Home


  • TUKUZE AKAUNTI AISEE

    !

    Siyo za insta wala facebuku!

    Ila za benki kuu,

    Na siyo kwa kuongeza wafuasi,

    Bali kwa kipato hata cha buku,

    Kitokanacho na kazi ya mikono yetu,

    Tuifanyayo mchana hata usiku,

    Tukuze kipato chetu.

    Kipato ni chanzo uhuru,

    Uhuru wa maisha mazuri,

    Na siyo  wa kujionesha bila senti,

    Kipato kitakusaidia mpaka wajukuu 

    Wao watafurahi hata kama siyo sikukuu

    Watafurahi kuwa ulikuwa mpambanaji mkuu

    Aliyewaachia urithi mkuu

    Tupambane!

    Weka moja ya kumi

    Ya kila upatayo makumi

    Iwe januari au  wa kumi

    Weka bila ya kukosa!

    Haiozi!

    Nikukumbushe tu kuwa kitabu cha MAISHA NI FURSA ZITUMIE ZIKUBEBE sasa kinapatikana tena kwa elfu sita (6,000/-)

    Tuma fedha sasa kukipata

    Tuma kwa mpesa 0755848391 au 

    Airtel money: 0684 408 755

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Godius Rweyongeza

    +255755848391

    Morogoro-Tz

  • MAiSHA NI FURSA: ZITUMIE ZIKUBEBE. Zipuuze Zikukikimbie


    Hakuna fursa ambayo huwa inapotea. Usipotumia vizuri fursa inayokuja kwako, kuna mtu ambaye ataitumia. Asiyejulikana.

    Huwezi kuongelea ulimwengu wa kompyuta na mapinduzi ya kompyuta kiujumla bila kumwongelea Gary Kildall. Huyu jamaa ndiye alipaswa kuwa Bill Gates wa nyakati zetu ila akachezea fursa..endelea kusoma ili ujue kilichotokea.

    Mwaka 1977 kampuni ya apple ilitengeneza kompyuta yao ya kwanza iliyojulikan kama APPLE 1. Hapo ndipo vuguvugu la PERSONAL COMPUTERS lilipoanzia. Zilikuwa bado hazijawa za mpakato kama ilivyo sasa hivi, ila kampuni ya APPLE ilikuwa imeleta mapinduzi makubwa.

    Kampuni ya IBM kwa kuona kuwa wanaachwa nyuma, walitengeneza timu ya dharula ya kushughulika na hili na suala. Lengo la hii timu ilikuwa ni kutengeneza PERSONAL COMPUTER haraka iwekezakavyo kabla hawakapoteza fursa ya kuwa sehemu ya mabadiliko.

    Hiyo timu ilianza kazi na mwaka 1980 kazi upande wa HARDWARE ukawa umekamilika. Kilichobaki ulikuwa ni mfumo wa kuiendesha kompyuta (OPERATING SYSTEM) ambayo wataalamu wa IBM hawakuwa na uwezo nayo. 

    Kutokana na uharaka ilibidi wamtafute Bill Gates awasaidie. Walipoenda kwa Bill Gates aliwapokea na kuwaelekeza kuwa kampuni yake haikuwa na mwelekeo wa kutengeneza mfumo huo (operating system) kwa siku za karibuni. Hivyo, aliwaelekeza kwa rafiki yake ambaye alikuwa tayari ametengeneza mfumo huo ambaye sasa ndiye Gary Kildall.

    Gary Kindall alikuwa mmoja wa watu wa kwanza kabisa kuona uwezekano wa kutengeneza kompyuta  binafsi (PERSONAL COMPUTERS), kiasi alishaanzisha kampuni inayotengeneza operating system iliyokuwa inaitwa Digital Research Inc. 

    Hivyo kumbe, Bill Gates alipowaelekeza watu wa IBM kwa huyu jamaa siyo kwamba alikuwa anatania, bali ulikuwa ukweli.

     Gary Kindall alipokea simu kutoka kwa Bill Gates ambaye alimwambia kuwa kuna watu wanakuja, hivyo atapaswa kuongea nao vizuri. Ila hakuambiwa ni watu gani? Garry Kindall akawa amechukulia poa hilo suala na hivyo akapanda ndege yake binafsi kwenda kwenye mishemishe nyingine.

    Watu wa IBM walipofika hawakumkuta Gary Kindall, hivyo walilazimika kuongea na mke wake. Hata hivyo mazungumzo yao hayakwenda vizuri. Kitu kitu kikubwa kinachosemekana kilifanya mazungumzo yao yasiende sawa, maana mke wa Gary alishindwa kuchukua badhi ya maamuzi kutokana na mme wake kutokuwepo.

    Hivyo watu wa IBM waliondoka kwa hasira bila mafanikio yoyote. Ilibidi wamrudie Bill Gates kumwomba msaada. Bill Gates kuona hiyo nafasi imerudi kwake mara ya 2, ikabidi aitumie.

    Alichofanya alinunua kampuni ambayo kiuhalisia siyo kwamba ilikuwa imetengeneza operating system ya kwake, bali ilikuwa imeiga kutoka kwa akina Gary Kindall. Hivyo, alichofanya Bill Gates alichukua SOFTWARE hiyo, na kuwapa IBM. Huo ukawa mwanzo wa Bill Gates kuwa Bill Gates na Gary Kindall kupotea kwenye ramani….

    Umejifunza nini hapa?

    Hakikisha unapata kitabu cha MAISHA NI FURSA: ZITUMIE ZIKUBEBE

    Lipia elfu 6 tu Leo uweze kupata kitabu. Ndiyo elfu sita (6,000). Changamka sasa

    Tuma fedha kwa 

    M-PESA 0755848391 au

    Airtel money: 0684 408 755

     jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Siku njema

    Godius Rweyongeza

    +255755848391

    Morogoro-Tz

    www.songambeleblog.blogspot.com

  • UCHAMBUZI WA KITABU CHA SUGU MAISHA NA MUZIKI. Mambo 14 niliyojifunza kwenye kitabu hiki kinachoeleza Maisha ya Sugu Kutoka Mtaani Mpaka Bungeni

    Mwishoni wa uchambuzi huu, nimeeleza jinsi unavyoweza kupata nakala ya kitabu hiki. Nipo tayari kukuchangia kiasi kidogo ili upate nakala ya kitabu hiki kizuri cha Kitanzania.

    Kwanza, karibu kwenye uchambuzi wa  cha SUGU. kitabu hiki kimeeleza maisha ya msanii Joseph Osmund Mbilinyi, maarufu kama Sugu. Ambaye ni mmoja kati ya wanahiphop wa kwanza hapa Tanzania, aliyeshiriki kikamilifu katika kuanzisha aina hii ya muziki na baadaye kuikuza. Sugu anasema yeye ni miongoni mwa wasanii wa kwanza kwanza kabisa walioanza kuchana kwa lugha ya Kiswahili na pia kuichana serikali bila kificho.

    Anasema kabla yake waliokuwa wanaimba aina hii ya muziki walikuwepo; ila hawakuwa wakichana kwa lugha ya Kiswahili, badala yake  walitumia kiingereza na tena waliiga wasanii wa kizungu waliokuwa maarufu kwa wakati huo. Kuchana kwa Kiswahili   kulimfanya kuwa mtu wa tofauti na hata kupendwa zaidi.

    Leo tunaenda kuona sehemu ya kwanza ya uchambuzi wa kitabu hiki cha SUGU: THE AUTOBIOGRAPHY: MUZIKI NA MAISHA. From The Streets To Parliament.
    Pale ambapo nitatumia lugha ya kishikaji ambayo sijazoea kutumia kwenye blogu hii, nitaomba uivumilie maana mwandishi kaitumia hapa na pale kwenye kitabu. Sasa bila kupoteza muda haya hapa ndiyo mambo 14 niliyojifunza kwenye kitabu

    1. Sugu anasema siyo kwamba amefika hapo kwa bahati au upendeleo kama wengi wanavyofikiri badala yake anasema amesota sana mpaka kufikia hatua ya kuwa SUGU! Ukurasa wa 42 wa kitabu.

    2. Sugu anasema amepitia mengi ikiwa ni pamoja na kufanya uhuni akiwa Mbeya Day, sekondari ambayo alisoma. Kitu kilisababisha mpaka afukuzwe shule na baadaye kuhama shule hiyo. Baadaye akiwa kijana alijaribu kwenda Afrika Kusini kutafuta maisha kitu ambacho hakikufanikiwa na baadaye akiwa tayari amekuwa mwanamziki alienda Ulaya pia kujaribu maisha, ila bado hakuweza kutoboa.

    Kila mara alipoenda nje ya nchi alikuwa akikutana na changamoyo kama kufungwa kwa mipaka au kuumwa (home sick) kitu ambacho kilikuwa kinasababisha arudi nyumbani.

    Kwenye hili nimejifunza kuwa; zile hadithi za kuwa ukienda sehemu fulani utatoboa haraka, zinaweza kuwa zinavutia, ila ukienda eneo husika wanaposema kuna maisha mazuri, ndipo unauona ukweli wenyewe   Kumbe usidanganyike kwa kutaka kukimbilia sehemu fulani, kisa eti unasikia kuna maisha mazuri, kuna uwezekano ukaenda huko na usiyapate hayo maisha mazuri.

    3. Sugu anatuonesha nguvu ya watu waliokuzunguka wanavyoweza kukufanya uinuke au uanguke. Na hili utaliona wazi kwenye maisha yake kuanzia utotoni mpaka ukubwani. Ni marafiki zake wa sekondari waliomfanya awe mhuni.
    Ni rafiki yake ndiye alimfundisha kuandika mistari kwa  Kiswahili badala ya kiingereza.
    Ni rafiki zake pia waliokuwa wakimpa konekisheni na watu muhimu kwa wakati huo
    Na ni rafiki zake au watu waliokuwa wamemzunguka kwa wakati huo waliojenga njama za kumwangusha na hata kupelekea yeye kustaafu muziki bila kutaka.

    4. Kwenye kitabu hiki anaonesha pia jinsi wazazi walivyo na nafasi kubwa kwenye maisha ya watoto wao. Anamkubali sana baba yake kwa mengi aliyoyafanya na hasa kikubwa kutafuta maisha na kuitunza familia yao vizuri.

    Pia kwenye kitabu amemweleza mama yake kama mtu ambaye alikuwa na mchango mkubwa kwenye uimbaji wake. Mama yake ndiye aliyemruhusu aingie kwenye gemu ya mziki. Hii ni kutokana na ukweli kuwa miaka hiyo, muziki ulikuwa unaonekana ni kitu cha hovyo. Wazazi hawakuruhusu watoto wao wawe wanamziki. Ila hali kwa mama yake Sugu ilukuwa tofauti. Alimruhusu.
    Pia mama yake ndiye aliyekuja kuwa mhimili mkubwa sana pale alipotaka kuacha mziki; mwishoni mwa miaka ya 90. Alimpa moyo kwa kusema aendelee.

    5. Sugu anasema alijenga historia ya kuwatoa wasanii wawili kwenye albamu yake ya milenia aliyoitoa mwaka 2000. Wasanii hao ni Afande Sele na Lady Jay Dee

    6. Sugu anaamini kuwa kusafiri kunakufanya ujifunze mambo mengi ambayo huwezi kujifunza kwa kukaa eneo moja. Na yeye anasema kwamba ameweza kujifunza mengi kwa kusaifiri nje ya nchi kukiko hata wasomi wanavyoweza kujifunza darasani.

    7. Sugu anasema kila mti wenye matunda huwa haukosi kupigwa mawe. Kwenye kitabu hiki anaeleza jinsi alivyopitia changamoto kadhaa ikiwa ni pamoja na kutopewa mauzo sahihi ya albamu zake. Kuendeshwa kwa kampeni za wazi za kumwangusha na baadhi ya watu wakiwemo wamiliki wa redio ya Clouds, kitu ambacho anasema yeye alikipinga vikali.

    8. Muda mwingine ni muhimu kuonesha msimamo wako ili kujenga heshima yako na mazingira mazuri ya kikazi.

    9. Usilewe sifa. Ukipata sifa weka kazi zaidi kwenye kile unachofanya. Achana kujisikia kupita kiasi kitu ambacho kinaweza kupelekea upotee kimziki. Yeye anasema ni kitu hikihiki ambacho kimewapoteza wengi kwenye gemu.

    10. Ukipata kazi, basi ifanye kwa bidii. Hiki ni kitu ambacho Sugu anakieleza kwa kina kwenye kitabu hiki na anaonesha wazi kuwa kila kazi ambayo aliwahi kupata alikuwa akiifanya kwa moyo wake wote.
    Aliwahi kuajiriwa kama mlinzi, lakini kwenye kitabu anaonesha kuwa alikuwa akiifanya kazi hii kwa kujituma na kwa moyo wake wote. Aliwahi kuajiriwa Uingereza kama mtu wa kubeba mizigo kwenye kampuni, kazi anayosema ilikuwa ngumu ila aliifanya kwa kujituma japo alikuwa haipendi kivile.

    11. Sugu anaamini kuwa mtu mzuri wa kushirikisha naye ‘kimziki’ ni yule ambaye mna historia kubwa kutoka utotoni na siyo yule ambaye harakati za kikazi zimewafanya mkutane anasema hivyo baada ya vikundi vyote alivyokuwa akijiunga navyo kuishia njiani kwa baadhi ya watu kuacha muziki.  Mfano ni mshikaji wake BBG.

    12. Sugu pia kaonesha kuwa kitu unachopenda sana ndicho huwa kinakuumiza sana. Yeye anasema wazi kuwa  kuna vitu vitatu ambavyo alikuwa anavipenda Sana.
    Familia yake ya nyumbani
    Muziki na
    Mrembo mmoja aliyekuwa anaitwa Prude.
    Ila hivi viwili vya mwisho vilimuumiza mara kwa mara na hasa mwaka 2002 alipostaafu mziki kwa kulazimika kufanya hivyo na wakati huohuo akawa ameachana na mchumba wake.

    13. Sugu anatufundisha pia kutokuwa ving’anganizi wa maamuzi hata kama ni mabovu. Anaonesha hili kwa jinsi alvyoacha muziki na kwenda nje nchi. Ila akiwa huko alishauriwa kurudi kwenye gemu, kitu ambacho alikifanya kwa mara nyingine na aliporudi akawa ameweza kuendeleza harakati zake.

    Kumbe ukifanya maamuzi, na baadaye ikatokea unataka kubadili hayo maamuzi (baada ya kuwa umejua kuwa  kuna maamuzi mengine bora ya hayo). Unaruhusiwa kubadili mtazamo. Siyo dhambi. Ila kwa maoni yangu mchambuzi; Ni dhambi kunga’ngania kitu kile kile hata baada ya kugundua kuwa uamuzi huo haukuwa sahihi.

    14. Sugu anasisitiza juu ya umuhimu wa kuwa na chanzo zaidi ya kimoja cha kukuingizia fedha. Anaeleza jinsi ambavyo muda mwingine alikuwa akihangaika na hasa ilipokuwa inatokea anafuria.

    15. Ni muhimu sana kutafuta fedha na kuwa nazo. Bila ya kuwa na fedha utalazimika muda mwingine kufanya vitu hata kama vinakuumiza au vinaenda kinyume kabisa na misingi uliyojiwekea kimaisha. Mfano mzuri wa hili ni Sugu kukubali kurekodi albamu mojawapo na jamaa ambaye alikuwa akiuza kazi zake bila kumlipa vizuri.

    Alifanya  hivyo baada ya kuwa anahitaji sana fedha za kwenda nje ya nchi ila hakuwa nazo. Hivyo, alilazimishwa kurekodi albamu na jamaa ambaye alikuwa anajua wazi kuwa anamwibia maana hilo ni sharti alilowewekewa. Aliambia kama unataka fedha, niachie albamu ili nikupe fedha.

    Pia sugu kaeleza kisa kingine ambacho kilimfanya akiuke misingi yake, ila alilazimika kufanya hivyo, maana hakuwa na fedha. Ulikuwa uzinduzi wa albamu yake ya nne. Alilazimika kufanya kazi na watu wa Clouds, ambao yeye anasema kuwa hakuwa akiwapenda ila hakuwa na jinsi ambavyo angeweza kuzindua kazi yake bila wao. Hivyo, alilazimika kufanya hivyo, kitu kikichopelekea kulipwa kidogo sana na matarajio yake, na bado akasumbuliwabkwa kutolipwa fedha yake yote mpaka leo (leo hapo inamaanisha wakati anaandika kitabu; pengine sasa hivi watakuwa wameshamlipa)!

    Ok kitabu hiki ni kizuri na kina mengi ya kujifunza ndani yake. Kitabu hiki kina kurasa 147, ambazo ni hakika huwezi kuzizungumzia kiundani kwenye uchambuzi mfupi kama huu. Kama utapenda kukisoma kitabu hiki, Niko tayari kukuchangia kiasi kidogo ili upate nakala yako. Kitabu hiki kinauzwa elfu 20. Binafsi nitakuchangia 5,000/- na wewe utalipia 15,000/- ila gharama za usafiri zitakuwa juu yako. Nitafanya hivyo kwa watu watatu tu.

    Kwa hiyo basi kama utapenda kupata nakala yako kwa bei hiyo, tuwasiliane Sasa 0755848391.

    Umekuwa nami,

    GODIUS RWEYONGEZA

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • Mitandao Mitano Ambayo Vijana wa Kitanzania Wanapenda Kutembelea Sana

     

    Siku ya leo nimeona nikuibie hili. Mtandao wa Alexa huwa una utaatibu wa kupangilia mitandao yote kutokana na wingi wa watembeleaji kutoka kwenye kila nchi.
    Kwa kutumia mtandao huu unaweza kujua nchi ipi, watu wake wanapendelea kutembelea mtando  upi.

    Na leo tunaenda kuona mitandao ambayo Watanzania wanapenda kutembelea sana. Hii ni muhimu kwako kuifahamu kwa sababu inaweza kukusaidia kufanya mengi.
    Moja; inaweza kukusaidia kujua wapi watu wanatumia muda wao kwa wingi, na hivyo kuweza kutumia jukwaa hilo vizuri. Pia, inasaidia kama unataka kufanya Ia matangazo, kujua wapi watu walipo ili utangazie huko.

    Kitu kimoja cha uhakika ni kuwa mitandao ambayo Watanzania wanapenda kutembelea itakushangaza. Ni tofauti na vile ambavyo wewe mwenyewe ulikuwa unategemea. Najua  wengi wanaweza kudhani labda WhatsApp ndio mtandao nambari moja unaopendwa kutembelewa. Ukweli ni kuwa  WhatsApp siyo mtandao nambari moja au mbili. Ifuatavyo sasa ni mitandao mitano ambayo vijana wa kitanzania wanapenda kutembelea:

    1. Google
    2. YouTube
    3. Facebook
    4. Yahoo
    5. Wikipedia

    Mitandao miwili ya ziada ambayo Watanzania wanapenda kutembelea ni
    6. Jamii Forums na
    7. Instagram

    Hiyo ndiyo mitandao inayotembelewa sana hapa Tanzania. Ni muhimu sana kwako kuifahamu kwa sababu Kuna fursa ndani yake. Unaweza kujua muda mwingine ukitaka kufanya kampeni fulani, utumie mtandao gani kufanikisha hiyo kampeni.

    Kwa sababu watu wake wako huku.

    Nimeandika kitabu kinachoitwa MAISHA NI FURSA;  ZITUMIE ZIKUBEBE. Kitabu hiki ninaenda kukizindua rasmi tarehe 1.10.2021.

    Ila habari njema ni kuwa leo hii unaweza kuweka oda ya kupata kitabu hiki. Na kwa atayaweka oda; 

    Kwanza atapata kitabu kwa bei ya punguzo. 

    Pili, nitampa vitabu vingine vya ziada kama zawadi; tena hivyo vitabu vingine vya zawadi nitavituma leo hii baada ya mtu huyo kuweka oda.

    Kuweka oda utalipia, elfu kumi tu (10,000/-) tu. Ila kwa kuwa utalipia elfu kumi leo hii, utpewa  vitabu vingine vitatu wakati ukiendelea kukisubiri kitabu cha maisha ni fursa, ZITUMIE ZIKUBEBE.

    Vitabu utatavyopewa kwa sasa ni 

    1. KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI

    2. SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA

    3. MAAJABU YA KUWEKA AKIBA.

    Rusha elfu kumi leo kwa namba 0755848391. Upate vitabu hivyo vitatu, na kitabu cha MAISHA NI FURSA, ZITUMIE ZIKUBEBE kitatumwa kwako tarehe 1.10.2021 bila wewe kuhitajika kuongeza senti ya ziada.

    Namba ya malipo ni 

    MPESA 0755848391

    Airtel money: 0684 408 755

     Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    NAKUKUMBUSHA TU: Ukituma elfu kumi leo. Taarifa zako zitatunzwa vizuri, na tarehe 1.10.2021 utatumiwa kitabu cha MAISHA NI FURSA; ZITUMIE ZIKUBEBE bila kuongeza senti ya ziada, wala bila kutukumbusha tukutumie.

    .

    Vitabu vyote ni soft copy.

    Ni mimi

    GODIUS RWEYONGEZA

    0755848391

    MOROGORO-TZ

  • ZEGE HALILALI

    Wajenzi wanalifahamu hili. Zege ikichanganywa, kwa vyovyote vile hata iweje, inapaswa kuisha, la sivyo ikilala, asubuhi, hutaikuta kama zege, badala yake itakuwa imekauka.

    Itakuwa siyo zege tena…
    Itakuwa haifai tena kwa ajili ya ujenzi.
    Ndio maana huwa wanaenda kwa kanuni ya zege HALILALI.

    Na wewe unaweza kujiwekea utaratibu kama huu. Kuna vitu katika maisha yako unapaswa kuvifanya kuwa kama zege. Na havipaswi kulala hata kidogo. Vifanye siku hiyohiyo na uvikamilishe.
    Kama kuna majukumu ya kuandika, hata kama ni maneno kidogo, hakikisha unayaandika kila siku bila kulaza kiporo. Maana zege halilali.
    Kama unapaswa kufanya mazoezi yafanye maana zege HALILALI.
    Kama unapaswa kuweka akiba leo, usiseme kwa kuwa kesho nitapokea fedha nyingine ngoja ya leo niitumie nitakuja kuweka akiba ya kesho au kesho kutwa. Kumbuka fedha ya leo inapaswa kuwekewa akiba yake na kesho inapaswa kuwekewa akiba yake pia.

    Kwako fanya vitu kama hivyo kuwa mwiko. Vifanye kuwa kama zege, maana ZEGE HALIPASWI KULALA.

    Ni kitu gani unaenda kukifanya kuwa kama zege leo?
    *******************************************************

    Nimeandika kitabu kinachoitwa MAISHA NI FURSA;  ZITUMIE ZIKUBEBE. Kitabu hiki ninaenda kukizindua rasmi tarehe 1.10.2021.

    Ila habari njema ni kuwa leo hii unaweza kuweka oda ya kupata kitabu hiki. Na kwa atayaweka oda;
    Kwanza atapata kitabu kwa bei ya punguzo.
    Pili, nitampa vitabu vingine vya ziada kama zawadi; tena hivyo vitabu vingine vya zawadi nitavituma leo hii baada ya mtu huyo kuweka oda.

    Kuweka oda utalipia, elfu kumi tu (10,000/-) tu. Ila kwa kuwa utalipia elfu kumi leo hii, utpewa  vitabu vingine vitatu wakati ukiendelea kukisubiri kitabu cha maisha ni fursa, ZITUMIE ZIKUBEBE.
    Vitabu utatavyopewa kwa sasa ni
    1. KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI
    2. SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA
    3. MAAJABU YA KUWEKA AKIBA.

    Rusha elfu kumi leo kwa namba 0755848391. Upate vitabu hivyo vitatu, na kitabu cha MAISHA NI FURSA, ZITUMIE ZIKUBEBE kitatumwa kwako tarehe 1.10.2021 bila wewe kuhitajika kuongeza senti ya ziada.

    Namba ya malipo ni

    MPESA 0755848391
    Airtel money: 0684 408 755
    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    NAKUKUMBUSHA TU: Ukituma elfu kumi leo. Taarifa zako zitatunzwa vizuri, na tarehe 1.10.2021 utatumiwa kitabu cha MAISHA NI FURSA; ZITUMIE ZIKUBEBE bila kuongeza senti ya ziada, wala bila kutukumbusha tukutumie.

    Karibu.
    Godius Rweyongeza
    +255755848391
    Morogoro-Tz

  • Karibu kwenye darasa la mwisho la kuandika kitabu kwa mwaka 2021

    Njoo ujifunze kila kitu unachohitaji kujua kuhusu uandishi wa vitabu

    Kwa mara nyingine tena, napenda kukutangazia kuwa dirisha la kujiunga na darasa la uandishi limefunguliwa. Ila zamu hii litakuwa darasa la mwisho kwa mwaka 2021.

    Kama una mpango wa kuandika kitabu kabla mwaka haujaisha, Basi jiunge na darasa hili.

    Nani anahitajika kwenye darasa?

    Mtu yeyote mwenye nia ya kuandika kitabu na kujifunza mambo yote yanayoendana na uandishi.

    Darasa litaanza lini na litafanyikia wapi?
    Darasa letu huwa linafanyikia WhatsApp na sasa hivi tumeongeza kipengele cha kujifunza kupitia telegram pia.

    Kwa darasa hili ambalo ni la mwisho kwa mwaka huu, tunategemea litaanza kati ya tarehe 15-20 mwezi 10. Wanadarasa tukishatimia tutapanga tarehe rasmi ya kuanza kati ya hizo, ila itakuwa kati ya 15-20 oktoba.

    Wanahitajika watu wangapi darasani?
    Wanahitajika watu watano tu. Darasa likijaa limejaa, kutakuwa hakuna nafasi ya ziada.

    Kuna gharama yoyote ya kuhudhuria darasa hili?
    Ndiyo. Kwa kawaida darasa hili huwa linalipiwa elfu sabini (70,000). Ila zamu hii wahudhuriaji wote wanapewa ofa ya kuhudhuria darasa hili kwa elfu hamsini tu (50,000/-)

    Mfumo tunaoutumia ni wa first come, first served

    Karibu ujihakikishie nafasi kwa kulipia kupitia 0755848391.

  • Fursa Tano Ambazo Vijana Wa Siku Hizi Wanachezea (SEHEMU YA TATU)

    Kama hukusoma sehemu ya pili bonyeza HAPA

    3. Fursa ya kufanya kazi kwa bidii

    Kwani kufanya kazi kwa bidii ni fursa? 

    Na hapa ningependa nikurudishe tena nyuma mpaka miaka ya akina Napoleon Bonaparte. Umewahi kumsikia huyu mtu? Bonaparte alikuwa mbabe wa vita wa nyakati zake na pengine mbabe wa vita wa nyakati zote. Alipigana Sana vita na kushinda kwa kishindo kila mara. Ila moja ya kitu kilichokuwa kinamfanya Bonaparte kuwa wa tofauti, ni juhudi zake katika kazi. Alikuwa na juhudi kazini kuzidi juhudi zenyewe, hahaha.

    Unaambiwa alikuwa anafanya kazi kiasi kwamba hata kama angekuwa bafuni, mtu akaja na nakala ya kusaini, alikuwa anatoka bafuni na sabuni mwilini, kusaini hiyo nakala Kisha anarudi bafuni kuendelea kuoga.

    Siku hizi vijana ni kama tumepotea vile. Unakuta mtu anasafu mtandaoni asubuhi, mchana mpaka jioni, huku akiwa hazalishi chochote. 

    Namkumbuka rafiki yangu aliyekuwa ananiambia eti mimi ninataka kazi ya kuwa naweka saini tu! Loo!

    Hivi ni kweli yupo mtu ambaye kazi yake ni kuweka saini tu? Ebu kwa mfano tuseme yupo. Kama kweli yupo, Basi walau kuna vitu viwili ambavyo nitakuwa na uhakika navyo kuhusu yeye.

    Kwanza ni mchapakazi. Anachapa kazi kwa viwango vya juu sana, kiasi kwamba ameaminiwa na kupewa kazi ya kusaini tu. 

    Maana kazi ya kusaini tu inakuhitaji uwe mfuatiliaji ili kuhakikisha unachosaini kipo sawa. La sivyo unaweza kujikuta unasaini vitu visivyoeleweka ukapoteza kazi yako, cheo na kila kitu na hata kuwaharibia wengine.

    Kazi ni gharama ambayo unapaswa kuilipa na kazi huwa haiangushi mtu.

    Nimeandika kitabu kinachoitwa MAISHA NI FURSA;  ZITUMIE ZIKUBEBE. Kitabu hiki ninaenda kukizindua rasmi tarehe 1.10.2021.

    Ila habari njema ni kuwa leo hii unaweza kuweka oda ya kupata kitabu hiki. Na kwa atayaweka oda;
    Kwanza atapata kitabu kwa bei ya punguzo.
    Pili, nitampa vitabu vingine vya ziada kama zawadi; tena hivyo vitabu vingine vya zawadi nitavituma leo hii baada ya mtu huyo kuweka oda.

    Kuweka oda utalipia, elfu kumi tu (10,000/-) tu. Ila kwa kuwa utalipia elfu kumi leo hii, utpewa  vitabu vingine vitatu wakati ukiendelea kukisubiri kitabu cha maisha ni fursa, ZITUMIE ZIKUBEBE.
    Vitabu utatavyopewa kwa sasa ni
    1. KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI
    2. SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA
    3. MAAJABU YA KUWEKA AKIBA.

    Rusha elfu kumi leo kwa namba 0755848391. Upate vitabu hivyo vitatu, na kitabu cha MAISHA NI FURSA, ZITUMIE ZIKUBEBE kitatumwa kwako tarehe 1.10.2021 bila wewe kuhitajika kuongeza senti ya ziada.

    Namba ya malipo ni

    MPESA 0755848391
    Airtel money: 0684 408 755
    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    NAKUKUMBUSHA TU: Ukituma elfu kumi leo. Taarifa zako zitatunzwa vizuri, na tarehe 1.10.2021 utatumiwa kitabu cha MAISHA NI FURSA; ZITUMIE ZIKUBEBE bila kuongeza senti ya ziada, wala bila kutukumbusha tukutumie.

    Karibu.

    Vitabu vyote ni soft copy.

    Ni mimi
    GODIUS RWEYONGEZA
    +255755848391
    MOROGORO-TZ

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • KITABU CHA SUGU: From The Streets To Parliament; MUZIKI NA MAISHA

    Leo wakati natembea hapa mtaani, nimekutana na mtu anauza vitabu kikiwemo hiki cha wasifu wa SUGU.

    Nilivyoambiwa bei ya kitabu tu, sikuchelewa kutoa fedha mfukoni kukichukua!
    Kinaeleza maisha yake kutoka mtaani mpaka kufika bungeni.

    Ndio naanza kukisoma hivyo maswali yako yote yatunze. Utaniuliza nikimaliza kukisoma.

    Kwa wale mnaopenda vitabu vyenye picha, hiki kinaweza kukufaa pia. Kina picha za hapa na pale kuanzia utotoni, harakati za mziki na hatimaye akiwa hungeni.

    Nimefanya uchambuzi wa kitabu hiki hapa. Naomba ubonyeze hapa ili uweze kujifunza yaliyomo kwenye hiki kitabu

    Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro-Tz

    Hakikisha Umesubscribe kwenye Channel yangu ya youtube kwa KUBONYEZA HAPA

    Jiunge na mfumo wa kupokea makala maalumu kwa njia ya barua pepe kwa KUBONYEZA HAPA

    Jipatie nakala za vitabu vyangu vya kiswahili kwa KUBONYEZA HAPA

    Kama ungependa kujifunza kuhusu uandishi kutoka kwangu wasiliana nami kwa 0755848391

    kila la kheri

  • Fursa Tano Ambazo Vijana Wa Siku Hizi Wanachezea (SEHEMU YA PILI)

     

    Leo tutaendelea na sehemu ya pili. Kama hukusoma sehemu ya kwanza; BONYEZA HAPA kwanza.

    2. Fursa ya kujifunza
    Acha nikurudishe nyuma tena, mpaka miaka ya akina Benjamin Franklin. Miaka hiyo walikuwa wanafanya apprenticeship kwa miaka 7-9. Huo ni muda ambao mtoto au kijana alikuwa ananolewa chini ya mtaalamu bila malipo. Kama kijana alifuatilia vizuri masomo yake basi ilikuwa inategemewa kuwa baada ya muda huo kijana atakuwa amenolewa na kunoleka. Na baada ya miaka hiyo 7,8 au 9 alikuwa anaweza kufanya kitu alichokuwa anaandaliwa kukifanya. Akina Darwin, wote walipitia kwenye kipindi hiki cha kujifunza kwa vitendo.

    Na hiki ndicho kimekuja kuzalisha ile dhana ya saa elfu kumi kwenye ulimwengu wa hamasa.
    Unaifahamu dhana ya saa elfu 10? Dhana hii imepewa unaarufu sana na mwandishi Malcon Gladwell. Kwenye kitabu chake cha Outliers, mwandishi kaainisha kuwa inachukua saa elfu kumi kwa mtu kuwa mbobevu kwenye jambo fulani.

    Yaani, kuwa hizi ni saa elfu kumi mbapo mtu anaweka akili yake, nguvu zake na kila rasilimali aliyonayo katika kufanyia kazi kipaji, ujuzi au kitu fulani. Na baada ya huo muda kama kweli mtu huyo atakuwa amejitoa na kujifunza kwa kina basi atakuwa ameweza kufanikiwa kufikia utaalam au ubobevu.
    Mwandishi anatolea mfano wa Bendi maarufu ya The Beatles. Hii ilikuwa bendi maarufu sana miaka ya 60 huko Marekani. Ilifanya maonyesho kwa weredi mkubwa na iliuza albamu nyingi kwa enzi zake. Mpaka leo hii inaaminiwa kuwa ni bendi bora kuwahi kutokea. Kama huamini kamuulize Google.

    Sijui kwa hapa Tanzania bendi maarufu miaka hiyo ilikuwa ipi. Ngoja kwanza nimpigie baba yangu, bila shaka ataniambia. Si unajua mimi kijana wa kisasa najua tu mambo ya akina Diamond, Alikiba na Harmonize? Hahaha

    Achana na hayo tuendelee bwana, Japo dhana ya saa elfu kumi imekuja siku za hivi karibuni, ila ilikuwepo tokea enzi hizo. Ndiyo maana enzi za akina Benjamin Franklin vijana walisota hiyo miaka 7-9. Kipindi ambacho sasa hivi kinaaminika kuwa kinaendana na hizo saa elfu kumi.

    Hata Benjamin Franklin alisota miaka 9 chini ya kaka yake akijifunza uchapaji wa vitabu tu. Ila walikuwa wanazingua kweli, au wewe unasemaje. Eti jamaa miaka 9 alikuwa anajifunza kuchapa vitabu tu! Loo!

    Ila kwa miaka hiyo ilikuwa lazima. Maana upatikanaji wa taarifa ulikuwa adimu sana. Siku hizi vijana tuna raha zetu asikwambie mtu. Kitu chochote kile unachotaka, unaingia Google tu na kukipata ndani ya sekunde chache. Halafu ninavyokujua wewe ukimaliza hapa utaenda kumtafuta Benjamin Franklin Google ili uone ninayosema ni sahihi au namsingizia. Kama nakuona vile.

    Wanasema kwamba taarifa zinazopatikana sasa hivi ni nyingi sana kiasi kwamba hata mfalme wa karne ya 15 hakuwa na uwezo wa kuzipata. Kabisa.

    Sisi tunayo hazina kubwa. Tuna mitandao ya kufundisha kwa video Kama YouTube.
    Tuna mitandao ya kufundisha kwa njia ya sauti tu.
    Tuna vitabu, ambavyo aidha vinapatikana kwa bei rahisi sana au bure kabisa. Wakati babu zetu hawakuwa na uwezo wa kupata hivi vitu vyote, kitu kilichowafanya waendelee kubaki nyuma. Ila sisi tunavyo vyote tena kiganjani.

    Leo hii ukiamua kujifunza kilimo cha kitunguu ni rahisi sana ukilinganisha na babu yako miaka 60. Halafu wewe hii fursa unaichukulia poa.

    Sisi hivi vitu tunavichukulia poa kwa maana tunaona vipo tu, ila kama nilivyokwambia jana, kama babu yako angekuwa anafufuka leo hii. Angeweza kukuchapa viboko maana unachezea fursa ya kujifunza.

    Leo hii kuna watu wanasema kuwa ile dhana ya saa elfu kumi unaweza kuipunguza kutokana na wingi wa maarifa. Unaweza kujifunza kwa kina kitu fulani tena kwa gharama nzuri na kupunguza hizo saa.
    Kitakachokufanya upunguze hizo saa ni

    Moja, kujifunza kutoka kwenye makosa ya watu wengine. Wewe huhitaji kurudia makosa ambayo yamefanywa na wengine badala yake unajifunza  na kuyaepuka hayo.
    Pili, kujifunza Kutoka kwa mambo ambayo watu wengine wamefanya vizuri ili uyafanye vizuri zaidi. Ni ujinga kurudia makosa ambayo yamefanywa na watu karne ya 19 wakati wameshayaandika na unaweza kuyasoma.

    Labda unajiuliza nijifunze nini?
    Nimeshasema, ila nasisitiza tena.
    Soma vitabu,
    Jifunze kupitia mtandaoni (huko Kuna blogu na tovuti zenye mambo mengi ya kukufaa).
    Hudhuria semina.

    Kwa leo napenda kuhitimisha na nukuu kutoka Alvin Toffler. Kwenye kitabu chake cha The Future Shock anasema, mjinga wa karne ya 21 siyo yule ambaye hajui kusoma, bali anayejua kusoma ila hasomi.

    Kijana kama unajua kusoma ila husomi basi wewe ni….(mimi naishia hapo, usije ukanipiga mawe bure)
        

    Nimeandika kitabu kinachoitwa MAISHA NI FURSA;  ZITUMIE ZIKUBEBE. Kitabu hiki ninaenda kukizindua rasmi tarehe 1.10.2021.

    Ila habari njema ni kuwa leo hii unaweza kuweka oda ya kupata kitabu hiki. Na kwa atayaweka oda;
    Kwanza atapata kitabu kwa bei ya punguzo.
    Pili, nitampa vitabu vingine vya ziada kama zawadi; tena hivyo vitabu vingine vya zawadi nitavituma leo hii baada ya mtu huyo kuweka oda.

    Kuweka oda utalipia, elfu kumi tu (10,000/-) tu. Ila kwa kuwa utalipia elfu kumi leo hii, utpewa  vitabu vingine vitatu wakati ukiendelea kukisubiri kitabu cha maisha ni fursa, ZITUMIE ZIKUBEBE.
    Vitabu utatavyopewa kwa sasa ni
    1. KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI
    2. SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA
    3. MAAJABU YA KUWEKA AKIBA.

    Rusha elfu kumi leo kwa namba 0755848391. Upate vitabu hivyo vitatu, na kitabu cha MAISHA NI FURSA, ZITUMIE ZIKUBEBE kitatumwa kwako tarehe 1.10.2021 bila wewe kuhitajika kuongeza senti ya ziada.

    Namba ya malipo ni

    MPESA 0755848391
    Airtel money: 0684 408 755
    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    NAKUKUMBUSHA TU: Ukituma elfu kumi leo. Taarifa zako zitatunzwa vizuri, na tarehe 1.10.2021 utatumiwa kitabu cha MAISHA NI FURSA; ZITUMIE ZIKUBEBE bila kuongeza senti ya ziada, wala bila kutukumbusha tukutumie.

    Karibu.

    Vitabu vyote ni soft copy.

    Ni mimi
    GODIUS RWEYONGEZA
    +255755848391
    MOROGORO-TZ

  • Fursa Tano Ambazo Vijana Wa Siku Hizi Wanachezea

    Ngoja kwanza, kwani fursa ni nini? Unafanyaje ili kujua kuwa kitu fulani ni fursa na kingine siyo fursa. Kwani fursa huwa zinavaa vazi gani haswa?

    Enewei, tuachane kwanza na maswali hayo japo nitayajibu mwishoni mwa makala haya, ila kwa sasa acha kwanza tuone fursa tano ambazo vijana wanachezea.  Hizi fursa, japo zinachezewa sasa hivi, hazikuwahi kuwepo miaka nyuma, ila zimejitokeza kwenye zama hizi na bado zinachezewa. Mababu zako wangekuwa wanafufuka na kuona jinsi unavyochezea fursa hizi, wangeweza hata kukupiga viboko! Hahaha, natania tu!

    Kwa kila fursa nitakueleza jinsi hali ilivyokuwa zamani, na jinsi hali ilivyo sasa hivi na mwisho kabisa, nitakueleza nini unaweza kufanya ili kuitumia fursa husika. Ngoja sasa tuanze.

    1. Fursa ya kunoa kipaji chako na kukitangaza kwa  gharama nafuu au bure kabisa

    Ngoja turudi nyuma mpaka karne ya 15,16,17, 18…mpaka karne ya 20. Hapa tunakutana na wanasayansi maarufu wa nyakati hizo, akina Isaac Newton, akina Michael Faraday, akina Einstein na wengineo. Pia tunakutana na wagunduzi wa nyakati hizo; akina Henry Ford, Thomas Edison na wengineo. Bila kusahau waandishi,wachoraji na wasanii wote wa zama hizo. Hao niliowataja hapo walikuwa maarufu au walau walifanya kazi zilizogusa jamii ya kipindi hicho, na nyingine bado zina msaada mkubwa mpaka leo hii. Kazi za watu kama Picasso, Leonard Da Vinci, Shakespeare na wengineo.

    Wakati hawa wanakuwa maarufu kwa gunduzi zao, maandishi ya ubunifu wao miaka hiyo, kuna wengine wengi walishindwa kutoboa kwa sababu ya kukosa namna ya kuwafikia watu sahihi ambao wangeweza kuwapa msaada wa kifedha kuwawezesha kunoa na kuinua vipaji vyao. Wengine walikosa nafasi kwenye majukwaa ili kuonesha kazi zao. Miaka hiyo kulikuwa na majarida na baadhi ya majarida, usingeweza kutoa chapisho lako kama wewe hukuwa mtu wa viwango fulani. Au kama hukuwa na konekisheni na mtu fulani.

    Mfano mzuri ni Michael Faraday, huyu alizaliwa kwenye familia ya kimasikini, kipindi hicho Uingereza ilikuwa imewatenga watu kwenye kundi la wenye nacho (royal class) na wasiokuwa nacho (servant class). Na Faraday alikuwa kwenye kundi la pili. Kumbe hakuwa na ruksa ya kuchapa kwenye jarida kutokana na kundi alilokuwemo. Stori yake nitaieleza siku nyingine, ila fahamu kuwa  jinsi alivyoweza kufikia viwango hivyo vikubwa mpaka kuwa mwanasansi mkubwa wa nyakati hizo, ilikuwa ni baraka kubwa sana kwake. 

    Kuna watu wengi enzi hizo walikuwa na vipaji hata kuwazidi wachoraji na wanasayansi wakubwa wa miaka hiyo. Ila hawakuweza kutoboa kwa sababu hawakuwa na konekisheni au fedha za kutosha. 

    Hiki kitu kwenye zama hizi kimepatiwa ufumbuzi kwa zaidi ya asilimia 80 Kama siyo 100 zote, hahaha. 

    Siku hizi ni rahisi sana kuanza kunoa kipaji chako hata kama huna konekisheni. 

    Kwa mfano ebu tuangalie miaka ya 1960. Kama wewe ungependa kuwa msanii na kutoa kazi yako, kulikuwa na mlolongo mrefu. Studio tu kurekodi wimbo wako ilikuwa mbinde. Na hapo hujaingia kwenye kuutangaza redioni, magazetini na kwenye runinga.

    Ila sasa tuangalie kinyume chake. Siku hizi ni rahisi sana. Kwanza, ukiwa na kipaji cha kuimba tu, utatunga wimbo. Utaenda studio na kurekodi wimbo wako bila shida yotote ile. Baada ya hapo unaweza kuanza kuusambaza kwa ndugu zako, marafiki zako wa karibu na watu wengine unaoweza kuwafikia. Badala ya kuutambulisha wimbo wako redioni, unaweza kuutambulisha wimbo wako mtandaoni na watu wakausikiliza. Wakiupenda watawatumia wengine pia. Na hao wengine watawatumia wengine zaidi. Unaweza kujikuta kipaji chako kinakufanya uwe maarufu ndani ya muda mfupi sana. 

    Lakini je, ni vijana wangapi wanatumia hiyo fursa?

    Ebu kwa mfano ona mambo yalivyokuwa kwa mwandishi. Kabla ya kuandika kitabu, ulipaswa kupata ruhusa kutoka kwa wachapaji wa vitabu iliyokuwa inasema, andika kitbu chako. Hapo ndio ulianza kuandika  kitabu chako, kisha baada ya hapo,  ulikipeleka kwa wachapishaji waliokupa ruhusa kukiandika ili wakisome. Kama wangekipenda, basi ulikuwa unapewa ruhusa ya kukichapa, ila kama hawakukipenda, uandishi wako ulikuwa unaishia hapo.  Kipindi hicho kuna waandishi wengi kweli walishindwa kutoboa. Pengine hata babu yako alishindwa kuandika kitabu kwa sababu hiyo. Hahaha, hapo nimechomekea tu.

    Ila sasa hivi mambo yamebadilika. Unaweza kuandika, kuchapa na kuuza kitabu chako ukiwa chumbani kwako. Unapata wazo na kuanza kuliandikia na baadaye unachapa na kuuza kitabu chako kwa njia ya mtandao. Unatengeneza fedha. 

    Siyo hivyo tu, nadhani siku za nyuma utakuwa ulisikia sana watu wanazungumzia bifu za wasanii na wamiliki wa vyombo habari na wasanii kutonufaika na kazi zao. Kama vyombo vya habari havikupenda kazi yako, basi 

     kiufupi hapo ulikuwa huwezi kusambaza kazi yako. Ila leo hii tunaye YouTube, habagui kazi za watu, wala hapendelei watu.

    Tunayo majukwaa mengi ya kuonesha kazi zetu kama mtandao wa Amazon ambapo unaweza kuuza vitabu na bidhaa zako nyingine. Mtandao huu wenyewe haubagui bidhaa yako. Wewe kama unayo bidhaa yako unaweza kuuza, na ukiweza kutengeneza bidhaa nzuri, soko litakukubali na kuipokea kwa mikono miwili. Kitu hiki babu yako asingeweza kukifanya miaka ya 1920. 

    Kumbe zama zimebadilika. Maisha yamebadilika na mtandao wa intaneti unaleta fursa nyingi kweli kwelikweli. Kazi ni kwako kuzitumia. 

    Kwa leo naishia hapa, ili nikuachie nafasi ya kutafakari ulichojifunza mpaka hapa. Kesho tutaendelea na fursa namba 2 inayochezewa na vijana kwenye zama hizi.

    Ila kuna kitu kimoja nimekumbuka, mwanzoni mwa makala hii, nilianza kwa kukuuliza, kwani fursa ni nini?

    Unafanyaje ili kujua kuwa kitu fulani ni fursa na kingine siyo fursa. Kwani fursa huwa zinavaa vazi gani haswa?

    Kujibu maswali hayo na mengine, nimeandika kitabu kinachoitwa MAISHA NI FURSA;  ZITUMIE ZIKUBEBE. Kitabu hiki ninaenda kukizindua rasmi tarehe 1.10.2021.

    Ila habari njema ni kuwa leo hii unaweza kuweka oda ya kupata kitabu hiki. Na kwa atayaweka oda; 

    Kwanza atapata kitabu kwa bei ya punguzo. 

    Pili, nitampa vitabu vingine vya ziada kama zawadi; tena hivyo vitabu vingine vya zawadi nitavituma leo hii baada ya mtu huyo kuweka oda.

    Kuweka oda utalipia, elfu kumi tu (10,000/-) tu. Ila kwa kuwa utalipia elfu kumi leo hii, utpewa  vitabu vingine vitatu wakati ukiendelea kukisubiri kitabu cha maisha ni fursa, ZITUMIE ZIKUBEBE.

    Vitabu utatavyopewa kwa sasa ni 

    1. KUTOKA SIFURI MPAKA KILELENI

    2. SEKTA 11 ZA KUTENGENEZA MAMILIONI YA FEDHA TANZANIA

    3. MAAJABU YA KUWEKA AKIBA.

    Rusha elfu kumi leo kwa namba 0755848391. Upate vitabu hivyo vitatu, na kitabu cha MAISHA NI FURSA, ZITUMIE ZIKUBEBE kitatumwa kwako tarehe 1.10.2021 bila wewe kuhitajika kuongeza senti ya ziada.

    Namba ya malipo ni 

    MPESA 0755848391

    Airtel money: 0684 408 755

     Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    NAKUKUMBUSHA TU: Ukituma elfu kumi leo. Taarifa zako zitatunzwa vizuri, na tarehe 1.10.2021 utatumiwa kitabu cha MAISHA NI FURSA; ZITUMIE ZIKUBEBE bila kuongeza senti ya ziada, wala bila kutukumbusha tukutumie.

    Endelea na SEHEMU YA PILI KWA KUBONYEZA HAPA

    Karibu.

    Vitabu vyote ni soft copy.

    Ni mimi

    GODIUS RWEYONGEZA

    0755848391

    MOROGORO-TZ

X