Category: A NOTE FROM SONGAMBELE

  • Hii Ni Zawadi Ya Kipekee ambayo Unaweza Kutoa Kwa Baba Yako (Happy Father’s Day)

    Kila mzazi huwa anapenda kuona mtoto wake anafanikiwa na kufanya makubwa. Anaweza akawa hasapoti ndoto yako.Anaweza akawa hayuko nyuma yako wakati wa mapambano, Ila ukifika ukifanikiwa atakuwa nyuma yako. Kumbe zawadi ya kipekee ambayo unaweza kutoa kwa wazazi wako ni kufikia ndoto zako. Jipe muda wa kufanyia Kazi ndoto zako na kuhakikisha kuwa haurudi nyuma…

  • Viashiria Vitano Kuwa Wewe Ni Genius (Kiashiria Namba Tano Ni Muhimu Sana Rafiki Yangu)

    Siku ya leo nimekuandalia video inayoeleza viashiria vitano ambavyo vinaonesha kuwa wewe ni Genius? Je, upo tayari kujua hivi viashiria? hakikisha umesubscribe kwenye channel yangu ya youtube kwa ajili ya mafunzo zaidi hapo baadaye.

  • Mwongozo Unapouhitaji Kufikia Ndoto Zako

    Jana nilikuwa naongea na rafiki yangu ambaye amechukua vitabu vya JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO pamoja na NGUVU YA VITU VODOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA Inaonekana rafiki yangu kaelewa vizuri sana dhana ya hivi kitabu. Anasema hivi, Unahitaji kuwa na ndoto KUBWA. Ila haitoshi. Ili uifanikishe hapo ndipo utapaswa kutumia nguvu ya vitu VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO…

  • JINSI YA KUJUA THAMANI YA MUDA WAKO

    Tuna rasilimali nyingi ambazo tunaweza kutumia kwenye maisha yetu ya kila siku. Rasilimali hizo ni kama Ardhi Madini Maji Fedha Muda …… Kati ya hizo rasilimali zote, muda ndio rasilimali ambayo ukiipoteza huwezi kuipata. Hivyo, unahitaji kuweza kuitumia vizuri rasilimali hii ya kipekee. Na leo nataka nikwambie namna ambavyo unaweza kujua thamani ya muda wako.…

  • Mwekezaji ni nani ?

    Je, Ni mtu kutoka nje ya nchi Kama ambavyo watu wengi wamekuwa wakiamini? Je, mtanzania mwenye kipato Cha kawaida anaweza Kuwa mwekezaji na anaweza kuwekeza wapi? 👇🏿👇🏿

  • Audiobook Ya Kitabu Cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA Sasa Ipo Tayari

    Moja ya kitabu muhimu ambacho nashauri usome ni kitabu Cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA. Kitabu hiki kimegawanyika kwenye sehemu kuu tatu.Sehemu ya kwanza inaeleza kwa Nini unapaswa kufikiri kikubwa lakini kuanza kidogo. Sehemu hii Ina sura sita. Sehemu ya pili ina inazungumzia kuhusu namna mafanikio makubwa yanavyoanzia kwenye tabia. Sehemu hii ina…

  • [ONYO] Kuanzia Leo Acha Kutumia Kauli Hii. Ona Kitakachotokea Ukiitumia

    Kauli yenyewe Ni Sina fedha/sina hela. Hii ni kauli ambayo moja kwa moja inakufunga na kukufanya usione upenyo wa kutoka. Ukisema sina hela maana yake unakuwa unainyima akili uwezo wa kufikiri nje ya boksi na kuona fursa gani zaidi unazoweza kupata. Badala ya kusema sina fedha, unaweza kujiuliza hivi hapa nawezaje kupata fedha? Au ni…

  • Uchambuzi Wa Kitabu Cha 5 Langues Of Love

    Kitabu: The 5 Languages of LoveMwandishi: Cary ChapmanMchambuzi: Hillary MrossoMawasiliano: +255 683 862 481 Ukiona hutaki kusikia chochote kuhusu upendo, mapenzi, mahusiano na maneno mengine ya kufanana. Basi ujue unahitaji sana kusoma kitabu hiki. Ndugu msomaji wa uchambuzi wa kitabu hiki, nakuahidi hiki ni kitabu bora sana kwako kukisoma. Mwandishi wa kitabu hiki amekiandika baada…

  • Unawezaje Kujiajiri kwa Mtaji Kidogo?

    Ebu fikiria kwamba ungekuwa wewe. Una mtaji kidogo na hutaki kuajiriwa ila una ndoto kubwa za kufanya makubwa hapa duniani. Una ndoto za kujenga biashara ambayo itakuwa kubwa na kukuingizia kipato kuliko hata kile ambacho ungepata kama mwajiriwa. Ungefanyaje kama ungekuwa na mtaji kidogo? Kuna watu ambao huwa wanasema kwamba ngoja nikaajiriwe kwanza, baadaye nikikuza…

  • Huu Ndio Ulevi Pekee Ambao Unapaswa Kuwa Nao

    Rafiki yangu mpendwa, najua umekuwa unasikia kuwa ulevi ni noma! Ulevi ni hatari. Mimi mwenyewe siyo kwamba napinga hili. Hapana, nakubaliana nalo kwa asilimia zote, ukweli ni wamba ulevi ni hatari kwa afya yako. Watu wanajiiingiza kwenye aina mbalimbali za ulevi. Kuna ambao wanaingia kwenye ulevi wa pombe, wengine madawa ya kulevya, wengine mitandao ya…

  • WEWE UBADILIKE PIA…

    Umewahi kuona hili … Watu wengi huwa wanapenda sana kuzungumzia mabadiliko ila ni wachache sana ambao huwa wapo tayari kuweka kazi ili kuhakikisha kwamba wanapata mabadliko ambayo wao wenyewe wanataka! Kwenye kila uchaguzi viongozi ambao huwa wanaahidi kuleta mabadiliko ndio ambao huwa wanapigiwa makofi yanguvu. Nataka nikwambie kitu rafiki yangu. na kitu hiki ni kwamba…

  • Huyu Ndiye Mtu Anayelipwa Kuliko Wote Hapa Duniani

    Rafiki yangu siku ya leo nataka nikueleze mtu ambaye analipwa kuliko wote hapa duniani. Hivi labda unafikiri mtu wa aina hii atakuwa yupi? Je, ni mtu ambaye amesoma sana?  Je, ni mtu ambaye amefanya kazi kwa siku nyingi kwenye kazi? Wengine wanafiriki kwamba mtu ambaye amefanya kazi kwa muda mrefu kwenye biashara au kampuni au…

  • Fanya Kitu Hiki Kimoja Tu Kwenye Biashara Yako (Funzo Kutoka Kwa Makampuni Makubwa Kama Google, Facebook Na Amazon)

    Unaendeleaje rafiki yangu wa ukweliLeo nataka tujifunze kitu kutoka kwenye mitandao mikubwa na makampuni makubwa unayoyafahamu. Na kitu hiki ni Kutengeneza mazingira ya kuwafanya wateja watumie muda mwingi kwenye biashara yako. Au kutengeneza (kuwa na) kitu ambacho kitawafanya watu wazidi kuja kwenye biashara yako kila mara. Hapa tujifunze kwa mitandao mingine mikubwa. Kila mara inatengeneza…

  • Unawezaje Kugundua Kitu Unachopaswa Kufanya Hapa Duniani?

    Mwishoni mwa mwezi uliopita nilikwenda Clouds Fm kwenye kipindi cha TEMINO. Kipindi kinachoendeshwa na Harris Kapiga pamoja na Adv. Henry Mwinuka. Sasa baada ya kipindi wakati nikiongea na Adv. Mwinuka kuna swali nilimwuliza, ndipo akawa ameniambia kwamba kipindi anaingia chuoni kuna vitu viwili alikuwa anapenda kufanya. Moja, ilikuwa ni utangazaji na pili ni sheria. Akawa…

  • Uchambuzi Wa Kitabu Cha UNFAIR ADVANTAGE

    Kitabu: UNFAIR ADVANTAGEMwandishi: Robert KiyosakiMchambuzi: Hillary MrossoMawasiliano: 255 683 862 481 UTANGULIZI Kama jina la kitabu hiki lilivyo, Unfair Adavantage, mwandishi anaeleza kwa undani namna alivyotoka kwenye ajira, namna alivyo anzisha biashara, namna alivyojifunza kwa undani masula ya kodi, hati fungani, mifuko ya pensheni, mifuko ya hifadhi ya jamii, mabenki na mifumo mingine ya kifedha,…

  • Kitu kimoja kitakachokusukuma wewe kuweza kufanya makubwa

    Habari ya upande wa huko rafki yangu wa ukweli, siku ya leo ningependa kukwambia kitu kimoja ambacho kitakusukuma wewe kuweza kufanya makubwa. na kitu hiki siyo kingine bali ni upendo. Upendo unapaswa kukusukuma wewe kufanya kitu kwenye maisha yako. Bila upendo sidhani kama kuna kitu cha maana ambacho utafanya hapa duniani. Upendo wa kazi Upendo…

  • Vitabu Vitano Ambavyo Kila Mfanyabiashara Makini Anapaswa Kusoma

    Kwanza kabla sijaandika mambo mengi sana siku leo. Ningependa kukwambia kwamba baadhi ya vitabu ambavyo ninaenda kukueleza hapa vinapatikana bure kabisa mtdanoni, hivyo, unaweza kupakua hivi vitabu bure. Labda unajiuliza unawezaje kupakua hivi vitabu bure mtandaoni? Hakikisha kwamba umeangalia hii video hapa, itakusaidia wewe kupakua vitabu hivi bure. Ila pia kuna vitabu vya kulipia ili…

  • Sababu 18 Kwa Nini Tunaandika Vitabu Na Kwa Nini Wewe Unapaswa Kuandika Cha Kwako

    Kuna watu wanafikiri kwamba wao hawawezi kuandika vitabu. na wengine wanafikrii kwamba ili uweze kuandika kitabu basi unapaswa kuwa na aina fulani hivi ya ugenius. Sasa siku ya leo nimeona siyo vibaya ngoja nikwambie sababu 18 kwa nini tunaandika vitabu na kwa nini wewe unapaswa kuandika kitabu chako. Je, upo tayari kuzijua hizi sababu. Kama…

  • Sala Muhimu Unayopaswa Kusali Kila Siku. Inaleta Matokeo Ya Haraka

    Unaendeleaje rafiki yangu wa ukweli. Najua umekuwa ukisali sala mbalimbali kwa siku nyingi. Ila leo ninataka kukwambia sala moja tu ambayo hujawahi kusali, na sala hii siyo nyingine bali kumwomba Mungu akupe usikivu. Uwe msikilizaji mzuri kuliko kuwa muongeaji mzuri. Tuna mdomo na masikio mawili. Ikimaanishabkuwa tunapaswa kuwa wasikilizaji wazuri kuliko kuwa waongeaji. Ila kinachotokea…

  • Kwa nini unajipunja hivyo?

    Wahaya wana usemi unaosema hivi, “endirira ekagaba emikira yayeyebwa”. Ukiniuliza tafsiri yake sijui ila nitakupa stori😂😂. Inasemekana hapo zamani za kale kulikuwa na mkutano wa wanyama. Kitu kikubwa kwenye mkutano huo ulikuwa ni ugawaji wa mikia. Mnyama aliyepewaa jukumu la kuwagawia wanyama wengine mikia ni mnyama mmoja ambaye kwa kihaya anaitwa NDIRIRA. Kiswahili chake sikijui…

X