Mwaka 1969 binadamu kwa mara ya kwanza aliingia mwezini. Unaambiwa kompyuta iliyotumika kipindi hicho kumwingiza mtu mwezini ilikuwa na uwezo mdogo sana, uwezo wake ulikuwa mdogo mno kiasi cha kuzidiwa na simu janja tunazotumia sasa.
Ila iliweza kutumika kutufikisha mwezini. Ndiyo maana nimekuwa nakushauri kuwa makini na vitu vidogo, kutokana na madhara au matokeo yatokanayo na vitu hivyo.
Mbu ni wadogo, ila madhara yake kwa watu ni makubwa. Wana uwezo wa kusababisha malaria ambayo najua unajua madhara yake.
Wewe pia usidharau hatua ndogo ndogo. Akiba kidogo kidogo unayoweka kila siku, ina uwezo wa kukufikisha mbali. Usidharau.
Maneno 500 ya kitabu chako unayoandika kila siku, Kuna siku yatakufanya wewe utambulike Kama mwandishi MBOBEVU.
Mazoezi hayo unayofanya kila siku, yanazidi kuimarisha mwili wako zaidi.
Ni kitu gani kidogo unekuwa unafikiria kufanya kwa siku nyingi, ila hujakifanya. Ebu nenda kakifanye leo.
Soma zaidi: NGUVU YA RIBA MKUSANYIKO
Umekuwa nami,
GODIUS RWEYONGEZA
Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA
Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA
Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA
Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391
kila la kheri
One response to “Usidharau vitu vidogo vina uwezo wa kukufikisha mbali Sana”
[…] NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA […]