-
Pale unapokuwa huoni matokeo
Ni rahisi kuacha kufanya pale unapokuwa huoni matokeo ya haraka. Ila ukweli ni kuwa kamwe usiache kufanya kwa sababu tu huoni matokeo ya haraka, badala yake endelea kukaza.
Kukomaa kwa muda mrefu kutakuweka kwenye hali ya kupata matokeo mazuri kuliko vile unavyofanya kwa muda mfupi na kuacha. Mfano, ukiwekeza mara moja na kuacha, au ukiweka akiba mara moja na kuacha, utashindwa kuona matokeo yanayotokana na mwendelezo na uvumilivu.
Mfano mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi. Unaweza kujichagua mwenyewe kwa kuhakikisha unakuwa na sera nzuri ambazo zitakuinua kiuchumi miaka mitano ijayo, kisha ukaamua kuwekeza kwa nguvu zote kwa miaka mitano ijayo bila ya kuacha, nakuhakikishia kuwa kama ukifuata sera zako bila kuacha kwa miaka mitano ijayo bila kuacha, utaweza kufanya makubwa sana.
2025 JICHAGUE MWENYEWE. Kuna ebook ya bure inayokuonesha namna na wapi ujichague mwenyewe mwaka 2025. Nitakuwekea hapa moja kesho, hakikisha unafungua makala hiihii kesho kwa ajili ya kujifunza zaidi
-
Nguvu ya Kuweka Malengo-1
Unapokuwa na malengo unapambana kwa vyovyote vile kuhakikisha unayafanikisha malengo Yako ndani ya muda husika.
Ila ukiwa huna malengochochote kinachotokea mbele yako ni lengo.
Hivyo basi jitahidi kuhakikisha kuwa na malengo, weka malengo yafanyie kazi.
kumbuka usipokuwa na malengo, chochote kitakachotokea mbele yako kitakuwa ni lengo.
-
NGUVU YAKO KUBWA IWEKE HAPA
Rafiki yangu, nguvu yako kubwa iweke kwenye kile unachofanya. Badala ya kuiweka nguvu kubwa kwenye vitu ambavyo hupendi.
Inawezekana kuna vitu hupendi kwenye siasa, kwenye michezo na mabo mengine. Ila ukwlei ni kuwa nguvu yako kubwa inapaswa kuwekwa kwenye vitu ambavyo unapenda.
Kama ni biashara, hapo ndipo unapaswa kuwekeza nguvu zako.
Kama ni kazi, iwekeze hapo.
Wewe ni zaidi ya hivyo vitu vinavyokusumbua na vinavyokupotezea muda wako.
Imeandikw name rafiki yako
Godius Rweyongeza
-
Namna ya kupangilia ratiba ya wiki hii kiporofessional
Namna ya kupangilia ratiba ya wiki hii kiporofessional
Rafiki yangu mpendwa, salaam
Miongoni mwa ujuzi muhimu sana ambao unahitaji ili kufanikisha malengo Yako ya mwaka 2025 ni ujuzi wa kuipangilia wiki yako. Wiki ni ndogo sana ila usipoipangilia vizuri inapotea na ukipoteza wiki nyingi mfululizo, mwisho wa siku unakuwa umeupoteza mwaka wako. Maana mwaka una wiki 52 tu. Na kumbuka wiki yoyote unayoipoteza, hairudi hata kidogo.
Sasa ya nini uupoteze mwaka mzima wakati Kuna uwezekano mzuri tu wa kufanya makubwa kwa kuanza kitu kidogo kama kuipangilia wiki yako.
Anza wiki hii kuipangilia kila wiki yako.
Ni majukumu gani uliyonayo?
Ili kuipangilia wiki yako kiprofessional, anza kwa kujiuliza ni majukum gani yaliyombele yako kwa wiki inayofuata?
Kisha yapangilie kulingana na umuhimu. Majukumu ambayo ni ya muhimu zaidi yape kipaumbele kwanza.
Kwenye siku yako usipange vitu VINGI VYA kufanya. Ukiweza kuwa na vitu vitatu tu vinatosha, vikizidi visiwe zaidi ya sita. Hii itakusaidia kufokasi kwenye mambo machache ila utakayoyawekea NGUVU kubwa na kuyafanikisha pia.
Unavyoianza wiki yako pia, hakikisha wiki hii unapanga muda wa kujisomea vitabu. Inashangaza kuona kwamba watu wanapangilia mpaka muda wa kula ila hawapangilii muda wa kujisomea. Changamoto kubwa ni kwamba, tumbo likiwa na njaa huwa linapiga kelele. Ndiyo utasikia mtu anasema; “nina njaa“. Ila akili yako ikiwa na njaa haisemi. Ila ilipata utapiamlo wa akili, utazidi kuwa nyuma mara zote. Hivyo, fanya kadiri uwezavyo kuhakikisha kwamba, kila siku unapata muda wa kujisomea.
Pata kozi yoyote fupi. Online kuna kozi nyingi fupi. Kwenye ratiba yako weka muda wa kujifunza kozi yoyote fupi kuhusiana na eneo ambalo ungependa kulifahamu kwa undani. Inawezekana Hilo eneo tayari unalifahamy vizuri tu, lakini Kuna jambo moja au mawili unaweza kujifunza kuongezea au kutanua kile ambacho tayari unajua.
Siwezi moja kwa moja kukwambia ujifunze kozi gani, ila fahamu ya kuwa kozi za namna hii zipo nyingi. Ni juu Yako kujua wapi unahitaji KUWEKEZA NGUVU ili uwe Bora zaidi. Maeneo ya kujifunza na kupata kozi kama hizi pia ni mengi, mfano skillshare, Udemy, Coursera, learn digital with Google, na nyingine nyingi kama zinavyoonekana kwenye picha hapo chini.
Pia hakikisha unaondoa vitu vyote ambavyo siyo sahihi, vitu kama mitandao ya kijamii, kuangalia video YouTube, TikTok. Kiufupi ni hivi, usiwekeze muda wako sehemu ambazo siyo sahihi, mara zote wekeza muda wako eneo sahihi ili uweze kupata matokeo sahihi.
Waangalie role models wako. Ni wazi kuwa Kuna watu ambao kwenye maisha Yako unatamani kuwa kama wao. Kwa Kila jambo unalotaka kufanya jiulize kama angekuwa [jina la role model wako] angefanya hivi? Kuna vitu VINGI unafanya ambavyo role model wako hafanyi. Viepuke.
Anza kufanyia haya kwa wiki hii, tukutane hapahapa kesho kwa ajili ya somo la jingine zuri kama hili.
Mpaka wakati mwingine.
Mimi ni Godius Rweyongeza.
Tuwasiliane 075584891
Kitu kimoja Cha ziada😁
Mwezi wa sita tunaenda kuwa na semina Babu kubwa.
Itafanyika tarehe 28 na 29 Juni. Itakuwa siku ya Jumamosi na Jumapili.
Hivyo, nichukue nafasi hii kukukaribisha sana kwenye semina hii ya kipekee rafiki yangu.
Kwa maelezo zaidi kuhusiana na semina jiunge kwenye kundi la semina hapa👇🏿
-
Jinsi Ya Kuandaa Kizazi Cha Wafanyabiashara
Juzi nilikuwa nasoma ujumbe wa mkurugenzi mkuu wa TELEGRAM.
Alizungumzia namna kampuni za kichina zinavyofanya vizuri na namna ambavyo zitafanya vizuri kwa siku zijazo kutokana na mfumo mzuri wa elimu walionao.Kitu hiki kimenitafakatisha sana na Leo nikaona nikuandalie ujumbe muhimu wa namna Leo hii tunavyoweza kuanza kuandaa kizazi kijacho Cha wajasiriamali, kizazi ambacho kinaweza kwenda kupambana huko duniani, na kuleta mapinduzi makubwa.
Kwa Nini nasema tuandae kizazi Cha wajasiriamali? Kwa sababu wajasiriamali ndiyo wanakuja na mawazo mengi ya kibunifu na ndiyo ambao wanaweza kukuletea mabadiliko MAKUBWA yajayo.
Kinachofanya wachina wanaonekana tishio Leo hii ni kwa sababu ya wajasiriamali na wabunifu walio nao. Na kitakachofanya sisi tufanye MAKUBWA ni kwa sababu ya wajasiriamali tulionao pia.
Hivyo basi rafiki yangu huu ni wakati wetu sisi kuanza kuandaa kizazi kijacho Cha wajasiriamali.Sasa tunawaandaaje. Kwanza, tuwaandalie mazingira ya kiushindani kama ambavyo anatuelekeza hapo mkurugenzi mkuu wa TELEGRAM. Pili, tuwaandalie mazingira ya kuanza kufanya biashara wakiwa wadogo. Aidha tunaweza kuwapa miradi midogo midogo nyumbani waisimamie.
Tatu, tushirikishane nao kwenye biashara zetu. Sambamba na shule nzuri tunazowasomesha, tushiie tu hapo, wakitoa shule au siku za wikendi twende nao kwenye biashara au kazi tunazofanya. Na wao washiriki pia.
Nne, Kuanzisha Mafunzo ya Ujasiriamali Mapema. Kwa kuwa hatutegemei kuwa na mfumo huu ukiwekwa kwenye elimu ka haraka. Basi tutakachofanya ni kuwapeleka watoto kwenye Mafunzo ya kibiashara sisi wenyewe au ili kuwafundisha misingi ya biashara, fedha, na ubunifu tangu wakiwa wadogo. Rafiki yangu Innocent huwa anatoa Mafunzo ya namna hii kila jumamosi.Tano, kuwahamasisha Kufikiri Kibiashara. Ni muhimu sana tuanze Kuwaelekeza watoto kuona fursa kwenye changamoto. Wajue wazo kuwa changamoto ni fursa. Kumbe, badala ya kutegemea ajira kama suluhisho pekee la maisha wafikiri nje ya hapo na tuwaelekeze hili mapema.
Badala ya kuwaambia kwamba nenda shule USOME kwa bidii ili uje uajiriwe. Tuwaambie waende shule, wajifunze kwa bidii ili waje watumie ujuzi watakaojifunza kusaidia KUTATUA matatizo Yao.
Sita, kuwajengea uwezo wa ubunifu na uvumbuzi. Kuwatia moyo kutumia mawazo yao kuunda bidhaa au huduma mpya zitakazosaidia kutatua matatizo ya jamii. Ni kwa namna Gani hili tunaweza kukifanya tukiwa nyumbani, ni kwa
1. Kuwazoesha kuwapa maswali badala ya majibu
2. Kutokuwa wepesi wa kujibu maswali Yao hata pale tunapokuwa tunajua majibu ya maswali Yao
3. Kutowaepusha na magumu hata pale tunapoweza kufanya hivyo.
Saba, kuwafundisha umuhimu wa akiba na uwekezaji . Kwa kila fedha unazowapa kwenda shule, waambie pia wajenge utaratibu wa kujilipa wenyewe kwanza kwa KUWEKA akiba. Akiba itawaba wakiwa wakubwa.Nane, kuwahamasisha kuchukua hatua bila hofu.
Utasikia mzazi anamwambia mwanae, ukikokoaea kufanya kitu fulani nitakuua. Na kauli nyingine nyingi hasi. Badala ya kuwatishia hivyo, wahamasishe wachukue hatua hata kama muda mwingine wewe mzazi unakuwa na hofu au wasiwasi.
Kuwaunganisha na wajasiriamali waliofanikiwa ukipata nafasi ya kushiriki semina au kukutana na watu waliofanikiwa nenda na wanao. Waone watu waliofanikiwa wanaongeaje, wanaishije, wanatendaje. Watajifunza mengi kwa kuona kuliko wewe kuwaambia kwa mdomo tu.Kuwajengea Uwezo wa Mawasiliano na Ushawishi
Ni muhimu sana tuwafunze watoto wetu umuhimu wa kuwasiliana na kuwasiliana mawazo Yao. Maana itafikia hatua watakuwa na wazo, na watatakiwa kuliwasilisha kwa wateja au wawekezaji. Sasa bila ya kuwa na ujuzi mzuri wa mawasiliano hawataweza kufanya makubwa.
Kuwafundisha maadili ya ujasiriamali. Maadili ya uaminifu, uvumilivu, bidii, na kujali n.k
Haya pia ni maadili muhimu ambayo yatawabeba watoto wetu.Hayo ni mambo machache ya kuanza nayo.
Wewe unaenda kuanza na jambo Gani
By the way mwezi wa sita tutakuwa na semina, Na Moja ya mada itakayofundishwa ni mada ya NI NAMNA YA KUANDAA KIZAZI KIJACHO CHA WAJASIRIAMALI chini ya mkufunzi wetu Innocent Kavishe.
Karibu sana kwenye semina hii ya kipekee.
Karibu sana kwenye semina ya biashara na uwekezaji mwaka 2025
Rafiki yangu mpendwa, kila mwaka huwa tunakuwa na semina tatu. Semina moja huwa inafanyika kuanzia tarehe 15-30 Januari KWA NJIA YA MTANDAO. Semina ya pili huwa inafanyika wikendi ya mwisho ya mwezi wa Juni (hii ni ya ana kwa ana), na semina nyingine huwa inafanyika septemba wiki ya mwisho (tarehe 24-30 septemba). Hii huwa inafanyika mtandaoni pia.
Semina ya mwezi wa sita huwa ni semina ya ana kwa ana, na kwa mwaka huu 2025 itafanyika tarehe 29-30 Juni. Itakuwa ni siku ya jumamosi na jumapili. Itafanyika KINGSWAY HOTEL MOROGORO.
Semina hii ya ana kwa ana imekuwa inafanyika na huu utakuwa ni mwaka wetu wa tatu mfululizo. Semina ya mwaka huu inaenda kuwa ya tofauti na ya pekee.
Hivyo, nichukue nafasi hii, kukukaribisha sana kwenye semina ya biashara na uwekezaji mwaka 2025.
Katika semina hii ya mwaka 2025 tumekuandalia mambo makubwa yafuatayo.
SIKU YA KWANZA 29.6.2025:
- MISINGI YA KUKUZA BIASHARA KWENYE ULIMWENGU WA LEO
- JINSI YA KUAGIZA BIDHAA NJE YA NCHI (CHINA)
- MAMBO YA KUZINGATIA BAADA YA KUSAJILI KAMPUNI
- KUTUMIA RASILIMALI ZA WATU WENGINE kwa VITENDO
- JINSI YA KUJENGA BRAND YAKO
- ELIMU YA KODI KWA WAFANYABIASHARA
SIKU YA PILI: 30.6.2025
- KUTOKA KUAJIRIWA MPAKA KUMILIKI BIASHARA (mwongozo kamili)
- ELIMU YA FEDHA NA UWEKEZAJI
- WANANDOA NA BIASHARA (misingi ya kusimamia biashara kama wenza na urithi kwa watoto)
- ITAWALE HOFU YA KUANZISHA NA KUKUZA BIASHARA
- ELIMU YA FEDHA KWA WATOTO NA NAMNA YA KUANDAA KIZAZI KIJACHO CHA WAFANYABIASHARA
- KUFIKIRI NJE YA 18 2025 (MWONGOZO KUSIMAMIA BIASHARA ZINAZOJIENDESHA)
Hizo ndizo mada ambazo tutazungumzia kwa undani mwaka huu. Kiukweli unaenda kuwa ni mwaka wa kipekee sana na mwaka wa kufanya makubwa.
Imani yangu ni kwamba wewe…………………………..utakuwa mmoja wa washiriki wa semina yetu ya mwaka huu. Umekuw unakosa semina za miaka mingine yote,mwaka huu usikubali kamwe kuikosa semina hii.
Pambana kadiri uwezavyo kuwepo kwenye semina yetu.
Ada ya semina itakuwa 170,000/- kwa atakayeshiriki semina hii kwa siku mbili.
Wakati kwa atakayeshiriki semina hii kwa siku moja ada ya semina itakuwa 100,000/- tu. Na atakayeshiriki semina kwa njia mtandao kwa siku zote mbili itakuwa 85,000/- tu
Njoo tuungane mwaka huu kwenye semina hii ya kipekee ili uweze kufanya makubwa kwenye eneo la biashara yako na maendeleo binafsi.Bonyeza hapa sasa.
Kuhusu malipo ya semina
Kwanza chagua aina ya package ambayo utashiriki. Kama utashiriki kwa siku mbili au kwa siku moja au kwa njia ya mtandao.
Unaweza kulipia ada yote ya SEMINA mara moja au unaweza kulipia kidogokidogo pia.
Kwa mfano, unaweza kuanza utaratibu wa kulipia kila mwezi kwa kuigawa ada yote ya semina kwa miezi minne ambayo tunayo mbele yetu. Ukilipia 50,000 kila mwezi kuanzia sasa. Mpaka kufikia siku ya semina ada yote ya semina itakuwa imeshakamilika.
Unaweza pia kuanza utaratibu wa kulipa kila wiki 15,000 tu.
Au kila siku elfu mbili tu.
Chukua hatua sasa uanze kulipia.
Namba ya malipo ni CRDB: 0150984455500 JINA ni SONGAMBELE CONSULTANTS
Au TIGO PESA: 19016638 jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS
Karibu sana rafiki yangu
NB: kwenye ukurasa unaofuata nimekuambatanishia ratiba kamili ya semina na wakufunzi watakaondisha siku hiyo. KARIBU SANA.
Ni mimi kijana wako
Godius Rweyongeza
0755848391
Morogoro-Tz
-
Njia Bora Ya Kufanya MAKUBWA Ni Hii by Godius Rweyongeza
Pengine umekuwa unajiuliza ni kwa namna gani naweza kufanya makubwa kwenye maisha yangu?
Ukweli ni kuwa haya makubwa unayotamani kuyafanya kwenye maisha yako, hayawezi kuja tu yenyewe bila ya wewe kufanya kazi.
Njia bora ya wewe kufanya makubwa ni kwa wewe kuhakikisha kwamba unatoka hapo ulipo na kwenda kufanya kazi. Kwenye ulimwengu wa leo sambamba na teknolojia zote ambazo zimegunduliwa, hakuna teknolojia ambayo imechukua nafasi ya kazi.
Hivyo basi fahamu wazi kuwa kazi ni kitu ambacho hutaweza kukikwepa kamwe. Kuwa tayari kufanya kazi na kuweka kazi pale panapostahili kazi ili uweze kupata matokeo ambayo unataka kupata.
Tuendelee mbele ili uweeze kuangalia video hii yenye somo kubwa sana kwako. Bonyeza hapa kuiangalia.
-
ukijua kitu kifanyie kazi
Utasikia mtu anakwambia kwamba hiki nakijua, nilijifunza chuo. Hiki nakijua…
Kama unakijua kwa nini hukifanyii kazi? Rafiki yangu kitu kikubwa ninachotaka kukwambia siku ya leo ni kwamba kujua pekee hakutoshi. Unapaswa kujua vitu na kuvifanyia kazi pia.
Hiyo ndiyo inaenda kuwa tiketi yako wewe kukfanya makubwa.
Haitoshi tu kwa wewe kujua kuweka akiba, bila ya kuweka akiba.
Haitoshi tu kwa wewe kujua kwamba ni muhimu kufanya mazoezi bila ya kuyafanya.
kuna watu wengi wanajua vitu ila hawavifanyii kazi.
sasa wewe utakuwa na tofauti gani na hao wengine.
wewe unapaswa kujua vitu na unapaswa kuvifanyia kazi pia.
-
Nguvu ya kushambulia
Kwenye timu ya mpira wa miguu huwa kuna wachezaji wa aina mbalimbali ila mojawapo ya wachezaji huwa ni washambuliaji. Hawa kazi yao huwa ni kuhakikisha muda wote wanasumbua kwenye lango la mpinzani ili mwisho wa siku waweze kuipatia timu yao ushindi.
Endapo washambuliaji hawatafanya kazi yao ya kushambulia na badala yake wakaanza kujilinda dhidi ya timu nyingine maana yake ni kwamba, hiyo timu haiwezi kushinda. Haiwezi kushinda kwa sababu hailengi hata kufunga goli hata moja. Na ushindi unakuja kwa kufunga.
Kadiri mnavyoshambulia kwa wingi ndivyo nafasi yenu ya kufanya vizuri inavyokuwa nzuri kuliko pale mnapokuwa hamshambulii
Kwenye maisha ya kawaida hivyo hivyo. Wale wanaoshambulia, wana nafsi nzuri ya kufanya vizuri zaidi kuliko wale wanaokuwa hawashambulii.
Wanaoshambulia ndiyo wanaofanya makubwa.
Pengine unaogopa kushambulia kwa sababu unaogopa unaweza kushindwa goli na hivyo kuonekana kama hujui? Si ndiyo?
Kwenye hili nikuletee nukuu muhimu sana ya Michael Jordan aliysema kwamba nimeshindwa mara nyingi sana, ndiyo maana nashinda. Kama unataka kushinda, shindwa kwanza.
Kushindwa ni tiketi yaw ewe kufanya makubwa sana.
Nimewahi kabisa mpaka kuandika kitabu kinaitwa. Nyuma ya ushindi, kuna kushindwa, kushindwa, kushindwa. Kama hujawahi kupata nakala ya hiki kitabu, nakushauri ujipatie nakala yako mapema iwezekavyo. Kitakusaidia kukupa mwanga wa namna unavyoweza kufanya makubwa, hata katika mazingira ambayo unapitia changamoto.
Kujipatia nakala ya kitabu hiki, naomba tuwasiliane kwa simu 0755 848 391
-
Shukrani
Moja ya kitu muhimu sana ambacho unapaswa kukifanyia kazi ni kuwa mtu wa shukrani. Kila siku inayokuja kwako ni nafasi nyingine ya wewe kushukuru.
Una mengi ya kushukuru kwenye maisha yako. Wengi huwa wanasubiri mpaka waone mambo makubwa ili waweze kushukuru. Ila ukweli ni kuwa kwa mambo yanayoendelea kwenye maisha yako, una mengi ambayo leo hii unaweza kukaa chini na kushukuru.
Kila siku chukua notebook yako. kisha
- Shukuru kwa ajili ya uhai wako
- Shukuru kwa ajili ya kuwa na familia yako
- Shukuru kwamba una mwenza
- Shukuru kwamba una watoto
- Shukuru kwamba umeweza hata kusoma hhii makala
- Shukuru kwamba bado unaendelea kuipambania ndoto yako
Hapa najaribu tu kukuonesha baadhi ya vitu ambavyo unaweza kuanza navyo kwenye kushukuru siku ya leo. Vipo vingi unavyoweza kushukuru na hivi ni baadhi tu.
Kazi inabaki kwako.
Siku ya leo ni jambo gani unaaenda kushukuru kwa kuwa nalo?
-
Watu
Ili ufanikiwe unahitaji watu, tena watu sahihi.
Hivyo basi rafiki yangu, pambana kuzungukwa na watu sahihi. Ukikaaa na watu ambao siyo sahihi watakuangusha.
Unajua kwa nini watakuangusha, watakuangusha kwa sababu fikra zao ni za kuanguka wala siyo za kuinuka.
Inabidi ukae na watu wenye fikra za kuinuka, ili uinuke.
Swali langu kwkao siku ya leo ni je, ni kwa namna gani unakaa na watu sahihi kwenye maisha yako?