Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Vitu viwili ambavyo hakuna MTU anapaswa kukuzidi

    Rafiki yangu, SIKU ya leo ningependa kukwambia vitu viwili ambavyo hakuna MTU anapaswa kukuzidi kwenye kuvifanya. Vitu hivi ni

    1. Kufanya kazi kwa bidii
    Acha watu wakuzidi kwenye mambo mengine yote ila wasikuzidi kwenye kufanya kazi kwa bidii.

    Kufanya kazi kwa bidii kupo ndani ya uwezo wako. Kwa hiyo kuanzia leo, acha watu wakuzidi kwenye vitu vingine Ila siyo kwenye kufanya kazi kwa bidii.

    2. Kujifunza kwa bidii
    Hiki Ni Kitu kingine ambacho hakuna mtu yeyote anapaswa kukuzidi kwenye kufanya. Hakikisha mara zote unazama kwenye kujifunza na kuelewa vitu kwa kiasi ambacho hakuna mtu mwingine mwenye elimu na uelewa mkubwa kukuzidi wewe.

    Kila SIKU jifunze. Jifunze kwa kusoma vitabu, jifunze kwa kuhudhuria semina na maonesho, jifunze kwenye kozi na maeneo mengine.

    Mara zote jifunze rafiki yangu. Hakuna mtu yeyote ambaye anapaswa kukuzidi kwenye kujifunza hata siku moja.

    NB: Kwa kuanzia, hakikisha umepata audiobook zangu tatu ili uanze kuzisikiliza. Audiobook zenyewe ni

    1. JINSI YA KUIFIKIA NDOTO ZAKO
    2. NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA
    3. MAISHA NI FURSA: ZITUMIE ZIKUBEBE

    Kila audiobook Ni 20,000/- Ila Leo nakupa ofa. Lipia audiobook moja nikupe audiobook nyingine mbili bure.

    Badala ya 60,000/- utaipia elfu 20,000 tu, nami nitakupa audiobook zote tatu.lipia Sasa kwa 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA. Baada ya hapo, nitakutumia audiobook zako.

    Umekuwa nami rafiki yako,
    Godius Rweyongeza
    0755848391

  • FANYA MAZOEZI

    Siku moja nilikuwa nasoma makala mtandaoni, kwenye makala hiyo mwandishi akawa amesema kwamba Michael Jackson ambaye ni gwiji kwenye muziki wa hiphop alikuwa ni mmoja watu waliokuwa wanafanya mazoezi kwa muda mrefu sana kabla ya kuonekana mbele ya watu. Kwa baadhi ya watu kitu hiki kilionekana cha ajabu sana, Ukilingananisha na kuwa Michael Jackson alikuwa akiimba na kucheza kwa namna ambayo ilikuwa inaonenekana ni njia ya asili. Inawezekanaje gwiji kama Michael Jackson awe anafanya mazoezi kwa muda mrefu hivyo?

    Na hiki ni siri ambayo nimegundua vijana wengi hawaielewi. Wapo wanaodhani kuwa ukishakuwa na kipaji peke yake basi anaweza kulala na kila kitu kikajipanga.

    Kama kuna kitu unapaswa kufahamu kwenye maisha yako ni kujua kwamba mazoezi ni jambo moja muhimu sana ambalo utapaswa kulifanyia kazi kwenye maisha yako. Tena utahitaji kuhakikisha kuwa unafanya mazoezi ya mara kwa mara kwenye kitu ambacho unafanya, kiasi cha kuweza kufikia ubobezi kwenye hicho kitu.

    Kila eneo lina vitu vyake vya kufanyia mazoezi. Kwa mwanasheria kuna vitu vyake ambavyo anapaswa kufanyia kazi maeozi.

    Mazoezi yanakujenga, mazoezi yanakuimarisha na njia ya wewe kupanda kutoka hapo ulipo kwenda unapotaka kwenda ni kufanya mazoezi.

    Tujifunze kwa wachezaji wa mpira wa miguu

    Wachezaji wa mpira wa miguu ni miongoni mwa watu ambao wanafanya mazoezi bila kuchoka. Kipindi ambacho ligi inakuwa imepumzishwa wenyewe wanaenda mpaka kambini. Na kambi hii inakuwa ni maalumu kwa ajili ya kufanya mazoezi ili waweze kufanya vizuri kwenye mashidano yanayofuata. Na siyo hilo tu, hata baada ya kuwa wamaenda kwenye mashidano huwa hawaachi kuanya mazoezi. Hiki kitu ndicho na wewe unapaswa kuwa nacho pia kwenye kazi na vile unavyofanya. Jijengee utaratibu wa kufanya mazoezi kwenye kazi au kitu unachofanya. Hakikisha kwamba unafanya mazoezi bila ya kuchoka.

    Mazoezi yanakuimarisha. Kadiri unavyokuwa unazidi kufanya mazoezi ndivyo unazidi kuimarika na kubobea zaidi.

    Mazoezi yanakuondolea hofur woga na wasiwasi. KILA MARA ukifanya mazoezi unairmarika na kukielewa kitu husika.

    Ebu fikiria unataka kuwa muongeaji mzuri mbele ya watu. (by the way, kuongea mbele ya watu ni kitu ambacho kinawashinda watu wengi sana na ni kituambacho unahitaji ukifahamu kwa uzuri sana).

    Sasa kitu hiki unaweza kukifanyia mazoezi kwa kuhakikisha kwamba kila siku unatenga nusu saa tu ya kufanya hivi. Kwenye hii nusu saa unaamua kuwa unaongea mbele ya watu na kuwasilisha mada yako ambayo umeandaa. Au hata kama hakuna mtu ambaye yuko mbele yako.

  • Hii ndiyo sababu kuu kwa nini unapaswa kutoa thamani kubwa kuliko mteja anavyokulipa

    Ni miaka kama mitano hivi imepita tangu nimegundua kanuni moja muhimu sana ambayo nimekuwa naitumia kwenye kila kitu ninachofanya. Na kanuni hii siyo nyingine bali ni kutoa thamani kubwa zaidi kwa mteja kuliko mteja anavyolipia.

    Tangu nimegundua kanuni hii nimekuwa naitumia kwenye vitabu vyangu vyangu vyote. Ambacho nimekuwa nafanya ni kuwa, kwa kitabu ambacho mteja analipia elfu ishirini, nahakikisha kwamba kinakuwa na thamani ya laki mbli na zaidi. hivyo, namwuzia mteja kitabu chenye thamani ya laki mbili na zaidi kwa elfu ishirini tu.

    Nafanya hivi siyo kwamba ninakuwa sijui, bali kwa sababu nataka mtu yeyote yule anayenunua kitabu au kupata huduma yoyote kwangu, apate thamani mara kumi zaidi na vile ambavyo analipia.

    Hii ni kanuni muhimu sana ambayo na wewe unapaswa kuizingatia na kuanza kuitumia kuanzia leo hii kwenye biashara yako. Hakikisha kwamba bidhaa au huduma unayoitoa kwa mteja inakuwa na na thamani mara kumi zaidi ya vile ambavyo anavyolipia.

    Tumia hii kanuni hata kwenye kazi. hakikisha kwamba unafanya kazi kwa viwango vikubwa mara kumi zaidi kuliko watu wengine wanavyofanya. Jitume mara kumi zaidi ya wengine. Soma vitabu mara kumi zaidi yaw engine. Jibrand mara kumi zaidi ya wengine. Hiki kitu kitakusaidia wewe kuweza kujenga jina lako na hata kujitofautisha.

    Unapaswa kufanya hivi, kwa sababu katika ulimwengu wa leo ni watu wachache sana ambao wanafanya hivi.  Wengi wanapenda njia za mkato za kupata mafanikio ila hawapendi kuweka kazi. kufanya kazi zaidi ya vile wanavyolipwa kujituma na kuwapa wateja thamani.

    Ukiweza kufanya hivi, maana yake utawateka wateja wako na kuwafanya waendelee kupata huduma kwako na hivyo kujenga jina katika namna ya kipekee ambayo hakuna mtu mwingine anaweza kujenga jina kama wewe.

    Kazi yako ya kufanya kuanzia leo hii ni kuanza kutoa thamani mara kumi zaidi ya vile unavyolipwa. Jiulize ni bidhaa ipi haitoi thamani mara kumi zaidi ya vile ninavyolipwa? Kama kuna bidhaa ya aina hiyo, basi anza kuiboresha ili iweze kutoa thamani kubwa zaidi kwa mteja kuliko vile anavyokulipa.

  • Hii ni tabia muhimu unayopaswa kuanza kuishi nayo kuanzia leo hii. (usishike simu kama kitu cha kwanza unapoamka asubuhi, na wala usishike simu kama kitu cha mwisho kabla ya kwenda kulala).

    Siku zinazidi kusogea kwelikweli. Mwaka uliokuwa mpya sasa hivi, tumeshaanza kuuaga taratibu. Siku siyo nyingi utaingia mtaani na kuanza kuzisikia nyimbo za krismasi zikipigwa. Ukiona hivyo, ujue kwamba mwaka unazidi kusogea na na siku siyo nyingi tutakuwa tunauaga. Lakini kabla mwaka huu haujaisha, kuna tabia ambayo ningependa uanze kuifanyia na kuachana nayo

    TABIA YA KUTOSHIKA SIMU YAKO KAMA KITU CHA KWANZA UNAPOAMKA ASUBUHI

    Kuna siku kulikuwa na kichekesho fulani hivi, kuwa mtu anaamka asubuhi kabla hata hajajua kama kichwa chake kimeshikana kiwiliwili chake anakuwa tayari ameshashika simu yake. Japo ni kichekesho ila kina ukweli mkubwa sana ndani yake. Asilimia kubwa ya watu, asubuhi kabla hata hajatoka kitandani, anakuwa tayari ameshika simu yake.

    Na ukifuatilia ni kitu gani cha msingi ambacho huyu mtu anakuwa anafanya na simu yake, huwezi kukiona, zaidi zaidi utakuta kwamba anajibu SMS hata zisizokuwa na maana. Au anaingia kwenye mitandao ya kijamii kuangalia watu wamekoment nini kwenye kitu alichopost jana yake. Sasa rafiki yangu, kuna kitu kimoja ambacho ningependa uweze kufahamu. Na kitu hiki syo kingine bali ni wewe kuepukana na kushika simu kama kitu cha kwanza unapoamka asubuhi.

    Ukiamka asubuhi, anza kwa kushukuru kwa kuiona siku nyingine mpya. Baada ya hapo anza kutahajudi.

    Kisha jiambie kauli chanya, kauli kama

    • Mimi ni bilionea.
    • Mimi ni sumaku ya fedha na fedha zinanifuata
    • Mimi ni mshindi na nimezaliwa kushinda.
    • Mimi nastahili kupata vitu vizuri na vizuri vimetengeezwa kw ajili yangu. Na nyinginezo nyingi.

     Katika huu muda hakikisha kwamba unapata maji ya uvuguvugu, kisha toka nje uvute pumzi kwa nguvu na ikiwezekana kukanyaga chini kwenye udongo il kuungana na asili na kufanya mazoezi. Baada ya hapo soma walau kwa dakika 20 tu.

    Itapendeza sana kama saa moja la kwanza baada ya wewe kuamka kama hutashika simu kabisa.

    Hii ndio kusema kwmaba ndani ya saa lako moja hili utakuwa umeweza kufanya makubwa, ikiwa ni pamoja na kupangilia asubuhi yako kwa kuweka to do list. Ukitoka hapo sasa unaweza kuendelea na mambo mengine.

    Hivyo hivyo wakati wa kulala. Usishike simu kama kitu cha mwisho kabisa kabla ya kulala. Tafiti nyingi zinaonesha kuwa unapaswa kushika simu walau saa mbili kabla ya kulala. Hii ni kwa sababu simu, ina mwanga ambao unaingiliana na usingizi. Hivyo, unaweza kujikuta kwamba unakosa usingizi muda mwingine, kumbe kinachokukosesha usingizi siyo kingine bali ni simu yako.

    Rafiki yangu, najua wazi kuwa simu ina manufaa mengi ila ninachokuomba ni kitu kimoja tu. Usishike simu kama kitu cha kwanza unapoamka asubuhi, na wala usishike simu kama kitu cha mwisho kabla ya kwenda kulala. Kila la kheri.

  • Je, kuuza vitu vya bei rahisi ni njia kutengeneza fedha nyingi kwa sababu bidhaa zinatoka kwa haraka?

    Mara kwa mara nimekuwa naandika kwenye blogu yangu na kutolea mfano namna ambavyo Bakhresa na Mo Dewji wanauza bidhaa za bei ya chini. mfano watu hawa unakuta wanauza mpaka viberiti, chumvi, pipi na vinginevyo ambavyo vinauzwa shilingi 50, 100, 200 mpaka 500.

    Nimekuwa nikitumia mfano huu kuhamasisha vijana mbalimbali kwamba wasidharau fedha kwenye maisha, badala yake kama mtu haoni sehemu yoyote ile ya kuanzia kwenye maisha kabisa, basi unaweza kuanza hata kwa kuuza kitu chochote kile cha bei ya chini kwa watu.

    Lengo likiwa ni kwamba kijana aanze kujishughulisha na hata kuingiza kipato. Nimekuwa nasema hivi kwa sababu, kwa mtu anayeanza, ni rashisi sana kwenda kwa watu kuuza bidhaa ya bei rahisi kuliko kwenda kwa watu kuuza bidhaa ya bei kubwa.

     Mtu anaponunua bidhaa ya bei ya chini labda (elfu moja), hajiulizi mara mbilimbili kama anapaswa kutoa fedha yake mfukoni au anapaswa kuendelea na maisha mengine. Tofauti na mtu anayenunua bidhaa ya laki moja. huyu kidogo ataanza kujiuliza na utahitaji kutumia nguvu kumshawishi.

    Sasa nadhani kutokana na msisitizo wangu huu wa kusisitiza vijana kuanza hata kuuza bidhaa za bei ya chini, umemfanya rafiki yangu kuuliza swali kama linavyoonekana hapa chini,

    Anasema je, kuuza bidhaa za bei rahisi ni njia rahisi ya kuvutia wateja na unaweza kutengeneza pesa nyingi pia kwa sababu huenda bidhaa zinatoka kwa haraka??

    Jibu ni hapana.

    Kuna njia kadha wa kadha za kutengeneza fedha na kuufikia utajiri kwa hiyo sidhani kama hii ni njia RAHISI.

    Unapokuwa unauza bidhaa za bei ndogo maana yake unavutia wateja wengi na matatizo yako yatakuwa mengi pia. Iko hivi, ukiuza bidhaa ya shilingi mia moja, utatakiwa kuuza kwa watu 100 ili ufikishe elfu kumi. Wakati huohuo mtu anayeuza bidhaa ye elfu tano, atatakiwa kuuza kwa watu wawili tu ili afikishe hiyo elfu kumi. Na kama unavyojua kushughulikana watu hakuwezi kukosa changamoto. Kwa hiyo, changamoto anazokuwa nazo mtu ambaye anauza bidhaa kwa watu mia moja ni tofauti kabisa na changamoto anazokuwa nazo mtu anayeuza bidhaa kwa watu wawili.

    Kuuza bidhaa za baei rahisi ni njia ya kuanza nayo kwa ajli ya kukuweka kwenye mwendo, lakini siyo kwamba ndiyo mwanzo na mwisho. Hata Bakhresa mwenyewe siyo kwamba anauza pipi ya 100 kama pipi ya 100. Badala yake hizo pipi zake anaziuza kwa jumla kwa watu wanaoenda kuuza kwa rejareja huko mtaani. Hivyo, yeye hashughuliki moja kwa moja na wale wateja wengi wanaonunua pipi ya 100. Bali wateja wachache wananunua mzigo wa bei kubwa.

    Kwa uzoefu wangu, wateja wanaoununua vitu vya bei rahisi huwa ni wasumbufu sana ukilinganisha na wateja wanaonunua vitu kwa bei kubwa.

  • KUWA ORIGINAL

    Siku moja mwaka 2016 wakati naanza uandishi nilikaa mezani na kufikiria kitu cha kuandika, ila nikawa nimeshindwa namna ya kuanza kuandika na hata nikawa sielewi nawezaje kuendelea kuandika. Baada ya kukaa kwa muda bila kuona matokeo yoyote yale, niliamua kuingia whatsap na nikawa nasoma makala za hapa na pale.

    Hapo ndipo nikakukutana na makala ya Daktari Makirita Amani, baada ya kuisoma na kuipenda, nikaamua kuondoa baadhi ya vipengele na kuifanya ile makala iwe ya kwangu.

    Nikabadili kichwa cha habari kidogo, nikaondoa na jina lake mwishoni na kitu chochote kile kilichokuwa kinaonesha kuwa yeye ndiye kaandika ile makala. Nikabandika jina langu, nikaanza kuisambaza hiyo makala kama ya kwangu. Nilikuwa na namba za watu kadha wa kadha, ambao walikuwa whatsap pia. Nikawatumia wote hao ule ujumbe wa ile makala.

    Baadhi ya watu wakaniuliza hii makala umeandika wewe, nikawa nimewajibu kuwa kweli nimeandika mimi. Na wengine wakatoa pongezi za hapa na pale ambazo kiuhalisia sikustahili kupokea.

    Sasa kwa bahati mbaya, sijui niseme bahati mbaya au nzuri. Ila naona hii ilikuwa ni habati nzuri. Katika kusambaza ile makala nikawa nimeituma na kwa Dkt. Makirita Amani mwenyewe.

    Siku hizo, whatsap haikuwa kama ilivyo sasa hivi ambapo unaweza kutuma kitu na kufuta. Kale ka kipengele ka delete for everybody hakakuwepo. Kama ulituma kitu kwa mtu kikaenda ulikuwa hauna namna ya kukifuta kabla hajakiona. Labda ukamwibie simu yake. Hahaha

    Baada ya muda kama ilivyotazamiwa ile makala Dr. makirita akawa ameisoma. Baada ya kuituma alinitumia ujumbe ambao nakumbuka ulikuwa unasema hivi,

    Godius hii makala mbona kama nimeaiandika mimi..

    Ukiendelea na tabia hii, hutajenga hadhira nzuri ya wasomaji. Maana watu watajua kuwa unachukua makala zangu na kuzifanya kuwa za kwako, kwa hiyo hakuna mtu ambaye atajisumbua kusoma maandiko yako. Badala yake atatafuta kusoma maandiko yangu.

    Kwa lugha nyingine ni kuwa hakuna mtu ambaye angejisumbua kusoma makala zangu ambazo nimekopi, na kuacha makala original za Dkt. Makirita. Kwa hiyo, nilipaswa kuwa original na kutoa kitu cha kwangu kama cha kwangu na siyo kukopi na kupaste.

    Huwa wanasema za mwizi ni arobaini, ila arobaini zangu zilifika siku hiyohiyo bila kuongeza siku ya ziada.

    Ilikuwa ni aibu kubwa kwa upande wangu, lakini ilibidi nianze kujikomaza kwa kuanza kuandika kidogo kidogo hata kama ninachokiandika siyo kizuri sana.

    Leo hii nafurahi sana kuwa nilikamatika siku hiyohiyo ya kwanza, la sivyo ningeendelea na hiyo tabia ya kuiba makala na kuzifanya kuwa za kwangu, mwisho wa siku ningelemaa na nisingeweza kuandika kitu cha maana.

    Kitu cha aina hii nimekuwa nakiona kwa vijana wengine pia ambao huwa wanaiba makala za baadhi ya waandishi huku wakizifanya kuwa za kwao. Ujumbe wangu kwao ni kuwa wanapaswa kuwa original, wakae chini na waanze kuandika, hata kama itakuwa kazi ngumu mwanzoni, ila kwa kujifunza na kufanya mazoezi endelevu, itafikia hatua ambapo watakuwa wanaandika maandiko mazuri na ya kipekee sana. ila wanapaswa kufanya mazoezi endelevu.

    Hakuna aliyezaliwa anajua kila kitu

    Hakuna aliyezaliwa anajua kila kitu. Ujuzi wowote ule unauona mtu anao, wewe pia unaweza kujifunza huo ujuzi na kuwa nao. Japo tangu zamani nilikuwa napenda kuandika, ila sikuwahi kuandika mpaka pale nilipoanza kujifunza kuandika. Mpaka leo hii naendelea kujifunza zaidi kuhusu uandishi kila kukicha. Kwenye vitabu ambavyo huwa nasoma kila mwezi, walau huwa kinakuwemo kitabu kimoja kuhusu uandishi. Achilia mbali kozi ambazo huwa nafuatilia hapa na pale na mafunzo mengineyo mengi.

    Kumbe unavyoona uandishi wangu wa leo, namna ambavyo napangilia mtiririko wa maneno na vitu vingine kama hivyo, siyo kwamba ni kwa bahati mbaya, bali ni mkusanyiko wa vitu ambavyo nimekuwa najifunza kwa siku nyingi, na bado sikomi kujifunza.

    Nikisoma kitabu cha mwandishi, sisomi tu ilimradi nimesoma, badala yake nakuwa naangalia ni kitu gani naweza kuondoka nacho kutoka kwenye hicho kitabu, lakini pia nakuwa naangalia mpangilio ambao mwandishi ametumia kwenye kuandika na namna gani ambavyo naweza kuutumia mimi pia kwa namna yangu. siyo kukopi kwake na kupaste.

    Makala zangu za kwanza hazikuwa bora sana, ila kwa sababu niliendelea kuandika ndio maana hizi za sasa hivi zinazidi kuwa bora zaidi. na hivyo kuendelea kunipa upekee zaidi.

    Kama kitu mtu anaweza kukipata kwa mwingne hakuna haja ya kuja kwako

    Kwa kitu chochote kile unachofanya, usiige na kukopi mtu fulani anavyofanya. Badala yake tafuta namna ya kujitofautisha wewe mwenyewe. Kama mtu anaweza kuona igizo fulani kwa mwingine ambaye ni OG, hakuna haja ya kuja kuangalia igizo kwako wewe ambaye unakopi. Kama mtu anaweza kusoma makala kwa mtu fulani ambaye ni OG, hakuna haja ya kuja kwako wewe ambaye ni unakopi.

    Kama mtu anaweza kusikiliza nyimbo kwa mtu fulani ambaye ni OG, hakuna haja ya mtu huyo kuja kwako ambaye ni gharasha. Kwa hiyo basi, tafuta uOG wako ulipo na ukuze huo.

    Hivi ndivyo unaweza kuishi maisha ambay ni original

    1.Usitake kuwa kama watu wengine. Kila mtu kaumbwa kwa ajili ya kusudi na jambo fulani, ukiamua kuiga maisha ya mtu mwingine maana yake huwezi kuwa wewe mwenyewe.

    2. usijilinganishe na watu wengine ambao wamefika sehemu au wameweza kufanyia kazi jambo fulani na kulifikisha kwenye viwango fulani. Mtu pekee ambaye unapaswa kujilinganisha naye ni wewe wa jana na wewe wa leo. Ni wewe wa mwaka jana na wewe wa leo hii

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro-Tz

    Subscribe kwenye channel yangu ya youtube kwa kubonyeza hapa

  • Maisha hayana fomula ila yanakuhitaji uwe na fomula

    Siku moja dereva mmoja wa bodaboda alikuwa anaendesha bodaboda yake kutoka eneo moja kwenda  jingine. Akiwa njiani, alipata ajali akawa ameanguka chini. watu walikimbia haraka kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wanamsaidia. Kitu cha kwanza watu walichoona ni shingo kupinda. Hivyo, walianza harakati za kumpa huduma ya kwanza na hapa waliamua kurudsha shingo kwenye eneo lake.

    Dereva akawa amejitahidi kuwaambia kwamba shingo yake ilikuwa haijapinda kugeuikia nyuma, badala yake alikuwa amevaa koti vifungo amefungia nyuma.

    Kwa vile alikuwa amepata ajali, watu walidhani hicho ni kiwewe tu cha ajali, hivyo dereva anaongea chochote tu kinachokuja kichwani mwake. Wakageuza shingo ii iangalie vifungo vilipo maana huko ndiko walijua kwa hakika ndipo shingo ilipaswa kuwa imeangalia, mwisho wa siku dereva akawa ameaga dunia.

    Tunachopata hapa ni kwamba maisha hayana fomula, ila wewe kama mtu binafsi unapaswa kuwa na fomula kwenye mambo yako. Kinachowakwamisha watu wengi kwenye maisha ni kwa sababu wanaishi maisha yasiyokuwa na fomula. Wanaishi tu ilimradi wameishi.  Unapaswa kuyaendea  maisha kwa fomula na haya hapa ni mambo yatakayokusaidia wewe kuwa na fomula

    Kwanza ni kuwa na malengo.

    Malengo ni fomula ambayo mtu binafsi unajiwekeaa. Hii ni fomula muhimu sana kwa sababu unapoweka malengo, maana yake unakuwa unajichagulia wapi unataka kwenda na wapi unataka kufika kwenye maisha. Unapoweka malengo maana yake, unakuwa unaamua ni kitu gani ambacho unataka kufikia kwenye maisha na kitu gani hutaki. Unatengeneza fomula ya maisha yako kwa sababu, bila ya hii fomula utajikuta kwamba unafanya kitu chochote kile kinachokuja mbele yako.

    Ila unapokuwa na malengo, maana yake unaachana na baadhi ya vitu na kuweka nguvu yako kwenye vitu vichache vyenye nguvu.

    Pili kwa kuipangilia kila siku yako na kila wiki yako.

    Hivi huwa unaweka to do list na kuorodhesha majukumu ambayo unapaswa kufanya ndani ya siku husika. Kama ulikuwa huweki hii orodha ya mjukumu yako ya kufanya ndani ya siku husika basi unapaswa kuanza kufanya hivyo kuanzia siku ya leo. Unajua kwa nini? Kwa sababu unapoweka to do list maana yake, unakuwa unachagua majukumu machache ambayo utafanya ndani ya siku husika na hivyo kuachana na majukumu yaliyo mengi.

    Tatu ni kwa kufanya tathimini. Tathimini ni pale ambapo unaangalia yale uliyoyafanya na namna yalivyokwenda. Ni pale unapoangalia na kuona kama uliyoyafanya yameleta tija na yanapaswa kuendelea kufanywa zaidi au la unapaswa kuishia hapo. maisha yako yanapaswa kuwa na tathimini ya siku, wiki, mwezi mpaka mwaka. Usiishi maisha bila ya tathmini. Hakikisha kwambna kila wiki na kila mwezi unakuwa na tathmini. Fanya tathimini yako na kila unapopata jambo la kuboresha, basi liboreshe na lifanyie kazi katika kuhakikisha kwamba  unazidi kuwa bora zaidi. lakini kikubwa zaidi unazidi kufanya maisha yako yawe na fomula.

    Kila la kheri

    Ni mimi rafiki yako wa ukweli

    Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro-Tz

  • Subscribe kwenye channel yangu ya YouTube Sasa.

    Rafiki yangu, hivi unajua kwamba huwa natoa baadhi ya mafunzo kwenye channel yangu ya youtube? Mara kwa mara nimekuwa nikitoa mafunzo huku. Na wewe unaweza kuyafuatilia kupiatia hapa.

    Subscribers kwenye channel hii walikuwa bado hawajafika hata elfu moja 😂😂, ila wiki hii ni muda wa kufanya hivyo, au wewe unasemaje?

    Bado watu 50 tu. wewe ukiongezeka sasa hivi watakuwa bado 49. Ebu tuhakikishe kwamba wiki tunafikisha subscribers elfu moja kwenye channel ya youtube. Bonyeza hapa kufanya hivyo.

    Tukutane tarehe 16 tukiwa na subscribers elfu na zaidi.

    Bonyeza hapa kufanya hivyo Sasa.

  •  Sababu Tano (05) kwa nini unapaswa kuukataa umasikini

    Limekuwa ni  kama jambo la kawaida kusikia watu wanajiita masikini, wanyonge. Kuna watu wanajisifia kuwa masikini kama vile kuwa maskini jambo la kheri au jambo la sifa. Kwa kulifahamu hili, siku ya leo ningependa kukupa sababu 15 kwa nini unapaswa kuukataa umasikini. Kweli kabisa, unapaswa kuukataa umasikini kwa nguvu zako zote.

    Kwanza kwa sababu umasikini dhambi.

    Ndio, umasikini ndio chanzo cha maovu. Kama hauna hela, utafikiria kwenda kuiba, kama hauna hela hela utafikiria kufanya maou ili upate chochote kile cha kuingiza mkono kinywani.

    Hakuna sifa yoyote ile kwenye umasikini ukatae kwa nguvu zako zote.

    Ukiwa hauna hela hata huduma nzuri hupati. Ukiumwa hospitali unapaona kama magereza wakati ni sehemu ya kwenda kupata tiba, unaogopa kwenda hospitali kwa sababu hauna hela.ila ukiwa na hela huduma zote nzuri zinakuwa kwa ajili yako. Watoto wako wanasoma shule yoyote unayotaka wewe, siyo shule ya mtaani kwako ambapo walimu wanafundisha kwa kuamua.

    Pili, umasikini hauwezi kukufanya usaidie jambo lolote lile

    Huwa kuna shughuli mbalimbali za kijamii ambazo watu huwa tunachangia, lakini huwezi kuchangia kwenye hizi shgughuli kama wewe ni masikini, sanasana utakuwa unazengea kwenye hiyo sherehe tu ili uone watu wanavyochanga ili na wewe uwanyanye hiyo pesa.

    Tatu, Umasikini unakunyima sauti

    Kinachotokea kwenye ngazi ya familia ndicho pia kinatokea kwenye ngazi za kimataifa. Nadhani umewahi kuona kwenye vikao, masikini anakosa sauti ya kuchangia hoja. Na hata akichangia hoja yake inaonekana ni ya kimasiikini na hivyo inatupiliwa mbali. Hivyo hivyo, kitu hiki ndicho kinatokea kwenye ngazi ya kimataifa. Nchi zetu zinashindwa kujihami na kuchangia hoja. Na hata zikichangia hoja, hoja zao zinakuwa hazina mashiko. Unajua kwa nini? kwa sababu, ni nchi masikini. Ili tuondoe umasikini wan chi, tunapaswa kuanza na mtu mmoja mmoja. Wewe ukiondoka kwenye umasikini, basi utakuwa umesaidia sana kuuondoa nchi hii kwenye umasikini. Anza leo hii mchakato wa kuondoka wewe mwenyewe kwenye umasikini

    Nne, Unatumia nguvu ileile kuwa tajiri kama ilivyo kuwa masikini

    Nguvu ileile unayoitumia kwenye kuwa masikini na kubaki masikini ndiyo nguvu ile ile inayohitajika ili kuwa tajiri. Sasa kwa nini usichague kuwa tajiri.

    Tano, Utajiri unakupa machaguo mengi

    Ukiw atajiri unakuwa na machaguo mengi sana ya kufanya kwenye maisha. Unaweza kununua kitu chochote kile unachotaka, unaweza kwenda popote pale unapotaka.

    Unaweza kuamua mtoto wako wasome shule yoyote. Unaweza kuamua kula chakula chochote, siyo kila siku ugali mlenda, halafu unadanngaya watu eti ooh, ugali mlenda ni mtamu sana. wakati hauna pesa ya kununua chakula kingine.

    Tafuta hela ili uwe na mchaguo mengi bila ya kuwa na ukomo.

  • Kwa Nini Watu Wenye Kipaji Hushuka Kiwango

    KIPAJI NI DHAHABU
    Rafiki yangu, nimeandika kitabu. Kinaitwa KIPAJI NI DHAHABU. Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa 0755848391 sasa

    Nadhani umewahi kusikia hili, kuwa wachezaji au wasanii au hata wawekezaji wameshuka viwango. Unakuta mtu mwanzoni alikuwa na kipaji na uwezo mzuri sana ambao alikuwa akiutumia kwa viwango vikuwa na viwango vya hali ya juu, ila kadiri siku zinavyoenda basi mtu huyo anazidi kushuka viwango mpaka kufikia hatua ambapo inadhihirika kuwa kiwango chake kimeshuka. Sasa kwa nini baadhi ya watu hushuka viwango?

    Kwenye makalaya leo tunaenda kuona sababu kwa nini baadhi ya watu hushuka viwango, na jinsi ambavyo wewe unaweza kuepuka hili.

    Moja ya kitu kinachofanya watu washuke viwango ni kukosa nidhamu ya kazi.

    Unakuta mtu alikuwa anajituma sana kwenye kazi mwanzoni alipoanza kufanyia kazi kipaji. Mtu yupo tayari kufanyia kazi kipaji chake kwa saa 15 na zaidi kila siku kwa siku saba za wiki bila ya kupumzika, ila pale anapoanza kufanikiwa na kuapata mafanikio mazuri anarelax na kusahau kabisa kuwa anapaswa kupambana kuhakikisha kuwa anaendelea kunoa kipaji chake.

    Tena wengine huwa wanapanda mpaka kufikia viwango vya juu kabisa, ila sasa kadiri ambavyo siku huwa zinaendelea basi huwa inafikia hatua ambapo huwa wanarudi nyuma kwa sababu ya kukosa nidhamu ya kazi. kama ambavyo tumeshaona mpaka hapa, ninachotaka ujue ni kuwa unapaswa kujituma kwenye kazi kama vile muda wote na mara zote wewe ni mchanga.

    Kingine ni kuendekeza Starehe sana kuliko kazi. Hiki ni kitu kingine ambacho kinawakumba watu wengi wenye vipaji. Mtu anapoanza kujulikana na kupata hela kutokana na kipaji chake, basi kinachofuata kinakuwa ni starehe. Sasa hiki kitu lazima baadaye kinawaponza watu kwa sababu starehe kwa vyovyote vile unapaswa kuzigharamikia.

    Njia ya kuondokana na hali hii ni kujifanya mara zote kama vile hauna pesa. kila ukipata fedha unaiwekeza sehemu ili tu uendelee kuweka juhudi zaidi na kupata fedha zaidi. Na kumbuka kuwa hapa nimeongelewa kuiwekeza fedha, wala siyo kitu kingine.

    Kuiga maisha ya baadhi ya watu. kadiri unavyokuwa unapanda viwango, ndio unakutana na watu wengine zaidi. sasa moja ya kitu ambacho kinaweza kukupumbza ni pale unapokutana na watu wengineambao wanaonekana kama hawaweki juhudi kwenye kazi ila wanapata matokeo mazuri. Hiki kitu kinaweza kukupumbaza na kudhani kuwa hata usipoweka juhudi wala kazi utapata matokeo mazuri tu. Ninachotaka kukwambia rafiki yangu ni kitu kimoja tu, na kitu hiki ni kuwa, juhudi na kazi kwenye kile unachofanya haziwezi kukuangusha.

    Lakini pia nataka ujifunze kutoka kwa jamaa mmoja ambaye niliwahi kusoma stori yake kwenye kitabu kimojawapo cha Robert Greene. Huyu jamaa alikuwa na kipaji ila alikuwa ni miongoni mwa watu ambao walikuwa wanafanya mazoezi sana nyuma ya pazia.

    Yaani, yeye alikuwa na fomula ambayo ni wachache sana wanaoifahamu. Fomula hii ilikuwa ni kwamba muda wa usiku alikuwa anachapa kazi na kujituma na kufanya mazoezi yote ambayo alikuwa anapaswa kufanya.

     Alikuwa anajituma sanasana nyuma ya pazia wakati wa usiku kiasi kwamba hakukuwa na mtu ambaye alikuwa anajituma kwa viwango kama vya kwake. Ila muda wa mchana alikuwa anajidai kama mla bata vile. Yaani, muda wa mchana alikuwa anarelax na kutulia. Ulipokuwa unafika wakati way eye kufanya maoonesho, alikuwa kiyafanya vizuri kiasi kwamba watu walikuwa wanashangaa kwa namna ambavyo alikuwa akifanya vizuri sana.

    Baadaye sana ndipo wachache walikuja kugundua kuwa huyu jamaa alikuwa akifanya mazoezi ya nguvu sana muda wa usikua na na kupumzika muda wa mchana. Hapa ninachotaka kukwambia siyo kwamba ufanye mazoezi muda wa usiku na muda wa mchana ulale, la hasha! Ila ninachotaka kukwambia ni kuwa unapaswa kufanya mazoezi ya kutosha nyuma ya pazia. Ili pale utakapofika muda wa wewe kuonekana mbele ya watu basi unafanya vizuri sana.

    Kitu kingine kinachowakwamisha watu wenye kipaji ni kujiona kwamba wameshafika, wakati safari yao ikiwa bado tu. Yaani, yale mafanikio ya muda mfupi yanamfanya mtu anafikiri kwamba tayari amefika wakati safari yake bado inaendelea.

    Rafiki yangu naomba kujua ni kitu gani ambacho kinakukwamisha wewe kwa muda huu. Ebu niambie hapa chini kwenye sehemu ya maoni.

    Makala zaidi za kusoma

X