Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • JINSI YA KUANZISHA MAZUNGUMZO NA MTU YEYOTE

    Kuanzisha mazungumzo na mtu hasa yule ambaye hujawahi kuonana naye, huwa ni kitu kigumu miongoni mwa watu. Umewahi kukutana na mtu ukatamani kuongea naye, halafu ukawa unajiuliza utaanzaje, halafu mara kama mlikuwa kwenye basi, yule mtu anashuka nakuondoka na humwoni tena kwenye Maisha yako.

    Imewahi kunitokea. Nilikutana na mrembo mmoja kwenye basi, lakini sasa kimbembe kilikuwa ni kwa namna gani naweza kuanzisha mazungumzo na huyu mtu.

    Je, nimwamabie kwamba habari, lakni hiyo ingeonekana kama ni salaam ya kawaida. Je, nimwambia nakupenda, ingeonekana nimeenda haraka sana,

    Nataka uwe mama wa Watoto wangu, ingeonekana JAMBO LA KITOTO…

    Nikakaa kimya, muda ukaenda na baadaye basi likafika mwisho wa safari, akashuka na kuondoka, mpoaka leo hii sijawahi kumwona.

    Kitendo cha kuanzisha mazungumzo miongoni mwa watu ni kitu kigumu kidogo. Na leo hii nipo hapa kukupa mbinu za kukusaidia uweze kuanzisha mazungumzo na mtu yeyote, popote pale utakapokuwa duniani.

    Unafunguaje mazungumzo na mtu mwingine

    Kitu kikubwa ambacho huwa kinawakwamisha watu kuanzisha mazungumzo na mtu mwingine ni namna ya kuanzisha hayo mazungumzo. Hivi kwa mfano, mtu unaanza kumwambiaje, unaongea naye kitu gani cha kufungua mazungumzo.

    Hapa kuna vitu vitatu ambavyo unaweza kutumia kwenye kufuyngua mazungumzo na mtu yeyote.

    Kwanza unaweza kumwonglea huyo mtu

    Pili unaweza kuongelea kuhusiana na hali ya wakati huo

    Na tatu unaweza kuongelea kuhusiana nan a wewe mwenywee

    Unaweza kuanzisha mazungumzo kwa kuuliza swali. Kwa kutoa wazo lako au unaweza kuongelea kuhusu jambo Fulani ambalo ni ukweli

    Unapoanza kuzungumza na mhusika, lengo la kwanza kabisa linakuwa ni kumfanya huyo mtu aoneshe nia ya kuzungumza na wewe. Kumbe mara nyingi njia bora ya kuanzisha mazungumzo ni kwa kuuliza swali ambalo anatakiwa kujibu. Ni njia nzuri ya kuanzisha mazungumzo.

    Njia nyingine ya kuanzisha mazungumzo ni kwa kuongelea jambo kuhusiana na hali inayoendelea. Kwa mfano, kama mpo kwenye darasa moja unaweza kuanza kwa kuuliza swali kama; unafikiri ni kitu gani kitakuwepo kwenye mtihani leo..

    Au kama mnaenda kwenye usaili; unaweza kuanzisha mazungumzo kwa kumwuliza mtu unafikiri ni kitu gani ambacho wasaili watakuwa wanahitaji kutoka kwetu? Au unafikiri ni maswali gani ambayo yataulizwa..

    Kama mmekutana kwenye mechi; unaweza kuanzisha mazungumzo kwa kumwuliza mwenzako kuwa ni unafikiri nani atashinda hii mechi?

    Kama mpo sokoni, unaweza kuanza kwa kumwuliza mhusika; naona unanunua nazi; nimekuw anatamani kwa siku nyingi kujua namna ambavyo inapikwa. Unaweza kunipa maelekezo kidogo tafadhali,

    Kama ni jirani yako, unaweza hata kuanza kumwambia kuwa naona bustani yako ni ya kijani, nini siri ya kuwa na bustani nzuri kama hii?

    Kama nilivyosema mwanzoni. Njia nyingine ya kuanzisha mazungumzo na mtu yeyote ni kwa kuanza kuzungumzia kuhusu huyo mtu. Kwa mfano;

    Mtu ambaye amevaa jaketi, unaweza kuanza kwa kumwambia hivi, waoo hongera naona una jaketi zuri kweli, unaweza kunieleza kidogo kuhusu hiyo alama kwenye jaketi inamaanisha nini?

    Au labda mmetoka kwenye kikao. Unaweza kuanzisha mazungumzo na mtu kwa kumwambia, yaani umetoa maoni bora kabisa siku ya leo ebu niambie kwa nini…..

    Nadhani wengi wanaogopa kuanzisha mazungumzo na polisi au wanajeshi. Unaweza kuanzisha mazungumzo  kwa kumuuliza. Ningependa kujiunga n jeshi la polisi, ni vitu gania mbavyo natakiwa kuzingatia?

    Kama mko kwenye sherehe, unaweza kuanzisha mazungumzo kwa kumuuliza mhusika; ni kwa namna gani umefika hapa, yupi ni ndugu yako, bwana harusi au bibi harusi

    Kama po mgahwani, unaweza kuanzisha mazungumzo kwa kumwabia mtu kuwa naweza kuungana na wewe kwenye meza tupate chakula kwa pamoja.

    Njia ya mwisho kabisa ya kuanzisha mazungumzo ni ya kujiongelea mwenywewe. Ila hii siyo njia bora Zaidi. Maana watu huwa hawapendi watu wanaojiongelea wao wenyewe. Kumbuka kama ambavyo Dale Carnegie anasaema; unapaswa kuonesha kuwajali wengine kuliko unavyojijali wewe mwenywew. Hivyo, unapojiongelea mwenyewe maana yake unakuwa hujaonesha kujali maslahi yao.

    Njia bora ya kuanzisha mazungumzo kwa kujiuzungumzia mwenyewe ni kuanza kwa kujitambiulisha. Jitambulishe hivi.

    Habari, kwa majina naitwa……………….(JINA LAKO)……………..na wewe jina lako ni……………………………………………….

    Hizo ndizo njia unazoweka kutumia kwenye kaunzisha mazungumzo na watu wentgine. Ni njia pi bora kwako ambayo unaenda kutumia siku ya leo. Ebu niambie ni pi ambayo umependa Zaidi.

    Ni ipi ambayo unaenda kuitumia…

    Ni ipi ambayo huwa unaitumia…..

    Tuwekee maoni hapa chini….

    Mimi ni Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro-Tz

  • Hii Ndiyo Sababu KwA Nini Watu Wengi Huwa Hawaweki Malengo

    Habari ya leo rafiki yangu wa ukweli. Hongera sana kwa siku nyingine njema sana rafiki yangu. Siku ya  leo nikwambie moja ya sababu kubwa kwa nini watu wengi huwa hawaweki malengo.

    Unajua kwa nini watu wengi huwa hawaweki malengo? Kuna sababu nyingi sana ila hizi ndizo zinawafanya watu wengi wasiweke malengo.

    Ya kwanza ni kwa sababu ya uoga; wengi wana uoga linapokuja suala zima la kuweka malengo. Mtu anaanza kufikiria kwamba nikiwe malengo, na nisipoyatimiza itakuwaje? Hiki kitu kinamfanya mtu aogope.

    SOMA ZAIDI: Uoga wako ndio umasikini wako

    Sasababu ya pili inayowafanya watu washindwe kuweka malengo ni kwa sababu hawajui namna ya kuweka malengo. Hiki ni kitiu kingine kikubwa kinachowakwamisha watu na hivyo kujikuta kuwa wanaishi maisha yao yote bila ya kuwa na malengo.

    sababu ya ta tatu ni kwa sababu wanajiona hawastahili kupata hivyo vitu vizuri. Ukijiona kwamba hustahili kuwa na hiyo nyumba nzuri. Husatahil kuwa na hilo gari zuri. Hustahili kuwa na huyo mchumba n.k. huwezi kuwa naye. Kitu chochote kile ambacho wewe mwenyewe unaona kwamba huwezi kufanikisha kwenye maisha yako, ni ukweli kuwa hutakaa ukifanikishe

    SOMA ZAIDI: Unafunga Sehemu Gani?

    Kwa hiyo, kinachotakiwa sasa hivi ni wewe kubadili mtazamo wako kwanza kwa kuhakikishakwamba unaondoa uoga, pili kaa chini ujifunze namna ya kuweka malengo. Kisha weka malengo hayo. Na mwishao jua kuwa unastahili kupata mazuri ambayo dunia inatoa. Unastahili kuwa na afya bora, hiyo nyumba nzuri ni stahiki yako, watoto wazuri, wenye tabia yako ni haki yako. 

    sasa kwa kuwa unastahili kupata hivi vitu anza kuvifanyia kazi. Anza kuvifanyia kazi ili uweze kuvifikia.

    Hizo ndizo sababu tatu ambazo zinawafanya watu wengi wasiweke malengo. Nimeona nikushirikishe hizi sababu, ni imani yangu kuwa unaenda kuzifanyia kazi na kuepuka zisikukwamishe. kama kuna watu wawili ambao unawafahamu wanaoweza kunufakika na hii makala, tafadhali watumia hii makala ili nao waweze kuisoma. Kama una makundi mawili ya whatsap ambapo unaweza kutuma hii makala, itume, nina uhakika kuna watu wawili ambao watanufaika..

    Uwe na wakati mwema.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza. Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza wasiliana naye kwa kupiga simu +25568408755

  • Vitu 13 ambavyo hakuna mtu anaweza kufanya Kwa niaba Yako

    Kuna vitu ambavyo unaweza ukawapa watu wengine wavifanye kwenye Maisha yako, lakini pia kuna vitu ambavyo huwezi kuwapa watu wengine wavifanye kwa niaba yako. Ni lazima uingie ulingoni na uvifanye mwenyewe.

    Watu wengi wamekuwa wanakosea hasa kwenye hili kwa kuacha kufanyia kazi vile vitu ambavyo wao wanapaswa kufanyia kazi, wanasubiri watu wengine waje wavifanyie kazi wakati hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kufanya hivyo vitu kwa niaba yao. Ukweli ni kuwa kuna vitu ambavyo unaweza kuwapa wengine, lakini wakati huohuo ni ukweli kuwa kuna vitu vingine ambavyo huwezi kuwapa wengine wavifanye kwa niaba yako. Hivyo unapaswa kuvifanya mwenyewe.

    Lengo la Makala hii ni kukuonesha wapi haswa kwenye Maisha yako unapaswa kuweka nguvu, huku ukijua wazi kuwa hakutakuwa na mtu yeyote ambaye ataweza kufanya hivyo vitu kwa niaba yako. Badala yake utapaswa kuhakikisha kwamba unavifanya hivyo vitu mwenyewe bila ya kusubiri mtu yeyote ambaye unaweza kuwa unamtegemea aweze kukusaidia wewe kwenye kuvifanyia kazi hivyo vitu ambavyo wewe mwenyewe unafikiria kwamba unaweza kufanyiwa.

    Sasa vifuatavyo ni vitu ambavyo huwezi kufanyiw ana mtu yeyote. Ni sharti uingie ulingoini uvifanye mwen ywe. Ni kama

    1. Kujiamini wewe mwenyewe

    Hakuna mtu ambaye anaweza kujiamini kwa niaba yako. Kujiamini ni jukumu lako, ni lazima mara zote uhakikishe kwamba unaonesha ujasiri na kujiamjni hata kama unapitia katika hali ngumu. Ukweli ni kuwa hata kama unapitia kwenye hali ngumu, kuna watu wengine ambao wanakuwa wanapitia kwenye hali ngumu zaidi yako. Hivyo, hakikisha kwamba mara zote jiamini, maana hiki kitu hakuna mtu ambaye ataweza kukifanya kwa niaba yako.


    1. Kuwapenda wazazi wako

    Kama una wazazi; hakuna mtu ambaye atakusaidia kuwapenda wazazi wako kwa niaba yako. Ni jukumu lako; wapende wazazi wako.


    1. Kumpenda mwenza wako

    Kama ilivyo kwa wazazi wako, mwenza wako pia hakuna ambaye anaweza kukusaidia kumpenda. Akikusaidia mwingine kumpenda, anakuwa amekusaidia kweli, hahah. Mpende na hakikisha analijua hilo. Mwambie hivyo mara kwa mara.


    1. Kufanya mazoezi

    Hakuna mtu anaweza kufanya mazoezi kwa niaba yako. Yaani, kwamba mtu akimbie kilomita moja kwa niaba yako. Hakuna kitu kama hicho, hili ni jambo ambalo wewe mwenyewe unapaswa kulifanya kwa uhakika. Hivyo, badala ya kusubiri mtu aje akufanyie kmazoezi; anza wewe kufanya mazoezi. Hata kama ni kwa dakika tano tu.


    1. Kula vizuri

    Kama ilivyo kwa mazoezi; hakuna mtu ambaye anaweza kula vizuri kwa niaba yako. Ni lazima uwe tayari kula vizuri kwa ajili ya afya yako mwenyewe.


    1. KUWEKA AKIBA NA KUWEKEZA

    Hakuna mtu ambaye anaweza kuwekeza fedha kwa niaba yako. Ukibahatika Rafiki yako atakupa zawadi ya kiasi kidogo cha fedha au atampa mwanao zawadi ya uwekezaji kwenye hisa au UTT ila kama unataka kujenga utajiri na uhuru wa kifedha, basi wewe unapaswa kuwa tayari kulifanya mwenyewe hili. Hiki kikombe hakikuepuki. Unapaswa kuwa tayari kunywa maji yake.


    1. Kujifunza na hasa kusoma vitabu

    Kama ilivyo kweli kuwa hakuna mtu anayeweza kwenda chuo kikuu kusoma kwa niaba yako; hivyo hivyo hakuna mtu ambaye anaweza kusoma kitab una kupata maarifa kwa ajili yako. Hii ngoma inakuhusu. Ni sharti ufanye mwenyewe.


    1. Kuanzisha biashara

    Una wazo la biashara? Sasa unataka nani alifanyei kazi kama siyo wewe. Hakuna mtu ambaye anaweza kuanzisha biashara kwa niaba yako. Ni sharti uanzishe biashara mwenyewe.


    1. Kuwapenda na kuwajali wanao

    Kama ilivyo kwa wazazi. Kama ilivyo kwa mwenza wako. Hivyohivyo kwa wanao. Hakuna mtu ambaye anaweza kuwapenda wanao kwa niaba yako


    1. Kupangilia ratiba yako

    Ratiba yako ya kila siku, ratiba yako ya wiki, ratiba yako ya mwezi, hakuna mtu ambaye anaweza kuipanga kwa niaba yako. Wewe ndiye unapaswa kuipanga na kuwa makini na ratiba yako ili uweze kuifuata kwa ufanisi ili uweze kupata matokeo makubwa.


    1. Kusamehe

    Hiki ni kitu kingine ambacho hakuna mtu anaweza kufanya kwa niaba yako. Samehe SONGAMBELE


    1. KUFANYIA KAZI NDOTO ZAKO.

    Kila mtu ana NDOTO zake. NDOTO za jirani Yako siyo za kwako. Ni kweli unaweza kuajiri watu, lakini Kuna nafasi Yako wewe kama wewe…unapaswa kuwaonesha wapi unaelekea na kuwapa mwongozo sahihi wa kufuata. Huwezi TU kubweteka na kumsubiri mtu akufanyie kazi NDOTO ZAKO. Kama angekuwa anajua SI angefanyia TU kazi NDOTO ya kwake.
    Unahitaji umpe mwongoZO

    Rafiki yangu, hivyo ni baadhi ya vitu ambavyo hakuna mtu anaweza kufanya kwa niaba yako. Nimeona ni vyema nikudokeze hivi vitu ili uepuke kuingia kwenye mtego wa kukaa kusubiri mtu avifanye kwa niaba yako.

    Huu ujumbe naomba uwafikie watu wote ambao wanakaa na kuilaamikia serikali kuwa haijawafanyia kitu Fulani. Ujumbe huu uwafikie wote wanaolalamika kuwa wazazi hawakuwasomesha. Japo una pointi nzuri kuwa wazazi wako hawakukusomesha, ila sasa wakati wa kupambania Maisha yako ni sasa. Hilo limeshapita, unachopaswa kufanya ni kuweka malengo na kuanza kuyafanyia kazi. Hakuna mtu ambaye anaenda kuyafanyia kazi haya malengo kwa niaba yako.

    Nadhani orodha hii ni ndefu, naomba mimi niishie.

    Kama unamfahamu mtu ambaye huu ujumbe unamhusu, ebu mtumie huu ujumbe aweze kuusoma

    Mwambie Godius Rweyongeza nampenda sana kutoka hapa mji kasoro pwani Morogoro mjini

    Kwa mawasiliano Zaidi godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Nipo kwenye mitandao ya kijamii

    Nipo kwenye mitandao ya kijamii

    kwa siku sasa, nilikuwa nimesitisha kuitumia mitandao ya kijamii yote isipokuwa mtandao wa whatsap na telegram. Ila kwamwaka huu ninaenda kuwa tena kwenye mitandao hii ya kijamii. Nitakuwa ninatoa mafunzo kwenye hii mitandao kama ambavyo nilikuwa nafanya mwanzoni

    ila maeneo yangu ya nguvu ambayo huwa natoa mafunzo, yataendelea kuwa yaleyale. kabla sijakwambia unaweza kunipataje kwenye mitandao hii ya kijamii, naomba ufahamu maeneo matatu ambayo ni lazima utapata mafunzo kutoka kwangu.

    Eneo la kwanza ni blog ya songa mbele (https://songambele.co.tz/)

    Eneo la pili ni YouTube channel yangu ambapo unaweza kuitembelea hapa (https://www.youtube.com/godiusrweyongeza)

    Eneo la tatu ni email, huku pia natoa mafunzo Kwa njia ya baruapepe Kila siku; kama Bado hijajiungabna mfumo wetu wa kupokea mafunzo Haya bonyeza hapa ((https://songambele.co.tz/zawadi)

    Sasa ukiachana na Hilo,mwaka huu kwenye mitandao yote kijamii nitakuwepo. Jiunge Mami kwenye hii mitandao. Kujiunga nami ni rahisi sana

    TikTok: https://www.tiktok.com/@godiusrweyongeza
    Instagram: https://www.instagram.com/godius_rweyongeza/
    Facebook: https://www.facebook.com/songambeletz
    Na songambele https://www.facebook.com/songambeleblog
    Twitter: https://twitter.com/godiusrweyongez

    Linkeldn: https://tz.linkedin.com/in/godius-rweyongeza

    Mwaka huu Mimi Kwa kushirikiana na timu yangu tunaenda KUWEKA mafunzo Kila siku. Kwenye hii mitandao. Ila hata hivyo nipende kukutaarifu kuwa endapo utakosa mafunzo kwenye hii mitandao ya kijamii

    Hutayakosa kwenye email, kwenye blogu na YouTube

    Endelea kuwa karibu nami

    Godius Rweyongeza
    +255678848396
    Morogoro-Tz

  • Hakuna kitakachobadilika kama wewe hutabadilika

    Hakuna kitakachobadilika, kama wewe hujabadilika.

    Kitu chochote unachotaka kibadilike, Anza wewe kukifanyia kazi.

    Kama mahusiano Yako unataka yabadilike Anza kuyafanyia kazi

    Kama ni Hali Yako ya kipato , chukua hatua, Anza kulifanyia kazi Hilo. Na pengine unaweza kuanza na programu yetu ya mafunzo ya kuongeza kipato mara mbili; ambayo unaweza kuyapata hapa

    Ebu labda nikiuulize, ni ni kitu gani ambacho ungepend kuona kinabadilika kwenye maisha yako. je, ni kwa namna gani upo tayari kulipa gharama kwa wajili yakufanjikisha hicho kitu.

    Na kumbuka kwamba kulipa gharama iyo kunatofautisha kati ya watu ambao huwa wanafanikisha malengo yao na wale ambao huwa wanaishi tu kuwa na matamanio juuu ya melengo, huku wakiwa hawachukui hatu yoyote.

    Badala tu ya kuishia kutamani kwamba ungeweza kufanya mabadiliko. sababisha mabadiliko kwelikweli bila ya kurudi nyuma.

    Uwe na wakati mwema

  • Usiogope kukosea

    Vitu vingi ambavyo huwa tunafanya kwenye maisha huwa vinahusisha makosa. Ni vigumu kuanza kufanya kitu kwa ufanisi wa asilimia 100 hasa unapofanya mara ya kwanza.

    Mtoto anapoanza kutembea, haanzi kutembea huku akiwa anatembea kwa usahihi asilimia 100. Anaanza kwa kuanguka, ila ni kupitia huku kuanguka ndiyo baadaye anaweza kutembea vizuri bila wasiwawasi wowote. Baadaye tunakuja kumwona huyo mtoto akikimbia mbio za marathon n.k

    Unaikumbuka siku yako ya kwanza kazini?

    Mara nyingi siku ya kwanza ya kufanya kitu huwa siyo bora sana. Ila kadiri unavyokuwa unafanya ndivyo unakuwa unazidi kuwa bora zaidi.

    Huwezi kusema kwamba mimi nasubiri kuw amkamilifu ili nianze. Hakuna kitu ambacho huw akinaanz akikiw ana ukamilifu wa asilimia 100.

    Simu za kwanza hazikuwa kamilifu.

    Ndege za kwanza hazikuwa kamilifu.

    Ukamilifu kwenye hii dunia haupo. Ndiyo maana utagundua kwamba kompyuta huwa zinakuja katika matoleo. Kuna toleo la kwanza, kuna toleo la pili na kuendelea.

    Hii haimaanishi kwamba uanze kutoa kazi ambazo hazina ubora, badala yake kila kazi ambayo utaweka mkono wako, hakikisha kwamba ndiyo kazi bora kuliko zote kwa wakati huo. Kama badaye kutatokea kwamba kunahitajika marejekebisho, au kuna vitu unatakiwa kuboresha basi utaboresha.

    Lakini pia, unapotoa kazi yako, kuna watu wanatoa mapendekezo yao ya nana gani uweze kuboresha kazi yako. Ni vitu gani zaidi ambavyo unaweza kuongeza ili kuifanya kuwa bora zaidi. Haya maoni, haya siyo ya kupuuza. Yafanyie kazi. Boresha kazi na ifanye kuwa bora zaidi.

    Baada ya kusema hayo,naomba nikutakie kila la kheriii.

    SOMA ZAIDI: Usiogope Kuuliza

    Makala  hii imeandikwa name rafiki yako

    Godius Rweyongeza

    0755 848 391

    Morogoro-Tz

    Tuwasiliane kwa godiusrweyongeza1@gmail.com

  • NJIA ZA KUEPUKA KUGHAIRISHA MAMBO 2024

    Rafiki yangu mpendwa salaam, hongera sana kwa siku hii nyingine nzuri sana. Leo hii ni tarehe 1.2.2024. ni siku nyingine bora kabisa. Tayari mwezi mmoja umepita tangu tuuanze mwaka mpya wa 2024, kazi imebaki kwako sasa. Ni kwa namna gani mpaka sasa unaendelea kufanyia kazi malengo yako? Unajiona ukiwa unaelekea malengo yako au unakwama sehemu? Kumbuka, mwaka mpya siyo mwaka mpya tena, na usipoanya kitu, maana yake huu mwaka unaenda kuupoteza wote, bila ya kuwa umefanya kitu cha maana.

    Kwanza labda nikuulize, una malengo ambayo unayafanyia kazi? Ukweli ni kuwa kama hauna malengo, kuna kosa kubwa ambalo unafanya. Hakikisha kabisa unakaa chini na kuweka malengo yako sasa.

    Maandiko mengi ambayo niliandika ndani ya mwezi wa kwanza, yalikuwa yakielekeza namna ya kuweka malengo 2024, namna ya kuyafanyia kazi  hayo malengo na mpaka kuyafikia. Kama kwa bahati mbaya hukufuatila haya mafunzo, nashauri, utembelee blogu yangu ya SONGAMBELE (www.songambele.co.tz) ili uweze kujifunza zaidi kuhusu haya mambo yote ambayo nakwambia.

    Nakushauhri pia uweze kujipatia nakala ya kitabu cha NGUVU YA KUWEKA MALENGO. Kitabu hiki ni mwogozo wa kuweka malengo. Kama kwa bahati mbaya mpaka hivi tunavyoingia ndani ya mwezi wa pili, unaingia bila ya kuwa na malengo. Basi, jiwekee mkakati wa kuhakikisha kwamba unakuwa na malengo, mapema sana ndani ya huu mwezi. Malengo ndiyo ramani pekee ambayo itakuongoza, wewe kuelekea na kufikia kule ambapo unataka kufika. Ukweli ni kuwa huwezi kufanikisha mambo makubw kama hauna malengo.

    Sasa kwa kuwa tumeshaongelea sana kuhusu malengo, ndani ya huu mwezi wa pili tutakuwa tunaongelea zaidi kuhusu NAMNA GANI AMBAVYO UNAWEZA KUACHA TABIA YA KUGHAIRISHA MAMBO.

    Kwa hiyo, ninaenda kuchukulia kwamba tayari una malengo, kama hauna malengo. Pata huo mwongozo ambao nimekuelekeza uupate, ndani ya huu mwezi wa pili nataka uache tabia ya kughairisha malengo na miipango yako ambayo umeiweka kwa ajilil ya mwaka wako 2024. Unaachaje tabia hii tabia.

    Sasa tuambatane kila siku kwenye makala ambazo nitakushirikisha karibia kwa mwezi mzima bila ya kuacha.

    Kugharisha mambo ni kuacha kufanya jambo ambalo liko mbele yako kwa sasa kwa huku ukiwa unajiambia kwamba jambo hilohilo utalifanya kesho au siku nyingine. Na muda mwingine unaweza kuwa hujiambii kwamba hilo jambo utalifanya kesho au siku nyingine, lakini unaweza kuwa kwenye fikra zako unaamua kwamba unafanya jambo jingine ambalo kwa muda huo unaona kwamba linafaa wakati jambo hilohilo ambalo unafanya siyo la muhimu kwa wkaati huo.

    Mfano, jukumu lako kuu kwa wakati huo linaweza kuwa ni kutafuta na kuwafikia wateja kadhaa kwa wakati huo. Lakini ukajikuta kwamba unaacha kufanya hilo jukumu na badala yake unaenda  facebook au kwenye mtandao mwingine wa kijamii na kujikuta kwamba unapoteza muda wako wa thamani huko. Mwisho wa siku uttajikuta unajiambia kwamba hii ndiyo inaenda kuwa ni mara yangu ya mwisho kufanya hili, halafu kesho yake jambo kama hilo hilo linajirudia. Unajuikuta kwamba umerudi kwenye hali hiyohiyo.

    Sasa ili tuweze kuachana na tabia ya kughairisha mambo unapaswa kuanza na kuingalia thamani ya muda wkao.

    Muda wako ni wa thamani. Najua hili siyo mara yako ya kwanza kuliskikia. Siyo mara yako ya kwanza kusiikia kwamba muda ni mali. Siyo mara yako ya kwanza kusikia kwamba muda unapaswa kuwa unautumia vizuri. Sasa kwa kuwa unajua haya mambo, ninachotaka kukwambia ni kukueleza kwa undani zaidi ni kwa namna gani muda ni wa thamani..

    Hivi inakuwaje muda unasemwa kuwa na thamani kiasi hicho. Yaani, muda unakuwaje mali? Hili limeanzaje?

    Ngoja nikuelekeze vizuri ili uweze kunielewa.

    Mimi, wewe na mtu yeyote unayemfahamu leo hiii hapa duniani, na hata wale usiowafahamu, sote kwa siku moja tuna saa 24. Hakuna mtu yeyote Yule ambaye ana muda mwingi zaidi ya mwingine. Mpaka leo hii unaposoma hapa, hakuna kifaa chochote kile ambacho kimegunduliwa ambacho kinaweza muda wa mtu yeyote.

    Sekunde moja ambayo imepita sasa hivi, naam, hii sekunde, haitakaa irudi tena. Ikishapita ndiyo itakuwa imepita, ni juu yako sasa kuhakikisha kwamba kila sekunde inayokuja kwako unaitumia vyema kabisa.

    Moja ya kipengele muhimu sana linapokuja suala zima la muda ni kwmaba muda huwezi kuukopa, wala kuukopesha. Muda siyo kama fedha. Na ndiyo maana unaambiiwa kila siku kuwa unaweza kukopa fedha, lakini huwezi kukopa muda. Limekaaje hili, ngoja nikuoneshe hapa..

    Tuanze na dhana ya kukopa na kukopesha fedha. Leo hii ukiwa hauna fedha, unaweza kwenda benki yoyote ile na kuwaambia kuwa ungependa kukopa kiasi fulani cha fedha, halafu hiyo benki, watakuwa tayari kutoa fedha na kukupa. Lakini huwezi kwenda benki kukopa muda.

    Leo ikitokea kwamba una fedha nyingi, unaweza kuwakopa rafiki zako. Au unaweza kuwekeza hizo fedha sehemu yoyote ile ambayo unataka wewe. Lakini ukweli ni kuwa huwezi kukopesha muda wako kwa mtu. Akautumia muda wako halafu akaja kukurudishia muda wako baadaye.

    Ndiyo maana tunapoanza kuliangalia suala zima la kughairisha mambo tunapaswa kuanza kuliangalia suala la muda wako. Maana vitu vyote tunavyovifanya kuelekea malengo yetu, na vitu vyote ambavyo hatufanyi, yote hayo tunayafanya ndani ya muda tulionao.

    Sasa swali langu la kwanza kwako ni kuwa muda wako una thamani kiasi gani?

    Njia rahisi ya kutambua thamani ya muda wako nia kuangalia kipato ambacho unaingiza sasa hivi

    Kama kwa sasa hivi unaingiza kipato cha milioni  moja kwa mwezi. Maana yake thamani ya saa lako moja ni milioni moja kugawa kwa siku thelathini, kugawa kwa saa 24. Yaani, (1,000,000/30/24) tunapata kuwa thamani ya saa lako moja ni sawa na 1,388.88

    Huwa napenda kuipima thamani ya muda wako kwa kuangalia zaidi kile kipato ambacho ungependa kufikia ndani ya huu mwaka.

    Kama huu mwaka ungependa kipato chako kiwe ni milioni mbili. Maana yake ni kwamba milioni 2,000,000/30/24. Maana yake thamani ya ya muda wako ni 2,777.77

    Ila ngoja ni kwambie kitu, kama umepiga kwa kutumia hizi hesabu na bado thamani ya muda wako ni chini ya elfu tano, sikiliza, weka kiwango cha chini kabisa cha thamani ya saa lako moja kuwa elfu tano. Hiki ndicho kinapaswakuwa kiwango chako cha chni kabisa kwa mtu wa nguvu kama wewe ambaye unafuatilia mafunzo yangu kila mara, ni kiwango amabcho unapaswakuanza kukifnayia kazi.

    Hii ndiyo kusema kwamba haupaswi kufanya kitu chochote ambacho ni cha viwango cha chini ya elfu tano kwa saa yako moja.

    Kama kitu unachofanya ndani ya muda wako ni cha thamani ya chini. Yaani, thamani yake ni chini elfu tano kwa muda huo. Ujue kwamba unajiumiza.

    Kwa kulijua hili litakusaidia wewe kuweza kujali muda wako zaidi na kuwekeza muda wako kwenye maeneo ambayo yanazalisha matokeo makubwa zaidi kuliko eneo jingine.

    sasaa baada ya kujua thamani ya muda wako, maana yake hii itakuongezea hasira ya kujali zaidi muda wako kuliko mtu mwingine yeyote.

    Lakini pia hutakubali kufanya majukumu ambayo yapo chini ya viwango vyako

    Sasa mtu mmoja aliniuliza, kuwa kama thamani ya muda ni elfu tano kwa saa. Lakini kuna saa ambazo ninakuwa sipo kazini, ambao ni muda kaupumzika.

    Ngoja nikwambie kitu.

    Muda wako unapaswa kuwa na thamani bila ya kujali ndani ya huo muda unafanya kazi au hufanyi kazi.

    Muda wakowote unapaswa kuwa na thamani, ngoja nikuelekeze zaidi.

    Namna unavyotumia muda wako wa ziada, muda wako wa mapumziko, ndivyo ambavyo utaweza kutumia muda wako wa kazi. Kama muda wako wa mapumziko unalewa, kwa kisingizio kuwa ni muda wako wa mapumziko. Ni ukweli kuwa huwezi kuzalisha matokeo muda wa kazi ukifika na huwezi kuwa na ufanisi.

    Jambo  hili litapekelea wewe kuwa ufanisi kidogo na kuzalishaji kidogo muda wa kazi. Kumbe, kwa sababu hiyo, unapaswa kuheshimu muda ambao hufanyi kazi, kama ambavyo unaheshimu muda wako wa kufanya kazi. Unapaswa kuheshimu muda wako wa kulala kama amabvyo unaheshimu muda wako mwingine. Kwa sababu hivi vitu vyote vinaungana, namna unavyotumia muda wako mwingine wa mapumziko, ndivyo ambavyo utatumia muda wako wa kazi. Ukitumia muda wako wa ziada, muda wa kazi pia hutaweza kuzalisha matokeo mazuri na yanayoeleweka.

    Sasa kazi ambayounapaswa kufanya siku ya leo ni moja hasa tunapoanza kuliongelea zaidi suala zima la kughairisha mambo. Jua thamani ya muda wako. Kama bado hujui thamani ya muda wako, yaani ksa saa moja, weka kiwango cha chini kabisa kuwa elfu tano, unawez akuweka kiwango chochote kile cha juu, ila isiwe chini ya elfu tano.

    Je, wewe umeifahamu thamani yako ya muda?

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza; kupitia mtandao wake wa songambele (www.songambele.co.tz)

    Kwenye mitandao ya kijamii. Godius Rweyongeza apatikana kama Godius Rweyongeza.

  • Vitu vitano ambavyo hakuna mtu yeyote anaweza kufanya Kwa niaba Yako

    Vitu vitano ambavyo hakuna mtu yeyote anaweza kufanya Kwa niaba Yako

    1. Hakuna mtu anaweza kukuamini wewe kama unavyojiamini. Wewe ndiye mtu Unayopaswa kujiamini Kwa asilimia zote hata kama wengine hawakuamini. Jiamini. Mwenyewe kwanza

    Ukiendelea kujiamini Kwa muda mrefu, hata kama wengine walikuwa hawakuamini, watakuamini TU. Jiamini.

    1. Hakuna mtu anayeweza KUFANYIA KAZI MALENGO Yako Kwa niaba yako. MALENGO Yako, yafanyie kazi wewe mwenyewe Kwa maana hakuna mtu wa kukusaidia kwenye Hilo.
    2. Kuanzisha biashara.
      Kama umekuwa unajiambia kuwa utaanzisha biashara na hujafanya hivyo, fanya hivyo. Hakuna mtu atafanya hili Kwa niaba Yako.
    3. Hakuna mtu atapenda watoto wako, mwenza wako, familia Yako Kwa niaba Yako. Ni jukumu lako
    4. Kufanya mazoezi. Hakuna mtu atafanya mazoezi Kwa niaba Yako.
      Hili jambo sharti ulifanye mwenyewe.

    Rafiki yangu, hayo ndiyo mambo matano ambayo hakuna mtu hata mmoja atayaganya Kwa niaba Yako. Unapaswa kuyafanya mwenyewe.

    Godius Rweyongeza
    +255755848391

  • Vitabu ambavyo kama mwanachuo unapaswa kujisomea.

    Hongera sana kwa kupenda kukisoma. Hii tabia nzuri ya kujisomea unapoianza ukiwa mwaka wa kwanza chuoni, itakupeleka mbali. Mpaka kuja kumaliza chuo, utakuwa mtu wa tofauti.
    Mtu wa tofauti kwenye tabia
    Mtu wa tofauti kwenye hatua unazochukua
    Mtu wa tofauti kwenye mtazamo na fikra.

    Hivyo, nikushihi sana usiache kujisomea vitabu hivi kipindi chote uwapo chuoni. Tenga muda wa kujisomea hata kama ni kidogo.
    Kisha soma.

    Vifuatavyo ni vitabu ambavyo kama mwanachuo unapaswa kuanza kujisomea.

    1. JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO.
    Hiki kitabu kitakupa mwongozo wa kuwa ndoto kubwa. Kitakufanya uanze kufikiri nje ya boksi. Wakati wenzako wanafikiri wamalize chuo, wapate kazi, wanakaoe na kuolewa. Wewe utakuwa na UNAFIKIRI zaidi ya hapo.

    Utakuwa ndoto kubwa ambazo zimekujaa na utakuwa tayari kuzifanyia kazi bila ya kurudi nyuma. Gharama ya kitabu hiki ni 25,000/- TU. Nakala ngumu. Lipia kwa TIGO PESA: 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA ili ukipate.

    2. NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA

    Hiki kitabu kitakuonesha kuwa ukiwa na ndoto kubwa unapaswa pia kuzifanyia kazi hata kama ni kidogo kidogo. Zifanyie kazi ndoto zako hatua kwa hatua. Anza hata kama ni kidogo. Kitu kidogo unachofanya Leo hii, kitakupeleka mbali kesho. Ukikifanya kwa uhakika na kwa msimamo.

    Kitabu hiki kimekuwa tiba kwa wengi, Nina uhakika kitakufaa na Wewe pia. Tena sana kwa maana ndiyo kwanza unaanza na tayari utakuwa na mwongozo sahihi wa kwenda nao ambao ni hiki kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA.

    Kipate Sasa hivi. ni 25,000/- TU. Wasiliana na 0684408755

    3. MAAJABU YA KUWEKA AKIBA pamoja na MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA HATIFUNGANI NA VIPANDE

    Hivi ni vitabu viwili ambavyo vitakupa msingi wa elimu ya fedha na hasa kwenye maeneo mawili muhimu sana. KUWEKA AKIBA na KUWEKEZA KWENYE HISA HATIFUNGANI NA VIPANDE.

    Kama mwanachuo, Anza kujijengea utaratibu wa KUWEKA AKIBA. Anza kuwekeza kwenye HISA, HATIFUNGANI NA VIPANDE. Kiasi hichohicho kidogo unachopata, tafuta namna ya KUWEKA AKIBA pia. Sikiliza ukilifanyia kazi hili, utanishukuru MAISHA Yako yote.

    Kuna watu utasoma nao mwaka wa kwanza Hadi mnamaliza wakiwa hawajui chochote kuhusu HISA, wataanza kazi wakiwa hawajui chochote kuhusu HISA HATIFUNGANI NA VIPANDE. Wachache watakuja kujua baadaye sana. Na wengine wanaoweza wasijue hiki kitu MAISHA Yao yote. Wewe kujua hivi VITU mara hii, ni hatua kubwa.

    Unachotakiwa kufanya Sasa ni kuhakikisha umepata nakala za hivi vitabu Sasa hivi. Kila nakala ni Kila nakala ni 25,000

    Pamoja na hivi pata hivyo vingine ambavyo nimetaja hapo juu.

    *Hitimisho*
    Kama utafanya tabia ya kusoma vitabu kweli kuwa sehemu ya MAISHA Yako ya Kila siku, itakufanya kuwa mbele ya wenzako hapo chuoni.

    Nikutakie Kila la kheri.

    Vitabu vyote nilivyotaja hapo juu, unaweza kuvipata kwa kuwasiliana na 0684408755

    Karibu sana.

    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • maeneo matano Unayopaswa kuyawekea NGUVU mwaka 2024 kwenye kusoma na kujifunza na vitabu Unayopaswa kusoma.

    Isifike hatua ukaona kwamba umeshajua kila kitu. Siku ambayo utaona umeshajua kila kitu ndiyo siku ambayo utaanza kupoteza. Mara zote kuwa unajifunza.

    Kujifunza kuwe sehemu ya maisha Yako. Kama ambavyo Huwa hakuna wakati unaposema sasa nimeshakula inatosha sitakula Tena. Hivyo hivyo, kujifunza. Isifike hatua ambapo utaona kwamba imetosha.

    Kila mara kuwa na kitabu unasoma. Jiunge na kozi na programu mbalimbali na jifunze bila kuacha.

    Halafu Yale unayojifunza; yafanyie kazi mara zote bila kuacha.

    Sijui unanielewa hapo?

    Sasa yafuatayo ni maeneo matano Unayopaswa kuyawekea NGUVU mwaka 2024 kwenye kusoma na kujifunza na vitabu Unayopaswa kusoma.

    1. Jifunze zaidi kuhusu PESA. Wengi wanajua kuhusu matumizi ya PESA, lakini hawajui kuhusu kutunza PESA na kuifanya PESA iwafanyie kazi. Mwaka huu jifunze zaidi kuhusu namna ya kuitumikisha PESA. Na itumikishe haswa PESA kuanzia mwaka hata kama ni Kwa kiwango kidogo.

    Vitabu Muhimu vya kusoma kwenye hili ni kitabu Cha
    👉MAAJABU YA KUWEKA AKIBA 
    👉MAAJABU YA KUWEKEZA KWENYE HISA HATIFUNGANI NA VIPANDE
    👉JINSI YA KUTENGENEZA MSHAHARA NJE YA MSHAHARA

    Anza na hivyo vitabu. Visome vizuri, mwenyewe utafurahi Kwa uamuzi huo utakaokupa umechukua.

    1. Jifunze zaidi kuhusu biashara.
      Ili uweze KUTENGENEZA kipato zaidi unahitaji kujifunza zaidi pia kuhusu biashara. Biashara ni njia ha KUTENGENEZA kipato zaidi ambacho hakina ukomo. Jifunze biashara na fanyia kazi Yale unayojifunza bila ya kurudi nyuma.

    Vitabu vya biashara ambavyo unapaswa kusoma 2024 ni pamoja na
    👉MAMBO 55 YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZIAHA BIASHARA
    👉NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA.

    Hivi vyote unaweza kuvipata Kwa kuwasiliana na 0684408755 Sasa.

    1. Jifunze kuhusu mtandao na JINSI ya kukutumia kwenye masoko na KUTENGENEZA fedha zaidi.
      Tofauti na zamani ambapo masoko yalikuwa yanafanyika Kwa njia za redio, runinga na magazeti. Leo hii unaweza kuwafikia wengi Kwa simu Yako TU. Unalionaje Hilo. Unachotakiwa kufanya ni kuwa na maarifa sahihi. Na maarifa haya sahihi utayapata kwenye vitabu hivi.
      👉zama zimebadilika: maisha yamebadilika, ajira hatarini na wewe badilika.
      👉JINSI ya KUTENGENEZA fedha Kwa Kile unachojua.
    2. Jifunze kuhusu KUWEKA MALENGO na kuyafanyia kazi.
      Hili ni eneo unalopaswa kulifahamu hasa Kwa mwezi huu wa Januari.

    Vitabu vya kusoma kwenye hili eneo
    👉JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO.
    👉NGUVU YA KUWEKA MALENGO.

    KUPATA vitabu hivyo, wasiliana na 0684408755

    1. Jifunze kuhusu kuongeza kipato chako. Hili litakusaidia mwaka huu kipato chako kisibaki palepale. Kuongeza kipato chako ni Muhimu sana. Maana kipato chako hakipaswi kubaki palepale.

    Vitabu Muhimu vya KUSOMA.
    👉VYANZO VINGI VYA KIPATO: Usipokuwa na VYANZO VINGI VYA KIPATO, utakuwa na VYANZO VINGI VYA mahangaiko.
    👉programu ya ONGEZA KIPATO CHAKO MARA MBILI.

    Hayo ndiyo maeneo Muhimu Unayopaswa kuyawekea NGUVU kwenye kujifunza mwaka 2024.

    Nikutakie Kila la kheri.

    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

X