Jinsi Ya Kuandaa Kizazi Cha Wafanyabiashara


Juzi nilikuwa nasoma ujumbe wa mkurugenzi mkuu wa TELEGRAM.
Alizungumzia namna kampuni za kichina zinavyofanya vizuri na namna ambavyo zitafanya vizuri kwa siku zijazo kutokana na mfumo mzuri wa elimu walionao.

Kitu hiki kimenitafakatisha sana na Leo nikaona nikuandalie ujumbe muhimu wa namna Leo hii tunavyoweza kuanza kuandaa kizazi kijacho Cha wajasiriamali, kizazi ambacho kinaweza kwenda kupambana huko duniani, na kuleta mapinduzi makubwa.

Kwa Nini nasema tuandae kizazi Cha wajasiriamali? Kwa sababu wajasiriamali ndiyo wanakuja na mawazo mengi ya kibunifu na ndiyo ambao wanaweza kukuletea mabadiliko MAKUBWA yajayo.

Kinachofanya wachina wanaonekana tishio Leo hii ni kwa sababu ya wajasiriamali na wabunifu walio nao. Na kitakachofanya sisi tufanye MAKUBWA ni kwa sababu ya wajasiriamali tulionao pia.
Hivyo basi rafiki yangu huu ni wakati wetu sisi kuanza kuandaa kizazi kijacho Cha wajasiriamali.

Sasa tunawaandaaje. Kwanza, tuwaandalie mazingira ya kiushindani kama ambavyo anatuelekeza hapo mkurugenzi mkuu wa TELEGRAM. Pili, tuwaandalie mazingira ya kuanza kufanya biashara wakiwa wadogo. Aidha tunaweza kuwapa miradi midogo midogo nyumbani waisimamie.

Tatu, tushirikishane nao kwenye biashara zetu. Sambamba na shule nzuri tunazowasomesha, tushiie tu hapo, wakitoa shule au siku za wikendi twende nao kwenye biashara au kazi tunazofanya. Na wao washiriki pia.

Nne, Kuanzisha Mafunzo ya Ujasiriamali Mapema. Kwa kuwa hatutegemei kuwa na mfumo huu ukiwekwa kwenye elimu ka haraka. Basi tutakachofanya ni kuwapeleka watoto kwenye Mafunzo ya kibiashara sisi wenyewe au ili kuwafundisha misingi ya biashara, fedha, na ubunifu tangu wakiwa wadogo. Rafiki yangu Innocent huwa anatoa Mafunzo ya namna hii kila jumamosi.

Tano, kuwahamasisha Kufikiri Kibiashara. Ni muhimu sana tuanze Kuwaelekeza watoto kuona fursa kwenye changamoto. Wajue wazo kuwa changamoto ni fursa. Kumbe, badala ya kutegemea ajira kama suluhisho pekee la maisha wafikiri nje ya hapo na tuwaelekeze hili mapema.

Badala ya kuwaambia kwamba nenda shule USOME kwa bidii ili uje uajiriwe. Tuwaambie waende shule, wajifunze kwa bidii ili waje watumie ujuzi watakaojifunza kusaidia KUTATUA matatizo Yao.

Sita, kuwajengea uwezo wa ubunifu na uvumbuzi. Kuwatia moyo kutumia mawazo yao kuunda bidhaa au huduma mpya zitakazosaidia kutatua matatizo ya jamii. Ni kwa namna Gani hili tunaweza kukifanya tukiwa nyumbani, ni kwa
1. Kuwazoesha kuwapa maswali badala ya majibu
2. Kutokuwa wepesi wa kujibu maswali Yao hata pale tunapokuwa tunajua majibu ya maswali Yao
3. Kutowaepusha na magumu hata pale tunapoweza kufanya hivyo.

Saba, kuwafundisha umuhimu wa akiba na uwekezaji . Kwa kila fedha unazowapa kwenda shule, waambie pia wajenge utaratibu wa kujilipa wenyewe kwanza kwa KUWEKA akiba. Akiba itawaba wakiwa wakubwa.

Nane, kuwahamasisha kuchukua hatua bila hofu.
Utasikia mzazi anamwambia mwanae, ukikokoaea kufanya kitu fulani nitakuua. Na kauli nyingine nyingi hasi. Badala ya kuwatishia hivyo, wahamasishe wachukue hatua hata kama muda mwingine wewe mzazi unakuwa na hofu au wasiwasi.

Kuwaunganisha na wajasiriamali waliofanikiwa ukipata nafasi ya kushiriki semina au kukutana na watu waliofanikiwa nenda na wanao. Waone watu waliofanikiwa wanaongeaje, wanaishije, wanatendaje. Watajifunza mengi kwa kuona kuliko wewe kuwaambia kwa mdomo tu.

Kuwajengea Uwezo wa Mawasiliano na Ushawishi
Ni muhimu sana tuwafunze watoto wetu umuhimu wa kuwasiliana na kuwasiliana mawazo Yao. Maana itafikia hatua watakuwa na wazo, na watatakiwa kuliwasilisha kwa wateja au wawekezaji. Sasa bila ya kuwa na ujuzi mzuri wa mawasiliano hawataweza kufanya makubwa.

Kuwafundisha maadili ya ujasiriamali. Maadili ya uaminifu, uvumilivu, bidii, na kujali n.k
Haya pia ni maadili muhimu ambayo yatawabeba watoto wetu.

Hayo ni mambo machache ya kuanza nayo.

Wewe unaenda kuanza na jambo Gani

By the way mwezi wa sita tutakuwa na semina, Na Moja ya mada itakayofundishwa ni mada ya NI NAMNA YA KUANDAA KIZAZI KIJACHO CHA WAJASIRIAMALI chini ya mkufunzi wetu Innocent Kavishe.

Karibu sana kwenye semina hii ya kipekee.

Karibu sana kwenye semina ya biashara na uwekezaji mwaka 2025

Rafiki yangu mpendwa, kila mwaka huwa tunakuwa na semina tatu. Semina moja huwa inafanyika kuanzia tarehe 15-30 Januari KWA NJIA YA MTANDAO. Semina ya pili huwa inafanyika wikendi ya mwisho ya mwezi wa Juni (hii ni ya ana kwa ana), na semina nyingine huwa inafanyika septemba wiki ya mwisho (tarehe 24-30 septemba). Hii huwa inafanyika mtandaoni pia.

Semina ya mwezi wa sita huwa ni semina ya ana kwa ana, na kwa mwaka huu 2025 itafanyika tarehe 29-30 Juni. Itakuwa ni siku ya jumamosi na jumapili. Itafanyika KINGSWAY HOTEL MOROGORO.

Semina hii ya ana kwa ana imekuwa inafanyika na huu utakuwa ni mwaka wetu wa tatu mfululizo. Semina ya mwaka huu inaenda kuwa ya tofauti na ya pekee.

Hivyo, nichukue nafasi hii, kukukaribisha sana kwenye semina ya biashara na uwekezaji mwaka 2025.

Katika semina hii ya mwaka 2025 tumekuandalia mambo makubwa yafuatayo.

SIKU YA KWANZA 29.6.2025:

  1. MISINGI YA KUKUZA BIASHARA KWENYE ULIMWENGU WA LEO
  2. JINSI YA KUAGIZA BIDHAA NJE YA NCHI (CHINA)
  3. MAMBO YA KUZINGATIA BAADA YA KUSAJILI KAMPUNI
  4. KUTUMIA RASILIMALI ZA WATU WENGINE kwa VITENDO
  5. JINSI YA KUJENGA BRAND YAKO
  6. ELIMU YA KODI KWA WAFANYABIASHARA

SIKU YA PILI: 30.6.2025

  1. KUTOKA KUAJIRIWA MPAKA KUMILIKI BIASHARA (mwongozo kamili)
  2. ELIMU YA FEDHA NA UWEKEZAJI
  3. WANANDOA NA BIASHARA (misingi ya kusimamia biashara kama wenza na urithi kwa watoto)
  4. ITAWALE HOFU YA KUANZISHA NA KUKUZA BIASHARA
  5. ELIMU YA FEDHA KWA WATOTO NA NAMNA YA KUANDAA KIZAZI KIJACHO CHA WAFANYABIASHARA
  6. KUFIKIRI NJE YA 18 2025 (MWONGOZO KUSIMAMIA BIASHARA ZINAZOJIENDESHA)

Hizo ndizo mada ambazo tutazungumzia kwa undani mwaka huu. Kiukweli unaenda kuwa ni mwaka wa kipekee sana na mwaka wa kufanya makubwa.

Imani yangu ni kwamba wewe…………………………..utakuwa mmoja wa washiriki wa semina yetu ya mwaka huu. Umekuw unakosa semina za miaka mingine yote,mwaka huu usikubali kamwe kuikosa semina hii.

Pambana kadiri uwezavyo kuwepo kwenye semina yetu.

Ada ya semina itakuwa 170,000/- kwa atakayeshiriki semina hii kwa siku mbili.

Wakati kwa atakayeshiriki semina hii kwa siku moja ada ya semina itakuwa 100,000/- tu. Na atakayeshiriki semina kwa njia mtandao kwa siku zote mbili itakuwa 85,000/- tu

Njoo tuungane mwaka huu kwenye semina hii ya kipekee ili uweze kufanya makubwa kwenye eneo la biashara yako na maendeleo binafsi.Bonyeza hapa sasa.

Kuhusu malipo ya semina

Kwanza chagua aina ya package ambayo utashiriki. Kama utashiriki kwa siku mbili au kwa siku moja au kwa njia ya mtandao.

Unaweza kulipia ada yote ya SEMINA mara moja au unaweza kulipia kidogokidogo pia.

Kwa mfano, unaweza kuanza utaratibu wa kulipia kila mwezi kwa kuigawa ada yote ya semina kwa miezi minne ambayo tunayo mbele yetu. Ukilipia 50,000 kila mwezi kuanzia sasa. Mpaka kufikia siku ya semina ada yote ya semina itakuwa imeshakamilika.

Unaweza pia kuanza utaratibu wa kulipa kila wiki 15,000 tu.

Au kila siku elfu mbili tu.

Chukua hatua sasa uanze kulipia.

Namba ya malipo ni CRDB: 0150984455500 JINA ni SONGAMBELE CONSULTANTS

Au TIGO PESA: 19016638 jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

Karibu sana rafiki yangu

NB: kwenye ukurasa unaofuata nimekuambatanishia ratiba kamili ya semina na wakufunzi watakaondisha siku hiyo. KARIBU SANA.

Ni mimi kijana wako

Godius Rweyongeza

0755848391

Morogoro-Tz


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X