Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Kipaji chako umekiweka wapi? Umeajiriwa, umejiajiri au huna ajira?

    KIPAJI NI DHAHABU
    Rafiki yangu, nimeandika kitabu. Kinaitwa KIPAJI NI DHAHABU. Ili kupata kitabu hiki, wasialiana na mi kwa 0755848391 sasa

    Dhahabu ni madini yenye thamani sana hapa duniani. Siku ya leo tarehe 29/3/2024 wakati naandika hapa, imabidi niangalie mtandaoni ili kuona bei halisi ya dhahabu sasa hivi kwenye soko la dunia. Ninachoona hapa ni kwmaba bei ya dhahabu kwenye soko la dunia siku ya leo ni kati ya dola 70,000 na dola 75,000 kwa kilo moja

    Hii ni thamani ya hiki kitu kinachoitwa DHAHABU.

     

    Dhahabu, kabla haijawa na thamani kubwa hivyo, huwa inapitia kwenye hatua mbalimbali, mojawapo ya hatua hiyo huwa ni KUICHOMA KWA MOTO WA KIWANGO CHA JUU SANA. Moto huu unaiunguza, ndipo baadaye tunakuja kupata dhahabu.

    Ila leo hiii sipo hapa kuongelea kuhusiana na biashar dhahabu, badala yake nipo hapa kuonge ana wewe kuhusiana na KIPAJI chako.

    Nimekuwa nikiongea na watu na kuwasisitiza kwambna kipaji chao ni DHAHABU.

    Naam, kipaji chako wewe….

    Ni dhahabu. Ni kwamba kipaji hiki hakitageuka kuwa dhahabu kwa sababu umesoma hapa. Au kwa sababu umesiki amtu akisema hivyo. Ni mpaka uwe tayari kukifanyia kazi. Na wakati  mwingine kwa kutokwa na jasho, damu na machozi ndipo uje kufikia wakati wa kuvuna mavuno mazuri.

    Kumbuka kipaji chako ni dhahabu, ila dhahabu hii isipofanyiwa kazi haitakuja kuleta matokeo.

    Hakikisha umepata nakala ya kitabu hiki hapa, cha KIPAJI NI DHAHABU, utajifunz amengi kutoka kwenye hikitabu kuhusiana na kipaji chako na jinsi unavyowez akukinoa kwa manufaa yako ya sasa na ya baadaye.

    Imeandikwa na Godius Rweyongeza

    SOMA ZAIDI: KIPAJI NI DHAHABU: Jinsi Ya Kukigundua, Kukinoa Na Kukitumia Kipaji Chako Kwa Manufaa

    Kitabu Cha KIPAJI NI DHAHABU

     

  • Acha Uvivu, Fanya Jambo Hili Kila Siku Bila Ya Kuacha

    Kufikiri ni jambo ambalo tunapaswa kulifanya kila siku. Wengi hudhani wanafikiri lakini kumbe siyo. Kufikiri ni kazi ambayo hatupaswi kuikwepa.

    Inapaswa kuwa sehemu aya maisha yetu ya kila siku. Hakuna mtu ambaye anawez akufanya hiki kitu kwa ajili yako. Kuna vitu unaweza kuwapa watu na wakafanya hivyho vitu ila huwezi kuifanya wewe.

    Jipe kazi ya kufikiri kila siku kwa kufuata utaratibu maalumu ambao nimeuleza kwenye makala hii Ufahamu Uovu wa Lazima Kwenye Maisha Yako

    Ifuatilie hii makala, nina uhakika utajifunza mengi na utanishukuru kwa hicho.

    MAPAKA WAKATI MWINGINE NIKUSHUKURU SANA KWA MUDA WAKO.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana na +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391

  • Nguvu Ya Mtazamo (Ninalipwa laki mbili ndiyo maana mimi ni maskini vs Ninalipwa laki mbili ndiyo maana mimi ni tajiri)

    Rafiki yangu, mtazamo ni moja ya kitu muhimu sana hasa linapokuja suala la mafanikio. Mtu afikirivyo ndivyo anavyokuwa.

    Hivyo, kama unataka kufanikiwa, unapaswa kubadili mtazamo wako kutoka kuwa mtazamo hasi na kuw amtazamo chanya. Unapaswa kubadili mtazamo wako na kuanza kuona uchanya kwenye kile unachofanya.

    Hali na matukio mbalimbali yanayotokea kwenye maisha yako, badala ya kuona katika namna ya uhasi, uone uchanya.

    Tukichukua watu wawili, ambao wanaishi maisha sawa, ila wanatofautiana tu mtazamo. Hawa watu wawili, baada ya  muda watakuja kuwa na maisha tofauti, huku mmoja akiwa amefanikiwa na mwingine akiwa na maisha yaleyale ya kulalamika.

    Kwa nini,

    Kwa sababu ya mtazamo.

    Tuchukulie hawa watu wawili wanalipwa laki mbili kila mwezi. Mmoja akawa na mtazamo kwamba sitaweza kutengeneza utajiri kwa sababu tu ya kipato ambacho naingiza. Na mwingine akasema kwamba nitatengeneza utajiri kutokana na kipato ninachoingiza.

    Unadhani ni nani atatengenenza utajiri? Ukweli ni kuwa, yule ambaye ana mtazamo chanya. Mtazamo wa kuona kwamba kile kiwango cha fedha alichonacho ni sehemu ya kuanzia. Huyu ndiye atakayetengeneza utajiri ukilinganisha na mtu ambaye ana mtazamo hasi.

    Ujumbe muhimu ambao nataka uondoke nao siku ya leo ni kuhakikisha unakuw ana mtazamo chanya. Fikra chanya zitakupelekea mbali kuliko utakapokuwa na mtazamo hasi.

    SOMA ZAIDI:

    1. Kauli Yenye Nguvu: Ni bora Ufe Ukiwa unafanya unachopenda…
    2. Athari Ya Mtazamo Wako Kwa Vitu Vinavyokutokea
    3. 2024 badili mifumo yako ya kufikiri

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Pesa Zako Zimejificha Kwenye Hiki Kitu

    Miaka kadhaa iliyopita, mtandaoni kulikuwa na picha ya mtoto mdogo iliyokuwa inasambaa kama moto wa kifuu.

    picha hii ilikuwa ikimwonesha mtoto mdogo tu, ambaye aliajiriwa na kampuni kubwa ya Google.

    Sasa swali kubwa ambalo unaweza kuwa unajiuliza, ilikuwaje huyu mtoto mdogo akaajiriwa na kampuni kubwa kama GOOGLE.

    Jibu ni moja tu, huyu mtoto alikuwa anajua ambacho watu wengi hawajui. 

    Kiufupi ni kwamba alikuwa ana ujuzi ambao watu wengine hawana. Na hiki ndiyo kitu ambacho kilimfanya huyu mtoto sasa kuwa na nafasi ya kuajiriwa kwenye kampuni kubwa kama google.

    Sasa ninachotaka kukwambia siku ya leo siyo kitu kingine bali ni kuwa na wewe pesa zako zimejificha kwenye kitu kimoja kikubwa sana. Na kitu  HIKI siyo kingine bali ni ujuzi.

    Swali ambalo ningependa ujiulize siku ya leo ni ujuzi gani ambao unao ambao watu watakuwa tayari kuulipia na hawatataka kukupoteza. Yaani, watu watakuwa tayari kulipa kiasi chochote kwa sababu tu ya ujuzi huo ulionao?

    Pesa zako zimejificha kwenye ujuzi.

    Kama leo hii hauna ujuzi wowote, ni muda wako muafaka sasa wa kuanza kujifunza ujuzi mpya.

    Na ubora ni kwamba kwenye ulimwengu wa leo ni rahisi sana kujifunza karibia ujuzi wowote. Hakuna kitu chochote kile kitakachoshindikana kwako wewe kujifunza kwenye ulimwengu wa leo.

    Unaweza kujifunza na kuelewa kitu chochote kile unachotaka.

    Kuna kozi nyingi mtandaoni ambazo unaweza kujifunza, jifunze kupitia hizi kozi.

    Kuna video nyingi mfano kwenye mtandao wa youtube tu, kuna video za kutosha ambazo zinaweza kukuelimisha kila kitu unachohitaji kujua kuhusu kitu chochote kile unachotaka

    Hivyo, kazi yako kubwa ambayo unapaswa kufanya rafiki yangu, ni kuhakikisha kwamba unakuwa na ujuzi, ujuzi ambao utajifunza na kuanza kuufanyia kazi mara mooja hasa kwenye ulimwengu wa  leo ambapo ujuzi ni kitu muhimu sana.

    SOMA ZAIDI: 

    Ile video ya yule mtoto wa miaka 13 aliyeajiriwa na google nakuwekea hapa chini,

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu. Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

     

    SOMA ZAIDI: Njia Saba (07) Bora Za Kutangaza Ujuzi Wako Kwa Watu

  • Unajua Nini Kuhusu Bitcoin?

    Habari za Bitcoin sijui. Ila Habari za HISA, HATIFUNGANI NA vipande, nazijua.

    Niulize chochote kuhusu HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE nitakujibu.

    Na Tena ukitaka kuwa deep, basi hiki kitabu Cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE kitakuhusu.
    Na halafu utakipata Kwa bei nzuri TU.

    Hardcopy ni 25,000/-
    Softcopy ni 10,000/-

    Tumia namba ya simu 0684408755

    Karibu sana


     

  • Mshangao! Jinsi Muda Ulivyo wa Dhahabu Kwa Mfanyabiahsara na Mtu yeyote makini

    Leo nakuruhusu ufanye kitu kimoja tu, uzunguke popote pale hapa duniani, halafu  uje kuniambia ni wapi umekuta wanaweza kuongeza kiwango cha muda ndani ya siku.

    Ni wapi ambapo mtu anaweza kuwa na saa moja, lakini akaomba kuuongezewa saa jingine zaidi na akaongezewa? Ni wapi ambapo mtu anaweza kukopesha muda wake wa leo ili aje alipwe kwa riba kesho yake?

    Ukweli, ni kuwa hakuna sehemu ambapo muda unaweza kuongezwa, muda ni rasilimali muhimu sana ambayo haiwezi kuongezwa au kupunguzwa.

    Hivyo kama wewe ni mfanyabiashara, moja ya kitu muhimu sana ambacho unatakiwa kuhakikisha kwamba umefanya ni kutumia muda wako vizuri. Unaweza kupoteza vitu vingine vyote ukavipata, ila huwezi kupoteza muda ukaupata. Muda ni zaidi ya mali. 

    Hivyo moja ya jambo ambalo unaweza kulifanya likawa kama favor kwako ni kutumia vizuri muda wako. Na hili unaweza kulifanya kuanzia sasa.

    njia bora ya kuanza kwenye hili ni kuhakikikisha kwamba unaanz akupangilia ratiba yako ya kila siku vizuri. Yaani, kila siku unapoamka asubuhi, hakikisha kwamba unapangilia ratiba yako vizuri. Ipangilie ratiba yako, kisha anza kufanya na kutimiza majukumu yako kulingana na majukumu ambayo yako mbele yako.

    Kitu kimoja kikubwa ambacho nigependa kujua kutoka kwako ni kwa namna gani unaenda kuupangilia muda wako kuanzia leo hii

    kama bado hujajua njia ya kukusaidia wewe kuupangilia muda wako ni hivi, 

    Anza kwa kupangilia kila saa la siku yako kuanzia unapoamka mpaka jioni.

    Kila sasa lipa mamjukum,u ambayo utakuw aunafanya na kukamiliusha ndani ya huo muda.

    Kisha endelea mbele kwa kuhakikisha kwamba unautumia vizuri muda wako.

    Kumbuka Muda Ni Dhahabu

     

    SOMA ZAIDI: Kitabu Cha KIPAJI NI DHAHABU

    Hii Ni Sentensi Iliyonichekesha

    UWEKEZAJI NI NINI?

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana na +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391

  • Mbinu Tano (05) Za Kudai Hela Uliyomkopesha Mzazi Wako

    1. SHERIA ya kwanza wazazi wape Hela ya kula
    2. SHERIA ya pili, usikopeshe Hela kama biashara Yako siyo kukopesha
    3. SHERIA ya tatu, wasaidie wazazi kuhakikisha wanakuwa na VYANZO vitakavyowaingizia KIPATO Ili wasikutegemee.
    4. SHERIA ya nne, ukimkopeshe mtu yeyote, mkopeshe Ile Hela ambayo wewe mwenyewe huihitaji.
    5. SHERIA ya Tano, kamwe watu wasijue lini Huwa unaingiza Fedha. Usihemke Kwa kupata PESA. Mara zote ishi maisha yaleyale ukiwa na Hela na ukiwa huna Hela
    Hizi ndizo SHERIA Tano

    SOMA ZAIDI:

    1. Kutana na mtu mwenye kumbukumbu kali kuliko wote
    2. Kwa nini watoto wanapoteza pesa ya wazazi baada ya kurithi?
    3. Sababu 5 Kwa Nini Haupaswi Kuomba Fedha Kwa Wazazi: Jifunze Kujitegemea na Kuwekeza Kwa Mafanikio
      Jifunze zaidi: www.songambele.co.tz

    By, Godius Rweyongeza

  • Huu Ndiyo Ustaraabu Wa Hali Ya Juu Ambao Unapaswa Kuwa Nao

    Rafiki yangu wa ukweli, salaam. Hongera sana kwa kazi, siku ya leo, nataka kuongea na wewe kuhusu ustaraabu.

    Mara nyingi watu huwa wanapenda kuonesha ustaraabu kwenye maeneo tofautitofauti. Ila leo hii ninataka nikwambie kuhusu ustaraabu wa hali ya juu ambao unapaswa kuwa nao.

    Na aina hii ya ustaraabu ambayo unapaswa kuwa nayo ni kufanya kile unachopasawa kufanya.

    Ndiyo, huu ndiyo ustaraabu wa hali ya juu kabisa.

    Kama wewe ni mwimbaji, ustaraabu mkubwa sana ambao unaweza kuwa nao ni kuimba.

    Kama wewe ni mwigizaji, ustaraabu mkubwa ambao unapaswa kuwa nao ni kuigiza.

    Kama wewe ni mchoraji, ustaraabu wa wachoraji ni kuchora, 

    Ustaraabu wa waandishi ni kuandika

    Ustaraabu wa dereva ni kuendesha kwa kufuata sheria za barabarani. Huo ndiyo ustaraabu pekee wa viwango vya juu.

    Ukiwa na ustaraabu ambao unakuzuia wewe kufanya kazi unayopaswa kufanya, basi huo ustaraabu unanipa mashaka kidogo. 

    Hivyo basi siku ya leo nikusihi kitu kimoja tu. Anza kuwa mstaraabu. Sawa ee. Fanyia kazi yale unayopaswa kufanyia kazi bila ya kuchoka wala kurudi nyuma. Huu ndiyo ustaraabu pekee ambao unapaswa kuwa nao rafiki yangu.

    Kama mpaka hapo umenielewa basi naomba unyooshe mkono juu.

    Mpaka wakati mwingine. 

    SOMA ZAIDI

    1. Jinsi Ya Kushughulika Na Fedha Unazopata Kutokana Na Kipaji Chako
    2. Kama unafikiri elimu Ni ghali, jaribu ujinga
    3. JE, WAJUA KWAMBA DAKIKA KUMI NA TANO ZINAWEZA KUKUFUNDISHA LUGHA MPYA? DAKIKA 15 MTANDAO NI ZINAKUPA NINI?

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana na +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391

  • Njia Tatu Za Uhakika Zitakazokusaidia Wewe Kuweka Akiba Bila Ya Kutoa (Namba 3 Ndiyo Yenyewe Haswa!)

    Wahenga wanasema kwamba ukiona vyaelea, basi ujue vimeundwa, hivyohivyo ndivyo ilivyokuwa kwa mji wa Babilon (Babeli) ambao kwa nyakati zake ulikuwa mji tajiri na wenye watu wenye utajiri.

    Simulizi zake na busara za nyakati hizo zimebaki vitabuni kwa ajli yetu sisi vijana wa miaka yetu kuzitumia kwa manufaa. Lakini moja ya kitu kimoja na kitu kikubwa ambacho tunajifunza kutoka kwa hawa watu ni kuweka akiba bila kukoma.

    Yaani, kila siku kuifanya kuwa siku ya kuweka akiba.

    Ukweli ni kuwa, kama una ndoto kubwa na malengo yoyote yale makubwa, ukweli ni kuwa hayo malengo, yatatimia tu kwa wewe kuwa na fedha. Asilimia kubwa ya ndoto ulizonazo zinahitaji fedha, ila cha kushangaza zaidi ni kwamba hizi fedha siyo kwamba unazo kama keshi mkononi mwako leo hii.

    na isitoshe kila siku kuna majukumu mapya ambayo yanazidi kujipenyeeza yakiwa yanahitaji fedha zako unazozipokea kila leo.

    sasa unafanyaje ili uweke akiba bila kuitumia.

    kwa leo ninaenda kukutajia njia tatu tu za uhakika ambazo zitakusaidia wewe kuweka fedha bila kuzitumia,

    1. kwanza ni kuweka fedha yako kwenye akaunti ya simu ambayo wewe mwenyewe hauna neno lake la siri. Hiki kitu kinaweza kuwa kimekuja kwako kama mshangao kidogo. Yaani, iweje niweke fedha kwenye akaunti ambayo mimi sina neno la siri. Ndiyo inawezekana, unachotakiwa kufanya ni hivi, unasajili laini yako. Halafu unamtafuta mtu ambaye unamwamini, mtu ambaye anaweza kukushikilia. Halafu mtu anakuwekea namba ya siri kwenye hii akaunti yako. Halafu unamwahidi kwamba naomba usinitajie namba ya siri mpaka pale nitakapokuwa nimeweza kuweka akiba ya kiasi kadhaa kwenye hii laini. Mfano, unaweza kumwambia kwamba usinitajie neno la siri mpaka pale nitakapokuwa nimeweza kuweka akiba ya milioni mbili kwenye hii laini. Kwa hiyo, laini unakuwa nayo wewe, umeisajili wewe ila kitu pekee ambacho hauna ni namba ya siri. Huyu mtu wako wa karibu anakupa tu namba ya siri unapokuwa umetimiza lengo la awali. na hapo ndipo unapata uwezo wa wewe kwenda kutoa hiyo fedha. Hii ni njia ya kwanza, kama hii ni ngumu kwako. Twende kwenye njia nambari mbili.
    2. Fungua akaunti kwenye benki ambayo hutachukua kadi, hutaiunganisha na njia yoyote ile ya kimtandao, na wala hutachukua checkbook ya kutolea fedha. Yaani, unabaki unajua akaunti ya benki tu. Unaanza kuweka akiba kwenye hii akaunti, hutoi pesa mpaka unapokuwa umeweza kufikia lengo lako.
    3. Weka hela yako Utt moja kwa moja. Tena ngoja kwenye hili nikushauri vizuri kabisa, sajili akaunti yako kwa simu. Hapo chini ninaenda kukuwekea njia sita za kufungua akaunti yako ya utt amis. Ukisajili akaunti ya UTT, usajili wako unakuwa haujakamilika, lakini kwa aina hii ya usajili, unaruhusiwa kuweka pesa na unanufaika na vitu vyote vizuri vinavyopatikana pale UTT AMIS, ila haurusiwi kutoa fedha. Sasa hii ni nzuri kwako, kwa sababu, usajili haujakamilika. Unaweza kuamua kuacha hivihivi siku zote, ukaja kukamilisha usajili wako pale unapokuwa umekamilisha lengo lako. Kwa maoni yangu, hii ndiyo njia bora zaidi kuliko zote. Ni njia bora kwa sababu tu, inakusaidia wewe kuua ndege wawili kwa jiwe moja. Unaweka akiba huku ukipata faida za kiuwekezaji. Inawezekana hapa unajiuliza, Hivi hii UTT ni nini? Inafanyaje kazi? Na mimi naweza kujiungaje? Nina mwongozo mzuri, kitabu ambacho kitakusaidia wewe kupata maarifa kamili kuhusu uwekezaji kwenye HISA, HATIFUNGANI na VIPANDE. Unaweza kupata kitabu hiki kwa kuwasiliana na +255 684 408 755. Fanya hivyo sasa hivi.

    Kwa leo hizi zinatosha au unasemaje rafiki yangu! Kikubwa ni kwamba uanze kuzifanyia kazi. Kamwe hutapata matokeo bila ya kuzifanyia kazi hizi mbinu. Ni mpaka uanze kuzifanyia kazi ndipo utakuja kupata matokeo ambayo yameelezwa au ambayo unatazamia kupata.

    Kitu kikubwa ambacho unapaswa kukifanyia kazi siku ya leo ni kuhakikisha umepata nakala nzuri sana za vitabu. Nakala hizi ni kitabu cha MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE pamoja kitabu cha MAAJABU YA KUWEKA AKIBA. Hivi vitabu vina mwongozo kamili hasa kuhusiana na mada ya leo ambayo nimeieleza hapa kwa kina.  Usichelewe kuwasiliana na +255 684 408 755 sasa ili uweze kujipatia nakala zako leo hii. Kila nakala ni 25,000/-. Jipatie nakala zako sasa.

    SOMA ZAIDI: Ijue Siri Ya Babiloni Kuwa Mji Tajiri Kuliko Yote Duniani

    Sababu 100 kwa nini unapaswa kuweka akiba ya pesa

    Rafiki yangu, kwa leo, naomba niishie hapo.

    Umekuwa nami rafiki yako wa ukweli,

    Godius Rweyongeza

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com
    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana na +255 684 408 755

    For Consultation only: +255 755 848 391

  • Imethibitishwa! Hii Ndiyo Kanuni Maalum Ambayo Unapaswa Kufuata Kwenye Biashara. Ifuate kwa faida yako,m ivunje kwa hasara yako

    Kila sehemu ina kanuni zake maalum ambazo kila mmoja anapaswa kuzifuata. Na kanuni huwa zikifuatwa, mara zote huwa zinaleta matokeo chanya, ila zikikiukwa au kupuuzwa, huwa unakuta kwamba unapata matokeo hasi.

    Mfano wa wazi kabisa kwenye hili ni kwenye kuendesha gari barabarani. Ukifuata kanuni za kuedesha gari barabaani, ni wazi kwamba utaweza kufika salama kule ambapo unaelekea, ila kwa upande mwingine ukiedesha gari kwa namna unavyotaka mwenyewe. Badala ya kupita kushoto ukapita kulia, sehemu yenye mataa ambayo yanayokuonesha kwamba unapaswa kutulia kwanza, wewe ukapitiliza tu moja kwa moja.

    Sehemu unapopaswa kwenda kwa mwendo wa 50 wewe ukaenda kwa 120

    Ni wazi kuwa huwezi kufika salama. Unaweza kufanikiwa kubahatisha mara moja, ila huwezi kufanya hivyo mara zote kwa mafanikio makubwa. 

    Sasa tunapoongelea biashara. Ina kanuni zake pia.

    Ukizifuata unatoboa, ila usipozifuata, ni wazi kuwa amambo mengi yanaenda kuwa magumu kwa upande wa wako.

    Unapoanzisha biashara, kuna mambo 55 ambayo unatakiwa kuzingatia kama ambavyo nimeyaeleza kwenye kitabu MABO 55 YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZISHA BIASHARA. Nakushauri uweze kupata nakala yako na ujisomee, utanishukuru sana kwa siku zijazo.

    Hakikisha unajipatia nakala ya kitabu hiki. Tumia namba ya simu +255 684 408 755

    Ila kwa leo ningepnda kuongelea kitu kimoja tu. kitu hiki ni muda wa kufungua na kufunga biashara yako.

    Unapoanzisha biashara yako, hakikisha kwamba unakuwa na muda maalum ambao unakuwa umefungua na muda maalum wa kufunga biashara yako. Hiki ni kitu kidogo sana lakini chenye nguvu kubwa sana.

    Kiufupi ni kwamba unapoanzisha biashara yako unapaswa kuanza kuiwekea misingi sahihi. Bila ya kuwa na misingi sahihi, huwezi kujenga biashara ya maana. Misingi sahihi ndiyo ambayo itakufanya uiendeshe biashhara yako bila stress hata kidogo.

    Na moja ya msingi muhimu ambao unapaswa kuuweka ni msingi wa kufungua na kufunga biashara yako.

    Ijulikane kabisa kwamba, muda wa kuingia kazini ni saa fulani na muda wa kutoka ni muda fulani. Kuwa na utaratibu kama huu hata kama kwenye biashara yako kwa sasa hivi uko peke yako.

    Kumbuka kwamba lengo la biashara yako siyo wewe kuendelea kufanya kila kitu peke yako. Badala yake ni kwamba lengo lako kubwa ni kuhakikisha kwamba hii biashara inakua na unakuwa na matawi pamoja na watu wengine ambao wanakusaidia kwenye kufanya na kutekeleza baadhi ya majukumu. Sasa haya majukumu huwezi kuyatekeleza kwa ufanisi bila ya kuwa na mpango wa muda maalum wa kuingia na kutoka.

    Ushauri wangu kwako kabla hujaenda kuweka muda wa kuingia na kutokia kazini kuwa saa tatu. Maana niliwahi kuongea na rafiki yangu mmoja akaniambia mimi muda wa kuingi na kutoka kazini ni saa tatu naingia, na saa kumi na moja nafunga.

    Ni kweli kwa upande wa benki kuna mengi ya kujifunza kutoka kwao, ila kwa upande wa muda naom,ba unisikilize.uKIWAIGA BENKI UTAPASAUKA MSAMBA.

    Unajua kwa nini nakwambia hivi, ni kiwa sababu benki huwa zinafanya kazi saa 24 siku saba za wiki. Kuna ATM za kutoa pesa benki, ambazo zinafanya kazi saa 24. Wewe biashara yako ina ATM kama hii. Ni kitu gani kwenye biashara yako ambacho kinafanya kazi saa 24 bila ya kuacha. JE, NI BLOGU AU TOVUTI?

    Najua unaijua vizuri biahsara yako, sihitaji nikuhubirie kwenye hilo, ila lifahamu. Na umakini wako wote uweke kwenye kuijenga vizuri kuanzia mwanzo,

    Sasa hivi benki zinakuja na ATM za kuweka pesa. Maana yake utakuwa na uwezo wa kuweka na kutoa benki muda wowote.

    Wewe unapoanza biashara yako, kuwa na utaratibu huu wa kuingia na kutoka na hasa muda wako uwe mapema.

    Mapema ikiwezekana saa 12, hiki kitu kitakusaidia wewe kuwa unawapata wateja wa asubuhi na mapema na wateja wa jioni baada ya wengine kuwa wamefunga. Katika ulimwengu ambao dunia inafanya kazi saa 24.

    Wewe pia unapaswa kuwa na muda mrefu ambao biashara yako itakuwa imefunguliwa kwa kuanzia. Na tunapoelekea, biashara yako inaweza kuwa imefunguliwa muda wote saa 24.

    Kwa leo nitaishia hapa, ila ukiendelea kufuatilia makala na mafunzo mengine ambayo ninatoa hapa kila siku, utazidi kujifunza zaidi hasa kuhusu biashara na namna ambavyo unaweza kuboresha kile unachofanya. 

    Kujifunza zaidi soma makala hizi

    1. Njia Tano Za kuwa na Ukuaji Kwenye Maisha, Biashara na Kila kitu unachofanya
    2. Ni muda Upi Sahihi Kuajiri Wafanyakazi kwenye Biashara?
    3. Sababu mbili Kwa Nini kila anayetaka kuwekeza anapaswa kuwa na biashara pia

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana na +255 684 408 755

    For Consultation only: +255 755 848 391

X