Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Malengo Yako Ya Mwaka 2024 Usimwachie Mungu

    Ni mwaka wa tatu sasa tarehe kama ya leo naandika makala  inayosisitiza kuhusu malengo na kwa nini haupaswi kumwachia malengo yako mungu. Mwaka juzi niliandika makala hii hapa. 

    Makala hiyo hapo juu ina swali zuri sana ambalo nimekuwa napenda kuendelea kuwauliza watu kila mara.

    Na hata juzi nilituma ujumbe kwa watu wa nguvu kupitia whatsap. Ujumbe huu ulikuwa na swali lililokuwa linauliza, umejiandaaje kwa ajili ya mwaka 2024? Lengo lako la mwaka 2024 ni lipi au unamwachia Mungu?

    Cha kushangaza ni kwamba asilimia kubwa ya watu walisema kwamba wanamwachia Mungu. Kwa sababu ni mweza yote,

    Ni alpha na omega.

    anajua kesho yako

    anachopanga yeye mwanadamu hawezi kupangua

    na mengine mengi.

    Ukweli ni kuwa malengo yako haupaswi kumwachia Mungu, japo ana sifa hizo ambazo watu wamekuwa wanatoa, ila ukweli ni kuwa Mungu mwenyewe anakuangalia wewe unavyofanya.

    Mungu hawezi kukubariki ukiwa umebweteka, huna malengo, huna mwelekeo wowote, upo tu hapo. Kitendo cha wewe kukaa chini na kuweka malengo ni sawa na sala ya kumwambia Mungu kwamba sasa naomba baraka zako uzielekeze hapa.

    Kitamfanya aachilie baraka zake kuelekea kwenye lengo lako, kuliko pale unapokuwa hauna lengo wala ndoto yoyote ile unayoifanyia kazi.

    Umekuwa unaishi kwa miaka mingi bila ya kuwa lengo lolote. mwaka huu fuata mwongozo huu hapa kuweka malengo. Hata kama hujawahi kuweka malengo, ebu ufanye mwaka huu kuwa mwaka wako wa kwanza wa kuishi kwa kufuata malengo.

    Kamwe usije kusema kwamba nimechelewa kuweka malengo. Muda bado, ndiyo kwanza kumekucha ndani ya 2024! Na kama unajua biashara mara zote ni asubuhi. Huu ndiyo muda wenyewe wa wwe kuutumia muda wako vizuri sasa.

    Ukiwa na malengo, utakuwa na kusudi, utakuwa unajuwa wapi unaelekea na nini ufanye ili uweze kufika huko.

    SOMA ZAIDI: Hatua Muhimu Katika Kuweka Malengo

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu.

    Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea.

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Salaam Za Kheri Ya Mwaka Mpya 2024 Kutoka Kwa Godius Rweyongeza

    Rafiki yangu mpendwa, salaam. Nichukue nafasi hii kukutakia kheri ya mwaka mpya 2024. Ule mwaka uliokuwa umeusubiri sasa ndiyo huu hapa umefika. Yale mambo yote uliyokuwa umesema kwamba utayafanya ndani ya huu mwaka, sasa ndiyo muda muafaka wa kuyafanya.

    Biashara uliyokuwa umesema kwamba utaanzisha mwaka 2024, hakikisha sasa unaianzisha. Akiba uliyokuwa umesema utaweka. Iweke.

    Kiufupi lengo lako kuu la mwaka huu hakikisha kwamba unalifanyia kazi bila ya kuacha.

    mwaka huu ufanye kuwa Baraka kwako. Na utaufanya hivyo kwa kufanyia kazi vile ulivyoopanga kufanya kuliko tu kuishia kusema kwamba utafanya.

    Tumezoea kwamba watu huwa wanasherehekea sikukuu nyingi ambazo hawajasbabisha wao. Sikukuu ambazo huwa zinatokana na kalenda. Sikukuu hizi ni pamoja na mwaka mpya huu ambao unasherehehekea leo, siku za iddi, pasaka, sikukuu zote za kiserikali, krismasi na yinginezo. Mwaka huu usiishie tu kusherehehea sikukuu zinazotokana na kalenda. Sherehekea matokeo uliyopata kutokana na kufanyia kazi malengo na ndoto zako.

    Kazi ya kufanya leo. Andika malengo yako makubwa ambayo utayafanyia kazi ndani ya mwaka 2024. Kila la kheri

    Soma zaidi:Kheri ya mwaka mpya 2022 

    Kheri Ya Mwaka Mpya Na Mambo 12 Unayopaswa Kufanya Kuanzia Leo

  • Kwaheri 2023: Mambo 12 Ambayo Mwaka 2023 Umenifunza

    Mwaka 2023 sasa unaisha.

    Umekuwa ni mwaka bora sana kwangu, na umekuwani mwaka ambao nimeweza kufanya mengi, kuna mengi ambayo naweza kuandika kuhusu mwaka 2023 ila kwa leo nitaandika haya ambayo mwaka 2023 umenifundisha.

    1. mwaka 2023 umenifundisha kuwa kuwa mtandao wa intaneti una mkono mrefu. Najua wengi tumezoea kusikia kwamba serikali ina mkono mrefu. Lakini mwaka 2023 umenifundisha pia kuwa mtandao wa intaneti una mkono mrefu. Kuna makala nimekuwa naandika kwenye hii blogu tangu mwaka 2016 mpaka leo. Baadhi ya hizo makala hazikusomwa sana mwanzoni, ila kadiri siku zinavyokwenda watu wanazidi kuzisoma na kunufaika nazo. Japo nilishaandika hizi makala kwa muda mrefu ila mpaka leo hii kuna watu wanazidi kunufaika na hizo makala, na hii ni kwa sababu tu zipo mtandaoni. zingekuwa sehemu nyingine wasingeziona. Na ndio maana nimekuwa nashauri watu wengi wawe na blogu badala tu ya wewe kuwa unaandika vitu vyako vizuri na kuviweka whatsap ambapo baadaye vinapotea. Kama hauna blogu, mwaka 2024 hakikisha kwamba unaliweka hilo kama lengo lako la kuhakikisha unakuwa na blogu na hasa kama unashirikisha maarifa kwa njia ya mtandao. CHochote kile unachoandika hata kama ni kidogo, kiweke kwenye blogu, kuna siku kitakuwa na manufaa kwa watu wengine.
    2. Mwaka 2023 umenifundisha kuwa kufanya kazi kwa bidii kunalipa japo unaweza usione matokeo ya kwa muda  mfupi muda mwingine. lakini unapaswa kuwa tayari kuwekeza  kwenye kufanya kazi kwa bidii kama ambavyo wakimbiaji wa Marathoni huwa wapo tayari kuwekeza kwenye kufanya mazoezi kwa miaka minne kabla ya KUKIMBIA marathoni ya dakika kadhaa.
    3. mwaka 2023 umenifundisha kuwa tatizo la ajira nchini Tanzania ni kubwa, lakini pia vijana hawapendi kufanya kazi. Hili nimeligundua baada ya kuanza kuajiri. Mwanzoni nilifikiria kupata watu sahihi ni rahisi sana maana vijana wengi hawana ajira, ila kilichotokea ni tofauti. Vijana wengi kweli hawana ajira, ila pia hawako tayari kufanya kazi. Wanapenda pesa ila hawataki kazi.
    4. Mwaka 2023 umenifundisha kuwa kuchukua hatua ya kwanza ni muhimu sana. Lakini pia sambamba na hili mwaka huu umenifundisha kwamba unapopanga kufanya kitu kifanye. Mwaka huu tulipanga kufanya semina; kutokana na sababu kadha wa kadha kuna watu walidhani haitawezekana kufanyika. na wengine walisema huwezi kufanya semina bila ya kuwa na udhamini wa taasisi kubwa kama benki n.k. na hata wengine waliokuwa wameonesha nia ya kuhudhuria semina hawakufanya hivyo. Ila kwa kuwa tulikuwa tumepanga kufanya semina. Hatukurudi nyuma. Mwezi wa sita tarehe 24 tuliweza kufanya semina moja nzuri sana hapa Mjini Morogoro, ilihudhuriwa na watu wasiozidi 12, ila ilikuwa ni moja ya semina bora sana za mwaka 2023. Na hiki kimetupa mwanya wa kufanya semina nyingine zinazofuata, mfano mwaka 2024 mwezi wa sita tarehe 29 tutafanya semina ya ana kwa ana maeneo ya ubungo Dar. Unaweza kujiandikisha mapema, ada yake itakuwa ni laki moja kwa kila mshiriki. kujiandikisha tuma ujumbe kwenda namba ya simu 0755848391 sasa.
    5. Mwaka 2023 umenifundisha kwamba haupaswi kutegemea kitu kimoja au namba moja. Kama ni simu na unaitumia kwa kazi, usiitegemee moja. Kama ni kompyuta na unaitumia kwa kazi, usiitegemee moja, kuna siku hiyo unayoitegemea inaweza kugoma. Kama ni wafanyakazi usimtegemee mmoja, siku akiacha kazi utapasuka moyo, nadhani labda mwenza tu ndiyo unapaswa kuwa naye mmoja, ila vingine tafuta namna ya kuwa na ziada ili ikitokea moja imepata shida au dharula nyingine unaweza kuendelea mbele.
    6. Mwaka 2023 umenifundisha kuwa ukiajiri, lipa watu wako kwa wakati hata kama malipo unayowapa ni kidogo. Kamwe usimcheleweshee mfanyakazi wako mshahara wake..Hili somo nimejifunza kwa taabu sana baada ya kumcheleweshea mmoja wa wafanyakazi wangu maokoto yake, akaacha kazi na alikuwa ni mtu wa muhimu sana. Kwa lugha ya sasa hivi ni kwamba sikuzingatia maokoto. MWAKA 2024 ZINGATIA MAOKOTO.
    7. Mwaka 2023 umenifundisha kwamba, unapaswa kutangaza bidhaa au biashara yako au kitu chochote unachofanya kwa njia zote unazoweza kutumia. Mitandao, redio, runinga, viperushi kutaja ila vichache, mwaka huu kila njia niliyotumia kwenye kutangaza kwa namna moja au nyingine imeniletea wateja.
    8. Mwaka 2023 umenifundisha kuwa popote unapokuwa, itangaze biashara au bidhaa yako. Nilikuwa nasafiri kwenda Dar, kwenye gari nilisimama kwa ajili ya kuongea na wasafiri kuhusu umuhimu wa kusoma vitabu. Huwezi amini, miongoni mwa wale waliosikia kile nilichosema kuhusu usomaji wa vitabu, walihamasika, na sasa kuna watu wawili ambao wamekuwa wasomaji wazuri wa vitabu. Hii yote ni kutokana na mazungumzo yangu mafupi siku hiyo kwenye basi wakati tunatoka Morogoro kwenda Dar.
    9. Mwaka 2023, umenifundisha kuwa uwekezaji unanipa ridhiko la moyo sawa na kuandika kunavyonipa ridhiko la moyo. Huu umekuwa ni mwaka ambao nimekuwa nikifanya uwekezaji kwa nguvu zote, na mara zote ambazo nimekuwa nafanya uwekezaji, nimekuwa najisikia vizuri.
    10. Mwaka 2023 umenifundisha kuwa unapofanya kazi, unapaswa kuifanya kwa ubora wa hali ya juu sana. Maana hiyo kazi itadumu, lakini pia itawafikia wengi. Kuna baadhi ya vitabu nimeandika zaidi ya miaka sita iliyopita. Ila watu wamevisoma mwaka huu na vimekuwa vitabu vyenye msaada mkubwa kwao. Laiti ningekuwa nimeviandika hovyo visingeweza kuwa vyenye msaada kihivyo. Vitabu hivyo ni pamoja na kitabu cha TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA ambacho ndani ya huu mwaka kimepata mpaka nafasi ya kuongelewa kwenye bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hii ilikuwa ni baada ya mbunge, mh. Shamsi Vuai Nahodha kuwa amekisoma na kukipenda. Kitu hiki kilifanya watu wengi wapende kujipatia nakala zao, na kweli kila aliyepata nakala alitaka na rafiki yake aipate. Hii yote ilikuwa ni kwa sababu, niliandika kitabu hiki vizuri mwaka 2018, na sasa watu ndiyo wanatambua uwepo wake na wanakisoma kwa nguvu zao zote. Na wewe pia usisite kujipatia nakala ya kitabu hiki cha TATIZO SI RASILIMALI ZILIZOPOTEA: tatizo ni rasilimali watu tunaowapoteza. Kupata nakala yako wasiliana na 0684408755 sasa.
    11. Mwaka 2023 umenifundisha kukaa na watu sahihi. Nikijaribu kuangalia mambo yote makubwa ambayo nimeyafanya mwaka 2023 ni kwa sababu nyuma yangu nilikuwa na watu sahihi walionizunguka, la sivyo mengi yasingewezekana.
    12. Mwaka 2023 umenifundisha kuwa hakuna elimu au kitu chochote unachojifunza kinachopotea. Unaposoma kitabu siyo kwamba unapoteza, na kama kuna baadhi ya vitu ambavyo hujatumia siyo kwamba ndiyo umepoteza. Ila kuna siku, saa na dakika kitu hicho utakitumia na kitakuwa chenye manufaa kwako.

    kuna mengi ambayo mwaka 2023 umenifundisha, ila kwa leo itoshe tu kusema kwamba hayo ndiyo masomo makubwa ambayo binafsi nimejifunza 2023.

    Wwewe mwaka 2023 umekufunza kitu gani? Mjadala huu unaendelea kwenye kundi la whatsap, hapa

    Au kwa email ambapo unaweza kunijibu kwa kunitumia ujumbe kwenda godiusrweyongeza1@gmail.com

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye ni kocha, mjasiriamali na mkufunzi. Unaweza kujifunza zaidi kwake kwa kujiunga na mafunzo ambayo huwa anatoa kwa njia ya barua pepe hapa.

    Kupata makala maalum ambazo huwa anaandika kwa watu maalum. Bonyeza hapa

    KUMBUKA:

    Ofa ya msimu wa sikukuu inaelekea kuisha. Mwisho ni tarehe 1.1.2024 saa sita usiku

    *Ofa ya kwanza*
    *Unapata vitabu 6 (softcopy kwa 20,000/- au vitatu kwa 10,000/-* 🤭

    Chagua hapa, nipe taarifa👇🏿

    1: JINSI YA KUTENGENEZA MSHAHARA NJE YA MSHAHARA
    2: NGUVU YA WAZO
    3: NGUVU YA KUWEKA MALENGO
    4: MWONGOZO WA WAPAMBANAJI
    5: MAMBO 55 YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZISHA BIASHARA
    6: VYANZO VINGI VYA KIPATO

    Lipia 10,000 upate vitabu VITATU, LIPIA 20000 Upate vyote SITA. ( Softcopy)

    Namba ya MALIPO ni. 0684408755 GODIUS RWEYONGEZA

    *Ofa ya pili*

    Unapata audiobook 6 kwa 15,000/- TU. Audiobooks zenyewe ni.

    1. NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA
    2. JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO
    3. MAISHA NI FURSA: ZITUMIE ZIKUBEBE
    4. JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO
    5. MAAJABU YA KUWEKA AKIBA
    6. KIPAJI NI DHAHABU

    Gharama ya hizi audiobooks ni zaidi ya ~100,000/~ ila kwa Sasa lipia 15,000/- TU upate zote sita.

    Namba ya malipo ni 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    *Hii ndiyo Ile ofa ushindwe mwenyewe*

    Wewe ofa Yako msimu huu ni ipi?

  • 2024 badili mifumo yako ya kufikiri

     

    Rafiki yangu, matokeo ambayo umepata ndani ya mwaka 2023, yanaweza yasibadilike kama hutabadilika. Unachohitaji kufanya mwaka 2024 ni kubadilika wewe. Kama hutabadilika au kubadili namna unavyofikiri, ukweli ni kuwa matokeo utapata matokeo yaleyale ambayo ambayo umepata 2023 au hata chini ya hapo.

     

    Napenda sana nukuu ya Robert Pirsing kama ilivyonukuwa kwenye kitabu cha Thinking In Systems,  anasema;

    If a factory is torn down but the rationality which produced it is

    left standing, then that rationality will simply produce another

    factory. If a revolution destroys a government, but the systematic

    patterns of thought that produced that government are left intact,

    then those patterns will repeat themselves. . . . There’s so much talk

    about the system. And so little understanding.

    —Robert Pirsig, Zen and the Art of Motorcycle Maintenance

     

    Akimaanisha

    I’ll provide a translation of the given text into Kiswahili:

     

    “Endapo kiwanda kitabomolewa lakini mantiki iliyosababisha kujengwa kwake ikabaki, basi mantiki hiyo itaunda tu kiwanda kingine. Endapo mapinduzi yanaharibu serikali, lakini muundo wa mawazo uliosababisha kuundwa kwa serikali hiyo unabaki salama, basi muundo huo utajirudia. … Kuna mazungumzo mengi kuhusu mfumo. Na uelewa ni mdogo sana.”

    —Robert Pirsig, Zen and the Art of Motorcycle Maintenance

     

    Hii maana yake nini, maana yake kitu kilicholeta matokeo ya kwanza, kama kitu hicho hakitaharibiwa au kubadilishwa, matokeo yataendelea kupatatikana.

     

    Mfano wengi tumekuwa tunaongelea kuhusu serikali na namna ilivyo na mfumo mbovu. Na hivyo fikra za wengi zimekuwa kwamba ikibadilishwa serikali basi matokeo ya tofauti yanaweza kupatikana. Lakini mabadiliko ya serikali yamekuwa hayaji na matokeo ya tofauti. Na kitu ambacho kimekuwa kinasababisha hilo ni ile fikra iliyojenga serikali, au misimamo iliyojenga serikali, au misingi iliyojena serikali bado haijaharibiwa. Misingi bado ni ile ile, hivyo anapobadilishwa mtu mmoja juu, wengine wote wanaendelea kukaa vilevile hata wakibadilishwa. Kumbe, njia ya kupata matokeo ya tofauti ni kubadili ile misingi na kuweka mfumo mpya ambao utaleta matokeo.

     

    Sasa achana na serikali. Hapa nakuongelea wewe, 2024 kama hutabadili mifumo ambayo umekuwa unaitumia utaendelea kupata matokeo yaleyale na hata chini ya hapo.

     

    Sasa unajiuliza ni mfumo upi unapaswa kuwa nao.

    KWANZA, anza kwa kuweka ratiba yako. Kuwa na ratiba yako ya kila siku, ambayo unaifuata.

    Pili kwenye siku yako, fanya majukumu ya muhimu tu kwanza. Majukumu ambayo siyo ya muhimu kamwe usiyafanye. Fanya majukumu ambayo ni muhimu pekee.

    Tatu,fanya majukumu machache, majuku mengine ambayo si ya muhimu zaidi wape wengine.

    Soma zaidi: Lengo Lako Kuu La Mwaka 2024 Ni Lipi? Au Ndio Unamwachia Mungu🤔?

    Karibu sana kwenye semina ya kufungua mwaka 2023. Kwenye hii semina nitaeleza hii mada kwa undani na kwa urefu kiasi kwamba utaweza kuilewa na kuitumia vyema sana.

    Ni semina ya siku 30.

    Itaanza tarehe 20 hadi tarehe 20  Februari, moja ya mada ambayo itafundishwa kwa kina ni hii.

    Gharama za hii semina ni elfu thelathini.

    Kujiunga na semina hii ni rahisi sana.

    Lipia 30,000/- kwa namba 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA. Ukishalipia, basi utaniambia nili nikuunge kwenye kundi maalumu la semina.

    NB: Ofa ya Krismasi bado inaendelea. Mwisho ni siku ya tarehe 1.1.2024 saa sita usiku

    *Bado siku mbili TU ya wewe kupata ofa hizi mbili*

    *Ofa ya kwanza*
    *Unapata vitabu 6 (softcopy kwa 20,000/- au vitatu kwa 10,000/-* 🤭

    Chagua hapa, nipe taarifa👇🏿

    1: JINSI YA KUTENGENEZA MSHAHARA NJE YA MSHAHARA
    2: NGUVU YA WAZO
    3: NGUVU YA KUWEKA MALENGO
    4: MWONGOZO WA WAPAMBANAJI
    5: MAMBO 55 YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZISHA BIASHARA
    6: VYANZO VINGI VYA KIPATO

    Lipia 10,000 upate vitabu VITATU, LIPIA 20000 Upate vyote SITA. ( Softcopy)

    Namba ya MALIPO ni. 0684408755 GODIUS RWEYONGEZA

     

    *Ofa ya pili*

     

    Unapata audiobook 6 kwa 15,000/- TU. Audiobooks zenyewe ni.

    1. NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA
    2. JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO
    3. MAISHA NI FURSA: ZITUMIE ZIKUBEBE
    4. JINSI YA KUONGEZA THAMANI YAKO
    5. MAAJABU YA KUWEKA AKIBA
    6. KIPAJI NI DHAHABU


    Gharama ya hizi audiobooks ni zaidi ya ~100,000/~ ila kwa Sasa lipia 15,000/- TU upate zote sita.

    Namba ya malipo ni 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    *Hii ndiyo Ile ofa ushindwe mwenyewe*


    Wewe ofa Yako msimu huu ni ipi?

  • Ushauri Muhimu Ambao Kila Kijana Anapaswa Kufanyia Kazi

    Huu ni ushauri ambao kila kijana anapaswa kuupata.Toka nyumbani anza kupambana na hali yako.

  • Usisubiri Mtu Yeyote Kuanza Kufanyia Kazi Ndoto Zako

    1. USISUBIRI YA MTU YEYOTE KUANZA KUFANYIA KAZI NDOTO NA MALENGO YAKO. Ndiyo unapawa kuwa na ndoto kubwa bila ya kusubiri mtu yeyote, ila ukweli ni kuwa ndoto kubwa na malengo makubwa bila ya kufanyia kazi, hayatakaa yatimie. Ndiyo maana unapaswa kuanza kufanyia kazi malengo na ndoto zako bila ya kusubiri ruhusa.

    Kwenye andiko langu la Jana ee mtu mkubwa….niliandika kuhusu kuwa na ndoto kubwa. Ndiyo unapawa kuwa na ndoto kubwa bila ya kusubiri ruhusa ya mtu yeyote, ila ukwlei ni kuwa ndoto kubwa na malengo makubwa bila ya kufanyia kazi, hayatakaa yatimie. Ndiyo maana unapaswa kuanza kufanyia kazi malengo na ndoto zako bila ya kusubiri ruhusa.Kuifanyia Kazi ndoto Yako ndiyo habari mjini.
     
    Huu ni upande wa pili wa shillingi. Upande wa kwanza ni KUWA NA NDOTO Kubwa upande wa pili unaosema baada ya kuwa na ndoto kubwa Sasa unapaswa kuzifanyia kazi.
     
    Ebu pata picha kama Dunia yote ikibadilika Leo hii unaposoma hapa na Kila mmoja akaanza kuwa bize na ndoto zake.
     
    Aliyekuwa anapiga umbea ukakuta ndiye Yuko bize na ndoto zake kubwa. Hataki utani, hataki umbea ila kipaumbele kwake ni kazi TU. Na kazi hiyo ni ndoto zake.
     
    Baada ya kuwa umeonana na huyo mtu pata picha ukatoka hapo ukaenda kukutana na mwingine ambaye siku za nyuma alikuwa anakaa kaa tu bila kufanya kitu chochote, lakini leo hii ukakuta jamaa huyu anapambana na kazi za ndoto zake….
     
    Mara Kila mmoja akawa amebadilika.
     
    Na hata lugha ikabadilika. Ukakuta watu hawaongei Tena lugha za kukatishana tamaa. Ukakuta watu wanaongea maneno ya kutiana moyo. Kila mmoja anapenda mafanikio ya mwingine.
     
    Dunia hii utakuwa nzuri sana, si ndiyo ee? Bila shaka…
    Nakuhakikishia kuanzia siku hiyo, hapa duniania hakutakuwa na vita. Hakutakuwa na marumbano..
    Watu hawatajiua wala kuwaua wengine…Naamini wasiwasi kuwa Moja ya kitu kinachofanya watu wajiue ni kwa sababu hawana ndoto, au kama wanazo basi hawazifanyii kazi, au kama wanazifanyia kazi basi wameanza TU kidogo na wamekatishwa tamaa.
     
    Lakini hicho nilichokiandika hapo ni kama stori ya Habunwasi. Haliwezi skutokea…
     
    Haliwezi kutoka kwa sababu watu wote duniania hawawezi kubadilika ndani ya siku Moja. Wanaohitaji kubadilika kwanza ni mimi na Wewe. Na baadaye watafuata watu wa karibu waliotuzunguka mimi na wewe.
     
    Ebu baada ya hapa Anza kujiambia MIMI ndiye ninapaswa kubadilika.
     
    Mimi mdiye ninapaswa kuwa na ndoto kubwa. Kuna stori kwenye Biblia kuwa Yesu (Nabii Issa) aliulizwa kuwa marafiki zako ni akina nani? Alisema marafiki zangu ni wale wanaolifuata neno la Mungu na kuliishi…
     
    Sasa na Mimi ukiniuliza kutoka moyoni kuwa marafiki zangu ni akina nani?
     
     
    Nitakujibu kwa kukwambia kuwa
    Marafiki zangu ni wenye ndoto kubwa na ambao wanaziishi hizo ndoto zao.  (kama mpaka Sasa hivi hauna ndoto kubwa, fanya kitu uwe Nayo, ili uendelee kuwa miongoni mwa marafiki zangu.
     
    Na njia zuri ya kuigundua ndoto Yako kubwa na kuanza kukifanyia kazi ni kuanza kusoma kitabu changu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO. MARAFIKI zangu wa kweli pia ni wale ambao wamesoma vitabu vyangu na wanajua vinaongelea Nini.
     
    Sikiliza, huwezi kukaa unasubiri upewe ruhusa ya kufanyia kazi ndoto yako ukaipata. Kila utakayemshirikisha ndoto yako kubwa atakuwa nay a kwake ya kusema, yupo atakayekwambia kwamba haijawahi kufanyika, mwingine atakwambia kuwa jambo kama hili haliwezekani, mwingine atakwambia kwamba halijawahi kufanyika, mwingine atakwambia kwamba, kama ingekuwa rahisi kila mmoja angekuwa anafanya na mengine…
    Ruhusa ya kufanyia kazi ndoto yako kubwa unapaswa kujipa wewe mwenyewe na siyo mwenza wako, serikali, mjomba au mtu yeyote unayemfikiria wewe…
     
    Nadhan na mimi naweza kukupa ruhusa pia, ebu  fumba macho kisha jiambie kwamba, kuanzia leo liwe jua au mvua, kiangazi au masika, nitafanyia kazi ndoto zangu…
    Kisha toka hapa nenda kafanyie kazi ndoto zako
     
     kwa leo inatosha.

    Kuna ofa ya krimasi. Unapata vitabu sita kwa elfu ishirini tu (softcopy)
    kama bado hujapata hii ofa changamka. Wasiliana nami kwa 0684408755

    Vitabu vilivyo kwenye ofa ni 


    1: VYANZO VINGI VYA KIPATO
    2: JINSI YA KUTENGENEZA MSHAHARA NJE YA MSHAHARA
    3: MWONGOZO WA WAPAMBANAJI
    4: NGUVU YA KUWEKA MALENGO
    5: NGUVU YA WAZO
    6: MAMBO 55 YA KUZINGATIA KABLA YA KUANZISHA BIASHARA

    Ukitaka vitatu kati ya hivyo, utavipata kwa 10,000/- tu.

    Kumbuka hii ni ofa ya muda mfupi tu. Ni au unalipia sasa hivi ili kupata hii 

  • Sababu Kumi Kwa Nini Haupaswi Kuongea Sana

    Unapokuwa unaongea au unawasilisha jambo lako kwa watu, usiwe mtu wa KUONGEA sana mpaka ukapitiliza.

    .jua lini unapaswa KUONGEA
    Lini unapaswa kusikiliza au kujenga hoja
    Lini unapaswa kuuliza MASWALI n.k

    Wewe kwenye mazungumzo Yako, usiongee sana. Sikiliza sana. Na hata pale unapoongea, ukigundua point unayoongea tayari watu wameshaielewa, usilazimishe kuendelea KUONGEA.

    Inatosha. Kama watu wameshaielewa pointi Yako, basi inatosha usiongee sana.

    Kamwe usiwe mtu wa KUONGEA sana kwenye mazungumzo Yako yoyote. Hizi hapa ni sababu Kumi Kwa Nini haupaswi kuwa mtu wa KUONGEA sana

    1. Kusikiliza ni muhimu: Kusikiliza kunaweza kutoa ufahamu mzuri wa mazingira na watu wanaokuzunguka.

    2. Kuepuka kutoa habari zisizo muhimu: Kuongea sana kunaweza kufichua mambo yasiyo ya lazima au yasiyo muhimu.

    3. Kuzuia kutokueleweka: Kuongea sana kunaweza kuchangia kutoeleweka vyema na kuchanganya mawazo yako.

    4. Kuheshimu muda wa wengine: Watu wengine wanaweza kuwa na majukumu mengine, hivyo ni vyema kuheshimu muda wao.

    5. **Kuepuka kuchoka wengine:** Kuongea sana kunaweza kuwachosha wengine na kusababisha kukosa hamu ya kusikiliza.

    6. Kujilinda kijamii: Mara nyingine, kutoa maelezo mengi kunaweza kusababisha kutoeleweka vizuri au hata kujionyesha sana.

    7. Kudumisha siri: Kuzungumza sana kunaweza kusababisha kutoa siri zisizo muhimu au za kibinafsi.

    8. Kujenga heshima: Kuongea kidogo mara nyingine kunaweza kuimarisha heshima yako mbele ya wengine.

    9. Kujifunza kutoka kwa wengine: Kusikiliza wengine kunaweza kutoa fursa ya kujifunza na kuboresha uelewa wako.

    10. Kusitisha ubishani usio na maana: Kuongea sana kunaweza kusababisha ubishani usio na tija au kuleta mfarakano.

    kAMA UMEIPENDA MAKALA HII, BASI UTAPENDA MAFUNZO MENGINE AMBAYO INATOA.

    Jiunge hapa

  • Ya Ngoswe Mwachie Ngoswe

    Moja ya ushauri maarufu sana ambao umekuwa unatolewa kwa watu ni ushauri wa kuwa mind your own business. Kwa lugha yetu sisi vijana wa siku hizi ni saawa na kusema kwamba pambana na hali yako.

    Yaani, kwamba achana na mabo mengine ya watu wengine halafu

    Nguvu zako

    Muda wako

    Akili yako

    Fedha zako na

    RASILIMALI ZAKO zote ziweke kwenye mambo yanayokuhusu wewe.

    Mambo ya wengine waachie na wao wapambana na mambo yao.

    Ya  Ngoswe mwachie ngoswe

    Ya Kaisari mwachie Kaisari…

    Ni mara ngapi wewe umekuwa unavunja ushauri huu? Badala ya kupambana na hali yako unapambana na hali za watu wengine.

    Unaanza kufuatilia maisha ya watu wengine,

    Wanaishije

    Wanatoka na nani

    Hali ya mahusiano yao ikoje

    AU MUDA MWINGINE UNAjiingiza kwenye mijadala isiyokuwa na ulazima wowote…

    Unaanza kujadili kati ya mtu A na B nani ana hela.

    Au kati ya fulani na fulani nani ana kipaji zaidi..

    Nani ana wafuasi zaidi kwenye mitandao ya kijamii.

    Wew haya hata uyafuatilie kiasi gani, hayakusaidii.

    Leo nataka nikurahisie tu.

    Kama kitu hakikuiuingizii pesa leo, au kama hakitakuja kukuingizia pesa siku zijazo. Usikifuatilie.

    Kama kitu siyo lengo lako kuu, usikipe muda wako

    Kama kitu siyo biashara au kazi yako, usikifanye kuwa biashara yako.

    Mimi kwa leo naishia hapo

    Kama bado hujapata ofay a vitabu sita kwa elfu 20 tu. Jua unajikwamisha. Hii ni ofa ya muda mfupi ambayo tumejadiliana na wasaidizi wangu kuwa itapaswa kuisha muda si mrefu. Kama bado hujapata hii ofa, sikiliza.

    Wasiliana na 0684408755 (whatsap/sms/simu). Kisha mwambie akupe ofa ya vitabu sita.

    Fanya hivyo haraka iwekezakavyo kabla ofa haijafungwa.

    Niliyekuandikia makala ya leo naitwa Godius Rweyongeza

    Nipo Morogoro nchini Tanzania

  • Vitu Vikubwa Vitano nilivyojifunza kuhusu MAISHA na biashara

    Rafiki yangu siku ya Leo Nina ujumbe mmoja TU kwako. Kama una kitu ambacho Wewe mwenyewe unafanya, na unajua kitu hicho kitaleta mabadiliko, mapinduzi au kitasaidia watu basi.

    1. Kifanye kwa moyo wako wote
    2. Jitume na kifanye kwa bidii sana kiasi kwamba hakuna mwingine anayeweza kukifanya kama Wewe
    3. Kifanye Kila siku bila kuacha na kwa muda mrefu bila kuacha.
    4. Usikifanye mara Moja TU, kisha ukasema sioni matokeo. Kifanye mara kwa mara na kwa muda mrefu bila kuacha.
    5. Jitahidi Kila mara kuhakikisha unawafilia watu wapya ambao mwanzoni ulikuwa hujawafikia.

    Nakuhakikishia ukifanya haya mambo matano, kwa uhakika, kwa msimamo na bila kuacha. Sharti utaona TU matokeo.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza
    Kujifunza zaidi kutoka kwake jipatie nakala za vitabu vyake. Unaweza kupata nakala hizi kwa kuwasiliana naye kwa 0684408755.

    karibu sana

  • Kosa Kubwa Ambalo Watu Wengi Hufanya

    Kwenye maisha kuna makosa ambayo watu huwa wanafanya. Ila hupaswi kufanya makosa ya nanma hii mengi, maana kadiri unavyofanya makosa haya mengi, maana yake unakuwa unajiuzuia ile nafasi yaw ewe kusonga mbele na kuweza kfuanya makubwa zaidi. Sasa unajua ni kosa gani kubwa ambalo watu hufanya?

    Kutojifunza baada ya kumaliza chuo.

    Ile baada ya mtu kuhitimu na kurusha kofia juu, ndiyo anakuwa amerusha kila kitu. Yaani, hataki tena masuala ya kusikia sijui kuna vitabu au kitu gani. Ukweli ni kuwa kama unataka kufika mbali kwenye maisha kusoma kunapaswa kuwa sehemu ya maisha yako.

    Nani amekwambia kwamba, ukijifunza kitu kimoja tu mara moja tu ndiyo unakuwa umebobea. Unapaswa kuendelea kujifunza kila siku bila ya kuacha. Kila siku, ya maisha yako iwe ni siku ya kujifunza.

    Kiukweli ili ufanikiwe kwenye maisha unahitaji zaidi ya elimu ya darasani. Unahitaji kujifunza vitu vingi. Unahitaji kujifunza biashara, unahitaji kujifunza mauzo, unahitaji kujifunza kuongea mbele ya watu, unahitaji kujifunza uandishi na mengine mengi.

    Soma na jifunze mara kwa mara. Iwe ni kupitia vitabuni, iwe ni kupitia kozi ambazo unaweza kusoma mtandaoni, kozi za kwenda sehemu na njia nyinginezo.

    Ningependa nimalizie makala ya leo kwa nukuu inayosema kuwa, mtu ambaye hasomi, ni mzee hata kama bado ana miaka 20 na mtu ambaye anasoma na kujifunza ni kijana hata kama ana miaka 80.

    Uwe na siku njema.

X