Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Uchambuzi wa Kitabu: The Leader Who Had no Title (Kiongozi Asiye na Cheo); Mambo 200 Niliyojifunza katika kitabu hiki.

    Mchambuzi: Hillary Mrosso
    Mawasiliano: 255 683 862 481

    Utangulizi
    Dhana ya uongozi imekuwa na maana nyingi, na watu wengi hawajui maana halisi ya uongozi, wengi wameshindwa kufanya makubwa, wengi wameshindwa kufanya maamuzi muhimu kwenye maisha yao kwasababu wanajiona hawapo kwenye nafasi ya kufanya hivyo. Mwandishi wa kitabu hiki, Robin Sharma anaweka wazi maana halisi ya uongozi, amefafanusha kwa kina umuhimu na nguvu ya uiongozi katika maisha ya kila binadamu, pia ameeleza dhima kuu ya ujumbe wake uliobeba kitabu hiki kuwa ili ufanikiwe na kufanya mambo makubwa huitaji cheo wala nafasi za uongozi, unahitaji tu kujitambua na kutumia nguvu ya uongozi iliyolala ndani yako ili ikusaidie kuwa kiongozi kwako mwenyewe na kwa jamii nzima. Karibu katika uchambuzi wa kitabu hiki tujifunza mambo 200 niliyoyaona katika kitabu hiki.

    1. Kila mmoja wetu amezaliwa na uwezo mkubwa wa kipekee sana, lakini wengi wanakufa wakiwa hawajautumia ukuu na upekee waliozaliwa nao.
    2. Watu wengi wanadhani wameshafanya kila walichotakiwa kufanya, wameshatumia kila uwezo, na vipaji walivyo navyo, ukweli ni kwamba kama bado unaishi bado kuna mengi makubwa unaweza kuyafanya zaida hayo uliyoyafanya.
    3. Usiruhusu ukaja kuwa na majuto kwenye maisha yako ya baadaye kwa kushindwa kufanya vitu muhmu ulivyotakiwa kuvifanya wakati huu. Mara nyingi ni rahisi sana kuchukulia mambo poa, kupuuzia vitu kwa kuwa vipo na vinaonekana kila wakati.
    4. Kama wazazi wako wote wapo, fanya kila unachoweza na kilichopo kwenye uwezo wako wote kuwafanyia mema, kuwaheshimu, kuwatembelea, kuwajali, usipofanya hivyo utakuwa mtu wa majuto wazazi wako watakapoondoka hapa duniani.
    5. Usomaji na kujifunza kupitia vitabu unakufanya kuwa mtu bora na inafungua milango mingi hata ile ambayo ulidhani haipo, inakufungulia dunia ya fursa, furaha, amani na kujiamini, kamwe usiache kujifunza kupitia usomaji wa vitabu.
    6. Mwandishi wa kitabu Robin Sharma anasema, watu bora ni wale wenye maktaba kubwa. Maana yake wanajielimisha kila wakati, wananunua vitabu na kuvisoma na kupata maarifa bora ambayo yanawafanya wawe watu bora.
    7. Huitaji cheo chochote ili ufanye makubwa kwenye maisha yako. Mwandishi wa kitabu hiki anasema ili ufanye makubwa kwenye maisha yako unahitaji tu kuwa binadamu anayepumua.
    8. Usisubiri uwe na cheo ndio uanze kufanya makubwa kwenye maisha yako, huitaji kuwa meneja, mkurugenzi, mbunge, diwani, au afisa fulani ili ufanye makubwa.
    9. Kama kuna ujumbe mkubwa kwenye kitabu hiki basi ndio huu; huitaji kuwa na cheo chochote kuwa kiongozi bora, huitaji cheo ili uwe na mafanikio.
    10. Mwandishi Robin ansema, kamwe usitetereshwe, au kuyumbishwa na mambo ya vyeo, maana vyeo ni mambo ya muda tu, huja na kuondoka, lakini unatakiwa kuwa kiongozi asiye na cheo.
    11. Mwandishi anasema, wakati mwingine kupotea njia ndio njia sahihi ya kuifahamu njia sahihi. Kuna nyakati zinapita kwenye maisha yetu na tunajiona tupemepotea na hutana tena msimamo, lakini huu ndio wakati sahihi wa kujua kwa usahihi tuhachotakiwa kufanya.
    12. Kuna wakati maisha yanatakiwa yakuangushe, yakuumize na kukukandamiza chini, ili uinuke na kujijenga na kujiimara kuwa mtu bora na imara.
    13. Chagua kwenye maisha yako kuwa hutayaendesha maisha yako kwa kufuata vibandiko au lebel kama vile umri, vyeo au nafasi za uongozi. Ishi maisha yako bila kujiwekea mipaka au ukomo wowote.
    14. Njia nzuri ya kufanya kampuni au shirika lolote kuwa na ufanisi mkubwa ni kuwajengea uwezo wa kiuongozi wafanyakazi wote, na kuwafundisha falsafa ya kuongoza bila cheo au wanaweza kufanya makubwa bila kuwa na cheo cha uongozi.
    15. Ili uwe kiongozi sio lazima uwe na cheo, uongozi wa kweli unahusiana kidogo sana na cheo, uongozi wa kweli ni uongozi usiozingatia vyeo ili kufanya mambo.
    16. Huitaji kuwa na cheo cha uongozi ndio ufanye maamuzi muhimu kwenye maisha yako. unaweza kufanya maamuzi bora na yenye maana kwenye maisha yako bila kuwa na cheo chochote.
    17. Namna tunavyoelewa na kufikiri kuhusu dhana ya uongozi ni muhimu sana, maana uongozi ndio huamua mafanikio ya mtu binafsi na ya kampuni au shirika.
    18. Kila mmoja wetu anatakiwa kuwajibika katika kutoa matokeo bora sana, na endepo kila mmoja atafanya kilicho bora, kila kitu kitakachofanywa kitakuwa bora sana na shirika litakuwa na huduma bora.
    19. Kila mtu ndani ya timu anatakiwa kufanya na kuamua kama mkurugenzi wa shirika, kila mtu ajione ana wajibu wote wa kufanya makubwa na kufanya maamuzi muhimu kwenye maisha yake na maisha ya shirika au kampuni bila kutegemea vyeo kufanya hivyo.
    20. Mahali popote ulipo ndio mahali sahihi pa kuonyesha uongozi wa kweli, ni sehemu ya wewe kuchanua na kutumia vipawa vyako kufanya makubwa. Na huitaji cheo cha uongozi kufanya hayo.
    21. Kila mtu anatakiwa kutengeneza ushawishi kwa chochote kila anachokifanya, kazi zako unazozifanya zinatakiwa kuwa kazi bora sana, ili ziweze kufanya maisha ya wengine kuwa bora kabisa.
    22. Kati ya uwezo mkubwa tulionao kama binadamu ni namna tunavyoweza kuchagua kuchukuliana na hali zozote za mazingira ambayo tunajikuta tupo ndani yake.
    23. Uongozi hauhusiani na mahali ulipo, au yale unayoyapata, uongozi ni zaidi sana namna unapofanya maamuzi muhimu kwenye maisha yako.
    24. Uongozi ni huduma bora unazotoa kwa ajili ya kuinua na kuyafanya maisha ya wengine kuwa bora zaidi, maisha ya wote wanaokuzunguka yanatakiwa kuwa bora kwasababu ya huduma na maisha unayoishi kama kiongozi.
    25. Kwa jinsi usivyojali kupata na kupokea mambo mengi ambayo wengi wanayataka wakiwa kazini, ndivyo unavyotengeneza nafasi kubwa ya kuyapokea mambo hayo.
    26. Wengi wanaingia kazini wakiwa na mitazamo kwamba endapo watapata nafasi ya uongozi au cheo ndio wataanza kufanya makubwa, wataanza kutoa huduma bora, na ndio watajisukuma zaida kufanya kazi kubwa ili kuleta matokeo makubwa.
    27. Mwandishi wa kitabu hiki anasema, namna nzuri ya kudhihirisha ubora wako wote sio lazima upewe cheo, au upewe fedha, au mali au zawadi, fanya makubwa bila cheo chochote, fanya makubwa bila kusubiria cheo.
    28. Mambo mengi kwenye maisha yetu tunayapata kwa kulipa gharama kwanza. Ni mghahawani tu ndio utapewa huduma ndio ulipie baadaye.
    29. Usijali kuhusu kupata zawadi au mambo mazuri kwenye maisha yako, kama unafanya mema, kama unajisukuma, kama unajitoa kufanya yaliyo bora usijali kuhusu matokeo maana yatakuja tu.
    30. Mwandishi anasema, hakuna jambo jema utakalolifanya litaenda bure, hivyo wekeza kwenye kufanya kazi, wekeza na chukua hatua za kufanyia kazi ndoto zako kila siku maana matokeo yake yatakuja tu.
    31. Tukijifunza kwa watu waliofanikiwa na kufanya makubwa hapa duniani kama vile Roosevelt, Mandela, Thomas Edson au Albert Einstein hawakufanya makubwa kwasababu ya fedha, au mali, walifanya makubwa kwasababu ya kiu ya kuleta mabadiliko na kuona maisha ya binadamu yanakuwa bora hapa duniani.
    32. Hapa haimaanishi kuwa fedha haina umuhimu kwenye maisha, pesa ina umuhimu sana kwenye maisha yetu, pesa itakupa uhuru, pesa itakupunguzia msongo wa mawazo, pesa itakufanya utoe huduma bora kwa unaowapenda, pesa itakufanya pia uwe na vitu vizuri na muhimu.
    33. Kuna msemo maarufu unasema, njia nzuri ya kuwasaidia masikini ni kutokuwa mmoja wao. Pesa itakufanya uwasaidie masikini.
    34. Siku zote za maisha yako kumbuka, huitaji cheo ili kuwa kiongozi, huitaji cheo au nafasi ya uongozi ili uonyeshe kuwa wewe ni kiongozi.
    35. Uongozi sio kwa ajili ya wakurugenzi, maafisa wa jeshi, au watu wanaoongoza mataifa, uongozi ni kwa ajili ya kila mtu.
    36. Kitu pekee unachotakiwa kuwa nacho ili uweze kukidhi vigezo vya kuwa kiongozi ni pumzi, unahitaji tu kuwa binadamu anayepumua.
    37. Tunatakiwa kukumbushwa zaida kuliko kutoa maelekezo, kwa asili binadamu hawapendi maelekezo, hawapendi amri, hivyo njia nzuri ya kufikisha ujumbe muhmu kwa mtu mwingine ni kuutoa kwa namna ya kumkumbusha.
    38. Uongozi sio kitu kigumu na maalumu sana ambacho kinapatikana kwa watu wachache waliotunukiwa shahada katika vyuo vikuu bora duniani kama Harvard.
    39. Katika ulimwengu tulionao sasa umejaa mambo mengi na kuendeshwa kwa mihemuko na hisia nyingi, kitu pekee kinachoweza kutufanya kufanya maamuzi sahihi na kuchukua hatua sahihi ni kuwa na uongozi makini na shahihi.
    40. Kila eneo la maisha yetu ili liwe bora, tunahitaji kusimika roho ya uongozi. Bila uongozi hakuna mipango, hakuna, malengo, hakuna mafanikio; uongozi ndio kila kitu.
    41. Ili tufikie kilele cha juu sana cha mafanikio kwenye maisha yatu, tunatakiwa kuonyesha uongozi kwenye afya zetu, kwenye mahusiano yetu, kwenye masuala yetu ya kifedha, na kwenye jamii yetu.
    42. Mwandish Robin Sharma amesisitiza sana kuwa, uongozi anaomaanisha hapa ni uongozi binafsi. Kwasababu usipoweza kujiongoza mwenyewe kamwe hutaweza kumuongoza mwingine.
    43. Jiongoze wewe mwenyewe kwanza kwa mafanikio makubwa, ndio utaweza kuongoza wengine kwa mafanikio makubwa.
    44. Tafuta kwanza nguvu zilizo ndani yako zikusaidie kabla hujaenda kutafuta nguvu za watu wengine kukusaidia. Jiangalie ndani yako, kama kuna kitu unachoweza kukitumia ili kikusaidie kuwa mtu bora basi fanya hivyo kwa nguvu zako zote.
    45. Mwandishi anasema wanaoishi kwa falsafa hii ya uongozi bila kuwa na cheo wana tabia ya kuamka mapema zaidi ya wengine wanapoenda kuianza siku yao.
    46. Benjamin Franlin, moja ya watu mashuhuri kuwa kuisha hapa duniani aliwahi kusema, kutakuwa na muda mwingi wa kulala baada ya kufa, hivyo usione kama unakosea unapojiongezea muda wa kufanya makubwa kwenye maisha yako wakati ukiwa hai.
    47. Jifunze kuamka mapema zaidi, ili upate muda mwingi wa utulivu kufanyia kazi ndoto na maono yako yanayokukosesha usingizi. Ukiweza soma kitabu cha 5 AM CLUB, ni kitabu bora sana kinachoeleza kwa kina tabia ya kuamka mapema umuhimu wa kuamka mapema na kuanza kuziishi ndoto zako, tafuta nakala yako uisome.
    48. Ndugu msomaji wa uchambuzi wa kitabu hiki tambua kuwa ni rahisi sana kulala sana, ni rahisi sana kutumia masaa mengi kitandani, mwandishi anasema tunapoteza muda wa thamani sana kwa kulala sana, amka mapema upambanie ndoto zako.
    49. Oneza muda wa kufanyia kazi ndoto zako kwa kujizoeza kuamka mapema kila siku, utaongeza masaa mengi kwa wiki kwa mwaka. Jilazimishe uamke mapema kabla ya dunia haijaamka ili ufanye makubwa.
    50. Ukiamka mapema zaidi kila siku, labda saa moja kabla ya muda wa zaida, kwa mwezi utakuwa una masaaa 30, sawa na wiki nzima, ambayo ni mengi sana na unaweza kuyatumia kufanyia kazi ndoto zako.
    51. Kama kiongozi unatakiwa kuboresha kila kitu kwenye maisha yako, kuwa na shauku na njaa kali ya kuboresha kila eneo la maisha yako, fanya hivyo kila siku.
    52. Wakati mwandishi anajaribu kuelezea umuhimu wa muda na Matumizi ya vipawa vyetu, ametumia muda mwingi kuelezea dhana ya kiongozi asiye na cheo maeneo ya makaburini ili kutukumbusha muda wetu wa kukaa hapa duniani ni mchache sana na pia tunatakiwa kutumia vipawa vyetu na uwezo tuliopewa kuboresha maisha ya dunia na sio kwenda navyo kaburini.
    53. Makaburi yanatukumbusha kuwa ndio sehemu ambayo tutakuja kuishia baada ya kuishi hapa duniani, hivyo, vitu vyote tulivyodhani ni muhimu maishani kama vile vyeo, fedha, nafasi kwenye jamii havitakuwa na maana tena.
    54. Kitakachokuwa na maana wakati huo ni endapo uliishi kama kiongozi bila kujali vyeo, utakufa kwa amani endapo utajua ulitumia vipawa vya uongozi vilivyo ndani yako ili uboreshe maisha yako na maisha ya wanaokuzunguka.
    55. Wakati mwingine inafaa kufikiria kuhusu kifo na siku zako za mwisho, maana zitakufanya ujitafakari na kuamsha moto wa kufanyia kazi maono na ndoto zilizopo ndani yako.
    56. Mwandishi wa kitabu hiki amefafanua baadhi ya mambo yanayoleta majuto siku zako za mwisho hapa duniani, (The 10 Human Regrets).
    57. Utafikia siku zako za mwisho ndipo utajuta kuwa ulipata nafasi na fursa nyingi nzuri za kuboresha maisha yako na kutumia vipawa vyako.
    58. Utakuja kujuta sana endapo utafika mwisho wa maisha yako, na kukumbuka hakuna hata mtu mmoja uliyemvutia na kumfanya bora kwa mtindo wa maisha uliyoishi.
    59. Utafikia siku zako za mwisho hapa duniani ukiwa na uchungu mwingi na majuto kwasababu ulishindwa kuchukua hatari zilizokuja kwako na hivyo hakuna makubwa uliyofanya na maisha yako hapa duniani.
    60. Utajutia sana utakapofika katika siku zako za mwisho hapa duniani, kwasababu ulishindwa kuishi kwa ujasiri, na hukuwa mfano bora kwa wengine.
    61. Kila mtu anatengeneza maisha anayoishi, hivyo amua kutengeneza maisha yako yawe jinsi unavyotaka kulingana na maono na ndoto zako.
    62. Jehanamu kubwa iliyopo hapa duniani ni kwa watu ambao wanakufa bila kuonyesha na kutoa ukuu na vipawa walivyozaliwa navyo. Wanapeleka utajiri na ukuu wao kaburini badala ya kuutumia wote kuibariki dunia na kuifanya kuwa sehemu bora sana ya kuishi.
    63. Siku zote mafanikio yanakuja kwa kuwa na nidhamu kubwa ya kufanya na kuchukua hatua ndogo ndogo kila siku bila kuacha. Tabia ndogo ndogo za kuleta mafanikio ni rahisi sana kuzifanya kila siku, ndio maana watu wengi wanafikiri haziwezi kuleta mafanikio kwa haraka, hivyo wanaachana nazo hawazifanyi.
    64. Mwandishi anasema, mafanikio yanahusisha vitabia vidogo vidogo tunavyoweza kuviishi kila siku bila kuacha. Ukiwa na tabia sahihi na ukaziishi kila siku bila kuacha, vinaleta matokeo makubwa sana baadaye, usipuuzie tabia njema kwenye maisha yako.
    65. Mwandishi ametolea mfano wa mkulima ambaye huotesha mbegu zake kila wakati, huandaa shamba lake kila wakati, hupalilia shamba lake kila wakati humwagilia maji shamba lake, na hatimaye wakati wa mavuno hufika na huvuna alichopanda, ndivyo inavyotakiwa kuwa kwenye tabia zetu za mafanikio.
    66. Kuna wakati unaweza juhudi sana, kuna wakati hakuna matokeo yataonekana, kila kitu kitakuwa giza, hapo ndipo unapohitaji uvumilivyo maana mchakato wa ukuaji huchukua muda. Tujifunze kwa wakulima.
    67. Kushindwa na kutofikia mafanikio makubwa ni matokeo ya kupuuzia hatua ndogo ndogo tunazoweza kuzichukua kila siku. Hakuna utakacho kifanya kisilete matokeo, hivyo wekeza kwenye kufanya mambo ambayo unataka yakuletee matokeo bora. Rafiki yangu Godius Rweyongeza ameandika kitabu “Nguvu ya Vitu Vidogo Kuelekea Mafanikio Makubwa” ni kitabu kizuri sana kinachoelezea umuhimu wa kufanya vitu vidogo ili kuleta mafanikio makubwa, kitafute ukisome.
    68. Inatakiwa ufikie mahali kwenye maisha yako uachane kabisa na kutoa sababu kwanini huwezi au hutaki kufanya mambo yanayoweza kukuletea mafanikio kwenye maisha yako. Izike kabisa tabia ya kutoa sababu kwanini huwezi kuishi tabia za mafanikio.
    69. Amua kuwa kiongozi kwako mwenyewe, shika hatamu na jiwekee utaratibu mzuri wa kuishi maisha yako, jisimamie na jiongoze bila huruma ili utekeleze mambo muhimu ya kukuletea mafanikio. Jiongoze kwa mafanikio kwa kutumia nguvu ya uongozi iliyopo ndani yako.
    70. Kuna nguvu kubwa sana ya uongozi na ushawishi ndani yako, amua kuitumia nguvu hiyo juu yako mwenyewe, kujiongoza na kujishawishi ili ufikie ndoto zako. Hapa huitaji cheo chochote kuwa kiongozi kwako mwenyewe.
    71. Tuishi siku zote tukijua, siku zetu zinahesabika na miaka yetu ya kuishi hapa duniani ni michache, tufanye tunayotakiwa kuyafanya kwa ubora mkubwa, tujitoe na kujisukuma kila siku kufikia malengo yetu kabla mwisho wa siku zetu kufika.
    72. Kuna wakati mabadiliko ya kweli kwenye maisha yanahusisha zaidi yakigusa hisia zetu, badala ya kuwa na mlolongo wenye mantiki, moyo ukiguswa ndio huleta mabadiliko, na sio kichwani tu.
    73. Unapokuwa na nguvu nyingi za kuamua na kufanya maamuzi, ndivyo hivyo maamuzi yako yanakuwa na nguvu. Jitambue kama kiongozi mkuu na una nguvu nyingi za kuyaamulia maisha yako.
    74. Utakuwa na amani sana pale utakapofikia mwisho wa siku zako za kuishi hapa duniani endapo utajua ulitumia kila kipawa ulichopewa na Mungu kwa ukamilifu, na umeacha kazi bora hapa duniani kwa ajili ya kuboresha maisha ya watu wengine.
    75. Utakuwa na mwisho mwema wa siku zako za kuisha hapa duniani pale utakapojua ulifanya mambo yote ambayo yalikuwa mbele yako kwa viwango vya juu sana na kwa umakini wa hali ya juu.
    76. Utakuwa na mwisho mwema wa siku zako hapa duniani pale utakapokumbuka uliinua maisha ya wengi, uliboresha maisha ya wengi na uliwasaidia wengi kwa kazi zako, vipawa vyako na mali zako.
    77. Utakuwa na mwisho wenye furaha plae utakapokumbuka jinsi ulivyopitia nyakati nyingi za giza, hofu, mashaka, kushindwa, kuanguka lakini kila ulipoanguka uliinuka na kusonga mbele kwa ujasiri.
    78. Utakuwa na amani sana katika siku zako za mwisho pale utakapokumbuka kuwa hukusubiria cheo au nafasi yoyote ya uongozi ili ufanye makubwa kwenye ofisi, shirika au kwenye jamii yako.
    79. Utajishikuru sana katika siku zako za mwisho hapa duniani endapo hukutegemea cheo au nafasi ya uongozi mahali popote ili uishi kama kiongozi au ufanye mambo yako kama kiongozi. Utajishukuru kwa kuwa ulikuwa kiongozi asiye na cheo.
    80. Kuna kauli moja yenye nguvu sana iliyowahi kusemwa na Dr. Martin Luther kuhusu kufanya mambo kwa ubora wa viwango vya juu, alisema, kama mtu ameitwa kama mfanya usafi wa mtaa, anatakiwa kufanya usafi kwa viwango vya juu sana kama Michelangelo au Beethoven na sanaa yake ya muziki, au kama mshairi maarufu Shakespeare na mashairi yake. Anatakiwa afanye usafi wa mtaa kwa ubora kiasi kwamba jeshi lote la malaika wa mbinguni na duniani watasimama na kusema, hapa anaishi mfanya usafi bora wa mtaa aliyefanya kazi yake kwa ubora sana.
    81. Mwandishi amemnukuu Dr. Martin Luther kutuonyesha kuwa tunatakiwa kufanya kwa ubora wa viwango vya juu sana mambo yote ambayo yataangukia kwenye mikono yetu. Hata kama ni kazi ndogo kiasi gani, jifunze kujitoa kwa uwezo wako wote kuifanya kwa viwango bora sana.
    82. Pale unapodhani huna nguvu zozote hapo ndipo unapopoteza nguvu zako. Wengi wanajiona dhaifu, hawana uwezo wa uongozi, na wana dhana kuwa kiongozi lazima awe na cheo kama vile meneja, afisa fulani hivi au watu wenye vyeo serikalini.
    83. Ulikuja duniani bila cheo chochote na utaondoka duniani bila cheo chochote, lakini uliumbwa na silika ya uongozi ndani yako, kuna nguvu zote za kukufanya kuwa kiongozi bora unayetamani kuwa. Na ili kufikia viwango vya juu vya utendaji huitaji cheo, unahitaji kutumia nguvu ya asili ya uongozi iliyopo ndani yako.
    84. Mafanikio kwenye maisha hayaji tu kwasababu una nyota nzuri, mafanikio yanahusisha sana juhudi za makusudi za kila siku. Huwezi kujikuta tu umefanikiwa bila kufanya kazi, bahati kwenye maisha zinatengenezwa kwa juhudi na hatua za kila siku.
    85. Tumia maisha na muda wako hapa duniani kufanya vitu vyenye maana, usikazane kushilikilia vitu vya kupita ukaacha kuwekeza kwenye vitu muhimu zaidi, kama vile tabia yako, na kuboresha ujuzi wako ili uwe mtu bora sana.
    86. Ondokana na maoni ya watu kuhusu wewe, watu wataendelea kuwa na maoni juu yako hata ufanye jambo zuri kiasi gani. Hivyo usijali kuhusu maoni ya watu, jishindanishe wewe na wewe mwenyewe, jifanye bora kuliko jana.
    87. Hata kama jamii nzima inakupongeza kwa kufanya mambo mazuri na makubwa, hutakiwi kuishia hapo, unatakiwa kuendelea kutoa ubora na kujisukuma kila siku ili ufanye makubwa zaidi ya unayoyaona umefanya.
    88. Usipokuwa na imani imara juu yako, usipojiamini na kujikubali, ni rahisi sana kuyumbishwa na jamii, unatakiwa kuwa na imani thabiti kwako mwenyewe kuwa bado unaweza kuzalisha matokeo chanya kwenye maisha.
    89. Kama vile mwanamahesabu maarufu Albert Einsein alivyowahi kusema, kama unafanya makuu kwenye maisha yako, utakutana na upinzani mkubwa sana kutoka kwa watu wenye mitazamo duni.
    90. Mwandishi anasema kama watu hawaelewi unachotaka kukifanya, kwanini uwaruhusu wa kuvute chini, usiwaruhusu wakuangushe maana hawajui maono na ndoto zako. Tumia mawe wanayokurushia kujengea malengo yako.
    91. Wakati mwingine wanaotukosoa sana wanatukumbusha kuwa tunachokifanya kina maana sana na kinawaumiza, au ni kitu bora sana. Hivyo wakosoaji wanatufanya tusilale na tuendelee kupambania ndoto zetu.
    92. Vyeo vinaleta nguvu, lakini nguvu hii huondoka pale mtu anapokosa cheo. Suala la vyeo kwenye maisha lisikuumize kichwa, wewe wekeza nguvu zako kwenye kujifanya kuwa mtu bora na kiongozi bora kwako mwenyewe.
    93. Fikiria nguvu anayokuwa nayo mtu anapokuwa kwenye cheo cha ukurugenzi, au afisa wa juu, au waziri anaweza kuamuru hiki na kile. Lakini vyeo hivyo ni vya muda mfupi, hutakiwi kuwekeza kwenye vitu vya muda mfupi hivyo, wekeza kwenye kuwa kiongozi bora asiye na cheo.
    94. Kuna nguvu nyingi sana za uongozi ndani yako kuliko nguvu zilizopo kwenye vyeo unavyopewa, tuna nguvu nyingi za asili za kutufanya kuwa viongozi, nguvu hizi zipo ndani yetu, tumezaliwa nazo, nguvu hizi ni nyingi sana, nguvu hizi za ndani zina nguvu kuliko nguvu zilizopo kwenye vyeo vya kidunia.
    95. Mwandishi anasema, tukizitambua nguvu ziliyopo kwenye nguvu za uongozi ulio ndani yetu, hatutababaika na vyeo au nafasi za kuwa kiongozi tunazopewa na jamii. Vyeo vya uongozi tunavyopewa na jamii ni vya muda, na nguvu yake ni ya muda, lakini asili na nguvu ya uongozi wa kweli hauitaji cheo kudhihirika na kufanya makubwa.
    96. Mbaya zaidi ni kwamba nguvu hizi za uongozi zimelala ndani ya watu wengi, hazijadhihirika, hivyo watu hawajajitambua na wanafikiri uongozi wa vyeo vya kupewa na jamii ndio bora na una nguvu.
    97. Nguvu za asili za uongozi zilizopo ndani yetu haziwezi kuchukuliwa na mtu yoyote, na wala hazitengemei mambo yanayoendelea huku duniani. Ni nguvu takatifu, ni nguvu za asili, ni silika ya kweli tuliyoumbiwa na Mwenyezi Mungu, ni nguvu kubwa mno za kiutawala na kiumiliki.
    98. Kila binadamu aliye hai hapa duniani anahizi nguvu za uongozi ndani yake, na anaweza kwenda kwenye eneo lake la kazi na kuzidhihirisha kwa viwango vya juu; na huitaji cheo kufanya hivyo.
    99. Kila binadamu aliye hai hapa duniani ana nguvu za uongozi ndani yake za ushawishi, kuhamasisha, na kuwatia wengine moyo ili watumie vipawa vyao na kuwa mifano ya kuigwa; na huitaji cheo kufanya hivyo.
    100. Kila mtu aliye hai hapa duniani anaweza kuwa chanzo cha mabadiliko chanya licha ya mazingira hasi yanayomzunguka; na huitaji cheo kufanya hivyo.
    101. Kuna watu walikuwa na vyeo vikubwa kazini, kwenye mashirika, kwenye jeshi, na serikalini, na watu waliwaheshimu sana kwasababu ya vyeo na nafasi zao, lakini baada ya kuondoka kazini na kurudi mtaani walidhani watu watawachukulia na kuwaheshimu kama mwazo, jambo ambalo haliwezekani, hivyo kupelekea wengi kuwa na msongo wa mawazo na kukosa furaha.
    102. Haijalishi nafasi yako kazini, au unaishi kona gani ya hii dunia, bado una nguvu, haki na wajibu wa kudhihirisha haki yako ya kuzaliwa ambayo ni uongozi. Hakuna atakayekuzuia kuionyesha, ni wajibu wako kuifanya ifanye kazi.
    103. Kuongoza bila cheo ni falsafa ya kidemokrasia kwenye uongozi, maana inampa kila mtu nafasi ya kutumia nguvu ya uongozi iliyopo ndani yake kufanya makubwa bila kusubiria vyeo.
    104. Hakuna mtu hapa duniani asiye na umuhimu, na hakuna mtu mwingine hapa duniani kama wewe, upo wewe tu hapa duniani, hivyo ishi kwa falsafa ya kuongoza bila cheo ili ufanye makubwa kwenye kazi, biashara na jamii yako.
    105. Hakuna kiongozi aliyefikia ubora wa juu kwa kuwa mtu wa vising’izio na sababu. Watu ambao wapo bize kutengeneza sababu na visingizio hawana makubwa waliyowahi kufanya, na wala hawatakumbukwa na historia kwa nguvu wanazowekeza katika kutoa sababu na visingizio.
    106. Watu wengi wanapenda sana kutoa sababu na visingizio vingi kama vile, mimi sio meneja kwa hiyo siweza kufanya kitu hiki kwa kiwango bora, mimi sio mkurugenzi ndio maana sijafanya jambo hili kwa kiwango kinavyotakiwa, au nikipewa cheo au uongozi kwenye shirika au cheo ndio nitaonyesha dunia mimi ni nani.
    107. Mwandishi anasema, wengi wanakwama na kuwa watu duni na wasio na utukufu au mafanikio makubwa kwenye maisha yao na kwenye jamii kwasababu wanaendekeza sana sababu na visingizio vya kutokufanya mambo muhimu kwenye maisha yao.
    108. Robin anasema, watu siku hizi wamekuwa waoga sana kuwa halisi, sio wabunifu tena, wanabadili tu kanuni zilizofanya mambo yaenda kipindi cha nyuma, hawana ujasiri wa kuvumbua kanuni mpya, wanagusa gusa tu na hawana uhalisia wowote kwenye kazi zao.
    109. Izoeshe akili yako ifanye kazi kwa namna ya ufumbuzi na ubunifu, mfano kila unapoianza siku yako, angalia ni jambo gani muhimu la kuboreha, usifanye mambo yako kwa mazoea, boresha kila idara kwenye maisha yako.
    110. Unajua unaweza kuwa duni au wa kawaida bila hata wewe kujua, kama hutajisukuma kila wakati na kuchukua hatua za ziada kila siku utashangaa unaishia kuishi maisha ya chini sana na utaona kawada tu, kila siku jifanyie tathimnini.
    111. Katika ulimwengu wa biashara, inahitaji sana ubunifu na kufanya mambo kwa namna mpya kila siku. Mwandishi anasema kama unataka biashara yako ife mapema, basi fanya mambo kwa mazoea bila ubunifu.
    112. Unahitaji kujua mambo mengi sana muhimu kuhusu biashara unayoifanya, huwezi kufanya biashara katika zama hizi kama vile ilivyofanyika miaka 10 iliyopita, dunia ya biashara na ushindani inadai ubunifu na uelewa mkubwa sana ili ikue na uyaone mafanikio kwenye biashara.
    113. Usiache kujifunza na kuwekeza katika kuwa mtu bora, biashara itakuwa bora kwa jinsi ulivyo bora, wekeza na tumia fursa za teknologia zilizopo kuinua na kuboresha biashara yako kila siku.
    114. Mwigizaji maarufu Steve Martin aliwahi kusema, kuwa mtu bora kweli kweli kiasi kwamba watu washindwe kabisa kukupotezea.
    115. Viongozi wanahakikisha yale yote muhimu waliyoyapanga kuyafanya wanayafanya bila kughairisha. Kamilisha kazi zako na mambo yote muhimu kwenye siku yako, haijalishi upinzani ni mkubwa kiasi gani, kamilisha kazi zako kwa viwango bora.
    116. Jiongezee mategemeo makubwa kutoka kwako mwenyewe, na jitoe kwa namna isivyo kawaida ili ukamilishe mategemeo makubwa uliyojiwekea. Tegemea makubwa na vitu vingi zaidi kutoka kwako mwenyewe kuliko kutegemea kutoka kwa wengine.
    117. Jinsi unavyojituma na kufanya kazi kila siku ndivyo unavyogundua nguvu za uongozi zilizopo ndani yako. Kazi zinakufanya uendelee kujigundua na kuibua vipawa na nguvu ambazo hukudhania kama unazo.
    118. Kazi ni jukwaa la kutufanya tugundue vipawa, ubunifu na nguvu zilizolala ndani yetu, kazi ni moja ya jambo ambalo linaongeza furaha katika maisha yetu, hivyo jitoe kufanya kazi bora kila siku.
    119. Moja ya kazi kubwa unayotakiwa kufanya hapa duniani na kuondoa kila aina ya ngome na imani potofu zinazoweka ukomo kwenye uwezo wako.
    120. Imani na mapokeo yanamchango mkubwa sana katika kuunda tabia zetu za kila siku, vitu tunavyoviamini kwa muda mrefu vinaushawishi sana kwenye tabia zetu za kila siku, na tabia ndio huamua maisha tunayoishi na matokeo yake.
    121. Watu sio duni tu kwasababu ni duni, watu ni duni kwasababu wana tabia duni; watu sio masikini tu kwasababu ni masikini, watu ni masikini kwasababu wanaishi tabia za kimasikini na wanaziishi kila siku.
    122. Watu ni viongozi na matajiri kwasababu wanaishi tabia za kiuongozi na za kitajiri kila siku; hivyo tunatakiwa tuyapitie tena maisha yetu tuone kama mwenendo wa tabia zetu unatupeleka kwenye mafanikio na ndoto zetu. Kuna rafiki yangu anaitwa Dr. Makirita Amani, ameandika kitabu kizuri sana kuhusu “Tabia za Kitajiri”. Kitafute kitabu hiki, ni kitabu bora sana kwa mafanikio na utajiri.
    123. Jihesabu kuwa wewe ni moja watu wanaweza kufanya makubwa, usijichukulie kama mtu duni, fukara na asiye na matumaini, jehesabu wewe kuwa mbarikiwa, mtu anayeweza kupata mafanikio, siku zote ishi maisha yako ukiwa na mawazo chanya.
    124. Tumia muda wa kutosha kujifunza ili kufikia ubobezi wa jambo lolote, bobea kwenye taaluma yako, biashara yako au kipaji chako. Utafiti unaonyesha ili kuwa mbobezi kwenye jambo lolote unahitaji zaidi ya masaa 10000 ya maandalizi na kujifunza sana.
    125. Njia ya mafanikio imejaa gharama nyingi sana, kuna vitu utaachana navyo, kuna vyakula hutakula, kuna vinywaji hutakunywa, kuna marafiki utaachana nao, kuna wengine watakutenga, kuna fedha utapoteza, kuna masaa mengi ya usingizi utapoteza ili kupigania ndoto zako.
    126. Unapoianza safari mara zote ni ngumu sana mwanzoni, ni nguvu kubwa sana inahitajika ili uanze jambo fulani, lakini unapolianza na linapokuwa kwenye mwendo ugumu unapungua. Mfano, wakati roketi inaanza kuruka kwenda kwenye anga la juu sana huwa inatumia nguvu na nishati nyingi sana kutoka katika anga la dunia; hivyo ndivyo ilivyo kwa mwanzo wa jambo lolote, mwanzo wa biashara, tabia mpya au mafunzo, utatumia nguvu nyingi mwanzoni mwa jambo.
    127. Unapokua kiongozi hutakiwi kuwa na kauli mbili, unasema hivi na kufanya vile, fanya unachosema na sema utakachofanya. Hutakiwi kuwa na maisha ya aina mbili, maisha yako ya mchana ndio yawe hayo hayo ya usiku.
    128. Jinsi unapojipa ruhusa ya kuwa muwazi, huru, halisi na wa mwenye akili kwa wengine ndivyo na wengine wanavyokuwa huru, wazi na halisi kwako. Wafanye watu wanaokua pamoja na wewe wajisikie wapo salama, huru na wazi.
    129. Nyakati ngumu huzalisha viongozi imara. Uwezo wa kustahimili dhoruba za maisha na namna ya kufanya maamuzi sahihi wakati wa nyakati ngumu ndio sifa kuu ya viongozi bora.
    130. Viongozi bora ni watulivu sana katika nyakati ngumu, mambo yanapoharibika na kwenda mrama, hapo ndipo ilipo sanaa ya uongozi bora.
    131. Nyakati za kiza huwa hazidumu, lakini watu imara hudumu kwenye nyakati zote, moja ya sifa ya kiongozi ni uvumilivu na matumaini makubwa kuwa haya yanayopita kwenye maisha yataisha, hayatadumu milele, hivyo hawapaniki.
    132. Mwandishi Og Mandino alinukuliwa akisema, atavumilia hadi afanikiwe, hajaja hapa duniani kushindwa. Yeye ni simba na sio kondoo anayehitaji kuongozwa na mchungaji, yeye ni simba na amekataa kuongea, kutembea na kulala na kondoo. Nitavumilia hadi nishinde.
    133. Nyakati ngumu zilizojaa changamoto ndio huibua namna bora ya kuishi, mipango mipya ya maisha na utaratibu imara wa kujenga biashara na uwekezaji. Ukiweza soma kitabu cha Dr. Myles Munroe kinachoitwa “Overcoming Crisis”, utajua umuhimu wa dhoruba, majanga, na changamoto kwenye maisha.
    134. Nyakati ngumu tunazopitia kwenye maisha ndio hufanya mambo magumu yaende, au yafanyike. Tunapopitia changamoto na hali nguvu huwa tunatumia nguvu na akili nyingi sana ili mambo yakae sawa na yaende, ndio kipindi hiki kigumu ndio hufanya mambo mangumu na tuliyoyaona hayawezekani kuwezekana na kufanyika.
    135. Hivyo ili tuwe bora na kujenga misuli ya kusimama kwenye nyakati ngumu inatakiwa tuache kuzikimbia changamoto, tuache kizikimbia hofu, tunatakiwa kufanya yale yote muhimu tunayoyahofia.
    136. Ukuaji upo katika ratiba ngumu, mafunzo magumu, na uzoefu wa kupitia changamoto na nyakati ngumu. Usikimbie changamoto zako, zikabili zikusaidie kuwa imara. Kama alivyoimba msanii nguli na maarufu wa wa Bongo Flava, Mwana FA, shida hazikwepeki, zipo ili zitutoe misuli, zitokomaze, zitotoe macho, zitutoe jasho, zitupe akili na zituandae kwa kesho.
    137. Mwanamama mashughuri Hellen Keller aliwahi kusema tusingekuwa na watu wastahimilivu na majasiri kama dunia ingekuwa na furaha na raha pekee. Maana yake anasema majanga, dhoruba, vita, kuonewa, ubaguzi, utumwa, kukosekana kwa haki na usawa, ndio kumezalisha watu mashujaa, watu mahiri na viongozi imara.
    138. Dhana ya uongozi inahitaji zaidi kutumia nyakati ngumu, changamoto za maisha kwa faida yako. Maana yake viongozi wanatakiwa kunufaika na kufaidika na changamoto za maisha ili wawe bora na imara.
    139. Unapofikia kwenye kingo za mwisho kabisa za uwezo wako, nakujiona huwezi kuendelea hata hatua moja, na mwili wako kuanza kujisikia hovyo hovyo na akili yako vikianza kupiga kelele kama vile unataka kufa kutokana na jinsi ulivyojisukuma kuchukua hatua zaidi, mwandishi anasema hapo ndipo unapojihisi kuwa upo hai kama binadamu na ukuaji mkubwa hutokea kwenye nyakati kama hizi.
    140. Chukua hatua hata kama haupo tayari, chukua hatua hata kama kuna hofu zinakutisha, chukua hatua hata kama unajisikia huwezi tena kuchukua hatua. Miili yetu ina tabia ya kutoa taarifa za vitisho kwamba tunaweza kufa, tunaumia nk pale unapochukua hatua za ziada. Ukiweza soma kitabu cha 25 Hours a Day cha Nick Bare, kitakupa sababu nyingi kwanini hutakiwi kuusikiliza mwili wako unapofanya maamuzi muhimu.
    141. Kila mtu anaweza kujiona yeye ni mshindi katika nyakati za amani ambazo hakuna upinzani, biashara inaenda vizuri, uchumi upo imara, na mambo mengine yanaenda. Lakini mwandishi wa kitabu hiki anasema ukitaka kujua upo imara kiasi gani, pitia changamoto na magumu bila kutetereka.
    142. Kila mara unapofanya vitu vinavyokutia hofu na mashaka unadhihirisha uwezo wa kiuongozi. Uwezo wa kiuongozi huonekana pale unapofanya mambo yako licha ya upinzani kuwepo.
    143. Watu majasiri hawazikimbii hofu, huwa wanazila hizo hofu kabla ya hofu kuwala wao. Usikubali hofu zikakumeza mzima mzima, una uwezo mkuu ndani yako wa kukabiliana na hofu zinazokuja kwenye maisha yako, kuwa wa kwanza kuzimeza hizo hofu kabla hazijakumeza wewe. Kama unaweza soma kitabu cha “How to Stop Worrying and Start Living” cha Dale Carnegie ujue namna ya kuachana na hofu.
    144. Kumbuka, hutajua una uwezo kiasi gani, au una nguvu kiasi gani, au unaweza kufika mbali kiasi gani kama hutaanza na hatua moja. Anza mapema ili ujue nguvu, uwezo na vipawa vyako.
    145. Kila wakati unapokuwa tayari kukabiliana na hatari, au unapoandamwa na hatari nyingi, ujue upo karibu zaidi na mafanikio.
    146. Itakugharimu sana kukaa kwenye mchakato, mchakato utadai zaidi matumizi ya nguvu na uwezo ambao hujawahi kuutumia ambao umelala ndani yako. Rafiki yangu Alfred Mwanyika ameandika kitabu kizuri sana kinachoitwa “Amsha Uwezo Wako Halisi”, Kitafute kitabu hiki ujisomee utajua mengi sana.
    147. Fanya kile kinachokitia hofu, fanya kile kinachokuogopesha kila siku, kwa kufanya hivyo utaondoka kwenye hofu, na utageuza hofu na mashaka yako kuwa nguvu za kukusukuma mbele zaidi.
    148. Watu unaowaona wenye bahati hawapati tu bahati, wanatengeneza bahati kwa kwa kuwa tayari kufanya mambo hatari kwa ujasiri na kutumia vizuri fursa zinazokuja mbele yao.
    149. Ondoka na acha kucheza ligi ndogo ndogo za daraja la kwanza, ingia kwenye ligi za mabingwa, ujifunza na kupambana na mabingwa wenzio. Wakati umefika uondoke kwenye ligi za mchangani, uingie kwenye ligi za mabingwa duniani.
    150. Huwezi kuingia kwenye ligi kubwa za mabingwa kama utaendelea kufikiri na kufanya mambo yako kama unajiandaa kucheza ligi za mchangani. Maandalizi ya kucheza ligi za mabigwa ni makali sana, yanahitaji kujitoa sana na kujisukuma sana maana hakuna myonge anayecheza ligi za mabingwa. Mwandishi na bilionea wa Marekani Donald Trump, aliandika kitabu kizuri sana, kuhusu namna ya kufikiri kama mabingwa na kufanya kama mabingwa, kinaitwa “Think Like a Champion”, kitafute ukisome.
    151. Matatizo ni matatizo pale tunapoyafanya kuwa matatizo. Namna unayochukuliana na changamoto zinazopita kwenye maisha yako ndio huamua namna unavyotumia matatizo kama fursa au matatizo kama matatizo. Angalia namna unavyoyatafsiri matatizo, usiyaangalie matatizo kama laana, au kitu hasi na kibaya kwenye maisha yako, yaangalie matatizo kama fursa za kukufanya uboreshe maisha yako, ili uwe bora kuliko changamoto unazopitia.
    152. Kama kuna kitu ni muhimu kwa mtu ambaye ni muhimu kwako, basi kitu hicho kinatakiwa kuwa na umuhimu kwako pia. Mfano, kama unaniona mimi nina umuhimu kwako, na pia nina kitu ambacho ni muhimu, kitu hicho ambacho ni muhimu kwangu kinatakiwa kiwe muhimu na kwako pia.
    153. Chagua vizuri maneno ya kuongea na watu, usiongee tu chochote kwa namna ambayo sio nzuri. Unaweza kuwa una ujumbe mzuri na muhimu lakini ukatumia lugha ambayo sio nzuri, ambayo inawashushia watu heshima, watu hawatakusikiliza wala kutekeleza ulichosema. Maneno yako yanaweza kuonyesha watu njia, maneno yako yanaweza kuwafanya watu wakaona fursa mpya, maneno yako yanaweza kuwafanya watu wakawa na furaha. Tumia lugha nzuri kufikisha ujumbe wako.
    154. Tumia lugha sahihi ya kuwasilisha ujumbe wako, hata kama jambo unalotaka kuliwasilisha kwa hadhira yako ni gumu kiasi gani, unapochangua maneno mazuri na ukalisema kwa namna nzuri watu watalielewa jambo hilo na watalifanyia kazi.
    155. Kabla hujaianza siku yako, changua mambo machache muhimu ambayo utayafanya siku hiyo, baada ya kuyachagua weka umakini wako wote na nguvu zako zote katika kuyafanya, kamwe usijihusishe na mengine, fanya hayo machache uliyoyachagua hadi yakamilike.
    156. Unaweza kutumia kanuni ya Pareto katika kufanya mambo yako; kanuni ya Pareto ni 20/80, kati ya mambo machache unayochagua kufanya ndio yatakupa matokeo makubwa au 20% ya mambo unayoyafanya ndio yatakupa 80% ya matokeo, na kinyume chake pia.
    157. Upande mwingine wa kanuni hii maarufu inaaleza kuwa endapo utafanya 80% ya mambo yako, utapata matokeo ya 20% tu, hivyo mambo machache tu muhimu utakayochagua kuyafanya ndio yanaweza kukupa matokeo makubwa. Tafuta kitabu kilichoandikwa na Richard Koch “The 20/80 Principle” ili ujufunze kwa undani kanuni hii.
    158. Chagua vitu vichache na nyeti sana uvifanye, vitakuwa na matokeo makubwa sana kwenye maisha yako, usifanye tu mambo mengi, chagua kwa umakini vitu nyeti, vichache na vifanye kwa nguvu, akili, na moyo wako wote.
    159. Mwandishi wa kitabu hiki anasema, huwezi kujulikana kwa kufanya mambo mengi, mambo mengi yatakuchosha na yanafanyika bila ufanishi, mambo mengi hayatakufanya uwe mbobezi. Mambo muhimu machache ndio yatakufanya kuwa mbobezi.
    160. Robin Sharma anasema, tuna nguvu ngingi sana kuliko nguvu ambazo tunasifiwa kuwa tunazo. Nguvu hizi mara nyingi huibuka pale changamoto zinapotokea kwenye maisha yetu. Endelea kujisukuma na kuchukua hatua hata kama unaona ndio kitu cha mwisho kabisa kufanya.
    161. Mambo yote ya mafanikio na kufanikiwa yanategemea sana maamuzi yetu. Hata kuamua kutoamua pia ni maamuzi.
    162. Wajapani wana msemo wao maarufu sana, unasema ukianguka au kuangusha mara saba, amka mara nane zaidi. Maana yake mchakato wa kuendea ukuu wako na mafanikio yako, kuna kila upinzani na kuna wakati utaanguka na kuangushwa, hivyo haijalishi unaanguka mara ngapi, unachotakiwa kufanya baada ya kuanguka ni kuinuka na kuendelea, na sio kulala hapo hapo.
    163. Kamanda wa kivita wa jeshi la uingereza kipindi hicho Winston Churchill aliwahi kusema, kamwe usikate tamaa, kamwe, kamwe, kamwe, usije kukata tamaa, kwa vitu vikubwa au vidogo kamwe usikate tamaa, endelea mbele kupigania ndoto na maono yako.
    164. Mwandishi anasema, ni bora ukaingia na kushindwa vibaya, kuliko kukaa tu nyumbani ukiwa unaangalia televisheni, maana ukishindwa utajifunza, ukianguka utainuka ukiwa imara na mwenye uzoefu zaidi.
    165. Inuka mara nane zaidi kwa kila ulipoanguka, changamoto zinakupima ni kwa kiasi gani unahitaji unachokitafuta. Ukiwa katika biashara ndio kabisaa, hutakiwi hata kuwa na wazo la kukata tamaa, maana ulimwengu wa biashara una mambo mengi mapya kila siku.
    166. Wakati wengine wakisubiria amri na matamko ya viongozi ndio waanze kuchukua hatua, wewe unatakiwa kuwa wakwanza kufanya mambo yote muhimu bila kusubiria matamko.
    167. Kama kuna kanuni muhimu ya mafanikio basi ni kujua namna ya kuishi na kuchukuliana na watu. Unahitaji watu ili ufanikiwe kwenye jambo lolote, biashara, kazi, elimu. Weka mahusiano yako yawe bora na watu, katika jamii yetu ya sasa watu wanaweka pesa mbele zaidi ya utu. Mwandishi anasema ukiwafanyia watu vizuri watakuletea fedha zao, na mali zao.
    168. Kama unataka kushinda, basi wasaidie wengine kushinda, kama unataka fedha wasaidie wengine kupata fedha hivyo ndivyo dunia inavyofanya kazi.
    169. Ni asili ya binadamu kuwa unapowasaidia na wao wanafanya kila wanachoweza kukusaidia pia. Unaweza ukawasaidia watu na usiwe na matarajio ya kuja kusaidiwa nao baadaye, lakini ukweli ni kwamba, lazima watakuja kukusaidia tu.
    170. Mwandishi Robin anasema, toa kile unachokitamani sana kupokea, mfano kama unapenda msaada basi toa zaidi misaada kwa wengine, wasaidie wengine, kama unataka upendo toa zaidi upendo, kama unataka heshima toa heshima.
    171. Kanuni hii ya utoaji ipo pia katika Biblia, Yesu Kristo aliwahi kuwaambia wanafunzi wake, “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa” Soma Kitabu cha Luka 6:38.
    172. Watu watashawishiwa zaidi na mwenendo na matendo yako kuliko kauli zako. Ni asili ya binadamu hawapendi kuongozwa au kuamrishwa, hivyo njia nzuri ya kuwafanya watu wanaokuzunguka kufanya unayoyataka, unatakiwa uwe mfano mzuri wewe mwenyewe.
    173. Mwanamahesabu Isaac Newton aliwahi kusema, ukiona naona mbali kuliko wengine ni kwasababu nimesimama kwenye mabega ya watu hodari. Hapa alimaanisha mafanikio yote niliyonayo, mambo yote ninayoyajua ni kwasababu nimejifunza kwa watu wakuu zaidi.
    174. Kuwa tayari kuwasilikiliza watu na kuongea na watu, wape watu heshima na utu, mnapokua pamoja na wenzako, onyesha ushirikiano, sio upo na watu huku unatumia simu yako, umeweka earphone masikioni.
    175. Mahusiano imara yanajenga uongozi imara. Kuwa tayari kushiriki kwenye mambo ya wenzako, onyesha kujali kwenye mambo ya wenzako.
    176. Jifunze kuwa msikilizaji mzuri, onyesha umakini wako wote unapomsikiliza mtu, sikiliza zaidi kuliko unavyoongea. Wengi wanadhani wale wanaoongea sana ndio wana majibu au wanajua mambo mengi, kumbe sio kweli.
    177. Uongozi sio kuongea sana, au kuongea kila mara, kuna watu wanadhani kiongozi ni mtu wa kuongea ongea sana, kushauri sana, kutoa maelekezo sana nk. Uongozi wa kweli ni kushuka chini na kuwa tayari kusikiliza watu wengine wanapoongea.
    178. Uongozi ni kuwa tayari kuwafanye wengine wasikike pia. Uongozi ni kuinua sauti za walio kimya na wao waongee na washauri na kutoa maoni yao.
    179. Kumbuka jambo hili kwenye maisha yako, kuwa watu wanapenda kufanya biashara au kufanya kazi na watu wanaowapenda. Hivyo kama huna mahusiano mazuri na watu hata ufanisi wako kazini utakuwa chini sana.
    180. Kila siku tenga muda wa kuzungumza na watu wako wa karibu, watu wako muhimu. Licha ya fujo zote za utandawazi na ulimwengu wa kidigitali tulio nao tenga muda kwa ajili ya kufanya mawasiliano muhimu. Hii ndio njia nzuri ya kukuza mahusiano.
    181. Hakuna aliye shujaa leo aliyefanya mambo yote mwenyewe bila msaada wa watu wengine. Wajali wengine, wape nafasi wengine wachanue, na wewe utachanua na kuwa mkuu sana.
    182. Ili uwe kiongozi bora inatakiwa uwe mtu bora kabisa. Hii ni kwasababu huwezi kuwapa watu nguvu kama wewe huna hizo nguvu.
    183. Huwezi kuwafanya wengine kuwa bora kama wewe sio bora. Huwezi kuwafanya wengine wajisikie vizuri kama wewe hujisikii vizuri mwenyewe.
    184. Watu wakiwa bora kila wanachokifanya kitakuwa bora, kazi zitakuwa bora, ofisi itakuwa bora, shirika litakuwa bora na watatoa matokeo au huduma bora sana.
    185. Tengeneza mkakati wa kufanyia kazi uwezo wako uliolala, tafuta namna unaweza kujiunganisha na uweze kutumia uwezo wako wa kipekee uliolala ndani yako bila kutumika.
    186. Jisafishe fikra zako na ondoa mawazo na imani hasi kuhusu uongozi, jitambue kwa viwango vya juu sana na wekeza nguvu zako kwenye uwezo wako uliolala ili utumike kukusaidia wewe na jamii nzima.
    187. Jifunze kwa nguvu zako zote namna unavyoweza kuitunza afya yako, maana bila kuwa na afya njema hutaweza kuhimili dhoruba na mikiki mikiki ya dunia hii. Mafanikio yanakuhitaji uwe na afya njema siku zote.
    188. Ili uendelee kuwa na afya njema, unatakiwa kuondoa hisia mbaya za chuki, uchungu, hofu na majuto ambazo zinaweza kudhorotesha nguvu zako na afya yako ukaishia kuwa mtu dhaifu.
    189. Ili uwe na afya bora ya mwili, akili na roho yako, inatakiwa uwe mtu wa rohoni, ishi na wekeza kwenye maisha ya rohoni. Mwandishi anasema kuna nguvu kubwa ya kufanya yasiyowezekana hapa duniani, nguvu hizo hazipo duniani bali zipo katika ulimwengu wa roho.
    190. Jiunganishe na chanzo cha uongozi, jiunganishe na Mungu wako, maana yeye ndie ametoa vipawa na kusimika roho ya uongozi ndani yetu, unaporudi na kujenga uhusiano imara na Mungu wako, maisha yako yatakuwa na ushawishi mkubwa sana na pia utakamilisha hata yale uliyoyaona hayawezi kukamilika. Kama unataka kuelewa zaidi kuhusu kusudi na chanzo cha uongozi ulio ndani yako nakushauri usome kitabu cha Dr. Myles Munroe, kinachoitwa The Spirit of Leadership.
    191. Wakati sahihi wa kufikiri ni alama gani utaiacha hapa duniani ni sasa. Wengi wanagundua vitu wanavyotakiwa kuvifanya wakati ambao muda umeenda sana, na wengine wanakumbuka wakiwa karibu na umauti. Weka mikakati sasa.
    192. Kipimo cha mafanikio kinatakiwa kiwe ni kufikia kuwa mtu bora, mwenye maadili bora sana, mwenye utu, mtu huru, asiye na huzuni, chuki, hofu. Na sio kupima mafanikio kwenye vitu vya muda na vinavyoharibika kama mali na fedha.
    193. Ndio maana watu wakivipoteza fedha, mali au utajiri wanaomiliki wanaishia kuchanganyikiwa, kupata maradhi na wengine wanajiua. Mwandishi anasema, fedha, mali ni vitu vya mud asana, na hivitakiwi kuwa ndio vitu pekee vinavyokutambulisha.
    194. Chukua Jukumu la kusimamia kulinda ufahamu na akili zako, usiruhuru tu kila kitu kingie tu kwenye ufahamu wako na kuanza kuzunguka zunguka humo hovyo. Mwandishi anasema usiruhusu hata sekunde moja wazo hasi likaingia kwenye fahamu au akili yako.
    195. Ufanye ufahamu na akili yako kuwa sehemu takatifu mno, weka ulinzi mkali kwenye mifumo yako yote ya fahamu ili isipitishe mambo hasi na yasiyofaa kwenye akili na fahamu zako. Ilinde akili na fahamu zako kama vile Mwenyezi Mungu alivyoilinda bustani ya Edeni, ili kuzuia vitu au watu waovu wasiingie humo.
    196. Fikra zako, akili zako na fahamu zako ni kiwanda na sehemu muhimu ya kuchakata taarifa. Usiruhusu mambo ambayo hutaki yatokee kwenye maisha yako yakaingia kwenye fahamu zako. Najua hili linaweza kuwa moja ya jukumu kubwa sana la maisha yako, unahitaji nidhamu kubwa sana kufanya jambo hili.
    197. Mahatma Gandhi, baba wa taifa la India na mwanamapinduzi na moja ya watu mashughuri sana waliowahi kuishi hapa duniani alisema, hatoruhusu watu kutembea kwenye fahamu na akili zake wakiwa na miguu yao michafu. Maana yake alikuwa hatoi ruhusa mawazo hasi, vinyongo, uchungu au mambo maovu kuingia katika fahamu zake.
    198. Jifunze kusamehe unaohitaji kuwasamehe, huitaji tena kuishi ukiwa umeshikilia mambo ya zamani, yaache yaliyopita yapite. Huwezi kuwekeza kwenye kufanya maisha yako ya baadaye kuwa bora kama bado umeshikamana na mambo ya kale.
    199. Mwandishi anasema, ni watu walioumizwa ndio huwaumiza wengine. Usiwe mtu wa visasa, visa na magomvi. Kuwa mtu huru, samehe, kuwa mtu wa upendo kwa wote. Uishi maisha yako kwa furaha.
    200. Mwandishi wa kitabu hiki anasema, anatamani sana maarifa na mafunzo yote uliyojifunza kwenye kitabu hiki umshirikishe na rafiki yako, mfanyakazi mwenzako, ndugu au jamaa yako. Unaweza kumnunulia kitabu hiki kama zawadi, au unaweza kumtumia linki ya uchambuzi huu akajifunza. Kama uchambuzi huu umekuwa muhimu kwako, basi mshirikishe na rafiki yako wa muhimu uchambuzi huu. _Gift The Leader Who Had No Title to coworkers, friends, family members, and even strangers. They will learn that they are meant to lead in all they do and live great lives.
      _
      @Hillary Mrosso_30 September 2022

  • Sababu tano kwa nini utahitaji kutoa kitabu chako kwa njia ya mtandao kwanza kabla ya kukitoa kwa njia ya nakala ngumu

    Unapozungumzia kutoa kiytabu chako kwa mfumo wanakala laini, basi swali ala kwanza ambalo watu huwa wananiuliza ni kuwa vipi kuhusu hakimiliki? Hili huwa ni swali kubwa sana ambalo watu huwa wanauliza. Kwenye makala ya leo ningependa kuongelea kwa nini unapaswa kutoa kitabu chko kwa mfumo wa nakala laini kwanza kabla ya kutoa kitabu hicho kwa nakala ngumu.

    Hata hivyo, ushauri huu haumfai kila mtu. Siyo kila mtu anapaswa kutoa kitabu kwa nakala laini kwanza, ila kama utaweza unaweza kuanza kutoa nakala laini halafu baadaye ukatoa nakala ngumu.

    Moja ni kwa sababu ni bei rahisi kutoa nakala laini kuliko ilivyo kutoa nakala ngumu

    Utoaji wa vitabu kwa mfumo wa nakala laini umerahisisha mambo mengi sana. zamani ilikuwa kwamba ili utoe kitabu chako basi ulipaswa kuwa chini ya taasisi au kampuni ya uchapishaji. Kampuni hii ilipaswa kupitia kitabu chako. Kama kampuni hiyo ingependa kitabu chako na aina ya uandishi wako basi ulikuwa na bahati, kitabu chako kilikuwa kinachapwa. Kama kampuni ilikuwa haitami kitabu chako, basi ulikuwa unaenda maji. Maana yake kitabu chako kisingechapwa. Ndio maana ukifuatilia historia nyingi za waandishi wakubwa zinhusisha kukatawaliwa mara nyingi kabla ya kucha vitabu vyao.

    Lakini hii tafsiri yake nyingine ni kuwa kwa kila mwandishi mkubwa unayemwona, kuna waandishi wengine wengi ambao hawakuweza kabisa kuchapa vitabu na vitabu vyao leo hii havipo kwenye mfumo wowote ule. Hii ni kutokana na mfumo wa uchapaji iwa vitabu wa wakati huo ulivyokuwa. Kama kampuni au taasisi ya uchapaji wa vitabu ilikukataa, basi ulipaswa kwenda kutafuta kampuni au taasisi nyingine na kama zingekataa zote, basi ndoto yako ilikuwa imefikia mwisho.

    Ila sasa siku hizi mambo yamebadilika. Yamebadilika kabisaa, yaani, unawez kuandika kitabu chako na kukiachapa kwa njia ya mtadao. Bila kuhitaji hizi kampuni kubwa ambazo zilikuwa zinaweka kiwingu kwa miaka mingi na kuzuia watu kufikia ndoto zao za uandishi.

    Kwa hiyo, badala yaw we kushindwa kuchapa kitabu kwa sababu ya hizi kampuni, unaweza kuchapa kitabu chako kwa njia ya mtandao na kuanza kufikisha ujumbe wako kwa jamii.

    Pili ni kwa sababu hauhangaiki kusambaza vitabu kwa watu

    Ukichapisha vitabu kwa mfumo wa kawaida, unakuwa unahitajika usambaze vitabu hivi, kwa watu. na mbaya zaidi ni pale unapokuwa umechapisha wewe mwenyewe. Maana wewe unahitajika usimamie ubora wa uchapaji wa kazi yako, unahitaji uhakikishe kuwa unasafirisha vitabu kutoka kwa mchapaji mpaka kwako, unatakiwa kutangaza vitabu vyako. Unatakiwa utume vitabu mpaka kwa mteja, endapo vitabu vitapotea njiani basi utatakiwakutuma vitabu vingine ili viweze kumfikia.

    Ila ukichapa kitabu chako kwa njia ya mtandao basi unakuwa hizo kadhia zote ambazo zinaweza kukupata.

    aMaana yake mtu atakinunua kwa njia ya mtandao, na wewe utakuwa umemaliza mchezo.

    Tatu ni kwa sababu unakuwa unatest mitambo

    Kuna wakati mwandishi unaweza kuandika kitabu ila ukawa huna uhakika kama kitabu hicho kitakubalika miongoni mwa wasomaji wako au la! Ununuaji wa kitabu kwa njia ya mtandao unakupa picha ya namna kitabu hicho kitakavyonunulika kwa njia ya kawaida.

    Na hiki hata kampuni na taasisi zinazofanya uchapishaji kwa njia ya asili zinakifanyia kazi sasa hivi. kuna kampuni sasa hivi hazichapishi kitabu chako, mpaka kitabu chako kiwe kimeuza nakala kadhaa kwa njia ya mtandao.

    Usihofu, kampuni hizi hazipo hapa Tanzania, zipo nje ya nchi.s

    Nne, ni njia nzuri ya mwandishi yeyote mchanga kuanza na baadaye kukuza jina lake kuwa jina kubwa

    Ksms wewe unayesoma ni rais Samia Suluhu, au ni waziri mkuu Kassim basi njia hii haikufahi, maana najua tu hata kabla hujamaliza kitabu chako, kampuni nyingi za uchapaji zinakuwa zimeshakufuata kwa kuutaka mswada wako. Ila kama wewe ndio kwanza unaanza na hauna mtaji wa kuchapa vitabu vyako mwenyewe, basi  hapa, basi hapa utapaswa kuandika na kutoa kitabu chako kwa njia ya mtandao. Gharam ayake ni kidogo au hakuna kabisa.

    Lkwa hiyo hiki kitu kinakufanya, unaanza kutoa ujuzi, kutumia kipaji chako au kufanya kitu unachopenda bila ya kuhitaji kuweka gharama ya ziada.

    Tano, sababu unaandika vitabu vingi ambavyo huwezi kuchapa kw wakati mmoja.

    Mimi karibia kila mwezi huwa naandika na kutoa kitabu kimoja. Sasa kutoa nakala za hivi vitabu kwa njia ya mtandao ni rahisi kuliko ilivyo kuhakikisha kwamba unachapa na kutoa nakala ngumu kila mwezi.

    Kama na wewe una spidi kkubwa ya uchapaji wa vitabu karibia kila mwezi, basi maana yake unaweza kuamua kuchapa baadhi ya vitabu kw anjia ya mtandao kwanza, halafu baada ya hapo vitabu vingine utachapa kwa njia ya kawaida.

    Rafiki yangu, hizo ndizo sababu tano kwa nini na wewe unahitaji kuchapa vitabu vyako kwa njia ya mtandao. Naomba nijue maoni yako hapa chini kuhusu hii mada ya leo ni yapi.

    Karibu sana.

    Makala hii imeandikwa name,

    Godius Rweyongeza

    Unaweza kunipata kupitia 0755848391

    Kama umependa makala hii, ni wazi kuwa utapenda mafunzo yangu ambayo huwa natoa kupitia kwenye channel yangu ya youtube. Hakikishaumesubsceibe leo hii kwenye channel hii nzuri kwa ajili yako.

    Kupata vitabu vyangu ambavyo nimeandika kwa njia ya mtandao, basi bonyeza hapa ili uchague kimoja, halafu unipigie uniambie kipi ungependa kupata ili nikutumie.

  • Watu hawawezi kukupuuza siku zote

    Siku ya leo nina ujumbe mfupi kwako rafiki yangu. Na ujumbe wangu Ni kwamba kama wewe unapambamia lengo au ndoto yako na unalifanyia kazi mara kwa mara, basi Kaa ukijua kuwa watu hawatakupuuza siku zote.

    Ndio wanaweza kukupuuza mara moja au mara mbili, Ila hawatakupuuza siku zote. Kuna siku watanyoosha mikono juu na kusema ngoja tufuatilie kwa kina kile anachofanya huyu mtu. Na kwa jinsi hii utakuwa umewapata.

    Kitu kimoja ninachotaka kukusihi Ni kuwa Mara zote hakikisha kwamba unaandaa kazi bora.

    Kazi yako yoyote iwe ni bora maana mara zote kuna mtu mpya ambaye hajawaji kufuatilia kazi zako na siku hiyo ndio ndio anafuatilia hiyo kazi.

    Kumbe kama leo kuna MTU anafuatilia kazi yako Mara ya kwanza, hakikisha kwamba hakutani na kazi ya viwango vya chini, badala yake, hakikisha kazi yako inakuwa bora, Mara zote na sehemu zote.

  • Sifa mbili ambazo ukiwa nazo, basi mafanikio kwako ni suala la muda tu

    Siku ya leo ningependa nikueleze sifa mbili ambazo ukiwa nazo, basi ujue kuwa mafanikio kwako litakuwa ni suala la muda tu. unajua sifa hizi ni zipi..

    Sifa ya kwanza ni sifa ya kufanya kazi kwa bidii

    Hakuna kitu chochote kile unachoweza kupata bila ya kufanya kazi, tena siyo tu kufanya kazi, bali kuhakikisha kwamba umefanya kazi kwa bidii na kwa kujituma.

    Kama rafiki yangu haufanyi kazi kwa bidii na kwa kujituma, sichelei kusema kwamba utasubiri sana kuweza kufikia mafanikio ambayo unapenda kufikia maishani mwako

    Sifa ya pili ni nidhamu

    Hii ni sifa nyingine muhimu sana, nidhamu yako itakuwezesha kufanikisha mambo mengi ambayo hakuna watu wengine wanaweza kufanikisha.

    Unahitaji kuwa na nidhamu kuanzia kwenye kazi yenyewe.

    Nidhamu ya pesa

    Nidhamu ya muda

    Yaani, nidhamu kwenye kila kitu. Na kwa kuwa watu wengi hawaelewi nidhamu  ni nini, niliwahi kuandaa makala inayoonesha kuwa nidhamu ni kitu gani, naomba uiangalie ili uweze kujua nidhamu ni kitu gani. BONYEZA HAPA kuiangalia

    lakini pia kuna makala ambayo niliwahi kuandaa inayoonesha aina tano za nidhamu unazopaswa kuwa nazo. BONYEZA HAPA kuisoma pia

    Kama bado hujasubscribe kwenye channel yangu ya youtube basi fanya hivyo sasa hivi.

  • Mwonekano wa Bustani Yangu

    Leo asubuhi nilienda bustanini kwangu. Wakati nikiwa bustanini, nilimtafuta rafiki yangu ambaye katika kuchati naye nikamwambia nipo bustanini. Na hapo nikamrekodia video fupi ya mwonekano wa Bustani yangu.

    Sina shaka na wewe ungependa kuiona. Na hata pengine kusema mawili matatu kuhusu hii Bustani.

    Japo nilikuwa sijapanga kurekodi video siku ya leo. Ila naamimi utakachoona utapata kitu hata Kama ni kidogo.

    Mpaka wakati mwingine

    Mimi Ni GODIUS RWEYONGEZA (Songambele)

  • Sababu 15 kwa nini haupaswi kuwa na plan B

    Kwenye uchaguzi wa mwaka 2015 kuikuwa na utani ambao ulikuwa unasambaa mtandaoni. Mmoja wa watu alitengeneza meme fulani hivi ambayo ilikuwa ikimwongelea waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa. Ilikuwa inasema kuwa kila mara unapaswa kuwa na Plan B kama Lowassa. Amekatwa CCM asigombee urais, amehamia CHADEMA, na sasa akishindwa kuingia ikulu kwa tiketi ya CHADEMA anahama nchi anaenda kugombea Senegal.

    Sina hakika sana kama nchi iliyokuwa inatajwa ilikuwa ni Senegal kweli, ila nina uhakika na kitu kimoja tu. kitu hiki ni kuwa baada ya uchaguzi wa mwaka 2015 hapa nchini Tanzania, kulikuwa na nchi nyingine hapa barani affrika iliyokuwa inategemea kufanya uchaguzi. Kwa hiyo, aliyetengeneza hiki kichekesho alikuwa akionesha kuwa endapo Lowassa atashindwa kuingia ikulu kwa tiketi ya CHADEMA basi angehama nchi, kwenda kugombea huko maana mara zote alikuwa na plan B.

    Ok ok, siku ya leo siko hapa kumwongelea Lowassa wala kuongelea siasa, ila nipo hapa kuongelea kitu kimoja tu. PLAN B. kumekuwe[o na maoni mengi sana ya watu wakisema kwamba unapaswa kuwa na plan B kwenye maisha yako.

    Tena watu wamekuwa wakisema hili kwa msisitizo mkubwa sana, kwamba endapo utashindwa kwenye plan A, yaani, ile plan ambayo unaifanyia kazi sasa hivi, basi utapaswa kuhamia kwenye plan B. Siku ya leo nipo hapa kukwambia kuwa haupaswi kuwa na PLAN B kwenye maisha yako na zifuatazo ni sababu 15 kwa nini haupaswi kuwa na PLAN B

    KWANZA, SIYO SALAMA KWA AFYA YAKO

    Wengi wanafikiri kuwa ukiwa na plan B, basi mpango fulani ukishindwa  utaachana nao na kuingia kwenye mpango mwingine. Hiki kitu ndicho kimewafanya watu wengi washindwe kuendelea kwenye maisha. Unakuta mtu ana mpango mzuri, ila sasa haufanyii kazi mpango wake kwa kujitoa kwa sababu ana mpango mwingine unaoelekeana na huo ambao anauita PLAN B.

    Tuchukulie mfano tu wa mtu ambaye amehitimu chuo na anatamani kuanzisha biashara. Unakuta mtu wa aina hii anashindwa kuanzisha biashara au hata akiianzisha hiyo biashara inashindwa kukua kwa sababu moja tu, mtu huyu muda wote anakuwa anafikiria kuwa nikizuga tu kwenye biashara na ikafeli naenda kutafuta kazi. Kwa hiyo, yeye muda wote anajua kuwa hata biashara isipofanya vizuri, yeye atakuwa na sehemu ya kuangikia ambayo ni ajira. Kitu hiki sasa hakiwezi kumfanya mtu ajisukume na kufanya makubwa zaidi. pale ambapo mtu anakuwa anajua kwamba kuna sehemu ya kuangukia basi, ujue wazi kuwa huyo mtu hatajisukuma kufanya makubwa.

    Kijana ambaye anajua wazi kuwa nyumbani kwao kuna kila kitu (wa kishua), hatajisukuma kufanya vitu na kupambana, badala yake atakuwa anjua kwamba hata asipofanya kitu chochote, pele nyumbani vitu si vipo tu.

    Wakati hali ni tofauti kwa kijana ambaye anakuwa anajua kwamba asipopambana basi siku hiyo hana ugali.

    Au yule anayekuwa anajua kuwa anapaswa kupambana kwa ajili ya wazazi wanaomtegemea yeye.

    Siku moja nilikuwa namsikiliza Les Brown kwenye mojawapo ya mazungumzo yake. Les Brown akawa amesema kwamba alikuwa anauza bidhaa nyumba kwa nyumba. Hivi unajua kweli mauzo ya nyumba kwa nyumba au unayasikia redioni tu.

    Mauzo ya nyumba kwa nyumba ni yale ambayo unakuwa unaenda unagonga nyumba moja baada ya nyingine na kuwaambia bidhaa uliyonayo, huku ukiwashawishi wanunue. Mfano, unachukua kitabu changu cha  NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA. Unaenda nacho nyumba kwa nyumba ukikiuza. Unagonga kila nyumba na kuwaambia kuwa hapa nina kitabu kizuri kinachoweza kukusaidia wewe kufanikisha lengo lolote kubwa kwa kuchukua hatua ndogondogo kila siku. Unatoa maelekezo kedekede, kisha unawaambia watu wakupe hela uwaachie kitabu.

    Sasa haya mauzo, yanahitaji moyo sana. Maana unapokuwa unagonga mlangoni mwa mtu, unakuwa huna uhakika kama huyo mtu anataka hiyo bidhaa au hataki. Unakuwa hujui kama huyo mtu atapenda kupata kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA au la hatataka,

    Hujui kama huyo mtu ana shida ya sabuni yako, au tayari anazo sabuni.

    Mauzo ya aina hii, kibongobongo wanafanya wachache sana, hata wale wanaozunguka mitaani na laini za simu hawajafikia hicho kiwango cha kugonga mlango mmoja baada ya mwingine. mara nyingi wanapita tu mtaani wanatembea.

    Sasa kwenye mauzo ya aina hii, kuna matatu ambayo unaweza kukutana nayo.

    • Mteja anaweza kukwambia, ndio nataka bidhaa. Tukitumia mfano wetu hapo juu, anaweza kusema anataka kupata kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA
    • Au anaweza kukwambia kwa sasa hapana, labda siku nyingine
    • Au anaweza kukwambia, hapana
    • Au anaweza kukwambia hapana pamoja na matusi juu yake.

    Sijui unanielewa. Sasa hakuna kitu kinakatisha tamaa kama majibu mawili ya mwisho, hasa unapokuwa unajijua una bidhaa nzuri ambayo ingeweza kumsaidia mteja kama ambavyo mimi nina kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA na ninajua sana kuwa kinaweza kukusaidia wewe. Rusha basi, elfu ishirini ili upate nakala yako (Hardcopy). Namba ya kurusha hela ni 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Kitu hiki, huwa kinawafanya watu wachache sana wajihusihe na na mauzo haya. Ila sasa, ubora wa mauzo haya ni kwamba, kadiri unavyokutana na watu wengi zaidi, ndivyo unavyouza zaidi. Ukikutana na watu kumi. Saba au nane watakataa, ila watatu au wawili watanunua. Kwa hiyo, unakataliwa sana ila pia unauza zaidi. Sasa Les Brown alisema kwamba, yeye alikuwa analazimika kuendelea na mauzo haya kwa sababu tu hakuwa na njia nyingine ya ziada kwenye maisha yake ya kupata kipato isipokuwa hiyo.

    Anasema kuna rafiki yake walianza pamoja hii kazi ila aliishia njiani,kwa sababu alikuwa na plan B. ila yeye hakuwa na plan nyingine yoyote ile isipokuwa kuhakikisha kwamba ameuza, maana la sivyo, mama yake asingeweza kupata chakula siku hiyo.

    PILI WATU WALIOFANIKIWA SIYO WALE WENYE PLAN B

    Watu wengi walioweza kufanikiwa kwenye maisha siyo wale waliofanya jambo fulani wakiwa na plan B kwenye kichwa chao, bali wale waliofanya lile jambo kwa moyo wote wakiwa wanajua kuwa ni au walifanye hilo jambo na kulifanikisha au la wafe wakiwa wanapambia hilo jambo.

    Siku moja nilikuwa nasikiliza hotuba ya Arnold Schwaznegger. Kwenye hiyo hotuba Arnold alisema kuwa yeye kwenye maisha hapendi kuwa nap la B.

    Mimi mwenyewe sipendi kabisa kuwa na plan B. kwa vyovyote vile, kwenye maisha watu wenye plan B huwa hawafanikiwi.,waliofanikiwa kwenye maisha ni wale ambao walikuwa na plan moja tu, wale walioweka nguvu na muda wao wote kwenye kitu kimoja na wakakifanya bila kurudi nyuma.

    TATU, UKIKWAMA UNARUDI NYUMA

    Unapokuwa na plan B. ukikutana na kikwazo kidogo tu, hapohapo unarudi nyuma. Maana unajua kuwa utaenda kuegemea sehemu fulani. Ila pale unapokuwa unajua kuwa ni lazima nifanye hiki kitu, au la nitakufa nikiwa napambia hiki kitu, basi utapambana kwa nguvu zako zote kuhakikisha kuwa kile kitu unakifanyia kazi bila ya kurudi nyuma.

    Moja ya kitu ambacho watu wengi wamekuwa hawafahamu ni kuwa vikwazo kwenye maisha lazima tu vitokee. Yaani, hakuna namna yoyote ile kwenye maisha unaweza kuishi bila ya kuwa vikwazo. Vikwazo vinatokea kwenye maisha, sasa utakuwa na plan B ngapi?

    Ndio maaana kwenye ndoa unaambiwa ukishakuwa na mwenza wako unakuwa naye milele. Kwa sababu wanajua kuwa kwenye ndoa kuna vikwazo vingi, sasa ebu fikiria kila mtu akiingia kwenye ndoa na plan B. Huyo mtu ataoa au ataolewa na wanagapi? Maana kila atakapokutana na kikwazo tu, maana yake ataachana na mwenza wake na kwenda kuolewa na mtu mwingine ambaye anadhani hana changamoto. Na mwenyewe akiwa na changamoto anaachana naye tena. Ndio maana unaambiwa uishi na mwenza wako kwenye shida na raha (NO PLAN B)

    Kwa hiyo, kama ilivyo kwenye ndoa, vivyo hivyo kwenye maisha. Uanapaswa kuchagua kitu kimoja na kuamua kukomaa na hicho kitu bila ya kurudi nyuma hata kama unakutana na changamoto kiasi gani.

    Ubora changamoto na vikwazo ambavyo unakutana navyo kwenye maisha, siyo kwambna ni vikwazo, badala yake kila unapokutana na changamoto au vikwazo kwenye maisha, maana yake unapata somo kutoka kwenye hivyo vikwazo na hizo changamoto, kitu ambacho kinakufanya uweze kuwa imara kwa siku ambazo zinazofuata.

    Ebu chukulia mfano wa kawaida tu,

    Ebu tuchukulie kwa mfano umeanzisha biashara, halafu kadiri unavyoenda unakutana na changamoto ya kutoona hela kwenye biashara yako. Mwanzoni unaanza kufikiri kuwa labda hawa watakuwa ni chuma ulete. Lakini kadiri unavyoendelea kufuatilia zaidi, unagundua kuwa siyo chuma ulete, ila tatizo liko kwako. unagundua kuwa tatizo umekuwa unachukua hela ya biashara na kuifanya kuwa hela yako.

    Yaani, umekuwa hutenganishi kati ya hela yako na hela ya biashara. Hivyo, unaamua kuwa kuanzis sasa utaanza kutengenisha kati ya hela yako na hela ya biashara. Unaamua wazi kuwa kamwe kwenye maisha yako, hutachukua hela ya biashara uitumie kma ya kwako. Badala yake utakuwa unajilipa wewe mshahara kama mfanyakazi kwenye biasahara yako na kiasi kingine utakuwa unakiacha kwenye biashara. Lakini unaenda mbali zaidi kwa kuhakikisha kwamba unatunza kumbukumbu za hela zote zinazoingia na kutoka kwenye biashara. Rafiki yangu, hiki kitu kidogo tu, kina nguvu kubwa sana. kubwa mno, nakwambia.

    Baada ya muda ni wazi kuwa utaanza kuona matokeo ya tofauti, na matokeo ya tofauti maana yake wewe umeshatatua changamoto au kikwazo kilichokuwa kinakurudisha nyuma na sasa unaendelea mbele. Siku nyingine ukikutana na changamoto au kikwazo kingine ni wazi kuwa hutarudi nyuma, badala yake utaendelea mbele zaidi.

    Mfano siku nyingine ukikutana na kikwazo cha mauzo kidogo, suluhisho la kikwazo hiki siyo kuacha kufanya ile biashara unayofanya na kukimbilia kufanyia kazi plan B. Badala yake suluhisho lake ni wewe kutafuta wateja zaidi. na ili kupata wateja zaidi maana yake unapaswa kujifunza mbinu mpya za mauzo na masoko. Kumbe ukiwa na plan B, maana yake unakosa akili ya kujiongeza na kufanya makubwa zaidi, ila ukiwa na plan hiyohiyo na ukakomaa nayo, unakuwa na akili ya ziada.

    Kabla sijamalizia hii pointi ningependa nitoa kwa ufupi sana hadithi ya Heran Cortes. Huyu jamaa alienda na jeshi dogo kupigana vita na jeshi kubwa. Walienda na boti na baada ya kuwa wameshuka salama kwenye boti, aliamuru boti zote zichomwe moto.

    Kitu hiki kilituma ujumbe kwa wanajeshi wake kuwa hakuna plan B. Maana yake, walipaswa kushinda hiyo vita, au la walipaswa kufia hapohapo.

    Sasa hiki kitu kina maana gani kwako, maana tumeshatoka kwenye hizo zama za kivita, ila kitu kimoja cha uhakika tunachojifunza kutoka hii stori fupi ni kutokuwa na plan B kwenye maisha. Plan B,  inakwamisha. Plan B inakufanya uwe na sehemu ya kuegemea na hivyo, unashindwa kutimiza wajibu wako kwa viwango vikubwa.  Niendelee au niishie hapa!

    Ebu basi subscribe kwenye channel yangu ya youtube kwanza halafu tuendelee. BONYEZA HAPA kufanya hivyo.

    NNE; HAUFIKIRII INJE YA BOKSI

    Siku za karibuni nimekuwa naongea na rafiki yangu mmoja ambaye huwa anafuatilia mafunzo yangu kwa njia ya mtandao. Anafanya kazi ya ubodaboda,ila anaonekana kama ameikatia tamaa. Maana ni kama haoni matokeo kwenye kile anachofanya na hata malipo yake anaona siyo makubwa sana. wiki iliyopita, nilimpa mbinu kadha wa kadha za kumsaidia kuongeza wateja zaidi na hivyo kulipwa zaidi.

    Sasa jana wakati naongea naye akaniambia ameanza kuona matokeo. Nikawa nimemwambia kuwa asifanye hicho kitu mara moja tu, badala yake awe na mwendelezo. Kwa siku ya jana nikamwambia kitu kimoja tu, nikawambia nenda ukannunue mfuko wa pipi. Halafu kwa kila abiria unayesafiri naye hakikisha kwamba unampa pipi ili aende anakula. Hiki kitu kilimshangaza kidogo ila alikifurahia sana.

    Akaanza kuniambia habari za basi ambazo huwa zinatoa pipi, biskuti na soda. Akaniambia kuna mwalimu wake alisafiri na basi wakampa pipi, soda na biskuti na tangu siku hiyo mwalimu huyo akawa ameapa kuwa atasafiri na basi hiyo hiyo siku zote ili apate soda, biskuti na pipi.

    Nikawa nimemwambia kuwa unapokuwa umesafiri na basi, unalipia nauli karibia elfu hamsini, sitini au sabini. Kwenye hiyo nauli yako, wenyewe wanatoa elfu mbili tu, wanakununulia wewe pipi mbili, soda moja na biskuti. Unapewa na huwasahau, sasa hiki kitu unaweza kukitumia. Ukimpa mtu pipi ya shilingi mia moja kutoka kwenye elfu mbli ya usafiri wako wa bodaboda unakuwa hujapunguza kitu kikubwa. ila unakuwa umejenga mteja wako wa nguvu maana siku nyingine yule mtu akitaka usafiri, hataanza kumtafuta bodaboda mwingne, badala yake atakutafuta wewe ili apate pipi ya kulamba njiani, wakati unamsafirisha. Daah, halafu darasa la kulipia kabia mimi nakupa bure hapa, hahaha.

    Kama nakuona na wewe unavyoenda kuitumia hii mbinu niliyompa jamaa jana. Hahaha

    Ila kitu kikubwa ninachotaka kumwambia ni kuwa mawazo ya kuboresha biashara au kitu chohote kile hayatoki kwa watu ambao wana plan B. mtu mwenye plan B akifeli anawaza kwenda kwenye kilimo, kwenye kilimo akilima tikiti zikamwangusha anawaza kwenda kwenye madini, kwenye madini akikutana na changamoto anawaza kwenda bandarini maana anasikia habari za watu wanaopata mabilioni. Akiwa hajatulia bandarini anasikia habari za watu wanaouza mbao Iringa anaenda Iringa. Akiika tu iringa, habari za kilimo cha mpunga Ifakara zinamfikia anahamia ifakara, sikiliza rafiki yangu, huwezi kutoboa kwenye maisha ukiwa na plan nyinginyingi hivyo. Kuwa na plan moja kisha komaa na hiyo.

    Ubora ni kuwa kadiri siku zinavyokuwa zinaendelea kusogea mbelea wewe mwenyewe unakuwa unazidi kuimarika na kuwa bora zaidi.

    Kabla sijaendelea mbele zaidi, naomba ufanye kitu kimoja. Weka barua pepe yako hapa chini,ili uwe unapokea mafunzo zaidi kutoka kwangu kwa njia ya baruapepe.  Fanya hivyo sasa hivi ili tuendelee

    TANO; PLAN B  INAKUKWAMISHA KUFANIKISHA PLAN YAKO KUU

    Ule muda unaouweka kwenye kufikiria plan B. Ule muda unaoutumia kufanyia kazi plan B, ni muda ambao unaupoteza, badala yake muda huu wote ungeweza kuuweka kwenye jambo lako kuu na kulifanyia kazi mpaka likafikia viwango vikubwa.

    Ujue unapokuwa na mambo mengi ambayo unafikiria kufanya, unakuwa hauweki akili yako na nguvu zako sehemu moja, ila unapokuwa na jambo moja na unapokoma na huilo jambo maana yake hata ukikutana na kikwazo au kitu chochote kile cha kukukwamisha, maana yake utapambana  kuhakikisha kwamba unalifanyia kazi jambo husika mpaka uweze kulifanikisha.

    SI TA; TAFITI ZINAONESHA KUWA PLAN B ni chanzo cha KUTOKUFANYA VIZURI

    Wanasayansi katika chuo kikuu cha Wharton na chuo Wisconsin walifanya utafiti kwa watu ambao waliwagawa kwenye makundi mawili. Kundi la kwanza lilikuwa la watu ambao walikuwa waliambiwa wafanye jambo fulani. Na kundi la pili liliambiwa lifanye jambo fulani, ila kwanza lilipaswa kufikiria endapo mambo hayataenda kulingana na matarajio yao itakuwaje. Kwa lugha nyingine ni sawa na kusema kwamba kundi la pili lilitakuwa kuwa na plan B.

    Mwisho wa siku majibu ya utafiti huo yalioonesha kuwa waliokuwa na plan B hawakufaya vizuri ukilinganisha na wale waliokuwa na plan moja tu.

    Mimi sina cha kuongeza, maana utafiti umeongea na umemaliza.

    Hivi nilisema kuna sababu 15 ee kwa nini haupaswi kuwa na plan B. Na bado unataka niendelee au niishie hapa! kama umependa makala hii, utapenda pia kitabu changu kipya cha JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO. Weka oda leo upate punguzo la kitabu hiki, soft copy itaanza kupatikana tarehe 10.10.2022. Na gharama ya softcopy ni 10,000/- ila ukilipia kabla ya tarehe 10, utaipata kwa elfu saba tu. Kwenye hiki kitabu nimejadili kwa kina mada hii ya plan B. Nina uhakika utaipenda tu. na sababu zilizobaki nimezimalizia kwenye kitabu.

    Umekuwa nami GODIUS RWEYONGEZA

    Asante sana kwa kusoma makala hii. hakikisha unajaza taarifa zako hapo chini ili uwe miongoni mwa watu ambao wataku wanapokea makala zangu kwa njia ya baruapepe. Huwa naandika makala nyingine zaidi na kuzituma kwa njia ya baruapepe. Ningependa na wewe uzipokee hizi makala, jaza taarifa zako hapa chini ili uzipate.

  • Viashiria 15 kuwa kipaji chako kitakufikisha mbali

    KIPAJI NI DHAHABU
    Rafiki yangu, nimeandika kitabu. Kinaitwa KIPAJI NI DHAHABU. Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa 0755848391 sasa

    Rafiki yangu mpendwa karibu sana kwenye makala ya siku ya leo. Na leo tunaenda kuona viashiria 15 vinayoonesha kuwa kweli hiki kipaji chako ulichonacho kinaenda kukufikisha mbali.

    1. upo tayari kuanza kidogo

    Kama upo tayari kuanza kidogo kisha kuendelea kukifanyia kazi kipaji chako ili kuhakikisha kwamba unakikuza na kukifikisha juu zaidi, basi hiki ni kiashiria tosha kuwa kipaji chako siku moja kitakufikisha mbali sana.

    2. Unafanya mazoezi mara kwa mara

    Bila kujali kuwa una kipaji kikubwa kiasi gani, mazoezi ni lazima ili uweze kukisukuma kipaji chako juu zaidi. kwa hiyo, kama una kipaji na unafanya mazoezi ya kipaji chako. Siyo mara moja na wala siyo mara mbili, bali kila siku. Basi ujue kuwa hiki kipaji chako kinaenda kukufikisha mbali kwelikweli.

    3. Unapenda kujifunza

    Kuna maarifa mengi yamejicficha kwenye vitabu. mtu ambaye hajifunzi na kupata maarifa mapya, ni mzee hata kama ana miaka 21 na mtu ambaye anajifunza na kupata maarifa, ni kijana hata kama ana miaka 75. Sasa wewe ni mzee au kijana? Kama wewe ni kijana, basi hiki ni kiashiria tosha kuwa unaenda kufanikiwa kwa viwango vikubwa

    4. Kufanya mambo ya msingi na kuachana nay ale ambayo siyo ya msingi’

    Ujue ndani ya siku kuna mambo  mengi ambayo unaweza kufanya, unaweza kuutumia muda kwenye kuchati, unaweza kuutumia muda wako kupiga soga na marafiki, unaweza kuutumia muda wako kwenye kuperuzi na mengineyo mengi. Ila kama kwa vyovyote vile unatoa muda wako na kuuwekeza kwenye kipaji chako na kufanya majukumu ambayo ni ya msingi kwako, hiki ni kiashiria tosha kwamba kwa vyovyote vile rafiki yangu, unaenda kufanikiwa kwenye kipaji chako na kipaji chako kitakufikisha mbali.

    Hivyo rafiki yangu, endelea kupambana na kufanya mambo ya msingi huku ukiachana na yale ambayo siyo ya muhimu.

    5. Kujihusisha na marafiki na watu chanya

    CHUMA KINANOA CHUMA. Huu ni usemi ambao huwa napenda kuusema na kuusisitiza, ningependa na wewe uufahamu pia, kuwa chuma, kinanoa choma. Hivyo, wale watu ambao unakuwa unatumia muda mwingi ukiwa nao, ni wazi kuwa wewe unaenda kuchukua tabia zao. Kama muda wako mwingi unautumia ukiwa na watu ambao wananoa vipaji vyao na kuvifanyia kazi, hicho ni kiashiria kingine kuwa wewe unaenda kufanya makubwa na kipaji chako.

    Nikiwa kwenye maonesho ya nanane na vitabu vyangu (2022)

    6. Una malengo na unayafanyia kazi

    Kama una malengo na hayo malengo unayafanyia kazi. labda ni malengo ya kufanya mazoezi, au malengo ya kujifunza, basi hiki ni kiashiria tosha kwamba unaenda kufanikiwa kwa viwango vikubwa sana. sasa swali langu kwako siku ya leo ni je, un malengo. Na je, hayo malengo unayafanyia kazi?

    7. Ukianguka unainuka

    Watu wengi huwa wanaanza vitu, pale wanapokutana na changamoto basi wanaachana na kile wanachofanya na hivyo kuendelea na maisha yao kama kawaida. Sikiliza rafiki yangu, changamoto ni moja ya kitu ambacho unahitaji kukifanyia kazi kwenye maisha yako. Changamoto hazijawahi kukosa kwenye maisha. Unapaswa kuzifanyia kazi, na kila unapoanguka, basi usisite kuinuka maana kuanguka ni sehemu ya maisha.

    8. Unapenda kujichangamotisha

    Ujue sisi binadamu hatupendi kufanya vitu vya tofauti. Mara zote huwa tunapenda kufanya vitu vilevile kwa namna ileile bila ya usumbufu wowote ule. Sasa kama unapeda kujichangamotisha na muda mwingine kuchukua hatua ambazo siku za nyuma ulikuwa hujawahi kuchukua, basi ukae ukijua kuwa hiki ni kiashiria tosha kuwa utafanikiwa sana na hicho kipaji chako.

    9. Upo tayari kwenda hatua ya ziada

    Wengi kwenye maisha wanapenda mabadiliko, ila hakuna ambaye yuko tayari kwenda hata hatua moja ya ziada ili kutengeneza hayo mabadiliko. Ila kama wewe unaenda hatua ya ziada na kufanya zaidi vile unavyopaswa kufanya, basi hiki ni kiashiria tosha kuwa unaenda kufanikiwa sana kwenye kile unachofanya.

    10.Unajiongoza

    Kuna watu wengi sana kama hawajielewi vile, ni mpaka awepo mtu wa kuwaongoza na kuwaonesha kitu gani cha kufanya, ndipo na wao wanaweza kufanya kitu. Kama hakuna mtu wa kuonesha au kuwaongoza kufanya hicho kitu, basi utakuta kwamba wale wanabweteka.

    Sasa kama unaweza kujiongoza kwenye majukumu yako na kuyafanya bila hata kuhitaji usimamizi, basi ujue wazi kuwa unaenda kufika mbali  sana na hicho kipaji chako.

    11. Unajikubali

    Kama hujikubal, basi hakuna mtu ambaye atakukubali. Rahisi tu kama hivyo.

    12. Unajali sana muda

    Muda ni mali. Hili wala hata halina ubishi, kama unatumia muda wako vizuri kwenye kunoa na kuendeleza kipaji chako badala ya kufanya mambo mengine ambayo hayana manufaa, basi hiki ni kiashiria iosha kuwa unaenda kufanikiwa sana na kipaji chako na utafika mbali.

    Rafiki yangu naomba utambue kwamba kwa siku tuna saa 24 tu. Sasa hizi saa unapaswa kuhakikisha kwamba umezitumia vizuri na kwa manufaa yako, kama wewe unautumia muda wako vizuri, basi hongera sana. Ila kama hautumii muda wako vizuri, basi jihoji mara mbilimbili ili kuanzia leo hii uanze kuutumia muda wako kwa manufaa na kwenye malengo na ndoto zako ambazo unafanyia kazi

    13. Una kocha

    Kama una kocha wa kukusimamia na kukufuatilia kwenye kile unachofanya, basi hiki ni kishiria kingine kuwa unaenda kutoboa. Asilimia kubwa ya watu wenye vipaji huwa wanakwama kwa sababu hawana msimamizi wa kuwafutilia kwa ukaribu, kitu ambacho huwa kinawafawanya wafanye vitu kwa motisha kwa siku chache na  baadaye kupoteza hiyo motisha. Ila unapokuwa na motisha na mtu wa kukusimamia nyuma yako, maana yake hata ukukikutana nchangamoto au kitu chochote, bado utajisukuma na kusongambele ili uweze kufikia malengo na ndoto zako.

    14. Unapata muda wa kupumzika

    Ni kweli kuwa unapaswa kupambana kwa ajili lya kuhakikisha unafanyia kazi kipaji, malengo na ndoto zako ili uweze kufikia malengo makubwa sana kwenye maisha. Ila pia unapawa kuwa na muda wa kupumzika ili usije ukafanya kazi kupitiliza mpaka ukapata burnout.

    Hiki ni kitu cha msingi ambacho huwa wanakifanyia kazi watu wanaofanikiwa na vipaji vyao, na wewe ukikifanyia kazi, basi hii itakuwa ishara tosha kuwa wewe unaenda kufanikiwa na kipaji chako.

    Unaweza kufanya kazi saa 18 kila siku jumatatu mpaka jumamosi, na jumapili ukapumzika na kupata muda wa kutosha wa kupumzika.

    15. unajali sana mahusiano yako

    Kama unajali sana mahusiano yako, mahusiano ya mwenza wako na familia yako. Basi ujue kwamba unaenda kufika mbali. Mwenza wako ni kiungo muhimu sana, kama mko sawa kwenye safari yenu ya mafanikio mtafika haraka, ila kama mnakinzana ni vigumu sana kufika.

    Sasa kuanzia leo hii, hakikisha kwamba mahusiano yako na mwenza wako unayatunza vizuri ili yaweze kukaa kwa usawa.

    Tofauti na hapo mimi nakutakia kila la kheri.

    Umekuwa name,

    Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro-Tz

  • Vitu 21 Ambavyo Ni Lazima Kufanya Hata Kama Una Kipaji Kikubwa

    KIPAJI NI DHAHABU
    Rafiki yangu, nimeandika kitabu. Kinaitwa KIPAJI NI DHAHABU. Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa 0755848391 sasa

    Rafiki, una kipaji si ndio! Hongera sana, mbali na kuwa una kipaji na unakifanyia kazi na una maono makubwa ya kukipeleka mbali kipaji chako mpaka kwenye ngazi za kimataifa. Ila kuna vitu vya msingi sana ambavyo hupaswi kuacha kufanya hata kama una kipaji kikubwa. kwenye hii sura ninaenenda kukushirikisha vitu 21 ambavyo hupaswi kuacha kufanya hata kama una kipaji kikubwa

    1. Unapaswa kuweka akiba.

    Rafiki yangu, bila kujali una kipaji kikubwa kiasi gani, haupaswi kuacha kuweka akiba. Mara zote hakikisha kwamba unaweka akiba kutokana na kiasi cha fedha ambacho unapokea. Hata kama ni kidogo kiasi gani. hakikisha kwamba mara zote unatoa kiasi kidogo na unakiweka kama akiba. Moja ya shida ambayo huwa inawakumba watu wenye vipaji wanapofikia umri wa kustaafu ni kuwa wanakuwa hawana akiba wala hela ambayo wanaweza kutumia. Yaani, mtu amekuwa anapambana kwa miaka mingi, ila sasa unapofika wakati kula matunda ya jasho lake, anakuwa hana matunda ya kula. Rafiki yangu, nataka wewe ujiondoe kwenye huu mtego kwa kuhakikisha kwamba unaweka akiba na kuwekeza. Na kiwango cha kuweka akiba siyo kikubwa sana, ni aslimia kumi tu ya kila kiasi ambacho kinaingia kwenye mfuko wako. Rafiki yangu, hiki ni kitu ambacho unapaswa kukipambania kila mara.

    Ila kwa hapa ningependa kukueleza mambo yafuatayo kuhusu uwekaji wa akiba

    Kwanza, leo hii nenda kafungue akaunti benki ambayo utakuwa unaweka akiba yako. Utafiti unaonesha kuwa watu wenye akaunti za benki, wanakuwa na utaratibu wa kujiwekea akiba, ukilinganisha na wale ambao hawana akaunti za benki.

    Anza kuweka akiba yako, hata kama ni kidogo. Ubora benki wanaruhusu kuweka kiasi cha chini ambacho ni elfu moja. hivyo, kila ukipata kiasi fulani cha fedha rafiki yangu, hakikisha kwamba unaweka akiba bila kukosa. Hiki kiasi hiki, kitakuja kukusaidia siku za mbeleni kwenye uwekezaji au hata malengo yako ya kukuza kipaji chako zaidi.

    NB: usiweke fedha yako chini ya godoro. Hizi zama za kuweka fedha chini ya godoro zimeshapitwa na wakati. sana tafuta kuweka akiba yako, sehemu ambayo huwezi kuifikia kwa haraka sana. Inaweza kuwa ni kwenye laini ya simu ambayo hujui namba yake siri yake ya mpesa.

    Inaweza kuwa ni benki au kwenye mifuko ya uwekezaji ya pamoja ya UTT. Kwa kuwa kitabu hiki siyo cha uwekaji wa akiba wala uwekezaji, basi naomba ukasome kitabu changu kinaitwa MAAJABU YA KUWEKA AKIBA na kingine kinaitwa MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE. Hivi vitabu viwili vitakufundisha kwa kina suala zima la fedha. Wasiliana nami kwa namba 0755848391 sasa.

    2. Unapaswa kuwekeza

    Rafiki yangu, kitu kingine muhimu sana ambacho unapaswa kujua na kukipa nguvu kubwa sana ni uwekezaji. Unapokuwa na kipaji, maana yake wewe unakuwa unafanya kazi kwa ajili ya kuingiza fedha. Usipokuwepo moja kwa moja maana yake siku hiyo hakuna kitu chochote kile ambacho kinaweza kufanyika kwa manufaa. Sasa kipaji chako kinakuwezesha wewe kupata fedha, na unapopata fedha unapaswa kuwekeza pia. Uwekezaji ni moja ya eneo ambalo linakufanya wewe uwe unapata fedha bila hata ya kuwepo kufanya kazi.

    Kwa hiyo basi rafiki yangu, napenda kukuhakikishia kuwa uwekezaji ni moja ya jambo muhimu sana kwenye maisha yako, ambalo unapaswa kufanya. Kwa hiyo, wekeza. Kwa kuwa wewe ni mgeni kwenye uliwengu wa uwekwezaji, basi hakikisha kuwa unaanza kuwekeza na kwa kuanzia, basi anza kuwekeza kwenye mifuko ya uwekezaji wa wa pamoja.

    Na ujue kiwango unachohitaji kuanza nacho ili uweze kuwekeza siyo kikubwa sana kama ambavyo unaweza kufikiria. Ni kiwango kidogo tu, ukiwa na elfu kumi unaweza kufungua akaunti kwenye mfuko wa umoja na baada ya hapo unaweza kuendelea kuwekeza zaidi na zaidi kwa kuweka kiwango cha chini cha elfu tano.

    Baada ya kuwa umefanya kazi kwa miaka yako yote, haupaswi kuwa mstaafu aliyefulia.

    Siku siyo nyingii nilikuwa nikisoma nikifuatilia historia ya Michael Jordan, nilichokuja kugundua kutoka kwa huyu jama ni kwamba, amewekeza kiasi cha kumwezesha kununua timu ya kikapu. Alipokuwa mchezaji, kile kiasi cha fedha alichokuwa analipwa alikuwa hatumii chote.

    Moja ya kitu kinachowafanya watu wenye vipaji bongo (wachezaji, wanariadha, wanamziki n.k) kufuria baada ya kustaafu ni kuwa pale wanapokuw wanaingiza fedha, basi wanaendekeza starehe kuliko wanavyowekeza. Hiki kitu unapaswa kuepukana nacho. Kuna madhara mawili ya kuendekeza starehe. Kwanza utajiona kama vile umefika kule unapotakiwa kwenda wakati bado ndio kwanza safari yako imeanza.

    Pili, ukiendekeza starehe utasahau kuchapa kazi na hivyo kushuka kwenye kiwango unachofanyia kazi kipaji chako. Unaukumba wimbo wa Tundaman na Chege wanaosema Starehe gharama?

    3. Unapaswa kujifunza na kufikiri kibiashara

    Kinachowakwamisha vijana wengi wa kitanzania kwenye vipaji vyao ni wao kufikiri kuwa; kwa kuwa wana vipaji basi wanapaswa kupambana wao kama wao tu. Sikiliza, kama unataka kipaji chako kifike mbali, basi kiweke kibiashara.

    Hii ndio kusema kwamba, angalia namna ya kuwahusisha watu wengine wakusaidie kwenye kipaji chako. Hawa wanaweza kuwa ni watu watakaokusaidia wewe kusambaza kile unachofanya, au wale watakaokusadia kuwafikia wateja wako. Kwa vyovyote vile, hakikisha kwamba kipaji chako hakikugandi, kifanye kuwa biashara ndio utafika mbali zaidi. Ndio maana huwa unaona wengine wanakuwa na meneja na vitu kama hivyo. Naombe nieleweke,kwenye hili kwamba, hakuna mtu ambaye huwa anafanya makubwa kwa kutumia dhana ya jeshi la mtu mmoja. Jeshi la mtu mmoja siyo practical kwenye ulimwengu wa leo. Ni kweli utaanza peke yako, lakini huwezi kutoboa kiwango cha kimataifa ukiwa ni jeshi la mtu mmoja! Unahitaji timu!

    4.Unapaswa kujifunza ujuzi wa kuongea na kuwasilisha kile ulichonacho mbele ya watu

    Hata kama una kipaji ni kama cha Khaby Lame, bado utapaswa kujifunza kuongea mbele watu. kwa sababu kuna siku utapaswa kuongea mbele ya watu. Watu watakuhoji na wewe utalazimika kuwasilisha mada mbele yao katika namna ambayo inaeleweka, kumbe kuongea mbele ya watu ni moja ya jambo ambalo haliepukiki rafiki yangu.

    5. Unapaswa kujenga tabia ya kusoma vitabu

    Vitabu ni nyenzo. Unajua nyezo lakini? Shule ya msingi tulijifunza kuwa kuna mzigo na jitihada. Hiki kitu kilikuwa kinarahisisha ufanyaji wa kazi. ambapo mtu ulikuwa na uwezo wa kusukuma mzigo mkubwa kwa nguvu kidogo. sasa vitabu pia ni wenzo daraja la kwanza! Vinakusaidia wewe kusukuma maisha na kusonga mbele kwa nguvu kidogo unayoweka kwenye vitabu.

    6. Kuondokana na uoga

    Uoga umewafanya watu wengi washindwe kufanyia kazi vipaji na uwezo wao. Uoga umewafanya watu washindwe kuthubutu, uoga umewafanya watu wapunguze kasi ya kufanyia kazi malengo yao. Rafiki yangu, ondokana na uoga, simama kisha songambele.

    7. Kuweka malengo na kuhakikisha kwamba unayafanyia kazi bila ya kuishia njiani

    Mwanzoni mwa mwaka watu wengi huwa wanaweka malengo ila waengi huwa wanaishia njiani. Kila mwaka unapasawa kuweka lengo ambalo utalifanyia kazi ili kuona wapi unafikisha kipaji chako.

    Linaweza kuwa ni lengo la kuongeza idadi ya watu wanaofuatilia kazi zako mitandaoni. Linaweza kuwa ni lengo la kuuza kazi zako kwa watu milioni moja. linaweza kuwa ni lengo la kuajiri mtu au watu kadhaa. linaweza kuwa ni lengo la kushirikiana na baadhi ya watu kwenye kazi zako n.k.

    Kwa vyovyote vile hakikisha kwamba unakuwa na malengo. Na malengo yako yanapaswa kuwa yamegawanywa kwenye malengo ya wiki, mwezi, mwaka na hata miaka mitano au kumi ijayo.

    Tonny Robinns aliwahi kusema kwamba, kuweka malengo ni hatua ya kwanza ya kubadili yasiyowezekana kuwa yanayowezekana.

    8. Kukubali kuwa maisha ni wajibu wako

    Kama kuna kitu ambacho kimekuwa kinawakwamisha vijana na watu wengi, ni pale ambapo wao wanafikiri kuwa maisha siyo wajibu wao, badala yake wanafikiri kuwa kuna mtu, ambaye anaweza kuwa ni serikali au mjomba ambaye anahusika na maisha yao. Naomba nikwambie hili na ulipokee rafiki yangu, ukweli ni kuwa maisha ni wajibu wako. Ukifeli ni juu yako na ukifanikiwa ni juu yako. Ukilifahamu hili, utaishi maisha kwa raha mustarehe sana rafiki yangu. Unajua kwa nini? Kwa sababu, hutakaa na kuanza kumsubiri mtu ili akusaidia kwenye kufanyia kazi maisha yako, badala yake utapambana kuhakikisha kamba maisha yanakuwa ni wajibu wako kwelikweli.

    Utaachana na malalamiko ambayo unatoa sasa hivi. badala ya kusema kwamba serikali haitoi ajira, wewe utapambana kuona ni kwa namna gani unaweza kutengeneza ajira. Ujue unaweza kuwa unalalamika kuwa hakuna ajira, kumbe wewe ndiye unapaswa kuwa mtoaji wa ajira.

    9. kuwa kiongozi

    Wengi huwa wanachanganya uongozi na cheo. Kitu hiki huwafanya wengi wafikiri kuwa kiongozi ni lazima uwe na cheo. Hapana.

     Haikuhitaji uwe na watu na watu wanakuja kwako kwako kuleta kesi ili uwe kiongozi. Maana yake unaweza kuwa mkulima ila wewe ni kiongozi, mwalimu bodaboda au yeyote ila ni kiongozi. Siku zote nimekuwa nawaambia watu kwamba kila mtu ni kiongizi tangu kuzaliwa kwake.

    Kama wewe unaweza kuamka asubuhi na kupangilia mipango yako jinsi itavyoonda na kujiwwkea ratiba nzuri na kuifuata basi wewe ni kiongozi. Kama wewe hauna mtazamo wa kushawishi watu kufanya vizuri zaidi katika shughuli zao basi wewe ni mfuasi.
    Hata kama utakuwa na cheo cha uongozi watu hawataweza kukufuata kwa sababu wanaona matendo yako hayaendani na kile unachosema.

    Kiongozi wa ngazi ya juu ambaye muda wote amejifungia hataki kuongea na watu wala hataki kuwa karibu na watu basi huyo sio kiongozi ni mfuasi.

    10. kuamka mapema

    Siwezi kukumbuk ni marangapi nimekuwa nikisisitiza juu ya umuhimu wa kuamka mapema, lakini bado nalazimika kuendelea kufanya hivi. kuamka asubuhi na mapeka kuna manufaa mengi sana.

    Kwanza unaamka muda ambao watu wengi wamelala. Hakuna kelele (labda kama unakaa ghetto na washikaji, wanaowasha muziki usiku kucha,hahah). Muda huo hakuna mtu wa kukupigia simu, labda kama utaamka kuongea na mchumba wako aliye Moshi wakati wewe uko Mwanza. Hakuna watu wanakuja kukugongea chumbani kwako. yaani, ni wewe tu na Mungu wako.

    Kitu hiki kinakupa nafasi nzuri tu yaw ewe kupata muda wa kufikiri, kupanga ratiba yako ya siku hiyo, kupanga watu ambao utaenda kuwapigia, kupanga watu ambao utaenda kukutana nao na mengine mengi. Kwa hiyo basi rafiki yangu, itumie nafasi ya kuamka asubuhi na mapema vizuri sana.

    Nakubaliana na Benjamin Franklin aliyewahi kusema kwamba, kuamka asubuhi na mapema na kulala mapema kunamfanya mtu awe na afya njema, tajiri na mwenye busara.

    11. kuinuka baada ya kuanguka

    Maisha ni safari rafiki yangu, na kama ilivyo safari yoyo tile. Lazima kwenye kusafiri kwako kuna sehemu ambapo utakutana na mlima, hivyo utapanda huo mlima, na kuna sehemu utakutana na bonde, utashuka. Rafiki yangu, hizi zote ni sehemu za maisha na zinatokea kwenye maisha yetu ya kila siku. Sasa inapotokea umejikwaa kwenye safari yako, basi usije ukarudi nyuma na kuacha kufanyia kazi kile unachopaswa kuwa unafanyia kazi. Endelea kupambana rafiki yangu, mpaka kieleweke. Ukianguka inuka. Inawezekana.

    12. Kuanza na kile ulichonacho

    Wengi huwa wanasubiri wawe na kila kitu ndio waanze, wewe usisubiri kuwa na kila kitu ili uweze kuanza. Anza na kile ulichonacho.

    • Usisubiri uwe maarufu ili unoe kipaji chako, anzia hapo hapo ulipo na hicho ulichonacho.
    • Usisubiri uwe kama rais Mwinyi ili uandike kitabu. Andika kitabu, halafu hiyo ngazi yake utaifikia mbele ya safari.
    • Usisubiri mpaka uwe na fedha ili uanze kuweka akiba, anza kuweka akiba kwa kiwango hicho hicho ulichonacho. Ngoja nikwabie kitu, asilimia kubwa ya vitu unavyohitaji kufanya, unaweza kuanza kuvifanya sasa hivi bilaya kuchelewa.

    13. epuka kujilinganisha na watu wengine

    Daah, kama kuna kitu kinawatafuta vijana wengi basi ni hiki; kujilinganisha.

    • Eti kwa sababu fulani kaajiriwa basi ngoja na mimi nipambane ili niajiriwe.
    • Eti kwa sababu fulani kajenga nyumba kijijini kwetu basin a mimi mpaka nikajenge.
    • Eti kwa sababu, fulani yuko kwenye mahusiano na mimi lazima nimpate wa kwangu. Haya bwana kampate,hahaha

    Ukijilinganisha, ni wazi kuwa hutaweza kuishi maisha yako kwa namna ambavyo unataka wewe. Maisha yako yatakuwa ni magumu sana,sana. Ishi maisha yako na furahia hilo. Furahia hatua wanazopiga wengine, maana siyo kila hatua lazima na wewe uipige kwa wakati huohuo.

    Wakati wengine wanajenga kijijini, wewe uko hapa unawekeza kwenye UTT. Mtu anaweka milioni 50 kwenye kujenga nyumba ya kuishi na familia yake, wewe unaweka milioni hamsini UTT, kwenye mfuko wa hatifungani, unaotoa gawio kila mwezi. Nani kawin hapa? Kama huelewi uwekezaji huu wa kwenye mifuko ya Utt, unaweza usinielewe ninachojaribu kukueleza hapa, ndio maana nakushauri upate kitabu changu cha maajabu ya kuwekeza kwenye hisa, hatifungani na vipande ili uweze kunielewa vizuri hapa. Ebu rusha elfu tano tu, kwenye simu yangu nikurushie hiki kitabu. Namba ya simu 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy0
    Kitabu hiki kinapatikana kwa elfu tano tu (sotfcopy)

    14. Epuka kufuatilia maisha ya watu wengine

    Moja ya kitu ambacho unahitaji kuhajkikisha kwamba unaachana nacho kama unataka kufika mbali na kuachana na suala zima la kufuatilia maisha ya watu wengine. Kuna watu wengine wanajua mwenendo wa maisha ya watu wengine, kuliko wanavyo jua kuhusu maisha yao. Hli ni kosa kubwa ambalo unaweza kufanya kwenye maisha yako. Hakikisha kwamba unayajua maisha yako kuliko mtu mwingine au kwa lugha nyingine jifuatilie wewe mwenyewe kuliko unavyomfuatilia mtu mwingine. hivi kwa mfano, kama wewe ungekuwa ni kampuni, je, watu waengewekeza kwenye hiyo kampuni kununua hisa zake, wewe mwenyewe ungewekeza kwenye kampuni wewe kununua hisa zako mwenyewe! Kama jibu ni hapana, maana yake unahitaji kujiboresha.

    Na njia nzuri ya kujiboresha, ni wewe kuacha kufuatilia maisha ya watu wengine, na kufuatilia zaidi maisha yako wewe mwenyewe.

    15.kutokuhofu kuhusu kile ambacho watu wengine wanafikiri juu yako

    Watu wengine wanasemaje kuhusu wewe? Kwa chochote kile unachokuwa unafanya, fahamu kuwa kuna watu ambao watakusema.

    Hata ukicheka, kuna watu watasema, hebu mwone na huyu anavyocheka. Sasa unataka nichekeje? Binadamu bwana…

    Kwa hiyo hilo lifahamu na wala lisikuchanganye.

    Kama kuna kitu cha kuondoka nacho hapa ni kuwa kila mtu ana kazi yake. Wewe kazi yako ni kuhakikisha kuwa kipaji chako king’aa. Wengine kazi yao ni kuhakikisha kuwa wanakusema.

    Nadhani umenielewa hapo.

    14. kuwa na mipango ambayo unaifanyia kazi

    Hakuna mtu ambaye huwa anaandika mipango ya kuwa mnene, mzembe,mjinga, asiyejali au baba/mama aliyetelekeza watoto.

    Lakini ukweli ni kuwa kama hutaweka mipango ya kuwa afya njema, mchapakazi, anayejali, ni sawa na kuweka mipango ya kuzembea.

    Kwa hiyo usije ukajishangaa umekuwa mnene, mzembe, asiyejali. Hukuweka mipango ya kuwa na hivi vitu, ila kwa kutokuweka mipango, unakuwa unastahili kuvipata.

    Nimeandika sana, sasa mpaka naandika kuandika faslsafa. Ebu niishie hapa mengine nayaacha kwa ajili ya siku zijazo.

    Kama una swali, maoni, au kitu chochote ungependa kusema, basi au hata ungependa kuchangia kidogo kwa ajili ya kuwezesha makala bora ziendelee kuwa hewani, basisi usisite kutucheki kupitia 0755848391.

    ©Haki zote zimehifadhiwa

    Nimesikiliza na nitasikiliza tena

  • Vitu vitano (05) Vitakavyokufanya uheshimike

    Rafiki yangu bila shaka unaendelea vyema kabisa. siku ya leo ningependa kukushirikisha vitu vitano ambavyo vitakufanya wewe uweze kuheshimika kwenye kazi, kwenye mahusiano na kwenye maisha kiujumla. Kwa hiyo, kama unataka kuheshimika rafiki yangu, hivi hapa ni vitu vitano ambavyo unapaswa kuanza kufanyia kazi mara moja.

    1. KITU CHA KWANZA NI KUCHAPA KAZI

    Kazi ni kitu ambacho kinampa mtu heshima. Na hata maandiko mbalimbali yamethibitisha na kusisitiza hili la kufanya kazi kwa namna tofauti tofauti, huku maandiko maarufu yakiwa yale yanayosema kwamba asiyefanya kazi basi asile. Rafiki yangu, kazi ni moja ya kipimo cha utu.

    Kwa hiyo, kama unataka kuheshimika kwenye jamii, basi fanya kazi.

    Kwa watu wengi unapoongelea kazi, basi kinachokuja kwenye kichwa chao au kwenye akili zao ni kuwa ajira.  Yaani, kazi fulani hivi ya kukaa ofisini huku kukiwa na kiyoyozi, huku wenyewe wakiwa wananesa kwenye kiti fulani hivi amazing! Rafiki yangu, kuna tofauti kubwa sana kati ya kazi na ajira.

    Kamusi ya Kiswahili sanifu inasema kazi ni shughuli anayofanya mtu kama vilekulima, kuandika au kufundisha.

    Huku ikisema kuwa ajira ni kazi izitolewazo au zifanywazo kwa malipo katika kampuni serikalini au kwa mtu binafsi.

    Kumbe kwa mantiki hiyo ndiyo kusema kwamba, kazi zipo nyingi. Kufanya kazi siyo lazima uwe umeajiriwa chini ya mtu, unaweza kufanya kazi hata kama hujaajiriwa. Unaweza kujishughulisha wewe mwenyewe. Kwa mfano unaweza kuanza kutengeneza vitumbua na kusambaza kwa kuanzia mtaani kwako. hivi kweli kitu kama hiki nacho kinaweza kukushinda?

    Kitumbua kimoja kinauzwa shilingi 100. Kila siku ukijiwekea lengo la kutengeneza vitumbua na kuuza vitumbua 500, maana yake kila siku utakuwa unaingiza kiasi cha shilingi  elfu hamsini.  ili uweze kufanikisha lengo lako hili la kuuza vitumbua 500 kila siku unahitaji walau uwe na kijana mmoja ambaye anajituma na anafanya kazi kwelikweli. Mmoja wenu, anaweza kuwa yeye au wewe anakaa chini na kutengeneza vitumbua, huku mwingine akizunguka mtaani na kusambaza vitumbua kwa watu wenye uhitaji, ikiwa ni pamoja na kwenda kwenye maeneo yenye mkusanyko mkubwa watu kama stendi na sokoni.

    Rafiki yangu, kwa jinsi hii unakuwa umejitengenezea kazi lakini wakati huohuo unakuwa tayari umetengenza ajira. Kwenye hiyo shilingi elfu hamsiini uliyouza ndani ya siku husika, ukitoa gharama au mtaji wa biashara yako. Huwezi kukosa kubaki na hela ya kwako, tena hela ya maana tu. ebu tuchukulie baada ya kutoa gharama zote ukabaki na elfu ishirini tu. Hii siyo hela kidogo, ukiwa unaingiza kiasi hiki cha hela kwa mwezi ni sawa na laki sita!

    Wewe unakuwa siyo mtu wa viwango vya kawaida. Mpaka hapo unakuwa umeua ndege wawili kwa jiwe moja, ukiendelea kukaza unashangaa baada ya miaka mwiili una kiwanda chako cha kutengeneza vitumbua. Usicheke, ujue hapa naongea vitu siriazi!

    Kwa hiyo, rafiki yangu, achana na dhana ya kulia kuwa hauna kazi kuanzia leo hii. tafuta kazi na anza kufanya kazi.

    • Inaweza kuwa ni kutengeneza vitumbua kama nilivyokwambia
    • Inaweza kuwa ni vitu vingine kama kuuza karanga, kulima mboga, na vitu vingine vingi
    • Nadhani kuna mawazo mengi ambayo unaweza kuanza kufanyia kazi leo hii, tena ambayo yanahitaji mtaji mdogo tu!

    Tatizo kubwa linalowakumba vijana wengi ni kudharau kazi wakati hawana kazi. Na hii zaidi ni kwa wasomi ambao wamehitimu vyuo na ngazi nyingine, wanaona kwamba baadhi yakazi siyo kazi za viwango vya, hivyo, kitu pekee ambacho wao wanaamua kufanya ni kukaa bila kufanya kazi.

    Rafiki yangu, kama hauna kazi na haujui kitu gani unaswa kufanya, basi usidharau. Chagua kazi yoyote ile kisha anza kuweka juhudi kwenye hiyo kazi. Ifanye ili iweze kukuingizia kipato.

    Siyo eti kwa sababu umesoma basi muda wote unabaki kusuka nywele huku ukihofia kwenda shambani kufuga na kulima, huku ukiendelea kulalamika kuw ahuna kazi.

    Kuuza vitu vya mia mia

    Hapo juu nimetolea mfano wa mtu ambaye ameamua kujiajiri kwa kufanya kuuza vitumbua. Tena nikatolea mfano kuwa kitumbua kimoja kinauzwa shilingi mia moja! (japo vipo vitumbua ambavyo vinauzwa zaidi ya hapo). sasa hapa ninachotaka kukwambia ni kuwa vitu vya mia mia vinawapa hela kuliko unavyoweza kufikiria.

    Ndio maana unaona mpaka mabilionea wanazidi kutegeneza vitu vya mia mia! Hivi kiberiti, kinauzwa shilingi ngapi vile… Huku mtaani kwetu kinauzwa shilingi mia moja sijajua huko kwenu. Mo Dewji ni bilionea mkubwa hapa Tanzania, ila huku mtaani kuna viberiti ambavyo ametengeneza yeye.

    Hivi, pipi zinauzwa shilingi ngapi vile…najua utaniambia bei tofauti zikiwemo za mia moja na mia mbili au hata zaidi..

    Kuna watu wenye hela zao, wamewekeza mabilioni ya hela wanatengeneza pipi eti. Tena pipi zingine zinauzwa shilingi hamsini tu za Kitanzania.

    Ninachotaka kukwambia ni nini? ninataka kukwambia kwamba usidharau vitu vidogo, maana hivi vitu vidogo mwisho wa siku huwa vinakuwa na matokeo makubwa kuliko unavyoweza kufikiri.

    2. KUTHIBITI HISIA ZAKO

    Najua kuna watu wengi ambao tunaishi nao kwenye jamii na huwa wanatukosea au hata muda mwingine kutulazimisha tuingie kwenye migogoro nao.

    Unaweza kushangaa unatembea mtu anakukanyaga halafu anakutukana. Au unaendesha gari, mtu akaku overtake katika eneo ambalo kisheria halafu anakuoneshea ile ishara fulani hivi ya kidole….

    Sasa haya yote watu wanaweza kuyafanya ili kukukasirisha wewe, ila moja ya kitu ambacho unahitaji kukifanya ni wewe kuthibiti hisia zako. muda mwingine watu wanapokuwa wanafanya vitu kama hivi, wewe unahitaji kuwa mpole na hata kuwachukulia kama watoto wadogo.

    Mtoto mdogo akikutukana, basi wewe utasema kwamba huu ni utoto. Sasa na kwa hawa inapaswa kuwa hivyohivvyo, badala ya wewe kukimbizana nao na kugombana nao, badala yake weka nguvu kubwa  kwenye malengo yako na ndoto zako. Wachkulie tu kama watoto wadogo, mtoto mdogo akikutukana ni wazi kuwa wewe huwezi kumtukana na kukasirika. Badala yake utasema huu ni utoto tu

    3. KUSIKILIZA ZADI YA UNAVYOONGEA

    Hiki ni kitu kingine ambacho kitakufanya uweze kuheshimika zaidi ujue dunia imejaa na waongeaji zaidi ya wasikilizaji, na kusikiliza ni ujuzi ambao unapaswa kuwa nao kwenye hizi zama.

    Mimi kuna watu huwa wananipigia simu na kuongea watakavyo, kwa sababu huw wanajua kuwa tu nitawasikiliza. Unkuta mtu shida yake siyo kubwa sana, ila sasa anahitaji mtu ambaye atamsikiliza kwa umakini na kumpa muda way eye kuongea. Kile kitendo cha mtu kusikilizwa kinampa pumziko la roho nay eye anakuwa kama ametua mzigo mkubwa.

    Rafiki yangu, anza kujenga utaratibu wa kusikiliza badala ya kuongea sana. nakuhakikishia kuwa utajifunz amengi kutoka kwa watu kuliko pale unapokuwa muongeaji sana.

    NNE, KUWAACHA WATU KWENYE NAFASI NZURI KULIKO ULIVYOACHA.

    Rafiki yangu, nataka nikupe zoezi moja kuanzia siku ya leo. Na zoezi hili ni kuwa, kila unapokutana na mtu, angalia ni kwa namna gani utamwacha katika hali nzuri kuliko ulivyomkuta. Unaweza kufikiri kwamba ili ufanye hili basi utahitaji kuwa na fedha, hapana.

    Moja unaweza kuongeza juhudi ambazo watu wanaweka kwenye kazi wanazofanya. Kuna watu wanafanya kazi au vitu ila hawajawahi kupata mtu wa kuwapongeza na kukubali kile wanachofanya. Sasa kwa nini wewe usiwape moyo na kuwaambia kwamba kile wanachofanya ni kitu kizuri na chenye manufaa kwa jamii. Nakwambia rafiki yangu, hiki ni kitu kidogo, ila chenye nguvu kubwa sana ambacho unapaswa kuzingatia.

    Je, na hilo rafiki yangu, linaweza kukushinda?

    5.  KUWA NA FEDHA ZAKO MWENYEWE

    Nadhani hili halina ubishi, kwenye hii blogu nimekuw anikiandika mara kwa mara kuhusu fedha. Lakini kwa lleo ningependa kusema kitu kimoja tu kuhusu fedha.

    Na kitu hiki ni kuwa, fedha inakufanya uheshimike hata kama ni mdogo, na kama hauna fedha unadharaulika hata kama ni mtu mzima.

    Mfano rahisi tu ni kwenye vikao vya familia. Mwenye fedha kwenye kikao anasikilizwa kuliko ambaye hana fedha.

  • Tofauti Kati Ya Kazi na Ajira

    Kazi ni kitu ambacho kinampa mtu heshima. Na hata maandiko mbalimbali yamethibitisha na kusisitiza hili la kufanya kazi kwa namna tofauti tofauti, huku maandiko maarufu yakiwa yale yanayosema kwamba asiyefanya kazi basi asile. Rafiki yangu, kazi ni moja ya kipimo cha utu.

    Kwa hiyo, kama unataka kuheshimika kwenye jamii, basi fanya kazi.

    Kwa watu wengi unapoongelea kazi, basi kinachokuja kwenye kichwa chao au kwenye akili zao ni kuwa ajira.  Yaani, kazi fulani hivi ya kukaa ofisini huku kukiwa na kiyoyozi, huku wenyewe wakiwa wananesa kwenye kiti fulani hivi amazing! Rafiki yangu, kuna tofauti kubwa sana kati ya kazi na ajira.

    Kamusi ya Kiswahili sanifu inasema kazi ni shughuli anayofanya mtu kama vilekulima, kuandika au kufundisha.

    Huku ikisema kuwa ajira ni kazi izitolewazo au zifanywazo kwa malipo katika kampuni serikalini au kwa mtu binafsi.

    Kumbe kwa mantiki hiyo ndiyo kusema kwamba, kazi zipo nyingi. Kufanya kazi siyo lazima uwe umeajiriwa chini ya mtu, unaweza kufanya kazi hata kama hujaajiriwa. Unaweza kujishughulisha wewe mwenyewe. Kwa mfano unaweza kuanza kutengeneza vitumbua na kusambaza kwa kuanzia mtaani kwako. hivi kweli kitu kama hiki nacho kinaweza kukushinda?

    Kitumbua kimoja kinauzwa shilingi 100. Kila siku ukijiwekea lengo la kutengeneza vitumbua na kuuza vitumbua 500, maana yake kila siku utakuwa unaingiza kiasi cha shilingi  elfu hamsini.  ili uweze kufanikisha lengo lako hili la kuuza vitumbua 500 kila siku unahitaji walau uwe na kijana mmoja ambaye anajituma na anafanya kazi kwelikweli. Mmoja wenu, anaweza kuwa yeye au wewe anakaa chini na kutengeneza vitumbua, huku mwingine akizunguka mtaani na kusambaza vitumbua kwa watu wenye uhitaji, ikiwa ni pamoja na kwenda kwenye maeneo yenye mkusanyko mkubwa watu kama stendi na sokoni.

    Rafiki yangu, kwa jinsi hii unakuwa umejitengenezea kazi lakini wakati huohuo unakuwa tayari umetengenza ajira. Kwenye hiyo shilingi elfu hamsiini uliyouza ndani ya siku husika, ukitoa gharama au mtaji wa biashara yako. Huwezi kukosa kubaki na hela ya kwako, tena hela ya maana tu. ebu tuchukulie baada ya kutoa gharama zote ukabaki na elfu ishirini tu. Hii siyo hela kidogo, ukiwa unaingiza kiasi hiki cha hela kwa mwezi ni sawa na laki sita!

    Wewe unakuwa siyo mtu wa viwango vya kawaida. Mpaka hapo unakuwa umeua ndege wawili kwa jiwe moja, ukiendelea kukaza unashangaa baada ya miaka mwiili una kiwanda chako cha kutengeneza vitumbua. Usicheke, ujue hapa naongea vitu siriazi!

    Kwa hiyo, rafiki yangu, achana na dhana ya kulia kuwa hauna kazi kuanzia leo hii. tafuta kazi na anza kufanya kazi.

    • Inaweza kuwa ni kutengeneza vitumbua kama nilivyokwambia
    • Inaweza kuwa ni vitu vingine kama kuuza karanga, kulima mboga, na vitu vingine vingi
    • Nadhani kuna mawazo mengi ambayo unaweza kuanza kufanyia kazi leo hii, tena ambayo yanahitaji mtaji mdogo tu!

    Tatizo kubwa linalowakumba vijana wengi ni kudharau kazi wakati hawana kazi. Na hii zaidi ni kwa wasomi ambao wamehitimu vyuo na ngazi nyingine, wanaona kwamba baadhi yakazi siyo kazi za viwango vya, hivyo, kitu pekee ambacho wao wanaamua kufanya ni kukaa bila kufanya kazi.

    Rafiki yangu, kama hauna kazi na haujui kitu gani unaswa kufanya, basi usidharau. Chagua kazi yoyote ile kisha anza kuweka juhudi kwenye hiyo kazi. Ifanye ili iweze kukuingizia kipato.

    Siyo eti kwa sababu umesoma basi muda wote unabaki kusuka nywele huku ukihofia kwenda shambani kufuga na kulima, huku ukiendelea kulalamika kuw ahuna kazi.

    Kuuza vitu vya mia mia

    Hapo juu nimetolea mfano wa mtu ambaye ameamua kujiajiri kwa kufanya kuuza vitumbua. Tena nikatolea mfano kuwa kitumbua kimoja kinauzwa shilingi mia moja! (japo vipo vitumbua ambavyo vinauzwa zaidi ya hapo). sasa hapa ninachotaka kukwambia ni kuwa vitu vya mia mia vinawapa hela kuliko unavyoweza kufikiria.

    Ndio maana unaona mpaka mabilionea wanazidi kutegeneza vitu vya mia mia! Hivi kiberiti, kinauzwa shilingi ngapi vile… Huku mtaani kwetu kinauzwa shilingi mia moja sijajua huko kwenu. Mo Dewji ni bilionea mkubwa hapa Tanzania, ila huku mtaani kuna viberiti ambavyo ametengeneza yeye.

    Hivi, pipi zinauzwa shilingi ngapi vile…najua utaniambia bei tofauti zikiwemo za mia moja na mia mbili au hata zaidi..

    Kuna watu wenye hela zao, wamewekeza mabilioni ya hela wanatengeneza pipi eti. Tena pipi zingine zinauzwa shilingi hamsini tu za Kitanzania.

    Ninachotaka kukwambia ni nini? ninataka kukwambia kwamba usidharau vitu vidogo, maana hivi vitu vidogo mwisho wa siku huwa vinakuwa na matokeo makubwa kuliko unavyoweza kufikiri.

X