Iga Ufe


Kuna baadhi ya vitu huhitaji kuiga kwa watu wengine.  Badala yake unapaswa kuvifanya kulingana na wewe mwenyewe.

Siyo kila kitu wanachofanya wengine kinaweza kukufaa na wewe pia. VIngine vinaweza kuwa sahihi kwao, lakini siyo sahihi kwako. Ni muhimu kwako kufahamu kipi ni sahihi kwako, na kuwekeza nguvu yako kubwa hapo.

Kuna watu wanakopa na mshahara wao unapoingia tu, wanakuwa haawana kitu ambacho kimebaki, wanaenda kulipa madeni na kuendelea kukopa zaidi. Hiki kitu kinaweza kuwa sahihi kwao, lakini siyo sahihi kwako. Iga ufe.

Kuna watu wakipokea fedha, wanafanya matumizi yote unayoyafahamu hapa duniani, halafu ndiyo wanasubiri kile kinachobaki waweke akiba. Hiki kitu kinaweza kuwa sahihi kwako, ila siyo kwako. Iga ufe.

Kuna watu hawana malengo wala ndoto zozote kubwa, wanaishi tu ilimradi maisha yameenda. Wanaishi kwa usemi kwamba kesho itajipa yenyewe, hawana haja ya kuihangaikia kesho. Hiki kitu kinaweza kuwa sahihi kwao, ila kwako. Iga ufe.

Fahamu yapi ni sahihi kwako kufanya. na wekeza muda wako kwenye hayo ambayo ni sahihi kwako kwa wakati huu. Achana na yale yote ambayo siyo sahihi.

soma zaidi 

Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana na +255 684 408 755

Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com


Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X