
Kwenye timu ya mpira wa miguu huwa kuna wachezaji wa aina mbalimbali ila mojawapo ya wachezaji huwa ni washambuliaji. Hawa kazi yao huwa ni kuhakikisha muda wote wanasumbua kwenye lango la mpinzani ili mwisho wa siku waweze kuipatia timu yao ushindi.
Endapo washambuliaji hawatafanya kazi yao ya kushambulia na badala yake wakaanza kujilinda dhidi ya timu nyingine maana yake ni kwamba, hiyo timu haiwezi kushinda. Haiwezi kushinda kwa sababu hailengi hata kufunga goli hata moja. Na ushindi unakuja kwa kufunga.
Kadiri mnavyoshambulia kwa wingi ndivyo nafasi yenu ya kufanya vizuri inavyokuwa nzuri kuliko pale mnapokuwa hamshambulii
Kwenye maisha ya kawaida hivyo hivyo. Wale wanaoshambulia, wana nafsi nzuri ya kufanya vizuri zaidi kuliko wale wanaokuwa hawashambulii.
Wanaoshambulia ndiyo wanaofanya makubwa.
Pengine unaogopa kushambulia kwa sababu unaogopa unaweza kushindwa goli na hivyo kuonekana kama hujui? Si ndiyo?
Kwenye hili nikuletee nukuu muhimu sana ya Michael Jordan aliysema kwamba nimeshindwa mara nyingi sana, ndiyo maana nashinda. Kama unataka kushinda, shindwa kwanza.
Kushindwa ni tiketi yaw ewe kufanya makubwa sana.
Nimewahi kabisa mpaka kuandika kitabu kinaitwa. Nyuma ya ushindi, kuna kushindwa, kushindwa, kushindwa. Kama hujawahi kupata nakala ya hiki kitabu, nakushauri ujipatie nakala yako mapema iwezekavyo. Kitakusaidia kukupa mwanga wa namna unavyoweza kufanya makubwa, hata katika mazingira ambayo unapitia changamoto.
Kujipatia nakala ya kitabu hiki, naomba tuwasiliane kwa simu 0755 848 391