Home


  • Namba Zetu Za Malipo

    Namba za malipo ya vitabu:

    Namba za lipa

    TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS

    M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

    Namba za kawaida

    AIRTEL MONEY: 0684408755
    TIGO PESA: 0655 848 392
    M-PESA: 0745 848 395

    Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255

    Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
    Airtel money: +255 684 408 755
    TIGO PESA: +255 655 848 392
    M-PESA: +255 745 848 395

    KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.

    Yafanyie kupitia

    1. CRDB BANK: 0150770710200
    2. NMB BANK: 22110047274

    Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA

  • Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa

    Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA

    Simu: +255 (0) 684408755

    Whatsap: +255 (0) 755848391

    Email: songambele.smb@gmail.com

    Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)

  • KIPAJI NI DHAHABU:Jinsi Ya Kukigundua, Kukinoa Na Kukitumia Kipaji Chako Kwa Manufaa

    ∞∞∞∞∞UTANGULIZI∞∞∞∞∞

    KIPAJI NI DHAHABU

     

    Nakumbuka mwaka 2013 nilikutana na vijana wenzangu ambao walikuwa kwenye mjadala mkali kuhusiana na Messi, Ronaldo na Neymar. Kwenye mjadala huu walikuwa wakijadili kuhusiana na uwezo wa wachezaji hawa, huku wengine wakisema kwamba Messi na Neymar wana kipaji ila Ronaldo akiwa anatumia nguvu.

    Nadhani kama wewe ni mpenzi wa soka, mijadala kama hii utakuwa unaifahamu ambavyo huwa inatokea sana. Na jinsi ambavyo huwa inateka umakini wa watu.

    Kwenye mijadala kama hii watu huwa wanatoa hoja zao kwa nguvu kuonesha kwamba mchezaji fulani ni mzuri na ana kipaji kuliko mwingine.

    Mijadala mingine ya aina hii huwa ni mijadala ya wasanii, ambapo huwa wanalinganishwa wasanii wawili. Umewahi kushiriki mjadala kama huo?

    Hivi kwanza wewe mwenyewe unakijua kipaji chako?

    Mjadala kama huu ndio ulinifanya nitafakari na kujiuliza hivi mimi mwenyewe nina kipaji gani? Je, hawa wanaozungumzia kipaji cha Messi, Neymar na Ronaldo wanajua vipaji vyao? Ukiwauliza wewe una kipaji gani wanaweza kukujibu? Na tokea hapo nikaianza safari ya kujitafuta ili niweze kujua kipaji changu. Maswali kama kipaji ni nini? Hivi ni kweli kila mtu amezaliwa na kipaji au kuna baadhi ya watu wachache tu ambao wamebarikiwa ndio walizaliwa na kipaji? Kipaji ni kitu cha kuzaliwa nacho au unaweza kukipata ukubwani?

    Safari hiyo tu imenifunza mengi ambayo unaenda kukutana nayo kwenye ebook hii hapa ya kipekee.

    Kila Mtu Kazaliwa Na Kipaji Ila Hapaswi Kulinganishwa Na Mwingine

    Nakummbuka Albert Einstein aliwahi kunukuliwa akisema kwamba kila mtu ni gwiji, ila tatizo ni pale ambapo unamhukumu samaki kwa uwezo wake wa kupaa.

    Hapo ndipo nilipogundua kumbe mimi na wewe tuna vipaji, ila sasa kipaji changu hakiwezi kufananishwa wala kulinganishwa na wewe.

    Ni wazi kuwa kwa vyovyote vile samaki hawezi kuwa gwiji kwenye somo la kupanda mti, kupaa wala kukimbia. Yeye uwezo wake mkubwa upo kwenye kuogelea na huko lazima atafanya vizuri tu.

    Sasa hivyo hivyo kwa kipaji chako. Hakiwezi kulinganishwa na mtu mwingine, unacho wewe na ni kwa ajili yako tu. Hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kuwa na kipaji kama cha kwako.

    Mgawanyo Wa Kitabu

    Kwenye ebook hii hapa nimeeleza kipaji kwa kina hasa ili hata kama ebook hii anaisoma mtoto wa miaka sita aweze kunielewa kuhusiana na kipaji.

    Kwenye sura ya kwanza nimeanza kwa kueleza kwamba kipaji ni kitu gani? Ambapo nimeeleza dhana nzima ya kipaji na jinsi kinavyofanya kazi.

    Kwenye sura ya pili nimeeleza namna ambavyo unaweza kugundua kipaji chako. Je, unajiuliza ni kwa namna gani ambavyo unaweza kugundua hicho kipaji chako? Basi nenda moja kwa moja kwenye sura ya pili.

    Kwenye sura ya tatu nimeonesha mbinu unazoweza kutumia kwenye kunoa na kuendeleza kipaji chako. Hapa utakutana na mbinu za kukusaidia wewe kuweza kupeleka kipaji chako mbali. Na kwenye sura ya nne tutaona kwa nini watu hawathamini vipaji vyao.

    Kwenye sura ya tano tutaona mbinu zitakusaidia wewe kutengeneza fedha kwa kutumia kipaji chako.

    Tunaishi kwenye ulimwengu wa intaneti. Na hapa tutaingia kwenye sura ya sita ambapo tutaona namna ambavyo unaweza kupeleka kipaji chako kwenye mtandao na kunufaika na inatenti.

    Kwenye sura ya saba  tutaona kipaji na elimu. Kwa nini elimu inapewa kipaumbele zaidi kuliko kipaji na je, kuna ulazima wowote wa kuendeleza kipaji chako au ukomae tu na elimu?

    Uko tayari kwa ajili ya safari hii ya kipekee? Basi wacha tuianze kama ifuatavyo.

  • Ugunduzi mkubwa wa Zama Hizi…

    Rafiki yangu moja ya ugunduzi mkubwa wa Zama Hizi ni kuwa wewe unaweza kubadili maisha yako na kuwa vyovyote vile unavyotaka.
    Unaweza kuwa Tajiri
    Unaweza kuufikia Uhuru wa Kifedha
    Unaweza kuwa na mahusiano mazuri
    Unaweza kuwa na familia bora n.k.

    Rafiki yangu yangu, hakuna ukomo wa vile unavyoweza kuwa au kufikia kwenye maisha. Labda tu ukijiwekea ukomo wewe mwenyewe.

    Kitu chochote ambacho akili yako inaweza kushikilia  na kukikubali, ujue kuwa hicho kitu kinaweza kufikiwa.

    Sasa labda nikuulize wewe, ni kitu gani unataka kufikia maishani mwako? Kiandike chini kisha anza kukifanyia kazi. Kumbuka,
    unaweza kubadili maisha yako na kuwa vyovyote vile unavyotaka.

    Umekuwa nami rafiki yako,
    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

    l

  • Usifanye kitu mara moja…

    Kama unataka kubobea kwenye kitu, usifanye hicho kitu mara moja. badala yake kifanya mara kwa mara na kwa mwendelezo. Kadiri unavyofanya kitu au kazi mara kwa mara inakupa nguvu na ufanisi na hata kujiamini.

    Marudio yako kwenye kufanya kazi yanakufanya uzidi kubobea na hatimaye unakuwa bingwa.

    Mchezaji bora wa mpira wa miguu siyo yule ambaye anafanya mazoezi mara moja, kisha akatulia. Bali ni yule anayefanya mazoezi ya mara kwa mara.

    Mwimbaji mzuri siyo yule anayeimba mara moja, kisha akasahau.. bali yule anayefanya mazoezi ya kuimba mara kwa mara.

    Hata kama unajua wazi kabisa kuwa una kipaji kikubwa cha kufanya vitu, usifanye  hicho kitu mara moja, kisha ukatulia, kuwa na mwendelezo kwenye kazi au kile ambacho unakifanya. Kadiri unavyokifanya kwa mwendelezo ndivyo unavyokuwa mbobevu.

    Unataka kuwa mwandishi mbobevu, basi usiandike mara moja tu na kutulia, badala yake andika mara kwa mara na maandiko mengi kadiri uwezavyo.

    Unataka kufikia uhuru wa kifedha? Usiweke akiba mara moja na kutulia, au usiwekeze mara moja kisha ukasahau kila kitu, badala yake endelea kuweka akiba mara na kila unapopata fedha mfukoni.

    Unataka kuwa mwimbaji wa kimataifa? Usiimbe mara moja tu na kusahau, kuwa na mwendelezo wa kile unachofanya.

    Rafiki yangu, mkusanyiko wa hivi vitu vidogovidogo unavyofanya mwisho wa siku vinakuwa vitu vikubwa, kweli.

    Hiki ni kitu kilichonisukuma kuandika kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA. Kitabu ambacho nina uhakika kitakusaidia na wewe kwenye hii safari ya kufanya makubwa

    Pata nakala yako siku ya leo,  utanishukuru siku zijazo.

    Nakala moja ni elfu 20,000/- tu za kitanzania. Utatumiwa popote pale ulipo. Kupata nakala hii, utatuma fedha kwa namba 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Mara tu baada ya kutuma fedha yako utatutaarifu, ili tukutumie nakala ya kitabu hiki. Unakipokea popote pale ulipo duniani.

    Ubora ni kuwa kuna audiobook pia. Je, ungependa kupata audiobook ya kitabu hiki cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA? Kama jibu lako ni ndio, basi umeshakipata mpaka hapo. Tuma elfu kumi tu kwa ajili ya audiobook, itume kwenda nambari ya simu 0684408755.

    Kumbuka. Hardcopy inauzwa kwa elfu 20,000/- na audiobook inauzwa kwa elfu kumi (10,000/-) tu.

    Kila la kheri.

  • Uchambuzi Wa Kitabu: 25 Hours a Day; Going One More to Get What You Want


    Mwandishi: Nick Bare
    Mchambuzi: Hillary Mrosso
    Simu: 255 683862481

    UTANGULIZI
    Karibu katika uchambuzi wa kitabu bora sana cha 25 Hours a Day. Kikiwa na maana ya kwenda hatua moja zaidi kupata kila unachokitaka. Mwandishi ametumia uzoefu wake wa kijeshi kutengeneza nidhamu kubwa kwenye maisha yake binafsi, maisha ya biashra na mafanikio. Kama unavyojua jeshini kikubwa ni nidhamu ya kufanya mambo. Jeshini hawataki maelezo kwanini umeshindwa kufanya jambo ulilotakiwa kufanya, jeshini ni matokeo ndio yanayotakiwa. Kama umekosa nidhamu, umakini, kujituma, na hamasa ya kufanyia kazi ndoto zako. Basi hiki ndio kitabu kinachokufaa zaidi kukisoma.

    Katika uchambuzi nimekuandalia mambo 75 niliyojifunza katika kitabu hiki. Karibu tujifunze.

    1. “Usipomlilisha ng’ombe wako atakufa”. Hii ni kauli inayotumika kila eneo la maisha, usipolisha ndoto zako zitakufa, usipolisha biashara zako zitakufa, usipolisha kampuni yako itakufa. Maana yake vitu havitatokea tu kwenye maisha yako bila kuvifanyia kazi ili vitokee.
    2. Vitu vikubwa unavyoviona vimetokea kwa watu wengine inamaana kuwa walivifanyia kazi, waliingia gharama kubwa kuvifanya vitokee. Jifunze kupitia wao, hasa uvumilivu na nidhamu iliyowafanya wafikie ndoto zao.
    3. Ili uweze kufanyia kazi ndoto zako lazima uwe na umiliki mkubwa wa muda, usikubali mambo na changamoto zikupeleke zinavyotaka, unatakiwa kushika usukani, uwe dereva na ufanye yale yalio ya muhimu kufikia ndoto zako.
    4. Kila unachotamani kukifanya kwenye maisha yako, itakuhitaji kujitoa vya kutosha kabisa. Mfano, mwandishi wa kitabu hiki Nick Bare anasema, chochote alichotamani kwenye maisha yake, aliingia gharama na kujitoa kukifanyia kazi kwa asilimia 100.
    5. Mwandishi wa kitabu hiki cha kipekee Nick Bare anasema, hakuna anayefanikiwa kwenye maisha yake kwa kutofanya chochote. Hakuna mafanikio yatakuja kwako ukiwa umekaa tu au umesimama tu, mafanikio yanataka ujitoe kwa viwango vya juu sana.
    6. Tunatakiwa kuwa na shauku na njaa kali sana ya kufanikiwa na kufanyia kazi malengo na ndoto zetu, chochote unachoona unapaswa kukifanya ili ufanikiwe unatakiwa kujitoa kwa asilimia zote ili ufanikiwe.
    7. Mwandishi anasema, vifuatilie vitu vigumu unavyotakiwa uvifanye ili ufanikiwe kwenye maisha yako. usiache magumu ndio yakufuate wewe, wewe ndio unatakiwa kuyafuata magumu na kuyatatua ili ukue na kufanikiwa.
    8. Kuwa tayari kukabiliana na mambo magumu na vikwazo kwenye safari ya maisha yako; mafanikio yamejificha kwenye mambo magumu yaliyopo kwenye maisha yako.
    9. Kuwa tayari kupokea upinzani kutoka kwa watu wako wa karibu, maana wanaweza kukukatisha tamaa, wanaweza kukuumiza, wanaweza kukutenga, wanaweza kukuonea wivu; mwandishi anasema kuwa tayari kukabiliana nayo.
    10. Kuna wakati miili yetu inachoka na inapeleka taarifa kwenye fahamu zetu ili tusitishe tunachokifanya. Mwandishi anasema, hali hiyo ikitokea hutakiwi kuacha unachokifanya badala yake unatakiwa kuendelea kufanya kazi.
    11. Mafanikio hayaji kwa watu wanaoacha kufanya jambo ambalo linawapeleka kwenye mafaniko yao pale wanapochoka. Mafanikio yanakuja pale unapoenda zaidi ya uchovu unaoupata kwenye mwili wako.
    12. Akili yako haitakiwi kukubaliana na kila kinacholetwa na mwili, kuna wakati akili zinataka tuendelee kufanya kazi na kujituma, lakini mwili hautaki unakwambia umechoka, unakuletea uchovu, maumivu, usingizi. Bare anasema, unatakiwa kuwa na nguvu juu ya mwili wako ili kufanyia kazi ndoto zako.
    13. Nick Bare, anasema wakati wakiwa katika ratiba za kijeshi, huwa hawaachi kwasababu wamechoka, au miili yao inaleta maumivu, wanaacha pale wanapokamilisha ratiba ya siku au jambo hilo au mtu anapoumia au kuvunjika.
    14. Ili kufanikiwa na kufikia mafanikio makubwa, nguvu za mwilini pekee hazitoshi, tunatakiwa kuwa na nguvu za akili ambazo hazitakubaliana na taarifa za mwili kwamba tumechoka, tunaumia, tunahitaji kupumzika, tuna njaa.
    15. Bare anatufundisha kuwa akili ndio inatakiwa kuendesha mwili na sio mwili uendeshe akili. Akili ikiwa na nguvu na ushawishi itakutoa kwenye kufanya mambo ya kinyonge, utajituma sana, utaondoka kwenye comfort zone.
    16. Furaha kubwa tunaipata pale tunapotatua mambo magumu kwenye maisha yetu. Zifuatilie ndoto unaziona ni ngumu kwenye maisha yako, ifuatilie biashara uanayoina ni ngumu kwenye maisha yako kuifanya, ifuatilie kazi unayoina ni ngumu kuipata au kuifanya na uifanye; endapo utafanikiwa kuvuka hapo utakuwa mwenye furaha sana.
    17. Nick Bare ansema, juhudi na kujitu kwenye maisha yake kunatokana na mfano mzuri kutoka kwa wazazi wake ambo walikuwa wanafanya kazi kwa bidii sana. Bare anasema kuna wakati anamuona baba yake akifanya jambo kwa kujituma kwa muda mwingi kuliko ilivyo kawaida.
    18. Ukiusikiliza mwili wako kwenye kila taarifa inayokupa hutaweza kukabiliana na mambo magumu yatakayotokea maishani mwako, hutafurahia mafanikio makubwa, utakuwa mtu wa kawaida na masikini.
    19. Usighairishe mambo muhimu kwenye maisha yako, usikatie tamaa ndoto zako au mafanikio yako. Kuwa msitari wa mbele kabisa kutetea ndoto zako, jitoe kwa isivyokawaida ili kufikia mafanikio yako.
    20. Unatakiwa kuwa na ufahamu wenye nguvu sana ili uamue kufanya mambo muhimu kwenye maisha yako. Usipofanya hivyo mwili utakunyanyasa sana, na hutaweza kufikia mafanikio yako unayoyatamani.
    21. Yafanye maumivu unayoyapata mwilini mwako ndio yawe mafuta, yawe kichocheo cha wewe kuzidi kusonga mbele na sio yawe ndio njia ya kuacha kufanya ulichokuwa unafanya. Yafanye maumivu yakusukume kuchukua hatua za ziada zaidi.
    22. Zivunje rekodi zako mwenyewe, vunja ukomo uliojiwekea, sehemu ambazo uliona huweza kuzifikia dhamiria kuzifikia hata kama ni kwa maumivu makali, utajiona mwenye furaha sana utakapofikia matumizi makubwa ya uwezo wako.
    23. Ondoa kabisa ukomo unaoletwa na mwili wako, hata kama mwili wako unakuomba upumzike au uache jambo muhimu unalolifanya kwasababu ya maumivu au uchovu, usikubali, ufanye mwili wako uwe sehemu kubwa ya kukulea mafanikio makubwa unayoyatamani.
    24. Usikubali mwili wako uwe kikwazo cha wewe kufikia ndoto zako, dhibiti hisia za mwili wako na ulazimishe mwili wako kufuata ratiba yako muhimu.
    25. Kabiliana vikali na hisia za uchovu na raha ambazo mwili unataka uzifuate ili uache kufanya mambo muhimu kwenye maisha yako. kabiliana vikali sana dhidi ya comfort zone.
    26. Mwandishi anaseama, alipoteza fedha nyingi, muda mwingi, na masaa mengi ya kulala alipokuwa anapambana kusimamisha biashara yake ya virutubisho, lakini hakukata tama hata siku moja.
    27. Mafanikio tunayoyataka kwenye maisha yetu yatatugharimu vingi sana, hvvyo ili kuyafikia hatutakiwi kuwa bianadamu wa kawaida, tunatakiwa kuwa wavulivu sana na kujifunza kwenye kila mabaya na mazuri yanayokuja.
    28. Bare anakiri kufanya makosa mengi sana kwenye safari yake ya mafanikio. Lakini anasema kwa kiasi kikubwa makosa hayo yalimfanya awe imara na kuongeza umakini kwenye kazi zake.
    29. Bare anasema, dhambi kubwa sio kufanya makosa, bali dhambi kubwa ni kufanya makosa na kutojifunza kutokana na makosa hayo.
    30. Makosa ni kiashiria kuwa kuna vitu unavifanya kwenye maisha yako, sehemu yenye usalama hakuna ukuaji, hakuna mapinduzi ya kweli hakuna mabadiliko.
    31. Watu wengi wanaona jambo zuri au kitu kizuri na kuishia kusema “natamani” ningefanya kama vile ili kuwa kama yeye, mwandishi anasema ondoa natamani au wish, fanya kazi inayohitajika kufika unayoyatamani kwenye maisha yako.
    32. Weka matendo kwenye matamanio yako, hakuna kitakachotokea kwa kuishia kutamani pekee. Wekeza nguvu, umakini na akili zako kwenye kufanyia kazi yale unayoyotamani kwenye maisha yako.
    33. Kama kweli una dhamira ya dhati kufikia mafanikio makubwa, basi unatakiwa kuachana na mambo yasio na tija kwenye maisha yako, weka kando kabisha mambo yote yasiyochangia ukuaji wako, au mafanikio yako.
    34. Watu wenye mafanikio wanaona mwanga na furaha kubwa iliyopo mbele ya changamoto wanazopitia. Hii ndio huwafanya wawe wavumilivu kukabiliana na changamoto wanazokuna nazo.
    35. Nick Bare anasema katika shule ya kijeshi alijifunza mambo magumu sana, alipitia nyikati nyingi ngumu na za giza ambazo zilimfanya imara sana. Mafunzo hayo aliyojifunza akiwa jeshini ndaio kwa kiashi kikubwa anayatumia katika kufanya jambo lolote hata kuanzisha kampuni yake ya Virutubisho.
    36. Kikubwa alijifunza nidhamu, bila nidhamu huwezi kukamilisha jambo lolote. Wengi wanashindwa kufanya makubwa kwenye maisha yao kwa sababu hawana nidhamu ya kuvumilia na kukaa kwenye jambo wanalolifanya ili likamilike.
    37. Nidhamu itakufanya kukabiliana na kuishi kwenye nyakati ngumu na kufanyia kazi malengo yako, nidhamu itakufikisha kwenye kilele cha ndoto zako.
    38. Mwandishi wa kitabu hiki anashuri tujifunze kama mashine. Anasema jigeuze uwe kama mashine linapokuja suala la kujifunza na kujiongeze maarifa.
    39. Hakuna kitu muhimu kwenye maisha yetu kama muda. Muda ndio huamua mafanikio yetu, muda ukishaenda hauudi tena. Muda ni maisha. Utumie vizuri kufanya yale muhimu kwenye maisha yako.
    40. Ili uwe na matumizi mazuri ya muda wako jifunze kuweka vipaumbele. Vipaumbele ndio vitakufanya utumie muda wako vizuri na kwa ufanisi mkubwa.
    41. Mwandishi anasema kwenye jambo lolote unalotaka kufanya kwenye maisha yako, kuna taarifa nyingi kuhusu jambo hilo kwenye mitandao kama google, youtube, nk. hivyo usiogope kuanza kwasababu ya kukosa taarifa.
    42. Bare anasema hana tabia ya kuhaika kuwatafuta watu hovyo ili kuuliza mawali au kuomba ushauri. Anasema kabla ya kufanya hivyo huwa anaingia kwenye mitandao na kuanza kutafuta taarifa za jambo hilo kwanza.
    43. Mwandishi Bare anasema, tunatakiwa kufaidika na fursa zilizopo mtandaoni za kujifunza, anasema kuna mitandao mingi sana ya kijamii kwa ajili ya jambo lolote lile, itumie kusaidie, mfano wa mitandao hiyo ni websites, podcasts, books, blogs, vlogs, YouTube.
    44. Kwa kujifunza utaokoa gharama kubwa sana unazaoweza kuingia, tafuta taarifa za awali wewe mwenyewe kwanza. Jipe Jukumu la kujielimisha ili uondoe mambo ambayo huyajui kuhusu kazi yako, biashara yako, afya yako, au fedha.
    45. Kujifunza ni uwekezaji muhimu sana kwako binafsi, wekeza kwenye kujifunza na kupata maarifa ya kutosha kuhusu jambo unalotaka kulifanya.
    46. Bare anasema kipndi akiwa katika mafunzo ya kijeshi huko Korea, alitumia muda wake wa ziada kujifunza sana namna ya kutengeneza kampuni, namna ya kutengeneza videos nzuri, namna ya kuchukua video, kuongea na kufundisha.
    47. Tumia muda wako wa ziada kujifunza sana, jua sana kila unachokifanya, kuwa na taarifa za kutosha kuhusu jambo hilo. Wekeza kwenye maarifa, jifunze kila siku kama mashine.
    48. Kuna maarifa bora sana katika kipindi hiki kuliko nyakati zote zilizowahi kupita hapa duniani. Bare anasema kipindi cha zamani watu walikuwa wanatunza na kuhifadhi taarifa kama dhahabu, lakini zama hizi mambo ni tofauti kabisa kila mtu anaweza kuwa na taarifa anazozitaka.
    49. Jilazimisha sana kupata maarifa, tengeneza kiu kali ya kujifunza, na kwa kufanya hivyo utakuwa mtu bora sana.
    50. Jua kwa hakika ni taarifa gani unazihitaji, na ukianza kuzitafuta zingatia hilo, usiwe mzururaji, na hujui unatafuta taarifa gani, usije kupoteza muda wako wa thamani.
    51. Maisha sio kitufe fulani unajibonyezea tu na mambo yanaenda, maisha sio hisia hisia fulani tu. Maisha yanataka kujitoa sana, maisha yanataka kazi kweli kweli, maisha hayataki njia za mkato. Maisha yanataka ufanye vitu, ufanye kazi ili mambo yatokee.
    52. Kuna watu wanahisia kwamba kwajinsi walivyo au kwa namna walivyo basi wanastahili kutunukiwa mambo mazuri kwenye maisha yao.
    53. Hakuna anayejali kuhusu wewe, hakuna anayekosa usingizi kutokana na shida zako. Hivyo amka pambana na ndoto zako umiliki maisha mazuri unayoyataka.
    54. Acha kuwa na mategemeo kuwa kwasababu upo mahali fulani, au uko na mtu fulani basi utakuwa na maisha mazuri au unastahili maisha mazuri. Fanyia kazi ndoto zako zinazokunyima usingizi, furaha na amani.
    55. Hakuna atakayekuja na furushi la fedha au dhahbu akupe akwambie,unajua wewe ni mtu mzuri sana au wewe ni mpole au mwema sana basi chukua hizi fedha kama zawadi, jambo hili haliwezi kutokea kwako; mambo mazuri hayaji usipojisukuma fanya kazi kubwa kufikia mafanikio unayoyataka.
    56. Kuna wengine wameridhika na vyeo walivyo navyo na kujiona wameshapata kila kitu. Hivyo wanakuwa na kiburi hawataki kujituma tena, wanaona wamefika. Mwandishi anasema hakuna kitu kibaya kama kupata cheo na kujisahau na kuacha kutumia uwezo wako kufanya mambo makubwa.
    57. Mwandishi anasema kuna wakati anaona hajapata kile anachokitaka, anachofanya ni kuwafikiria wale walio na kitu hicho na gharama kubwa walioingia kupata kitu hicho. Kwa kufikiria hivyo anajisukuma zaidi kufanyia kazi malengo yake.
    58. Kama umeshindwa kuzalisha fedha mwaka huu unatakiwa kujiuliza tatizo ni nini? Nini hukufanya, nini ambacho unatakiwa kufanya ili uzalishe fedha unazotakiwa kuwa nazo.
    59. Jua huna wa kumlaumu kwa umasikini wako, kukosa fedha, kazi au maisha mazuri unayoyataka. Jipe Jukumu la kutengeneza maisha yako yawe bora, acha lawama na uvivu.
    60. Jiondoe kwenye comfort zone, ondoka kabisa kwenye maisha ya usalama. Ingia kwenye mapambano, kuondoa umasikini na ujinga kwenye maisha yako.
    61. Kuondoka kwenye comfort zone ni kufanya zaidi ya hisia za mwili wako, hata kama unahisi umechoka au maumivu, hata kama itakugharimu upoteze masaa mengi ya usingizi, itakugharimu kuacha baadhi ya ratiba za kula, itakugharimu kuacha na marafiki wasio na mchango maishani mwako.
    62. Kuondoka kwenye comfort zone, ni kuweka nidhamu kali sana ili ukamilisha jambo unalolifanya hata kama huna hamu au hamasa ya kufanya jambo hilo.
    63. Kuondoka kwenye comfort zone ni kuacha kutoa sababu kwanini hujafanya jambo ambalo ulitakiwa kulifanya.
    64. Kuondoka kwenye comfort zone, ni kujisukuma isivyo kawaida katika kutumia uwezo wako wote kufikia ndoto zako na mafanikio unayoyatamani.
    65. Kuondoka kwenye comfort zone, ni kuacha kujihurumia, kuwa mtu wa matokeo, kuwa mtu wa matendo kuliko maneno pekee.
    66. Kuondoka kwenye comfort zone, maana yake ni kuachana na raha za muda mfupi kwa ajili ya kuwekeza nguvu zako zote kujenga maisha yako ya sasa na ya baadaye yawe bora.
    67. Kuondoka kwenye comfort zone, ni kuanzisha biashara, kuipambania na kuwa tayari kupokea changamoto zote bila kukata tamaa.
    68. Bila nidhamu hutawaweza kujitoa kikamilifu kufanyia kazi ndoto zako. Hutakuwa na umakini hutakuwa na muda wa kufanya mambo muhimu.
    69. Unapofanya jambo lolote lililopo kwenye ratiba yako, lifanye kwa nguvu zako zote, akili yako yote, hisia zako zote. Nenda mzima mzima kulifanya jambo hilo.
    70. Usifanye jambo huku nusu ya akili yako ipo kwenye mambo mengine, unapojitoa jitoe kweli na sio nusu nusu. Zamia kabisa hadi jambo unalolifanya liishe.
    71. Toa asilimia 100 za umakini wako, akili yako, nguvu zako, kwa kufanya hivyo utazalisha kazi bora, na ufanisi wako utakuwa wa Kiwango cha juu sana.
    72. Unapjitoa asilimia 100 kwenye kufanya jambo lolote, maana yake utakuwa na wakati mzuri wa kutumia uwezo wako wa zaida uliolala, ubunifu wako na nguvu zako zilizolala ambazo hukujua kama unazo.
    73. Usikubaliane na ukomo uliojiwekea kwamba ndio mwisho wako hapo. Usikubaliane na maoni ya watu walioweka ukomo kwenye uwezo wako. Hapa una jambo kubwa la kuwahahikishia kuwa hawakuwa sahihi kukuwekea ukomo kwenye maisha yako.
    74. Weka jitihadi za ziada kuwenda mbali kabisa na ukomo uliojiwekea na waliokuwekea watu wengine. Wewe una uwezo wote wa kufanya makubwa na kufanikiwa kwa viwango vya juu sana.
    75. Kila siku inayokuja kwenye maisha yako, hakikisha unaishinda siku hiyo, hakikisha unapata ushindi, usiache siku hiyo ikushinde. Maana yake fanya yote muhimu uliyoyapanga kuyafanya ndani ya siku hiyo.

    Asante kwa kusoma uchambuzi wa kitabu hiki, mshirikishe na mwingine maarifa haya.

    @Hillary Mrosso_09.09.2022

  • Aina Tatu Za Ujuzi Unaohitaji Ili Kuongeza Thamani Yako Na Kula Mema Ya Nchi

    Kwenye hii makala ningependa tuongelee aina tatu za ujuzi ambao ukiwa nao kwenye hizi zama ni wazi kuwa unaenda kufanya vizuri na hata kuweza kufikia viwango vikubwa na vya hali ya juu sana kuliko unavyotegemea. Najua umewahi kushauriwa kujifunza aina nyingi za ujuzi, ila kwenye aina hizo zote za ujuzi ambao umewahi kushauriwa kuwa nao, hapa kuna aina tatu tu za ujuzi ambapo ukiwa na ujuzi mmojawapo ni wazi kuwa utaweza kufika mbali na hata kufanya makubwa zaidi.

    Kama umewahi kusikia kuwa kuna watu wanakula mema ya nchi, basi kwa aina hizi za ujuzi ambao utajifunza hapa, ukiweza kuzifanyia kazi vizuri, ni wazi kuwa na wewe lazima tu utaenda kula mema ya nchi. Nadhani mpaka hapo umenielewa vizuri. Sasa aina zenyewe za ujuzi hizi hapa:

    Ujuzi wa kwanza ni ujuzi wa uandishi.

    Na hapa siyo tu kuandika, bali kuandika ilimradi umeandika, bali kuandika andiko ambalo linavutia na linashawishi watu kusoma na hata andiko ambalo linasukuma watu kutoa fedha mfukoni na kukulipa wewe.

    Lakini ngoja kwanza tujiulize hili swali la muhimu

    Uandishi Ni Kitu Gani?

    Uandishi ni ujuzi wa kuwasilisha mawazo kwa watu kwa lengo la kuhamasisha, kuelemisha, kuburudisha, kuchekesha au lengo lolote lile analokusudia mwandishi. 

    Uandishi umebaki kuwa ni ujuzi muhimu sana kwenye uliwengu wa leo. Mbali na kuwa sasa hivi kuna watu wanapenda kuangalia video kwenye mitandao inayoonesha video kama youtube na tiktok, au picha kwenye mitandao ya picha kama instagram, ila ukweli ni kwamba, uandishi unabaki kuwa moja ya ujuzi muhimu sana kwenye zama za leo. Uandishi haujachuja na pengine ni ujuzi ambao unaweza kukutoa wewe hapo.

    Zama Zimebadilika

    Kwanza nipende kutangulia kwa kusema kwamba tunaishi kwenye ulimwengu ambao umebadilika sana. Yes sure, ulimwengu wa sasa umebadiika sana kuliko ilivyokuwa zamani. Kuna kipindi ambacho watu walikuwa wanawinda kwa ajili ya kupata chakula.

    Baadaye kikaja kipindi ambapo watu walikuwa wanalima kupata chakula, na tena baadaye kikaja kipindi ambapo watu walikuwa wanafanya kazi viwandani kwa ajili ya mshahara ambao ungetumika kununu chakula. Ulimwengu wa sasa hivi umehamia mtandaoni. Na hata unasoma makala hii mtandaoni.

    Uandishi umebaki kuwa mfalme kwenye ulimwengu huu wa mtandao. Kwa hiyo hizi picha zinazosambaa mtandaoni na kuvuma, hazisambai tu kwa ajili ya kusambaa, nyingi zinazosamba, utakuta kwamba zina maneno fulani, hata kama maneno kidogo. na hayo maneno yanaandikwa au kuandaliwa na mtu mwenye uelewa mzuri wa uandishi. Kwa hiyo vitu kama nukuu au maandishi mengine yanayosambaa kwa kasi, niseme pia ni sehemu ya uandishi. Ukiujua uandishi vizuri vitu vingine vidogo havitakuhangaisha.

    Uandishi ni ujuzi wa karne ya 21

    Ukiwa vizuri kwenye uandishi, hutakaa uhofie uwepo wa vitu vingine kama mitandao ya picha au video kwa sababu, huku kama mwandishi bado unafit vizuri tu.

    Kwa mfano, unaweza kuandika andiko lako, na kulisoma kwa sauti au hata kuligeuza kwenye video kwa kuongeza picha na vitu mbalimbali. kwa hiyo ukajikuta kwamba unafanya vizuri kwenye ulimwengu wa uandishi lakini pia unafanya vizuri kwenye ulimwengu wa sauti na video pia.

    Kwenye ulimwengu wa leo baadhi ya taaluma zinachukuliwa na mashine. Kwa mfano, taaluma ya ukarani inachukuliwa na mashine, sasa hivi kuna roboti ambazo zinaweza kufanya upasuaji, kwa hiyo kama wewe ni daktari, upo hatarini kuondolewa na mashine.

    Siku hizi kuna hoteli na migahawa haina wahudumu au zina mhudumu mmoja tu. tangu unafika kwenye hoteli mpaka unatoka, unahudumiwa na mashine tu, kwa hiyo kama wewe ulikuwa ni mhudumu wa hoteli au mgahawa, kazi yako ipo hatarini…..

    VIDEO FUPI YA ROBOTI ZINAVYOHUDUMIA WATEJA HII HAPA

    Sasa vipi kuhusu uandishi..

    Ndio, kuna roboti ambazo zinaandika pia…Hahah

    Lakini ni kitu gani kinaufanya uandishi kuwa kitu cha kipekee?

    Ni kweli kuna roboti ambazo zinaweza kuandika, lakini hizi roboti haziwezi kuja na kitu original (O.G). Zinaandika kwa kutumia taarifa ambazo zipo mtandaoni kwa sasa. lakini haziwezi kutengeneza kitu cha tofauti ambacho hakijawahi kuwepo…na wala hicho kitu hakitatokea kwa siku za karibuni kwa sababu uandishi ni kitu ambacho kinahusisha hisia pia.

    Mwandishi anapokuwa anaandika, kuna hisia fulani hivi anakuwa nazo, kwa hiyo uandishi ni kama sehemu ya kuhamisha zile hisia na kuziweka kwenya maandishi

    Mashine hazina uwezo wa kuwa na hisia

    Kwa mfano mtu anayeandika juu ya sherehe ya jana iliyofana. Hisia anazokuwa nazo wakati anaandika andiko lake, ni hisia ambazo roboti haiwezi kupata.. hata kama roboti ilikuwepo kwenye sherehe, haiwezi kuwa na hisia hizo…Ebu sema oyooo…

    Kwa hiyo hicho kitu kinafanya sasa uandishi uwe wa kipekee na ujuzi ambao unapaswa kuwa nao kwenye karne hii ya 21

    Lakini pia kama ambavyo nimekwambia, ukijua uandishi tu, unaweza kwenda mbele na kuhakikisha kwamba, unautumia kwenye maeneno mengine kama mafunzo ya picha, mafunzo ya sauti, video n.k.

    Ukiujua uandishi vizuri unaweza kuutumia kwenye mauzo na ukafaa.. unaweza kuhamia kwenye kilimo na ukaandika kitu kinachoeleweka na watu wakakisoma

    Unaweza kuandika kuhusu michezo

    Unaweza kuhamishia uandishi wako kwenye tasnia ya uigizaji. Yaani, popote pale utakapoenda na ujuzi wako wa uandishi, unakubalika. Hapa ningekuwa naandika kwa kimombo, ningesema the sky is the limit, ila kwa kuwa siandiki kwa lugha hiyo, naacha sisemi. hahaha

    Halafu kabla sijasahau, ujue uandishi ni ujuzi ambao ukishaujua,, umeujua!

    Kuna ule usemi wa kwamba kama ipo ipo tu… Ni kweli kwamba utapaswa kuendelea kunoa ujuzi wako wa uandishi mara kwa mara. Ila walau kuna kitu kimoja ambacho mimi nina uhakika nacho, uandishi ni kitu ambacho hakiwezi kuondolewa kwako… ukishaujua umeujua na unaweza kukuumia kwenye sekta yoyote ile…

    Ufanye uandishi ukutambulishe kwa namna kipekee

    Nimesema kwamba zama za sasa zimebadilika, nimesema kwamba uandishi ni kitu pekee ambacho kwa sasa hakitachukuliwa na roboti, lakini pia nataka niseme kwamba, utumie uandishi kukutambulisha na kujenga ujuzi mpya katika namna mbayo hakuna roboti inaweza kufanya kufanya kazi yako.

    Ebu fikiria kama wewe ni daktari na tayari roboti zimeshaanza kutibu watu, sasa unaonaje ukiunganisha utalaamu wako na uandishi (idea sexing), hapa uhakika ni kwamba, uandishi unaenda kukutambulisha vizuri sana.

    Kumbe kwa kuunganisha uandishi na kitu chochote kile ambacho unajua sasa hivi, utakuwa mtu wa pekee na wa tofauti sana.

    Kama wewe ni mhasibu, ukiongeza na uandishi kwenye uhasibu wako, utakuwa umetengeneza kitu kingine cha tofauti.

    Kama wewe ni mwalimu, ukiongeza na uandishi, utakuwa umetengeneza kitu kingine cha tofauti kabisa.

    Sasa nataka kuanzia leo uanze kuufanyia kazi uandishi. Swali langu kwako unaenda kuwa unaandika kuhusu kitu gani? Ni kitu gani?

    Kama mpaka hapo huelewi ni namna gani unaweza kuandika, naomba upate kitabu changu cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU. Hiki kitabu kitakufumbua macho kwa namna ambayo hukutegemea kwenye suala zima la uandishi.

    Kwenye makala hii nilitaka tu kukuonesha nguvu ya uandishi, na jinsi ambavyo uandishi ni ujuzi muhimu unaopaswa kuwa nao kwenye hizi zama tunazoishi kwa sasa.

    Ujuzi wa pili ni UJUZI WA KUUZA

    Huu ni ujuzi mwingine muhimu sana. Ujue kwa namna moja au nyingine katika maisha utalazimika kuuza. Ukisimama mbele ya watu kuongea ujue unauza. Ukimshawishi mtu au ukitaka mtu akubali falsafa au hoja yako basi ujue kwamba unakuwa unafanya mauzo, ukitaka kumpata mwenza lazima utatakiwa kufanya mauzo, na hata kama unahubiri bado ni uuzaji, ukitaka mwajiri wako akuongezee mshahara hayo ni mauzo pia.

    Kwa hiyo jifunze namna bora ya kuuza ambayo itawafanya watu wanunue unachouza. Jua saikolijia ya watu ili ikusaidie katika aina ya mauzo unayofanya.

    Ukiweza kuwa muuzaji mzuri basi ni wazi utaongeza thamani yako kwa viwango vikubwa sana. Ila kama haujui kuuza utalala njaa rafiki rafiki yangu.

    Unaweza kushangaa na kujiiuliza hivi kuwa si bora niwe na bidhaa nzuri? Ndio unapaswa kuwa na bidhaa nzuri, ila kama huwezi kuiuza haitasaidia. Bidhaa nzuri bila kujua kuuza vizuri utakaa nayo wewe tu.

    Kwenye kitabu cha Rich Dad Poor Dad, mwandishi amesema kwamba kuna siku alikutana na mwandishi mchanga ambaye alikuwa anataka kujua ni kwa jinsi gani anaweza kutengeneza fedha kupitia uandishi.

    Kiyosaki akawa amemwambia kwamba anapaswa kujifunza kuuza. Kiyosaki aliendelea kumwambia yule mwandishi mchanga kuwa, mimi sio mwandishi bora ila muuzaji bora. Hata ukichukua kitabu changu, hakuna sehemu utakuta imendikwa kuwa mimi ni mwandishi bora. ila imeandikwa kuwa mimi ni muuzaji bora (bestselling author).

    Kwa hiyo kitu kimoja cha kuondoka nacho siku ya leo ni kuwa unapaswa kuhakikisha unajifunza uuzaji.

    Uuzaji ndio unaleta fedha kweye biashara na kwenye maisha ya kila siku. Bila kufanya mauzo biashara zinakufa, bidhaa zinakufa, vipaji vinapotea na mengine mengi.

    Lakini kinyume chake ni tofauti, ukiweza kufanya mauzo vizuri, maana yake utapata fedha na ukiwa na fedha hakuna kitu ambacho kinaweza kukushinda kufanya. Na mauzo ndiyo yanaleta fedha.

    Ukifuatilia vizuri, watu wanaolipwa zaidi hapa duniani siyo watu wengine bali ni watu wa mauzo (salesmen and women). Watu ambao wameujua vizuri ujuzi huu hawalipwi mshahara, bali wanalipwa kwa kamisheni.

    Watanzania wengi hawajui malipo ya kamisheni hivyo huwa wanapenda mshahara, ila malipo ya kamisheni ukiyaelewa vizuri, unaweza kumwabia bosi wako leo aache kukulipa kwa mshahara, badala yake akulipe kwa kamisheni.

    Unajua kamisheni ipoje, malipo ya kamisheni ni pale ambapo mnakubaliana na mtu uakulipe kulingana na mauzo unayokuwa unafanya. Kadiri unavyoongeza juhudi kubwa zaidi kwenye kuuza na kufanya mauzo zaidi, ndivyo ambavyo unaweza kulipwa zaidi.

    Kwa mfano mkkikubaliana kuwa ulipwe kwa kamisheni ya asilimia 5, 10 au 20 malipo yako yatakuwa hivi kwa kila mauzo utakayofanya.

    KAMISHENI YA ASILIMIA
    Mauzo5%10%20%
    10,0005001,0002,000
    100,0005,00010,00020,000
    1,000,00050,000100,000200,000
    10,000,000500,0001,000,0002,000,000
    100,000,0005,000,00010,000,00020,000,000

    Kwa aina hii ya malipo, ukomo kwenye kulipwa ni wewe mwenyewe. Yaani, wewe ndiye unaweza kuamua ulipwe sana au ulipwe kidogo kwa sababu kadiri unavyokuwa unaweka juhudi kwenye kazi ndivyo ambavyo unalipwa zaidi. hivyo, juhudi zaidi maana yake zinaleta matokeo makubwa zaidi.

    Sasa unajifunzaje ujuzi huu. Anza kwa kusoma kitabu cha How I raised myself from failure to success in selling. Hiki kitabu kitakupa mwongozo na mbinu za mauzo ambazo huwezi kuzipata sehemu nyingine.

    Ukizutimua mbinu zilizo kwenye hiki kitabu, ni uhakika kuwa utaweza kufika mbali, tuwasiliane kwa songambele.smb@gmail.com ili niweze kukutumia kitabu hiki usome.

    Ujuzi wa tatu ni KUNENA

    Siku moja kuna kijana alimwuliza Warren Buffet kuwa ni ushauri gani ambao unaweza kuutoa kwa kijana mwenye umri wa miaka 21 au 22 kuhusu mafanikio? Bila kusitasita Warren Buffet alimweleza kuwa ushauri wangu kwa kijana mwenye umri wa miaka 21 au 22 ni kuwa ajifunze na kuelewa kwa undani ujuzi wa kuwasilisha hoja kwa watu, na hii inaweza kuwa ni kwa njia ya maandishi au kuongea.

    Kama umegundua kitu, ni kuwa makala hii inajihusisha zaidi na ujuzi huu mmoja wa kuwasilisha hoja zako kwa watu. ila ujuzi huu tumeugawa kwenye aina tatu ndogo za ujuzi ambapo hapa tayari tumeongelea ujuzi wa kuandika, ujuzi wa kuuza na sasa tunaongelea ujuzi wa kunena.

    Huu ni ujuzi mwingine ambao unaweza kuongeza kipato mpaka asilimia 50 au hata zaidi.

    • Wanasiasa
    • Wafanyabiashara
    • Wanamichezo na wengine wengi huwa wanatumia huu ujuzi

    Huu ni ujuzi wa tatu muhimu sana. Kunena au kama kunavyofahamika kwa kiingereza ni public speaking. Huu ni ujuzi mwingine ambao ukiwa nao utaongeza thamani yako kwa viwango vikubwa sana.

    Ni wazi kuwa huwa tunapenda sana watu ambao huwa wanaongea na kutoa hoja zinazovutia. Kuna mtu akisimama kuongea mwili unasisimuka kwa kuona jinsi anavyowasilisha mada yake. Hiki ni kitu ambacho na wewe unaweza kukijua na kukifanyia kazi kwa manufaa yako. Wanasiasa wanatumia sana hiki kitu wakati wa kampeni kwa ajili ya kuomba kura. Wasemaji wa timu za mpira wanatumia ujuzi huu pia kwa ajili ya kuvuta umakini kwenye vyombo vya habari.

    Kila siku tunakutana na watu na tukiwa na watu hawa tunaongea, tunawasilisha na kujadili mada, tunacheka na kufurahi

    Lakini unahitaji kujifunza kunena. Na kunena ni zaidi ya kuongea. Najua utauliza sasa kunena ni nini? Kwa haraka tu naweza kusema KUNENA ni KUONGEA NA WATU WAKASILIZA.

    Sasa kuongea na watu wakusikilize wewe ni kazi. Na sio kazi ndogo. Nadhani imewahi kukutokea  unaanza kumsikiliza mtu ila unagundua kuwa hana pointi za maana. Yaani amesimama mbele yako na wewe unaona wazi kwamba hakuna kitu cha maana anaongea.

    Omba isikutokee wewe. Na namna nzuri ya kuomba ni kujifunza uneni kuanzia leo hii

    Sasa zifuatazo ni mbinu saba unazoweza kutumia kwa haraka ili kuongeza ujuzi wako wa kunena.

    Moja ni kutafuta fursa ya kuongea mbele ya watu, kwa kuanzia unaweza kuanza na hadhira ndogo tu watu wachache pengine hapo hapo nyumbani. Unaweza kuwakusanya ndugu zako wa karibu na kunza kufanya mazoezi mbele yao. Na hata muda mwingine siyo lazima uwaambie.

    Kama huwa mnasali pamoja pale nyumbani unaweza kuwashawishi kuongeza na kipengele cha neno la Mungu, halafu kile kipande cha kufafanua neno la Mungu ukakibeba wewe, na ukautumia huo kama muda wako wa kuwasilisha yako na sehemu ya kujifunza uneni.

    Lakini pia unaweza kuandaa kikundi cha watu na kuwaeleza kuwa utakuwa unafanya mazoezi ya kuongea mbele yao, hivyo unaomba wakupe mrejesho baada ya kuwa umewasilisha mada yako. Sana sana hawa wawe ni watu ambao wanaweza kukupa mrejeho bila ya kukuogopa.

    Pili ni tenga muda wa kufanya mazoezi kwaa ajili ya kunoa ujuzi wako huu. Dakika kumi mpaka thelathini kila siku zitafanya kazi.

    Tatu, hakikisha umeandika kwanza hotuba yako, kisha ifanyie mazoezi. Hiki ni kitu kidogo sana ila chenye nguvu kubwa sana. Kanuni muhimu kwenye kufanya mazoezi unayopaswa kuitumia ni kuwa, kama utatakiwa kuongea kwa dakika 12, basi utapaswa kujiandaa kwa  dakika 120 kabla ya kutoa hotuba yako.

    Nne, jifunze kwa kusoma vitabu. hiki kitu kitakufanya uongeze maarifa na kuielewa mada husika kwa undani, hivyo utaweza kuwasilisha mada yako huku ukiwa na uelewa mkubwa zaidi. Kadiri unavyosoma ndivyo unavyojua zaidi na watu wanapenda kusikiliza mtu mwenye kitu cha kusema na kadiri watu wengi wataavyokuwa tayari kukaa chini na kukusikiliza, ndivyo ambavyo kipato chako kitakuwa kinaongezeka zaidi.

    Tano ukiwa kwenye kikundi cha watu, chagua mtu mmoja ambaye utakuwa unamwagalia wakati unaongea. Ujue ni muhimu sana kuangalia watu wakati uhnatoa hotuba yako, sasa ukianza kuongea mbele ya watu, kama unaogopa kuwaangalia watu, chagua mtu mmoja ambaye utamwangalia na kisha unaweza kuhama kutoka kwake na kuwangalia mwingne kadiri muda unavyoendelea.

    USHAURI WANGU: Chagua aina moja ya ujuzi ambao unaweza kuanza kuufanyia kazi leo.

    Usianze na kila ujuzi. Anza na ujuzi mmoja, ufikishe kwenye viwango vikubwa. Kisha kuza ujuzi mwingine. Mwisho wa siku utajikuta umeweza kujenga kila ujuzi.

    Rafiki yangu hizo ndizo aina tatu za ujuzi ambao unapaswa kuwa nao.

  • Kitabu ChaNGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA: Utangulizi wa kitabu kama ulivyoandika kwenye kitabu chenyewe

    Habari ya siku ya leo rafiki yangu, siku ya leo ningependa nikushirkishe Utangulizi wa kitabu cha NGUVU ya vitu vidogo kama ulivyoandikwa kwenye kitabu chenyewe. Nina hakika wewe mwenyewe utaufurahia, baada ya kuwa umesoma Utangulizi huu, usisite kujipatia nakala ya kitabu hiki kwa kuwasiliana nami mwandishi kwa simu 0755848391. Sasa utangulizi wenyewe huu hapa chini.

    Gharama ya kitabu hiki ni 20,000/- za kitanzania

    Hivi umewahi kujiuliza kuwa vitu vidogo vinaweza kukusaidia kitu gani maishani mwako?

    Hivi kwa mfano, kitu kidogo kama kuamka asubuhi na mapema kinaweza kukusaidia nini maishani mwako kikifanywa kila siku na kwa mwendelezo? Au je, kitu kidogo kama kuwekeza au kuweka akiba kikifanywa kila mara kwa muda mrefu kinaweza kukusaidia nini? Kwenye kitabu hiki hapa tunaenda kuona nguvu ya vitu vidogo na jinsi nguvu hii inavyoweza kukusaidia wewe kufikia mafanikio makubwa maishani mwako.

    Mara nyingi sana watu huwa wana ndoto kubwa na malengo makubwa ya kufikia kifedha, kimahusiano, kibiashara au kikazi. Lakini cha kushangaza ni kwamba huwa hawafanyii kazi hizo ndoto kubwa walizonazo bali huwa wanasubiri itokee siku moja ya muujiza ambapo ndoto yao itatimia kwa asilimia zote.

    Kitu hiki hakiwezekani. Ni wazi kuwa lako la mwaka haliwezi kutimia siku ya mwisho ya mwaka baada ya wewe kuwa umekaa mwaka mzima bila ya kufanya kitu chochote, badala yake kama kweli utaweka kazi na kufuata hatua zote unazopaswa kufuata ili kulifikia hilo lengo lako la mwaka basi utalifikia kwa kufanya vitu kidogo kidogo kila siku.

    Kitu chochote kikubwa kinaweza kufanikishwa kwa kuchukua hatua ndogondogo na kwa mwendelezo na hatimaye kuzifanya ziwe hatua kubwa. Mafanikio makubwa siyo kufanya vitu elfu moja mara moja, ila kufanya vitu vidogo mara elfu moja, yaani, kwa mwendelezo na bila kuchoka. Hivi vitu vidogo hatimaye vinapelekea kitu kikubwa na mafanikio makubwa.

    Confucius, mwanafalsafa wa Kichina aliwahi kunukuliwa akisema kwamba, “safari ya maili elfu moja huanza na hatua moja”. Hii ndiyo kusema kwamba mambo makubwa siku zote huwa yanaanza kwa hatua ndogondogo kisha kuendelea kukuzwa. Hakuna kitu kikubwa ambacho unakiona leo hii ambacho kilianza kikiwa kikubwa hivyohivyo. Ndiyo maana wahenga walisema kwamba; “hata mbuyu ulianza kama mchicha.” Jogoo anayewika kuna siku alikuwa kifaranga.

    Ukitaka kugundua kwamba vitu vikubwa huanza kwa udogo basi unaweza kuangalia ujenzi wa ghorofa. Huwa unaanza kwa hatua ndogo ndogo za kuchimba msingi, baadaye huwa wanaanza kuweka jiwe au tofali moja baada ya jingine hatimaye kitu kilichokuwa chini huwa kinaendelea kusimama na kufikia hatua ya kuwa kitu kikubwa sana.

    Siku moja nilikuwa nasoma historia ya jengo ambalo limo kwenye maajabu saba ya dunia. Jengo hili siyo jingine bali ni jengo la Taj Mahal. Hili ni miongoni mwa majengo yaliyojengwa kwenye karne ya 15, na jengo lenye historia ndefu na kubwa sana. Unajua jengo hili lilijengwa kwa miaka mingapi? Unaweza kuwa sahihi. Lilijengwa kwa miaka ishirini na mbili (22). Kila siku watu walikuwa wanaweka tofali moja, siku nyingine tofali jingine, siku nyingine nondo, hatimaye lile jengo lilikamilika baada ya miaka 22!

    Wajenzi hawakusubiri mwaka wa 22 ili wajenge hilo jengo. Ila walikuwa wakilifanyia kazi hilo jengo hatua kwa hatua kila siku bila kuchoka. Hili nalo litupe picha ya kuwa vitu vikubwa vinawezekana kufanyika na kuja katika uhalisia endapo vitafanyiwa kazi kwa kuanza kidogo kidogo, na kwa mwendelezo na kupewa muda ili viweze kuanzia chini na kukua.

    Usidharau vitu vidogo. Kuna mfano, wa nyuki aliyeingia kwenye sikio la tembo na kuanza kupiga kelele. Tembo yule alianza kuruka huku na kule ili nyuki yule atoke kwenye sikio lake ila nyuki hakutoka. Tembo alianza kuangusha miti na kujibamiza kwenye miti pengine akidhani kwamba huyo nyuki atatoka ila huyo nyuki hakutoka. Baada ya muda mrefu wa kuhangaika, tembo alianguka na hivyo akawa amepoteza maisha. Kinaweza kuonekana kama kitu cha kushangaza, ila vitu vidogo muda mwingine huwa vina madhara makubwa sana.

    Mbu ni wadogo, ila madhara yake ni makubwa. Sindano ni ndogo ila kikuchoma, wewe mwenyewe ni wazi kuwa utakipata cha mtema kuni. Kwa hiyo basi, nikuombe kuwa ujenge utaratibu wa kuheshimu vitu vidogo maana vinaweza kukupelekea kwenye mafanikio makubwa au la vikakupelekea kwenye anguko kuu maana kuna nguvu katika vitu hivi vidogo. Nguvu hii inaweza kukuinua ukiitumia vizuri ila ukiitumia vibaya itakuangusha. Na nguvu hii ndiyo tunaenda kuiona kwenye kitabu hiki hapa.

    Endapo utakisoma kitabu hiki na kuanza kufanyia kazi yale utakayojifunza, sipati picha jinsi ambavyo utaanza kujenga six packs ambazo umekuwa unatamani kwa siku nyingi, akiba utakayoweka, vitabu utakavyoweza kuandika, utakavyoweza kukamilisha majukumu yako kwa wakati, jinsi utakavyoboresha mahusiano yako na mengine mengi.

    Kila la kheri

    Godius Rweyongeza

    Februari 15,2020

    Morogoro-Tz

    kitabu hiki cha NGUVU YA VITU VIDOGO kinapatikana pia kwa mfumo wa audiobook kama inavyoonekana hapo juu na sample ya audiobook hii ha[o chini

    Rafki yangu, huo ndio utangulizi kutoka kwenye hiki kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA, nashauri sana uhakikishe kwamba umepata kitabu hiki cha kipekee. Gharama ya kitabu hiki ni 20,000/- tu. Ili kupata nakala ya kitabu hiki, tuma wasiliana na 0755848391 ili aweze kukutumia kitabu hiki popote pale utakapokuwa.

  • Vitabu Viwili Unavyopaswa Kuhakikisha umesoma mwezi huu wa tisa

    Habari ya leo rafiki yangu, siku ya leo ningependa kwa ufupi nikwambie vitabu vitano ambavyo unapaswa kusoma ndani ya mwezi huu wa tisa.

    Bila kupoteza muda, vitabu vyenyewe ni

    1. The school of money

    Hiki ni moja ya kitabu muimu sana ambacho unapaswa kusoma hasa kuhusiana na suala zima la fedha. Kitabu hiki ndani yake kimeeleza mbinu na kanuni za kukusaidia wewe kuweza kupiga hatua na kusongambele kwenye suala zima la fedha. Kama kuna kitabu kimoja cha fedha utapaswa kusoma ndani ya mwezi huu wa tisa, basi soma kitabu hiki cha The school of money. Kama utahitaji kupata softcopy ya hiki kitabu, basi unaweza kunitumia ujumbe kwa namba ya 0755848391 ili nikueleze namna ya kuipata.

    2 NGUVU YA VITU VIDOGO KUELEKEA MAFANIKIO MAKUBWA

    Najua kuwa una malengo na ndoto kubwa za kufanyia kazi na hata kufikia mwaka huu, ila unajua nini. Malengo yako haya, unahitaji kuyafanyia kazi hata kwa udogo. Hii ndio dhana nzima ya kitabu cha nguvu ya vitu vidogo kuelekea mafanikio makubwa. kwenye hiki kitabu unaenda kujifunza mbinu na kanuni za kukusaidia wewe kuweza kufanyia kazi na kufikia lengo au ndoto yoyote ile kwa kuanza kidogo. Hatua ndogondogo mwisho wa siku zinaleta matokeo makubwa.

    Kitabu hiki kinapatikana kwa mfumo wahardcopy na audiobook

    Gharama ya hardcopy (nakala ngumu) ni 20,000/- unatumiwa kitabu hiki popote pale ulipo duniani.

    Gharama ya audiobook ni 10,000/- tu. na hii utaipata bila kujali upo wapi hapa duniani, ndani ya dakika chache tu baada ya kulipia.

    kitabu cha NGUVU YA VITU VIDOGO

    Hivi ni vitabu viwili ambavyo unapaswa kusoma ndani ya mwezi hu wa nane rafiki yangu.

    Ubora ni kuwa kitabu kimojawapo kimesomwa kwa sauti na unaweza kukisikiliza kwa sauti, hivyo unakuwa huna shida ya kukaa chini na kuanza kukisoma moja kwa moja. Hiki kitu kinakufanya uweze kwa hakika kusoma vitabu viwili kwa mwezi huu na kuvimaliza. Kama utapata vitabu hivi viwili, kimoja unaweza kukisiliza kwa njia ya sauti, huku kingine ukiwa unakisoma kwa njia ya kawaida. Hiki kitu kitakusaidia sana kuweza kupata maarifa sehemu mbili na kunufaika kwa ukubwa sana.

    Rafiki yangu, soma vitabu hivi viwili, nina hakika utanishukuru sana kwa miezi ijayo na miaka inayofuata.

    Sina cha kukusaidia zaidi ya kusema wasiliana na mimi sasa ili uweze kupata hivi vitabu vyote viwili kwa wakati mmoja.

    Mimi hapa sina la ziada

    Akhsante

  • JINSI UBUNIFU UNAVYOWEZA KUKUINUA KWENYE BIASHARA

    Siku moja nilikuwa naongea na rafiki yangu Edius Katamugora, akawa ameaniambia juu ya kinyozi aliyekuwa anatengeneza app ya kuwakumbusha wateja kurudi kunyolewa. Yaani, app yenyewe ingekuwa inafanya kazi hivi,

    Pale Ambapo ungekuwa unaenda kunyoa kwa yule fundi kinyozi, angekuwa anachukua namba yako, saa chache baada ya kuwa umenyoa app ingekutumia ujumbe kukushukuru kwa kuja konyoa. Wakati app hiyohiyo ikikutumia ujumbe wiki mbili mbeleni ikikumbusha kunyoa kwa mara nyingine. Maana kwa kawaida Ndani ya wiki mbili nywele zinakuwa zimeshaota, kiasi cha kuhitaji kunyoa tena. Huu ni ubunifu.

    Siku nyingine nilikutana na jamaa ambaye alikuwa anatunza namba Simu za wateja wanaofanya miamala kwake, siku nyingine ulipokuwa unaenda kufanya muamala kwake badala ya kuanza kukuuliza namba yako ni ipi, alikuwa anakuuliza unatuma kwenye namba ileile au tofauti. Ukisema ileile basi hapohapo alikuwa anaendelea na muamala bila kukuuliza namba yako.Huu pia ni ubunifu mwingine.

    Ubunifu kwenye biasharani moja ya kitu muhimu Sana ambacho Unahitaji kulifanyia kazi. Ubunifu unawapa sababu ya wateja kuja kwenye BIASHARA yako badala ya biashara za watu wengine.

    • Unaweza Kuwa ubunifu wa KUWEKA benchi za watu kukaa.
    • Unaweza pia kuwa ubunifu wa kukumbuka kitu alichonunua mteja mara mwisho au mbacho anapendelea kununua mara kwa mara.
    • Unaweza Kuwa ubunifu wa kuwapa watoto pipi moja ya shilingi 50 kila wanapokuja kununua dukani kwako. Si unajua watoto huwa wanatumwa sana na wazazi, ukibuni kitu Cha kuwapa motisha, unashangaa kila wanapotumwa wanakuja dukani kwako kununua.
    • Unaweza kuwa mbunifu kwa kuwapa wataje wako ofa, hata ya  kitu kidogo pale wanaponunua kwako mara kwa mara.
    • Kwa vyovyote vile ubunifu Ni moja ya kitu muhimu sana unachohitaji.

    Ubunifu unakutofautisha wewe na watu wengine ambao wanakuwa wanafanya kitu Cha kwako. Ubunifu unawapa watu sababu ya kuja kununua kwenye biashara yako badala ya kwenda kununua kwingine [MSISITIZO].

    Na ubunifu siyo tu kwenye biashara,ubunifu unaweza kuutumia kwenye Kipaji chako, elimu yako, mahusiano, n.k. Ndio maana nimeandika kitabu Cha akili ya Diamond Kitabu kinachoeleza mambo 50 ya kujifunza kutoka kwa Dimond Platnumz Kuhusu Ubunifu, Kipaji Na Mafanikio. Unaweza kukipata kwa kuwasiliana na 0755848391

    Ubunifu kwenye biashara.

    Hivi ninapoandika HAPA, naendelea kusoma kitabu cha THE SCHOOL OF MONEY. Juzi wakati nakisoma nilikutana na kitu ambacho kilinifurahisha sana. Ilikuwa Ni hadithi fupi ya dereva teksi ambaye aliongeza ubunifu kwenye Kazi yake na kuanza kulipwa mara mbili mpaka mara kumi zaidi ya alivyokuwa analipwa mwanzoni.

    Mwandishi anaieleza siku alivyoshuka uwanja wa mdege (airport) na kukutana na dereva huyo. Dereva yule alivyosimamisha teksi tu, wakati anaingiza mizigo ya abiria wake kwenye gari alimpa abiria wake karatasi. Kwenye karatasi hiyo kulikuwa na maono makubwa ambayo dereva huyo anayafanyia kazi na msimamo ambao dereva anausimamia kwenye uendeshaji teksi.

    Kitu hiki kilimshangaza kidogo mwandishi maana hakuwahi kuona dereva wa aina hii popote pale duniani. Mwandishi wa kitabu hicho aliposoma kwenye Ile karatasi mojawapo wa kauli, ilisema lengo langu ni kusafirisha na kuwafikisha abiria kwa usalama wa hali ya juu.

    Wakati mwandishi akiwa anaendelea kutafakari Hilo, dereva alikuwa amemaliza kupakia mizigo yake, na hivyo muda huohuo aliingia kwenye teksi yake.

    Alivyokaa tu kabla ya kuwasha teksi kuondoka, alimwambia abiria wake huwa ana utaratibu wa kuwapa abiria wake kahawa, hivyo alimkaribisha aweze kupata kahawa.

    Abiria alikataa kwa kusema hapendi kahawa Bali anapenda kinywaji Baridi. Palepale dereva akamtolea soda nzuri na kumpa yule mteja wake. Hiki kitu kilimshangaza abiria kiasi akawa anakuuliza mbona napata huduma za viwango vya kifalme?

    Baadaye abiria alifunguka na kumwuliza dereva teksi, huwa unafanya hivi kwa abiria wako wote? Hapo ndipo dereva yule alijieleza kwa kusema kuwa KWELI huwa anafanya hivyo kwa kila abiria. Akaendelea kwa kueleza historia yake ya siku za nyuma.

    Ambapo hapo zamani alikuwa kama madereva teksi wengine. Alikuwa analalamila kuwa maisha Ni magumu. Sasa siku moja alikaa na kutafakari kuona utofauti gani yeye anao ambao watu wengine hawana. Alichokuja Kugundua Ni kuwa yeye na madereva wengine walikuwa wanafanya kazi yao kwa mazoea.

    Teksi zao wote zilikuwa chafu. Walikuwa hawachukui mawasiliano ya wateja wao baada ya kuwabeba ili waendelee kuwasiliana na endapo siku nyingine hao abiria wana safari wawasiliane nao waweze kuwasafirisha kwa mara nyingine.

    Dereva huyo anasema tangu siku hiyo hakuwahi kurudi nyuma na Wala hakuwahi kufanya kazi yake kama ambavyo mtu mwingine alikuwa akifanya. Alijitofautisha.

    Kitu hiki kilimfanya kwanza asiwe tu anakaaa kwenye vijiwe bila mwelekeo, maana watu wengi walikuwa wkintafute huyo dereva, na hata mwandishi kukutana na yule dereva ilikuwa ni kama bahati, siku hiyo. Maana dereva huyo yuko bize muda wote akisafirisha abiria wanaompigia na abiria wengine wapo tayari kulipia fedha yao mapema ili tu waweze kusafirishwa na yule dereva.

    Huo pia ni ubunifu.
    Na wewe Unahitaji kufanya ubunifu kwenye biashara yako au kitu chochote unachofanya. Wape watu sababu ya kuja kununua kwako badala ya kwenda kununua kwa mwingine.

    Wape watu sababu ya kufanya biashara na wewe na siyo mwingine. kuwa mbunifu.

    Ubunifu wa KUONGEZA teknolojia.

    Moja ya kitu ambacho nimekuwa nikiwaambia watu wengi ni kuwa kwenye Biashara yoyote Ile unayofanya unapaswa kuangalia namna gani unaweza KUONGEZA teknolojia. Ukifuatilia Biashara nyingi zinazofanyika kwenye kipindi Cha leo, utagundua kuwa kitu kikubwa ambacho Biashara hizi zimefanya Ni KUONGEZA teknolojia au intaneti kwenye biashara ambazo zikikuwepo kwa siku nyingi zilizopita.

    Watu wamekuwa wanauza na kununua vitabu Vitabu kwa siku nyingi kabla ya amazon. Walichofanya Amazon Ni KUONGEZA teknolojia au intaneti kwenye uuzaji wa vitabu. Badala ya mtu kuhangaika kurafuta vitabu umbali mrefu, Sasa anaweza kuvinunua akiwa chumbani kwake tu.

    Amazon wanafanya Biashara ya kuuza vitabu, Ila Biashara ya kuuza vitabu siyo ngeni kwenye macho ya watu. Ni Biashara ambayo imekuwepo kwa siku nyingi sana ila Amazon wameipa uhai zaidi kwa kuiongezea teknolojia na intaneti.

    Wewe pia kwa Biashara yako unayofanya unaweza kufanya kitu Kama hiki. Unaweza KUONGEZA teknolojia au intaneti. Huo Ni ubunifu rafiki yangu

    Usiache kuchukua kitabu changu cha JINSI YA KUIBUA UBUNIFU ULIO NDANI YAKO kwa 7,000 tu/- softcopy. Hki pia kimebuniwa kwa namna ya kipekee. Na kinauzwa kwa njia ya kibunifu ya mtandao, hahaha

    Ukifanya kitu unachopenda ubunifu unakuw amwingi

    Kuna siku nilikuwa nikiongea na mteja wetu mmoja ambaye yuko mkoani Mara (Msoma mjini). Siku hiyo alikuwa amepokea kitabu cha jinsi ya kufikia NDOTO ZAKO na kuanza kukisoma.

    Kitu cha pekee nilichopenda kutoka kwake ni usemi wake anaosema kuwa ukifanya kitu unachopenda, Ubunifu unakuwa mwingi.

    Na hiki kitu nimeona nikushirikishe na wewe pia.

    Kuna utafiti unaonesha kuwa watu wengi wanakufa siku ya jumatatu baada ya kula Bata wikendi halafu jumatatu wanaamka na kwenda kufanya kazi wasiyopenda. Hicho kitu tu, kinawakatisha tamaa.

    Ndiyo maana nimeupenda huu usemi, kiasi cha kuwa tayari kukushirikisha huu usemi na wewe.

    Ujumbe mkubwa ninaotaka kusisitiza hapa ni kuwa ukifanya kitu unachopenda, ubunifu unakuwa mwingi.

    Ukifanya kitu unachopenda hutachoka Ukifanya kitu unachopenda ubunifu unakuwa mwingi.

    Thomas Edison alikuwa analala saa tatu kwenye maisha yake na kuamka mapema kwenda kazini. Siku moja aliulizwa kwa nini unafanya sana kazi.

    Aliwajibu watu kwa kuwaambia kuwa sijawahi kufanya kazi.

    Umeona ee! Alikuwa anafanya kitu anachopenda. Hivyo, kwake hakuona kama hiyo ilikuwa kazi.

    Hivi wewe unafanya unachopenda kweli? Unafanya unachopenda?

    Ngoja nikukumbushe, “ukifanya kitu unachopenda, ubunifu unakuwa mwingi”.

    Ubunifu Unaboresha Biashara Yako

    Kama wewe umekuwa mtumiaji wa muda mrefu kidogo wa mtandao wa WhatsApp utagundua kuwa mtandao huu umekuwa unafanyiwa marekebisho ya hapa na pale kila mara. Kuna kipindi haya mambo ya status au WhatsApp business hayakuwepo.

    Nakumbuka suala zima la kubold, italicize, underline na strikethrough na yenyewe hayakuwepo.

    Ila kadiri siku zilivyoendelea yamewekwa. Hayo ni machache tu kati ya marekebisho mengi ambayo wamefanya.

    Ninachotaka kukwambia ni kwamba kwenye biashara yako, ni vizuri kuwa mtu wa kufiria nje ya boksi na kufikiria zaidi ya hapo ilipo kwa sasa.

    Ubunifu utaitofautisha sana biashara yako na biashara za watu wengine. Maana hata ukisema ufanye biashara ambayo haijawahi kufanywa hapa duniani. Ndani ya miezi sita tu, kuna watu watakuona ukiifanya na wenyewe wataanza kuifanya. Kumbe basi, kitu pekee ambacho kinaenda kukutofautisha wewe na wengine ni ubunifu.

    Ubunifu Siyo Mpaka Uwe Na Wazo Ambalo Halijawahi Kuwepo

    Wengi wanapofikiria ubunifu basi wanadhani, mbunifu yeyote anapaswa kuja na wazo la kipekee sana na wazo ambalo halijawahi kuonekana. Unaweza kuja na wazo la kawaida, ila kwenye biashara yako likawa linaleta mapinduzi.

    Inashauriwa walau kila siku uwe unafikiria mawazo ya kawaida kumi tu na kati ya hayo utoe moja au mawili ambayo utayafanyia kazi. Ukiwa mtu wa kufikiria hivi ni uhakika kuwa mwaka mmoja baadaye, kama ni biashara, lazima tu utakuwa umeisukuma mbali.

    Ubunifu Siyo Mpaka Uwe Profesa

    Ubunifu ni kitu tunazaliwa nacho. Ndiyo maana utagundua kwamba kila mtoto huwa anapenda kuumba vitu mbalimbali kwa kutumia udongo, mchanga au malighafi zozote anazoona zinamfaa.

    Kwa hiyo hiki kiwe kiashiria kwako kuwa UBUNIFU ni kitu tunacho, tumezaliwa nacho na tunaenda nacho popote. Kadiri ambavyo utautumia ubunifu kwenye kazi, biashara au eneo lolote, ndivyo utakavyoimarika zaidi na zaidi.

    Moja kati ya vitu muhimu sana katika biashara, mahusiano na kazi ni ubunifu. Ni kupitia ubunifu mtu unaweza kuja na mbinu mpya za kuongeza wateja, ni kupitia ubunifu unaweza kujua ni bidhaa gani ukiiboresha zaidi itakuongezea wateja zaidi. Ni kupitia ubunifu utajua ni bidhaa gani ukiipunguza  au ukiiondoa kwenye mfumo wako wa biashara utakuwa hujapungukiwa na kitu. Kwa hakika binafsi nauita ubunifu moyo wa biashara.

    Sasa ubunifu ni nini?

    Mpaka hapa utakuwa unajiuliza huu ubunifu unaoongelewa ndio unafananaje? Ndio nini haswa?

    Vyanzo mbali mbali vimeudadafua ubunifu kama matumizi ya njia bora zaidi zinazokidhi kutatua changamoto mpya, changamoto ambazo tayari zipo lakini hazijapatiwa ufumbuzi bado, au changamoto zilizopo kwenye soko au jamii kwa kipindi husika.

    Hata hivyo kwa mantiki ya andiko hili, tutatumia maana ifuatavyo UBUNIFU NI HALI YA KUJA NA WAZO JIPYA LA KUBORESHA, KUIMARISHA AU KUBADILISHA KITU KATIKA NAMNA YA UPEKEE.

    Ubunifu katika biashara ni wa aina mbili. Kwanza kuna ubunifu mlalo na ubunifu sambamba.

    Ubunifu mlalo ni aina ya ubunifu ambapo mtu unakuwa na kitu kimoja ila unakikuza kitu hicho hicho zaidi na zaidi. Mfano mtu unagundua kwamba kalamu za aina fulani zinapendwa sana na watu katika eneo langu. Basi unaongeza uzalishaji wa kalamu za aina hiyo hiyo ili ziwe nyingi zaidi. Huu ndio unaitwa ubunifu mlalo.

    Ubunifu sambamba. Huu ni ubunifu ambao unatokea pale unapokuwa unazalisha kitu kimoja ila ukagundua kwamba ili kitu hiki kifanye kazi vizuri basi hapa tunahitaji kitu kingine cha ziada. Kwa kutumia mfano wetu hapo juu. Unazalisha kalamu ila unagundua kwamba ili kalamu yako ifanye kazi vyema basi inahitaji daftari. Hivyo unaanza kuzalisha na daftari. Huu ndio  ubunifu sambamba. Ubunifu sambamba tunaweza kuuona katika maeneo mengi sana kwenye maisha yetu. Ukiangalia uwepo wa simu umesababisha uwepo wa laini za simu. Huu ni ubunifu sambamba. Uwepo wa viatu umezalisha uhitaji wa soksi huu nao ni ubunifu sambamba.

    Mtu anayeuza runinga lazima tu atatakiwa kuwa na remote na hata ving’amuzi, huu pia ni ubunifu sambamba.

    Jinsi ya kutumia aina hizi mbili za ubunifu.

    Bila shaka mpaka hapo utakuwa unajiuliza, hivi hizi aina mbili za ubunifu zitanisaidiaje kwenye biashara zangu?

    Jibu ni rahisi sana. Kama kuna biashara yako unafanya sasa hivi. Angalia ni bidhaa gani inapendwa zaidi na watu. Ukishaipata bidhaa ya namna hii basi izalishe zaidi na hakikisha unaongeza mauzo. Kumbuka mapato makubwa sana kwenye biashara yako hayatoki kwenye kuuza kila kitu. Ila yanatokea kwenye kuuza bidhaa chache kwa wingi sana. Sasa hapa unahitaji kukaa chini na kujiuliza ni bidhaa gani hizi chache ambazo nikizizalisha kwa wingi zitaongeza mapato makubwa sana.

    Au ni bidhaa gani nikiziongeza kwa wingi kwenye mzunguko bado nitazidi kuuza sana. Hapa utakuwa umetumia ubunifu mlalo.

    Unaweza pia kutumia ubunifu wima kwa kuangalia aina ya bidhaa ambayo ukiizalisha itakuwa inaendana na ile ambayo ulikuwa hapo awali. Jiulize ni bidhaa gani inaweza kwenda sambamba na bidhaa ninayouza sasa hivi na ikauza vizuri bila shida? Mfano rahisi sana ni pale unapokuwa unauza majiko ya gesi. Unaweza kuongeza kitu cha ziada kwa kuuza vyombo vingine vinavyotumika jikoni. Ukiweza kuvijua vitu hivi vinavyoenda sambamba na ile bidhaa ya awali baasi hapo utakuwa umetumia ubunifu sambamba.

    Kwani kuna ulazima wa kutumia ubunifu kwenye biashara?

    Zama zimebadilika, maisha nayo yamebadilika, lakini pia mfumo wa uendeshaji wa biashara umebadikika.

    Katika zama za sasa biashara zinazoendeshwa kibunifu ndizo biashara zinazopendwa na watu. Kwa hiyo ubunifu sio tena suala la hiari, ni lazima. Tungekuwa kwenye miaka ya 50 na 60 kabla uhuru ambapo maduka na wafanyabiashara walikuwa wachache sana, hapo suala la ubunifu tungeliweka pembeni na kushughulika na mambo mengine. Ila kwenye zama hizi hapa hakuna jinsi ubunifu ni lazima.

    Lazima kuwepo na sababu za kwa nini watu waje kununua kwako na sio kwa rafiki yako mwenye duka na anauza bidhaa kama unazouza. Sasa hapo ubunifu ndipo unaingilia katikati. Kwa hiyo ubunifu ni lazima wala sio ombi!

    Ubunifu ni muhimu kwenye biashara, michezo, sanaa, uigizaji, ufundishaji, mziki, upambaji n.k. yaani maisha na ubunifu ni vitu ambavyo hatuwezi kabisa kuvitenganisha 

    Sasa kama ubunifu ni muhimu kwa nini watu sio wabunifu?

    Mbali na kwamba tumeona ubunifu ni muhimu sana kwenye biashara na maisha ya kawaida bado ubunifu haujapewa kipaumbele hata kidogo kwenye bara la Afrika. Kuna watu wengi sana wamezaliwa na vipaji vikubwa sana vya kubuni na kuja na mbinu mpya ila bado hawajavitumia. Hizi hapa ni sababu zinazofanya watu wafanye vitu kwa namna ile ile kila siku bila kuongeza thamani za kibunifu.

    1.  KILA MTU ANAFANYA HIVYO

    Mara nyingi sana watu wapo katika mazingira ambayo kila kinachofanyika basi kinafanyika kwa namna ile ile tu.

    Yaani kwamba ameamka asubuhi, ameoga na kuzunguka  huku na kule, na kila mtu anafanya hivyo basi na yeye anaishi hivi. Maisha haya hayawezi kuzalisha wabunifu wakubwa. 

    2. BABU ZETU WALIKUWA WANAFANYA HIVI

    Hivi ushawahi kuthubutu kufanya kitu ukasikia mtu anakwambia “usifanye hivyo, babu zetu hawakuwahi kufanya kitu kama hicho“. Yaani watu wanatengeneza sheria zao wenyewe, wanazipitisha wao wenyewe na kutaka ziwe sheria za watu wote.

    Sasa kwamba baba au babu alikuwa anafanya vile ina athari gani na mimi nikifanya kwa namna nyingine. Maneno haya yanatumiwa sana na watu ila kiukweli ni kwamba hata hayajengi na hayana mantiki. Hivyo ni vyema kabisa kwa wewe kama wewe kujua kwamba tunapaswa kubuni na kuja na mbinu mpya za kibunifu kila wakati.  Kuendelea kufanya vitu kwa namna ile ile kila siku hakuwezi kukuinua na kutusogeza mbele Tanzania na Afrika nzima kiujumla. Nipo nafikiri kama Albert Einstein angeendelea na fikra zile zile za mababu wetu walikuwa wanafanya hivi angeweza kugundua sheria MC²?

    Hivi kama Mark Zuckerberg angeendelea kushikilia imani ya kwamba babu zetu walikuwa wanawasiliana hivi, angeweza kuja na mtandao wa kijamii wa facebook. Ebu watanzania badilikeni kabisa. Achana na mambo ya babu zetu walikuwa wanafanya hivi au vile. Sasa zama zimebadilika, maisha nayo yamebadilika hivyo na wewe unahitaji kubadilika, kubuni na kuja mbinu mpya zitakazoisaidia jamii. Acha ya kale yaitwe ya kale ila sasa panga mambo mapya ya kibunifu.  

    3. KELELE ZA DUNIA

    Tunaishi kwenye dunia yenye kelele nyingi sana. Kuanzia asubuhi utasikia miziki inapigwa kila kona, magari yanapita kwenye maeneo yetu ya kazi, watu wanaongea na kupiga kelele. Yaani ni vurugu mechi.

    Bila ya mtu kuamua kuthubutu kujitenga na dunia kwa muda ili kutulia na kujitafakari basi maisha yataendelea hivi hivi tu. Kutokana na hali  hii basi hapa mtu unahitaji muda wa kupumzika, kujitenga na watu na kufikiri kwa kina juu ya maisha yako, biashara, mahusiano n.k hapa ndipo unaweza kuja na mawazo mapya ya kuendeleza na kuibua ubunifu wako

    4. UOGA

    Hivi watu watanichukuliaje? Hili ni swali lililo kwenye akili za watu walio wengi sana. Hii ni kutokana na ukweli kwamba mtu alikuwa amezoeleka kwa namna ya kawaida kwa watu na yeye tayari amehajijengea picha ya namna hiyo kama vile ni kweli. Ingawa sio. Huu uoga huu sio wa kuendekeza hata kidogo. Vijana wa Tanzania na Afrika, umefika wakati wa kuchukua hatua kubwa sana na kuhakikisha kwamba tunaibua ubunifu ulio ndani yetu.

    5. UKOSEFU WA VIPAUMBELE

    Watu wengi huwa hawana utaratibu wa kupangilia kazi wanapoamka asubuhi.  Hivyo kujikuta wanafanya kazi kwa mazoea. Kufanya kazi kwa mazoea hakuwezi kuleta ubunifu kazini. Hivyo wewe kama mbunifu unahitaji kutenga muda kidogo wa kuhakikisha unafanya kitu kwa kukiboresha zaidi na zaidi.

    Usijifanye umebanwa kiasi kwamba huwezi kuangalia ni kitu gani bora zaidi unaweza kufanya ili kuboresha biashara au kitu chochoe unachofanya.

    Na hili litawezekana kama utapangilia ratiba yako kila siku unapoamka.

    Haya ndio mambo matano yanayoua ubunifu katika bara letu la Afrika na haswa Tanzania yetu. Ukiyaepuka haya rafiki yangu nina hakika utakuwa mbunifu mzuri kwenye eneo lako la kazi, biashara, michezo kutaja ila vichache.

    Hatua tatu za ubunifu

    Ubunifu hupitia katika hatua mbalimbali mpaka kitu kinapokuja kuonekana. Sio tu suala la kulala na kuamka ukisema mimi ni mbunifu.

    Ukizipitia hatua hizi utakuwa mbunifu mzuri sana katika dujinia hii.

    1. Hatua ya kwanza ni kutambua. Hii inaweza kuwa ni

    • Kujitambua wewe mwenyewe. Wewe ni nani? Kitu gani ambacho unaweza kukibuni? Ujuzi gani ulio nao unaweza kukuogezea ubunifu ukawa bora zaidi!
    • Kutambua kile unachohitaji, (je unahitaji kubuni nini? Mwonekano wake ukoje? Je,mwonekano unaweza kubadilika baadae? Kitu gani kinakusukuma wewe kusema hivyo?

    2. KUKIFANYIA KAZI. (ACTION)
    Ukishatambua wewe ni nani?
    Kitu gani unahitaji ili kuwa bora zaidi. Sasa hatua inayofuata ni kufanyia kazi kile kilicho ndani yako. Kuhakikisha kwamba unakiboresha. Hapa utahitaji kutumia nguvu na muda wako kubadili kile kilicho akilini mwako. Kama akilini mwako kuna mawazo hakikisha kwamba unayafanyia kazi.Yaweke katika matendo.

    Soma Zaidi; Vitu Utakavyojifunza Kwenye Kurasa Za Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni

    3.Matokeo

    Angalia kile kinachofanya kazi na kile ambacho hakifanyi kazi.

    kinachofanya kazi endelea nacho. Kisichofanya kazi achana nacho.

    Tukutane siku nyingine kwenye makala ya kuelimisha na kuhanasisha kama hii.

  • Vitu vitano ambavyo hupaswi kuvipoteza kwenye safari yako ya mafanikio

    Siku ya leo nataka nikwamie vitu viwili vikubwa sana ambavyo hupaswi kupoteza kwenye safari yako ya kufikia ndoto zako.

    Kwanza usipoteze ndoto yako kubwa

    Hiki ni kitu muhimu sana. ukipoteza ndoto zako maana yake unapoteza ile motisha na ile nguvu ya kukusukuma wewe kuweza kufanya kitu cha tofauti. Mara zote na sehemu zote hakikisha kwamba haupotezi ndoto yako kubwa uliyonayo.

    Ndoto kubwa ndiyo inakupa motisha na nguvu ya kusongambele mara zote.

    Pili haupaswi kupoteza kitu ambacho umetafuta kwa hela yako

    Kama kuna kitu umekinunua kwa hela yako, hela ambayo umeitafuta kwa nguvu zako zote, usikubali kitu hiki ukipoteze kirahisi. Kitunze vizuri kwelikweli.

    Tatu, usikubali kupoteza uaminifu ambao watu wanao juu yako

    Kama kuna watu wanakuamini, usikubali kupoteza uaminifu huo kwa vizutu vya kijinga.

    Nne, usikubali kupoteza mahusiano yako

    Mahusiano yako ni muhimu kwa ajili ya mafanikio yako. Hakikisha unayapa kipaumbele mahusiano yako

    Tano, usikubali kupoteza afya yako.

    Afya yako ni muhimu sana kwako. hakuna hata mtu mmoja ambaye huwa anaweza kufanikiwa kwa viwango vikubwa bila ya afya. Ukifanikiwa huku ukiwa unaumwa, hutaweza kufurahia mafanikio hayo makubwa uliyokutana nayo.

    /

  • NGUVU YA KUFANYA MAZOEZI

    Ukitoa jasho jingi wakati wa mazoezi, utavuja damu kidogo wakati wa vita

    Siku moja rafiki yake Kobe Bryant alimtembela Kobe,  sasa wakati wanaongea wakawa wamekubaliana kuwa kesho yake alfajiri yule rafiki yake Kobe ambaye pia alikuwa kocha angekuja kushirikiana na Kobe kwenye kumsaidia kufanya mazoezi. Wakawa wamekubaliana muda wa kukutana ambao ulikuwa ni saa kumi alfajiri sana. Kisha wakaagana, wakati wanaagana yule rafiki yake Kobe Bryant alimwacha Kobe anafanya mazoezi.

    Rafiki yake Kobe Bryant alikuwa na uhakika kuwa Kobe hawezi kuamka na kuwahi kesho muda huo waliokubalilana, hivyo hata kesho yake alivyokuwa akielekea uwanjani alikuwa na uhakika kabisa kuwa Kobe hawezi kuwa amefika uwanjani, ila cha kushangaza ni kuwa alikuta kobe tayari ameshafika uwanjani akiwa anafanya mazoezi. Lakini kilichomshangaza zaidi ni kuwa Kobe Bryant alionekana kama mtu ambaye alikuwa akifanya mazoezi kwa muda mrefu kabla yake. Kadiri rafiki yake huyo alivyofuatilia alikuja kugundua kitu kimoja kikubwa sana, aligundua kuwa kobe Bryant alikuwa ni mmoja wa watu ambao walikuwa wanathamini sana mazoezi na hivyo alikuwa anaweka nguvu kubwa sana kwenye kufanya mazoezi.

    Moja ya kitu ambacho watu wengi huwa wanachukulia poa sana ila nimekuja kugundua kuwa watu ambao wanafanya vizuri karibia kwenye kila sekta wanakitumia ni kufanya mazoezi ya kutosha nyuma ya pazia. Hiki ni kitu cha kushangaza sana, ila ni kitu ambacho kinafanya kazi na ni kitu ambacho wewe mwenyewe unahitaji kuhakikisha kwamba unakifanyia kazi kwenye maisha yako.

    Lakers at Wizards 12/3/14

    Kobe Byrant

    Mazoezi yanakujenga

    Sina shaka umewahi kusikia usemi kwamba practice makes perfect. Yaani, kwamba mazoezi ndiyo yanakuimarisha na kukufanya kuwa bora zaidi. kuna siku nilikuwa nasoma kitabu cha Steve Jobs, kinaitwa Presentation Secrets of Steve Jobs.

    Ujue Steve Jobs ni miongoni mwa watu ambao walikuwa akitoa hotuba za kipekee sana kwenye maisha yake. Hotuba zake zilikuwa zikivutia watu kiasi kwamba watu walikufunga safari kutoka mbali na tena wengine walikuwa wakilipia miezi mingi kabla ya siku yake ya kutoa hotuba ili tu wapate viti vya mbele siku anapotoa hotuba.

    Hata leo hii ukifuatilia hotuba zake mtandaoni, utagundua kuwa ni miongoni mwa hotuba chache ambazo zimeangaliwa mara nyingi zaidi kuliko waneni wengine. Sasa nini siri iliyo nyuma ya hotuba hizi? Siri kubwa sana iliyo nyuma ya hotuba hizi ni kuwa, Steve Jobs alikuwa akifanya mazoezi na kujiandaa kwa siku nyingi kabla ya siku yenyewe ya tukio. Unaambiwa alikuwa akijiandaa kwa siku `100 kabla ya siku yenyewe ya hotuba.

    Mtu akikukwambia siku 100 za maandalizi kabla ya siku ya hotuba unaweza kuchukulia poa, ila ukweli ndio huo. Mazoezi ni moja ya kitu muhimu zaidi kwenye kitu chochote kile unacahofanya.niambie kitu chochote kile unachotaka kufanya, nami nitakwambia kwamba fanya mazoezi.

    • Unataka kufaulu mitihani, basi fanya mazoezi mengi kabla ya siku za mitihani.
    • Unataka kujifunza lugha ya kigeni kama kiingereza, kifaransa, kichina au kiarabu, basi fanya mazoezi ya kutosha.
    • Unataka kunoa kipaji chako na kukifanya kiwe bora zaidi, fanya mazoezi.
    • Unataka kuandika maandiko mazuri kama mimi, basi fanya mazoezi.

    Kwa kitu chochote kile unachotaka kufanya na kukifanikisha kwa viwango vikubwa basi fanya mazoezi.

    Kijana mmoja siku moja alisikia stori ya Michael Jackson, ujue michae Jackson ni mmoja wa wasanii ambao wameacha alama kubwa mpaka leo na mpaka leo hii bado anakumbukwa sana kwa miziki yake na jinsi ambavyo alikuwa akitikisha dunia kwa miondoko yake kwenye muziki.

    Sasa kijana huyu aliambiwa kuwa Michael Jacksoni alikuwa akifanya mazoezi kwa saa zaidi ya 8 kila siku, alishangaa sana. Tena alianza kubisha kwa kusema kwamba Michael Jackson alikuwa mchezaji (dancer) kwa asili hivyo hakuhitaji kufanya mazoezi. Ila ukweli unabaki kuwa mazoezi ndiyo mama wa kila kitu.

    Watu wengi unaowaona kwamba wana vipaji vya asili kabisa, au vipaji vya kuzaliwa navyo, siyo kwamba walizaliwa wakiwa hivyo, bali ni mazoezi ya kutosha ndiyo yanawafanya waweze kuwa walivyo.

    Unachopaswa kufahamu ni kuwa kuna watu wengi sana ambao wana vipaji ila hawajaweza kufanya vizuri kwa sababu tu hivyo vipaji vyao hawakuvifanyia mazoezi. Mazoezi kwenye maisha ndiyo kila kitu.

    Ebu chukulia mfano tu wa kawaida wa mchezaji wa mpira aliye kwenye timu ya taifa ni wazi kuwa kabla ya kucheza kwenye timu ya taifa anakuwa tayari ameshachezea timu nyingi sana huku nyuma ya pazia. Na kama ni mazoezi anakuwa ameshafanya mengi na ya kutosha, lakini kadiri anavyokua anakuwa ndivyo anaongeza mazoezi zaidi kwenye kile anachofanya.

    Ndiyo maana utasikia kuwa timu ya taifa imeweka kambi eneo fulani, lengo lake likiwa kwamba wachezaji wake waweze kufanya mazoezi.

    Wachezaji kama akina Ronaldo au Messi, mbali na umaarufu wao wote, ila bado leo hii wanaendelea kufanya mazoezi mengi na ya kutosha bila ya kurudi nyuma. Hiki kitu kinatuonesha kuwa kama kuna siri ya pekee ambayo tunahitaji kuikumbatia basi ni kufanya mazoezi.

    Mazoezi yanakujengea kujiamini

    Kadiri unavyofanya mazoezi zaidi, ndivyo unavyoongeza kujiamini kwenye kile ambacho unafanya. hivyo basi kama unataka kujiamini zaidi, ongeza mazoezi ambayo unafanya. Na hili lipo wazi kabisa, kama kuna watu wawili ambao wanapaswa kusimama mbele ya watu na kuongea, mmoja akajiandaa kwa siku nyingi nyuma ya pazia.

    Akafanya mazoezi kwa kujiuliza maswali ambayo watu wanaweza kumuuliza wakati anawasilisha mada yake na hata kuyaandalia majibu, akajipanga atakavyowasilisha pointi moja baada ya nyingine, lakini pia akajipanga mpaka namna atakavyovaa siku ya tukio. Na mwingine akapuuzia kufanya maandalizi na mazoezi, mpaka dakika za mwisho kabla ya kusimama mbele ya watu ndio akaanza kujiandaa. Ni wazi kuwa aliyejiandaa kwa siku nyingi atakuwa anajiamini zaidi kuliko yule ambaye hakujiandaa.

    Mazoezi yanakujegea kujiamini

    Kanuni muhimu kwenye mazoezi

    Kama kuna kitu muhimu sana ambacho unahitaji kukifahamu linapokuja suala zima la mazoezi ni kuwa, usifanye mazoezi unapojisikia kufanya mazoezi. Usifanye mazoezi mara moja kisha kusahau na kuja kufanya mazoezi siku nyingine nyingi za baadaye.

    Mazoezi yanapaswa kuwa sehemu ya maisha yako ya kila siku. Kadiri kitu unavyokuwa ukiyafanyia kazi ndivyo ambavyo unakuwa unazidi kuimarika zaidi na zaidi kwenye hicho kitu. Hivyo, kitu kikubwa na cha msingi ni kuwa usisubri mpaka siku ambapo utaweza kufanya mazoezi kwa mara moja, tu endelea kufanya mazoei kila siku bila ya kurudi nyuma. Yafanye mazoezi kuwa sehemu ya pili ya maisha yako.

    Fanya mazoezi kwa bidii zako zote, ila unapoenda kuonesha kitu ulichofanyia mazoezi kifanye kama vile umezaliwa nacho.

    Tayari tumeona kuwa hakuna mtu ambaye anazaliwa akiwa anajua kila kitu kiasi kwamba hatahitaji kufanya mazoezi. Tayari tumeona kuwa watu wote wanaofanya makubwa kwenye kila sekta wanafanya mazoezi makubwa nyuma ya pazia. Yaani, wanafanya mazoezi mpaka ile dakika ya mwisho.

    Sasa siku siyo nyingi kuna kitabu nilikuwa nasoma, japo sikumbuki vizuri ni kitabu gani na wala sikumbuki jina la mhusika aliyedokezwa kwenye kile kitabu, ila ninachokumbuka kwenye kile kitabu walikuwa wakimwonglea mwigizaji mmoja ambaye alikuwa akifanya vizuri sana.

    Yaani, kuna igizo moja ambalo alikuwa akiliigiza kwenye kila jukwaa, na watu wengi walikuwa wakilipenda. Sasa baada ya igizo hilo kuwa maarufu, mwandishi wa habari alienda kumhoji ili aweze kupata mawili matatu, kutoka kwa mwigizaji yule.

    Hivyo, mwandishi alienda nyuma ya pazia (eneo ambapo waigizaji wanakaa kabla ya kuingia jukwaani kuigiza). Kilichomshangaza mwandishi wa habari ni kuwa alikuta mwigizaji yule akiwa bado anafanya mazoezi kwenye zile dakika za mwisho kabla ya kuonekana kwenye jukwaa. Hivyo, mwandshi wa habari alipaswa kusubiri kwa muda mrefu kabla ya kuonana na mwigizaji, pale mwigizaji alipomaliza kufanya mazoezi, akiwa anaelekea jukwaani, ndipo mwandishi wa habari alipata kumuuliza swali. Inakuwaje unafanya mazoezi wakati umekuwa ukiigiza igizo hilohilo kila mara?

    Yule mwigizaji alisema, kwa sababu mazoezi ndiyo yananifanya kuwa imara zaidi na yananifanya nijiamini ninapoenda kuigiza.

    Rafiki yangu,  unaona ee, mazoezi yana nguvu kubwa sana.

    Kama kuna vitu vitatu ambavyo ninaweza kukwambia uvipe kipaumbele kwenye maisha yako, kipaji chako, biashara yako n.k. basi vitu hivyo vitakuwa kama ifuatavyo,

    • Kwanza yatakuwa ni mazoezi
    • Pili ni mazoezi na
    • Tatu ni mazoezi

    Naam, nne ni mazoezi tena. Usipuuze mazoezi maana mazoezi yana nguvu kubwa sana, hivyo usiyachukulia poa hata kidogo.

    Kitu kimoja nilichokuja kujifunza kuhusiana na mazoezi ni kuwa unapaswa kufanya mazoezi ya kutosha nyuma ya pazia, ila unapoenda mbele ya watu wasilisha kama vile ulizaliwa hivyo. Wasilisha kama vile huwa hufanyi mazoezi.

    Kufanya mazoezi ni mama wa kujifunza

    Wakati nasoma O-level kuna mwalimu  mmoja ambaye alikuwa akipenda sana kutwambia usemi wa kilatini. Usemi huu unasema hivi, repetitio est mater studiorum. Ukimaanisha kuwa mazoezi ndiyo mama wa kujifunza au kusoma. Kadiri unavyofanya mazoezi zaidi, ndivyo unaimarika na kuwa bora zaidi, na kadiri unavyopuuzia mazoezi ndiyo unazidi kudorora.

    Kiwango kimeshuka

    Sina shaka umewahi kusikia watu wakisema kwamba mtu fulani kiwango chake kimeshuka siku hizi. Na hasa kwa wachezaji. Wengi huwa unakuta kwamba kiwango chao kinashuka kwa sababu tu kupunguza kufanya mazoezi au kutofanya mazoezi kabisa.

    Mwingine huwa unakuta kwamba anapokuwa chini anakuwa anajituma sana anafanya mazoezi, ila kadiri anavyokuwa anazidi kukua na kufikia viwango vya juu, basi analewa ule umaarufu na fedha kitu ambacho kinamfanya aache kufanya mazoezi na mwisho wa siku anajikuta ameshuka kiwango.rafiki yangu, usikubali kiwango chako kishuke kwa sababu ya kutofanya mazoezi. Kumbuka mazoezi ndiyo mama wa ujuzi wowote unaotaka kujenga.

    Upo tayari kujiandaa kwa miaka minne?

    Mashindano ya olympiki ni miongoni mwa mashindano yenye nguvu sana. Yanapendwa na watu lakini pia washiriki wake huwa wanajiandaa kwa kipindi kirefu kabla ya mashindano yenyewe. Washiriki wa mashindano hayo wanajiandaa kila siku kwa kipindi cha miaka minne kwa ajili ya shindano ambalo linadumu kwa dakika kadhaa kisha kupotea. Na ndani ya dakika hizo ndipo mshindi huwa anapatikana na kupewa zawadi nono.

    Sasa swali langu kwako siku ya leo ni kwamba je, na wewe upo tayari kuweka kazi na juhudi kwa kipindi cha miaka minne, mitano sita mpaka kumi mfululizo kabla ya kupata matokeo na kula vinono ambavyo ungependa kupata? Unapaswa kuwa tayari kufanya hivi kwa sababu mafanikio makubwa huwezi kuyapata kwa usiku mmoja tu. Mafanikio makubwa ni matokeo ya vitu vidogo vidogo ambavyo unafanya kila siku vikiunganishwa kwa pamoja. Usiidharau siku moja na kukaa ukisubiri ufike mwisho wa mwaka ambapo utapata mafanikio makubwa, badala yake fanya kitu leo. Ukiunganisha hivi vitu vidogo vidogo, mwishoni mwa mwaka utakuwa umeweza kufanya makubwa.

    Siku moja Piccasso alikuwa akitembea mjini, alikutana na mama mmoja ambaye alimwomba amchoree picha. Kwa harakaharaka yule mama alichukua penseli na karatasi , kisha akampa Picasso. Picasso alichora hiyo picha ndani ya sekunde 30, ikawa imekamilika. Ilikuwa inapendeza sana. Sasa baada ya kuwa amemaliza kuchora hiyo picha, Picasso alimwambia yule mama kuwa hii picha ina thamani ya dola milioni moja.

    Yule mama alishindwa kujizuia na kumwuliza, unafanyaje kuchora picha ndani ya sekunde 30 yenye thamani ya milioni. Na mimi ningependa kujifunza huu ujuzi ili niwe nalipwa milioni ndani ya sekunde thelathini.

    Huku akiwa na tabasamu usoni, Picasso alijibu kwa kusema kuwa, imemchukua miaka thelathini ya mazoezi kuweza kuchora picha ndani ya sekunde 30 yenye thamani zaidi ya dola milioni moja.

    Lada hapa swali langu kwako ni kuwa je, upo tayari kuweka muda wa kutosha kufanya mazoezi ili uweze kubobea kwenye ujuzi na kile ambacho umeamua kufanyia kazi?

    Pablo Picasso katika ubora wake

    Hivi Ndivyo Mazoezi Yanaweza Kukufanya Ule Meza Moja Na Mfalme

    Katika mazingira yetu ya sasa hivi wafalme sio watu waliozoeleka sana kulinganisha na kipindi cha nyuma. Zamani kidogo ulikuwa unakuta kabila au nchi fulani ina mfalme wake ambaye watu wote wanamsikikiza na sauti yake iko juu kwenye masuala ya utawala.

    Lakini pia mfalme kama kiongozi alikuwa anapata vitu vyote vizuri. Yaani kwake nguo zilikuwa ni nguo bora sana kuliko mtu mwingine, chakula chake kilikuwa ni chakula bora sana, malazi yake yalikuwa ni ya kipekee sana. Sio hivyo tu hadi usafiri wake ulikuwa ni wa kipekee, ardhi ya mfalme ilikuwa ni ardhi yenye rutuba kweli kweli. Kwa mazingira ya sasa hivi mfalme ndio raisi wa nchi.

    Lakini kwa mantiki ya andiko hili mfalme sio rais tu. Naomba nitoe maana ya mfalme kulingana na ujumbe wa leo. Mfalme ni mtu ambaye amefikia mafanikio makubwa iwe ni kiuchumi, kiuongozi, kiroho, kimahusiano, n.k

    Mtu ambaye wewe ungependa kukutana naye au pengine umekuwa na shauku ya kukutana naye kwa siku nyingi sana ila hutapata nafasi hiyo kutokana na utofauti uliopo kati yako na yeye kimafanikio.

    Hawa ni watu ambao stori za kitaani huwa tunaishia kusema walikuwa na bahati. Pengine huwa tunasema walibahatika kurithi mali za mjomba, baba, shangazi au ndugu fulani. Au ni wale watu ambao wengine wanasema alikutana na jini likampenda basi likampa utajiri. Hahaha.
    Na pengine wapuuzi wengine wanasema amejiunga freemason.

    Je, kuna watu ambao umewahi kusema maneno kama haya juu yao. Je, kuna watu wa namna hii ambao ungependa kukutana nao ila hujui utawezaje? Leo hii ninakuja kwako na namna rahisi sana ya kukuwezesha kukutana na watu hawa na pia mbinu hizi zitakuwezesha kuwa mmoja wao.

    Moja anza kwa kujiuliza una nini? Ni kitu gani ambacho unaweza kuanza nacho kikakusogeza mbele. Je, una kisomo fulani? Au una kipaji fulani? Au utaalamu fulani?

    Ukishajua kile ulichonacho kinachofuata ni wewe kuamua kuwa gwiji kwenye hicho kitu. Usihangaike na mengine. Ebu tuchukulie mfano umejikuta wewe una ujuzi na kisomo cha sheria. Basi unaamua kukomaa hadi kuwa gwiji wa sheria. Mpaka kieleweke. Hakikisha kama katika nchi hii wanatafuta wanasheria watatu mabingwa basi na wewe unakuwepo. Suala hili halitakuchukua mwaka mmoja au miwili. Ni suala la muda mrefu. Kuanzia miaka saba mpaka kumi na tano!!!!!!!!!

    Lakini ukiweza kutoboa hapa. Jua utakula meza moja na wafalme. Kwanza utakuwa mtu ambaye anafutwa sana jambo ambalo litapelekea wewe kulipwa sana. Jambo ambalo litapelekea wewe kupata vizuri sana ambavyo ulikuwa unatamani (gari, nyumba, n.k)

    Jambo hili halitawasili kwako kirahisi rahisi kama unavyofikiri, litahitaji kuwekeza katika kusoma. Litahitaji pia uwekeze katika kufanya mazoezi ya kitu hicho.

    Ebu tuchukulie mfano wetu hapo juu. Umejikuta una kisomo cha sheria, basi utapaswa kufanya mazoezi ya masuala ya sheria kila iitwayo leo. Utahitaji kusoma sana vitabu vya sheria kuliko mtu mwingine aliyekuzunguka. Kumbuka, ukitoa jasho jingi sana wakati wa mazoezi, utatoa damu kidogo wakati wa vita.

    Huwezi kuwa komando kwa mazoezi ya mgambo

    Wakati naelekea kumalizia andiko langu, ningependa kusistiza kitu kimoja. Kwa vile nimesema unapaswa kufanya mazoezi, usiishie tu kujionesha kuwa na wewe unaweza kufanya mazoezi, kama utaamua kweli kufanya mazoezi basi unapaswa kuwa tayari kufanya mazoezi kwelikweli kulingana na kitu chako. Ufanye mazoezi kulingana na kule unapotaka kufika. Ni wazi kuwa huwezi kuwa komando kwa kufanya mazoezi ya mgambo. Huwezi kuwa mwana

    Sasa kabla sijamalizia kuna vitu muhimu hapa ambavyo ningependa kusisitiza kuhusu kufanya mazoezi.

    • Mazoezi yanaweza kukusaidia kufanya yasiyowezekana yakawa yanayowezekana.
    • Ukifanya mazoezi ya kutosha wakati wa amani, utatoka damu kidogo wakati wa vita.
    • Mazoezi yanakufanya kuwa imara zaidi.
    • Mazoezi yanaweza kukufanya ufikie kitu chochote kile unachotaka.
    • Mazoezi yanaweza kumfanya kilaza kuwa gwiji, yanaweza kumfanya mchezaji wa kawaida kuwa mchezaji wa kimataifa, mwimbaji wa kawaida kuwa  mwimbaji mwenye jina kubwa,  na yanaweza kufanya maajabu kwako pia. Na hapa huhitaji konekisheni, wala kipaji bali unahitaji mazoezi.
    • Kujifunza peke yake bila mazoezi hakuna maana Ebu fikiria ukae ujifunze kuhusu mbinu zoote za kushona suti, bila kuzifanyia kazi. Au ujifunze kuhusu kucheza kucheza kinanda bila ya kufanyia mazoezi haya maarifa uliyojifunza. Ni wazi kuwa kwa vyovyote vile huwezi kubobea, hivyo raha ya maarifa na kila kitu unachojifunza ni kukifanyia mazoezi.
    • Unapofanya mazoezi ni sawa na mtu ambaye anakuwa anafanya uwekezaji. Muunganiko wa mazoezi yale unayokuwa unafanya mara kwa mara baada ya muda unaleta matokeo makubwa.

    Katika andiko linalofuata tutaona dhana ya saa elfu kumi kwa undani zaidi na jinsi ambavyo unaweza kuitumia hii dhana kwa manufaa makubwa kwako.

X