kuu, usikipe muda wako
Kama kitu siyo biashara au kazi yako, usikifanye kuwa biashara yako.
Mimi kwa leo naishia hapo
Kama bado hujapata ofay a vitabu sita kwa elfu 20 tu. Jua unajikwamisha. Hii ni ofa ya muda mfupi ambayo tumejadiliana na wasaidizi wangu kuwa itapaswa kuisha muda si mrefu. Kama bado hujapata hii ofa, sikiliza.
Wasiliana na 0684408755 (whatsap/sms/simu). Kisha mwambie akupe ofa ya vitabu sita.
Fanya hivyo haraka iwekezakavyo kabla ofa haijafungwa.
Niliyekuandikia makala ya leo naitwa Godius Rweyongeza
Nipo Morogoro nchini Tanzania