
Utasikia mtu anakwambia kwamba hiki nakijua, nilijifunza chuo. Hiki nakijua…
Kama unakijua kwa nini hukifanyii kazi? Rafiki yangu kitu kikubwa ninachotaka kukwambia siku ya leo ni kwamba kujua pekee hakutoshi. Unapaswa kujua vitu na kuvifanyia kazi pia.
Hiyo ndiyo inaenda kuwa tiketi yako wewe kukfanya makubwa.
Haitoshi tu kwa wewe kujua kuweka akiba, bila ya kuweka akiba.
Haitoshi tu kwa wewe kujua kwamba ni muhimu kufanya mazoezi bila ya kuyafanya.
kuna watu wengi wanajua vitu ila hawavifanyii kazi.
sasa wewe utakuwa na tofauti gani na hao wengine.
wewe unapaswa kujua vitu na unapaswa kuvifanyia kazi pia.