Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Kitu muhimu unachopaswa kukifanya unapokuwa unakutana na mtu

    Niwe mkweli, hiki kitu mwenyewe kimekuwa kinanipa shida sana. Watu wengi wanaomba kuonana namimi halafu muda mwingine wanakuwa hawajajipanga. Na muda mwingine wanaomba tu kuonana na mimi ilimradi…. Lakini pia mimi siwaambii muda ambao nitaweza kuwa nao.

    Nimejifanyia tafakari kwa watu wengi ambao wameomba kuonana na mimi ndani ya mwaka 2023, nimegundua kitu hiki kimejirudia sana. Hivyo, nimeamua mwaka 2024, ninaenda kufuata utaratibu wangu kama ifuatavyo.

    Kabla ya kuonana utaniambia tunataka tuongee nini.

    Kama kuna gharama ambazo utakuwa unapaswa kulipia utalipia mapema.

    Halafu tutapanga muda wa kuonana na kikao hicho kitadumu kwa muda gani.

    Ukichelewa, imekula kwako. Muda wako umeenda.

    Usipofika kwa wakati na hakukuwa na taarifa mapema, basi muda wangu wa kuondoka ukifika nitaodnoka. Hili litanisaiaidia kuonana na watu wachache, ila ambao wako siriazi na ambao tutafanya mambo ya maana.

    Nimejieleza mwenyewe leo hii, lakini pia na wewe angalia kwenye ratiba zako. Hivi kwa mfano, mwaka huu umekutana na watu wangapi? Je, ni muda kiasi gani umepoteza kwa vikao ambavyo havikuwa na tija?

    Hilo liondoe kwenye ratiba zako. Mwaka 2024, usirudie kosa hilohilo, la sivyo litakukwamisha kusonga mbele.

    Kama umenielewa gonga cheers, kisha mshirikishe rafiki yako makala hii aweze kusoma.

    Kila la kheri.

  • Je, kuna ulazima wowote ule wa kuandika majukumu yangu chini naweza kuyakumbuka?

    Kwenye makala ya jana nilikwambia kwamba unapaswa kuandika majukumu yako yak la siku. Unapaswa kuhakikisha kwamba umeyaandika chini. Lakini., Inawezekana wewe ukawa na kumbukumbu nzuri, hivyo ukajiambia kwamba sipaswi kuwa naandika vitu vyangu chini.

    Siku ya leo nipo hapa kukwambia kuwa hata kama una kumbukumbu nzuri. Hata kama unayesoma hapa ni profesa. Bado unapaswa kuandika chini majukumu yako utakayoyafanya ndani ya siku husika. Huandiki chini m ajukumu yako ya siku husika kwa sababu utasahau, bali unaandika chini ili uweze kuipa akili na kichwa chako nafasi ya kufikiria mambo mengine ya maana zaidi.

    Hivyo, ile nguvu ambayo ungeitumia kwenye kukumbuka ratiba yako ya siku, unaitumia kwenye kwenye mambo mengine yatakayokupa matokeo makubwa zaidi.

    Sijui umenielewa hapo? Ee, usije kusema ooh, unajua mimi nina kumbukumbu kubwa bwana sihitaji ratiba. Hapana,  andika chini, ratiba yako.

  • Kitu kimoja unachopaswa kuanza kufanyia kazi mara moja

    Rafiki yangu mpendwa salaam, bila shaka unaendelea vizuri.

    Hivi umewahi kujiuliza ni kwa nini unakuwa unapoteza muda kwenye siku yako? Unajua kwa nini hili linatokea? Moja ya kitu kinachokufanya upoteze sana muda wako ni kwa sababu, hujapangilia vizuri siku yako. Yaani, chochotfe kile kinachokuja mbele yako wewe unafanya. Ukweli ni kuwa unapoianza siku yako, unapaswa kuutumia muda wako kwenye kuipangilia siku yako.

    Ndiyo, andika saa kwa saa kitu ambacho unaenda kufanyia kazi ndani ya siku husika.

    Kisha fuata hiyo ratiba yako.

    Hiki kitakusaidia kuepukana na muda mwingi ambao ungeupoteza ndani ya siku yako. Lakini pia kitakusaidia kuiendea siku yako katika namna ambayo itakuzalishia matokeo.

    Kwenye ratiba yako weka vitu ambavyo utafanya na vitakuletea matokeo. Kama kitu hakitaleta matokeo sasa au siku zijazo, kiondoe. Kipaumbele chako kiwe ni yale majukumu yako ya muhimu tu.

    Sijui umenielewa.

    Ebu anza leo. Ni kwa namna gani unaenda kupangilia ratiba yako siku ya leo? Ni vitu gani ambavyo unaenda kuondoa kwenye maisha yako ambavyo umekuwa unafanya ila havina manufaa?

    Nitumie ujumbe whatsap kwa 0755848391

    Emai: godiusrweyongeza1@gmail.com

    Kila la kheri

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Kujifunza kuhusu uandishi wa makala. BONYEZA HAPA

  • NJE YA KUMI NA NANE: fikiri, Hoji Na Uliza Maswali Katika Ulimwengu Ambao Hautaki Uwe Hivyo.

    Rafiki yangu, kama kwenye maisha yako bado hujafikia hatua ambapo wewe unaweza kufikiri nakuhoji na kuuliza maswali vitu. Basi bado hujaianza safari yako ya maisha. Hii ni hatua muhimu sana ambayo unapaswa kuifikia.

    Tuli[pokuwa wadogo tulikuwa tunapenda sana kuuliza maswali. Kuanzia maswali ya Mungu ni nani? Mpaka maswali ya watoto wanatoka wapi? Ila baada ya kukua inaonekana kuna ustaarabu ambao unakuja ghafla. Na ile shauku ya kujua vitu ambayo unakuwa nayo tangu utotoni inapotea. Leo hii nipo hapa kukwambia kuwa unapaswa kuendelea

    Kufikiri

    Kuuliza maswali

    Kuhoji

    Na kufanya maamuzi yako mwenyewe.

    Hakuna mtu ambaye anaweza kufikiri kwa niaba yako. Usimwongope yeyote.

    Watu wengi, viongozi wengi hawapendi kabisa uulize maswali au uhoji au ufikiri kwa namna yako. Ukionekana unafikiri, unahoji na kuuliza maswali na kufanya maamuzi yako mwenyewe unaonekana wewe ni tishio kwao na kwa uongozi wao!

    Ndiyo maana hata mfumo wa elimu ulipokuja hapa barani kwetu Afrika uliletwa katika mfumo huuhuu. Kwamba wapokeaji wa elimu wasiwe watu wa kufikiri, bali wawe watu wa kupokea maagizo na kuyafanyia kazi.

    Unaweza kudhani ni utani, unaweza kusema haka ka jamaa kanapata wapi ujasiri wa kusema haya, kama huniamini mimi basi iamini hata hii barua aliyoiandika Mfalme Leopord wa Pili kwa ajili ya wamisionari waliokuwa wanaeneza injili Afrika.

    Kwenye barua yake ameandika hivi; wafundishe hawa watu kusoma lakini siyo kufikiri.

    Hii dhana ya kufikiri, kuhoji na kuuliza maswali inaleta utata miongoni mwa watu wengi.

    Kwenye dini ukionekana unauliza maswali sana, watakwambia kwamba umeanza kuasi. Hivyo ili usionekane kama mtukutu unapaswa kufuata kila kitu kinachoelezwa au unachoambiwa. Kama una swali kafie nalo mbele huko…

    Kwenye elimu mpaka vyuo vikuu hivyohivyo, ukionekana unauliza sana, inaonekana unataka kuwa *challenge* maprofesa. Wanaweza mpaka wakakufelisha hivihivi..

    Wanafunzi wenzako wakiona unauliza sana maswali, wataanza kudhani ni utukutu tu au unajionesha.

    Sasa nataka nikwambie kitu kimoja tu, hoji kila kitu kwenye maisha yako. Uliza kila kitu, hata hili andiko unaruhusiwa kulihoji  na kuuliza. Ni kwa jinsi hii ndiyo utaweza kuupata ukweli kamili wa kile ambacho kineongelewa au ambacho unaanmbiwa. Na hivyo utaishi maisha yenye uhuru sana.

    NB: Hiyo barua ya mfalme Leopord wa pili wa wabeljiji unaweza kuipata mtandaoni. Andika, King Leopords letter to African Missionaries.

    Utakachosoma huko siri yako.

    Uwe na siku njema sana

    SOMA ZAIDI: Vitu viwili vinavyokufanya ushindwe kufikia ndoto zao

    Makala ya hii imeandikwa na Godius Rweyongeza

    0755848391

    Morogoro-Tz

  • Hiki ni kitu ambacho kinaenda kukupa matokeo makubwa kama utakifanyia kazi

    Rafiki yangu mpendwa salaam,

    Bila shaka unaendelea vyema na kazi zako. Hongera sana kwa kazi. Siku ya leo ningependa nikwambie kitu kimoja ambacho kinaenda kukupa matokeo makubwa.

    Kitu hiki siyo kingine bali ni kufanya kazi ambayo unapenda. Kama unahairisha sana kufanyia kazi majukumu yako, kuna uwezekano mkubwa kuwa unafanya kazi ambayo wewe mwenyewe hupendi. Kama utaanza kufanya kazi ambayo unapenda, ni wazi kuwa utajikuta kwamba unaifanya kwa bidii na kwa muda mrerfu na hata bila kuhairisha.

    Muda mwingine unaharishisha majukumu ambayo unapasw akuwa unayafanyia kazi kwa sababu huyapendi. Fanya kile unachopenda na ukweli ni kuwa hutajihisi kama unafanya kazi. Na hili litakufanya uweze kupata matokeo makubwa huku ukiwa unajisikia vizuri kwa kile unachofanya.

    Ujumbe wangu wa leo kwako ni mmoja tu; kama unataka kupata matokeo makubwa fanya kazi ambayo unapenda.

    Thomas Edison ni mmoja wa watu waliokuw awanafnaya kazi sana na kwa muda mrefu. Siku moja aliulizwa ni kwa nini anafanya kazi muda mrefu sana. Alijibu kwa kutoa jibu la kushangaza sana. Alisema, sijawahi kufanya kazi; inashangaza sana.

    Unajua kwa nini alisema kwamba sijawahi kufanya kazi. Alisema hivyo kwa sababu, alikuwa anafanya kazi anayoipenda na hivyo alikuwa hajisikii kama anafanya kazi japo alikuwa anafanya kazi kwa muda mrefu kuliko watu wote wlaiokuwa wamemzunguka.

    Kama huwezi kunisikiliza mimi, basi msikilize vizuri Thomas Edison.

    Kila la kheri.

    Makala imeandikwa na Godius Rweyongeza.

    Unaweza kuwasiliana na mwandishi kwa 0755848391 au baruapepe ya godiusrweyongeza1@gmail.com

    Kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza, jiunge na mfumo wake wa kupokea mafunzo kwa baruapepe. hapa chini

    Je, na wewe ungependa kujifunza uandishi? BONYEZA HAPA

  • Muda Ni Dhahabu

    Muda ni kitu pekee ambacho watu wote tunacho Kwa usawa. Ni muhimu sana kwangu kuhakikisha kuwa nakutumia vizuri muda wangu Kwa Manufaa. Hata kama Sina utajiri wa fedha ninaweza kubadili utajiri wa muda kuwa wa fedha.

    Muda ni DHAHABU, ninapaswa mara zote kuhakikisha nakutumia vizuri.

    Asante.

  • Utajiri ni hatima ambayo Kila Mmoja anapaswa kuipambania

    Kujenga utajiri ni mtazamo. Napaswa kubadili mtazamo wangu na kuona kuwa inawezekana kujenga utajiri mkubwa.

    Watu wengi wanakuwa na imani mbalimbali Kuhusu utajiri, wanaona utajiri ni mbaya na matajiri ni wabaya. Mtazamo huu huu unawafanya wengi washindwe kujenga utajiri Kwa sababu huwezi kupata kitu ambacho wewe Mwenyewe unaona ni kibaya.

    Ili kujenga utajiri unapaswa kuwa na mtazamo chanya kuwa utajiri ni mzuri na unapaswa kuupenda utajiri.

    Utajiri ni baraka. Ukiwa nao unakuwa msaada Kwa wengine usipokuwa nao unakuwa karaha Kwa wengine

    Utajiri ni mzuri.
    Utajiri ni hatima ambayo Kila Mmoja anapaswa kuipambania

    Asante
    Godius Rweyongeza
    www.songambele.co.tz

  • Mambo kumi yatakayokusaidia kulianza juma hili ukiwa mbele ya watu wengine

    1. Kwenye kila hatua unayofikia, bado kunakuwepo na hatua nyingine kubwa mbele yako ambazo unaweza kupiga, kwa hiyo usijizuie kupiga hatua kwenye Maisha yako kwa sababu ya mafanikio ya muda mfupi ambayo unapata. Badala yake kila mara jiulize ni kwa namna gani naweza kutumia matokeo ya sasa kwenda mbele zaidi.
    2. Unachohitaji wewe ni kuendelea mbele hata kama unapitia kwenye changamoto. Kitendo cha wewe kuendelea mbele kitaonesha kuwa wewe ni shujaa
    3. Watu wanaofanya vitu vya tofauti siyo kwamba wana muda mwingi wa kutosha kama unavyofikiri, nilichogundua ni kwamba mtu yeyote wa kawaida anayeweza kupangilia ratiba yake ya kila siku na akaifuata hiyo ratiba, anaweza kufanya makubwa kuliko mtu  anayesubiri kuwa na muda wa kutosha ili afaie kazi anachotamani.
    4. Kuwa na ndoto kubwa ni kitu kmoja, ila kufanyia kazi ndoto zako kubwa ni kitu kingine. Wewe kuwa upande wa kufanyia kazi ndoto zako.
    5. Ndoto yako kubwa kwa vyovyote vile inahitaji fedha, kuwa mtumiaji mzuri wa fedha, wekeza, na kila fedha inayoingia mfukoni mwako itumie vizuri kwa manufaa yako ya sasa na baadaye.
    6. Kama unataka kuishi Maisha ya kawaida, fanya vitu vya kawaida, kama unataka kufanya mambo ya tofauti, fanya vitu vya kawaida katika namna ambayo siyo ya kawaida.
    7. Mambo mengine yote yanaweza kusubiri, ila usisubirishe ndoto zako anza kuzifanyia kazi ndoto zako. anza kuzifanyia kazi ndoto zako hata kwa udogo.
    8. Kuna vitu viwili ambavyo kama bado hujavifanikisha basi unapaswa kuendelea kupambana mpaka kieleweke, endelea kupambana bila ya kurudia nyuma. Kitu cha kwanza ni kuwa na uwekezaji ambao unakuingizia fedha hata kama umelala na hapa siongelei fedha za kawaida, bali naongelea fedha za kuishia Maisha unayotaka , kama bado hujafikia hiki kiwango, basi usilale Rafiki yangu, endelea kupambana mpaka kieleweke.
    9. Kitu cha pili ambacho kama hujakifikia ni kuwa biashara ambayo inaweza kujiendwesha yenyewe bila ya kukuhitaji wewe. Kama bado hujafikia kwenye hivi viwango, basi unapaswa pia kuendelea kupambana bila ya kurudi nyuma mpaka kieleweke.
    10. Ishi Maisha yako, usiige Maisha ya watu wengine, unapoanza kuishi Maisha ya watu wengine, moja kwa moja unakuwa unajinyima fursa ya kuwa wewe halisi na kuonesha kile ambacho wewe mwenywewe unaweza kufanya..

    Hayo kwa leo yanatosha. Nikutakie mwanzo mwema wa juma hili hapa.

    Kila la kheri na waslimia sana Rafiki zako walio karibu na wewe.

  • Weka akiba kwa manufaa yako

    Ni vigumu sana kupata suluhisho la kudumu kwa njia za mkato. Suluhisho la kudumu, linahitaji njia ya uhakika ambayo utaifuata mpaka kufikia suluhisho.

    Kama una changamoto ya akiba, kukopa siyo suluhisho. Ila kuthibiti matumizi yako, kuongeza kipato na kuwa na vyanzo vingi vinayokuingizia kipato ndiyo suluhisho.

    Anza kuweka akiba leo, maana akiba ni mbegu ambayo unaitunza siyo kwa ajili ya leo tu bali kwa ajili ya siku nyingi zijazo. Weka akiba leo kwa manufaa yako ya siku nyingi zijazo.

    Kupata kitabu cha maajabu ya kuweka akiba ni rahisi sana. Wasiliana na 0684408755

    Fanya hivyo sasa ili kujipatia nakala yako sasa.

  • Hili Ndilo Suluhisho la Kudumu Kwa Tatizo La Ajira Linaloendelea

    Rafiki yangu mpendwa, bila shaka unaendelea vizuri, changamoto kubwa kwenye zama tunazoishi sasa hivi ni ajira. Kuna vijana wengi ambao wamehitimu chuo ila hawana ajira, kila siku wanahangaika kuomba kazi kwenye taasisi moja baada ya nyingine. Ukweli ni kuwa kwenye zama tunazoishi sasa hivi hakuna ajira kama ilivyokuwa kwenye zama za viwanda. Hata hivyo kazi za kufanya zipo nyingi na mahitaji ya msingi kabisa ya kila siku ya mtu yapo palepale. Kila siku kuna watu ambao wanahitaji kula, kila siku na watu ambao wanaendelea kutafuta elimu, watu wanaendelea kujenga kila siku…

    Kumbe tatizo siyo kazi maana zimejaa ila watu wa kufanya hizo kazi ndiyo hawapo.

    Kama unaweza kuchagua kazi yoyote ile na kujikita kwenye hiyo, ukaifanya kwa ubora na kutoa thamani kubwa kwa watu, maana yake mwisho wa siku utapata fedha kutoka kwa hao watu.

X