-
Kuandika ni Kutunza Kumbukumbu
Marcus Aurelius alikuwa na utaratibu wa kuandika kwenye notebook (tuiite hivyo) kila siku. Kila siku aliandika kitu alichojifunza, iwe ni kitabuni au kutoka kwa watu aliokutana au katika vyanzo vingine.
Kile ambacho mwanzoni alikuwa anaandika kwa ajili yake, baadaye kilikuja kuonekana ni cha msaada mkubwa, mpaka maandiko yake yakakusanywa kwenye kitabu kimoja ambacho leo hii kinafahamika Kama Meditations.Huwa napenda kuwaambia watu kuwa kwenye maisha haya kila mmoja ana jambo lake anaweza kuandika kwa ajili yake mwenyewe, familia, au hata kwa ajili ya wengine.

Naomba unisikilize rafiki yangu. Huhitaji kuwa Reginald Mengi ili uandike kitabu chako.
Inawezekana watoto wako tu kuna vitu hawajui kuhusu wewe. Sasa itakuwaje,
Hilo mimi nina uhakika nalo.
UNAPOANDIKA KITABU, unatoa nafasi ya mambo yako na historia kuendelea kujulikana kwa urahisi hata kwa miaka mingi ijayo.
Mimi nina uhakika, sambamba na mali zote utakazoacha, moja ya kitu ambacho wajukuu wako watajivunia, ni kitabu utakachokuwa umeandika. Mfano, kama mimi babu yangu angekuwa ameandika kitabu. Ningekuwa naringa sana hapa mjini. Kwanza historia yake ambayo huwa nasimuliwa nusunusu kila siku, ningeipata kwa ukamilifu bila chenga. Hili lingekuwa ni jambo zuri sana kwangu.

Mfano mdogo tu, tuchukulie historia yako. Kuna watu huwa wanafikiria kwamba ili aandike historia ya maisha yake anapaswa kuwa maarufu sana. Wengi hutolea mfano wa Mengi au Mkapa na kuonesha kwamba wanapaswa kuwa kwenye viwango hivyo ili waandike vitabu.


Wewe pia itakuwa hivyo endapo hutaandika kitabu. Wajukuu wako watakuwa wanahadithiwa historia kidogo kidogo. Vistori ambavyo havina kichwa wala miguu na hivyo hawataweza kujua historia yako kamili. Ila kama utakuwa umeiandika, wataiona kwa uzuri.

Hivyo, fikiria kuhusu kuandika kitabu cha historia ya maisha yako mara moja.
Sasa kama ungependa kupata mwongozo wa kuandika kitabu
Usimamizi
au hata kuandikiwa kitabu chako
Nitumie namba yako ya simu sasa hivi ili tuweze kuwasiliana.
Tuma namba yako ya simu kwa kujibu email hii. Asante sana -
Mafanikio Katika Biashara
Ili uweze kufanikiwa katika biashara yako kuna mbinu na hatua za kufuata. Ndani ya ebook hii kuna mbinu na hatua madhubuti za kuzingatia katika mafanikio ya biashara yako. Soma kupitia hapa

Zingatia mambo yafuatayo
soma zaidi; Kitu Kinachofanya Mabadiliko Kuwa Magumu Kwenye Biashara Yako
-
Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuongez Kujiamini
Rafiki yangu mpendwa, watu wengi wamekuwa wanahangaika sana na kujiamini. wengi huwa wanakosa kujiamini hasa wanapokuwa mbele ya watu. Kwa kulifahamu hilo, nimeandaa ebook fupi yenye suluhisho juu ya hili tatizo ambalo limekuwa linawakumba watu wengi. Ebook hii unaweza kuipata kirahisi sana kupitia link hii hapa
BONYEZA HAPA KUPATA EBOOK yako
Asante sana
-
Ushauri wa Bilionea Pavel Durov Kuhusu Kozi Ya Kusoma Chuo
Pavel Durov ambaye ni bilionea na mwanzilishi wa telegram kwenye channel yake ya telegram ametoa ushauri kwa wanafunzi ambao wanatafuta kitu gani cha kusoma.
Anasema hivi,
Ikiwa wewe ni mwanafunzi unayechagua nini ubobee, basi chagua HESABU. Itakufundisha kutegemea akili yako mwenyewe bila kuchoka, kufikiri kwa mantiki, kugawa matatizo vipande vipande, na kuyatatua hatua kwa hatua kwa mpangilio sahihi. Huo ndiyo ujuzi wa msingi utakaohitaji kujenga kampuni na kusimamia miradi. 
Huu ni moja ya ushauri muhimu sana hasa ukizingatia bilionea huyu ni mwanzilishi wa kampuni kubwa na kabla ya hii aliwahi kuanzisha kampuni nyingine.
Bilionea huyuhuyu siku za nyuma aliwa kusema kwamba wachina wanafanya vizuri kwenye sekta nyingi kwa sababu hesabu wamezipa kipaumbele kwenye mfumo wao wa elimu na hivyo akawa anashauri nchi mbalimbali kuiga mfumo wa elimu wa china
WEWE UNA MAONI KUHUSIANA NA HIKI ANACHOSEMA DUROV?
-
Jinsi Ya Kuandika Kitabu Kirahisi Hata Kama Uko Bize

Kuandika kitabu ni ndoto ya watu wengi, lakini mara nyingi hukwamishwa na sababu moja kubwa: “Sina muda.” Lakini je, kweli muda ni kikwazo au ni kukosa mbinu sahihi za kutumia muda tulio nao? Siku za nyuma nimewahi kuandaa video YouTube yenye kichwa cha “Jinsi ya kuandika kitabu kirahisi hata kama uko bize”, kama hujawahi kuiangalie itazame tena hapa. Ila kwa Leo ningependa nikushirikishe haya.
- Una dhamira ya kuandika kitabu?
Kabla hujashika kalamu au kufungua kompyuta, jiulize: Kwa nini ninaandika kitabu hiki? Je, ni kushirikisha uzoefu, kufundisha, au kujenga chapa binafsi? Dhamira hii itakusaidia kusimama imara hata pale unapokuwa umechoka au ratiba imekuwa ngumu.
2. Tumia Muhtasari (Outline) Kama Ramani
Unapokuwa bize, huwezi kuanza kila siku na wazo jipya. Njia bora ni kuandika muhtasari wa sura zako kabla hujaanza kuandika. Hii ni kama ramani ya safari. Inakuokoa muda na inakusaidia kujua ni wapi pa kuanzia kila siku.
Mfano:
- Sura ya 1: Historia yangu
- Sura ya 2: Changamoto kubwa niliyokutana nazo
- Sura ya 3: Mafanikio yangu ya kwanza
Na kuendelea…
unaweza kupata msaada zaidi wa hili kwa kusoma kitabu Cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU. Kupata nakala Yako, wasiliana NAMI Sasa kwa 0655848392. Karibu sana.
3. Andika Kidogo Kidogo Lakini Kila Siku
Uandishi wa kitabu si lazima uwe kazi ya siku nzima. Unaweza kuandika maneno 200–500 kila siku, hata ukiwa unasubiri foleni au mapumziko kazini. Ukiandika maneno 300 kwa siku, kwa wiki utakuwa na zaidi ya maneno 2,000. Hiyo ni karibu sura moja!
Mbinu nzuri:
- Chagua saa moja maalum kwa siku (mfano, kabla ya kulala au asubuhi kabisa)
- Weka alama ya “niliandika leo” kwenye kalenda yako
4. Andaa ‘Draft ya Kwanza’ Isiyo Kamili
Unapokuwa bize, jaribu kujizuia kutaka ukamilifu kwenye awamu ya kwanza. Lengo la awali ni kuandika maudhui Yako. Suala Zima la kurekebisha na kusahihisha ni kazi ya baadaye. Hivyo basi, Kuwa mwepesi kuandika, mzito kuhukumu.
5. Tumia Teknolojia Kukusaidia
Siku hizi kuna zana nyingi zinazoweza kusaidia watu walio bize:
- Voice-to-text apps (zungumza badala ya kuandika)
- Note-taking apps kama Google Keep, Simplenote na notes
- Kuandika kwenye simu wakati unasafiri au unasubiri huduma
6. Kumbuka: Huwezi Kumaliza Kitu Usichoanza
Usisubiri hadi uwe na muda mwingi. Hakuna wakati “kamili” wa kuanza kuandika. Wakati ni sasa. Uandishi ni safari inayohitaji hatua moja kila siku.
Ukiwa bize haina maana huwezi kuandika kitabu. Unachohitaji ni mbinu, dhamira, na nidhamu. Kwa kuandika kila siku hata kidogo, kwa kutumia muhtasari, na kwa kuweka akilini kwamba ukamilifu huja baadaye, unaweza kuandika kitabu kizima ndani ya miezi michache tu.
Je, umekuwa ukiota siku moja kuandika kitabu? Usingoje tena. Anza leo hata kama ni kwa aya moja tu. Kwa msaada zaidi sisi Songambele Consultants tunaweza kukushauri kwenye mchakato mzima WA kuandika kuhariri na kuchapa kitabu chako
Tuwasiliane kwa kutumia simu 0755848392
Tazama video kamili hapa:
📺 Jinsi ya Kuandika Kitabu Kirahisi Hata Kama Uko BizeImeandikwa na GODIUS RWEYONGEZA
-
Nini Cha kufanya unapokutana na changamoto.
Hongera sana kwa kuendelea kupambana rafiki yangu.
Kwenye MAISHA Kuna wakati mambo yanakuwa yanaenda ndivyo sivyo. Mipango Yako unaenda kinyume na matarajio Yako.
Leo ningependa nikwambie tu, inapotokea mipango Yako umependa kinyume, fahamu kuwa
1. Unapaswa kukaa chini na kujitafakari upya. Kushindwa au kuanguka si KITU kibaya, ubaya ni pale unapokataa kukaa chini na kujifuñza kutokana na kushindwa huko. Hivyo Kaa chini ujitafakari, umeshindwa wapi? Kwa Nini umeshindwa? Ni KITU Gani unaweza kufanya ili utoke hapo na kwenda HATUA ya ziada? Tumejifunza Nini?
2. Panga upya. Kila unapojitafakari, panga upya, uone ni HATUA Gani zaidi utachukua baada ya hapo? Ni nini unaenda kufanya baada ya hapa?
3. Chukua HATUA kimkakati zaidi? Baada ya kuwa umeanguka, tayari umeshajua wapi umekosea, kinachofuata ni wewe kuanza kufanyia kazi malengo Yako kimkakati zaidi?
4. Jifanyie tathimini Kila mara. Kila mara jifanyie tathmini kuona mwenendo wako. Uko wapi, unaelelea wapi na Nini zaidi tunafanya.Imeandikwa na Godius Rweyongeza
0755848391
-
Salaam za semina na pongezi kutoka kwa washiriki wote wa semina wa biashara na Uwekezaji 2025

Rafiki yangu mpendwa, salaam. Leo ningependa tu kukutaarifu kuwa semina yetu ya biashara na Uwekezaji imeweza kufanyika kwa kishindo kikubwa sana.
Semina hii ya pekee imefanyika tarehe 28 na 29 kwenye ukumbi wa KINGSWAY HOTEL MOROGORO MJINI
Washiriki wametoka pande mbalimbali za Dunia kuja hapa Morogoro kujifuñza maarifa sahihi ya biashara na Kila KITU kimekwenda kama kilivyokusudiwa.

Kwa Leo ningependa nikudokeze VITU 10 tu kuhusiana na semina hii
- Tumejifunza kuhusu Kuweka malengo binafsi na ya biashara na njia Bora ya kuyafanyia kazi. Huku tukiona kwamba njia ya kufanyiia kazi malengo kwa wiki 12 badala ya miezi 12 ni Bora zaidi.

- Tumejifunza kuhusu masuala yote yanayohusiana na kampuni, HATUA zote za usajili, Faida na hasara za kuwa na kampuni. Na mengine mengi mazuri kuhusu kampuni
- Tumejifunza kuhusu elimu ya Kodi. Hii ni elimu adimu ambayo siyo rahisi kuipata, ila sisi tumeipata. Masuala yote yanahohusiana na ulipaji wa Kodi, sasa tunayafahamu vizuri sana.
- Tukaona isiwe kesi, tukaendelea mbele zaidi kujifuñza namna ya KUANZISHA BIASHARA ya pamoja kama wenza. Hivi hiki kitu kinawezekana, na kama kinawezekana kivipi? Kwa maarifa tuliyoondoka nayo, tuna uhakika wa KUANZISHA BIASHARA kama wenza bila wasiwasi wowote.
- Tumebadilishana mawazo, tumekonekti, tumeshauriana, tumeelekezana Nini Cha kufanya kwenye biashara zetu. Kila mmoja sasa ameondoka na mwongozo kamili wa kufanyia kazi. Na Bado tutakuwa wote kwa kipindi Cha mwaka mmoja ujao tukizidi kupambana zaidi kuelekea kwenye malengo yetu.

- Tumejifunza kuhusu masuala ya benki, tumepata konekisheni za kibenki kutoka kwa watalaam.
- Lakini sote tunajua wazi kuwa wakati tunaendelea kupambana na mambo MAKUBWA na biashara ni vizuri pia kuwaandaa watoto kwa ajili ya hiyo baadaye. Tulichokifanya ni kwamba tumejifunza pia namna ya kuwaandaa.
- Biashara Zina misingi yake, namna ya kuziendesha, Kuweka MIFUMO imara na kujenga timu Bora. Hivi ni VITU vya Msingi sana ambavyo tumeweza kujadiliana kwa kina kwenye semina hii.
- Utt amis wameungana nasi kwenye semina hii kutufundisha Uwekezaji kwenye taasisi hii ya UTT AMIS. Mambo yamekuwa ni moto🔥
- Kuagiza mizigo china, ni KITU ambacho watu wengi wangependa kujifuñza. Tumeona hili kwa undani pia
Kiukweli tunekuwa na siku mbili Bora sana hapa duniani. Tumezitumia vyema
Kujitafakari,
Kujipanga upya
Na sasa tupo tayari kusongambele

NB: Kama hukushushiriki semina na ungependa kuendelea kupata mafunzo haya yote. Habari njema ni kwamba mafunzo haya yote yanapatikana. Tutapata video zote za mafunzo. Utalipia 50,000/- tu BEI YA OFA. Cha kufanya wasiliana NAMI kwa 0755848391 sasa Ili tuweze kuanza kufanyia kazi haya pamoja.
-
Jinsi ya kuchagua Watu Sahihi na Vitabu Sahihi Kwa Maendeleo Yako Ya Miaka Mitano Ijayo
Katika makala ya jana rafiki yangu. Niliandika Siri ya Mabadiliko ya Kweli. Miaka Mitano Ijayo Utakuwa Jinsi Ulivyo Isipokuwa Kwa Vitu Hivi Viwili. Baada ya kuelewa kuwa watu unaokutana nao na vitabu unavyosoma vina mchango mkubwa katika kukufanya mtu tofauti baada ya miaka mitano, swali linalofuata ni: unawachaguaje watu sahihi? Na unachaguaje vitabu vitakavyokujenga kweli?
Hii si kazi ya kubahatisha. Ni mchakato unaohitaji umakini, nidhamu, na maamuzi ya makusudi. Makala hii inakuonyesha njia ya kuchagua vyanzo hivi viwili vya mabadiliko ili kuimarisha safari yako ya mafanikio.
1. Jinsi ya Kutambua Watu Sahihi wa Kukua Nao
Kila mtu anayekuzunguka ana athari katika namna unavyofikiri na kutenda. Ili ukue:
a) Tafuta Watu Wenye Maono na Nidhamu
Watu wanaojitambua na wenye mwelekeo wa maisha hukupa msukumo wa kufanya makubwa. Hawapotezi muda kwenye manung’uniko au visingizio. tafuta watu wa namna hii rafiki yangu.
b) Watafute Waliofika Unakotamani Kufika
Kama kuna watu wamefikia mafanikio na hatu ambayo wewe unatamani kuwa umefikia, hawa ni washauri wa kweli. Wanaweza kuwa wafanyabiashara waliobobea, viongozi wa kiroho, au hata walimu wa kawaida lakini wenye hekima ya maisha. Ukiwapata watu wa namna hii kamwe usiwaachie, washikilie na uende nao ili wakusaidie kuweza kufikia ndoto zako kubwa.
c) Jihadhari na Watu Wanaopunguza Ndoto Zako
Wapo watu ambao kila mara huona sababu ya kwa nini jambo haliwezekani. wanadogosha lengo lako na ndoto zako. Wanaeneza hofu na mashaka. Epuka kuwaruhusu wawe sauti kuu katika maisha yako. Kumbuka kwamba ukikaa na waridi lazima utanukia. Sasa kazi ni kwako kuhakikisha kwamba unachagua waridi linalokufaa. La sivyo yeyote utakayechagua atakuwa sehemu ya maisha yako.
d) Jiunge na Mitandao ya Ukuaji
Kuna vikundi vya watu wanaojifunza pamoja – iwe ni vikundi vya kusoma, vya maadili ya kazi, au vya ujasiriamali. Huko ndiko mahali pa kukutana na watu sahihi.
2. Mambo ya Kuzingatia Katika Kuchagua Vitabu vya Kujenga Maisha Yako
Vitabu ni marafiki wasiochoka kukuinua. Lakini si kila kitabu kinajenga. Ili upate thamani:
a) Soma Vitabu Vinavyoendana na Malengo Yako
Kama lengo lako ni kuimarika kifedha, soma vitabu vya fedha. Kama unataka kuimarika kiroho, tafuta vitabu vya kiroho. Usisome tu kwa sababu “kila mtu anasoma.” Kumbuka vitabu vipo vingi na siyo vitabu vyote vinakufaa wewe. Kitabu ambacho kinasomwa na mwingine kinaweza kisiwe kizuri kwako, ndiyo maana wewe mwenyewe unapaswa kuwa mtu wa kuchagua kwenye hili suala.
b) Angalia Waandishi Wenye Matokeo Yanayoonekana
Soma vitabu vilivyoandikwa na watu walioishi kile wanachofundisha. Mfano: Mwandishi wa kitabu cha biashara ambaye ana biashara hai, au mshauri wa ndoa mwenye ndoa yenye afya.
c) Usipuuze Vitabu vya WASIFU NA TAWAFIFU (Biographies)
Kusoma maisha ya watu waliopitia magumu na kufanikiwa hukufundisha hekima ya kipekee isiyopatikana darasani. Wasifu wa watu kama Nelson Mandela, Wangari Maathai, Steve Jobs au Elon Musk unaweza kuwa chachu ya mafanikio yako. Hakikisha vitabu vya namna hii unakuwa navyo vingi na uvisome mara kwa mara. Anza na hiki hapa chini kwa kuwasiliana nami kwa 0755848391 au 0684408755 sasa

d) Kuwa na Mpango wa Kusoma
Chagua angalau kitabu kimoja kwa mwezi, ukigawanya kwenye ratiba ya kila siku. Ni bora usome kurasa 10 kwa siku kwa nidhamu, kuliko kusoma kurasa 100 mara moja kisha ukaacha. Ukiweza kusoma kurasa kumi kila siku kwa mwezi utakuwa umeweza kusoma kurasa 300 kwa mwezi. Hii ndiyo kusema kwamba kila mwezi utakuwa unaweza kumaliza kitabu kimoja. Kwa mwaka utakuwa umeweza kumaliza vitabu siyo chini ya 12. Kwa hakika utakuwa unaweza kupiga hatua kubw aukilinganisha na asilimia kubwa ya watu ambao huwa hawasomi vitabu.
3. Chukua Hatua Leo: Unda Mazingira ya Mabadiliko
- Fanya orodha ya watu watatu unaopaswa kuwasogelea kwa ajili ya kujifunza kutoka kwao.
- Andika vitabu vitatu unavyotamani kusoma ndani ya miezi mitatu ijayo.
- Anza sasa – usingoje “wakati mzuri.” Mabadiliko huanza pale mtu anapochukua hatua ya kwanza.
Watu sahihi ni daraja la mafanikio yako. Vitabu sahihi ni ramani ya safari yako. Usisubiri miaka mitano ikupite ukiwa bado palepale. Chagua kwa makusudi marafiki wa kukuinua na maarifa ya kukujenga.
Kwa hiyo, swali ni hili:
Leo unamruhusu nani akuathiri, na unasoma nini kila siku?
Je, ungependa mapendekezo ya vitabu bora au njia za kuwapata washauri wa kukuinua? Acha maoni yako au tuandikie kupitia songambele.smb@gmail.com tungependa kusaidia safari yako ya ukuaji.
-
Siri ya Mabadiliko ya Kweli. Miaka Mitano Ijayo Utakuwa Jinsi Ulivyo Isipokuwa Kwa Vitu Hivi Viwili
Katika safari ya maisha, watu wengi hutamani kubadilika, kuboresha maisha yao, na kufikia mafanikio makubwa. Lakini wengi hukata tamaa baada ya miaka kupita bila kuona tofauti kubwa. Swali ni: kwa nini baadhi hubadilika na kupiga hatua, huku wengine wakibaki vilevile?
Msemaji na mwandishi maarufu, Charlie “Tremendous” Jones, alitoa kauli yenye nguvu sana:
“Miaka mitano kuanzia sasa, utakuwa mtu yule yule wa leo isipokuwa kwa watu uliokutana nao na vitabu ulivyosoma.”
Hii si tu kauli nzuri ya motisha ni kanuni ya maisha. Inatufundisha kuwa mabadiliko ya kweli hayatokei kwa bahati, bali kwa maamuzi ya kila siku ya kujifunza na kujizunguka na watu sahihi.
1. Watu Uliokutana Nao: Msingi wa Ukuaji wa Kijamii na Kiakili
Watu tunaowaruhusu kuingia kwenye maisha yetu wanaweza kutuinua au kutuvuta chini. Marafiki, washauri, wakosoaji, na hata wapinzani wote huathiri namna tunavyofikiri, tunavyoongea, na tunavyotenda.
- Kukutana na mtu mwenye maarifa kunaweza kufungua milango ya fursa mpya.
- Mshauri mzuri anaweza kukuokoa na makosa ambayo yangegharimu miaka ya maisha yako.
- Rafiki mbaya anaweza kuchelewesha ndoto zako kwa kukushawishi kushughulika na mambo yasiyo na maana.
Jiulize: Ni watu wa aina gani nimewakaribisha katika maisha yangu? Wananisaidia kukua au wananikandamiza?
2. Vitabu Ulivyosoma: Mbegu za Mabadiliko ya Akili
Kitabu kizuri kinaweza kubadilisha fikra zako milele. Kinaweza kukuamsha toka usingizini wa kiakili na kukuonyesha namna mpya ya kuona dunia. Kusoma ni kama kuzungumza na watu wakuu ambao huenda huna nafasi ya kukutana nao ana kwa ana.
- Kitabu cha kifedha kinaweza kukuonyesha namna ya kutoka kwenye madeni.
- Kitabu cha motisha kinaweza kukuamsha uanze kuchukua hatua ulizokuwa unahofia.
- Kitabu cha maarifa kinaweza kukufanya kuwa mtaalamu katika eneo fulani na kukuongezea kipato.
Jiulize: Ni vitabu gani vimenisaidia hadi sasa? Na ni vitabu gani ninahitaji kuvipitia ili kufikia ndoto zangu?
3. Chukua Hatua: Fanya Uchaguzi wa Kukua
Usingoje miaka mitano ipite bila mabadiliko. Anza leo kwa:
- Kutafuta watu chanya wanaokutia moyo, wanaojua zaidi yako, na wanaotamani kuona unafanikiwa.
- Kujipangia mpango wa kusoma angalau kitabu kimoja kila mwezi. Hata ukianza na kurasa chache kwa siku, utaona matokeo.
Miaka mitano si mbali. Itafika, iwe umebadilika au la. Swali ni: utakuwaje baada ya miaka hiyo? Utakuwa mtu mpya, mwenye fikra kubwa, malengo makubwa, na hatua kubwa au utakuwa bado unalalamikia maisha yale yale?
Jibu liko mikononi mwako. Anza leo kukutana na watu sahihi na kusoma vitabu bora. Hapo ndipo mabadiliko ya kweli huanzia. Na kama unataka kupata vitabu vya kweli vya kubadili maisha yako. Tuwasiliane sasa kupitia 0755 848 391 au 0684408755
Pia nichukue nafasi hii kukukaribisha kwenye channel yetu ya telegram ambapo naweka makala mpya kila siku ambazo unaweza kuzitumia kujifunza na kuchukua hatua. Jiunge na channel yetu hapa.
Je, upo tayari kuwekeza katika mabadiliko yako?
Tuandikie vitabu gani vimekugusa au ni watu gani wamekuwa chachu ya mafanikio yako. Tunapenda kusikia kutoka kwako! Tuandikie kwenye email ya songambele.smb@gmail.comPia usisahau kujiunga na semina yetu ya mwezi huu wa sita ambayo itafundisha mambo mengi kwa undani.
-
Kama haliwezekani kwao, haimaanishi kwamba haliwezekani kwako
Rafiki yangu jambo ambalo watu wengine wanafikiri kwamba haliwezekani kwako siyo kwamba haliwezekani bali linawezeakana. Inawezekana jambo hilo haliwezekani kwao, lakini siyo kwamba haliwezekani kwako. Hivyo, basi zamu ijayo ukisikia mtu anakwambia kwamba jambo hilo haliwezekani, basi jua kwamba linawezekana vizuri tu.
Leo nimekuandallia ebook nzuri sana kuhusu hili suala la kuwezekana. Naomba uisome hapa.