Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Jinsi Ya Kutengeneza Mshahara Nje Ya Mshahara

    JINSI YA KUTENGENEZA MSHAHARA NJE YA MSHAHARA


    ni kitabu kilichoandikwa na Godius Rweyongeza kinachoeleza namna mtu yeyote anavyoweza
    1. Kuongeza kipato chake Cha Sasa hivi
    2. Kufanya uwekezaji
    3. Kutengeneza KIPATO chenye hadhi ya MSHAHARA wake wa Sasa.
    Kinapatikana Kwa nakala ngumu na nakala laini.

    Wasiliana na +255 684 408 755 kupata nakala Yako sasa

  • Njia Tano (05) Za kuwa na Ukuaji Kwenye Maisha, Biashara na Kila kitu unachofanya

    Rafiki yangu, hongera sana kwa siku hii ya kipekee. Leo ni siku nyingine bora kwa ajili yako. Hakikisha kwamba unaitumia vyema siku ya leo. Na moja ya kitu muhimu sana ambacho unapaswa kukifanyia kazi kuanzia leo ni kukua.

    Ukuaji ni moja ya kitu muhimu sana hasa unapokuwa unataka kufanya makubwa. Unaanzia hapo hapo ulipo, unafanya yale unayoweza kufanya sasa hivi., lakini habari njema ni kwamba haupaswi kuendelea kubaki hapohapo. Unapaswa kuendelea kukua mara zote.

    Jichukulie wewe kama kampuni. Kama ungekuwa kampuni, watu wangekuwa wanahamasika kuwekeza kwenye kampuni hii (ambayo ni wewe) au wasingekuwa na hamu kabisa? Ni kitu gani kingewafanya wawe na hamu ya kuwekeza kwenye hii kampuni au kukosa hamu kabisa?

    Na swali tamu sana kuhusu hili ni kwamba je,. Wewe mwenyewe kama ungekuwa unawekeza kwenye kampuni ambayo ni wewe, ungewekeza kwenye wewe?

    Kama unaona kwamba kuna mapungufu, basi hayo mapungufu unapaswa kuyafanyia kazi kwa kuboresha zaidi. Ili uwe bora.

    Usikubali kuendelea kuwa pale kila siku.

    Kuhakikisha kwamba hauendelei kuwa hivyo hivyo kila siku, nimekuandalia vitu vitano muhimu sana ambavyo unapaswa kuzingatia ili kuwa na ukuaji kwenye hicho unacahofanya.

    Kitu cha kwanza ni kwa wewe kuhakikisha kwamba unakuwa mtu wa kujifunza kila siku. Mara zote jifunze, bila ya kuchoka. Kujifunza ni chanzo cha wewe kuendelea kuwa na maarifa mapya kila siku. Kama unataka kuwa na matokeo ya tofauti, endelea kujifunza kila siku, na hasa jifunze kupitia usomaji wa vitabu.

    SOMA ZAIDI: Ujumbe Muhimu Kwa Wasomaji Wote Wa Vitabu

    Kitu cha pili ni kwamba unapaswa kuboresha kile unachofanya. Mara zote boresha, maboresho haya yanaweza kutokana na namna unavyoona kwamba hiki kitu cha sasa kinafanyika, na sasa kinapaswa kuboreshwa zaidi. Lakini pia maboresho haya yanaweza kutokana na mrejesho ambao unaupokea kutoka kwa wateja. Kadiri unavyopokea mrejesho kutoka kwa wateja, boresha ili kupata mrejesho ambao ni bora zaidi ambao utakufanya ukue zaidi na zaidi.

    SOMA ZAIDI: AINA TATU ZA UJUZI UNAOHITAJI ILI KUONGEZA THAMANI YAKO NA KULA MEMA YA NCHI

    Tatu ni kufanyia kazi kile unachojifunza. Yaa, nakumbuka kwenye nambari moja nilikwamabia kwamba unapaswa kujijengea utaratibu wa kujifunza na hasa kwa kusoma vitabu, lakini kitu kingine muhimu sana ni kwamba unapaswa kufanyia kazi kile ambacho unajifunza kwa vitendo. Mara zote fanyia kazi kile unachojifunza. Ukichukua kitabu na kukisoma, kamwe, usibaki tu kuwaambia watu kuwa ulisoma hiki kitabu. Badala yake, soma hicho kitabu kwa lengo kwamba utapata kitu ambacho utafanyia kazi kwenye maisha yako au biashara yako. kitu hiki utakachopata kama utakifanyia kazi, ni wazi kuwa utakuwa una uwezo wa kukua na kutoka hapo ulipo na kwenda hatua ya ziada.

    SOMA ZAIDI: Kitu kimoja unachopaswa kufanyia Kazi kwa uhakika 2024

    Nne, penda na kuwa mtu wa kutumia teknollojia. Ukweli ni kuwa teknolojia mpya zinazidi kugunduliwa kil asiku. Na kadiri hizi teknolojia zinavyozidi kugunduliwa ndiyo kunakuwa na mabadiliko makubwa ambayo yanayokea. Ikumbatie teknolojia, na itumie teknolojia na hasa kwenye biashara yako.

    JIFUNZE ZAIDI: Jinsi Ya Kudandia Teknolojia Mpya

    Kitu cha tano na cha mwisho ambacho kitakufanya uwe na ukuaji kwenye maisha, kwenye biashara na kwenye maisha yako kiujumla ni kujifanyia tathmini. Tathmni ni moja ya kitu muhimu sana , ili kuona ni wapi umetokea, ni wapi umefikia na wapi unaelekea. Kwenye kila kitu ambacho unafanya, jifanyie tathmini. Tathmini ni muhimu kwa ukuaji wako. Hivyo mara zote jifanyie tathmini.

    Kama una mtoto utakuwa unajua wazi kuwa kila mwezi mtoto wako lazima apelekwe hospitali kwa ajili ya kliniki. Lengo la hii kiniki ni kujifanyia tathmini. Na lengo la tathmini hii ni kukusaidia kuboresha kile unachofanya, ili uweze kupata matokeo makubwa zaidi.

    SOMA ZAIDI: Kafanyaje huyu?

    kwa leo naishia hapo.

    Mimi naitwa Godius Rweyongeza

    Kwa mawasiliano zaidi: 0655848392

    Karibu sana

  • Huu Ndiyo Uwekezaji Bora Ambao Unapaswa Kuupa KIPAUMBELE sasa

    Hata kutunza familia ni uwekezaji. Ila uwekezaji baba ambao unapaswa kufanya mara zote ni

    1. KUWEKEZA KWENYE biashara. Huu ni uwekezaji Muhimu ambao Kila mmoja anapaswa kuufahamu. Sote tunamfahamu Warren kama mwekezaji Bora kuwahi kutokea, ila ukweli ni kuwa Warren Buffett siyo TU mwekezaji kwenye solo la HISA,Bali amewekeza kwenye biashara yake.


    Hivyo, WEKEZA kwenye biashara

    Anzisha biashara, endesha biashara Yako, KUZA BIASHARA Yako.

    Ukiwa na biashara unaweza kufanya karibia chochote unachotaka.

    Unaweza KUWEKEZA KWENYE biashara nyingine zaidi. Unaweza KUWEKEZA KWENYE soko la HISA n.k

    Hivyo, Anza KUWEKEZA KWENYE biashara kama ulikuwa hujaanza. Huku ukiendelea na mpango wako wa KUWEKEZA KWENYE soko la HISA na hasa Kwa kuanzia KUWEKEZA KWENYE VIPANDE

    Kama ungependa ushauri zaidi kuhusu uwekezaji.  Tafadhali wasiliana nami Kwa 0655848392

    Karibu sana

  • Huu ndio uwekezaji Bora kuliko wote

    Rafiki yangu, Kuna uwekezaji Bora kabisa kuliko uwekezaji wowote. Unajua uwekezaji huu ni upi?

    Ni KUWEKEZA KWENYE maarifa. Huu ndiyo uwekezaji Bora kabisa.

    WEKEZA kwenye maarifa mara zote

    WEKEZA kwenye maarifa.

    WEKEZA kwenye KUSOMA VITABU

    Hu ndiyo uwekezaji Bora kwako Kufanya.

  • Nimeandaa kozi fupi kwa ajili yako

    Rafiki yangu…………….

    Moja ya kitu ambacho ninapokea karibia kila siku, ni ombi la watu wakiniomba vitabu mbalimbali vya kiingereza. Wapo wanaoomba niwatafutie hivi vitabu kwa njia ya mtandao, halafu niwatumie.

    Sasa kitu kimoja ninachojua ni kwamba, nikipakua kitabu nikakutumia, ninakuwa sawa na mtu ambaye nimekupa samaki. Unajua ninaposema kwamba ninakuwa kama mtu ambaye nimekupa samaki ninamaanisha nini?

    Ili unielewe vizuri tuanze na usemi wa kihenga unaosema kwamba;

    Give a man a fish, and you feed him for a day; show him how to catch fish, and you feed him for a lifetime.

     

    Ikiwa inamaanisha kuwa;

    Mpe mtu samaki, nawe utamlisha kwa siku moja; mwonyeshe jinsi ya kuvua samaki, nawe unamlisha maisha yake yote.’

    Sasa mimi sitaki nikulishe kwa siku moja kwa kukupa samaki

    Nataka ujue kuvua..

    Siyo tu ujue kuvua, bali ujue kuvua na uwe na bwawa lako mwenyewe ambapo utaweza kuvua bila bughudha.

    Ndiyo maana, nimeamua kukuandalia kozi fupi tu, inayokuonesha namna ya kupakua vitabu mtandaoni.

    1. Ina njia ya uhakika
    2. Imetumiwa na watu zaidi elfu moja kwa mafanikio. Ukiitumia wewe pia utafanikiwa pia
    3. Ni rahisi kufanyia kazi.
    4. Ni njia ambayo utaitegemea kwa miaka yako mingi inayokuja. Nimekuwa naitumia kwa zaidi ya miaka sita sasa. Itumie kwa manufaa yako pia.

    Kupata njia hii na mengine zaidi. Utapayapata kupitia kozi hii fupi ambayo nimeandaa.

    Kujiounga na kozi hii fupi, utalipia kiwango cha shilingi elfu kumi tu. Na ukwlei ni kuw autaotoka kiasi kikubwa sana kwa kujiunga na kozi hii ya kipekee. Unachotakiwa kufanya sasa ni kujiunga na hii kozi.

    Lipia elfu kumi,

    Lipia kwa namba ya simu; 0684 408 755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    BONYEZA HAPA KUPATA KOZI

  • Kitu kimoja ambacho kimenishangaza

    Juzi nilijaribu kutuma hiki kitabu cha MAAJABU YA KUSOMA VITABU kwenye makundi ya whatsap. Cha kushangaza ni kwamba kuna watu hawajawahi kupata hiki kitabu. Walikisoma na wengi waliweza kupata mrejesho ambao ni chanya, namna ambavyo kimebadili maisha yao.

    Wengine walishakisoma, ila kitendo cha kurudia kukisoma juzi, kiliwapa hamasa kubwa kwa mara nyingine na kuwafanya wajisikie wapya.

    Nimeona kwamba inawezekana hata hapa, inawezekana kuna watu hawajahi kupata hich kitabu au wengine wameshakisona na wangependa kukipata kwa mara nyingine. Ndiyo maana nimeona kwamba nikutumie na wewe….

    KWA HIYO, kama wewe umeweza kusoma hiki kitabu, inawezekana ukakisoma tena, kitakufaa sana.

    Kama hujawahi kukisoma, sasa ni muda mzuri wa wewe kukisoma.

    BONYEZA HAPA KUKIPAKUA

    Ukiataka kupata vitabu zaidi: wasiliana na 0684408755

    Mimi ni Godius Rweyongeza

    Karibu sana.

    NB: Unaweza pia KUPATA VITABU VYANGU ONLINE HAPA

    au HAPA

    JIFUNZE ZAIDI KWENYE BLOGU KWA KUBONYEZA HAPA

    JIFUNZE ZAIDI KWENYE YOUTUBE CHANNEL KWA KUBONYEZA HAPA

  • Jinsi ya kupakua vitabu unavyopenda kwa njia ya mtandao.

    Karibia kila siku huwa napokea ujumbe wa mtu ambaye ananiambia kwamba angependa kupata kitabu fulani na hasa vitabu vya kiingereza.

    Inawezekana na wewe kuna kitabu ambacho umekuwa unatamani kupata kwa siku sasa, ila hujui namna ya kukipata. Karibu kwenye kozi hii fupi.

    Ambapo unaenda kujifunza namna ya kupakua kitabu chochote (online). Hii ni kwa vitabu vya kiingereza tu.
    Kwenye kozi nitakuonesha hatua kwa hatua namna ya kufanya hivyo.
    Nitakuonesha machimbo mbalimbali muhimu vilipo vitabu ambayo unaweza kuyatumia mwenyewe kutafuta na kupata vitabu unavyotaka kwa uhakika wa asilimia (95-99.999) bila kukosa!

    Kama upo tayari.

    Utalipia 10,000/- tu. Kisha nitakuunga kwenye hii kozi. Na utapata mafunzo haya.

    Hutatoa tena gharama yoyote kununua softcopy ya kiingereza.

    Kama upo tayari, lipia 10,000/-
    Namba ya malipo ni 0684 408 755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Lipia sasa ili upate hii kozi.

    AU

    BONYEZA HAPA KUPATA KOZI

  • Hiki ni kitu muhimu ambacho kitakusaidida kuendelea kuwa na wateja wa kudumu

    Rafiki yangu mpendwa, salaam, hongera sana kwa kazi. Siku ya leo nilitaka kukwambia njia moja ya uhakika na ambayo itakufanya wewe uendelee kuwa na wateja wa kudumu kwenye biashara yako. Njia hii siyo nyingine bali ni njia ni kuhakikisha kila wakati unakuwa na mfumo ambao utafuita wateja wapya, unafuatilia wateja wapya na unatoa mafunzo endelevu.

    Inawezekana kuna wateja ambao hawajui chochote kuhusu biashara yako, lakini kitendo cha kuwa wanapata mafunzo endelevu, ambapo wanapata kuelimishwa na kuambiwa vitu kadha wa kadha kuhusu biashara yako, kunawafanya waendelee kuifuatilia biashara yako kwa ukaribu. Na kunawajengea hamu ya kutaka kupata bidhaa zako.

    Unachotakiwa kufanya siku ya leo, ni kujiuliza ni njia gani ambazo ninaenda kutumia ili kuhakikisha kwamba ninakuwa na mfumo ambao unatafuta wateja kila mara, mfumo ambao unafuatilia wateja kila mara, kutoa mafunzo kwa wateja na kuwageuza mpaka kuwa wateja kamili?

    Ukishauweka huu mfumo. Ni wazi kuwa kila mara kutakuwa na mteja ambaye anataka kununua kutokana na mafunzo ambayo atakuwa amepata kutoka kwako.

    Karibu sana

    Imeandikwa na Godius Rweyongeza. 

    Kupata mafunzo zaidi, unaweza kujipatia nakala za vitabu vya Godius Rweyongeza. Wasiliana na Godius Rweyongeza kwa simu; 0684408755

    Kupata kozi na programu mbalimbali tulizonazo. Wasiliana nami kwa 0678848396

  • Vitu viwili Vitakavyokufanya uweze kupata matokeo makubwa Kwa uhakika

    Vitu viwili Vitakavyokufanya uweze kupata matokeo makubwa Kwa uhakika

    Rafiki yangu, Kuna vitu viwili vya uhakika vitakavyokupa matokeo makubwa mara zote. Vitu hivi ni kuhakikisha

    1. unaFIKIRI Kwa ukubwa mara zote. Kamwe kwenye maisha Yako usiwe na malengo madogo, usiwe na ndoto ndogondogo. Mara zote fikiri Kwa ukubwa, angalia ni Kwa namna gani unaweza kwenda zaidi ya hapo ulipo.

    SOMA ZAIDI: Unawezaje Kujiajiri kwa Mtaji Kidogo?

    3. Maarifa sahihi. Maarifa sahihi ni kiungo kingine Muhimu sana. Hakikisha kuwa Kila siku unasoma kitabu.

    Kila siku jifunze na kamwe usikome kujifunza.

    Soma zaidi: Mwongozo Sahihi Wa Kufikia Malengo Na Ndoto Zako

    Muhimu zaidi, yake unayojifunza, hakikisha kuwa unayafanyia kazi Kila siku. Na hakikisha pia umepata kitabu cha NGUVU YA KUFIKIRI KWA UKUBWA.

    Asante sana

    Uwe na wakati mwema. Kupata nakala na vitabu vya GODIUS RWEYONGEZA wasiliana na 0684408755

    Kupata huduma nyingine za Godius Rweyongeza 0678848396

  • JINSI YA KUEPUKA TABIA YA KUGHAIRISHA MAMBO -2

    Nilisemaje, mwezi huu; naam, mwezi huu nitakuwa naeleza kwa undani Zaidi kuhusu tabi aya kughairisha na namna ambavyo unaweza kuondokana tabia hii. Tayari niliandika Makala ya utangulizi siku ya juzi. Kama ulikuw abado hujasoma hii Makala, basi ni muda wako wa kuhakikisha kwamba umeisoma hapa.

    Sasa siku ya leo; ninaenda kukushirikisha nguvu ya kauli unazojiambia zilivyo na uwezo wa kukufanya uwe mtu wa kughairisha mambo au kukusaidia uepuke hilo. Wahenga wetu walikuwa  ni watu makini sana tokea enzi na enzi. Ndiyo maana walikuwa aksema kuwa maneno huumba. Na ukweli ni kuwa maneno yanaumba. Unachotakiwa kufanya ni kuyatumia maneno yako vizuri.

    Kwa hiyo, badala ya kujiambia kwamba nitafanya kesho.

    Badala ya kusema kwamba hili siwezi kulifanya, jiambie maneno na kauli chanya.

    Mfano unaweza kuwa umechoka; badala ya kusema kwamba nitfanya kesho. Unaweza kusema kwamba japo nimechoka, ngoja nianze kufanya kidogo.

    Maneno unayojiambia y anaumba. Badala ya kujiambia maneno hasi.

    Badala ya kusema kwamba leo hili haliwzekani kufanyika; sema kwamba  ninaenda kuanza kufanyia kazi lengo langu hata kama ni kidogo. Nitapata motisha Zaidi kaditi ambavyo nitakuwa nazidi kufanyia kazi lengo langu.

    Ni kwa namna gani kujiambia maneno hasi kumekuwa kunachangia kwako kwenye kushindwa kufanikisha mnalengo yako?

    Ni hatua gania ambazo unaenda kuchukua sasa hivi ili uondokane na hili?

    Soma sehemu ya kwanza hapa: NJIA ZA KUEPUKA KUGHAIRISHA MAMBO 2024

X