Category: A NOTE FROM SONGAMBELE

  • Mtag ambaye ungependa ujumbe huu umfikie

    Kwenye vipindi mbalimbali vya redio huwa kuna kipindi cha kutuma salamu na ujumbe. Kama kuna mtu ambaye leo hii ungependa ujumbe huu umfikie mtag hapa ili aje auone. UWE NA SIKU NJEMA

  • Hiki Ndiyo Kiwango cha mafanikio ambayo unapaswa kuyapigania

    / Rafiki yangu aliwahi kuniambia kwamba kuna wakati aliangalia tamthiliya. Kwenye tamthilya hii kuna jamaa aliachwa na mke wake. Mke alimwacha kwa sababu jamaa hakuwa na hela. Badala ya kukimbilia kuingia kwenye mahusiano mengine ili amuoneshe ex wake kwamba hajamkomoa kwa kuachwa. Jamaa aliamua kuanza kupambana ili kujenga biashara na kuzisaka hela. Akapambana kwelikweli kiasi…

  • Kitu Hiki Unapaswa Kukibadili Mara Moja

    Moja ya siku ambayo watu huwa wanaadhimisha ni siku ya kuzaliwa. Ukiachana na sikukuu ya kuzaliwa kuna sikukuu maarufu sana ambazo huwa tunaadhimisha, ikiwa ni pamoja na Eid, Pasaka, Krismasi, Mwaka mpya na nyingine.. Ukiziangalia hizi sikukuu zote zina kitu kimoja ambacho kinaziunganisha. Hizi sikukuu zote huwa zinatokea kwa sababu ya kalenda. Ni sikukuu za…

  • Anza na kile ulichonacho

    Tuanze na kile tulichonacho. Tufanye kinachowezekana sasa hivi kabla ya kuja kufanya yasiyowezekana. Rafiki yangu mpendwa salaam, umekuwa unajiuliza ni kwa namna gani unaweza kufanya makubwa kwenye maisha yako. Njia bora ya wewe kufanya makibwa ni kwa wewe kuanza na yale ambayo unaweza sas hivi. Kufanya kinachowezekana sasa hivi kabla ya kuja kufanya yasiyowezekana. Wengi…

  • Watu 60 Walioshindwa Karibia Kwenye Kila Kitu Na Bado Wakashinda Kwa Kishindo

    Watu 60 Walioshindwa Karibia Kwenye Kila Kitu Na Bado Wakashinda Kwa Kishindo Katika maisha, kila mmoja wetu anakutana na changamoto, vikwazo, na kushindwa mara kwa mara. Lakini je, unajua kuwa watu wengi maarufu na wenye mafanikio makubwa walipitia hali ngumu zaidi, kushindwa tena na kabla ya kufanikiwa kwa kishindo? Kitabu hiki “Watu 60 Walioshindwa Karibia…

  • Penye Changamoto Pana Fursa.

    Ndiyo maana tunapaswa kupambana. Maisha muda mwingine yanabadilila kwa sababu Kuna changamoto, Bila ya hizi changamoto mambo MAKUBWA tunayoona Leo tusingekuwa tunayaona. Leo ngoja nikupe Mifano ya vitu vilivyogunduliwa baada ya kuwepo kwa changamoto 1. Penicillin: Alexander Fleming aligundua penicillin, dawa ya kwanza ya antibiotic, baada ya kukutana na changamoto ya kutafuta njia ya kuzuia…

  • Maisha ni wajibu wako, ukishinda ni juu yako, ukishindwa ni juu yako pia

    Usije ukafanya kosa la kutaka kuwaachia wengine jukumu la maisha yako. Hakuna mtu anayeweza kujali kuhusu maisha yako kama wewe mwenyewe. Wewe ndiye mtu wa kwanza unayepaswa kujali kuhusu maisha yako kabla ya mtu mwingine yeyote.Na unapaswa kulifanyia kazi kwa uhakika bila ya kurudi nyuma wala kukubali kukwamishwa na mtu au kitu chochote.Kuwa na ndoto…

  • Kwa Nini KUWEKA akiba ni Muhimu Hata Kama Hujui Lini Utakufa

    Vipi usipokufa na huna akiba na ukaishi mpaka miaka 80 au 90? Ni kweli kwamba kifo ni jambo lisilotarajiwa, lakini pia ni kweli kwamba unaweza kuishi maisha marefu. Bila akiba, maisha hayo marefu yanaweza kuwa magumu na yenye changamoto nyingi za kifedha. Hapa kuna sababu za kwa nini kuweka akiba ni muhimu hata kama hatujui…

  • MAMBO MUHIMU KUHUSU KUWEKA AKIBA

    Kwenye somo la leo ninakueleza kwa undani mambo ya msingi na ya muhimu sana ambayo unahitaji kuzingatia linapokuja suala zima la kuweka akiba. Kuna makosa ambayo umekuwa unayafanya, lakini habari njema ni kwamba haya makosa unaweza kuyaepuka. Haya yote yameelzwa kwa kina kwenye somo la leo. Hakikisha umelfuatilia somo hilimpaka mwisho. Kujipatia nakala za vitabu…

  • Kitu Aambacho Kimekuwa Kikikwamisha Watu Wengi. Kinakukwamisha Na WEWE pia?

    Kama kuna mtu ambaye unaona kwamba ameweza kufikia mafanikio makubwa, basi ujue kwamba kuna gharama ambazo ameliipa na wewe hujalipa hizo gharama, unapaswa kuwa tayari  kulipa gharama ambazo mtu huyu amelipa ili uweze kufikia kwenye ngazi ambazo yeye amefikia. Kama unataka kujenga biashara kubwa ambayo itakufikisha kwenye ngazi ya ubilionea unapaswa kuwa tayari kulipa gharama…

  • Shhh! Sikiliza Vizuri; pesa ya akiba siyo pesa ya kula

    Ukikosa pesa ya kula, pambana kadiri unavyoweza kuhakikisha kwamba unaipata sehemu nyingine ila siyo kwenye akiba Yako Akiba iwekwe kwa lengo maalum. Ni muhimu zaidi kama akiba itawekwa sehemu ambayo huwezi kufikia kwa haraka. Hii itakusaidia kutokuwa unaifikiria mara kwa mara, kitu kitakachokupelekea wewe kuitoa. Kama Bado hujajipatia nakala ya kitabu Cha MAAJABU YA KUWEKA…

  • Kuandika kunahitaji Nidhamu. Unakuwa na vitu Gani vingi vinavyokufanya usiandike?

    Unakuwa na vitu Gani vingi vinavyokunya ukose hata dakika 15 za Kuandika kila siku? Kuandika kunahitaji nidhamu. Kama ambavyo kusoma darasani kunahitaji nidhamu ili ufaulu, Kuandika pia kunahitaji nidhamu. Nidhamu ya Kuandika. Ukiona mtu ameandika na kitabu chake kimekamilika, ujue Moja ya gharama aliyoilipa ni nidhamu ya kukaa chini na Kuandika.Kuandika hata pale alipokuwa hajisikii…

  • Vitu Vinavyofanya Wengi Washindwe Kufikia Malengo Na Ndoto Zao

    Kwanza ni kuiga watu wengine. Mwandishi wa vitabu John Mason, anasema kwamba imitation is limitatiom, akimaanisha kwamba kuiga ni kikwazo kikubwa sana ambacho kinawazuia watu wengi kuweza kufanyia kazi malengo na ndoto zao na hata kuweza kuzifikia. Ukweli ni kuwa, kama una malengo na ndoto kubwa, kamwe usiige wengine wanafanyaje. Badala yake amua kufanya vitu…

  • Ufanye nini Unapojihisi kama kukata tamaa kwenye kuandika

    Kama unahisi kama kukata tamaa kwenye kuandika kitabu chako, basi kitu kikubwa sana ambacho unatakiwa kufanya ni kuhakikisha kwamba unakaa chini na kujiuliza kwa nini ulianza kuandika kitabu hiki? Ni manufaa gani ambayo watu watapata kutokana na kusoma kitabu chako? Ni hasara gani ambazo watu watapata kwa kusoma kitabu chako? Je, unakubali kweli kwamba usiache…

  • Vitu vidogo ambavyo watu wanapuuza, ila vinawanyima mafanikio makubwa

    Rafiki yangu wa ukweli, salaam. Hongera sana kwa siku hii nyingine ya kipekee sana. Leo ikiwa ni tarehe 30/7/2024, ni siku nyingine ambayo unapaswa kwenda kupambana. Siku ya leo, nimeona nikwambie vitu vidogo ambavyo watu wanapuuza, ila mwisho wa siku vinakuwa na madhara makubwa.Ndiyo, ni vitu vidogo, lakini ukivipuuza, madhara yake yanakuwa ni makubwa sana.…

  • Njia Rahisi Ya kuandika Kitabu Hata Kama Uko Bize

    Habari rafiki yangu, Watu wengi wana malengo ya kuandika vitabu lakini hukosa muda wa kuandika kutokana na majukumu mengi yanayowabana. Mara nyingi wanapanga kuandika jioni baada ya kazi, lakini wanajikuta wamechoka na hawawezi kuandika tena. Je, kuna njia rahisi ya kuandika hata kama uko bize? Ukweli ni kuwa njia hiyo ipo. Amka asubuhi na mapema,…

  • Kanuni Ya Imani Ya PESA

    Ni kutafufa PESA ili ifike hatua hata kama watu hawakuheshimu basi waheshimu PESA zako. PESA ni kitu ambacho unapaswa kukipambania kila kukicha, asubuhi mchana na jioni. Zipende PESA kwa sababu bila ya kuzipenda hazitakupenda. Maana fedha Ina tabia ya kwenda kwa watu wanaoipenda. Kwa hiyo kuanzia leo, ipende fedha nayo itakupenda.

  • Hiki Kitu Ambacho Kinaua Ndoto Zako Kwa Ukubwa

    Nitaifanya kesho anajua ndoto za watu wengi. Ukweli ni kuwa huwezi kuendelea kusema kwamba nitaifanya kesho badala ya kuchukua hatua na kufanya kitu Leo.  Muda mzuri wa kufanya jambo lako na kulifanikisha ni Leo. Chukua hatua Sasa.  Utajishukuru kesho kuwa Leo uliweza kuchukua hatua kuliko ambavyo utajilaumu. Uwe na siku njema Godius Rweyongeza  0755848391 Morogoro;…

  • Kitu Muhimu Ambacho Kila mwandishi anapaswa kuwa anafanya

    moja ya kazi muhimu sana ambayo kama mwandishi unapaswa kuhakikisha kwamba umeifanya ni kuandika. hauwi mwandishi kwa kujiita tu mwandishi, bali unakuwa mwandishi kwa kuandika. Mwandishi anaandika. Hivyo wito wangu mkubwa kwako wewe mwandishi ni kwamba ukae chini na uandike kitabu chako au makala ambayo unafikiria kuandika bila ya kurudi nyuma. Naomba unisikilize vizuri.Kwa kawaidaDaktari…

  • Unahitaji kuwa mtu wa pekee ili kuandika kitabu?

    Watu wengi huwa wakifikiria kuhusu kuandika kitabu, basi kitu cha kwanza ambacho huwa kinakuja kwenye akili yao ni kwamba unapaswa kuwa mtu wa pekee kabisa. Nakubaliana na watu hawa kwamba ili kuandika kitabu chako unapaswa kuwa wa pekee. Na upekee mkubwa ambao unauhitaji wewe ili kuandika kitabu chako na kukikamilisha ni NIDHAMU YA KUKAA CHINI…

X