-
Hii ndiyo njia rahisi ya wewe kujipoteza
Rafiki yangu, kama kuna njia rahisi ya wewe kujipoteza ni kufanya vitu kama ambavyo kila mtu anafanya. sote tunajua kwamba vitu ambavyo watu wengi huwa wanafanya huwa siyo sahihi. Na njia ya pekee ya wewe kuishi maisha ya kawaida, ni wewe kufanya vitu kama ambavyo kila mtu anafanya.
Hii ni njia ambayo haifanyi kazi, na laiti kama hii njia ingekuwa inafanya kazi maana yake watu wengi wa kawaida wangekuwa matajiri wakubwa sana au la wangekuwa na mafanikio ambayo siyo ya kawaida. Lakini hali siyo hivyo.
Kumbe vitu ambavyo watu wengi wafanya siyo sahihi. Na kitu kufanywa na watu wengi hakikifanyi kuwa sahihi.
EBU KWA MFANO tuchukulie tu maisha ya kawaida ambayo mtu anaishi. Anaambiwa kwamba nenda shule usome kwa bidii, na kweli anaenda shule anasoma kwa bidii, kisha baada ya shule anatafuta kazi. tuchukulie huyu mtu amepata kazi, baada ya hapo anaenda kazini. Akifika kazini, anaambiwa kwa kuwa sasa una mshahara, wewe unaweza kupata mkopo ambao utakufaa.
Anachukua mkopo.
Wakati huohuo, anakuta kwamba kuna sheria ambayo inamtaka kujiunga na mashirika ya MAFAO, hivyo anaanza kuaminishwa kwamba ukiweka hela yako, hutahitaji kushughulika na pesa zako tena. Na wala hutahitaji kujiandaa kwa ajili ya kuja kustaafu, badala yake sisi, tutakufanyia kila kitu.
Anaanza kuishi maisha yake kihivyo, mpaka anafikia miaka ya kustaafu ambapo anakuja kupewa MAFAO yake, hapo ndio anagundua kwamba hayatoshi. Muda huu sasa ndio anaanza kufunguka ili aweze kutafuta ajira na kazi nyingine.
Habari njema ni kwamba unaweza kujiondoa kwenye huu mnyororo wa watu wengi, na kujiweka kwenye mnyororo wa watu uwachache.
Kwenye jamii yoyote ile huwa kuna wachache waliofanikiwa. Na hawa watu ukiwafuatilia, utagundua kitu kimoja kutoka kwao. Kitu hiki ni kufanya vitu kwa namna ya upekee, tofauti na watu wengine
Hawa ndio wale ambao utakuta wanajilipa wenyewe kila baada ya kuwa wamepata kipato chao.
Hawa ndio wale ambao utakuta kwamba wanawekeza na kuchukua kiasi cha fedha na kukifanya kiwafanyie kazi.
Hawa ndio wale ambao utakuta kwamba hawana chanzo kimoja cha kipato. BADALA YAKE wanakuwa na vyanzo kadha wa kadha vya kipato na wanavitumia hivyo vyanzo kuhakikisha kwamba wanafanya makubwa zaidi.
SOMA ZAIDI: Baadhi Ya Vyanzo Vya Kipato Ambavyo Unaweza Kuwa Navyo
Hawa ndio wale ambao huwa hawanunui vitu kuwaridhisha watu wengine. Badala yake huwa wananunua kutokana na uhitaji wao kwa wakati husika.
Rafiki yangu, ninachotaka kukusisitiza siku ya leo ni kwamba wewe unaweza kujiingiza kwenye kundi la watu wachache sana ambao wanafanya makubwa. Na hili linawezekana vizuri sana. Ila utahitaji kuzingatia yafuatayo.

Kwanza, utahitaji kujisukuma kwenye kila kitu unachofanya. Na kuhakikish kwamba hicho kitu unakifanya kwa namna ya utofauti ukilinganisha na watu wengine. Jisukume kwenye kitu chochote unachofanya na hakikisha kwamba kila unachofanya, unakifanya kwa viwanvo vikubwa sana. Naam, unakifanya kwa viwango vikubwa sana kuliko ambavyo umewahi kukifanya.
Kiasi kwamba mtu yeyote atayeona kazi yako, aseme kweli hii kazi imefanywa na mtu fulani.
Soma Zaidi: TABIA ZA WATU WANAOLIPWA SANA
Pili, utahitaji ujiepushe na mambo mengine yote ambayo hayachangii kwenye kufikia ndoto zako. na hapa namaanisha mambo mengine yote. Kama umekuwa unaangalia runinga kila siku. Kuanzia sasa hivi, anza kujiuliza, hivi runinga inasaidiaje kwangu kwenye kufikia ndoto zangu. Ukifuatilia kwa umakini utagundua kwamba, runinga haina manufaa yoyote yale kwako. Hivyo, unaweza kuiweka pembeni ili uweze kufanyia kazi majukumu yale machache ambayo yatakuwa na manufaa kwako.
Kama umekuwa unafuatilia maisha ya watu wengine, jiulize ni kwa namna gani kufuatilia maisha ya watu wengine kumekuwa na manufaa kwangu? Utagundua kwamba kufuatilia maisha ya watu wengine hakuna manufaa yoyote yale kwako. Hivyo, badala ya wewe kuanza kufuatilia maisha ya watu wengine, weka nguvu sasa kwenye kujifuatilia wewe mwenyewe. Weka nguvu kwenye kufuatilia mipango yako na mambo mengine ambayo yanakuhusu wewe mwenyewe.
Usiwe mtu wa kufuatilia maisha ya watu wengine hata kidogo.
Tatu, usiige maisha. Uwepo wa mtandao wa intaneti na mitandao ya kijamii. Uwepo wa runinga na vitu vingine umewafanya vijana wengi waishi maisha ya kuigiza kwa wingi kuliko uhalisia. Wengi watanunua vitu hata kama hawahivitaji. Wanasahau kwamba Warren Buffet anasema sheria kuu mbili unazopaswa kuziangatia ni moja, kutokupoteza fedha. Na mbili ni kutosahau sheria ya kwanza.
Rafiki yangu, kwa leo ningependa niishie hapo. Naamini kuna kitu utakuwa umepata kutoka kwenye hii makala ya leo. Kama wewe umeweza kunufaika hata kwa kupata kitu kimoja tu unachoweza kufanyia kazi. basi kuna wengine wanaweza kunufaika pia. Ebu washirikishe rafiki zako wawili tu hii makala ili na wao waweze kuisoma na kunufaika nayo.
Mwisho kabisa, ningependa nikukaribishe uweze kupata vitabu vyangu. Mimi ninavyo vitabu vizuri ambavyo unaweza kusoma na vikakunufaisha, Orodha yangu ya vitabu vyangu vyote unaweza kuiangalia hapa.
Chagua kimoja, kisha nicheki kwa 0755848391 ili uweze kupata nakala ya kitabu chako.
Bila kuongeza kitu cha ziada. Nikutakie siku njema sana.
-
Kinachokukwamisha wewe ni hiki hapa

Rafiki yangu, umewahi kujiuliza ni kitu gani kinakukwamisha wewe kuweza kufanya makubwa. Kama kuna kitu kinakukwamisha wewe na watu wengine wengi, basi kitu hiki ni kufanya kazi kama vile una muda wote hapa duniani. Yaani, unaanza kufanya jukumu lako bila ya kuwa na lengo wala mwelekeo wowote. Kitu kinachokufanya ufanye jukumu hilo kwa muda mrefu sana kuliko unavyokuwa unatazamia.
Unaweza usijue hili. Kwa sababu kama hauna mpango, utaona uko sahihi kwa kile utakachokuwa unafanya. Ila nikuhakikishie kwamba ukiwa na mpango, rafiki yangu, mambo yako, utayafanya vizuri, kwa kujisukuma na kujituma zaidi.
Ninachotaka ufahamu ni kuwa kama unataka kuutumia muda wako vizuri na kwa manufaa makubwa sana, basi unapaswa kuwa na ukomo kwenye muda wako.
1. kuanzia unapoamka asubuhi, hakikisha kwamba unapangilia siku yako kwa kuweka majukumu yote utakayoyafanya ndani ya hiyo siku. Usikubali kuipitisha siku bila ya wewe kuwa na mpango ambao unaoufanyia kazi ndani ya hiyo siu
2. Muda ambao wewe unautumia kupangilia siku yako au wiki yao, siyo kwamba huo muda unakuwa unaupoteza. Hapana, badala yake huo muda unakuwa unautumia kwa manufaa makubwa. Hivyo, usije kusema kwamba nimepoteza muda kwa kupangilia siku yangu. Badala yake unakuwa umeokoa muda, maana muda ambao hapo baadaye ungekuja kuupoteza utauokoa kwa kufanya majukumu ya maana.
3. Ukishapangilia siku yako, kinachofuata ni wewe kufuata huo mpangilio wako ambao umeuweka kama ulivyo. Kufanya majukumu yako muda ambao unapaswa kuyafanya bila kuacha, kitu hiki kitakufanya uweze kuutumia muda wako kwa manufaa makubwa.
Asante sana, nikutakie siku njema rafiki yangu.
Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshaji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE
Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.
Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap. Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA
-
Jinsi ya kuwa mtu mwenye msaada kwa wengine
Huwa inatokea kwamba mtu anasoma makala yangu ambayo niliandika siku nyingi za nyuma, kisha mtu huyo anasema kwamba hiyo makala imemsaidia sana.
Mfano leo hii wakati naandika makala hii nimeagalia maoni kwenye blogu kwenye makala za nyuma nimeona kwamba, maoni ya jana yaliwekwa kwenye makala ya ambayo mimi niliandika mwaka jana mwezi wa 11.
kwangu hiki siyo kitu cha kushangaza kwa sababu wakati mwingine unaweza kukuta mtu kaweka maoni kwenye makala ambayo niliandika hata miaka mitano iliyopita.
wakati mwingine mimi nakuwa nimeshaandika na kusahau kuwa niliandika hiyo makala.
lakini andikko hilo linakuwa lenye msaada kwa mwingine.KITU HIKI ndicho kinanileta kwenye ujumbe wa leo ambao ningependa kukwambia. NA UJUMBE huu ni kwamba, kamwe usipitishe siku bila ya kufanya kitu ambacho utaona kwamba kinaongeza thamani kwa watu wengine. Kila siku fanya kitu ambacho kitaongeza thamani kwenye maisha ya mtu mwingine. Hiki kitu kinaweza kisisaidie mtu uliyemlenga leoleo. lakini kwa sababu umekifanya, kinaweza kumfikia huyo mtu hata baada ya miaka kadhaa.
sasa swali langu kwako siku ya leo ni kuwa ni kitu gani ambacho unaenda kufanya ambacho kitakuwa chenye msaada kwako na kwa wengine hata kwa siku zijazo.
USIWE mbinafsi kwa kutaka kufanya vitu ambavyo vitakunufaisha wewe tu.
Asante sana na kila kheri -
Epuka hiki Kitu kama unataka kufanya makubwa
/
Rafiki yangu, najua unataka kufanya makubwa kwenye maisha yako. Hongera sana kwa kuwa na ndoto kubwa sana.
Ebu kwwanza, kabla sijakwambia kitu cha kuepuka kama unataka kufanya makubwa. Naomba kwanza uandike malengo yako na ndoto zako hizi kubwa chini. Ziandike kabisa, ili ujue ni kitu gani unataka kufanikisha kwenye maisha yako.Hongera kwa kuweza kufanyia kazi hilo.
Sasa kwa kuwa una malengo na ndoto kubwa hivyo, kuna kitu kimoja ningependa ukifanyia kazi siku ya leo. Na kitu hiki siyo kingine bali ni kuhakikisha kwamba unajituma na unafanya vitu vya tofauti. Huwezi kuendelea kufanya vitu vilevile kila siku huku ukitegemea kupata matokeo ya tofauti.Ni lazima uwe tayari kujisukuma kidogo, ni lazima uwe tayari kufanya mambo ya tofauti, ili uweze kupata matokeo ya tofauti ambayo hujawahi kuyapata.
Hiki ndicho kitu kikubwa sana ambacho ninataka kukwambia siku ya leo rafiki yangu.
Kifanyie kazi hiki, utanishukuru kesho.
Kila la kheri
Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshaji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE
Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.
Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.
Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA

uNGEPENDA KUPATA HIVI VITABU, TWANGA 0755848391 -
Jinsi ya kunufaika na muda wako wa safarini

Kwa namna moja au nyingine KATIKA maisha yetu ya kila siku Kuna kusafiri.
Unaweza kuwa unasafiri umbali mrefu sana kama kutoka mkoa mmoja KWENDA mwingine.Lakini muda mwingine Unaweza kuwa unasafiri eneo fupi tu. Dakika kumi, kumi na tano au SAA moja.
Bila kujali, umbali unakwenda, Bado safari Ni safari na muda huu unapokuwa unatoka eneo moja kwenda jingine Unaweza kuutumia kwa manufaa.
Huu muda wa Kutoka eneo moja kwenda jingine ukiuunganisha kwa siku, kwa wiki na kwa mwaka utajikuta kwamba unapata muda mwingi sana. Brian Tracy anasema kwa mwaka mmoja muda ambao MTU anakuwa safarini ni sawa na mhura mmoja wa chuo.
Kumbe huu muda huu ukiutumia vizuri ni wazi kuwa utajifunza mengi, na pengine hata kitu ambacho umekuwa unatamani kujifunza kwa siku nyingi utakielewa.
Ebu chukulia umekuwa unatamani kujifunza uandishi kwa siku nyingi. Ukaamua tu kuhakikisha unautumia muda ule wa safari kusikiliza vitabu na kozi za uandishi, na Kisha ukawa unatenga dakika chache tu za kuandika kila siku. Ni wazi kuwa baada ya muda utabobea.
Au kama umekuwa unapenda kujifunza mauzo. Unaweza kuutumia muda huu wa ziada kusikiliza mafunzo ya sauti ya mauzo ambayo yatakufanya uweze kubobea kwenye mauzo.
Kumbe basi, wito wangu kwako Ni mmoja TU rafiki yangu, kuanzia Leo hii, hakikisha kwamba unautumia vizuri Sana muda wako wa safari.
Utumie kujifunza na hasa kujifunza kwa kusikiliza mafunzo ya sauti. Yaani, AudiobooksHizi zitakupa maarifa yenye manufaa makubwa.
Rafiki yangu, tunahitaji kuleta mapinduzi kwenye jamii zetu. Na hatuwezi kuleta mapinduzi kwa kuendelea kufanya Mambo Yale Yale ambayo tumekuwa tunafanya kila siku. Badala yake fanya mambo ya TOFAUTI kidogo kabisa. Kama kusikiliza mafunzo ya maana wakati wengine wanapoteza muda huo kwa kuchati, kusikiliza miziki na vinginevyo.
SOMA ZAIDI: Jinsi ya kupata mafunzo yenye hadhi ya chuo
Kila la kheri
Kama ungependa kupata vitabu sauti vya Kiswahili. Basi akuhakikishia kwamba vipi. Tuwasiliane sasa kwa 075584391 ili uweze kuvipata au BONYEZA HAPA
Kisha andika AUDIOBOOKS

-
Unataka kufanya vitu vya tofauti? Siri hii hapa
Watu wanaofanya vitu vya tofauti siyo kwamba ni watu ambao wameshuka kutoka mbinguni. Siyo watu ambao wana vitu vya kipekee kukuzidi wewe. Siyo watu ambao wana elimu kubwa kulliko wewe. Isipokuwa ni kuwa wana sifa moja kubwa ambayo inawatofautisha wao na wewe.
Na sifa hii siyo nyingine, bali ni sifa ya kuamua kufanya jambo na kuhakikisha kwamba wanalifanya bila ya kurudi nyuma.
Hii ni sifa ambayo na wewe unapaswa kuwa nayo pia rafiki yangu.
Kuazia leo hii fahamika kama mtu ambaye akiamua kufanya jambo analifanya kweli.
Na kwa sababu ninataka ufahamike hivyo kuanzia leo hii. Nataka uanze kuchukua hatu akuanzia sasa hivi.
Ebu sasa hivi andika chini jambo ambalo unaamua kufanyia kazi kuanzia leo hii.
Kisha nenda kalifanyie kazi kuanzia leo hii.
Lifanyie kazi kila siku kwa siku zijazo mfululizo bila kuacha.
Jipe walau changamoto ya kufanya hilo jambo kwa siku 100 zijazo bila ya kuacha. Ukiweza kufanya hili jambo kwa siku hizi 100 bila kuacha, ni wazi kuwa utakuwa umeweza kujijengea nidhamu kubwa sana. lakini pia utakuwa umejenga njia nzuri yaw ewe kuweza kulifanya hilo jambo.
Na baada ya hapo utakuwa hauzuiliki wala kurudi nyuma hata kidogo
Chukua hatua leo hii
Kila la kheri
-
Siri itakayokuwezesha wewe kufanya makubwa

Rafiki yangu wa ukweli, sina shaka wiki yako umeianza vizui sana. Hongera sana kwa kazi.
Siku ya leo ningependa tu kukwambia kuwa kama unataka kufanya makubwa kuna vitu muhimu sana ambavyo unapaswa kuzingatia nakuhakikisha kwamba umevifuata. Vitu hivi ni pamoja na na wewe kufanya majukumu makubwa kwanza asubuhi kabla hujafanya kitu kingine.
Kama una majukumu mawili, basi nguvu yako kubwa unapaswa kuilekeza kwenye jukumu ambalo ni kubwa kwa upande wako.. Yaani, lile jukumu ambalo usipolifanya, litakuwa na madhara makubwa aidha ya muda mfupi au ya muda mrefu kwa upande wako. Ni jukumu ambaloendapo likifanyika kwa ukamilifu, litaleta matokeo mazuri. Haya majukmu mengine yanaweza kusubiri lakini hili halipaswi kusubiri.
Mara nyingi watu wengi huwa wanaliogopa na kulikwepa hili jukumu. Kitu ambacho huwa kinawafanya wakimbilie kufanya majukumu madogo madogo ambayo hayana nguvu huku wakiacha majukumu ambayo yana nguvu. Ninachotaka kukwambia siku ya leo ni kwamba, kama uanataka kufanya makubwa. kuwa tayari kufanyia kazi majukumu ambayo muda mwingine yanaonekana ni magumu.
Ni kwa sababu haya majukumu ndiyo ambayo yanaweza kukusogeza wewe kule unapotaka kufika.
Haya majukumu japo yanaogopesha lakini ndiyo ambayo yatachangia kwenye kulipwa kwako kwa asilimia 80, ukilinganisha na majukumu ambayo ni asilimia 20 ambayo siyo ya muhimu sana ambayo unakuwa unafanya.
Kazi yako siku ya leo ni kujua ni kuhakikisha kwamba unayajua majukumu yako ambayo ni ya muhimu sana, kisha kuyafanya hayo kwanza kbla hujafanya majukumu mengine.
Kwenye mambo 10 ambayo unapaswa kufanya leo, siyo yote yana umuhimu na nguvu sawa. Ni baadhi tu, au machache kabisa ambayo yana nguvu kubwa. wekeza kwenye haya machache.
Kila la kheri
-
usipofanyia kazi ndoto zako kuna mtu atakuajiri ili ufanyie kazi ndoto zake

Rafiki yangu, watoto wadogo huwa wanaongoza kwa kuwa na ndoto kubwa sana. Ukiongea na mtoto yeyote yule mdogo atakwambia ndoto zake kubwa, tena kwa kujiamini.
Ongea na MTU mzima sasa. UNAWEZA kutamani kuzaba baadhi ya watu vibao. Watu walewale ambao walikuwa na ndoto kubwa utotoni, kwa sasa hawana tena hizo ndoto kubwa.
Ndoto ileile waliyokuwa nayo utotoni ukiwakumbushia wataanza kukupa sababu kibao kuonesha kwa Nini HAIWEZEKANI kufanyika.
Watakwambia uchumi mgumu.
Watakwambia vyuma vimekaza.
Watakulerea sababu nyingine kibao.Rafiki yangu, wewe ni mmoja wa hao watu?
Ndoto Yako. Naam ndoto Yako Ni kitu muhimu ambacho haupaswi kupoteza. Na ukiona umepoteza ndoto zako, ujue tu lazima Kuna MTU anaenda kukuajiri ili ufanyie kazi ndoto zake.
Unajua kwa nini?
Kwa sababu dunia haipendi kukaa na utupu. Popote pale kunapokuwa na utupu dunia inatafuta sababu ya kuhakikisha pamejaa.
Kama sehemu Haina mazao Basi itakuwa na magugu.
Kama sehemu ubongo hauna mawazo chanya, basi utakuwa na mawazo hasi.Kumbe na wewe usipofanyia kazi ndoto zako, lazima tu kutakuwa na mtu ambaye atakuajiri ili ufanyie kazi ndoto zake. Kama MTU hatakuajiri ufanyie kazi ndoto zake. Basi visingizio vitakumeza, kwenye kufanyia kazi ndoto zake.
Sasa rafiki yangu, kuanzia leo amua kitu kimoja tu. Kufanyia kazi ndoto kwa kufa na kupona. Pambania ndoto zako rafiki yangu hata kwa kuanzia chini Sasa hivi.
Kila la kheri
Sasa kitu kikubwa cha kufanya leo ni wewe kuhakikisha kwamba unaanza kufanyia kazi.
-
Hivi ndivyo unapaswa kugawanya muda wako Kama una ndoto kubwa

Rafiki yangu mpambanaji, bila shaka unaendelea vizuri kabisa. Hongera sana kwa hilo. Siku ya leo ningependa kuongea na wewe machache rafiki yangu mwenye ndoto kubwa.
Ukweli ni kuwa inachukua muda kufikia mafanikio makubwa: unapaswa kuyapambania mafanikio Yako makubwa Kama vile hakuna Kesho. Muda wako wewe mpambanaji unapaswa kuwa umegawanywa sehemu za muhimu tu.
Muda wa kufanyia kazi ndoto zako. Hapa unafanya kila linalowezekana kuhakikisha umezipambania ndoto na malengo Yako kila wakati. Unafanya kazi kwa bidii na haurudi nyuma
Inachukua Muda kufikia ndoto kubwa Ila inawezekana.PILI ni muda wa familia au watu wako wa KARIBU. Huu Ni muda mwingine ambao unapaswa kuwa KARIBU na familia yako au watu wako wa KARIBU.
Ni hivyo tu. Vingine vilivyo nje ya hapo havipaswi kupata muda wako.
Weka muda wako, NGUVU zako na Akili zako kwenye hivyo vitu viwili tu.Nina vitabu viwili vinavyokufaa sana wewe mpambanaji. Kwanza ni JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO
Na pili Ni kitabu Cha mwongozo wa wapambanaji. Hustlers Guide. Hivi vitabu viwili hivi, vina mwongozo na kila kitu unachohitaji kujua kuhusu kufanyia kazi malengo na ndoto zako mpaka vikatimia. Cha kufanya hapa Ni kitu kimoja tu. Wasiliana nami kwa 0755848391 ili uweze kupata Nakala zako mapema.
vitabu vyote viwili Ni 30,000/- kimoja ni hardcocopy (JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO) NA gharama yake Ni 20,000/-
na mwongozo wa wapambanaji ni softcopy. Gharama yake ni 10,000/-. Vipate vyote, utanishukuru baadaye.

Nakutakia kila la kheri.
-
Ufanyeje pale bidii yako inapotumika kama mtaji kwa watu wengine
Siku moja kuna rafiki yangu aliniuliza swali, alitaka kujua kuwa unafanyaje pale ambapo unakuwa na bidii na watu wanajua kuwa una bidii ila wanataka wakutumie.
Leo ningependa kujibu swali hili kwako wewe ambaye unaona kwamba una bidii na watu wanaitumia hovyo. Kwanza ningependa kwa kuanza kusema kwamba unapaswa kuwa na bidii kwenye kazi zako. hakikisha kazi yako yoyote ile unayogusa unaifanya kwa bidii, na siyo tu unaifanya kw abidii, bali unaifanya kwa ubora wa hali ya juu sana.
Kama wewe unaona kwamba lazima bosi wako awepo ili ufanye kazi. HUFAI.
Kama unaona kwamba bosi wako akitoka unapumua kwa nguvu kwa vile ametoke. Jua kwamba hufai.
Kama muda wa kazi unachati, unaongea umbea na unajificha kwenye migongo ya watu wngine. Hufai pia.
Rafiki yangu, wewe unapaswa kuwa mchapakazi wa hali ya juu sana. chapa kazi mara zote na sehemu zote, chapa kazi kwelikweli kiasi kwamba asipo mtu ambaye anapaswa kukuzidi kwenye kuchapa kazi.
Na kwenye hii dunia kuna vitu viwili ambavyo haupaswi kuruhusu mtu yeyote akuzidi kwenye kuvifanya, vitu hivi ni kufanya kazi kwa bidii na kujituma.
Kama kuna watu wanakuzidi kwenye hivyo vitu viwili. Basi funguka sasa hivi.
SASA baada ya kuwa nimesema hayo yote kuhusiana na kuchapa kazi kwa bidii. Inawezekana kuna watu watataka kukutumia wewe kwa manufaa yao zaidi kwa vile wanaona unachapa kazi kw abidii.
Na kama unasema watu wanakutumia, kwa lugha nyingine unamaanisha kwamba unafanya kazi kwa viwango vikubwa ukilinganisha na malipo ambayo unapata. Hivyo, unalipwa kiasi kidogo ukilinganisha na vile anavyopaswa kuwa analipwa.
Laiti ungekuwa unalipwa vizuri usingesema hivyo.
Kwa hiyo, kama unaona kwamba haulipwi kama vile unavyostahili unaweza kufanya yafuatayo.
Kwanza, unaweza kuamua kuacha kazi ili uweze kuweka juhudi zako sehemu nyingine ambayo itakulipa kulingana na kazi yako. Huu ni ukweli ambao pengine hukuutegemea lakini unapaswa kuubeba na kuufanyia kazi bila yakuchelewa.
Pili, kama unaona hiyo ni ngumu, basi unapaswa kuonana na bosi wako na kumwambia kuwa anapaswa kukuongeza malipo ili yaendane na viwango vya kazi unayoweka. Hapa nenda na vielelezo vyote ambavyo utahitaji kuonesha kwa bosi wako ili kuthibitisha hilo
Na tatu na mwisho, ni kwenda kwa bosi mwingine ambaye anaweza kukulipa kiwango unachoona unastahili.
Hayo ndiyo mambo matatu ambayo utahitaji kufanyia kazi rafiki yangu,ili kuhakikisha kwamba u
KITU Kikubwa zaidi ni kwamba haupaswi kuja kuzama kwenye kukazania kulipwa na bosi wako na wakati huohuo thamani na ufanisi wako ukapungua. Muda wote huo, ufanisi wako unapaswa kuwa unaongezeka.
Na hata wachezaji wa mpira huwa wanapandishwa viwango vya malipo kutokana na vile wanavyokuwa wanazidi kuwa bora zaidi kwenye kazi zao. Hivyo, kwa msingi huo basi, unapaswa kuongeza uchapaji wa kazi, ufanisi na ubora wa kazi bila kuacha ili kuendelea kupanda viwango
Kila la kheri
Makala hii imeandikwa na Godius Rweyongeza.
Godius Rweyongeza ni mwandishi wa vitabu zaidi zaidi ya 20. Na ni mwendeshaji wa mtandao wa Songambele. Amekuwa akiandika kwenye huu mtandao huu tangu mwaka 2016. Kitabu chake cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni kimekuwa #1Best Seller kwa muda sasa kwenye mtandao wa GETVALUE
Baadhi ya makala za Godius Rweyongeza zimechapwa kwenye magazeti makubwa nchini Tanzania likiwemo gazeti la MWANANCHI.
Kupata vitabu vya Godius Rweyongeza unaweza kwa kuwasiliana na 0755848391/ +255755848391 kwa simu au whatsap.
Mtandaoni, vitabu vyake unaweza kuvipata kupitia mtandao wa GETVALUE kwa KUBONYEZA HAPA