-
Namba Zetu Za Malipo
Namba za malipo ya vitabu:
Namba za lipa
TIGO PESA: 19016638 Jina ni SONGAMBELE CONSULTANTS
M-PESA: 5564517 jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA
Namba za kawaida
AIRTEL MONEY: 0684408755
TIGO PESA: 0655 848 392
M-PESA: 0745 848 395Kote jina ni GODIUS RWEYONGEZA
NB: Kama namba ya malipo anatumiwa mtu ambaye yuko nje ya nchi. Iandikwe Kwa kuanza na +255
Kwa hiyo namba zinazotumwa nje ya nchi zitakuwa
Airtel money: +255 684 408 755
TIGO PESA: +255 655 848 392
M-PESA: +255 745 848 395KOTE Jina ni GODIUS RWEYONGEZA
Kama malipo yatakuwa yanafanyika kupitia benki.
Yafanyie kupitia
- CRDB BANK: 0150770710200
- NMB BANK: 22110047274
Kote jina ni GODIUS GORDIAN RWEYONGEZA
-
Wasiliana na Godius Rweyongeza Sasa
Habari yafuatayo ni mawasiliano Unayoweza kutumia kumpata GODIUS RWEYONGEZA
Simu: +255 (0) 684408755
Whatsap: +255 (0) 755848391
Email: songambele.smb@gmail.com
Kupata vitabu vyake wasiliana Moja kwa Moja na +255 (0) 684408755 (more…)
-
Hakuna mtu Ambaye Anaenda Kupiga Kazi Kwa Ajili Yako
Ngoja nikwambie kitu, hakuna namna ambavyo wewe unaweza Kuepuka kazi katika suala zima la kufanikiwa. Kama unataka kufanikiwa sharti uwe tayari kuweka kazi itakayokufikisha kule unapotaka kufika.
Usije unategemea kwamba MTU yeyote atafanya kazi kwa ajili yako.
Nakumbuka siku za nyuma niliwahi kuandika Makala hapa nikasema kwamba hakuna MTU ambaye anaweza kupiga Push-Up kwa ajili yako.
Hii ndio kusema kwamba, Kama unataka afya njema, fanya vitu vitakavyokupa afya njema. Hakuna mtu anaweza kufanya hivyo vitu kwa ajili yako.
Kama unataka kufikia utajiri wa kifedha, sharti ukubali kufanya vitu vitakavyokufikusha kwenye mafanikio ya kifedha. Hakuna mtu atakusaidia wewe kufikia huko.Sasa kazi ni kwako rafiki yangu. Ebu jiulize unataka kufikia kitu gani maishani mwako, halafu jiulize je, upo tayari kulipa gharama ya kukufikisha huko?
Kama haupo tayari kulipa gharama sahau kuhusu kufikia mafanikio unayotaka….
Hakikisha umejiunga na mfumo wetu wa kupokea Makala maalumu kwa watu maalumu. Jaza taarifa zako hapo chini.
-
Siku 30 Za Kushinda Kwa Kishindo (Juzuu 1)
Katika moja ya semina ambazo Zig Ziglar alikuwa anatoa kuna mtu mmoja ambaye alihamaki siku moja na kumwuliza, “hivi kwa nini hizi hamasa zenu huwa hazidumu?” Huku akiwa ametulia, Zig Ziglar alijibu kwa kusema kuwa hamasa ni kama kuoga, ukioga leo unapaswa kuoga na kesho. Tena wakati mwingine ukioga asubuhi utapaswa kuoga mchana na jioni au hata zaidi ya hapo. Hakuna mtu ambaye huwa analalamika kwa sababu ameoga mara nyingi. Kiufupi ni kwamba, usipooga kila siku utajikuta kwamba unanuka. Wewe mwenyewe bila kuambiwa na mtu yeyote utajistukia na kuanza kuwaogopa watu. Ni kitu gani kinakufanya uogope watu na kushindwa kuchangamana nao. Jibu ni kwa sababu hujaoga na unatoa harufu. Sasa inapokuja kwa hamasa inakuwa hivyo hivyo. Hamasa haidumu, hivyo inapaswa kuchochewa kila siku. Kuna watu wengi wamesahau ndoto za maisha yao, kwa sababu tu ya kukosa hamasa ya kuziendea ndoto zao. Zipo njia kadha wa kadha za kuongeza hamasa, ila moja ya njia hizo ni kusoma vitabu ambavyo vinaokuongezea hamasa ya kufanya makubwa. Tayari nimeakuandikia kitabu cha Jinsi Ya Kufikia Ndoto Zako, kitabu ambacho kinaeleza kwa kina jinsi ambavyo unaweza kufikia ndoto zako. Sasa kwenye kurasa za kitabu hiki unaenda kukutana na tafakari fupi ambazo utakuwa unasoma kila siku kabla ya kwenda kufanyia kazi ndoto yako na hivyo kupata hamasa na nguvu ya kuendelea kufanyia kazi ndoto zako. Ikumbukwe kwamba, hamasa sio kitu ambacho kinadumu, hivyo kila siku utahitaji kuendelea kujihamasisha na kitabu hiki kitakuwa kimbilio lako mara nyingi tu.
Kwenye kitabu hiki kuna tafakari 366 sawa na tafakari za mwaka mzima mrefu. Kama unasoma kitabu kwenye mwaka mfupi, yaani, mwaka ambao tarehe 28 ndio mwisho wa mwezi wa pili, basi tafakari ya tarehe 29 mwezi wa pili utairudisha nyuma siku moja au kuipeleka mbele siku moja. Hivyo, kutakuwa na siku ambapo utasoma tafakari mbili.
Kila tafakari imeanza na nukuu na mwishoni mwa kila tafakari nimekuwekea hatua ya kuchukua. Hizi ni hatua ambazo unaweza kufanyia kazi mara moja tu.Yaani, kuanzia leo hii. Ni imani yangu kuwa ukifanyia kazi utakayojifunza humu basi utaweza kufika mbali sana. Kila la kheri.
Godius Rweyongeza
Morogoro
21 Novemba 2020
-
Utapata Kile Unachotaka Kama Utawasaidia Watu Kiasi Cha Kutosha
Utapata kile unachotaka kama utawasaidia watu kiasi cha kutosha kupata kile wanachotaka-Zig Ziglar.
Ili wewe kupata kile ambacho unataka maishani unapaswa kuwa tayari kuwasaidia watu kupata kile wanachotaka wao. Kadiri unavyowasaidia watu kupata kile wanachotaka, ndivyo na wewe unakuwa kwenye njia ya kupata kile unachotaka. Kwa hiyo, kazi yako kubwa unayopaswa kufanya ni kutafuta kujua kitu ambacho watu wanataka, kisha kuwapatia hicho kitu tu. baasi.
Na hii ndiyo njia ambayo unaweza kutumia kutimiza ndoto kubwa. unaweza kuanza kidogo huku ukitafuta kuwapa watu kile kitu ambacho wao wanataka. Kisha kwa kutumia hicho kitu kidogo, ukaendelea kukikuza na kuifanyia kazi ndoto yako.
Kwa mfano unaweza kunzisha bishara yenye lengo la kuwasaidia watu, kisha kwa kutumia hiyo, watu wakakulipa.
watu watakulipa kwa kutatua tatizo lao ambalo wewe umetatua. kwa hiyo basi, kitu kikubwa unachopaswa kushughulika nacho kuanzia sasa hivi, ni wewe kuanza kutatua matatizo ya watu. tatua matatizo ya watu, fedha itafuata.
-
Jinsi Ya Kufanyia Kazi Ndoto Zako Wazazi Wanapokuwa Wanakupinga
Karibia kila wiki huwa naandika makala moja inayohusu ndoto na jinsi ambavyo unaweza kufiki andoto zako kubwa ulizojiwekea maishani. Kwenye makala ya jumapili ya leo ninaenda kuandika kuhusu tena kuhusu hii mada ya kipekee. Ambayo kila nikishika kalamu kuandika basi najikuta nahamasika zaidi kufanyia kazi ndoto zangu mwenyewe. Halafu eti nikishika kalamu wakati natumia kibodi ya kompyuta…
Kwanza kabla sijaandika sana, nipende kukutaarifu kuwa kitabu changu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO kina mambo mengi ndani yake ambayo yatakusaidia wewe kuweza kufikia ndoto zako. Maswali mengine napokea kuhusiana na hii mada ila nimeshayaandikia majibu kwenye hiki kitabu. Pata nakala laini kwa elfu kumi tu na nakala ngumu kwa elfu ishirini. Namba ya mawasiliano na ya kurusha fedha ni 0755848391.
Baada ya kusema hayo, nataka kwanza nikupe stori.
Miaka ya 1850 wazazi kwa kuona kuwa kijana wao angefaa kuwa mchungaji/padre walimpeleka kwenda kusoma na kupata mafunzo ya uchungaji. Kijana alisoma kwa bidii, ila ndani yake alikuwa akisikia kwamba kuna kitu anapenda kufanya nje ya uchungaji. Hivyo, baada ya kumaliza masomo kijana kwa mshangao mkubwa aliwashangaza wazazi wake kwa kusema kwamba alikuwa anaenda kuzunguka dunia huku akitafuta mimea na wanyama mbalimbali. Wazazi wake walitaka kijana awe mchungaji mara moja , ila kijana aliomba kwanza azunguke dunia walau mara moja halafu baada ya hapo atakuja kuendelea na uchungaji.
Kijana ninayemwongelea hapa ni Charles Darwin. Leo hii dunia inamfahamu vizuri huyu jamaa kama gwiji wa sayansi ya mageuzi (evolution). Hivi umewahi kusikia habari kwamba huyu jamaa alipaswa kuwa mchungaji/padre wa kanisa la anglikana?
Wazazi wake walikuwa wanapenda kweli awe mchungaji lakini kumbe yeye moyoni mwake kabisa alikuwa na kitu kingine alichokuwa anapenda kufanya.
Na wewe unaweza kukuta kwamba una ndoto kubwa ya kufanyia kazi kwenye maisha yako, ila sasa wazazi wako, ndio kikwazo kwako. Wenyewe wanataka ufanye kitu fulani ambacho ni kingine kabisa. sasa unafanyaje? Unafanyaje kwenye mazingira kama haya. Na hiki ndicho mwenzetu mmoja alitaka kujua
SOMA ZAIDI: Kwa nini wazazi wanawalazimisha watoto kusoma kozi wanazopenda wao
KWANZA UNAPASWA KUIJUA NDOTO YAKO KWA KINA
Unapaswa kuijua ndoto yako na wapi hasa unataka ndoto yako ikupeleke. Uwe na picha kubwa ya miaka kumi na ishirini ijayo. Hii ni picha ambayo hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kuiona. Hata ukiwaambia wazazi wako ni wazi kuwa hii picha hawawezi kuiona, badala yake wataona kwamba umekengeuka.
Wazazi kama walivyo watu wengine kwenye jamii, kuna maisha fulani ambayo wanataka kukuona ukiwa unaishi. Sasa ukienda kinyume na hayo maisha, basi wazazi kama wazazi, watataka wakurudishe ili uweze kwenda mstari. Mstari ambao jamii imechora na kusema kwamba haupaswi kuvukwa na mtu, hata kama watu hawasemi ila mstari huu upo vichwani mwa watu na mtu yeyote yule anayetaka kuuvuka huu mstari, ni sawa na mtu anayeenda na kinyume na taratibu za jamii.
Na unapokuwa na ndoto kubwa sana, maana yake unaenda kinyume na vitu vingi ambavyo jamii inaamini. Kwa mfano, utakuwa unaenda kinyume na umasikini ambao umetawala kwenye jamii na badala yake utataka kutengeneza utajiri mkubwa. Au utakuwa unaenda kinyume na imani fulani ambayo inaaminika kwenye jamii, huku wewe ukiona kwamba unaweza kuigeuza.
Mfano, rafiki yangu Kunyaula, yupo hapahapa Morogoro. Yeye ndoto yake kubwa ni kuona kwamba watu wanaacha kunywa soda na badala yake watu wanakunywa juisi freshi kabisa za matunda aliyotengeneza yeye kwenye kampuni yake ya Kunyaula FOODS….
Hii ni ndoto kubwa na ya kipekee ambayo inaenda kinyume na imani za watu wengi, lakini sasa hiyo ndio ndoto yenyewe. Ukija Morogoro, hakikisha unafika KFFJ na unapata walau hata juisi moja. Juisi zake ni za viwango vya tbs. Sijaona mtu mwingine akitengeneza juisi za viwango kama huyu jamaa hapa Tanzania. Namba yake ni hii hapa +255788080405
Mkurugenzi wa KFFJ akiwa kazini. Juisi zao ni za viwango vikubwa. Wapo Morogoro na delivery wanafanya pia. Watwangie tu kwa +255788080405
ukifika Mororogoro, usiondoke bila kufika KFFJ kwa Kunyaula
Enewei tuendelee..
Siku siyo nyingi nilikuwa nasoma kitabu cha JONATHAN LIVINGSTONE SEAGULL. Hiki kitabu kimeandikwa kwa mfumo wa hadithi ila kina mafunzo makubwa sana kuhusu kufuata ndoto zako najinsi ambavyo unaweza kuzifikia.
Kama sijakosea Seagull ni nyange kwa Kiswahili. Kitu kikubwa ambacho nyange wanafanya ni kutafuta chakula na kurukaruka mwaloni au sehemu yoyote iliyokaribu na maji ili kutafuta chakula. Hakuna zaidi ya hapo.
Lakini sasa nyange mmoja alikuwa anajulikana kama Jonathan Livingstone alikuwa na ndoto ya kupaa na kufika juu mawinguni kama tai. Hii ndoto hii, nadhani unaweza kuona jinsi ambavyo inaenda kinyume na mazoea au mstari ambao nyange wenyewe wamechora. Ebu ngoja hata nikuulize wewe, umewahi kuona nyange anapaa juu maiwnguni kama tai? Umewahi kuona hicho kitu?
Na ikitokea ukaona kitu kama hicho si utashangaa? Sasa hiyo ndiyo ndoto ambayo Jonathan Livingstone Seagull alikuwa nayo. Alitaka kupaa mpaka juu mawinguni zaidi hata ya tai.
Kilichotokea kilikuwa ni kukataliwa na wazazi wake na hata jamii nzima ya nyange. Kwa hiyo akaishi peke yake na baadaye akakutana na nyange wengine waliokuwa na ndoto kama hiyo, wakaungana na akawa ameweza kutimiza ndoto zake.
Kwa hiyo, unapokuwa ana ndoto kubwa ujiandae kabisa kuwa kila mtu atakuwa na maneno yake juu ya ndoto yako.
Juzijuzi tu nilikuwa naasoma kichekesho mtandaoni kilichosema kwamba. UKIZALIWA AFRIKA ni kama kuna sheria hivi ambayo haijaandikwa sehemu ila ipo vichwani mwa watu kuwa lazima tu utakuwa mkulima.
Hivi bado najibu swali au nimeenda nje ya mada…Basi naomba nihitimishe pointi yangu ya kwanza kwa kusema kwamba, unapokuwa na ndoto kubwa, hakikisha kwamba unaijua kwa undani kabisa na wapi unataka ikupeleke.
- SOMA ZAIDI: Hii Hapa Ndiyo Sababu Kuu Inayopaswa Kukusukuma Wewe Kutimiza Ndoto Yako
- Kwa nini hufikii ndoto zako
- Kwa Nini Watu Wengi Na Hasa Vijana Wanashindwa Kuzifikia Ndoto Zao
Sitaandika sana kuhusu hili, maana kuna makala za kukusidia kwenye hili. Kwa kuwa leo nataka nijikite zaidi kuhusu namna unavyoweza kushughulika na wazazi ambao hawasapoti ndoto zako, ila hapa nataka tu nikudokeze kuwa unapaswa kuanza kuifanyia kazi ndoto yako. Anza kuifanyia kazi hata kwa udogo, usisubri mpaka uwe na kila kitu. Hatua ndogo ndogo zitakufikisha kwenye ndoto yako rafiki yangu. Hii ni toafauti na na mtu ambaye anakaa bila kufanya kitu chochote kile. kwanza angalia picha hii hapa chini.
Umeiona picha hiyo. Haya ni mashindao ya wanyama na wanyama wengine tayari wameshaanza kukimbia ila kamnyama kamoja bado kamelala humo ndani. Kanajua kukimbia kweli kuliko hao wengine wote, ila sasa asipotoka na kukimbia, hatashinda.
hiki kitu ndio nataka nisisitize na kwako. unaweza kuwa una ndoto kubwa. au una kipaji na unataka ukifikishe mbali. nisikilize, kama hutaanza kukifanyia kazi hutakaa ukifanikishe. Kwa, hiyo, anza kuifanyia kazi ndoto yako kuanzia sasa hivi.
- SOMA ZAIDI: Usikubali Kuendelea Kubaki Hivyo hivyo
- KANYAGA MAPIGO YOTE YA KUITWA MTU WA KAWAIDA
- KAMA HUWEZI KUKIFANYA KWA VIWANGO VIKUBWA, KIFANYE HATA KWA VIWANGO VIDOGO
Kama nilivyosema kwamba unapokuwa na ndoto kubwa, hakuna mtu ambaye anaweza kuiona picha kubwa unayokuwa nayo. Siyo hata mwenza wako. Kwa hiyo, linapokuja suala zima la wazazi, kaa chini ongea nao. Waambie kwamba mimi ndoto yangu ni hii na ninaenda kuwa naifanyia kazi, hii ndoto itakuwa na manufaa yafuatayo kwwangu, kwenu na kwa taifa…
Hivyo naomba mnichae kwanza niifanyie kazi ndoto yangu.
NNE: WAAMBIE WAZAZI WAKUPE MUDA KWANZA KUIFANYIA KAZI NDOTO YAKO
Kama bado wazazi hawakuelewi, basi omba wakupe muda wa kuifanyia kazi ndoto yako. Waambie kwamba ninaenda kuifanyia kazi ndoto yangu kwa mwaka mmoja au mwili kwanza, kama nitakuwa bado sijapata kitu chochote wala kufikia sehemu yoyote ile nitaachana na ndoto yangu na kuendelea nakile mnachotaka.
Kuna watu wametumia hii mbinu na imewasaidia.
Ndani ya hiyo miaka uliyowaambia hakikisha kwamba unafanya kitu chako kwa ubora kiasi wkamba mpaka miaka hiyo hii inafika mwishoni, wewe tayari umepiga hatua fulani, lakinip ia wazazi wako tayari wamekuwa mashabiki wa kile unachofanya.
TANO, USIWATEGEMEE WAZAZI WAKO KWA KIPATO WALA CHAKULA
Ngoja nikwambie ukweli usiopenda kUusikia. Ukweli ni kwamba wazazi wako wanakuzuia wewe kufanyia kazi ndoto zako kwa sababu tu unaenda kuwa mzigo kwao. Wanataka ufanye kitu fulani walau uweze kuingiza kipato uache kuwasumbua. Lakini pia na wao wanataka wapate kitu chochote kutoka kwako. hahah
Sasa ukilijua hili halitakusumbua. Badala yake utapaswa kuhakikisha kwamba hatua ya kwanza unaanza kujitegemea. Usiseme kwamba unafanyia kazi ndoto yako, unatoka nyumbani na baadaye jioni unarudi unategemea chakula cha wazazi.
Anza kubeba jukumu la maisha yako kwa asilimia 100. Waambie wazazi wako kuwa hata kama sijaajiriwa ila mimi sitawategemea ninyi kwa kitu chochote. Sitategemea chakula wala malazi kutoka kwenu. Nitapambambmana na hali yangu. walau anzia hapo.
Ukiweza hata kuanza kujihudumia wewe, utafikia hatua ambapo na wenyewe utakuwa unawarushia kiasi fulani cha kutumia. Kitu ambacho wanataka.
Wao wanahofia kwamba ukifanyia kazi ndoto zako, hutapata hela… utaendelea kuwa mzigo kwao. Wewe bado tu hufunguki mshikaji wangu… Au basiiiiiiii.
Kuna usemi kuwa nabii hakubaliki nyumbani. Kwenye biblia Yesu hakukubalika nyumbani kwao na hata walimuua. Ila ukristo ulikuja kukubalika maeneo mengine kuliko hata unavyokubalika nyumbani kwao. Leo hii ni asilimia mbili tu ya wayahudi ambao ni wakristo. Wengine wote wanaendelea na maisha yao kama kawaida.
Kama umetumia mbinu hizo hapo juu na hazijakubalika, basi utapaswa kutoka nyumbani na kwenda kupambana maeneo ya tofauti kidogo nje ya nyumbani. huku kutakuwezesha wewe kukaa mbali na watu ambao wanakukatisha tamaa au kukurudisha nyuma au kukudhoofisha kwa namna yoyote ile. Lakini pia kwa kuwa utaenda kwenye mazingira mapya ambayo hakuna mtu anayekujua, utakuwa na uhuru wa kufanya kitu hchochote kile bila ya kuogopa, badala yake utakuwa tayari kuipambania ndoto yako.
Kwa leo nataka niishie hapa. Kama kuna hoja zaidi basi tuendeleze mjadala kwenye eneo la maoni. Mimi mwenyewe nitakuwepo kujibu hoja yoyote zaidi itakayojitokeza.
Mpaka wakati mwingine, mimi ni Godius Rweyongeza kutoka songembele.
Kupata makala zaidi kutoka kwangu, hakikisha kwamba umejiunga na mfumo wetu wa kupokea makala maalumu kwa kujaza taarifa zako hapa chini.
Umeshajiunga na THINK BIG FOR AFRIKA wewe?
Mmhh yaani na wewe? Hata kusema tu ngoja nifoward haka ka makala kwenye grupu moja la WhatsApp 😂😂. Au basi!
-
Historia ya Kiswahili
Ukisoma historia ya Kiswahili unaona kwamba kilianza kimasihala tu. Kilianza kutumiwa maeneo ya Pwani na baadaye kikasambaa kuja bara na mpaka leo hii, kina wazungumzaji zaidi ya milioni 150. Ni lugha pekee barani afrika ambayo siyo ya kigeni ila watumiaji wengi.
Ninataka kusema nini sasa hapa.
Ninataka niseme kwamba, kitu chochote kikubwa huwa hakianzi kwa ukubwa wake.
Mbuyu huwa unaanza kama mchicha.
Wewe pia kwa ndoto yako pia. Usitegemee kwamba ndoto yako kubwa utaifanikisha ndani ya siku moja au wiki. kuwa na ndoto kubwa ila anza kuifanyia kazi kidogo kidogo bila kurudi nyuma.
Juhudi zako kidogo kidogo zinaweza zisionenake ndani ya siku moja, ila baada ya muda hizo juhudi zitakusanyika na kutengeneza kitu kikubwa.
Ebu fikiria kwa mfano una ndoto ya kuandika kitabu…
Ukiangalia vitabu vilivyo vingi vina kurasa 200 mpaka 400. Ukifikiria hili tu unakata tamaa. Lakini kabla hili halijakukatisha tamaa, nataka nikwambie kwamba unaweza kuandika kitabu chako kwa kuanza kidogo..
Of course kidogo mwanzoni kitaonekana kama siyo chochote. Utakuwa kama unachota maji kutoka baharini kuweka nchi kavu. Lakini hichohicho kidogo ukikifanya kwa uendelevu, mwisho wa siku kitakuwa kikubwa…
Kwa hiyo, kitabu chako unaanza kukiandika hivi,,
Unakiandika kama unavyoandika ujumbe mfupi…
Kwani wewe kwa siku unaandika jumbe ngapi au unajibu jumbe ngapi ambazo zinatumwa kwako…
Hivi hizi jumbe unazoandika kila siku baada ya mwaka tukiziunganisha ni sawa na kitabu chenye ukubwa gani? sasa na kitabu chako nataka ukiandike kama unavyoandika ujumbe mfupi…
Badala ya kusubiri ukiandike chote kwa pamoja na kwa siku moja. anza kuandika maneno 100 tu kila siku. Maneno 100 ni sawa na ujumbe mfupi na unaweza kuyaandika ndani ya dakika tatu tu…
Sasa kila siku ukiandika maneno 100 baada ya mwaka ni sawa na maneno 36,500. Hiki tayari ni kitabu kikubwa.
Hivi ndivyo ndoto kubwa zinavyofanyiwa kazi….
Inawezekana wewe ndoto yako siyo kuandika kitabu ila pointi kubwa ninayotaka nikwambie ni kwamba, kwa ndoto yoyote ile uliyonayo basi fikiria namna unavyoweza kuanza kuifanyia kazi leo hii. Na usifanye kazi kwa siku moja kisha ukaacha, endelea kuifanyia kazi kila siku mpaka kieeweke.
Ila kama una ndoto ya kuandika kitabu kweli.. pengine kozi yangu ya uandishi inakuhusu, japo sasa hivi imejaa wanafunzi. Ila wasiliana nami, ntajua namna ya kukupitisha mlango wa nyuma ili ujiunge.
Umekuwa nami.
GOdius Rweyongeza kutoka SONGAMBELE
Tuwasiliane kwa 0755848391
Morogoro-Tz
NB: Ile ofa ya ebooks zangu tatu bado inaendelea kuna watu wanachangamka kujinyakulia hizi ebooks za kipekee, sasa sijui wewe umekwama wapi.
Nashauri sana upate hizi ebooks maana zitakusaidia sana. ebooks zenyewe niNGUVU YA WAZO: Jinsi WAZO LINAVYOWEZA KUBADILI DUNIAKIPAJI NI DHAHABU: Jinsi ya kugundua, Kunoa na kuendeleza kipaji chakoMITAJI 8 ILIYOKUZUNGUKA NA JINSI YA KUITUMIA.Hizi ebooks ni za kipekee sana, na siyo za kukosa kiukweli. Pata ebooks hizi kwa gaharama ya 12,000 tu leo hii. Utatuma fedha kwa 0755848391 jina ni Godius Rweyongeza. Baada ya hapo utanitumia ujumbe nikutumie hivi vitabu.
Ikumbukwe kwamba hivi vitabu gharama yake ni zaidi ya elfu 30+
Baadaye….
MAKALA YA LEO
PODCAST YA LEO -
IJUE NJIA YA KUFUATA
Kama haujui njia ambayo unapaswa kuchukua basi njia yoyote ile itkupeleka
Ebu fikiria kitu kama hiki hapa, umeenda stendi ili kukata tiketi, halafu unampa mkata tiketi pesa yako. Na unamwambia kwamba unaomba akupe tiketi unadhani atakuwambiaje? Au au nadhani swali gani atakuuliza? Unaelekwa wapi? Ebu fikiria unamjibu kwamba sijui. Atakwambia kwamba kama haujui basi rudi nyumbani, kitu kama hiki ndicho huwa kinatokea kwa watu wengi kwenye maisha, yaani huwa kinawatokea watu wengi maishani. Yaani, huwa wanapita kwenye misha bila ya kuwa na mwelekeo. Ni sawa na kwamba huwa wanachukua njia yoyote maishani mwao. Hawajui haswa ni wapi wanaelekea.
Huyu hapaswi kuwa wewe. Hakikisha kwamba unakuwa na ramani ya wapi unaelekea. Jua nini unapaswa kufanya na kw anini unataka kuelekea huko. Jua ni watu gani ambao utapaswa kwenda nao ili uwezeu kufika na gharama ambazo utapaswa kulipa ili kufikia huko. Kama ni fedha jua kiwango cha fedha kitakachohitajika hataka kama ni kwa kukadiria, kisha anza kuweka mkakati wa kuhakikisha kuwa unapata kiasi hicho cha fedha
-
Matendo yako, Ndio matendo yako
Miongoni mwa ukweli ambao unapaswa kuufahamu ni kwamba matendo ndiyo yanapaswa kutangulia matokeo na siyo matokeo yatangulie matendo.
Yaani, huwezi kuwa na afya njema kwanza, halafu eti ndio ukaja kuanza kula vizuri. Hapana
Unakula vizuri ndio maana una afya njema.
Unafanya mazoezi ndio maana una afya njema.
Unaweka akiba benki ndiyo maana una fedha ya kutosha.
Unawekeza ndio maana utajiri wako unazidi kukua
Kiufupi hakuna namna ambavyo unaweza kupata matokeo kabla ya kutanguliwa matendo.
Sasa hapa kazi ni kwako, kujua ni matokeo gani ambayo wewe unataka. Kisha sasa kuwa tayari kukwekazi ili kufikia hayo matokeo.
PODCAST YA LEO
MAKALA YA LEO
NB: Hivi jana nilikwambie kweli? Kama sikukwambia ni kwamba, kwa sasa hivi kuna ofa ya vitabu vitatu ambavyo unaweza kuipata kwa 12,000 tu. ni vitabu vitatu vya kipekee. na ninafikiri kwa mwaka huu, hii inaweza kuwa ofa yangu ya mwisho. ichangamkie rafiki yangu.
Tuma elfu kumi na mbili leo 12,000 na utumiwe ebooks tatu zenye thamani kubwa sana.
eBOOKS hizi ni pamoja na
NGUVU YA WAZO: Jinsi Wazo Linavyoweza Kubadili Dunia
KIPAJI NI DHAHABU: jinsi ya kugundua, Kunoa na kuendeleza Kipaji Chako
MITAJI 8 ILIYOKUZUNGUKA NA JINSI YA KUITUMIA.
Malipo yatatumwa kwa namba 0755848391 jina ni GODIUS RWEYONGEZA. Baada ya hapo usisahau kunitaarifu ili nikutumie ebooks hizi za kipekee. -
Nyakati Ngumu Hazina Ukomo
Leo nimekumbuka mwaka 2018 na 2019 jinsi watu walivyokuwa wanalalamika kwamba vyuma vimekaza. Kuna watu wengi walikuwa wanasema kwamba hawawezi kufanyia kazi malengo yao kwa sababu tu vyuma vimekaza.
Nakumbuka kila nilipokuwa nikiongea na watu, kitu muhimu nilichokuwa nikiwasisitiza kilikuwa ni kwamba, USISUBIRI VYUMA VILEGEE. Badala yake katika kukaza hukohuko, wewe mwenyewe pambana kuhakikisha kwamba kila kitu kinanyooka.
Baadaye mwaka 2020 kuliltokea ugonjwa wa UVIKO-19. Basi sasa kipindi hiki kisingizio kilikuwa ni UVIKO.
Ulipokuwa unaongea na mtu, kwa nini huweki akiba, sababu ilikuwa ni UVIKO-19
Mwingine ungemwuliza kuhusu ndoto yake, basi alikuwa anasema kwamba UVIKO-imenizuia kuifanyia kazi.
Kiufupi, kila kitu kilikuwa kinaelekezwa kwenye UVIKO-19.
Na sasa siku za karibuni umetokea mfumuko wa bei..
Kila kitu sasa kinaelekezwa kwenye bei za vitu kupanda.
Nataka nikwambie kitu……….hakuna wakati ambao mambo yatakaa yawe safi kabisa bila shida yoyote. Yaani, yanyooke kwa asilimia 100. Nyakati ngumu huwa haziishi. Unachohitaji ni wewe kuwa mgumu.
Muda mwingine unaamua tu kufanya kitu hata kama mambo mengine yanaonekana yanakwenda kinyume chako, maana ukisubiri kila kitu kikae sawa. UTASUBIRI SANA.
Unakumbuka miaka ya 2010 kusajili lailni ya simu kulikuwaje? Ulikuwa unaenda kwa wakala,anajaza fomu fulani hivi baadaye unapewa lalini yako na kuondoka.
Wakati mwingine ulikuwa unakuta laini imesajiriwa, unapewa laini yako unaondoka.
Vigezo havikuwa kama sasa hivi, si ndio?
Hii mitandao ya simu haikusubiri mpaka ijue kila kitu ndio ianze. Walianza, halafu haya mambo mengine ya kiteknlojia wameyachukua humu njiani.
Nataka hiki kitu kikupe funzo na wewe pia.
Usisubiri mpaka kila kitu kikae sawa eti uanze. Anza, halafu mambo mengine, utakuwa unaboresha kadiri unavyoenda.
Sikiliza, nyakati ngumu huwa haziishi kwenye maisha. Nyakati ngumu zipo na zitaendelea kuwepo. Kitu kikubwa ni wewe kuamua kuwa mgumu pia kwenye kazi zako.
Haya maisha usipojitoa kufanyia kazi ndoto yako. Kila wakati kutakuwa na sababu ya kukuzuia usiifanyie kazi.
Kama siyo vyuma kukaza basi ni UVIKO-19, kama siyo UVIKO basi mfumuko wa bei.
Kuwa mgumu, pambania ndoto zako.
hiki kitu kinanifanya nikumbuke kitabu cha NYUMA YA USHINDI: Kuna kushindwa, Kushindwa, Kushindwa. Ni kitabu ambacho unapaswa kusoma pia maana ndani yake utajifunza mengi. Kupata kitabu hiki, wasiliana nami kwa 0755848391. kwa sasa hivi kuna ebooks au softcopy tu. na inapatikana kwa 5,000/- tu.
jiunge na mfumo wetu wa kupokea makala maalumu kwa watu maalumu hapa chini
-
Je, Kuna Namna Na Kutengeneza Fedha Kupitia Affiliate Marketing Ukiwa Nchini Tanzania?
Habari ya huko upande wa pili. Mimi kutokea hapa mkoani Morogoro naendelea vizuri tu.
Siku ya leo napenda kujibu swali la mmoja wetu hapa kwenye jukwaa ambaye ameniuliza kama kuna namna ya kutengeneza fedha kupitia affiliate marketing ukiwa hapa nchini Tanzania.
Na mimi kwa ufupi napenda kusema kwamba INAWEZEKANA.
Ila naomba usome ujumbe huu mpaka mwisho, ili uweze kuelewa hii dhana ya affiliate marketing kwa undani.
Kwanza kabisa tujibu swali la inawezekanaje?
Napenda kusema kwamba inawezekana kupitia mtandao wa GETVALUE. Ambao ni mtandao wa Kitanzania kabisa, na ndani yake unaweza kuchukua bidhaa zinazouzwa humo, ziwe ni ebooks au kozi mbalimbali na kuwashirikisha watu wengine, ambapo mtu akinunua hiyo kozi au ebook basi wewe unapata kamisheni yako. Mtandao wa GETVALUE unakulipa asilimia kumi ya kila bidhaa itakayolipwa kupitia kwako.
Kwa hiyo kama kozi inauzwa kwa gharama ya laki moja. Punde tu baada ya hiyo ebook kununuliwa kwenye akaunti yako utaingiziwa elfu kumi ambayo unaweza kuitoa hapohapo au ukasubiri iongezeke pale watu watakaponunua kozi au ebooks zaidi kupitia kwako .
Mfano mzuri ni kitabu changu hiki cha Kutoka Sifuri Mpaka Kileleni. Hiki kitabu unaweza kukipata kwenye mtandao wa GETVALUE. Na ebook inauzwa elfu kumi.
Kwa hiyo kama wewe ukiitangaza na mtu akainunua kupitia link maalumu ya affiliate marketing ambayo ni ya kwako. kikiuzwa tu, unapata elfu moja hapohapo bila ya kuchelewa.
Kadiri utakavyouza kitabu kwa watu wengi zaidi ndivyo utakavyopata kiasi kikubwa zaidi…
Nadhani upande huo umeisha…
Ukitaka kujua namna ya kutengeneza akaunti ya affiliate marketing, unaweza kuangalia video hii hapa chini
Sasa hapa nataka niongee kitu, ambacho ni zaidi ya kutengeneza akaunti.
Mpaka hapa umeshajua kwamba inawezekana wewe kutengeneza akaunti ya affiliate marketing, na umeshajua kwamba unaweza kupata hela kwa njia hii.
Sasa kifuatacho nataka nikwambie kwamba, unapaswa kukifanya kwa uendelevu. Kwa miaka ambayo nimekuwa naandika na kuuza vitabu, nimegundua kwamba huwezi kumwambia mtu mara mmoja kwamba una kitabu akanunua, kuna watu ni wagumu kununua. Na hili siyo kwenye vitabu tu, lakini pia kwenye karibia kila bidhaa kutoka kwenye kila sekta. Ndio maana kampuni za magari zinajitangaza kila siku. Ndio maana kampuni za simu zinajitangaza kila siku pia. Kwa sababu kuna watu hawachukui hatua mara moja.
Hivyo, basi, kama unategemea kuingiza kipato kwa hii njia, hakikisha kwamba, unatangaza na kuwakumbusha watu wako mara kwa mara ili waweze kununua na hatimaye wewe uweze kuingiza kipato kizuri tu.
Pili ni kwamba, tangaza bidhaa ambazo ni nzuri kwa watu wako, ili wakinunua hizi bidhaa, mwisho wa siku waweze kurejea kwako kujua bidhaa gani zaidi wanaweza kununua, na hivyo uendelee kutengeneza pesa kupitia hao watu kwa mara nyingine.
Tatu, weka mpaka utaratibu wa kuwaelimisha watu wako. Ili kupitia elimu unayotoa, watu wahamasike na waweze kuchukua hatua, kitu kitakachopelekea wewe kupata kiasi fulani cha fedha.
Baada ya kusema hayo, naomba sasa uingie kwenye mtandao wa GETVALUE.CO halafu ujinyakulie kitabu changu cha JINSI YA KUFIKIA NDOTO ZAKO.
Vitabu vyangu vingine hivi hapa.
Mpaka wakati mwingine, mimi sina la ziada
-
Songambele
Rafiki yangu, muda wote na mara zote unapaswa kuwa mtu wa kusonga mbele. Usikubali kukwama na wala kubaki eneo lile bila ya kusongambele.Vitu ambavyo vinakaa sehemu moja bila ya kusongambele huwa vina sifa mbaya kweli.
Maji yaliyotuama, ndio huwa yanazalisha mbu wa malaria. Hata mdomo wako ukiufunga bila kuongea kwa muda mrefu unatoa harufu mbaya.Kwa kawaida asili haipendi kitu kikae bila ya kuwa kwenye mwendo. Ndio maana dunia linajizungusha kwenye mhilimi wake kila sekunde, matokeo yake ni usiku na mchana pamoja na majira (kiangazi, vuli, kipupwe..)
Ardhi ikikaa bila ya kupandwa kitu, utakuta kwamba ndani yake yanaota majani (magugu)
Hata watalaam wa afya hawashauri ukae eneo moja bila kuzunguka na kule.
Kwa hiyo, mara zote jiulize unapiga hatua? Unafanya kitu cha kukufanya usonge mbele.
Usikubali kubaki eneo moja ukiwa umetuama kama maji…songambele la sivyo utazalisha mbu wa malaria.Waingereza nao wana usemi wao, unaosema kwamba the idle mind is the devils workshop. Ukimaanisha kuwa akili inayokaa bure ni karakakana ya shetani.
Sasa wewe unataka akili yako ichezewe na shetani..ukiona unakaa bila ya kufanya kitu, ujue kwamba unakaribisha shetani. Kwa hiyo badala yake songambele.
Nipo najiuliza ni kitu gani kinakuzuia wewe kusonga mbele? Je, ni kwa sababu huna mtaji? Je, ni kwa sababu ni kwa sababu unajiuliza kuhusu wazo lako la biashara ni bora au siyo?
JIFUNZE ZAIDI: USIISHIE TU KUKAA KWENYE KOCHI NA KUSEMA ONE DAY YESKumaliza tatizo hilo, nimekuandalia ofa ya vitabu vitatu kwa gharama ya elfu 12,000 tu. Hii ni ofa ambayo nadhani itakuwa ya mwisho mwisho kwa mwaka huu. siriaz! Unaweza usipate ofa nyingine kutoka kwangu mpaka mwaka huu unaisha. Kwa hiyo cha kufanya, ni wewe kuhakikisha kwamba unaichangamkia.
Tuma 12,000/- leo nikutumie ebooks tatu ambazoMITAJI 8 ILIYOKUZUNGUKA NA JINSI YA KUITUMIA
NGUVU YA WAZO (the Powe Of An Idea): Jinsi wazo linavyoweza kubadili dunia pamoja na
KIPAJI NI DHAHABU: Jinsi ya kukigundua, kukinoa na kutumia kipaji chako.
Hizi ni ebooks tatu za kipekee sana kutoka kwangu ambazo zenye thamani kubwa sana ambazo unaenda kupata kwa bei ya ofa. Nadhani hii inaweza kuwa miongoni mwa ofa zangu za mwisho kabisa kwa mwaka huu. ichangamkie sasa…
Mpaka wakati mwingine, mimi ni Godius Rweyongeza kutoka SONGAMBELE
0755848391
Morogoro-Tz