Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • Usitafute ukamilifu mwanzoni mwa kuandika Kitabu Chako, tafuta kuanza

    Lakini ninachoandika mbona siyo kizuri, anajiuliza mmoja wa waandishi. Ukweli ni kuwa wewe mwanzoni Anza kuandika TU, andika hata kama mwanzoni huoni huo uzuri. Baadaye utaboresha

  • Usisubiri Uwe na Muvi Kichwani Ili uandike kitabu chako. Una mengi ya kuandika leo

    Anayekwambia kwamba usubiri mpaka uwe na muviq kichwani Ili uandike kitabu chako anakudanganya. Wewe hapo ulipoq na ninavyokuona wewe una mengi ya kuandika

    • elimu Yako
    • uzoefu wako
    • utalaam wako
    • kitu unachopenda kufuatilia
    • changamoto zinazoikumba jamii Yako
    • Kitu unachopenda kufuatilia
    • changamoto zinazoikumba jamii
    • na mengine mengi

    haya yote yanaweza kuwa chanzo Cha wewe kuandika na kukamilisha kitabu chako.

    Kila la kheri

    kupata usimamizi au msaada wa kuandika Kitabu Chako tumia 0678 848 396

  • Aina Tano Za Uwekezaji Ambazo Unaweza Kufanya Leo Hii, Zikakupa Faida Hapa Duniani Na Hata Pale Uakapokuwa Umetangulia Ahera

    Kuna aina za uwekezaji ambazo unaweza kufanya leo hii, zikaweza kukuletea faida ukiwa hapa duniani, hata itakapofika hatua ukatangulia mbele ya haki, bado utakuwa unaengeneza faida hapa duniani. Unajua aina hizi za uwekezaji ni zipi?

     

    Aina ya kwanza ni uwekezaji kwenye hisa

    Kama utachagua aina nzuri ya uwekezaji na ukaufanya kwa msimamo, nakuhakikishia kuwa utatengeneza faida ukiwa hapa duniani, na uaengeneza faida ukiwa ahera. Kiufupi ni kwamba wale watu utakaokuwa umewaacha, wataendelea kupata gawio kwa siku nyingi sana hata baada yaw ewe kuwa umetoka hapa duniani.

    Uwekezaji kwenye hisa ni njia nzuri ya kutengeneza faida ukiwa hapa duniani. Unapowekeza katika hisa za kampuni ambazo zina faida, unaweza kupata gawio la faida na pia thamani ya hisa zako inaweza kuongezeka kwa muda. Hata baada ya wewe kufariki, wale walioachiwa urithi wako wanaweza kuendelea kupata gawio na faida kutokana na uwekezaji huu.

     

     

    Aina ya pili ni uwekezaji kwenye vipande.

    Vipande au mutual funds ni njia nyingine bora ya uwekezaji. Kwa kuwekeza kwenye vipande, unakuwa unachangia kwenye mfuko ambao unawekeza kwenye hisa na dhamana mbalimbali. Hii ni njia nzuri ya kupunguza hatari na kuongeza faida. Faida zinazopatikana zinaweza kuendelea hata baada ya kifo chako, na hivyo kuwanufaisha warithi wako.

    Kama ulivyo uwekezaji kwenye hisa. Uwekezaji kwenye vipande na hasa utt amis, ni sehemu nzuri sana ambayo itakuwezesha kuengeneza faida hapa duniani. Na haa baada ya  ya wewe kuwa umeaga dunia, wau utakaowaacha hapa duniani, wataendelea kuengeneza faida kwa siku nyingi zitakazofuata.

     

    Aina ya tatu ni uwekezaji kwenye hatifungani.

    Na hasa hatifungani za serikali. UNAJUA KWA NINI? KWA sababu ni ukweli kuwa serikali haiwezi kuffilisika na hata kuacha kuwalipa wananchi wake. Hivyo, ukiwekeza kwenye hatifungani za serikali maana yake utaweza kupata  faida ukiwa bado hapa duniani, lakini habari njema zaidi ni kwamba, kama utaaga dunia, basi uwekezaji wako bado utaendelea kuwanufaisha wale autakaokuwa umewaacha.

    Aina ya nne ni ya uwekezaji ni uandishi wa kitabu. Kitabu ni kitu kingine ambacho kama utakifanya, kitakufanya upate faida hapa duniani, lakini pia hata baada ya kuwa umetoka hapa duniani, bado utaendelea kuengeneza faida zaidi.

    Kuandika na kuchapisha vitabu ni uwekezaji wa kipekee. Vitabu vinaweza kuuza kwa muda mrefu na kuleta mapato kupitia mauzo na mirabaha. Ikiwa kitabu chako kitakuwa maarufu, kitaleta faida kwa muda mrefu, hata baada ya wewe kufariki, na faida hizi zinaweza kuendeleza familia yako au mirathi yako.

     

    Aina ya tano ni uwekekezaji kwenye katika Mali Isiyohamishika

    Kununua ardhi au majengo ni uwekezaji thabiti ambao una faida ya muda mrefu. Thamani ya mali isiyohamishika kawaida huongezeka kwa muda, na unaweza kupata mapato ya kodi kama ukiamua kupangisha. Hata baada ya wewe kuondoka duniani, mali hizi zinaweza kuendelea kuleta faida kwa warithi wako.

    Aina ya sita ni Uwekezaji katika Biashara

    Kuanzisha na kuendesha biashara yenye faida ni njia nzuri ya kutengeneza kipato kikubwa. Biashara inaweza kuendelea kuendeshwa na warithi wako na kuleta faida kwa muda mrefu hata baada ya wewe kufariki. Kumbuka hapa biashara ninayoongelea siyo hizi biashara nyingi ambazo zimekuwa zinafanywa kwa mazoea na watanzania walio wengi. Bali ni biashara ambazo zinajiendesha zenyewe kwa faida kubwa.

    Aina ya saba ni uwekezaji kwenye elimu ya watoto.

    Kwa kuwa watoto wako ndiyo watakuwa wanaendesha hivi vitu na wanapaswa kuendelea kuviendesha kwa siku nyingi zinazokuja, basi unapaswa unapaswa kuwajengea msingi mzuri wa kujifunza  na kuwap elimu sahihi. Ili kazi yako kubwa isiishie tu kwenye kuanzisha hivi vitu, bali watoto wako waweze kuendelea kuendesha hivi vitu kwa siku nyingi zinazokuja.  Hivyo wajengee sehemu sahihi.

     

    Hizi aina za uwekezaji ni uhakika, zitakupa faida ukiwa hapa duniani na hata baada ya kuwa umeaga dunia. Kwa kuchagua uwekezaji mzuri na kwa kufanya maamuzi ya busara, unaweza kuhakikisha kuwa una faida hapa duniani na pia baada ya kuondoka duniani, wale unaowaacha wanaweza kufaidika kwa muda mrefu pia.

    Makala hii imeandikwa n Godius Rweyongeza

    Kujifunza zaidi kuhusiana na aina hizi mada ambazo nimeeleza hapa. Hakikisha unapata nakala mbil za vitabu. Kwanza ni kitabu cha maajabu ya kuwekeza kwenye hisa, hatifungani na vipande pamoja na kitabu cha Jinsi ya kuw amwandishi mbobevu.

    Kupata nakala yako ni rahisi sana. Lipia 25,000 ambayo ni gharama ya kila nakala. Tuma kwa 0684 408 755 ili uweze kutumiwa nakala yako. Baada ya kufanya malipo, tafadhali wasiliana na namba hiyo hiyo kwa ajili kufanya utaratibu wa kutumiwa vitabu vyako.

     

     

  • Gharama ya uandishi wa kitabu ni uwekezaji. Hii hapa ni sababu Kwa Nini?

    Gharama unayotumia mwanzoni kwenye kuandika Kitabu Chako, ni uwekezaji.

    Kitabu kikishakamlika.
    Kitaendelea kuwepo maisha yako yote na hata baada ya wewe kuaga Dunia.

    Uandishi wa kitabu ni kazi unayofanya mara Moja ila unalipwa maisha yako yote.

    Hata baada ya kufa, kitabu kinakutengenezea faida ukiwa duniani na hata ukiwa ahera.

    Godius Rweyongeza 

    +255755848391

  • Muda wa kuandika Kitabu unausubiri utoke wapi?

    Utasikia mtu anakwambia nasubiri siku niwe na muda wa kutosha Ili niandike.

    Sikiliza. Tena sikiliza vizuri. Muda wa kutosha haupo.
    Hakuna mwandishi mwenye muda wa kutosha.
    Kila mwandishi yuko bize.

    Ila muda mchache TU anaopata anaandika. Hata wewe Fanya hivyo.

    Kusubiri muda wa kutosha Ili uandike kitabu chako ni uongo. Hatusubiri tuwe na muda wa kutosha Ili tule, hatusubiri tuwe na muda wa kutosha Ili tuonge. Hata kama tuko bize, tutatafuta muda TU Ili tule na kuoga

    Sasa inakuwaje tunasubiri muda wa kutosha Ili TUANDIKE? Tunasubiri muda huu utoke wapi?

    www.songambele.co.tz

  • Ile kozi fupi inayokuelekeza namna ya kupakua vitabu mtandaoni hii hapa

    Habari ya leo rafikii yangu, umeshaipata ile kozi fupi ambayo inakuelekeza hatua kwa hatua namna ya kupakua vitabu mtandaoni?

    Kama hukupata hii kozi, muda wako mzuri wa kuipata ni sasa.

    Unaweza kuipata sasa.

    Itakusaidia wewe kuweza kupakua kitabu chochote kile mtandaoni. Itakusaidia wewe kuondokana na hali ya kulipia kila kitabu kila unapokihitaji.

    Utalipia mara moja na kutulia. na utaweza kupakue maelfu kwa maelfu ya vitabu.

    KOZI HII FUPI GHARAMA YAKE NI  10,000/- TU

    LIPIA KWA NAMBA YA SIMU 0684 408 755

    Najua kuwa ungependa kupata ushauri wa karibu zaidi moja moja kwa moja kutoka kwangu.

    Nitafute tuone ni lini nitakuwa na muda, ili nikupangie ratiba ya kuongea na wewe. Utalipia kiasi kidogo tu.

    Saa moja ni laki moja mazungumzo kwa njia ya mtandao.

    SAA MOJA NI LAKI MBILI NA NUSU MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA. Malipo yanafanyika kwanza, kisha unapewa tarehe (appointment) tutakapoweza kuongea.

    Tumia namba ya simu +255 755 848 391 kuwasiliana nami.

    Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza ambaye anaishi Morogoro nchini Tanzania.

    Unaweza kujifunza zaidi kutoka kwa Godius Rweyongeza kupitia youtube channel yake hapa

    Kwa ushauri niandikie songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu ambavyo ameandika Godius Rweyongeza, wasiliana naye kwa +255 684 408 755 na orodha ya vitabu vyenyewe unaweza kuiona HAPA. Chagua unachopenda, kisha twanga,  +255 684 408 755

    Kujiunga na programu yetu ya uandishi. Wasiliana na +255 678 848 396

    For Consultation only: +255 755 848 391  au godiusrweyongeza1@gmail.com

  • Usifanye kosa la kujiajiri kama hujui hiki kitu

    Una mpango wa kujiajiri? Hakikisha kuwa hauchukui hatua ya kujiajiri kama huna ufahamu wa jambo hili Moja.
    Jambo hili ni kwamba, kama huwezi kujisimamia mwe yewe kutekeleza majukumu Yako, usijiajiri.

    Kama Bado unasubiri watu wakusimamie ndiyo utekeleze majukumu Yako, usianzishe biashara ya namna yoyote.

    Pengine unajiukiza Kwa Nini.
    Jibu la haraka ni Kwa sababu hiyo biashara Yako itakufa.

    Jibu refu
    Ni kwamba kama unaanzisha biashara na uko pekee Yako maana yake hakutakuwa na mtu wa kukusimamia. Mtu ambaye atakufuatilia mwenendo wako wote hatua Kwa hatua, kujua kama umefanya na kukamilisha majukumu husika au hujafanya.

    Sasa kwa kuwa mtu wana mna hii atakuwa hayupo, na wewe mara zote huwa unategemea kusimamiwa.

    Nakuhakikishia kwamba itakuwa vigumu sana kwako kufika mbali.

    Kitu cha kipekee ambacho unahitaji ni uwezo wa wewe kujisimamia. kujisimamia kwenye kufanya kazi na majukumu mengine

    Kama huwezi kufanikisha hili, basi hata usithubutu kujiajiri. Huo ndio wosia wangu kwako.

    Kuna mambo 55 ya kuzingatia kabla ya kuanzisha biashara, mambo haya yote yameelezwa kwenye hiki kitabu. Kupata nakala yako, wasiliana na +255 684 408 755
    Hakikisha unajipatia nakala ya kitabu hiki. Tumia namba ya simu +255 684 408 755

  • App hii hakikisha unaiweka kwenye simu yako, tena iweke sasa hivi

     

    Mara kwa mara huwa nikikutana na app ambayo ni nzuri, basi huwa siachi kukushirikisha na wewe ili uweze kunufaika na kile kilichomo kwenye app husika. Nimekuwa nikifanya hivyo hapa mara kwa mara.

    Siku kadhaa zilizopita nilikutana na app inayoitwa the secrets of the billionaires mind, niliipakua na kuiweka kwenye simu yangu. Kiukweli imekuwa ni moja ya app bora kabisa ambazo na wewe unapaswa kuwa nazo.

    App hii ni kitabu. INAELEKEZA HATUA KWA HATUA NAMNA UNAVYOWEZA kuwa na fikra za kibilionea.

    Mwandaaji wa hii app amejikita zaidi katika kubadili namna unavyofikiri.

    Badala ya kufikiri katika namna ya ukawaida, uanze kufikiri kama bilionea.

    Ni fikra zetu ndizo zinatufanya kuwa tulivyo.

    Hii ndiyo kusema kwamba kama tunataka kubadili matokeo tunayopata sasa hivi, tunapaswa pia kuwa tayari kubadili namna yetu ya kufikiri ya sasa hivi.

    Sura zilizo kwenye hiki kitabu hazijazungumzia zaidi kuhusu pesa.

    Lakini ni ukwlei kuwa ukiweza kuwa na fikra za kibilionea kama hizo ambazo mwandishi ameeleza kwenye hii app. Na kama matendo yako yatakuwa ya kibilionea, ni wazi tu kuwa suala la kuufikia ubilionea litakuwa ni suala la muda tu.

     

    Utaweza kuufikia ubilionea bila ya shida yoyote.

     

    Hakikisha unapakua app yako sasa hivi, naamini baada ya kuwa umesoma kilichomo, utarudi hapa na kutoa mrejesho wako binafsi.

     

    Makala hii imeandadaliwa na rafiki yako wa ukweli

    Godius Rweyongeza

    Tuwasiliane kwa namba ya simu 0684408755

  • Jack Welch: Safari ya Uongozi na Urithi Wake Katika Ulimwengu wa Biashara

    Jack Welch, ambaye jina lake kamili ni John Francis Welch Jr., alizaliwa tarehe 19 Novemba 1935, huko Peabody, Massachusetts, Marekani. Alijulikana sana kama mkurugenzi mtendaji wa General Electric (GE) kuanzia mwaka 1981 hadi 2001. Chini ya uongozi wake, GE iliongezeka thamani kutoka dola bilioni 12 hadi zaidi ya dola bilioni 410, jambo lililomfanya kuwa mmoja wa wakurugenzi watendaji maarufu na wenye mafanikio makubwa katika historia ya biashara.

    Sababu za Kuandika ebook hii

    Kitabu hiki kimeandikwa ili kutoa mwanga kuhusu maisha na kazi za Jack Welch, na jinsi alivyobadilisha tasnia ya biashara kwa ujumla. Welch alijulikana kwa mbinu zake za uongozi za ubunifu na ufanisi, pamoja na falsafa zake ambazo zimekuwa mfano wa kuigwa na viongozi wengi duniani. Kwa hiyo, tunalenga kutoa maelezo ya kina kuhusu safari yake, mafanikio yake, na changamoto alizokabiliana nazo, pamoja na mafunzo muhimu ambayo yanaweza kusaidia viongozi wa sasa na wa baadaye.

    Muhtasari wa Yaliyomo

     Utangulizi

    Kitabu hiki kinaangazia maisha na kazi ya Jack Welch, mtendaji mashuhuri ambaye alibadilisha kabisa sura ya General Electric na kuacha urithi mkubwa katika ulimwengu wa biashara. Tunachunguza safari yake ya uongozi, falsafa zake, na athari zake kwa kampuni na tasnia kwa ujumla.

     Sehemu ya Kwanza: Maisha ya Awali na

     Elimu

    Tunatazama familia na asili ya Jack Welch, pamoja na malezi na elimu yake. Hii inajumuisha maisha yake ya shule, uzoefu wa elimu, na hatua za kwanza za kazi ambazo zilimjenga kuwa kiongozi wa baadaye.

     Sehemu ya Pili: Kazi ya Mapema na Kupanda Ngazi

    Sehemu hii inafafanua kazi za mapema za Jack Welch kabla ya kujiunga na GE, na jinsi alivyopanda ngazi ndani ya kampuni hiyo hadi kufikia nafasi ya juu ya uongozi.

     Sehemu ya Tatu: Uongozi wa General Electric

    Hapa tunachunguza jinsi Jack Welch alivyochukua uongozi wa GE, mikakati aliyotumia, na mabadiliko aliyoyafanya ndani ya kampuni. Tunazingatia pia jinsi alivyoboresha ufanisi na kuongeza thamani ya kampuni.

     Sehemu ya Nne: Mafanikio na Migogoro

    Tunachunguza mafanikio makubwa ya Jack Welch pamoja na migogoro na changamoto alizokabiliana nazo. Tunaangalia mifano ya migogoro mikubwa na jinsi alivyopata ufumbuzi wake.

     Sehemu ya Tano: Falsafa ya Uongozi

    Sehemu hii inaeleza falsafa za uongozi za Jack Welch, mbinu zake za uongozi, na umuhimu wa ubunifu na kubadilika. Tunachunguza pia uhusiano wake na wafanyakazi na jinsi alivyounda timu imara.

     Sehemu ya Sita: Kuondoka GE na Maisha Baada ya GE

    Tunachunguza kuondoka kwa Jack Welch kutoka GE na urithi aliouacha. Pia, tunaangalia maisha yake baada ya GE, ikiwemo ushauri na uandishi wa vitabu.

     Sehemu ya Saba: Athari na Urithi

    Sehemu hii inaeleza athari za Jack Welch kwa GE na tasnia ya biashara kwa ujumla. Tunachunguza mchango wake kwa uongozi wa kisasa na mifano ya viongozi walioathiriwa naye.

     Hitimisho

    Tunamalizia kwa muhtasari wa mafanikio ya Jack Welch, masomo makuu kutoka kwa maisha na kazi yake, na maoni ya mwisho na ushauri kwa wasomaji. Kitabu hiki kitatoa mwanga wa kina kuhusu maisha ya Jack Welch na jinsi alivyoathiri ulimwengu wa biashara. Tunatumaini kitakuwa chanzo cha motisha na mwongozo kwa wajasiriamali na viongozi wa baadaye

    Kupata ebook hii, lipia 4,000 tutakutumia yote sasa hivi. Ukilipia 10,000 utatumiwa ebooks tatu hii pamoja na nyingine mbili ambazo utapewa orodha na utachagua.

    Kupata ebook hizi, lipia kwa namba ya simu +255 684 408 755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

  • Wilbur na Orville Wright: Wawezeshaji wa Ndoto ya Kuruka


     Utangulizi
    Wilbur na Orville Wright, maarufu kama Ndugu wa Wright, wanajulikana kama waanzilishi wa safari za anga. Walifanikisha ndoto ya kuruka kwa kutumia mashine nzito kuliko hewa. Safari yao ya kuvumbua ndege iliyo na injini na inayoweza kudhibitiwa imekuwa msukumo mkubwa kwa wanateknolojia na wavumbuzi duniani kote. Ebook hii itachunguza maisha yao, kazi zao, na mafanikio yao kwa undani, hatua kwa hatua.

     Sura ya 1: Maisha ya Awali
     1.1 Kuzaliwa na Utoto
    Wilbur Wright alizaliwa tarehe 16 Aprili, 1867, na mdogo wake Orville alizaliwa tarehe 19 Agosti, 1871. Walizaliwa huko Millville, Indiana, na kukulia huko Dayton, Ohio. Baba yao, Milton Wright, alikuwa mchungaji wa Kanisa la United Brethren, na mama yao, Susan Koerner Wright, alikuwa mhandisi mwenye kipaji cha kiufundi.

     1.2 Shule na Masomo
    Ndugu wa Wright walihudhuria shule za umma lakini hawakumaliza masomo yao ya sekondari. Licha ya kutoendelea na elimu rasmi, walikuwa na shauku kubwa ya kujifunza, wakisoma kwa bidii vitabu na magazeti mbalimbali. Walikuwa na urafiki wa karibu, na walishirikiana katika miradi mingi ya uhandisi na kiufundi tangu utotoni mwao.


X