Home


  • Unapaswa kuwa na vyanzo vingi vya kipato, la sivyo utakuwa na vyanzo vingi vya mahangaiko

    Rafiki yangu mpendwa Salaam

    Sina shaka unaendela vizuri kabisa

    Siku ya leo nataka kukwambia kwamba unapaswa kuwa na vyanzo vingi vya kipato la sivyo utakuwa na vyanzo vingi vya mahangaiko. Hata hivyo, kabla hujaishia hapa na kwenda kukimbizana kuanzisha vyanzo vingi vya kipato. Ningependa tu uwe na subira, nasema uwe na subira kwanza ili usome makala hii mpaka mwisho ndiyo uende kufanyia kazi kile utakachojifunza.

    Kuwa na maarifa nusu ni hatari sana. Hivyo kusoma makala nusunusu ni hatari na kunaweza kusiwe na manufaa kwako kama kuisoma makala yote kamil.

    Namaanisha nini ninaposema vyanzo vingi vya kipato

    Vyanzo/chanzo kwa umoja ni chimbuko la kitu fulani. Vyanzo vya kipato ni chimbuko la fedha ambazo unakuwa unapata. Hivyo ninaposema kwamba uwe na vyanzo vingi vya kipato, maana yake uwe na machimbuko mengi yanayokuingizia kipato kwenye akaunti yako ya benki.

    Chanzo maarufu ambacho kimezoeleka kwa watu wengi, ni chanzo cha mshahara. Hata hivyo, kwenye ulimwengu wa leo, kuwa na vyanzo vingi siyo tena ombi. Ni lazima

    Na ukweli ni kwamba siyo vigumu kiviiile kutengeneza vyanzo vingi vya kipato kwenye ulimwengu wa leo. Lakini pia siyo rahisi kama unavyoweza kufikiria.

    Changamoto iliyopo unapokuwa na chanzo kimoja cha kipato

    Unapokuwa na chanzo kimoja cha kipato ni kwamba chanzo hicho kinaweza kukwama kipindi fulani na hivyo kukufanya usiweze kuingiza pesa kama ambavyo unakuwa unataka. Au pale chanzo hicho kinapochelewa kuingiza kipato na kama ulivyokuwa unategemea basi moja kwa moja unakuwa unaenda kugonga mwamba.

    Jinsi ya kuondokana na changamoto ya chanzo kimoja cha kipato

    KWENYE biashara na kwenye maisha, hakuna namba mbaya kama sifuri na moja. kitu chochote kile unachozidisha na mojakinabaki kuwa vilevile. Wakati ukizidisha kitu chochote na sifuri kinabaki kuwa sifuri.

    Hivyo rafiki yangu, ninachotaka kukwambia hapa ni kwamba unapaswa kuepuka kitu hiki kwenye maisha yako rafiki yangu. Epuka kuwa na chanzo kimoja cha kipato kadiri uwezavyo. Usiwe mtu ambaye unasema kwamba hauna kitu cha kufanya (Yaani 0) na wala usiwe mtu ambaye unategemea chanzo kimoja cha kipato. Badala yake kuwa na vyanzo vingi vya kipato. Yaani, walau kuwa na vyanzo vinne au vitano na zaidi vya kipato.

    Usipokuwa na vyanzo zaidi ya kimoja cha kipato, ni suala la muda tu utaanza kuwa na vyanzo vingi vya mahangaiko. Unajua kwa nini? kwa sababu utaanza kujiingiza kwenye kukopa,  utaanza kujiingiza kwenye vikoba, utaanza kufanya vitu vingi ambavyo siyo sawa na mwisho wa siku utakuta kwamba umeanza kuwa na vyanzo vingi vya mahangaiko.

    Suluhisho la hili rafiki yangu ni kuhakikisha kwamba unakuwa na vyanzo vingi vya kipato. Vyanzo vingi vya kipato vitakusaidia wewe kujiondoa kwenye majanga kama hayo ya mikopo lakini pia kukupa kipato pale unapokuwa unakihitaji.

    Kuhakikisha kwamba unapata mwongozo wa kukutosha kwenye kutengeneza vyanzo vingi vya kipato. Nimeandaa ebook. Ebook yenyewe hii hapa

    Kwenye ebook hii unaenda kujifunza yafuatayo.

  • NGUVU YA KUCHUKUA HATUA YA KWANZA: Na Kwa Nini UnAHITAJI Kumaliza Kile Ulichoanza

    pata kitabu hiki kwa shilingi 20,000 hardcopy na 10,000 softcopy
    pata kitabu hiki kwa shilingi 20,000 hardcopy na 10,000 softcopy

    Rafiki yangu mpendwa, Salaam

    Juzi tumezindua kitabu kipya cha NGUVU YA KUCHUKUA HATUA YA KWANZA. Na kwa nini unapaswa kumaliza kile ulichoanza. Hiki ni moja ya kitabu kizuri sana ambacho unapaswa kuhakikisha kwamba umepata nakala yake mapema.

    Najua, umekuwa unataka kufanya makubwa.

    Lakini changamoto yako kubwa imekuwa aidha ni kuchukua hatua ya kwanza. Au la umekuwa unachukua hatua ya kwanza lakini umekuwa humalizi kile ulichoanza.

    Ukisoma hiki kitabu, siyo tu kwamba utaanza kuchukua hatua ya kwanza. Bali pia utakuwa na uwezo wa kumaliza kila unachoanza.

    Hiki ni kitabu kwa watu ambao wako tayari kuchukua hatua. Lengo la hiki kitabu siyo kwamba usome na uanze kujisifia kwamba umesoma kitabu. Bali ni kitabu cha vitendo zaidi.

    Yaani, ukisome, uchukue hatua na ukamilishe kile ulichodhamiria kufanya.

    Najua umekuwa unapata changamoto kwenye hilo suala. Kinachofuata baada ya hapa ni wewe kulipia hiki kitabu ili uweze kukipata mikononi mwako.

    Gharama ya hiki kitabu (softcopy) ni 10,000/- ila tuna ofa ambayo inaisha kesho jioni.

    Kwa ofa hii unaenda kupata kitabu hiki kwa shilingi elfu saba 7,000/-

    Changamka sasa ili uweze kupata kitabu chako. Leo hii.

    Lipia 7,000 ili upate nakala laini (softcopy) yako sasa hivi. Tuma fedha yako kwa namba ya simu 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Kumbuka, Hii ni nguvu ya kuchukua hatua ya kwanza na kwa nini unapaswa kumaliza kile ulichoanza.

  • Leo siku ya kitabu duniani…..

    Frederick Douglass alizaliwa akiwa mtumwa kwenye mashamba ya huko Maryland nchini Marekani. Akiwa na umri wa mwaka 1 alitenganishwa na mama yake, ambapo hiki kinasemekana kilikuwa ni kitu cha kawaida sana kufanyika miongoni mwa watumwa.

    Hivyo, Frederick Douglass alikuja kukutana mama yake mara nne zaidi kwenye maisha yake kabla mama yake hajaaga Dunia.

    Akiwa kama mtumwa na miaka 8 aliepelekwa Kwa mmiliki wake mpya. Akiwa huko mke wa yule mmiliki wake akawa ameanza kumfundisha kusoma na kuandika. Hata hivyo, kabla masomo ya kusoma na kuandika hayajachanganya, yalisitishwa baada ya mmiliki wake kugundua kuwa mke wake alikuwa anamfundisha Frederick Douglass kusoma na kuandika.

    Yule bwana alisema kwamba kisheria watumwa hawaruhusiwi kufundishwa Wala kuandika. Na isitoshe mtumwa akifundishwa kusoma atakuwa hashikiki. Kitu hiki kiliachavalama kubwa kwenye kichwa Cha Frederick Douglass. Kuanzia hapo akaanza kutafuta kila namna ya kujifunza kusoma maaana alishaona NJIA pekee ya yeye kutoboa kimaisha ilikuwa ni kujua kusoma na kuandika.

    Ilimchukua Frederick Douglass miaka saba mpaka kujua kusoma na kuandika. Akawa ameanza kusoma vitabu, hasa vile vilivyokuwa vinahamasiha kukomesha utumwa

    Baadaye kwenye maisha yake Frederick Douglass alikuja kuwa mtu mkubwa sana. Mshauri mzuri Kwa Marais wawili wa Marekani. Abraham Lincoln na rais Andrew Johnson

    Ebu pata picha mtu ambaye alikuwa mtumwa, hakusoma shule Wala chuo chochote alivyoweza kufikia HATUA ya kufanya makubwa kiasi hicho.

    Nimeamua nianze na stori hii ya Frederick Douglass Leo hasa ukilinganiaha kuwa Leo ni siku ya kitabu duniani.

    Tunaishi kwenye zama zenye vitu vingi sana, ila kitu ambacho Bado hakijapoteza nguvu yake ni kusoma na kujifunza.

    Kusoma siyo tu kwamba kilikuwa muhimu enzi za akina Frederick Douglass, Bali mpaka Leo hii.
    Kwenye kitabu Cha Future shock, mwandishi Alvin Toffler

    Anasema mjinga wa Karne ya 21 siyo yule ambaye hajui kusoma na kuandika. Bali mjinga wa Karne ya 21 ni yule anayejua kusoma na kuandika ila hasomi wala kuandika….

    Sasa basi Leo ikiwa ni siku ya kitabu duniani. Nipende kukusisitza sana juu ya umuhimu wa kusoma vitabu, kama ambavyo nimewahi kuandika na kusisitiza juu ya umuhimu huu kwenye kitabu changu Cha MAAJABU YA KUSOMA VITABU

    Hiki ni kitabu hiki Huwa nakitoa Bure kama zawadi Kwa watu wangu wa nguvu kama wewe. Kama hujawahi kusoma kitabu hiki, Sasa huu ndiyo muda wako wa kukisoma.
    Kipate hapa.
    Au unaweza Kusikiliza kilichosomwa Kwa sauti hapa.👇🏿👇🏿

    Aidha Kwa upande mwingine siku ya Kimataifa ya kusoma vitabu au International Book Day inaadhimishwa kila mwaka tarehe 23 Aprili. Lengo la sikukuu hii ni kusherehekea vitabu na kusisitiza umuhimu wa usomaji, kukuza utamaduni wa kusoma na kuboresha uelewa wa kijamii kwa ujumla.

    Siku hii ilitangazwa na Shirika la Umoja wa Mataifa kwa Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) mnamo mwaka 1995, na tarehe ya maadhimisho 23 Aprili ikichaguliwa kuwa heshima ya waandishi wawili maarufu William Shakespeare na Miguel de Cervantes, ambao walifariki siku hiyo hiyo mwaka 1616.

    Siku ya Kimataifa ya Vitabu inaadhimishwa kwa njia mbalimbali duniani kote, ikiwa ni pamoja na matamasha ya vitabu, hafla za kusoma, mihadhara, na shughuli za kupata vitabu vya bure au vitabu kupunguzwa bei. Siku hii pia hutumika kutoa hamasa kwa watu wote, hususan vijana, kuanza kusoma vitabu na kuendeleza utamaduni wa kusoma kama sehemu muhimu ya maisha yao ya kila siku.

    Rafiki yangu nataka uitumie vizuri siku ya Leo.
    Na Kwa kuwa ni siku ya kusoma vitabu duniani. Leo utapata ebooks zangu zote kwa sh 7,000/- tu badala ya 10,000/-

    Audiobooks utazipata Kwa 5,000/- badala ya 10,000/-

    Changamka Sasa upate ofa hii. Hii ni ofa ya Leo. Na ni ofa ya Leo tu. Mwisho ni saa nne usiku.

    Cha kufanya, fanya malipo ya kitabu chochote unachopenda kwa Namba ya simu 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA. Kisha niambie ni kitabu kipi umelipia nikutumie.

    Enjoy siku ya kitabu duniani

    Cheers!

    Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • Hiki ni kitu kitakachobadili maisha yako yote kuanzia leo……

    Mwaka Jana kwenye maonesho ya nanenane nikikutana na Dada Mmoja. Huyu dada alikuwa akipanga Kwa miaka mingi kuandika kitabu ila akawa haandiki.

    Sasa Leo hii alikuwa na swali Moja tu kwangu

    “Godius”, alisema. “Hivi Nina shida Gani? Kwa nini kila mwaka napanga kuandika ila sijawahi kuandika? “Nifanyeje ili niweze kuanza kuandika” Aliendelea

    Nilikaa naye na kuongea naye, leo hii tayari ameandika kitabu Cha kwanza kinekamilika. Sasa hivi anamalizia kuandika kitabu Cha pili.

    Kilichomkuta hugu dada kinawakuta watu wengi pia.

    Ebu Kwa mfano pata picha ni mara ngapi umekuwa unataka kuanza mazoezi.
    Ni mara ngapi umepanga kuweka akiba lakini hujafanya hivyo. Au ni mara ngapi umehamasika kujifunza na kusoma kitabu lakini hukufanya hivyo?.

    Hivi unajua hii tabia imekugharimu kiasi gani? Yaani, kutokuchukua kwako HATUA unajua kumekusababishia Nini?.
    Ni wazi kuwa laiti kama ungekuwa umeanzisha biashara yako ungekuwa tayari unafanya kile unachopenda. Au kama ungekuwa umeamua Kwa dhati kuandika basi ungekuwa umeshaandika kitabu chako.

    Ni wazi kuwa ungekuwa umeweza kuweka akiba pia, maana tangu mwaka ule ulipopatavkazi, mpaka Leo hii usingekuwa unahangaika, tayari ungekuwa na akiba yako ya kutosha tu.

    Lakini Leo hii unajionaje?

    Tukirudi kwa dada yetu tukiyeanza naye hapo mwanzo. Alikuja kugundua kuwa kuandika kitabu siyo kitu kigumu sana baada ya kuwa amechukua HATUA kama nilivyokuwa nimewelekeza.

    Unaweza kuangalia picha hii hapa chini kuona anachosema yeye mwenyewe Kwa maneno yake.

    Unajua nilifanyaje mpaka huyu dada akaweza kufanya haya yote.
    Nilimweleza vitu viwkubwa.

    1. Kwanza nilimweleza NGUVU YA KUCHUKUA HATUA KWANZA. Na nikamwonesha kwamba anapaswa kuweka kitabu chake kwenye uhalisia. Kuhakikisha kinakamilika.

    2. Lakini sikuishia hapo, nilimpa pia mwongozo wa kitabu kinachoitwa JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU.

    Hivi ni vitu viwili ambavyo nataka na wewe upate siku ya Leo.

    Chukua HATUA Leo hii upate
    Kitabu Cha NGUVU YA KUCHUKUA HATUA YA KUCHUKUA chenye mwongozo kamili wa kukusaidia wewe kuanzia kufanyia KAZI kitu chochote ambacho umekuwa unatamani kufanya.

    Mtu yeyote ambaye amekuwa anakwama kuchukua HATUA ya kwanza. Anaweza kuchukua HATUA ya kwanza baada ya kusoma hiki kitabu.

    Mtu yeyote ambaye amekuwa akiwaza kuanzisha biashara, ataweza kuanzisha biashara yake bila shida yoyote mara tu baada ya kusoma hiki kitabu.

    Mtu yeyote ambaye amekuwa anakwama kuweka akiba, ataanza kuweka akiba mara baada ya kuwa ameanza kusoma kitabu hiki Cha NGUVU YA KUCHUKUA HATUA YA KWANZA.

    Kama umekuwa unapanga mipango yako ila unashindwa kuifanyia KAZI suluhisho hiki ni kitabu.

    Na sasa upo kwenye nafasi ya kufanya maamuzi yatakayobadili maisha yako. Nafasi ya wewe kuanza kufanyia KAZI vile vitu ambavyo umekuwa ukitamani kufanya au kuendelea na maisha yako ya kawaida.

    Kama utaamua kuendelea na maisha yako ya siku zote maana yake utaendelea kupata matokeo yaleyale ambayo umekuwa unapata mara zote na siku zote….

    *Lakini kama unataka kitu Cha tofauti kitokee kwenye maisha yako. Kama unataka kubadili mwelekeo wa maisha yako, utapaswa kufanya kitu Cha tofauti fanya Uamuzi wa tofauti na chukua HATUA ya kwanza Sasa
    Na HATUA hii ni kulipia ili kupata ebook ya kitabu Cha NGUVU YA KUCHUKUA HATUA YA KWANZA.
    Lipia Sasa hivi ili uweze kupata kitabu chako.

    Gharama ya kitabu ni 10,000/- ila Kwa ofa ya Eid unakipata Kwa 7,000/- tu.

    Aidha, ktabu Cha JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU kinapatikana Kwa 10,000/-

    Ila kama utalipia vitabu vyote viwili Kwa Leo utavipata Kwa 15,000)- tu.

    Sikikiza, chukua HATUA Sasa hivi.
    Lipia kitabu hiki Kwa 0684408755 Jina ni GODIUS RWEYONGEZA.

    Kwa kusoma vitabu hivi nakuhakikishoa kitu kimoja. Zile ndoto zako ambazo umekuwa nazo Kwa siku Sasa. Yaani, Ile ndoto yako ya kuanzisha biashara itatimia.
    Ndoto yako ya kuandika itatimia.
    Ndoto yako ya ndoto ya kuweka akiba na kujenga utajiri itatimia.

    Nakuhakikishia kitu kimoja tu baada ya kusoma kitabu hiki. KUCHUKUA HATUA YA KWANZA NA KUANZA. Na siyo tu kwamba utachukua HATUA ya kwanza. Bali utakuwa na uwezo wa kukamikisha kile ukichoanza bila shida yoyote.

    Kwa kusema hivi basi fanya kitu kimoja. Lipia 7,000/- kitabu Cha NGUVU YA KUCHUKUA HATUA YA KWANZA Leo hii.

    Au lipia 15,000/- upate vitabu viwili. Kitabu Cha NGUVU YA KUCHUKUA HATUA YA KWANZA pamoja na JINSI YA KUWA MWANDISHI MBOBEVU

    Badala ya 20,000/- jumla utalipia 15,000/- tu.

    Malipo yote yafanyike Kwa 0684408755 Jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    Fanya hivyo Sasa hivi.

    Ni Mimi Godius Rweyongeza
    0755848391
    Morogoro-Tz

  • Fanya kazi na kitu unachotaka kufanya kwa ubora

    Katika kazi au kitu chochote kile utakachoamua kufanya. Weka moyo, akili na kila kitu kwenye hicho kitu. Yaano, zama kabisa kwenye kile kitu kiasi kwamba hakuna kitu ambacho kinapaswa kukutoa wewe kwenye reli ya kukamilisha hicho kitu.

    Yaani, kwenye hili nataka upate mfano wa simba. Si unamjua Simba si mnyama mkubwa kuliko wote mbugani. Simba si mnyama mwenye akili sana kuliko wote. SIMBA si mnayama mwenye nguvu sana kuliko wote mbungani.

    Lakini cha kushangaza ni kwamba simba ara zote anaitwa Mfalme wa nyika. Unajua kwa nini anaitwa mfalme wa Nyika.

    Sababu ni moja tu

    Ni kwa sababu huwa anathubutu, na huwa akiamua kufanyia kazi jambo lake huwa harudi nyuma. Hiki ni kitu ambacho kinamtofautisha na wanyama wengine.

    Mpaka kuna usemi unaosema kwamba ni bora kuwa na kundi la kondoo ambalo linaongozwa na simba kuliko kuwa na kundi la simba linaoongozwa na kondoo.

    Kwa nini? Kwa sababu simba akiamua, ameamua. Harudi, na wala harembi mwandiko. Sasa katika mazingira kama hayo, simba akiwa na kondoo ni wazi kuwa kondoo nao watafuata mkondo wake.

    Lakini kondoo akiwa anaongoza kundi hilo, basi ni wazi kuwa akiongopa na akageuza mbio, basi ni wazi kuwa  hata wale simba watakimbia

    Kwenye maisha yako rafiki yangu. Kuwa simba.

  • Tumezindua kitabu kipya! Haya hapa ni mambo ya msingi sana unayopaswa kufahamu kuhusu hiki kitabu

    Rafiki yangu mpendwa, Salaam
    Moja ya kitu ambacho huwa kinanipa furaha kubwa ni pale ambapo huwa naandika kitabu, na kukikamilisha. Ni vigumu sana kueleza kwa UNDANI mchakato wote wa kuandika kitabu kwa ukamilifu. Ila furaha ile unayoipata baada ya kumaliza kuandika kitabu, ni furaha isiyo na kifani! Hivi unaijua furaha isiyo na kifani kweli……Hahaha

    Enewei, leo tarehe 21/4/2021 ni moja ya siku kama hizo.
    Ni siku ambapo nina furaha kubwa kutambulisha kwako kitabu cha NGUVU YA KUCHUKUA HATUA YA KWANZA. NA KWA NINI UNAHITAJI KUMALIZA KILE ULICHOANZA.
    Kitabu hiki kinapatikana katika mfumo wa nakala ngumu na nakala laini. Na utatumiwa popote pale utakapokuwa duniani.

    Labda kwanza tujiulize unaenda kujifunza nini kwenye hiki kitabu na kwanini unapaswa kununua hiki kitabu?
    Kama kichwa cha kitabu kinavyosema. Kwenye hiki kitabu unaenda kujifunza nguvu ya kuchukua hatua ya kwanza. Lakini siyo tu kwamba tutaishia kukuonesha wewe nguvu ya kuchukua hatua ya kwanza, bali tutaona kwa nini haswa unapaswa kumaliza kile unachopanga.

    Watu wengi sana huwa wanakuwa na ndoto kubwa za kuanzisha na kufanyia vitu. Ila kiuhalisia huwa hawafanyii kazi hivyo vitu. Hivyo, mwisho wa siku huwa wanaendelea kuwa na ndoto kubwa ambazo huwa hawazifanyii kazi.

    Unakuta mtu aliyekuwa na ndoto ya kuandika kitabu, ni mwaka wa saba ila hajaandika.
    Unakuta mtu alikuwa anasema kwamba ataanzisha biashara tangu mwaka 2010 mpaka leo hii bado anasema tu kwamba ataanzisha biashara.
    Unakuta mtu alikuwa anasema kwamba atawekeza au atamfungulia mwanae akaunti, tangu amezaliwa mpaka leo hii mtoto anaelekea kuanza shule, akaunti haijafunguliwa.
    Sasa kwenye hiki kitabu tunaenda kuona NGUVU YA KUCHUKUA HATUA YA KWANZA.

    Lakini haitoshi tu kuchukua hatua ya kwanza.

    Kumaliza kile ulichoanza ni jambo la msingi na sekondari kabisa. Hivyo hatuishia tu kuona kwamba unapaswa kuanza kufanyia kazi vitu. Bali unapaswa kumaliza kile ulichoanza. Yaani, ukifanyie kazi mwanzo mpaka mwisho.

    Siyo uanze kuweka akiba leo. Kesho uache
    Siyo uanze kufuga kuku leo, kesho ndiyo tukukute umeanza kulima tikiti, kesho kutwa tukukute umeagiza mzigo china, na siku nyingine tukukute umeanza kuwekeza kwenye cryptocurencies.

    Kumbe kwa mantiki hiyo ni kwamba, unapaswa kuanza. Lakini siyo tu kuanza, bali kabisa kuhakikisha umekamilisha kile ulichoanza.

    hiki kitabu ni mwongozo. Na ni mwongozo unaopaswa kuufuata.
    Kama nakuona vile kitakavyokusaidia kuondokana na lile tatizo lako ambalo limekuwa linakusumbua la kukosa mtaji. ANZA.
    Umekuwa unahofia kuongea mbelea ya watu. ANZA, KUJENGA UWEZO WAKO WA KUONGEA MBELE YA WATU.
    Umekuwa unatata kuweka akiba. ANZA tena leo hii.
    Umekuwa unatamani sana kusoma vitabu. Unasubiri nini. ANZA
    Umekuwa unataka kufanya kitu gani….ANZA.

    Kitabu sasa kipo tayari. Ni juu yako sasa kuchukua hatua ya kwanza ya kupata kitabu hiki.
    Kisha baada ya KUCHUKUA HATUA YA KWANZA. Utapaswa kusoma kitabu hiki na kukimaliza mpaka mwisho. Hapo utakuwa umeanza vizuri kwenye NGUVU YA KUCHUKUA HATUA YA KWANZA.

    Njoo ujipatie nakala yako siku ya leo rafiki yangu
    Nakala ngumu yakitabu ni 20,000/- utaongeza 5,000 ya kutumiwa.
    Na nakala laini ni 10,000/-

    Ila siku ya leo nina ofa.
    Kama utachukua nakala laini softcopy na kulipia siku ya leo. BADALA YA KULIPIA 10,000/- unaenda kupata hiki kitabu kwa 7,000/-

    Hii ni ofa ya IDDI na itadumu kwenye hiki kipindi cha EID tu. Hivyo, itaduu mpaka tarehe 25. Baada ya hapo, hutaweza kupata hiki kitabu kwa hiyo bei.
    Cha kufanya sasa hivi ni kitu kimoja tu. Wasiliana na 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA

    ViTU VYA NYONGEZA UTAKAVYOPATA ENDAPO UTACHUKUA KITABU HIKI LEO HII
    Kwanza, utapata usimamizi wangu wa karibu wa siku 30. Utachagua kitu chochote ambacho umekuwa unatamani kufanya. Halafu utaniambia na nitakufuatilia kwa siku 30 mfululizo kuona mwnendo wako na namna unavyokifanyia kazi.
    Pia, utapewa zawadi ya kitabu cha NGUVU YA KUWEKA MALENGO.
    Njoo upate nguvu ya KUCHUKUA HATUA YA KWANZA. Ili uweze kujifunza NGUVU LIYOLALA kwenye kuchukua hatua ya kwanza.
    Lipia 7,000/ sasa kwa 0684408755 jina ni GODIUS RWEYONGEZA.
    Lipia sasa upate kitabu chako.

    NB: Hardcopy haina ofa kwa sasa hivi.
    Ila softcopy, unaipata kwa 7,000 badala ya 10,000

    Ni mimi rafiki yako
    Godius Rweyongeza
    0755848391
    MOROGORO

  • Fanya kitu hata kama ni kidogo

    Fanya kitu kimoja kila siku ambacho kinakuogopesha. Fanya kitu hata kama ni kidogo. VItu vidogo mwisho wa siku ndyo huwa vinaleta matokeo na mafanikio makubwa sana. Kuna watu wanafikiria kuwa na mtaji mkubwa wa kuanzisha biashara. Kuna watu wanafirikia juu ya kuja kuwa mabilionea.

    Hilo lengo ukiliangalia ni lengo kubwa sana. Lakini  sasa kulifanyia kazi kwenye uhalisia, ni kazi.

    Ndiyo maana unahitaji kulifanyia kazi hata kama ni kidogokidogo . Pata picha kila siku ukifanya jambo moja dogo, tena ukalifanya kwa mwendelezo na bilakuacha, ni wazi kuwa baada ya muda utakuwa umeweza kufanya makubwa.

    Mfano, kama kila siku ukiweka akiba, ni wazi kuwa akiba hii kidogokidogo, baada ya muda itakuwa imeweza kuwa akiba kubwa sana kuliko unavyoweza kufikiria.

  • Omba Utapewa

    MOJA YA ujuzi ambao una-paswa kuwa nao ni ujuzi wa kuomba. Yaani, kuomab kitu unachotaka kutoka kwa watu wenye nacho. Hiki ni kitu ambacho watu waliofanya makubwa huwa wanafanya.

    Wanaofanya makubwa siyo kwamba wanaweza kufanya kila kitu hapa duniani. Hapana, wanaweza kufanya vitu vichache, ila sasa kwa vile vitu ambavyo hawawezi, basi wanaomba wengine waweze kuwapa msaada. Hiki ni kitu ambacho nimeona nikwambie na wewe rafiki yangu. Mara ukiwa na jambo, omba

  • Usifanye Kosa Hili Unapotaka Kufanya Uwekezaji

    Hongera sana Kwa siku hii ya kipekee rafiki yangu.
    Nadhani unajua ni Kwa Namba Gani nimekuwa nakusisitiza kufanya uwekezaji.

    Wakati mwingine unaweza kusikia watu wakiongelea Kuhusu uwekezaji ukaona nguvu hii iliyolala kwenye uwekezaji, basi ukaamua kwamba na wewe utaenda kuwekeza. Lakini sehemu yako ya kukimbilia ikawa ni kupata mkopo.

    Rafiki yangu, ninachotaka kukwambia siku ya Leo ni kuwa usikope Kwa ajili ya kwenda kuwekeza. Iwe ni Kwa ajili ya Kununua hisa, hatifungani au vipande.

    Badala ya wewe kukopa Kwa ajili ya hivi vitu, fanya hivi:
    Anza kuwekeza kidogokidogo
    Hata kama ni kiasi kidogo sana.
    Anza kufanya uwekezaji Sasa.
    Huu uwekezaji utakufaa sana Kwa siku zijazo.

    Unajua Kwa Nini nakwambia usikope Kwa ajili ya kwenda kuwekeza?
    Nakwambia usikope Kwa ajili ya kwenda kuwekeza Kwa sababu mrejesho unaoupata kutoka kwenye uwekezaji wako, unaweza kuwa ni mdogo kuliko hata riba unayopata. Hivyo kitu hiki kikasababisha wewe ushindwe kulipa mkopo wako Kwa kutumia uwekezaji uliofanya. Badala yake ukalazimika kutumia vyanzo vingine kulipa mkopo.

    Hivyo basi, badala ya wewe kukopa. Kuwa tayari kuanza kuwekeza kidogokidogo. Wekeza hata kama siyo kiasi kikubwa. Nakuhakikishoa hiki kiasi baada ya muda kitakuwa kikubwa kuliko unavyofikiri.

    Muda pekee unapaswa kukopa Kwa ajili ya kufanya uwekezaji
    Kama kweli ukalazimika kukopa Kwa ajili ya kuwekeza. Basi muda pekee unapaswa kukopa Kwa ajili ya kufanya uwekezaji ni pale unapokuwa unakopa Kwa ajili ya kuendesha maisha.
    Kama unakopa Hela ya kula. Kitu ambacho haupaswi kuwa unafanya
    Kama unakopa Kwa ajili ya kuendesha maisha yako ya kila siku, basi hakikisha kwamba kwenye kukopa Kwako. Unakopa Kwa ajili ya kufanya uwekezaji pia. Kwenye kile kiasi ulichokopa, toa kiasi kidogo, Kisha kiwekeze.

    Kila la kheri.

  • Kazi Yako Ya Kwanza


    Rafiki yangu mpendwa salaam. Najua kuwa unapambana sana kwenye shughuli zako za kila siku. Hongera sana Kwa hilo.

    Siku ya Leo ningependa kukwambia kitu kimoja kikubwa sana. Kitu hiki ni kuwa kama unataka kufanikiwa kwenye maisha basi fahamu kuwa KAZI yako ya kwanza kabisa ni kuhakikisha haufi.
    Hakikisha unaendelea kuishi.

    Hilo, ukishalifanikisha kinachofuata ni wewe kuendelea kupambania ndoto na malengo yako makubwa. Kama kweli utayapambania Kwa ustadi wa hali ya juu. Ni wazi tu kuwa Kuna siku, lazima tu utafanikiwa.

    Kwa sababu kanuni ya asili ilivyo ni kuwa hakuna juhudi ambazo Huwa zinapotea Bure. Kwa hiyo, hiki unachofanta Sasa hivi na vingine ambavyo umewahi kufanya, vitaunganisha nguvu na kukuletea wewe mfanikio makubwa.

    Hivyo, hakikisha unaendelea kuishi
    Jilinde
    Ilinde afya yako
    Kisha pambania malengo yako

X