Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Hatutoki Hapa Mpaka Tushinde

    Kwenye makala ya jana, kama utakumbuka, niliekeza juu ya fikra ambavyo zinaweza kukupelekea wewe kupata au kutopata matokeo.

    Lakini niligusia hadithi fupi ya wanajeshi walioenda kupigana na jeshi kubwa, kapteni wa jeshi hilo akawa anawaambia kuwa hatutoki hapa mpaka tushinde.

    Leo hii nipo hapa Kwa mara nyingine KUELEZA zaidi juu ya hii dhana ya hatutoki hapa mpaka tushinde.

    Kwa lugha nyingine naweza kuiita ung’ng’anizi.

    Fikra ya aina hii unaihitaji sana hasa unapoendea MAFANIKIO MAKUBWA. Ni mara nyingi sana utahitaji kusema, sitoki hapa mpaka nitoboe.

    Kuna wakati unahitaji kuonana na mkuu Fulani, halafu wasaidizi wake wanakuzia usionane naye, jiambie sitoki hapa mpaka nionane naye.

    Nakumbuka siku kadhaa zilizopita nilitoka ofisini kwangu saa 11 hivi, kwenda kwenye duka la Airtel. Nilikuwa nahitaji router Kwa ajili ya ofisi yangu.

    Tangu asubuhi, nilikuwa nimetingwa na majukumu, hivyo sikuweza Kutoka mapema, na hii jioni saa 11, ndiyo ulikuwa muda wangu pekee

    Laiti ningesema kesho, nisingepata pia muda wa kufanya hivyo asubuhi, maana muda wangu hasa wa asubuhi Huwa nauheshimu sana.

    Lakini isitoshe hiyo router ilitakiwa kuwepo ofisini KABLA ya saa Moja kesho yake, la sivyo kazi zisingefanyika Kwa ufanisi.

    Kilichotokea, nilichukua boda chap Kwa haraka kuwahi kwenye ofisi za Airtel na pale nilikuta wamefunga.

    Kitu cha kwanza kabisa, niligonga mlango.

    Kwa bahati nzuri mlangoni walikuwa hawajatoa Ile alama ya PUSH. lakini wakati huohuo walikuwa wamewekwa alama ya CLOSED.

    Nilichofanya niliPUSH mlango. Ila haukufungua maana ulishafungwa, ilibidi nitulie mlangoni.

    Mdada mmoja wa ndani akaanza kunionesha kuwa pamefungwa, na Mimi nikawa namwonesha kuwa pameandikwa PUSH.

    Mwisho alitoka jamaa mmoja (nadhani ndiye baunsa wao😁😁) akafungua mlango.

    Alivyofungua mlango TU, nikamwambia nilichokuwa nataka, na nikamwambia naihitaji sasa hivi. Nikamalizia Kwa kusema, siondoki hapa mpaka nipate hii router.

    Jamaa akasema, ebu ngoja niongee na wenzangu.

    Wakati huohuo, bodaboda niliyekuwa nimekuja naye alikuwa hataki kuondoka (inaonekana naye alikuwa kinga’anganizi!). Alishaona FURSA, nadhani alikuwa anajisema kimoyomoyo,  huyu jamaa nimekuja naye bora nisiondoke haraka, maana asipohudumiwa nitakuwa boda wa kumrudisha, napiga Hela mara mbili😁.

    Akawa akiniambia wamefunga tuondoke. Ilibidi nimpuuze tu.

    Baada ya muda Sasa, ndipo yule bausa alirudi na kuniruhusu niingie ndani na huduma nikapata.
    Sitoki hapa mpaka kieleweke.

    Kwenye biashara na kwenye maisha, hasa unapokuwa unapambania ndoto zako kubwa, unahitaji kuamua nitapambania malengo na ndoto zangu kubwa bila ya kurudi nyuma, mpaka kieleweke. Ni au nifanikishe hizi ndoto zangu kubwa, au nife nikiwa nazipambania.
    Sing’atuki hapa, mpaka kieleweke.

    Wakati mwingine kwenye kung’angania hatupata kile tunachotaka siku hiyohiyo, itatuchukua muda kuweza kufanikisha hicho tunachotaka, ila ukweli ni kuwa, tukiwa ving’ngang’anizi ni wazi kuwa lazima tu tutatoboa.

    Rafiki yangu, kwa leo nadhani inatosha, utakuwa umeweza kupata mengi kutoka kwenye somo la leo. Mimi nikutakie kila la kheri

    Tukutane kesho kwenye somo jingine zuri kama hili, lakini kabla kabisa hujaondoka kabisa. Hakikisha umesoma makala hizi

    1. Kitu Kimoja kinachokwamisha mafanikio ya watu wengi
    2. Kama haupo tayari kupoteza, hautaokota
  • Vita Ya Maisha Anashinda Mtu Anayefikiri Anaweza

    Tarehe 25/9/2016 niliandika makala hii inayoeleza Jinsi Ya Kuepuka Kujiua Mwenyewe Kiakili

    Mwishoni nikahitimisha Kwa kusema kwamba vita vya maisha anashinda mtu ANAYEFIKIRI ANAWEZA.

    Leo hii nimerudia kuisoma hii makala, nilichogundua ni kwamba hii makala Bado Ina nguvu Leo hii sawa na nilivyoandika takribani miaka 7 iliyopita.

    Ukweli ni kuwa kile unachojaza kwenye akili Yako Ndicho unakuja kupata kwenye uhalisia.

    Kile unachojiambia na kuaminisha ubongo wako, Ndicho kinatokea.

    Miaka mingi iliyopita kuna wapiganaji walienda kupigana na jeshi kubwa. Jeshi ambalo lilikuwa limewazidi Kila kitu.
    Wingi wa wanajeshi
    Ubora wa vifaa

    Na ukweli mwingine ni kuwa Hilo jeshi lilienda kupigana ugenini.

    Kilichotokea. Kapteni wa jeshi baada ya wanajeshi kushuka Kutoka kwenye boti zao, aliamuru meli zote zichomwe moto. Halafu akatangaza mbele ya jeshi lake na kuwaambia, mnaona hizo meli zinavyoungua, hii ndiyo kusema kwamba, hatutoki hapa, labda tushinde

    Kitendo hiki Cha kuchoma boti zote moto kiliamsha Ari wa kupambana miongoni mwa wanajeshi.

    Kila mmoja akaanza kufikiri juu ya ushindi
    Kila mmoja akaanza kuishi kiushindi.
    Na jeshi lilipigana mpaka likashinda.

    Ninachotaka ufahamu siku ya leo ni kwamba, ushindi wa kwanza kabisa tunaupata akilini. Halafu baada ya hapo ndipo tunakuja kupata ushindi kwenye uhalisia.

    Mwandishi wa kitabu Cha the secret of the millionaires mind kwenye hili amesisitiza kitu kikubwa sana.

    Anasema,
    BE-DO-HAVE
    KUWA-FANYA-PATA

    Ili nisikuache hewani, nitaelekza hili Kwa undani kidogo

    KUWA

    Unajua hii maana yake nini? Yaani, kuwa unachotaka, Anza kufikiri katika Ile namna.

    FANYA

    Sasa baada ya kuwa umetengeneza fikra sahihi, kinachofuata ni wewe kuanza kuishi Kile ulichotengeneza kwenye fikra zako.

    Kwa mfano, kama umetengeneza fikra ya kuwa bilionea. Kinachofuata ni wewe kuanza kuishi kama MABILIONEA wanavyoishi.

    Ukitengeneza fikra ya ukurugenzi, Anza kuishi kama wakurugenzi wanavyoishi.

    Fikra zako Sasa, zilete kwenye uhalisia.

    Halafu mwisho Sasa ndiyo utakuja

    ku PATA hicho kitu ambacho umekijengea fikra Kwa muda mrefu na kukifanyia kazi.

    Kinachowakwamisha Wengi ni kwamba wanataka wapate kwanza, halafu ndiyo waje wawe na fikra chanya.

    wewe kuwa tofauti kidogo, anza kwa kuhakikisha kwamba unakuwa na fikra chanya, kuwa na picha ya kule unapoelekea na jione kama mtu ambaye tayari amefikia hilo lengo, halafu baada ya hapo. Pambana sasa ili kufikia malengo na ndoto zako hizo kubwa.

    SOMA ZAIDI

    1. Badili Fikra zako Ili Ubadili Maisha Yako
    2. Mbinu za kutimiza malengo yako

    RAFIKI YANGU,Kwa leo inatosha. Tukutane kesho, kutakuwa na mwendelezo wa makala hiihii hapahapa.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana na +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 39

    For Consultation only: +255 755 848 391

  • MAAJABU! Hii Ndiyo Siri Usiyoijua Kuhusu Watu Waliofanikiwa

    Rafiki yangu wa ukweli, salaam. Hongera sana kwa siku hii nyingine ya kipekee sana. Nina uhakika leo inaenda kuwa ni moja ya siku yako bora kabisa

    Moja ya kitu ambacho watu wengi wamekuwa hawafahamu ni siri kutoka kwa watu waliofanikiwa. Wengi hudhani kuwa hawa watu waliofanikiwa, basi wamekuwa hivyo aidha kwa kuzaliwa, au walikutana na bahati tu hapa njiani.

    Hiki kitu kimekuwa kinawasukuma wengi kutafuta njia za mkato za kutafuta mafanikio. Ila ukweli ni kuwa hakuna njia za mkato, ambazo unaweza kutumia ili kufikia mafanikio makubwa, na mara nyingi, njia za mkato ndizo huwa ni njia mbaya zaidi.

    Ni njia mbaya zaidi kwa sababu, kwa sababu zinakufanya unapoteza siyo tu muda, bali rasilimali pia. Njia za mkato ndiyo njia ndefu zaidi kwenye kufanikiwa na kufikia mafanikio makubwa.

    SOMA ZAIDI: Njia PEKEE Ya Mkato Itakayokupa Mafanikio Makubwa Ni Hii Tu

    Kitu pekee ambacho unapaswa kujua kuhusu watu waliofanikiwa ni kwamba hawa watu siyo kwamba wamefanikiwa ndani ya siku moja tu. Hapana.  Hawa watu wamekuwa wanafanya kitu kimoja kwa muda mrefu.

    Kitu kimoja unachopaswa kufahamu, kabla hujakata tamaa, kabla hujaona kwamba hiki ninachokifanya hakiwezekani. Kitu kimoja unachopaswa kufahamu ni kuwa unapaswa kuendelea kufanyia kazi malengo na ndoto zako kubwa kwa muda mrefu bila ya kuacha.

    Kama kitu unachokifanya hujakifanya kwa bidii zako kwa miaka zaidi ya mitano, basi jua wazi kuwa unapaswa kuendelea kupambania malengo na ndoto zako kubwa mara zote.

    Rafiki yangu, nadhani kwa leo inatosha. tukutane kesho kwa makala nyingine bora kabisa kama hii.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana na +255 684 408 755

    For Consultation only: +255 755 848 391

  • INAUMIZA SANA! Kosa Kubwa Unalofanya Linaloathiri Ubongo Wako Na Namna yako Ya Kufikiri (Ukikabiliana na hili kosa, utabadili maisha yako kiujumla)

    Nimekuwa mkulima tangu nimezaliwa mpaka leo hii. Kiuhalisia nimekuwa nikiwaambia watu kuwa kitu ambacho kitanipa ubilionea ni kilimo. Na huu ndiyo ukweli, na kuthibisha hilo chuoni nilibobea kwenye kilimo, nikiwa najua kabisa Kilimo tu lazima kitanitoa siku moja.

    Moja ya kitu ambacho huwa tunakilinda sana kwenye kilimo ni bustani yako au shamba. Ukweli ni kuwa kwenye shamba langu mimi siwezi kukubali mtu yeyote aingie tu hovyohovyo na kufanya chochote. Lina ulinzi, na nikigundua mtu kaingia, inaweza kuwa kesi kubwa.

    Hiki kitu siyo kwangu tu, ila ni kwa wakulima wengi. Hakuna mkulima yeyote kwa mfano ambaye anaweza kuruhusu mtu aingie shambani kwake na kuweka sumu, au uchafu wa namna yoyote ile ambao hautakiwi. Kama wewe unaweza kumruhusu mtu afanye hivyo kwenye shamba lako nadhani unaweza kuandika maoni yako hapo chini, ili tujue.

     

    Sasa ebu pata picha ya shamba, ni kitu ambacho tunakilinda kwa nguvu zote. Ila cha kushangaza ni kwamba tunasahau kitu kimoja muhimu sana ambacho tunapaswa kukilinda kwa nguvu zetu zote. na kitu hiki siyo kingine bali ni uboongo wetu.

    Ubongo wako wewe ndiyo. 

    yaani, inashangaza kuona kwamba unalinda sana bustani, ila linapokuja suala zima la ubongo wako unabugi. Unaacha watu wanaweka sumu na kiila aina ya uchafu.

    Mpaka hapo unaweza kuwa unajiuliza, kuwa hili linawezekanaje? Ukweli ni kuwa hili linawezekana kwa kile unachokuwa unaruhusu kuingiza kwenye ubongo wako.

    Pale unaporuhusu habari hasi ziingie kwenye akili yako, maana yake unakuwa umeamua kuweka sumu kwenye ubongo wako.

    Pale unaporuhusu habari za kukatisha tamaa, umbea na vingine vyote vinavyoenana na hivyo, maana yake unakuwa umeamua wewe mwenyewe kwa ridhaa yako mwenyewe kuingiza habari hasi kwenye ubongo wako.

    Kitu kama hiki siyo kitu ambach ounapaswa kuruhusu kiendelee kwenye ubongo wako. Hapana, badala yake ni kwamba unapaswa kulinda ubongo wako na kila kitu kinachoingia kwenye ubongo wako kwa nguvu zako zote.

    Uko ulivyo kwa sababu ya kile unachoingiza kwenye ubongo wako. Hii ndiyo kusema kwamba kama unataka kupata matokeo ya tofauti, sharti, uwe tayari, kuingiza vitu ambavyo vitakupelekea wewe kupata hayo matokeo.

    NA VITU MUHIMU AMBA YO UNAPASWA KUANZA KUINGIZA KWENYE AKILI YAKO KUANZIA LEO 

    1. Maarifa chanya. Yaani maarifa ambayo yanakusukuma wewe kusongambele na siyo kurudi nyuma.
    2. maarifa haya unaweza kuyapata kupitia vitabu, soma vitabu vingi kadiri uwezavyo. Unaweza kuanza na kitabu changu ambacho nakitoa bure kabisa. KIPATE HAPA CHINI, KINATUMWA KWENYE EMAIL, hviyo jaza email yako ili uweze kukipata.

    3. Maarifa haya pia unaweza pia kuyapata kupitia kujifunza kwenye semina, mafunzo mbali mbali kama makala nk.

    4. Maarifa haya unaweza pia kuyapata kupitia makala mbalimbali kama hii hapa

     

    Ikumbukwe kuwa, jukumu la kutunza bustani ya akili yako ni jukumu lako. hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kufanya hili jukumu kwa niaba yako. Jukumu hili kama kupiga push up, hakuna mtu ambaye anaweza kupiga pushup kwa niaba yako hata siku moja. Unapaswa kulifanya wewe mwenyewe

    SOMA ZAIDI: Vitu 13 ambavyo hakuna mtu anaweza kufanya Kwa niaba Yako

    Hivyo ni wajibu wako kuhakikisha kwamba umelifanyia kazi hilo jukumu bila ya kurudi nyuma.

    Kwa leo naomba niishie hapa

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana na +255 684 408 755

     

    For Consultation only: +255 755 848 391

  • Hii Ndiyo Kanuni Ya Fedha Ambayo Inavunjwa Na Wengi

    Fedha ina kanuni zake ambazo unapaswa kuzifahamu na kuzitumia vizuri. Moja ya kanuni hii ni kanuni ya rasilimali na dhima. Hiii ni muhimu sana kwako eafiki yangu kifahamu ili usije ukaingia kwenye mtego.

    Kulingana na kanuni hii ni kwamba unapaswa kununua zaidi rasilimali (assets) kwa sababu hizi rasilimali ndizo zinakuingizia fedha mfukoni kuliko unavyonunua dhima (liabilities).

    Kabla ya kununua kitu chochote jiulize hivi je, hiki ni rasilimali (asset) au dhima (liability) kama kinatoa fedha mfukoni basi jua wazi kuwa hiyo ni dhima.

    Kazi yako ya kwanza inakuwa ni wewe kuhakikisha kwamba unawekeza kwenye rasilimali zaidi.

    Inashauriwa kama unataka kununua dhima, utafute fedha mara mbili zaidi na uiwekeze kwenye rasilimali. Kwa mfano kama unataka kununua gari, jiulize naweza kununua mawili. Kama huwezi kununua magari mawili, maana yake unapaswa kuweka juhudi zaidi ili upate fedha ya kununua magari mawili kwanza ambayo umeiwekeza, kisha sas andiyo ununue gari yako.

    SOMA ZAIDI: Sheria Muhimu Katika Kutengeneza Pesa Na Kuwa Tajiri

    Kwa leo inatosha au unasemaje.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana na +255 684 408 755

    For Consultation only: +255 755 848 391

  • Kwa nini pesa ina majina mengi

    Pesa, fedha, hela

    Ikiwa kanisani au kwenye nyumba za ibada inaitwa saka

    Ikiwa kwenye vyombo vya usafiri inaitwa nauli

    Ikiwa shuleni kwenye vombo vya kisheria inaitwa dhamana.

    Ikiwa chuoni inaitwa bumu

    Ikitoka kwa mfadhili inaitwa msaada

    Majina mengine ya pesa ni kodi, bili, ushuru, miamala, n.k

    Huku mtaanii kwetu wanaiita maokoto, mkwanja, mshiko, mapesa n.k.

    Pesa ina majina mengi kutokana na matumizi yake mengi. Pesa ni moja ya kitu ambacho inatumika kwa wingi kuliko kitu kingine chochote. Hapa duniani pesa ni ya pili kwa umuhimu, ukiachana na oksjjeni, pesa ndiyo inafuata kwa kuwa na mtumzi mengi na makubwa.

    Hivyo ni wazi kuwa kitu ambacho kina matumizi mengi lazima tu kiwe na maneno mengi kulingana na watu ambavyo wanaona kwamba wanaona kinafaa. 

    Ni jina gani la pesa wewe unapenda kutumia?

    SOMA ZAIDI: Pesa ni nini?

  • Elimu Ambayo Haifundishwi Shuleni (part 1)

    Tangu ukiwa mtoto unaambiwa kwamba nenda Shuleni, usome Kwa bidii Ili Uje Upate ajira. Umependa Shuleni, umesoma Kwa bidii SI ndio?

    Hongera sana. Leo nipo hapa kukwambia mbali na hayo yote tuliyojifunza Shuleni, Bado Kuna mambo ya msingi sana kwenye maisha ambayo hukufundishwa, na mambo Haya ni ya msingi mno, kiasi kwamba haupaswi kuyapuuza. Yajue uyatumie Kwa manufaa yakuinue, au Yapuuze uendelee kubaki hivyohivyo na pengine kurudi chini zaidi

    Katika video ya leo nimeeleza juu elimu isiyofundishwa Shuleni, ikiwa ni sehemu ya kwanza kabisa.

    Ifuatilie vizuri. Usisahau KUWEKA maoni Yako Ili tuweze kuendelea mbele kuandaa sehemu ya pili ya video hii

    Masomo mengine muhimu: Hii nidyo sababu kuu kwa nini unapaswa kuhudhuria semina ya kuongeza kipato chako mara mbili mwaka huu

     

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana na +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Hivi Ndivyo Vitu Ambavyo Vinakukwamisha Wewe Na Nini Cha Kufanya

    UNAENDELEAJE RAFIKI YANGU WA UKWELI, Karibu Tena kwenye blogu yetu kwa ajili ya mafunzo mengine mazuri ambayo nimeandaa kwa ajili yako. Siku ya leo  nina ujumbe mfupi tu kwa ajili yako. na ujumbe huu siyo mwingine bali ninataka kukwambia kuwa;

    Asilimia kubwa ya vitu ambvyo vinakuzuia wewe kufanikiwa ni vitu ambavyo viko ndani ya uwezo wako. Ukiweza kuvuka hivi vikwazo ambavyo vipo ndani ya uwezo wako. Utaweza kufanya makubwa sana.

    Vikwazo hivi ambavyo vipo ndani ya uwezo wako ni pamoja na

    1. Uzembe. Ukiachana na uzembe na kuchapa kazi, utaweza kufanikisha makubwa
    2. Kutokuwa na ratiba. Hiki ni kitu kingine ambacho ndani ya uwezo wako. Ukianza kuipangilia ratiba yako, itakusaidia sana kufanya makubwa bila kusukumwa na mtu yeyote. Ratiba yako inapaswa kuwa imebana muda wote, kiasi kwamba upatikanaji wako uwe ni mgumu mara zote.
    3. Kutokufanya maamuzi. Muda mwingine kutokufanya maamuzi kunakukwamisha sana wewe kupiga hatua. Inawezekana ni kuchelewa kufanya maamuzi, au kutofanya maamuzi kabisa. Unachotakiwa kufahamu ni kuwa maamuzi ni sehemu ya maisha yako. hakuna namna ambavyo unaenda kuyaepuka. Kitu kikubwa ni kwamba unapaswa kuyafanya kwenye maisha yako ya kila siku. Usiogope kufanya maamuzi hata kama muda mwingine yanakuogopesha.
    4. Kutaka kufanya kila kitu mwenyewe. Hiki ni kitu kingine ambacho kinakwamisha watu wengi. Ukweli ni kuwa huwezi kufanya kila kitu mwenyewe. Ni lazima uwe tayari baadhi ya vitu vingine kuwapa wengine wafanye. Maisha ni kusaidiana, ukitaka kupambana na kila kitu, ukweli ni kuwa hutaaweza. na kama utaweza basi itakuwa ni kwenye ngazi za chini kabisa. Unachohitaji wewe kufanya vitu katika ngazi za juu, na ili uweze kufanya vitu katika ngazi hizi za juu, unahitaji watu. Usemi wa kiafrika unasema kwamba ukitaka, kufika haraka tembea peke yako, ila ukitaka kufika mbali, nenda na watu. Sasa swali langu kwako ni je, unataka kwenda haraka au unataka kufika mbali?
    5. Kutokufanya kazi kwa viwango vikubwa. Hiki ni kitu kingine ambacho kipo ndani ya uwezo wako.

    Ukweli ni kuwa kazi yoyoote ile ambayo wewe unashika, unapaswa kuifanya kwa viwango vikubwa kiasi kwamba uwashangaze watu watu watakaoshika kazi hiiyo. Je, umekuwa unafanya hivi. Au watu wamekuwa wanashika kazi hiyo na kuona kwamba wewe unashangaza kwa kutofanya kazi kwa ubora. Kama ni hivyo, basi unapaswa kurekebisha ambacho umekuwa unafanya, ili uweze kufanya kazi zako kwa viwango vikubwa na vya hali ya juu.

    Rafiki yangu Hivyo Ndivyo Vitu Ambavyo Vinakukwamisha Wewe Na hizo ndizo hatua unazopaswa kuchukua. na hatua hizi unapaswa kuzichukua leo hii.

    Nakutakia siku njema.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Unaweza kujifunza zaidi kwa kufuatilia makala za Godius Rweyongeza kwenye youtube channel yake ambayo unaweza kuipata kwa kubonyeza hapa

    mafunzo mengine zaidi huwa anayotoa kupitia email. unaweza kujaza taarifa zako hapa ili mmoja wa wale ambao wananufaika na mafunzo yake kwa email

    Kila la kheri

    Godius Rweyongeza

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Mambo 15 ambayo Godius Rweyongeza anashauri Uanze Kuyafanyia kazi Mara Moja

    Habari ya Leo. Hongera sana Kwa siku hii nyingine njema sana

    1. Tuitumie Leo kufanya makubwa. Kila mmoja Kwa jukumu lake analopaswa kufanya, alifanye Kwa weredi mkubwa

    2. Mabadiliko Unayotaka kuyaona Anza kuyasababisha mwenyewe siku ya Leo Kwa kufanya jambo lolote hata kama ni Dogo.

    3. Ukitimiza wajibu wako na Kila mmoja akatimiza wajibu wake, hii dunia Itakuwa sehemu nzuri sana kuishia.

    4. Vitu vingi ambavyo vitakupa MAFANIKIO MAKUBWA vinahitaji uvifanye Kwa kurudia rudia mara Kwa mara. Uwekeze mara Kwa mara, ujifinze mara Kwa mara, uongeze kipato chako mara Kwa mara n.k

    5. Usiischoke safari ya KUELEKEA malengo na ndoto zako kubwa. Endelea kupambania Kila siku.

    6. Ukweli ni kuwa usipofanyia kazi NDOTO ZAKO hakuna mtu atazifanyia kazi Kwa niaba Yako

    7. Muda Mzuri Wa kupanda mti ulikuwa ni miaka 20 iliyopita, ila muda mwingine Mzuri zaidi ni Sasa

    8. Kama Kuna jambo linakukwamisha, jifunze Hilo jambo kupitia usomaji wa vitabu.

    9. Mara zote kuwa unasoma kitabu.

    10. Kama hauna ndoto kubwa sahau kuishia maisha yenye mafanikio makubwa

    11. Fikiri Kwa ukubwa

    12. Jihusishe na watu chanya

    13. Pangilia siku Yako Kila siku

    14. Anzisha biashara 2024.

    15. Shukuru Kwa mambo mazuri mengi uliyonayo. Familia, wazazi, watoto, mwenza, afya njema kuiona siku ya Leo ……

    SOMA ZAIDI: 

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu.

    Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea.

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Kwa Nini tunahitaji HAMASA Kila siku

    Siku Moja Zig Ziglar alikuwa anaongea mbele ya umati, ndipo kijana. Mmoja akasimama na kumuuliza swali gumu Kwa kusema, Kwa Nini hizi HAMASA Huwa hazidumu?

    ZigZiglar alimjibu Kwa kusema kwamba HAMASA ni kama kuoga. Hauogo TU mara Moja na kuacha, Bali unaoga Kila siku, kwako Kila siku, inakuwa ni sehemu ya kuoga.

    HAMASA ni kama kuoga tunaigitaji Kila siku, hakuna siku ambayo mtu utasema kwamba nimeacha kuoga kwa sababu nimeshaoga sana. Kila siku ni nafasi nyingine ya kuoga, kama ulivyooga jana. 

    Hapa chini kuna sababu kumi kwa nini tunahitaji kuwa na motisha kila siku:

    1. Kuendeleza Utendaji: Motisha inatusukuma kufanya kazi kwa bidii na ufanisi zaidi katika shughuli zetu za kila siku. Bila motisha, utakwama na utajikuta kwamba huwezi kufanya chochote.

    Soma Zaidi: Vitu Vitatu (03) Vitakavyoongeza Ufanisi Kazini Kwako

    2. Kuwajibika: Motisha inatusaidia kuwa na uwajibikaji kwa malengo yetu na kufanya maamuzi sahihi katika kufikia mafanikio.

    Soma zaidi: Kitabu: How to Win Friends and Influence People

    3. Kukabili Changamoto: Motisha inatupa nguvu ya kukabiliana na changamoto mbalimbali tunazokutana nazo katika maisha.

    Soma zaidi: NYUMA YA USHINDI

    4. Kuweka Lengo: Motisha inatusaidia kuweka malengo na kufanya jitihada za kufikia malengo hayo kila siku. Kumbuka Kila siku ni siku inayohitaji motisha na HAMASA, bila hili kwenye malengo Yako hutoboi.

    Soma zaidi:NGUVU YA KUWEKA MALENGO

    5. Kuendelea Kujifunza: Motisha inatuchochea kutafuta maarifa zaidi na kuendelea kujifunza ili kukuza ujuzi wetu. Kumbuka maarifa ni Muhimu hasa kama tunataka kupata MAFANIKIO MAKUBWA. Bila kuendelea kujifunza utajikuta kwamba umepitwa na vitu vingi.

    Soma zaidi: Mambo 5 ya kujifunza kutoka Kwa Wajasiriamali Wenye Mafanikio

    6. Kuboresha Uhusiano: Motisha inaweza kuboresha uhusiano wetu na wengine kwa kutupatia nguvu ya kufanya mazungumzo na kushirikiana.

    7.  Kudumisha Mtazamo Chanya: Motisha inatusaidia kuwa na mtazamo chanya kuelekea maisha na kuvumilia changamoto zinazojitokeza.

    8. Kupunguza Stress: Motisha inaweza kupunguza viwango vya stress na wasiwasi kwa kutupa lengo na kusudi la kufanya kazi.

    9. Kuimarisha Afya: Motisha inaweza kuhamasisha mazoezi na mtindo bora wa maisha, hivyo kuchangia katika afya njema.

    10. Kufikia Mafanikio: Hatimaye, motisha inatuwezesha kufikia mafanikio na furaha katika maisha yetu kwa kutimiza malengo na ndoto zetu.

    SOMA ZAIDI: Audiobook Ya Kitabu Cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA Sasa Ipo Tayari

    Kiufupi ni kwamba tunahitaji motisha Kila siku Kwa sababu motisha inaambukizwa. Ni kama joto. Ukiwa na HAMASA na motisha Kila siku, unaweza kuwaambukiza na wengine ambao wamekuzunguka kuwa na HAMASA pia.

    Hivyo, kuwa na HAMASA rafiki yangu.

    Kila la kheri.

    Imeandaliwa na

    Godius Rweyongeza

    Unaweza kujifunza zaidi Kutoka Kwa GODIUS RWEYONGEZA

    Kupiti YouTube channel yake hapa

X