Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Aina Tano (05) ya watu ambao kila mfanyabiashara anapaswa kujenga nao urafiki wa karibu

    Rafiki yangu wa ukweli salaam. Hongera sana kwa siku hii nyingine ya leo. Leo nataka kukwambia aina tano ya watu ambao kama mfanyabishara unapaswa kuanza kujenga nao urafiki mapema.

    Unapaswa kuanza kujenga urafiki wa namna hii mapema sana bila kujali biashara yako ni ndogo au kubwa.

    #1. ni wanasheria.

    Hawa ni watu muhimu sana kwenye ulimwengu wa biashara. wanaweza kukushauri mambo mengi, kuanzia kwenye mikataba (ukweli ni kwamba kama mfanyabiashara kuna mikataba mingi ambayo utaingia, na wafanyakazi, na washirika, wasambazaji n.k), mpaka kwenye maamuzi fulani ya kisheria ambayo utatakiw akufanya kwenye safari yako ya biashara.

    watakushauri mengi kuanzia kwenye mikataba ya wafanyakazi na hata namna bora ya kuondoa wafanyakazi bila mkono wa sheria kukupitia. Na mengine mengi.

    hivyo, moja ya kipaumbele chako kiwe ni kujernga uhusiano wa karibu na wanasheria. Kama kwenye mzunguko wako hauna mwanasheria, basi ni muda muafaka wa kufanya hivyo.

     

    #2. Washauri wa kodi

    hawa ni watu muhimu sana. Wanajua mengi kuhusu kulipa kodi ambayo hujui, wanajua namna ya kukusaidia kulipa kodi sahihi kwa wakati sahihi. Ukiw ana hawa watu watakusaidia sana kulipa kodi inayoendana na kile unachotakiwa kulipa

     

    #3. Wahabibu

    Hawa ni watu wengine muhimu sana ambao unapaswa kujenga nao ukaribu. Hawa watakusaidia sana kwenye kutunza hesabu za biashara yako vizuri.

     

    #3. Watu wa masoko

    Ni wazi kuwa biashara yako itakuwa na kitengo cha masoko. Hivyo, unahitaji pia kuhakikisha kwamba unakuwa na watu wa namna hii. Watu hawa wa masoko watakusaidia kwenye kutangaza bidhaa zako unazouza na kulifikia soko lako vizuri.

     

    #4. graphic designers

    Hawa watakusaidia kudizaini kazi zako na hasa katika mfumo wa video na picha. Kummbuka picha moja inaongea maneno milioni.

     

    #5. kocha

    Unahitaji kuwa na kocha ambaye atakushikiria hasa kwenye kufuatilia malengo na ndoto zako ili uweze kuzifanyia kazi kama ulivyoziweka. Bila ya kuwa na mtu wa namna hii, utajikuta kwamba unaweka malengo ila huyafanyii kazi. Au unaanza kuyafanyia kazi ila hayatimii.

     

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Epuka Makosa Haya Matano (05) Kwenye Biashara Yako

    Rafiki yangu mfanyabiashara, Leo nataka nikuainishie MAKOSA matano ambayo wafanyabiashara Wengi hufanya. Tafadhali hakikisha kwamba unayaeouka Haya MAKOSA Kwa manufaa ya biashara Yako ya Sasa na baadaye

    Kosa la kwanza: kutioipa biashara Yako jina.

    Labda nianze Kwa kukuuliza jina biashara Yako ni lipi? Kama biashara Yako Haina jina unakosea sana.
    Mtoto akizaliwa anapewa jina
    Wewe pia una jina.
    Mpaka mbwa na paka Wana majina.
    Sasa wewe unashindwaje kuipa jina biashara Yako.

    Ni Muhimu biashara kuwa na jina, maana kikawaida biashara Huwa inachukuliiwa kama kiumbe hai. Na hii itakusaidia wewe kujitofautisha wewe na biashara Yako.

    Hivyo, kazi Yako kubwa ya Leo ni kuhakikisha biashara Yako Ina jina

    Kama ungependa kupata mwongozo Kamili wa kupata jina zuri la biashara, basi, pata nakala ya kitabu Cha MAMBO 55 YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZISHA BIASHARA. Kitabu kina mwongozo Kamili, wa kupata jina zuri Kwa ajili ya biashara Yako, unaweza kupata mwongozo huu Kwa kuwasiliana na +255 684 408 755. Kitabu softcopy ni 10,000/- na hardcopy ni 15,000/- (usafiri ni juu Yako mwenyewe).

    Kuna mambo 55 ya kuzingatia kabla ya kuanzisha biashara, mambo haya yote yameelezwa kwenye hiki kitabu. Kupata nakala yako, wasiliana na +255 684 408 755
    Hakikisha unajipatia nakala ya kitabu hiki. Tumia namba ya simu +255 684 408 755

    Kosa la pili ni kutoipa kipaumbele biashara yako.

    Biashara yako unapaswa kuipa kipaumbele kikubwa sana kuliko kitu kingine chochote. Kama huipi biashara yako kipaumbele unaiua mwenyewe.

    Kama umeajiriwa, hakikisha unakuwa na ratiba yako umeigawa mara mbili. Muda wa kazi za mwajiri na muda wa biasahra yako. Usifanye hilo kosa ambalo wengine huwa wanafanya.

    SOMA ZAIDI: Kitu Muhimu Unachopaswa Kufahamu Kabla ya Kuvuna Mafanikio yoyote

    Kosa la tatu: usikubali ujinga kwenye biashara Yako

    Ndiyo usikubali ujinga wowote aidha Kutoka Kwa watu unaofanya nao kazi, washirika, au hata wateja. Kuwepo na misingi ambayo inasimamiwa kwenye biashara yako. Kwenye ubora, kwenye huduma, kwenye viwango ambavyo wafanyakazi wanapaswa kufikia na kamwe usikubali ujinga.

    Kosa la nne: usikubali huduma mbovu zitolewe Kwa wateja.
    Kwa mteja wako yeyote ambaye anapata huduma kwenye biashara Yako, usikubali apate huduma mbovu. Kama Sasa hivi huduma hazijakaa vizuri Anza kurekebisha Hilo. Ili uwe na huduma ambazo ni bora, huduma za viwango vya juu.

    Kosa la tano: usikubali kuwa na siku ambayo hujaipangilia.

    Kama mfanyabiashara kosa kubwa unaloweza kufanya ni kutokuwa na ratiba. Hakikisha unakuwa na ratiba ambayo utakifanyia kazi ndani ya siku Yako. Usifanye kitu chochote ambacho hakipo kwenye ratiba yako.

    SOMA ZAIDI: Uchambuzi wa Kitabu: The Leader Who Had no Title (Kiongozi Asiye na Cheo); Mambo 200 Niliyojifunza katika kitabu hiki.

    Kosa la sita: Usikubali kuendesha biashara Yako bila kutunza kumbukumbu.

    Kumbukumbu za PESA. Kumbukumbu za Kila mteja ambaye amenunua. Kumbukumbu zote ziwekwe sawa, maana kesho na keshokutwa hizi kumbukumbu zitakuwa na maana Kwa biashara Yako.

  • Huu Ndiyo Muda Mzuri wa Kusema Kwamba Umefanya Mauzo Kwenye Biasshara yako

    Kuna mambo 55 ya kuzingatia kabla ya kuanzisha biashara, mambo haya yote yameelezwa kwenye hiki kitabu. Kupata nakala yako, wasiliana na +255 684 408 755
    Hakikisha unajipatia nakala ya kitabu hiki. Tumia namba ya simu +255 684 408 755

    Rafiki yangu wa ukweli, salaam. Hongera sana kwa siku hii njema ya leo.

    Kwenye biashara kuna kitu kimoja tu ambacho watu huwa wanakosea. Na kitu hiki huwa ni kuhesabu vifaranga kabla havijatotolewa. Yaani, kuhesabu kwamba wameuza wakati bado kabisa hawajauza.

    Unakuta mtu anahesabu kwamba ameuza pale anapoahidiwa na mteja kwamba atakuja.

    Au anahesabu kwamba ameuza pale mteja anapokuja kwenye biashara yake na kupita, huku akisema kwamba atarudi kununua. 

    Ukweli ni kuwa hivi vitu vyote havikufanyi kuuza.

    Hata kama mteja amechukua mzigo na kuondoka nao, ila kama bado hajakupa hela, fedha, au kama hajaweka fedha hii kwenye akaunti yako. BADO UNAKUWA HUJAUZA.

    Hata kama mteja amekuahidi sana kwamba lazima atakuja tu kulipia. Unahesabu umeuza pale unapokuwa umepokea fedha mfukoni au kwenye akaunti ya biashara.

    Huu ndiyo muda pekee wa wewe kuhesabu umeuza.

    Kabla ya hapo inakuwa bado.

    Sasa leo, nataka ujiulize ni mara ngapi umekuwa ukijidanganya kwamba umeuza kwenye biashara yako wakati hujauza?

    Kazi yako kubwa ya kufanya siku ya leo ni kuhakikisha kwamba unaanza kuhesabu mauzo ambayo umefanya kwa kupokea fedha na siyo kuhesabu mauzo ya kudhania ambayo hujapokea fedha yake.

    Kama bado ulikuwa hujapata nakala ya kitabu hiki cha MAMBO 55 YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZISHA BISHARA hakikisha kwamba umepata nakala yako siku ya leo. Kupata nakala ya kitabu hiki ni rahisi sana. Wasiliana na nami kwa +255 684 408 755 sasa kupata nakala yako.

    Kuna mambo 55 ya kuzingatia kabla ya kuanzisha biashara, mambo haya yote yameelezwa kwenye hiki kitabu. Kupata nakala yako, wasiliana na +255 684 408 755
    Hakikisha unajipatia nakala ya kitabu hiki. Tumia namba ya simu +255 684 408 755

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Aina za mazoezi Unayopaswa kuwa unafanya

    Mazoezi ni sehemu muhimu ya maisha yetu. Kuna aina tatu ya mazoezi ambayo unapaswa kufanya kila siku, unajua ni aina zipi?

    Mazoezi ya mwili. Kama kukimbia, Kwa siku tenga walau musu saa Kwa ajili ya hili

    Mazoezi ya akili. Haya niazoezi unayafanyia Kwa kujifunza, KUSOMA VITABU na kupata mafunzo ya semina n.k

    Mazoezi ya kiroho. Haya unayafanyia Kwa kupata muda wa jahajudi salaam n.k

    Inashautiwa walau kuwa na dakika 20 Kwa ajili ya Kila kimoja Kila siku

    Hizi ni aina za mazoezi ambazo unapaswa kuwa unafanya mara zote.
    Wewe unafanya zipi Kwa Sasa, na Nini mpango wako?

    SOMA ZAIDI: AKILI YA MKULIMA: mambo 12 ya kujifunza kutoka kwa mkulima unayopaswa kuyatumia kwenye maisha yako ya kila siku

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Jinsi Ya Kujilipa Mshahara Kutoka Kwenye Biashara Yako. Njia Mbili Zilizothibitishwa

    Changamoto kubwa ambayo imekuwa inawakumba wafanyabiashara wengi ni kuchanganya pesa zao na pesa za biashara. Makala ya leo, inaenda kuwa mwarobaini wa hili.

    Sikiliza uhusiano mkubwa uliopo kati yako wewe na biashara yako ni kwamba wewe ni mmiliki wa biashara, lakini fedha za biashara haupaswi kujimilikisha na kuzifanya kuwa za kwako. Fedha za biashara ni za biashara. wewe unapaswa kupata pesa kutoka kwenye biashara yako kwa njia mbili tu.

    Njia ya kwanza ni kama mshahara, wewe kama mfanyakazi kwenye biashara yako basi unastahili kupata mshahara. na njia ya pili ya wewe kupata pesa kutoka kwenye biashara yako ni gawio au faida.

    Nje na hapo fedha ya biashara ni ya biashara na fedha ya kwako ni ya kwako.

    lakini si tunaanzisha biashara ili tupate fedha?

    Najua unajiambia hivyo, ndio. ni kweli. ila sikiliza. Biashara yako ni kama kiumbe hai, inahitaji kula, inahitaji kupumua na inahitaji kukua. Endapo haitapata vitu muhimu kwa ajili ya biashara yako kukua, ukweli ni kwamba biashara hii haitakua.

    Hivyo, usiibemende biashara yako kwa kuchukua hela za biashara ya kujimilikisha. Ziache fedha za biashara ziendelee kuwa za biashara

    Tena biashara inapaswa kuwa na akaunti yake benki. Na wewe unapaswa kuwa na akaunti yako pia.

    Hela yako ikae kwenye akaunti, na helaya biashara iwe kwenye akaunti yake. Usizichanganye.

    Hapa najua unajiuliza mbona lakini muda mwingine huwa naongeza hela kwenye biashara, hili nalo limekaaje?

    Ndiyo, kama unaongeza hela kwenye biashara maana yake kuna kitu umeona kwamba kikipata nguvu utakuja kupata faida zaidi hapo baadaye. Kama kwa sasa faida ulikuwa unapata milioni kwa wiki, maana yake unatazamia utapata milioni na nusu. Kitendo cha wewe kuongeza fedha kwenye biashara hakikupi wewe uhuru wowote wa kuifanya hela ya biashara kuwa ya kwako.

    Najua unajiuliza swali jingine, kuwa je, kwa mfano, nikipata shida wakati hela ya biashara ipo nifanyeje?

    Jibu langu ni kwamba, ukipata shida, tumia mshahara wako. Kama mshahara unaupata kutoka kwenye biashara yako haukutoshi, ongeza bidii ili mshahara huo uweze kupanda.

    Ninaposema ongeza bidii maana yake, weka mkazo kwenye mauzo,ili uweze kuuza zaidi na hatimaye uweze kupata mshahara mkubwa zaidi kutoka kwenye biashara yako.

    Sasa swali jingine unalojiuliza, ni je, nijilipe shilingi ngapi kutoka kwenye biashara yangu?

    Jibu lake ni kwamba, kuna aina mbili za malipo ambayo unaweza kupata kutoka kwenye biashara yako.

    Aina ya kwanza ni malipo ya mshahara ambao uko fixed. Yaani, unajiwekea kiwango maalumu cha mshahara ambacho utakuwa unapokea kila wiki au kila mwezi.

    Ni muhimu kuhakikisha kwamba unakuwa na kiwango ambacho kitakuwezesha kukidhi mahitaji yako ya kila siku, ili usije ukajikuta umechukua hela ya biashara katikati ya wiki au mwezi.

    aina ya pili ya kujilipa kwenye biashara, ni kwa kamisheni.

    Hii ni njia nzuri kama utakuwa tayari kupambana na kuweka kazi zaidi. Hii itakupa changamoto ya kuisukuma biashara yako iende viwango vya juu mara zote. kama upo tayari kwa ajili ya hii changamoto, basi hii ndiyo njia bora kwako ambayo itakufaa kujilipa.

    Kwa njia hii ni kwamba, unaweka kiwango cha mshahara wako kuwa asilimia ya mauzo unayokuw aumefanya. mfano unaweza kuweka asilimia tano au kumi. Hii inamaanisha kwamba kwa kila mauzo utakayofanya, utapata asilimia tano tu. Mfano ukifanya mauzo ya milioni moja, unapata kamisheni yako ya ya asilimia tano ambayo ni sawa na shilingi elfu hamsini. Ukijisukuma zaidi, maana yake utapata kamisheni kubwa zaidi na hivyo kuwa na mshahara zaidi.

    najilipaje hiyo hela nachukua tu pale ninapopaswa kuchukua au inakuwaje yani?

    Utaratibu wa kujilipa jilipe kama ambavyo ungekuwa unawalipwa wafanyakazi wengine. Jilipe hela kupitia akaunti ya benki. Toa kwenye akaunti ya benki kwenda akwenye akaunti yako, na matumizi yawe ni mshahara au kamisheni.

    Una swali la ziada kuhusu hii mada ya leo. Kama lipo inawezekana swali lako limejibiwa kwenye kitabu cha MAMBO 55 YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZISHA BIASHARA. Hakikisha umepata kitabu hiki kizuri sana kwa kuwasiliana na +255 684 408 755. Fanya hivyo sasa hivi ili uweze kupata nakala yako,

    Kuna mambo 55 ya kuzingatia kabla ya kuanzisha biashara, mambo haya yote yameelezwa kwenye hiki kitabu. Kupata nakala yako, wasiliana na +255 684 408 755
    Hakikisha unajipatia nakala ya kitabu hiki. Tumia namba ya simu +255 684 408 755

    La sivyo, mimi nakushukuru sana kwa muda wako siku ya leo. HAKIKISHA UMEJIUNGA NA WATU WANAOPOKEA MAKALA MAALUM KUTOKA KWANGU kila siku. Kujiunga, jaza taarifa zako hapa chini

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Kanuni Ya Miezi Sita Kwenye Biashara, Na Kwa Nini Kila MfanyaBiashara Anapaswa Kuifahamu

    Kuna kanuni ya miezi sita kwenye biashara ambayo wafanyabiashara wengi hawaifahamu. Ni kanuni muhimu ambayo kama mfanyabiashara unapaswa kuifahamu. Kutoifahamu kanuni hii kutakuponza sana

    Kanuni hii inasema kwamba, ukianza kufanya biashara, ndani ya miezi sita ya kuanza biashara kuna watu wengine wataanzisha biashara kama hiyo.

    HII kanuni inafahamika kama kanuni ya copy cat.

    ikimaanisha kwamba baada ya miezi sita kuna watu watakuwa wanafnaya biashara kama ya kwako uliyoanza kufanya baada ya miezi sita.

    Kuna watu watazalisha bidhaa kama hizo miezi sita baada ya wewe kuwa umeanza kufanya uzalishaji.

    Kwa hiyo hakuna kitu unachofanya kwenye biashara yako ambacho kipo salama ambacho watu hawatakuja kukifanya.

    sasa ili kujiweka katika mazingira ambayo watu hawataweza kukutoa kwenye biashara unapaswa kuzingatia mambo sita yafuayo

    1. Ni ubunifu. Yaani mara zote kuwa mbunifu kwenye kila kitu unachofanya. kuwa mbunifu kiasi kwamba watu wengine wawe mara zote wanatafuta namna ya kuweza kuendana na kile unachofanya na kile unachobuni.
    2. Jifunze kila mara. kuwa mtu wa kujifunza mara zote, wengi watakuwa wanaiga kwako ila siyo watu wa kujifunza. wewe kuwa mtu kujifunza na hasa kwa kusoma vitabu, majarida yanayoelimisha na kuhududhuria semina na mfunzo muhimu sana.
    3. kuwa na mfumo ambao wengine hawawezi kuufanyia kazi. Inawezekana ni mfumo wa namna ya kuhudumia wateja kwa namna ya kipekee. Au inawezekana ni mfumo wa kuwa na wafanyakazi ambao ni bora kabisa kwenye biasahra yako. Hakikisha unakuwa na kitu ambacho hakuna mtu mwingine mwenye nacho na kifanye kwa ubora wa hali ya juu sana bila ya kuacha hata kidogo.
    4. Kuwa mtu wa kupokea maoni kutoka kwa wateja wako. Kwa kuanzia nashauri, upokee hasa maoni kutoka kwa wateja wako. Hawa ni watu ambao wametumia bidhaa zako na hivyo wakikwambia kitu, ni uhakika kwamba wanakuwa wanamaanisha hicho wanachokisema.
    5. Hata hivyo, ukipokea maoni kutoka kwa wale watu ambao hata hawajatumia bidhaa zako maana yake ni kwamba utakuwa unapokea maoni kutoka kwa watu ambao hawajapata uhondo wa kile ambacho umetengeneza. na inawezekana wasije hata siku moja kununua kutoka kwako.
    6. Amua kufanya kitu ambacho utafahamika nacho kwacho. Ndiyo, najua kuna vitu ambavyo unaweza kufanya, lakini kwa kuanzia fanya kitu ambacho utafahamika nacho kwacho. Kifanye kwa ubora mkubwa sana

    rafiki yangu, hayo ndiyo mambo matano ya msingi sana ambayo unapaswa kufanya, ambayo yatakufanya uwe mbele ya watu wengine mara zote. Badala ya mara zote kuendelea kuwa unaiga kwa wengine. Yatakufanya kuwa mbunifu mara zote na kuja na vitu vya tofauti.

    Kuna mambo 55 ya kuzingatia kabla ya kuanzisha biashara, mambo haya yote yameelezwa kwenye hiki kitabu. Kupata nakala yako, wasiliana na +255 684 408 755
    Hakikisha unajipatia nakala ya kitabu hiki. Tumia namba ya simu +255 684 408 755

    SOMA ZAIDI: Mambo Muhimu Ya Kuzingatia Wakati wa Kuanzisha Biashara

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana na +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Viashiria kumi na sita (16) Kuwa Umebeba Ajira Za Watu

    Rafiki yangu mpendwa salaam, ujue mara kwa mara nimekuwa nakwambia kwamba inawezekana wewe umezaliwa kuajiri na siyo kuajiriwa. Siku ya leo ninaenda kukuonesha viashiria ishirini ambavyo vinaonesha kuwa wewe umebeba ajira za watu.

    Baada ya kuwa umesoma hapa sasa, kazi itabaki kwako kuhakikisha umefanyia kazi haya utakayokuwa umejifunza au la

    1. Kiashiria cha kwanza kwamba umebea ajira za ni ndoto yako kubwa

    Kama una malengo na ndoto kubwa, fahamu wazi kuwa haya malengo na hizi ndoto kubwa unaweza kuzikuza mpaka kufikia hatua ambapo watu watahitajika ili kukusaidia ili kuzifanikisha. Ni ukweli kuwa hakuna ndoto kubwa ambayo unaweza kuifanikisha peke yako. Ndoto kubwa zinahitaji watu pia.  Hivyo, kama una ndoto kubwa hakikisha unazifanyia kazi maana hizi ndizo zitakupelekea wewe kwenye kuajiri wengine.

    2. kiashiria cha pili kuwa umebeba ajira za ni kipaji chako

    Kiashiria cha pili kuwa umebeba ajira ni kipaji chako. Kama una kipaji ni wazi kuwa hiki kipaji, huwezi kukifanyia kazi peke yako. Unahitaji watu kufanyia kazi kipaji chako na kukifanikisha. Hiki ni kiashiria kingine kuwa inawezekana umebeba ajira za watu.

    3. kiashiria cha tatu kuwa umebeba ajira za watu hicho kitu unachopenda kufanya

    Kama kuna kitu unachofanya na unaona kwamba unapenda kukifanya hicho kitu, hiki ni kiashiria kingine tosha kwamba inawezekana wewe umebeba ajira za watu. Kwenye hili unaweza kuwa unajiuliza, kivipi? Ngoja nikuelekeze vizuri ili uweze kunielewa. kama unafanya unachopenda maana yake kinaeanda kuwagusa watu wengi. Itafikia hatu ambapo utakuwa na majukumu mengi ambayo utakuwa unapaswa kuyafanyia kazi. Baadhi ya haya majukumu sasa watahitajika watu wa kuyafanya na kuyatekeleza. Na hapo ndipo utakapoajiri!

    3. kiashiria cha nne kuwa umebebea ajira za ni changamoto ambazo zinaikumba jamii

    Kama kuna changamoto ambazo unaziona kwenye jamii na unaona unaweza kuzitatua, hicho ni kiashiria kwamba umebeba ajira za watu. Unachotakiwa kufanya ni kuchukua hatua na kutatua hizo changamoto unazoona. na hapa siyo tu kwamba unakuwa umebeba ajira za watu, lakini pia unakuwa umebeba suluhisho la matatizo na changamoto kubwa zinazowakumba watu.

    4. Kiashiria cha tano kuwa umebeba ajira za watu ni ushauri ambao watu huwa wanakuja kukuomba

    Kama kuna watu wanakuja kwako kukuomba ushauri kwenye jambo fulani, fahamu wazi kuwa umebeba ajira zao. Unachotakiw kufanya ni kuhakikisha kwamba unaweka vizuri kile unachojua, ili kiweze kuwasaidia watu katika ngazi kubwa na katika viwango vikubwa. Nimeeleza hili kwa undani zaidi kwenye kitabu cha TENGENEZA FEDHA KWA KUUZA KILE UNACHOJUA.

    Unaweza kupata nakala ya hiki kitabu mtandaoni moja kwa moja kupitia HAPA au kwa kuwasiliana nami kwa +255 684 408 755

    SOMA ZAIDI: KITABU: TENGENEZA FEDHA KWA KUUZA KILE UNACHOJUA

    5. Kiashiria cha Tano ni kuwa na Uwezo wa Kujenga Timu:

    Kujenga na kuongoza timu ni sifa muhimu kwa wale wanaotaka kuwaajiri wengine. Watu wenye uwezo wa kufanya kazi na kusimamia wafanyakazi wanaweza kufanikiwa katika kuendesha biashara na kutoa ajira. Hii inamaanisha kwamba kama una uwezo mzuri wa kuwasiliana na kuwasilisha kile ambacho kimoo ndani yako  kwa timu yako, kutoa majukumu yanayoeleweka kwa timu yako, kuwa na namna ya kuifuatilia timu yako na kuifanyia tathmini ili iweze kuzalisha matokeo n.k.

    6. Kiashiria cha Sita ni Kuwa na Ujasiri wa Kuchukua Hatari:

    Kuna hatua nyingi za hatari ambazo utapaswa kuchukua kwenye maisha yako ya kila siku.kama hiili unaona liko sawa kwako, basi huu ni muda wako wa kujiandaa kuja kuajiri siku moja.

    SOMA ZAIDI: Haya Ndio Maneno Yanayotumiwa Na Watu Kujifariji Linapokuja Suala La Pesa

    7. Kiashiria cha saba ni uwezo wa Kusimamia Rasilimali:

    Hili somo wengi linawapiga chenga. Kusimamia rasilimali kama vile fedha, wafanyakazi, na vifaa ni muhimu katika uendeshaji wa biashara. Watu wenye uwezo wa kusimamia rasilimali hizi wanaweza kuwa na uwezo wa kuajiri na kusimamia wafanyakazi.

    8. Kiashiria cha nane ni Kuwa na Mtazamo wa Muda Mrefu:

    Biashara siyo kitu cha kufanya ndani ya siku moja. ni kitu cha muda mrefu, hivyo mtazamo wa muda mrefu ni kitu cha muhimu sana hasa tunapoongea biashara.

    Jinsi Ya Kubadili Mwelekeo Wa Kile Umachofanya Bila Kuathiri Matokeo (True Story)

    9. Kiashiria cha Tisa ni Uwezo wa Kuhamasisha Wengine:

    Hiki ni kipengele kingine muhimu sana hasa unapokuwa unafanya kazi na watu. Kuna wakati ambapo utapaswa kuwa mkali, n akuna wakati ambapo utahitaji kuwahamasisha wengine kazi ifanyike. Kuna wakati watu watatakiwa kufanya kazi kwa muda mrefu zaidi ya ule muda wa kawaida. haya yote utaweza kuyafanikisha kama utakuwa mtu wa kuhamasisha watu na kuwafanya waone maono makubwa ambayo wewe mwenyewe utakuwa unaona.

    10. Kiashiria cha kumi ni kuwa na Uwezo wa Kufanya Maamuzi ya Haraka:

    Katika biashara, mara nyingi kuna haja ya kufanya maamuzi haraka ili kukabiliana na mabadiliko ya haraka katika soko au mazingira ya biashara. Watu wenye uwezo wa kufanya maamuzi ya haraka na kwa ufasaha wanaweza kufanikiwa katika kuajiri na kusimamia wafanyakazi. na ukweli ni kuwa zipo nyakati nyingi ambazo utatakiwa kufanya maamuzi ya haraka. Ni nyingi zipo mbele yako. Kitu kikubwa unachopaswa kuwa tayari kuzikabili.

    SOMA ZAIDI: Mambo Matano Unayopaswa Kufahamu Ili Utengeneze Marafiki Wazuri Na Wa kudumu

    11. Kiashiria cha kumi na moja ni kuwa na Uwezo wa Kujifunza na Kubadilika:

    Biashara mara nyingi inahusisha kujifunza kutokana na makosa na kubadilika kulingana na mabadiliko katika mazingira ya biashara. Watu wenye uwezo wa kujifunza na kubadilika wanaweza kufanikiwa katika kuendesha biashara na kutoa ajira kwa wengine.

    Miaka ya nyuma mtandao wa intaneti ulipoingia mjini ni biashara chache zilikuwa tayari kubadilika na kuukumbatia huu mtandao wa intaneti, leo hii hizi biashara biashara zimeweza kukua sana. Kwa upande mwingine kuna biashar aambazo zilipuuza hii mitandao, nyingine zimetoweka kwenye biashara na nyingine sasa hivi ndio zinajikongoja kuingia kwenye hii mitandao. Ukweli ni kuwa kama mfanyabiashara unapaswa kuwa tayari kujifunza kila maa bila ya kuacha.

    Wakati mwingine kujifunza kitu kimoja tu mfano kwenye kitabu unaweza kuwa ni uamuzi wenye busara sana. Hivyo, ni muhimu sana kwako kuhakikisha kwamba unajifunza na unabadilika pale inapohitajika.

    Kutana na Mwajiriwa Ambaye Haitaji Mshahara Ila Anafanya Kazi Kwa Bidii. Nakushauri Baada Ya Kusoma Makala Hii Umwajiri Huyu Jamaa. Kitu Kimoja Cha Ziada Ni Kwamba anafanya Kazi saa 24/7

    12. Kiashiria cha kumi na mbili kuwa na Uwezo wa Kufanya Kazi Kwa Timu:

    Wakati shuleni wengi tunafundishwa kufanya kila kitu peke yako. Kwenye biashara hali ni tofauti, uwezo wa kufanya kazi kwa timu na kushirikiana na wengine ni muhimu katika biashara. Kama una uwezo wa kufanya kazi kwa ushirikiano na kusaidiana na wenzao wanaweza kuwa na uwezo wa kufanikiwa katika kuajiri na kusimamia timu yako.

    ACTIVE MODE ACTIVATED

    12. Kiashiria cha kumi na mbili ni uwezo wa Kufanya Mawasiliano

    Mawasiliano mazuri ni muhimu katika biashara na uongozi. Watu wenye uwezo wa kufanya mawasiliano mazuri na kusikiliza wengine wanaweza kufanikiwa katika kuajiri na kusimamia wafanyakazi\

    Njia Tano Za kuwa na Ukuaji Kwenye Maisha, Biashara na Kila kitu unachofanya

    13. Kiashiria cha kumi na tatu ni kuwa na Maono ya Ubunifu:

    Ubunifu ni muhimu katika kufanikiwa katika biashara. Watu wenye uwezo wa kuona njia mpya za kufanya mambo na kubuni suluhisho mpya wanaweza kuwa na uwezo wa kuajiri na kusimamia wafanyakazi. Kiukweli ubunifu ni m oyo wa biashara na biashara yoyote ambayo haina ubunifu ni suala la muda tu hiyo biashara itatoweka kwenye soko. Unahitaji ubunifu kwenye uzalishaji wa bidhaa, unahitaji ubunifu kwenye kufanya masoko, unahitaji ubunifu kwenye kuuza. Yaani, karibia kila kitu ni ubunifu.

    SOMA ZAIDI: JINSI UBUNIFU UNAVYOWEZA KUKUINUA KWENYE BIASHARA

    14. Kiashiria cha kumi na nne ni kuwa na Uwezo wa Kufanya Kazi Kwa Bidii:

    Biashara mara nyingi inahitaji ufanye kazi kwa bidii. Muda mwingine inahitaji ufanye kazi muda mwingi zaidi ya kawaida, na hata muda mwingine ufanye kazi siku za sikukuu. Mfano Rweyongeza hapa nipo naandika makala hii ikiwa ni siku ya pasaka saa tano asubuhi, muda ambao najua wazi kuwa watu wengine wapo wanakula bata au wanapanga kwenda kula bata.

    Jack Ma kuna siku aliwahi kusema kwamba wakati mwingine unahitaji kufanya kazi kwa takribani saa 16-18 kwa siku. Hii yote ni kwa ajili ya biashara yako. Kama unaona hizi gharama unaweza kuzilipa, inawezekana siku siyo nyingi utahitajika kuajiri na utakuwa boss kwenye biashara yako. Jiandae sasa.

    SOMA ZAIDI: Gharama Sita Unazopaswa kulipa ili kufikia ndoto zako.

    15. Kiashiria cha kumi na tano kufanya Maamuzi Yasiyoepukika

    Mara nyingine katika biashara, kunahitaji kufanya maamuzi ambayo siyo rahisi na hata wewe mwenyewe yanakuogopesha. Kwa lugha nyigine, haya ni maamuzi magumu.

    wakati mwingine unaweza kufanya maamuzi kama haya, ila yakawa siyo maamuzi maarufu, watu kwenye timu yako wakayapinga, kwa sababu hawaoni kule unapoona wewe. sasa unahitaji kuwa mtu wa kufanya maamuzi na kuyasimamia. Watu wenye uwezo wa kufanya maamuzi magumu na kusimamia matokeo yake wanaweza kufanikiwa katika kuajiri na kusimamia wafanyakazi.

    SOMA ZAIDI: KONA YA SONGA MBELE; Jinsi Ya Kuongeza Ufanisi Kazini

    16. Kiashiria cha kumi na sita ni uwezo wa Kusimamia Muda:

    kWENYE biashara muda ni kitu chenye thamani kubwa sana. Kama mfanyabiashara hauna muda wa kutosha wa kufanya kile kitu. Kama mfanyabiashar aunapaswa kuhakikish kwamba umewekeza muda wako na unautumia vyema kabisa bila ya kuupoteza.

    Usimamizi wa muda ni muhimu katika biashara na uongozi. Watu wenye uwezo wa kusimamia muda wao na wa wafanyakazi wao vizuri wanaweza kufanikiwa kwenye biashara

    SOMA ZAIDI: Wafanyabiashara Waliofanikiwa Wanavyotunza Muda

  • UTABIRI: Kitu Kimoja Ambacho Ni Uhakika Hakitatokea Maishani Mwako

    Rafiki yangu wa ukweli, bila shaka unaendelea vyema kabisa na shughuli zako za kila siku.

    Siku ya leo nimekuandalia makala ya kushangaza kidogo. Na makala hii ni utabiri.

    Mimi syo mtu ninayeamini sana kwenye tabiri, unabii na vitu vinavyoendana na hili.

    Ila leo nimevutwa kukupa utabiri huu, na ninatoa utabiri huu nikiwa na uhakika kuwa lazima huu utabiri utatokea kwenye maisha yako. Nina uhakika kabisa wa asilimia 100.

    Utabiri wangu unasema kwamba huwezi kufikia malengo ambayo hujaweka. Rafiki yangu, tuwe tu wakweli, kama hujaweka malengo, kama hauna malengo ambayo unapaswa kufikia ni wazi kuwa huwezi kufikia malengo hayo.

    Kiufupi ni kuwa huwezi kufikia malengo ya kitu ambacho wewe mwenyewe hauna.

    Hivyo, njia bora ya wewe kufikia malengo yako ni kuanza kuweka hayo malengo sahihi kwanza.

    Kisha kuanza kuyafanyia kazi.

    Nje na hapo tusidanganyane, hutaweza kufanikisha na kufikia hayo malengo ambayo wewe mwenyewe hauna.

    Hivyo, kazi yako kubwa ambayo unapaswa kuifanya siku ya leo ni kuhakikisha kwamba umeweka malengo. Weka malengo ambayo utaanza kuyafanyia kazi mara moja kuanzia leo hii.

    Ni hivyo tu.

    Uwe na siku njema sana rafiki yangu.

    Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli.

    SOMA ZAIDI: NGUVU YA KUWEKA MALENGO

  • Iga Ufe

    Kuna baadhi ya vitu huhitaji kuiga kwa watu wengine.  Badala yake unapaswa kuvifanya kulingana na wewe mwenyewe.

    Siyo kila kitu wanachofanya wengine kinaweza kukufaa na wewe pia. VIngine vinaweza kuwa sahihi kwao, lakini siyo sahihi kwako. Ni muhimu kwako kufahamu kipi ni sahihi kwako, na kuwekeza nguvu yako kubwa hapo.

    Kuna watu wanakopa na mshahara wao unapoingia tu, wanakuwa haawana kitu ambacho kimebaki, wanaenda kulipa madeni na kuendelea kukopa zaidi. Hiki kitu kinaweza kuwa sahihi kwao, lakini siyo sahihi kwako. Iga ufe.

    Kuna watu wakipokea fedha, wanafanya matumizi yote unayoyafahamu hapa duniani, halafu ndiyo wanasubiri kile kinachobaki waweke akiba. Hiki kitu kinaweza kuwa sahihi kwako, ila siyo kwako. Iga ufe.

    Kuna watu hawana malengo wala ndoto zozote kubwa, wanaishi tu ilimradi maisha yameenda. Wanaishi kwa usemi kwamba kesho itajipa yenyewe, hawana haja ya kuihangaikia kesho. Hiki kitu kinaweza kuwa sahihi kwao, ila kwako. Iga ufe.

    Fahamu yapi ni sahihi kwako kufanya. na wekeza muda wako kwenye hayo ambayo ni sahihi kwako kwa wakati huu. Achana na yale yote ambayo siyo sahihi.

    soma zaidi 

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana na +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • KIPAJI NI DHAHABU: Ila hapa kuna vitu vitano ambavyo kila mwenye kipaji anapaswa kufahamu

    Juzi kuna mtu alinifuata kikashani kwangu whatsap na kuniuliza, mbona kijana yule mwenye kipaji ameshindwa kusaidiwa? 

    Nilimwuliza kijana yupi? baadaye kidogo alinitumia picha za yule kijana pamoja na kazi alizofanya. 

    Nilitakafari hili kidogo, ila nikaja kugundua kwamba watu wenye vipaji kuna vitu vitabo muhimu ambavyo hawafahamu.

    Ningependa na wewe ufahamu hivi vitu, kuanzia leo hii, nina uhakika vitakuwa vitu vyenye manufaa makubwa sana kwako.

    1. kipaji ni dhahabu, ila ni ukweli kuwa kipaji hakitageuka kuwa dhahabu bila ya wewe kukifanyia kazi
    2. Usitegemee kamba kipaji chako kitaanza kukulipa siku hiyohiyo. Kinachukua muda.
    3. Ikitokea kipaji chako hakijakulipa, usikate tamaa na kuacha kukifanyia kazi. Kumbuka kwamba kila kitu huwa kina majira yake.
    4. Ni muhimu sana kufahamu misingi sahihi ya kutengeneza fedha kwa kutumia kipaji chako badala ya kuanza kusubiri watu waje wakufadhili, wakudhamini. Ukweli ni kuwa ukisubiri watu wa namna hii waje, unaweza kujikuta kwamba unakata tamaa na hata unashindwa kufanyia kazi kipaji chako kwa uhakika kabisa.
    5. inapotokea majibu uliyokuwa unategemea yaje haraka hayajatokea, usikate tamaa wala kuishia njiani. Endelea kupambania kipaji chako bila ya  kurudi nyuma. Kipambanie mpaka kieleweke

    hayo ni mambo matano tu ambayo nilitaka uyajue kuhusu kipaji siku ya leo.

    KIPAJI NI DHAHABU
    Rafiki yangu, nimeandika kitabu. Kinaitwa KIPAJI NI DHAHABU. Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa +255684408755 sasa

    Hakikisha umepata kitabu changu cha KIPAJI NI DHAHABU: Ni moja ya kitabu kizuri sana ambacho unapaswa kusoma. Kimeeleza kila kitu kuhusu kipaji na jinsi unavyoweza kutumia kipaji chako kwa manufaa.

    Kupata nakala ya kitabu hiki hakikisha umewasiliana na 0684 408 755 sasa

    SOMA ZAIDI:

    1. Sababu 15 kwa nini haupaswi kuwa na plan B
    2. Sababu Kumi Kwa Nini Haupaswi Kuongea Sana

X